Sukuma Proverbs

1253. UDIZUKILILA AHA JAZWILA NOGE UGUNWELA.

Olihoyo munhu uyo ohadikijaga gukila mongo uyo galigonyama. Umunhu ng’wunuyo, ohadikijaga gugukilila umongo gunuyo, aha jazwila noge, kunguno ya bhujidigwa bhokwe bhunubho. Hunagwene abhanhu bhagang’wila giki, “udizukilila aha jazwila noge ugunwela.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agahadikilaga gwita mihayo ya bhubhi umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agitaga mihayo iyo idulile gung’wenhela makoye umubhutumami bhokwe kunguno ya bhujidigwa bhokwe bhunubho. Uweyi agapandikaga makoye ga guduma uguilela chiza ikaya yakwe kunguno ya bhujidigwa bhokwe bhunubho, umuwikaji bhokwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo agahadikija gugukilila mongo aha shimu, kunguno nuweyi agahadikijaga gwita mihayo iyo idulile gung’wenhela makoye umuwikaji bhokwe bhunubho. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “udizukilila aha jazwila noge ugunwela.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya guzunya guhang’wa na bhichabho ulu bhahubhaga, kugiki bhadule gujilabhila chiza ikaya jabho jinijo, umuwikaji bhobho.

1Samweli 12:20-21.

2Wafalme 17:13.

Mwanzo 3:1-19.

Mwanzo 19:15-26.

KISWAHILI: USIVUKIE PALE ZILIPOVUJIA DAMU PUANI UTAZAMA.

Alikuwepo mtu aliyelazimisha kuvuka mtu uliokuwa umemzuia. Mtu huyo, alilazimisha kuvukia pale zilipovujia damu puani, maana yake penye kina kirefu, kwa sababu ya kutokukubali kuonywa kwake na wenzake. Ndiyo maana watu walimwambia kwamba, “usivukie pale zilipovujia damu puani utazama.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hulazimisha kufanya mambo yanayoweza kumletea matatizo, katika maisha yake. Mtu huyo, hufanya mambo yawezayo kumletea matatizo katika utekelezaji wa kazi zake kwa sababu ya ugumu wake wa kukubali kushauriwa na wenzake, maishani mwake. Yeye hupata matatizo ya kushindwa kuilea vizuri familia yake hiyo, kwa sababu ya ugumu wake huo wa kupokea ushauri wa wenzake, katika maisha yake.

Mtu huyo, hufanana na yule aliyelazimisha kuvukia mto penye kina kirefu, kwa sababu naye hufanya mambo yawezayo kumletea matatizo katika maisha yake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “usivukie pale zilipovujia damu puani utazama.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kukubali kushauriwa na wenzao wanapokosea katika utekelezaji wa majukumu yao, ili waweze kuzitunza vizuri familia zao, maishani mwao.

1Samweli 12:20-21.

2Wafalme 17:13.

1252. DAGELANILILE BHOSE HALUZOGA LWA MINZI.

Imbuki ya lusumo lunulo ihoyelile higulya ya bhushigani bho nigini hikanza lya gulya jiliwa. Unigini ulu obyalwa agatumilaga mabhele kunguno agabhizaga adina mino agagudula gulya jiliwa. Giko lulu, uluguzwa amino gakwe agandyaga ugulya ijiliwa kihamo na bhanhu abhatale. Agisangijaga mligele lya bhanhu bhatale. Hunagwene abhanhu bhenabho, bhagayombaga giki, “dagelanilile bhose hauzoga lwa minzi.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhali na ng’wigwano go gubhakalibhusha abhichabho abho bhashiganile gwingila muluganda lobho, umukikalile kabho. Abhanhu bhenabho, bhagisumbyaga bhabhakalibhusha abhichabho abho bhashiganile ugwingila umuluganda lobho lunulo, kunguno ya ng’wigwano gobho ugogutumama milimo kihamo chiniko, umuwikaji bhobho. Abhoyi bhagapandikaga matwajo mingi umukaya jabho kunguno ya ng’wigwano gobho gunuyo ugogutumama milimo yabho kihamo umukikalile kabho kenako.

Abhanhu bhenabho bhagikolaga nabho bhagankalibhusha nigini gulya kihamo nabho aho gazwa amino gakwe, kunguno nabhoyi bhagabhakalibhushaga umuluganda lobho abhichabho abho bhashikanile ugwingila moyi, umuwikaji bhobho. Hunagwene bhagayombaga giki, “dagelanilile bhose hauzoga lwa minzi.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na ng’wigwano go gwikalibhusha kutumama milimo yabho kihamo, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi umukaya jabho jinijo.

