sayings

1553. SUKUMA: UYU ALI NTEMI O MAKOYE.

Akahayile kenako kingila kuli ntemi uyo wikalaga musi ya Tanzania. Untemi ng’wunuyo oliadabhadegelekaga abhanhu bhakwe chiza kunguno ya gwicholela solobho yakwe weyi yiyene. Uweyi obhenhelaga makoye mingi abhanhu bhakwe umuwikaji bhobho. Hunagwene bhagayomba giki, “uyu ali ntemi o makoye.”

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo alinawiyumilija bho gukinda bhudamu wingi umuwikaji bhokwe bhunubho. Umunhu ng’wunuyo, agatumamaga milimo midamu mingi mpaka oyimala chiza kunguno ya wiyumilija bhokwe bhunubho umukikalile kakwe kenako. Uweyi agadujaga uguyutongela chiza ikaya yakwe kunguno ya wiyumililaja bhokwe bhunubho umuwikaji bhokwe bhunubho.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nabho bhagiyumilija aho bhabhitilaga mumakoye ga gwingila kuli ntemi obho, kunguno nuweyi agiyumililjaga gutumama milimo midamu mpaka oyimala na gupandika sabho jagudula gutumamila uguyitongela chiza ikaya yakwe. Hunagwene agalitanaga ilikoye ilitale giki, “uyu ali ntemi o makoye.”

Akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya gubhiza na wiyumilija bho gwigulambija gutumama milimo yabho chiza, kugiki bhadule kupandika sabho ja gutumamila na mbango ja kujilela chiza ikaya jabho jinijo, umuwikaji bhobho bhunubho.

Ayubu 1:20–22.

Zaburi 46:1–2.

Isaya 41:10.

Mathayo 11:28.

Wafilipi 4:13.

Warumi 8:28.

SWAHILI: HUYU NI MFALME OF MATATIZO.

Msemo huu unatokana na mfalme aliyeishi mahali fulani nchini Tanzania. Mfalme huyu hakuweza kuwasikiliza watu wake vizuri kwa sababu ya maslahi yake binafsi. Mtu huyo alisababisha watu wake kupata matatizo maishani mwao. Ndiyo maana watu hao walisema kwamba, “Huyu ni mfalme wa matatizo.”

Msemo huu hulinganishwa kwa mtu anayekabiliwa na hali ngumu sana inayohitaji ujasiri mkubwa, hekima, uvumilivu, na azimio la kushinda maishani. Mtu huyu hupitia changamoto kadhaa kwa wakati mmoja, hasa wakati tatizo moja linapokuwa mzigo mkubwa zaidi miongoni mwa mengine yote kwa sababu ya uvumilivu wake huo maishani mwake. Yeye huweza kuwaongoza wanafamilia wake vizuri kwa sababu ya ujasiri na uvumilivu wake huo maishani mwake.

Mtu huyu hufanana na wale waliopitia matatizo kutoka kwa mfalme wao, kwa sababu naye pia hupitia kipindi kigumu sana maishani lakini hukataa kukata tamaa maishani mwake. Mtu kama huyo hutafuta ushauri, huomba kwa Mungu, hufikiri kwa makini, na huchukua hatua zinazofaa kushinda tatizo maishani. Ndiyo maana huiita changamoto kubwa kwa kusema “Huyu ni mfalme wa matatizo.”

Msemo huu huwafundisha watu kwamba: Baadhi ya matatizo ni makubwa kuliko mengine, na yanahitaji umakini na hekima zaidi. Matatizo magumu hayapaswi kutufanya tupoteze tumaini. Uvumilivu ni muhimu tunapokabiliwa na changamoto kubwa. Watu wanapaswa kutafuta ushauri wa busara wakati tatizo linakuwa gumu sana kulishughulikia peke yao. Sala na kumtumaini Mungu ni muhimu wakati wa shida. Kila tatizo linapaswa kushughulikiwa kwa uangalifu na kwa busara, badala ya kupitia hofu au kukata tamaa. Matatizo yanaweza kuimarisha tabia ya mtu anayeyakabiri kwa ujasiri na imani.

