stories

336. KALAGU – KIZE. IGAGI LYA HA LUB’IMBI UDULIB’UTA – ILUMBUYO.

Imbuki ya kalagu yiniyo yingilile kub’ub’uti wigagi lya halub’imbi. Iligagi linilo, lilijimanijkijo ja ngelelo go kikolo ja ng’wa munhu, na wandijo  b’ojikolo ja ng’wa ungi. Ulu munhu ulib’inza iligagi linilo mumho ojijimija ijimanikijo jinijo. Hunagwene abhanhu bhagaganaga giki, ‘igagi lya halub’imbi udulib’inza.’ Uungi oshosha giki, ilumbuyo.

Ikalagu yiniyo igalenganijiyagwa kuli munhu uyo aliha guntola ilumbuye. Uilumbuye ng’wunuyo alisawa nigapi linilo ilyaha lub’imbi. Gashinaga lulu, ilemejiwe uguntola munhu uyo alinduguye ogubyalwa munda yimo. Hunagwene abhanhu bhagiganilaga kiki, ‘igagi lya ha ulub’imbi udulibuta:- Dada yako.’

Ikalagu yiniyo yalanga bhanhu higulya ya kudiimila malagilo gali wiza umuchalo jabho, kugiki bhadule kupandika matwajo mingi umuwikaji bhobho.

Mambo ya walawi 8:9.

Mambo ya walawi 20:17.

2 Samweli 13:11 – 12.

Waroma 27:22.

KISWAHILI: KITENDAWILI  – TEGA

MUWA WA MPAKANI HUUKATI: – DADA YAKO

Chanzo cha kitendawili hicho chatokea kwenye ukataji wa muwa wa mpakani. Muwa huo ni kitambulisho cha pale ambapo mali ya mtu inaishia na pale inapoanzia mali ya mtu mwingine. Mtu akiukata muwa huo, maana yake ameiondoa alama ya kitambulisho cha mpaka huo. Ndiyo maana watu huambiana kwamba, ‘muwa wa mpakani huukati: mwingine hujibu – dada yako.’

Kitendawili hicho hulinganishwa kwa mtu ambaye hutaka kumuoa dada yake. Dada huyo ni sawa na muwa huo wa mpakani. Kumbe basi, mtu haruhusiwi kumuoa ndugu yake wa tumbo moja. Ndiyo maana watu huambiana kwamba, ‘muwa wa mpakani huukati: mwenzake hujibu, dada yako.’

Kitendawili hicho hufundisha watu juu ya kushika maagizo yaliyomema katika jamii, ili waweze kupata mafanikio mengi maishani mwao.

Mambo ya walawi 8:9.

Mambo ya walawi 20:17.

2 Samweli 13:11 – 12.

Waroma 27:22.

cane

 

ENGLISH: I HAVE A RIDDLE – LET IT COME

THE BORDERLINE SUGARCANE THAT SHOULD NOT BE CUT:- YOUR SISTER.

The source of this riddle comes from cutting borderline sugarcane. Such sugarcane functions as an identification post that marks the end of someone’s property and the beginning of another one’s property. Cutting the borderline sugarcane means disturbing some other people’s possessions.

This riddle can be compared to someone who wants to marry his sister. The sister is likened to the borderline sugarcane that a brother cannot dare to cut it, which implies that a brother is not allowed to marry his sister.

This riddle teaches people to abide by societal principles that make them become good members of the society who are capable of nurturing their families in a morally accepted manner.

Leviticus 8: 9.

Leviticus 20:17

2 Samuel 13:11 – 12.

335. MHUNDU JILIGILING’HANYA HA KAWINGA KA NHYEHU.

Imbuki ya kahayile kenako yingilile kub’utuji bho mhundu hawinga bho bhanhu bhalyehu. Ulu munhu uyo alitola alinhyehu, abhanhu nabho bhagayegaga bhayutula na mhundu. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘mhundu jiligiling’hanya ha kawinga ka nhyehu.’