Kutoka 2:16-19.

2Wafalme 9:17.

Ayubu 21:11.

KISWAHILI: TUMEKUTANIKA WOTE KWENYE MTUNGI WA MAJI.

Chanzo cha methali hiyo huongelea juu ya ufikaji wa muda wa kula chakula kwa mtoto. Mtoto akizaliwa hutumia maziwa kwa sababu ya kutokuwa na meno ya kumwezesha kula chakula. Hivyo basi, akiota meno yake huanza kula chakula pamoja na watu wazima. Yeye huingia kwenye kundi la watu wazima. Ndiyo maana watu hao husema kwamba, “tumekutanika wote kwenye mtungi wa maji.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa watu wale ambao wanaushirikiano wa kuwakalibisha wenzao wale waliofikia hatua ya kuingia kwenye kundi lao, katika maisha yao. Watu hao, hukusanyika kwa lengo la kuwakaribisha wenzao hao waliofikia kipindi cha kuingia kwenye kundi lao hilo, kwa sababu ya uelewano na ushirikiano wao huo wa kufanya kazi zao kwa pamoja, maishani mwao. Wao hupata mafanikio mengi katika familia zao hizo kwa sababu ya uelewano na ushirikiano wao huo, katika maisha yao.

Watu hao, hufanana na wale waliomkaribisha mtoto kula pamoja nao alipoota meno, kwa sababu nao huwakaribisha wenzao wale waliofikia muda wa kuingia kwenye kundi lao, maishani mwao. Ndiyo maana wao husema kwamba, “tumekutanika wote kwenye mtungi wa maji.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na ushirikiano wa kukaribishana kufanya kazi zao kwa pamoja na uelewano, ili waweze kupata mafanikio mengi katika familia zao hizo, maishani mwao.

Kutoka 2:16-19.

2Wafalme 9:17.

Ayubu 21:11.

1251. MHIYA YA GWIKUGA UDITUULA MMHINDA YA NUMA.

Aho kale ulihoyi munhu uyo agikuga hela. Aho ojikuga ohela jinijo, umunhu ng’wunuyo, agajituula kumhinda ya kunuma ukunu ajile umulendo lokwe lunulo. Gashinaga abhiye bhamona aho ajilituula umumhinda yakwe ya kunuma yuniyo, bhujisola bho nduhu ugumana uweyi.

Ogashiga ikaya ujikagayiwa umhinda yakwe yiniyo, ubhawila abhiye giki, ojimijaga hela ijo oliojikugaga umunzila ujituula mmhinda ya kunuma. Hunagwene abhiye bhenebho bhagang’wila giki, “mhiya ya gwikuga udituula mmhinda ya numa.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agapandikaga sabho ujikenagula sagala umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agajitumilaga isabho ijo agajipandikaga bho gujigulila maginhu ayo gadina solobho yose yose kunguno ya gugayiwa witegeleja umukatumile ka sabho jakwe jinijo. Uweyi agajimalilaga isabho jakwe kuma mihayo ga sagala bho guileka ikaya yakwe igukoyaga na nzala, umuwikaji bhokwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo agikuga hela ujituula sagala mpaga nose jujimila, kunguno nuweyi agajipandika isabho ujimalila mmamihayo ga sagala mpaga ikaya yakwe yayukosa ya nzaga, umukikalile kakwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “mhiya ya gwikuga udituula mmhinda ya numa.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na witegeleja bho gujitumamila chiza isabho ijo bhagajipandikaga umubhutumami bhobho, kugiki jidule gubhambilija ugujibheja chiza ikaya jabho, umuwikaji bhobho.

Luka 12:16-18.

KISWAHILI: FEDHA YA KUOKOTA USIIWEKE KWENYE MFUKO WA NYUMA.

Hapo zamani alikuwepo mtu aliye okota pesa. Alipoziokota hivyo, mtu huyo, aliziweka kwenye mfuko wake wa nyuma huku akiendelea na safari yake. Kumbe wenzake waliomuona alipokuwa anaziweka pesa hizo kwenye mfuko wake huo wa nyuma wakazichukua bila ya yeye kuelewa.