Kwa hiyo, msemo huu huwahimiza watu kutoshindwa na “mfalme wa matatizo.” Hata ugumu mkubwa zaidi unaweza kushughulikiwa kwa imani, hekima, uvumilivu, na azimio.

Ayubu 1:20–22. Majaribu Makuu ya Ayubu. Ayubu alipoteza mali zake, watoto wake, na afya yake. Mateso yake yalikuwa makubwa, lakini aliendelea kumtambua Mungu. Hadithi yake inafundisha kwamba hata matatizo makubwa sana hayapaswi kuharibu imani yetu.

Zaburi 46:1–2. “Mungu ndiye kimbilio letu na nguvu zetu, msaada wetu wa milele wakati wa shida.” Kifungu hiki kinafundisha kwamba matatizo yanapozidi, Mungu hubaki kuwa chanzo cha nguvu na ulinzi.

Isaya 41:10. “Msiogope, kwa maana mimi nipo pamoja nanyi; msifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wenu.” Mstari huu unawakumbusha watu kwamba hawapaswi kukabiliana na magumu makubwa peke yao kwa sababu Mungu yuko pamoja nao.

Mathayo 11:28. “Njooni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.” Yesu anawaalika watu wanaobeba mizigo mizito waje kwake kwa ajili ya faraja na nguvu.

Wafilipi 4:13. “Nayaweza yote katika Kristo anitiaye nguvu.” Hii inafundisha kwamba nguvu za Mungu zinaweza kumsaidia mtu kukabiliana na hali zinazoonekana kuwa ngumu.

Warumi 8:28. “Nasi tunajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi kwa manufaa ya wale wampendao.” Hii inatoa tumaini kwamba hata uzoefu wenye uchungu na mgumu hatimaye unaweza kuchangia kusudi la Mungu.

Msemo “Huyu ni mfalme wa matatizo” unatukumbusha kwamba baadhi ya changamoto zinaweza kuonekana kuwa kubwa kuliko uwezo wetu wa kibinadamu wa kuzitatua. Hata hivyo, watu hawapaswi kujisalimisha kwa hofu au kukata tamaa. Wanapaswa kutafuta hekima, kubaki wavumilivu, kusaidiana, kuomba, na kumwekea Mungu tumaini lao.

Tatizo kubwa zaidi si mwisho wa safari kila wakati; kwa imani, hekima, ujasiri, na uvumilivu, tatizo gumu linaweza kuwa fursa ya kukua na ushuhuda wa uaminifu wa Mungu.

 

ENGLISH: THIS IS A KING OF PROBLEMS

This saying originates from a king who lived some where in Tanzania. This king could not listen to his people because of his personal interest. He caused his people to face a number of problems in their lives. That is why they said, “This is a king of problems.”

This saying is compared to a person who faces an extremely difficult situation that requires great courage, wisdom, patience, and determination to overcome in life. This person undures a number of challenges at the same time, especially when one particular problem becomes the greatest burden among all the others because of his patience in life. He managed to run well his family members because of his courage and pacience in life.

This person resembles those who indured a number of problems from their king, because he also passes through a very difficult period in life but refuses to give up in life. Such a person seeks advice, prays to God, thinks carefully, and takes appropriate steps to overcome the problem in life. That is why he names challence by saying “This is a king of problems.”

This saying teaches people that: Some problems are greater than others, and they require greater attention and wisdom. Difficult problems should not make us lose hope. Patience and perseverance are important when facing serious challenges. People should seek wise counsel when a problem becomes too difficult to handle alone. Prayer and trust in God are essential during times of trouble. Every problem should be approached carefully and wisely, rather than through fear or despair. Difficulties can strengthen a person’s character when they are faced with courage and faith.

This saying therefore encourages people not to be defeated by a “king of problems.” Even the greatest difficulty can be approached with faith, wisdom, patience, and determination.

Job 1:20–22. Job’s Great Trials. Job lost his possessions, his children, and his health. His suffering was enormous, yet he continued to acknowledge God. His story teaches that even very serious problems should not destroy our faith.

Psalm 46:1–2. “God is our refuge and strength, an ever-present help in trouble.” This passage teaches that when problems become overwhelming, God remains a source of strength and protection.

