Kashinje Zacharia

555. UYO AGAFUGAGA MABHELE NGOKO JIDINAHILA ADALALAGA.

Imbuki ya lusumo lunulo yingilile kubhufugi bho mabhele. Amabhele  genayo, gagafugagwa nulu gagasegesagwa mpaga gapya chiza. Aliyo lulu, ulu galisegeswa chiniko gagamalaga likanza lilihu gagufugagwa, nulu gagusegesagwa huna gapya. Ulu gupya gagisungulaga amaguta gabhiza galihigulya amabhele gasaga hasi. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘uyo agufugaga mabhele ngoko jidinahila adalalaga.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo olagana, uyo atogilwe gwigusha n’ung’wiye uyo bhitolile nawe bhujiku pe. Umunhu ng’wunuyo agadumamaga ugutumama imilimo yakwe ulu wela ubhujiku, kunguno ya gwikala na tulo ningi iyo adaimalile ibhujiku. Uweyi agikolaga n’unsegesi o mabhele uyo adalalaga kunguno ya gugwandya unimo guniyo ngoko jidinahila, kulwakubhiza n’uweyi igigushashaga n’uyo bhitolile nawe bhujiku pe. Umunhu ng’wunuyo agikalaga agutindilaga ilimi, kunguno adalalile ibhujiku. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, ‘uyo agufugaga mabhele ngoko jidinahila adalalaga.’

Ulusumo lunuyo lolanga bhanhu gubhiza n’ikanza lya gwibhegeleja uigutumama imilimo yabho iyo igabhapandikalaga jililwa, kugiki bhadule gwinja makoye ga nzala aha kaya jabho.

(Marko 13:36-37).

KISWAHILI: ACHEKECHAYE MAZIWA KABLA YA JOGOO KUWIKA HUWA HALALI.

Chanzo cha methali hii chatokea kwenye uchekechaji wa maziwa. Maziwa huchekechwa kwa muda mrefu sana ndipo yaive. Kuiva kwake ni kufikia hatua ya kujitenga mafuta kuwa juu ya maziwa. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘achekechaye maziwa kabla ya jogoo kuwika huwa halali.’

Methali hii hulinganishwa kwa mwana ndoa ambaye hucheza na mwenzi wake usiku kucha. Mtu huyo hushindwa kufanya kazi kesho yake, kwa sababu ya kuwa na usingizi mwingi ambao hakuumaliza vizuri usiku uliopita. Yeye hufanana na yule anayechekecha maziwa kabla ya jogoo kuwika maana hufanya kazi hiyo usiku kucha bila kulala, kwa sababu naye hucheza na mwenzake wa ndoa usiku kucha, hali ambayo hunfanya aonekane mchovu wakati wa mchana. Mtu huyo hushinda kutwa nzima akisinzia kwa sababu ya kutolala vizuri usiku uliopita. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, ‘achekechaye maziwa kabla ya jogoo kuwika huwa halali.’

Methali hii hufundisha watu kutenga muda wa maandalizi yatakayowawezesha kuyatekeleza vizuri majukumu yao yanayowawezesha kupata chakula, ili waweze kupata mafanikio mengi katika kuzijenga vizuri familia zao. Muda wa maandalizi hayo utawawezesha kuondoa tatizo la njaa kwenye familia zao.

(Marko 13:36-37).

nhungulume2

african-couple

 

ENGLISH: HE WHO SHAKES MILK BEFORE COCKCROW NEVER SLEEPS.

The origin of this proverb is the act of shaking curdled milk to separate it from fat. This is done for a relatively very long time until the fat comes on top of the milk. That is why people say, ‘He who shakes milk before cockcrow never sleeps.’

The proverb is used comparatively to warn a married person who plays with his/her spouse all night long to desist from that behavior, because that person would always be unable to work the next day due to lots of sleep from the previous night. That person is like the one who shakes milk before cockcrow who does that all night without sleeping as he/she, too, plays with his/her spouse all night, which makes him/ look tired in during daytime. That person succumbs to sleeping all day because of not sleeping well the night before. That is why people tell him/her, ‘He who shakes milk before cockcrow never sleeps.’

The proverb teaches people to set aside time to prepare for their activities that bring food on the table, so that they can be more successful in building better families. Preparations will allow them to eliminate the problem of hunger in their families.

(Mark 13: 36-37).

554. ABHABHILI BHALI BHABHILI.

Imbuki ya kahayile kenako yilolile bhanhu abho bhali bhabhili umubhutumami bhobho. Abhanhu bhanebho bhagadulaga gugumala nimo uyo guli ntale bho gutumila likanza liguhi, kunguno ya wilunguja bhobho bhunubho. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘abhabhili bhali bhabhili.’