Alipofika nyumbani alizikosa pesa zake hizo kwenye mfuho huo wa nyuma, akawaambia wenzake kwamba, amepoteza pesa alizoziokota njiani akaziweka kwenye mfuko wake huo wa nyuma. Ndiyo maana wenzake hao walimwambia kwamba, “fedha ya kuokota usiiweke kwenye mfuko wa nyuma.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huzitumia hovyo mali anazozipata, katika maisha yake. Mtu huyo, huzitumia mali anazozipata kwa kununulia vitu visivyo na faida yoyote ile kwa sababu ya kukosa umakini katika matumizi ya mali zake hizo. Yeye huzimalizia mali zake kwenye mambo ya hovyo na kuiacha familia yake katika matatizo ya njaa kwa sababu ya kukosa umakini katika matumizi ya mali zake hizo, maishani mwake.

Mtu huyo, hufanana na yule aliyeokota pesa akaiweka hovyo mpaka ikapotea, kwa sababu naye huzimalizia kwenye mambo ya hovyo mali anazozipata mpaka familia yake hufikia hatua ya kukumbwa na tatizo la njaa, katika maisha yake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “fedha ya kuokota usiiweke kwenye mfuko wa nyuma.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na umakini wa kuzitumia vizuri mali wanazozipata katika utekelezaji wa majukumu yao, ili ziweze kuwasaidia katika kuziendelea vizuri familia zao, maishani mwao.

Luka 12:16-18.

1245. FUJAGA NDIMU, UTIZE’ FUJA NHO-LA


 

 

 

SWAHILI: KOSEA KULENGA MNYAMA MAWINDONI, USIKOSEE KUOA.

Kumekuwa na mjadala mkubwa kuhusu nafasi ya mwanamke katika mila za Kiafrika. Hili lilinifanya niwe na utafiti wa kina kwenye kabila la Wasukuma, ambapo wazee wa Wakisukuma (takribani 12) walithibitisha kwamba, ili familia ifanikiwe, jukumu la mwanamke haliepukiki. Kwa hivyo miongoni mwa Wasukuma, mwanamke katika familia anachukuliwa kuwa msaidizi wa karibu wa mumewe katika utunzaji na uhandisi wa shughuli zote za nyumbani.

Kwa hiyo wanaume wa Kisukuma hutumia methali hii “Fujaga ndimu, utize’ fuja nho-la.” Ili kutoa ufahamu kwa vijana wa kiume na wa kike kabla ya kupambanua kuingia katika maisha ya familia.

Methali hii ya Wasukuma inaonesha utimilifu mkubwa wa mwanaume na mwanamke katika familia yao, ikimaanisha kuwa mwanaume anapooa mwanamke shupavu, mwenye moyo mzuri, mwenye nidhamu, Wasukuma huamini kuwa familia nzima itafanikiwa kwa sababu mwanamke na mwanaume wanaweza kusaidiana vizuri katika maisha ya familia

Hivyo basi, wanawake wanapaswa kuelewa kwamba, wana nafasi au wajibu mkubwa wa kutekeleza katika familia zao. Wanapaswa kufurahishwa na hali yao kama wanawake katika familia na jamii zao.

Mwanzo 2:18 “Bwana Mungu akasema, si vema huyo mtu awe peke yake; nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.”

Marko 10:6-8 “…Mungu akamfanya mume na mke, kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.

Waefeso 5:31 “Lakini kila mmoja wenu ampende mkewe kama nafsi yake mwenyewe; na mke na amheshimu mumewe.

 

ENGLISH: MISS A TARGET WHEN HUNTING, RATHER THAN MARRYING A WRONG WOMAN.

There has been a great discussion on the role of women in the African traditions. This made me have a serious search on the Sukuma Ethnic group, where the Sukuma elders (about 12) confirmed that, in order for the family to prosper, the role of a woman is inevitable. Thus among the Sukuma, a woman in a family is regarded as the closer helper of her husband in keeping and engineering of all domestic activities. Hence the Sukuma men use this proverb “Fujaga ndimu, utize’ fuja nhola.” So as to give awareness to young men and women before discerning to enter family life.

This Sukuma proverb shows the great complementarity of man and woman in their family, meaning that when a man marries a strong, good hearted, disciplined woman, the Sukuma believe that the whole family will be prosperous because the woman and man can really help each other in family life

Hence, women should understand that, have a great role or duty to perform in their families.  They should be happy with their status as women in their family and society.

Gen 2:18 “Then the Lord God said, it is not good that the man should be alone; I will make him a helper fit for him.”