Isaiah 41:10. “Do not fear, for I am with you; do not be dismayed, for I am your God.” The verse reminds people that they do not have to face great difficulties alone because God is with them.

Matthew 11:28. “Come to me, all you who are weary and burdened, and I will give you rest.” Jesus invites people who carry heavy burdens to come to Him for comfort and strength.

Philippians 4:13. “I can do all things through Christ who strengthens me.” This teaches that God’s strength can help a person face circumstances that appear impossible.

Romans 8:28. “And we know that in all things God works for the good of those who love him.” This gives hope that even painful and difficult experiences can ultimately contribute to God’s purpose.

The saying “This is a king of problems reminds us that some challenges may appear greater than our human ability to solve them. However, people should not surrender to fear or despair. They should seek wisdom, remain patient, support one another, pray, and place their trust in God.

The greatest problem is not always the end of the journey; with faith, wisdom, courage, and perseverance, a difficult problem can become an opportunity for growth and a testimony of God’s faithfulness.

1552. SUKUMA: UYU OMALAGA AMAWE.

Akahayile kenako kufamilile kukikajile kajiafrika umo amawe gatumamilagwa bho kuzengela numba, gutuula mbimbi na kushera bhusu. Ugukuminga mawe ga gukoma guzengela numba jadakilagwa nguzu na wiyumilija kunguno ya kusola liwe limo limo. Umunhu uyo omalaga mawe yolechaga giki, otumamaga nimo ndamu ugogugakuminga amawe genayo agagudula guzengela numba. Hunagwene abhanhu bhagayomba giki, “uyu omalaga amawe.”

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agigulambijaga kutumama milimo yakwe mpaga oyimala chiza, umuwikaji bhokwe bhunubho. Umunhu ng’wunuyo, agatumila uwasa na pye ijo alinajo bho gubhushigila ubhulingisilo bhokwe kunguno ya wigulambija bhokwe bhunubho umukikalile kakwe kenako. Uweyi agapandika sabho ningi noyi aha kaya yakwe yiniyo kunguno ya wigulambija bhokwe bhunubho ubho guyitumama mpaka uyimala chiza imilimo yakwe yiniyo, umuwikaji bhokwe bhunubho.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo agakuminga mawe ga gudula guzengela numba, kunguno nuweyi agigulambijaga gutumama milimo yakwe chiza mpaga opandika sabho ningi aha kaya yakwe yiniyo, umuwikaji bhokwe bhunubho. Hunagwene abhanhu bhaganyombaga giki, “uyu omalaga amawe.”

Akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya gubhiza na wigulambija bho gwiyumilija guitumama chiza imilimo yabho yiniyo, kugiki bhadule kupandika sabho ningi, umukaya jabho jinijo.

Yohana 19:30.

2 Timotheo 4:7.

Wagalatia 6:9.

Waebrania 12:1.

 

SWAHILI: HUYU AMEMALIZA MAWE.

Msemo huu unatokana na jamii za kitamaduni za Kiafrika ambapo mawe yalitumika sana kwa ajili ya kujenga nyumba, uzio, mahali pa moto, kusaga nafaka, na kuweka mipaka. Kukusanya mawe ya kutosha kulihitaji, nguvu, na uvumilivu kwa sababu ilibidi yakusanywe moja baada ya jingine. Mtu alipokuwa “amemaliza mawe,” ilimaanisha kwamba kazi ngumu ya kukusanya au kutumia mawe yote yaliyopatikana ilikuwa imekamilika. Ndiyo maana watu walisema kwamba, “huyu amemaliza mawe.”

Msemo huu hulinganishwa kwa mtu yule ambaye anabidii ya kufanya kila linalowezekana kukamilisha kazi, bila kuacha chochote kisichofanywa maishani mwake. Mtu huyu hutumia fursa, na rasilimali zote zilizopo katika kukamilisha lengo lake kwa sababu ya bidii yake hiyo maishani mwake. Yeye hufanikiwa sana katika familia yake kwa sababu ya kufanya kazi kwa bidii ya kutosha kuzikamilisha vizuri kazi zake maishani mwake.