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagikalaga chiza na bhichabho. Uwikaji bho bhanhu bhenabho bhulisawa na winga, ubho bhuli na bhuyegi bhutale, kunguno yabhoyi gwikala na b’uyegi bhunubho. Ubhunubho hu winga bho nhyehu, uyo agabhizaga na bhuyegi bhutale umukikalile kakwe. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘mhundu jiligiling’hanya ha kawinga ka nhyehu.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya gub’iza na bhulyehu ubhogudula gwikala chiza na bhanhu, umukikalile kabho.

Ufunuo 19:7=9.

Matendo ya mitume 2:46.

KISWAHILI: VIGELEGELE VINASIKIKA KWENYE HARUSI YA MPOLE

Chanzo cha msemo huo chatokea kwenye upigaji wa vigelegele kwenye harusi ya watu wapole. Mtu anayeoa akiwa mpole, watu nao hufurahia sherehe yake kwa kupiga vigelegele. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘vigelegele vinasikika kwenye harusi ya mpole.’

Msemo huo hulinganishwa kwa watu ambao huishi vizuri na wenzao. Maisha hayo ni sawa na harusi yenye furaha kubwa, kwa sababu ya wao kuishi kwa furaha na watu wao. Hiyo ndio harusi ya mpole, ambaye huwa na furaha kubwa maishani mwake. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘vigelegele vinasikika kwenye harusi ya mpole.’

Msemo huo hufundisha watu juu ya kuwa na upole wa kuwawezesha kuishi vizuri na wenzao, maishani mwao.

Ufunuo 19:7=9.

Matendo ya mitume 2:46.

black-and-white wedding

couples

 

ENGLISH: JOYFUL VOICES ARE HEARED AT A GENTLE’S WEDDING

The source of this saying is wedding ceremony where couples are presumed to be gentle in terms of their behaviour. When a gentle man/woman marries people enjoy his/her wedding by singing joyful songs. This is why people say, ‘joyful voices are heard at a gentle’s wedding.’

Such a saying can be compared to people who live well with their neighbours. This kind of life can be likened to happy marriage because they live happily with their neighbours.

This saying teaches people about being gentle enough in order to be able to live peacefully with others.

Revelation 19: 7 = 9.

Acts 2:46.

334. GUKO NGILI ISE O NG’WAMBI.

Imbuki ya lusumo lunulo yingilile kub’itoji abho b’iyambilijaga uguitumama imilimo yabho.  Abhanhu bhenabho bhali nkima na ngosha abho bhalib’itolile. B’iyambilijaga gufuga, nulu gusegegesa mabhele. Unkima onkangililaga ungosha, bho gujishindika ijisabho ijojalijitungilile mlusunda, ulugoye lutungwa kumahaba, nang’hwe ungosha onkangililaga unkima. Bhuli ng’wene uluonkangilila ung’wiye ijisabho jinijo, oyombaga giki, ‘guko ngili ise o Ng’wambi.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kubhitoji abho bhali na bhumo, umukikalile kabho. Abhanhu bhenabho, bhagaitumamaga imilimo yabho bhogwiyambilija chiza. Bhagabhalangaga na bhazenganwa b’abho akajile ka gwikala na bhumo bhunubho, umuwikaji bhobho wa witoji.

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu abho witolile higulya ya gub’iza na b’umo, bho gwiyambilija utuitumama imilimo yabho, umuwikaji bhobho.

Mwanzo 2:18.

Tobithi 8:4-8.

KISWAHILI: HUKO NGILI BABA WA NG’WAMBI

Chanzo cha methali hiyo chaangalia wanandoa ambao husaidiana katika kufanya kazi zao. Watu hao ni mwanamke na mwanaume waliofunga ndoa. Wao husaidiana kuchekecha maziwa. Mwanamke humsukumia mwanaume kibuyu kwenye maziwa hayo, ambacho huzungushiwa kamba iliyohufungwa kwenye mlingoti juu, ili kiweze kuning’inia, naye mwanaume hukisukuma kibuyu hicho kuelekea kwa mwanamke. Kila mmoja amsukumiapo mwenzake husema hivi, ‘huko ngili baba wa Ng’wambi.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa wanandoa ambao wana umoja maishani mwao. Watu hao hufanya kazi zao kwa kusaidiana vizuri. Huwafundisha pia majirani zao namna ya kuishi katika umoja huo, katika maisha yao.