Mk 10:6-8 “….God made the male and female, for this reason a man shall leave his father and mother and be joined to his wife, and the two shall become one flesh…”

Eph 5:31 “however, let each one of you love his wife as himself, and let the wife see that she respects her husband.”

 

1242. WITUNGULAGA ING’HINDA HIYIKU ISAJI IMBA UGUITALIGULA GINEHE!

Aho kale olihoyi munhu uyo agayitungila ing’hinda yakwe hiyiku lisaji aho lyalililalile. Aho lyamisha iliyiku linilo ligandya guyumpeja umunhu ng’wunuyo kugiki linkunde kunguno lyali likali noyi. Hunagwene abhanhu bhagang’wila giki, “witungilaga ing’hinda hiyiku isaji imba uguitaligula ginehe!”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agagikoloshaga mamunhu mashilimu umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agacholaga mamihayo bho gugikolosha amamunhu amashilimu ayo gagankanyaga ikesi kunguno gajimanile sheria, umuwikaji bhogo. Uweyi agamalaga isabho jakwe bho gugalipa amamunhu ayo agagikoloshaga genayo ulugankinda ahibhanza, kunguno gamanile uguyomba.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo agaitungila inhinda yakwe hiyiku isaji, kunguno nuweyi agagikoloshaga mamunhu mashilimu ayo gajimanile isheria ja hibhanza, umuwikaji bhogo. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “witungilaga ing’hinda hiyiku isaji imba uguitaligula ginehe!”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya guleka gwichobhela mamihayo bho gubhikolosha abhichabho, kugiki bhadule gujilanhana chiza isabho jabho, umukaya jabho jinijo.

Mithali 21:24-25.

Mithali 18:23.

KISWAHILI: UMEIFUNGIA NJUGA KWA MAKISAI KICHAA SIJUI UTAIFUNGUAJE!

Hapo zamani alikuwepo mtu aliyeifungia njuga yake kwa makisai kichaa wakati akiwa amelala. Alipoamka makisai huyo alianza kumfukuza ili amugonge kwa sababu alikuwa mkali mno. Ndiyo maana watu walimwambia kwamba, “umeifungia njuga kwa makisai kichaa sijui utaifunguaje.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huwachokoza watu waliowajanja, katika maisha yake. Mtu huyo, hutafuta kesi kwa kuwachokoza watu hao wenye ujanja wa kujua sheria ambao humshinda kesi kwa sababu ya uelewa wao mzuri wa sheria hizo, katika maisha yao. Yeye huzimaliza mali zake kwa kuwalipa watu hao wenye ujanja wa kuongea vizuri mahakamani wanapomshinda kesi kwa sababu ya wao kuzijua vizuri sheria za hapo mahakamani.

Mtu huyo, hufanana na yule aliyeifungia njuga yake kwa makisai kichaa akashindwa kuifungua, kwa sababu naye hujitafutia kesi kwa kuwachokoza watu wanaozijua sheria vizuri, ambao humshinda kesi na kumlipisha, katika maisha yake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “umeifungia njuga kwa makisai kichaa sijui utaifunguaje.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuacha kujitafutia kesi kwa kuwachokoza wenzao, ili waweze kuzitunza vizuri mali zao, katika familia zao.

Mithali 21:24-25.

Mithali 18:23.

ENGLISH: YOU HAVE TIED A BELL TO A CRAZY OX, I DO NOT KNOW HOW YOU WILL UNTIE HIM!

Once upon a time, there was a man who tied his rattle to a crazy ox during sleeping time. When the ox woke up started chasing him to hit him because of being too fierce. That is why people told him that, “you have tied a bell to a crazy ox, I do not know how you will untie him!”

This proverb is compared to the person who provokes clever people in his life. Such person, looks for a case by provoking those people who are clever to know the law enough to win the case because of their good understanding of those laws, in their lives. He ends his wealth by paying those people who have skills to speak well in court when they win the case because they know well the rules of those courts.

This person resembles the one who tied his bell to a crazy ox and failed to untie him, because he also seeks a lawsuit by provoking people who know the law well, who normally win the case and tell him to pay them. That is why people tell him that, “you have tied a bell to a crazy ox, I do not know how you will untie him!”

This proverb imparts in people an idea of stopping provoking their people, so that they can take good care of their properties, in their families.

Proverbs 21:24-25.

Proverbs 18:23.