Mtu huyu hufanana na yule aliyemaliza mawe yote ambayo alikuwa yakiyakusanya kwa ajili ya ujenzi wake kwa sababu naye pia hufanya kazi kwa bidii hadi zinakamilika, hakati tamaa licha ya magumu anayokumbana naye maishani mwake. Ndiyo maana watu husema kwamba, ” huyu amemaliza mawe.”

Msemo huu huwafundisha watu kuhusu: Uvumilivu na azimio katika kukamilisha majukumu ya mtu. Umuhimu wa kutumia rasilimali zilizopo kwa busara. Kujitolea kukamilisha kile ambacho mtu amekianza. Kutambua kwamba kila juhudi ina mipaka yake na kwamba uvumilivu mara nyingi huleta mafanikio maishani. Kuthamini kufanya kazi kwa bidii katika kuyafikia malengo maishani.

Yohana 19:30. “Imekwisha.” Yesu alikamilisha kazi ya wokovu ambayo Baba alikuwa amempa.

2 Timotheo 4:7. “Nimepigana vita vizuri, nimemaliza mbio, nimeilinda imani.” Paulo anazungumzia kukamilisha utume wa maisha yake kwa uaminifu.

Mhubiri 7:8. “Mwisho wa jambo ni bora kuliko mwanzo wake, na uvumilivu ni bora kuliko kiburi.” Kumaliza vizuri ni bora kuliko kuanza tu.

Wagalatia 6:9. “Tusichoke katika kutenda mema, maana kwa wakati unaofaa tutavuna mavuno tusipokata tamaa.” Uvumilivu huleta thawabu yake.

Waebrania 12:1. “Na tupige mbio kwa uvumilivu katika mashindano yaliyowekwa kwa ajili yetu.” Waumini wanahimizwa kuvumilia hadi watakapokamilisha wito wao.

Kwa hiyo msemo huu “huyu amemaliza mawe” unaashiria mtu ambaye amechoka kila juhudi, amekamilisha kazi ngumu, au ametimiza wajibu muhimu kwa uaminifu. Unahimiza uvumilivu, bidii, na azimio la kumaliza kile ambacho mtu amekianza.

 

ENGLISH: HE HAS FINISHED THE STONES.

This saying originates from traditional African communities where stones were commonly used for building houses, fences, fireplaces, grinding grain, and marking boundaries. Gathering enough stones required patience, strength, and perseverance because they had to be collected one by one. When someone had “finished the stones,” it meant that the difficult task of collecting or using all the available stones had been completed. That is why people speak about him, “he has finished the stones.”

This saying is compared to a person who has done everything possible to accomplish a task, leaving nothing undone in his life. This person exhausts all available opportunities, resources, or solutions in pursuing a goal because of his hardworking in life. He becomes successful in his family because of working hard enough to exhaust all available opportunities in life.

This person resembles the one who finished all the stones which was collecting because he also works diligently until the work is finished, never giving up despite hardships in his life. That is why people speak about him, “he has finished the stones.”

This saying teaches people about: Perseverance and determination in completing one’s responsibilities. The importance of using available resources wisely. Commitment to finishing what one has started. Recognizing that every effort has its limits and that perseverance often leads to achievement. Appreciating hard working in life.

John 19:30. “It is finished.” Jesus completed the work of salvation that the Father had given Him.

2Timothy 4:7. “I have fought the good fight, I have finished the race, I have kept the faith.” Paul speaks of faithfully completing his life’s mission.

Ecclesiastes 7:8. “The end of a matter is better than its beginning, and patience is better than pride.” Finishing well is better than merely starting.

Galatians 6:9. “Let us not grow weary in doing good, for at the proper time we will reap a harvest if we do not give up.” Perseverance brings its reward.

Hebrews 12:1. “Let us run with perseverance the race marked out for us.” Believers are encouraged to endure until they complete their calling.

Therefore this saying “He has finished the stones” symbolizes a person who has exhausted every effort, completed a demanding task, or faithfully brought an important responsibility to its conclusion. It encourages perseverance, diligence, and the determination to finish what one has begun.