Methali hiyo hufundisha watu wa ndoa juu ya kuwa na umoja wa kuwawezesha kusaidiana katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku, maishani mwao.

Mwanzo 2:18.

Tobithi 8:4-8.

africa uganda

THERE IS NGILI; THE FATHER OF NG’WAMBI.

This saying is based on couples that help each other in their daily activities. It pictures a hanging calabash with little milk in it being tied to one of the roof poles. The wife and husband push it (the calabash) to each other in an attempt to shake the milk. Each of them pushes it by saying, ‘there is Ngili, the father of Ng’wambi.’

This saying can be comparable to married couples who live in unity throughout their lives. They work together by helping each other in viarious activities. They also teach their neighbours on how to live in peace, and unity in their lives. That is why they say to each other, ‘there is Ngili; the father of Ng’wambi.’

The saying teaches married couples how to maintain their unity by living in peace so as to fulfill their tasks of taking care of their families.

Genesis 2:18.

Tobithi 8: 4-8.

333. GILAGA GITUMO WAGILILA HA LUB’ELE.

Imbuki ya lusumo lunulo yingilile kubhuleki bho ng’wana gong’ha ha lub’ele lo ng’wa nina. Ung’wana ulu ubyalwa agong’haga lub’ele halinina mpaka okula wikoma gulya. Ulu ukula ung’wana ng’wunuyo agabishiyagwa ogila ugong’ha. Ulu ubishiwa agagilaga ugong’ha na adalashokela. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘gilaga gitumo wagilila ha lub’ele.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo witaga mihayo ya bhub’i, uyo agawilaga giki oye ugwiita imihayo yiniyo gitumo oyela gong’ha ha lub’ele lo ng’wa nina. Abhanhu abho umunhu ng’wunuyo ob’itilaga imihayo yiniyo, hab’o hagang’wilaga umhub’i ng’wunuyo giki, ‘gilaga gitumo wagilila ha lub’ele.’

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya goya gwita mihayo yabhub’i, na gub’awila abhahub’i bhoye ugwiita imihayo imib’i yiniyo, gitumo bhagilila ha lub’ele lo b’aninabho.’

Wakolosai 3:5.

KISWAHILI: ACHA KAMA ULIVYOACHA ZIWA

Chanzo cha methali hiyo chatokea kwenye kuacha kunyonya kwa mtoto kwenye ziwa la mama yake. Mtoto akizaliwa hunyonya maziwa ya mama yake, mpaka anakua kiasi cha kutosha kula chakula. Akikua mtoto huyo huachishwa kunyonya ziwa na mama yake. Akiachishwa hivyo, mtoto huyo hukoma kunyonya na hatarudia. Ndiyo maana watu huambiana kwamba, ‘acha kama ulivyoacha ziwa.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu aliyefanya kitu kibaya kwa wenzake, ambao humwambia akome kufanya hivyo, kama alivyo koma kunyonya ziwa kwa mama yake. Watu hao aliowatendea kitendo hicho, yule mkosefu, huumia sana mpaka kufikia hatua ya kumwambia mtu huyo kwamba, ‘acha kama ulivyoacha ziwa.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuacha kutenda matendo mauvu katika jamii, kwa sababu matendo hayo huwaumiza sana wenzao. Ndiyo maana wao humwambia, mtu huyo aache maovu hayo kama alivyoacha kunyonya ziwa kwa mama yake.