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kubhanhu abho bhali na wiyambilija bhutale umubhutumami bho milimo yabho. Abhanhu bhenabho bhagilungujaga ijinaguitumama imilimo yabho bho wanguwangu na chiza, mpaga bhadula guimala bho likanza liguhi noyi, kunguno ya wilunguja bhobho bhunubho.

Uwilunguja bhobho bhunubho, bhugabhinhaga nguzu bhuli ng’wene ija gwigulyambija gutumama milimo, kunguno ya wilunguja bhobho bhunubho. Hunagwene abhanhu bhagayomgaga giki, ‘abhabhili bhali bhabhili.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu gubhiza kihamo ijinagwiyambilija uguyitumama imilimo yabho, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi ayo gadulile gujibheja chiza ikaya jabho.

KISWAHILI: WAWILI NI WAWILI.

Chanzo cha msemo huu chaangalia watu ambao ni wawili katika utekelezaji wa majukumu yao. Watu hao huweza kufanya kazi kubwa kwa muda mfupi na kuimaliza, kwa sababu ya umoja wao huo wa kusaidiana vizuri. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘wawili ni wawili.’

Msemo huou hulinganishwa kwa watu wale ambao hufanya kazi zao kwa kushirikiana vizuri. Watu hao hujibidisha kufanya kazi zao kwa haraka na vizuri hadi hufaulu kuzimaliza kwa muda mfupi, kwa sababu ya umoja wao huo.

Umoja huo huwapa nguvu kila mmoja wao za kujibidisha kufanya kazi, kwa sababu ya faraja yao hiyo ya kuwa pamoja. Umoja huo pia huwawezesha kushirikiana katika kuyatatua matatizo mbalimbali katika maisha yao. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘wawili ni wawili.’

Msemo huu hufundisha watu kuwa na umoja wa kuwawezesha kusaidiana katika kuyatekeleza vizuri majukumu yao, ili waweze kupata mafanikio ya kuziendeleza vizuri familia zao.

modelo-mocambicana

bhashule

ENGLISH: THE TWO ARE TWO.

The orogin of this saying is individuals who are two in execution of their responsibilities. Such individuals can do a great job in a short period of time and finish it because of their unity and support. That’s why people say, ‘The two are two.’

The saying is used comparatively to refer to people who do their jobs in good cooperation. Such people do their work quickly and efficiently, until they are able to finish it within the shortes time possible, because of their unity.

The union empowers each of them to work hard, because of shared comfort. The union also allows them to work together to solve various problems in life. That’s why people say, ‘the two are two.’

The saying teaches people about being united to enable them to help each other in fulfilling their responsibilities, so that they can find success for the betterment their families.

553. NDEGE YA HASI.

Imbuki ya kahayile kenako yilolile ndege iyo yili ya hasi. Indege yiniyo idalalaga ung’wigulya guti umo jigalalilaga indege ijingi. Iyoyi igapelelaga hasi pye amakanza gayo. Hunagwene abhanhu bhagiyiitanaga giki, ‘ndege ya hasi.’

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agitaga bhukengeji bhogudebha ijenheleja ja jito jitale ijo jigigelaga umuchalo jakwe. Umunhu ng’wunuyo, agagatumilaga chiza amasala gakwe, mpaga obhupandika ubhung’hana bho jito jinijo. Uweyi agikolaga n’indege ya hasi, kunguno nuweyi agabhucholaga ubhung’hana bho musilili, kugiki abhanhu bhakije ugundebha igiki alikengela mhayo nebhe. Hunagwene agiitanaga giki, ‘Ndege ya hasi.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu gudebha gwita bhukengeji ubho bhudulile gubhambilija ugubhudebha ubhung’hana bho mihayo iyo igigelaga umuchalo jabho, kugiki bhadule gwikala  bho mholele na bhichabho umukikalile kabho.

(Mathayo 2:1-5; Mathayo 2:16-17).

KISWAHILI: NDEGE YA CHINI.

Chanzo cha msemo huu chaangalia ndege ambayo huwa chini. Ndiyo hiyo, hairuki kama zirukavyo ndege zingine. Yenyewe hukimbia ikiwa chini wakati wote. Ndiyo maana watu huiita kwamba ni ‘ndege ya chini.’

Msemo huu hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hufanya utafiti wa kumwezesha kuelewa chanzo cha matukio makubwa ya kijijjini kwake. Mtu huyo hutumia vizuri akili zake zote, hadi anafikia hatua ya kupata ukweli wa tukio hilo lililotukia kijijini kwake. Yeye hufanana na ndege ya chini, kwa sababu naye hufanya utafiti kwa kuchungua kisirisiri chanzo cha matukio ya pale kijijini kwake. Yeye hufanya kazi hiyo chinichini, ili wengine wasiweze kumtambua kuwa anafuatilia tukio fulani la pale kijijini kwao. Ndiyo maana yeye hujiita kwamba ni ‘ndege ya chini.’