1523. SUKUMA: B’ALINIKANDIJA.

Imbuki ya kahayile kenako yandija kuli munhu uyo wikalaga muchalo ja Ng’watuju. Umunhu ng’wunuyo, witaga mihayo yawiza kunguno ya nhungwa jakwe ijawiza jinijo umuwikaji bhokwe. Aliyo lulu, abhanhu bhanhayaga shibhi kunguno ya wilu bhobho bhunubho. Hunagwene agayomba giki, “b’alinikandija.”

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo alinikujo lya witegeleja bho gwiyumilija ulu bhalindukila abhiye umuwikaji bhokwe bhunubho. Umunhu ung’wunuyo, bhaganhaga shibi na gunkolya abhangi kunguno ya wilu na bhudaki bhobho. Uweyi agiyumilija umumihayo yiniyo mpaga odula guyilela chiza ikaya yakwe yiniyo, kunguno ya likujo na witegeleja bhokwe bhunubho umukikalile kakwe kenako.

Umunhu ng’wununyo agikolaga nuyo agiyumilija aho oyombagwa shib’i na bhiye, kunguno nuweyi agiyumilijaga ulu alidalahwa na gusigwa na bhiye mpaga odula guyilela chiza ikaya yakwe yiniyo, umuwikaji bhokwe bhunubho. Hunagwene agayombaga giki, “b’alinikandija.”

Akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya gubhiza ni kujo lya witegeleja bho gwiyumilija ulu bhaliyombwa shibhi na bhichabho, kugiki bhadule gujilela chiza ikaya jabho jiniyo, umuwikaji bhobho bhunubho.

Akahayile kenako kalibhizukija abhanhu giki imihayo imibhi igaminyaga ng’holo ja bhanhu, gashinaga lulu, yigelelilwe bhajitumile indemi jabho bho gubhalela chiza abhichabho, umukikalile kabho kenako.

Zaburi 34 34:13.

Mithali 16:28.

Mathayo 5:11.

Waefeso 4:29.

SWAHILI: WANANIBEZA.

Asili ya msemo huu inaweza kufuatiliwa hadi kwa mtu aliyeishi katika kijiji cha Mwatuju. Mtu huyo aliwatendea wengine mema kwa sababu ya mwenendo wake mzuri maishani mwake. Hata hivyo, watu walimsema vibaya kwa sababu ya wivu wao. Ndiyo maana alisema “wananibeza.”

Msemo huu hulinganishwa kwa mtu mwenye hekima nzuri ya kubaki mvumilivu wakati wengine wakimtukana maishani mwake. Mtu huyu hushutumiwa kwa uwongo, hukosolewa, au hunenwa vibaya na wengine kwa sababu ya wivu, chuki, au kutoelewana. Hata wakati hajafanya kosa lolote, watu huendelea kueneza maneno mabaya juu yake. Hata hivyo, yeye huweza kuwalea vyema wanafamilia wake kwa sababu ya hekima yake hiyo nzuri ya kubaki mvumilivu anapokabiliwa na matatizo katika maisha yake hayo ya kila siku.

Mtu huyo hufanana na yule aliyebaki mvumilivu na mtulivu wakati wengine wakimtukana, kumdhihaki, au kumsengenya, kwa sababu naye pia huchagua hekima na tabia njema ya kubaki mvumilivu badala ya kulipiza kisasi anapotendewa ubaya na wengine maishani mwake. Ndiyo maana yeye husema kwamba “wananibeza.”

Msemo huo huwafundisha watu kuhusu: kuepuka umbea na maneno maovu, kuheshimu hadhi ya wengine, kuwa wavumilivu wanapokabiliwa na ukosoaji, kusema ukweli na wema, pamoja na kuelewa kwamba watu wema wakati mwingine huchukiwa bila sababu.

Msemo huo huwakumbusha watu kwamba maneno yanaweza kuumiza mioyo, na watu wanapaswa kutumia ndimi zao kwa kujenga amani badala ya kuharibu mahusiano.

Zaburi 34 34:13, “Uzuie ulimi wako na uovu na midomo yako isiseme uongo.”

Mithali 16:28, “Msengenyaji hutenganisha marafiki wa karibu.”