Wakolosai 3:5.

woman breatfeeding

 

ENGLISH: STOP AS YOU STOPPED FEEDING AT YOUR MOTHER’S BREAST

This proverb has its origin in breastfeeding. It is obvious that when a baby is born, it begins by feeding at its mother’s breasts until when it is old enough to eat other food stuff.

At the time the baby begins eating other food stuff the mother can stop him/her from breastfeeding.

This proverb can be compared to a person who does something wrong to his/her friends then warned against it. The warning can be associated with stopping such a wrong behaviour in the same way he/she stopped sucking from his/her mother’s breasts.’

This proverb teaches people to stop doing bad things in the society because they hurt others. That is why they tell wrong doers to stop their evil deeds in order not to harm the society.

Colossians 3: 5.

332. NG’HULU JAWIZA, JIGALAJA MBITI HA NYANGO

Imbuki ya lusumo lunulo yingilile kuli nigini na nina. Unigini ng’wunuyo olatogilwe kulila ahikanza lya b’ujiku. Lushugu lumo, unina agankanga unigini giki, ‘ululamane ulila naguguponya hanze uliwe mbili.’ Ahikanza linilo aliyomba, imbiti nayo yalihoyi aha nyango. Naigwa imihayo yiniyo. Kuyiniyo lulu, imbiti yiniyo yaduka yalindilaga giki iguponegejiwa akana ize ikalye, nose ub’ujiku wela. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki ng’hulu jawiza, jigalaja mbiti hanyango.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agalindilaga gupandika sabho, nulu jiliwa, bho gwikuga, giki munhu agujigwisha, bho nduhu ugutumama  nimo gose gose. Umunhu ng’wunuyo adulile nulu gucha na nzala, guti ni mbiti yiniyo iyo igelewa b’ujiku, kunguno bhuli ng’wene adatogilwe uguponya sabho jakwe. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘ng’hulu jawiza jigalaga mbiti hanyango.

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya gutumama milimo ya gubhapandikila sabho, bho nduhu gulindila ja guponyiwa na bhangi, kugiki abhoyi bhajikuge.

KISWAHILI: HABARI NZURI ILIMLAZA FISI MLANGONI

Chanzo cha methali hiyo chatokea kwa mtoto na mama yake. Mtoto huo alipenda kulia wakati wa usiku. Siku moja mama yake alimtisha mtoto huyo, kwa kumwambia hivi, ‘ukiwa unalia nitakutupa nje uliwe na fisi.’ Wakati mama huyo akiongea hivyo, fisi naye alikuwepo mlangoni. Akayasikia maneno hayo. Kwa hiyo, fisi huyo alibaki amesubiri kwamba atatupiwa mtoto aje amle, mwishowe usiku ukapambazuka. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘habari nzuri ilimlaza fisi mlangoni.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu yule asubiriye kupata mali au chakula kwa kuokota, kwamba mmoja atadondosha, bila kufanya kazi yoyote. Mtu huyo huweza hata kufa kwa njaa, kama yule fisi aliyepambazukiwa usiku, kwa sababu kila mtu hapendi kutupa mali zake, au kupoteza. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘habari nzuri ilimlaza fisi mlangoni.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kufanya kazi mbalimbali ziwezazo kuwapatia mahitaji yao yakiwemo yale ya chakula, badala ya kusubiri kuokota au wengine wapoteze, ili wao waweze kuokota.

hyena

mother

ENGLISH: GOOD NEWS MADE A HYENA SLEEP AT THE DOOR

The source of this proverb is a child who used to cry at night. One day the mother of the child threatened to hrow out the child to be eaten by hyena. The hyena was around the door when the mother was threatening the child. Hearing the mother’s threat, the hyena hid itself near the door waiting for the meat. It waited the whole night with no success. That is why people say, ‘good news made a hyena sleep at the door.’

The proverb is likened to lazy people, who dream to have possessions or abundant food without struggling for them. They just wait with hope that someone will drop possessions for them to pick. Such people are likely to starve to death.

The proverb teaches people to work hard so as to be self sufficient in different sorts of life, including food and other necessities.