Msemo huu hufundisha watu kuelewa namna ya kufanya utafiti wa kuwawezesha kuelewa chanzo cha matukio ya kwenye maeneo yao, ili waweze kuishi kwa amani na wenzao katika maisha yao.

(Mathayo 2:1-5; Mathayo 2:16-17).

ndege

ndege1

 

ENGLISH: A GROUND PLANE.

The origin of this saying is a plane that stays on the ground. Yes, it does not fly like other planes. It runs on the ground all the time. That is why people call it ‘a ground plane.’

The saying is used comparatively to refer to a person who conducts research to understand the cause of major events in his village. The person makes good use of all his senses until he/she finds out what happened. He/she is like a ground pplane, because he/she conduct his/her research secretly. He/she works undercover so that others may not recognize that he/she is persuing a local event in their village. That is why he/she calls himself a ‘ground plane.’

The saying teaches people about understanding how to do research to enable them understand the cause of events in their environment, so that they can live in harmony with their peers.

(Matthew 2: 1-5; Matthew 2: 16-17).

552. LUBHUNDA MIYAGA.

Imbuki ya kahayile kenako ilolile bhubhundi bho miyaga bho jivumva jilebhe, nu bho ningi uyo alinduja. Ubhubhundi bho miyaga bhunubho bhuli bho jisumva ijo jigasamaga huna lwingila luyaga umuno gojo. Ijoyi jigihayaga giki jilina bhudula bho gulubhugila luyaga lutale.

 Ulu ningi nduja ubhakinda abhiye agihaya giki n’uweyi agabhundaga miyaga, kunguno adahebhagwa umumbina jakwe. Hungwene agiitanaga umugiji o miyaga ng’wunuyo giki, ‘Lub’unda miyaga.’

Akahayile kenako kagalenganijiyaga kuli munhu uyo alina nguzu ja gutumama milimo iyo igamalilaga makoye umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agatumamaga milimo ya gubhatongela chiza abhiye, kugiki bhadebhe ugugamala amakoye gabho bho gutumama milimo yabho chiza.

Uweyi agikolaga nu lubhunda miyaga, kunguno n’uweyi alina nguzu ja guyihebha imilimo yakwe chiza. Imilimo yiniyo igamalilaga makoye aha ng’wakwe. Hunagwene abhanhu bhagang’witanaga giki, ‘Lubhunda miyaga.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu gubhiza na nguzu ja guyitumama imilimo yabho chiza, kugiki bhadule gubhingija abhanhu bhabho makoye ga gugayiwa jiliwa umuwikaji bhobho.

(Mathayo 27:45-54; Marko 1:21-28; Matendo ya Mitume 16:2; 1Wathesalonike 4:11-12).

KISWAHILI: MBUGIA UPEPO.

Chanzo cha msemo huu chaangalia ubugiaji wa upepo wa kiumbe fulani au wa manju ambaye huwashinda wenzake katika michezo ya ngoma. Ubhugiaji huo ni wa kiumbe ambacho huachana ili kuruhusu upepo ungie mdomoni. Chenyewe hujidai kuwa na uwezo wa kubugia kimbunga kiwezacho kuzoa vitu mbalimbali.

Hali hiyo hutokea wakati manju anayesifika akiwashinda wenzake kwenye michezo ya ngoma, anajitapa. Yeye hujiita majina ya kuonesha kwamba ana uwezo mkubwa kuwazidi wenzake, ili waendelee kumwogopa. Ndiyo maana yeye hujiita kwamba ni ‘mbugia upepo.’

Msemo huu hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ni mwenye nguvu za kumwezesha kufanya kazi zile ziwezazo kumuondolea matatizo kwa haraka maishani mwake. Mtu huyo huyatekeleza majukumu yake ya kuwaongoza vizuri wenzake, ili waelewe namna ya kuyatatua matatizo yao kwa kufanya kazi vizuri na kwa bidii.

Yeye hufanana na mbugia upepo, kwa sababu naye ana nguvu za kuzitekeleza kazi zake vizuri hadi kuzimaliza. Kazi hizo humsaidia katika kuyatatua vizuri matatizo yake. Ndiyo maana watu humwita kwamba ni ‘mbugia upepo.’

Msemo huu hufundisha watu kuwa na nguvu za kuyatekelezea majukumu yao vizuri, ili waweze kupata mafanikio yawezazo kuwatatulia matatizo mbalimbali maishani mwao.

(Mathayo 27:45-54; Marko 1:21-28; Matendo ya Mitume 16:2; 1Wathesalonike 4:11-12).

nkima ntumami

ntumami

 

ENGLISH: A WIND SWALLOWER.

The origin of this saying is ghostly nature of a particular creature or a maestro that overpowers his/her colleagues in dance competitions. The creature opens its mouth to allow wind to enter. It claims to be able to swallow a storm, which can take on many objects.