Mathayo 5:11, “Heri ninyi watu watakapowatukana na kuwanenea kila aina ya uovu kwa ajili yangu.”

Waefeso 4:29, “Msiruhusu maneno yoyote mabaya yatoke vinywani mwenu, bali yale tu yafaayo kwa kuwajenga wengine.”

ENGLISH: THEY TALK BADLY ABOUT ME.

The original of this saying can be traced back to a person who lived in Mwatuju village. This person did good deeds to others because of his sound conduct in his life. However, people spoke against him because of their jealousy. That is why he says “they talk badly about me.”

This saying is equated to a person who has decent wisdom of remaining patient while others insult him in his life. This person is falsely accused, criticized, or spoken against by others because of jealousy, hatred, or misunderstanding. Even when he has done nothing wrong, people continue spreading negative words about him. He however, managed to nurture well his family members because of his decent wisdom of remaining patient while facing difficulties in his daily lives.

This person resembles the one who remained patient and calm while others insulted, mocked, or gossiped about him behind his back because he also chooses wisdom and good character of remaining patient instead of revenge in his life. That is why he says “they talk badly about me.”

This saying teaches people about: avoiding gossip and evil speech, respecting the dignity of others, being patient when facing criticism, speaking truthfully and kindly, as well as understanding that good people are sometimes hated without reason.

This saying reminds people that words can wound the heart, and therefore people should use their tongues to build peace instead of destroying relationships.

Psalm 34 34:13, “Keep your tongue from evil and your lips from telling lies.”

Proverbs 16:28, “A gossip separates close friends.”

Matthew 5:11, “Blessed are you when people insult you and falsely say all kinds of evil against you because of me.”

Ephesians 4:29, “Do not let any harmful talk come out of your mouths, but only what is helpful for building others up.”

 

 

 

1522. UYUJA NANG’HO GUJUPUNGUGIJIWA KUGIKI UYUTOB’ELA GODI YA GUGWINHA IKUJO.

Imbuki ya kahayile kenako ilolile ikanza lya bhukoloni. Ahikanza linilo ulu giki munhu alina ng’ombe ningi japungujiyagwa jasaga ngehu. Giko lulu ulu giki munhu adina ng’ombe ogabhilagwa inguno hayo nuweyi abhize nsabhi oguyutob’ela godi ya gung’wenhela ikujo lya gusab’a ng’ombe. Hunagwene umunhu nsabhi owilagwa giki, “uyuja nang’ho gujupungugijiwa kugiki uyutob’ela godi ya gugwinha ikujo.”

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu nsabhi uyo alina witegeleja bho gwicholela sabho na kujitumila bho wizanholo chiza umuwikaji bhokwe bhunubho. Umunhu ng’wunuyo agigulambijaga gutumama milimo yakwe chiza mpaka opandika sabho ja gudula gubhambilija bhanhu bhingi kunguno ya witegeleja bhokwe bhunubho umukikalile kakwe. Uweyi agadujaga gwambililja bhanhu bhingi umuchalo jakwe kunguno ya witegeleja bho gutumama milimo yakwe mpaga opandika sabho jagugunana bhiye umuwikaji bhokwe bhunubho.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nu nsabhi o ng’ombe uyo agabhambilija bhiye mpaga nabho bhusabha kunguno nuweyi agabhutumilaga ubhusabhi bhokwe bho gubhambilija bhiye umuwikaji bhokwe bhunubho. Hunagwene agabhawilaga abhiye bhenabho bhuli ng’wene giki, “uyuja nang’ho gujupungugijiwa kugiki uyutob’ela godi ya gugwinha ikujo.”

Akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya gubhiza na wigeteleja bho gwicholela sabho na gujitumamila bho gubhambilija bhichabho chiza, kugiki bhadule gujibheja chiza ikaya jabho jinijo, umuwikaji bhobho bhunubho.

2Wakorintho 9:8-9.

Yoshua 14:4.

Marko 12:44.

KISWAHILI: UWE UNAENDA NA WEWE KUPUNZIWA ILI UWE UNATOZWA KODI UPATE RIDHIKI.

Chanzo cha msemo huo huangalia kipindi cha ukoloni. Kipindi hicho, kilintaka mtu aliyekuwa na ng’ombe kuwapeleka ng’ombe wake kwa kiongozi ili wakapunguzwe na kubhaki nao wachache. Hivyo basi, mtu yule ambaye hukuwa na ng’ombe aligawiwa ili naye aweze kuwa tajiri wa kulipa kodi ya kumpatia heshima. Ndiyo maana mtu aliyekuwa na ng’ombe aliambiwa kwamba, “uwe unaenda na wewe kupunguziwa ili uwe unatozwa kodi ya kukupatia heshima.”

Msemo huo, hulinganiswa kwa mtu tajiri mwenye umakini wa kutafuta mali na kuzitumia kwa ukarimu wa kumpatia heshima maishani mwake. Mtu huyo hujibidisha kufanya kazi zake vizuri mpaka anapata mali za kumwezesha kusaidia watu wengi kwa sababu ya umakini na ukarimu wake huo katika maisha yake hayo. Yeye hufanikiwa kuwasaidia watu wengi katika kijiji chake kwa sababu ya umakini na ukarimu wake huo katika maisha yake hayo.

Mtu huyo, hufanana na yule tajiri wa ng’ombe aliyewasaidia wenzake mpaka nao wakatajirika, kwa sababu naye pia huutumia utajiri wake kwa kuwasaidia wenzake maishani mwake. Ndiyo maana yeye humwambia kila mmoja wao kwamba, “uwe unaenda na wewe kupunguziwa ili uwe unatozwa kodi ya kukupatia heshima.”

Msemo huo, huwafundisha watu juu ya kuwa na umakini wa kujitafutia mali za kuwawezesha kutumia katika kuwasaidia wenzao vizuri, ili waweze kuzilea vyema familia zao, maishani mwao.

2Wakorintho 9:8-9.

Yoshua 14:4.

Marko 12:44.

ENGLISH: YOU SHOULD ALLOW YOUR WEALTH TO BE REDUCED SO THAT YOU MAY PAY THE TAX OF RESPECT.

The origin of this saying dates back to the colonial period. During that time, people who owned many cattle were required to surrender some of their cows to local leaders so that the wealth could be shared with those who had none. In this way, poorer people could also own cattle, become economically stable, and be able to contribute taxes that earned them dignity and respect within society. Because of this practice, wealthy people were advised that, “You should allow your wealth to be reduced so that you may pay the tax of respect.”

This saying is used to describe a wealthy person who works hard to gain riches and then uses those riches generously for the benefit of others. Such a person understands that true respect does not come merely from possessing wealth, but from using it wisely and compassionately to help fellow human beings. Through seriousness, hard work, and generosity, that person succeeds in supporting many people within the community.

This person resembles a rich man who helped his companions until they also became prosperous, because he used his wealth to uplift others in his life. That is why he encourages people by saying, “you should allow your wealth to be reduced so that you may pay the tax of respect.”

This saying teaches people to work seriously in search of wealth so that they may use it to help others, support their families, and improve the well-being of their communities.

Second Epistle to the Corinthians 9:8–9.

Book of Joshua 14:4.

Gospel of Mark 12:44.

 

 

 

 

1520. SUKUMA: B’IZAGA NA SUNGE YA NG’HANA.

Imbuki ya kahayile kenako ifumilile kukikalile kabhasuguma. Abhanhu bhenabho bhabhuchaga sunge ya jiliwa guti mandege, busiga nulu jiliwa jingi ulubhajile ku nimo guti go winga bho bhazenganwa bhabho. Hunagwene bhagiwilaga bhuli ng’wene giki, “b’izaga na sunge ya ng’hana.”

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agayegaga nijo alinajo na adikalaga na wiminholo umuwikaji bhokwe bhunubho. Umunhu guti ng’wunuyo, agalonjaga mbango, bho gutumama milimo yakwe bho bhutungilija na wizanholo kunguno ya nhungwa jakwe ijawiza jinijo, umuwikaji bhokwe bhunubho. Uweyi agabhalelaga chiza abhanhu bha ha kaya yakwe yiniyo kunguno ya bhutungilija bhokwe bhunubho, umukikalile kakwe kenako.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga na bhasuguma abho bhagachala sunge ukuwinga bho mazenganwa bhabho, kunguno nuweyi agabhalelaga chiza abhanhu bha ha kaya yakwe mpaka bhakula chiza, umuwikaji bhokwe bhunubho. Hunagwene agang’wilaga bhuli ng’wene giki, “b’izaga na sunge ya ng’hana.”

Akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya gubhiza na bhutungilija bho guyega na ginhu ijo bhalinajo, na kutumama milimo yabho bho wizanholo na widohya, kugiki bhadule kujilela chiza ikaya jabho umuwikaji bhobho bhunubho.

Wafilipi 4:11–12.

1 Timotheo 6:6.

Waebrania 13:5.

Mithali 15:16.

SWAHILI: UWE NA ZAWADI YA KURIDHISHA.

Asili ya msemo huo inaweza kufuatiliwa hadi kwenye maisha ya kitamaduni ya wasukuma. Watu hawa hubeba chakula kwenye ndoo zao wanapoenda kwenye sherehe za majirani zao zikiwemo zile za harusi kama michango yao kwenye sherehe hizo. Ndiyo maana wao huambiana kwamba “uwe na zawadi ya kuridhisha.”

Msemo huo hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huridhika na kile alicho nacho na haishi na uchoyo au wivu usioisha maishani mwake. Mtu kama huyo huthamini baraka, hufanya kazi kwa uaminifu, na huepuka malalamiko yasiyo ya lazima kwa sababu ya tabia yake hizo njema maishani mwake. Yeye huwalea vyema wanafamilia wake kwa sababu ya uaminifu wake huo katika maisha yake ya kila siku.

Mtu huyo hufanana na wale wasukuma waliotuma zawadi nzuri kwenye harusi za majirani zao kwa sababu naye pia huwalea vyema wanafamilia wake kama zawadi yake kwao, maishani mwake. Ndiyo maana huwafundisha kwa kusema “uwe na zawadi ya kuridhisha.”

Msemo huo huwafundisha watu kuhusu kuridhika, kuwa na shukrani, unyenyekevu, na amani ya moyo. Unawakumbusha kwamba kuridhika huleta furaha, huku uchoyo mara nyingi ukileta migogoro, wivu, na huzuni. Mtu mwenye shukrani huthamini baraka za Mungu na anaheshimu ustawi wa wengine.

Wafilipi 4:11–12. “Nimejifunza kuridhika katika hali yoyote.”

1 Timotheo 6:6. “Utauwa pamoja na kuridhika ni faida kubwa.”

Waebrania 13:5. “Ridhika na ulicho nacho.”

Mithali 15:16. “Afadhali kuwa na kidogo pamoja na kumcha Bwana, kuliko kuwa na mali nyingi pamoja na masumbufu.”

ENGLISH: HAVE A GIFT OF SATISFACTION.

The origin of this saying can be traced back to the traditional life of the Sukuma people. These people carry food in their bucket while going to their ceremonies like weddings of their neighbors as their contributions to such party. That is why they encourage one another by saying “have a gift of satisfaction.”

This saying is compared to a person who is content with what he or she has and does not live with endless greed or jealousy in life. Such a person appreciates blessings, works honestly, and avoids unnecessary complaints because of his sound behavior in life. He nicely nurtures his family members because of his being honest in his daily life.

This person resembles those who sent nice gifts to the weddings of their neighbors because of he also nurtures well his family members in his life. That is why he encourage them by saying “have a gift of satisfaction.”

This saying teaches people about contentment, gratitude, humility, and peace of heart. It reminds them that satisfaction brings happiness, while greed often brings conflict, envy, and sorrow. A thankful person values God’s blessings and respects the welfare of others.

Philippians 4:11–12. “I have learned to be content whatever the circumstances.”

1 Timothy 6:6. “Godliness with contentment is great gain.”

Hebrews 13:5. “Be content with what you have.”

Proverbs 15:16. “Better a little with the fear of the Lord than great wealth with turmoil.”