The self praise happens a maestro beats his/her contestants. When it so happens, he/she calls himself/herself praise names to show that he/she has great powers over his/her contestants so that they will always be scared of him/her. That is why he/she calls himself/herself ‘a wind swallower.’

The saying is used comparatively to refer to a person who has the power to do tasks that can get him out of trouble quickly in life. The person carries out his/her responsibilities to properly guide others to understand how to solve their problems, by working effectively and diligently. He/she is like a wind swallower, because he/she also has the power to carry out his tasks well. Such activities help him/her to solve his/her problems properly. That is why people call him ‘a wind swallower.’

The saying teaches people to carry out their tasks properly, so that they can achieve the best they can to solve a variety of problems in their lives.

(Matthew 27: 45-54; Mark 1: 21-28; Acts 16: 2; 1Thessalonians 4: 11-12).

551. KALAGU – KIZE: ULU UDATUMILILE LUKULUME ADUTUMAMA UNIMO – SIMU.

Imbuki ya kalagu yiniyo yilolile simu na lukulume. Isimu yiniyo, jili ginhu ja gwiyombeja ulu yukandwa bho lukulume. Gashinaga lulu, ulu munhu adatumilile lukulume bho guikanda, idutumama unimo goyo. Hunagwene abhanhu bhagiganilaga giki, ‘ulu udatumillie lukulume adutumama unimo’ bhashosha, ‘Simu.’

Ikalagu yiniyo yigalenganijiyagwa kuli namhala uyo agayitongelaga chiza ikaya yakwe. Unamhala ng’wunuyo agabhapangilaga abhanhu bhakwe imilimo iya gutumama bhuli lushugu. Uweyi agabhalanjaga inzila ja gubhatongela chiza abhichabho umukikalile kabho.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga n’ulukulume ulo lugaikandaga isimu yatumama unimo goyo, kunguno n’uweyi agaipangilaga imilimo ikaya yakwe mpaga yang’wigwa chiza. Hunagwene abhanhu bhagiganilaga giki, ‘ulu udatumilile lukulume adutumama unimo’ bhashosha, ‘Simu.’

Ikalagu yiniyo yalanga bhanhu gudebha kubhatongela chiza abhanhu bhabho bho gubhapangila imilimo ya gutumama, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi umuwikaji bhobho.

(Kutoka 20:12; Mathayo 4:18-22; Mithali 4:1-4).

KISWAHILI: KITENDAWILI  – TEGA: USIPOTUMIA DOLE GUMBA HATAFANYA KAZI – SIMU.

Chanzo cha kitendawili hiki chaangalia simu na dole gumba. Simu ni chombo cha mawasiliano yanayofanyika baada ya kubonyezwa kwa kutumia dole gumba. Kumbe basi, mtu asipotumia dole gumba lake kukibonyeza, hakitafanya kazi yake. Ndiyo maana watu hutegeana kitendawili kwamba, ‘usipotumia dole gumba hatafanya kazi’ na kujibu, ‘Simu.’

Kitendawili hiki hulinganishwa kwa mzee yule ambaye anafahamu kuiongoza vizuri familia yake. Mzee huyo huwapangia watu wake kazi za kutekeleza kila siku. Yeye huwafundisha watu namna ya kuongoza wenzao katika maisha yao.

Mtu huyo hufanana na dole gumba ambalo huiwezesha simu kufanya kazi kwa kuibonyeza, kwa sababu naye huwapangia majukumu watu wa familia yake, nao humwelewa na kuyatekeleza vizuri. Ndiyo maana watu hutegeana kitendawili, ‘Usipotumia dole gumba hatafanya kazi’ na kujibu, ‘Simu.’

Kitendawili hiki hufundisha watu kuelewa namna ya kuwaongoza watu wao kwa kuwapangia majukumu ya kutelekeza, ili waweze kupata mafanikio mengi maishani mwao.

(Kutoka 20:12; Mathayo 4:18-22; Mithali 4:1-4)

simu

simu1

 

ENGLISH: I HAVE A RIDDLE – LET IT COME: IF YOU DON’T USE YOUR THUMB HE WON’T WORK – A PHONE.

The origin of this riddle is a phone and a thumb. The phone is a tool for communication that works after being tapped with a thumb. However, if a person does not use his/her thumb to press it, it will not do its job. That’s why people pose a riddle, ‘if you don’t use your thumb, he won’t work’ and reply,  ‘A phone.’

This riddle is used comparatively to refer to a family head who knows how to lead well his/her family by way of assigning family members daily tasks to perform. He/she teaches them how to lead their peers in their lives. He/she person is like a thimb that enables the phone to work after pressing it, because he/she also assigns responsibilities to the members of his/her family, who understand and carry out the instructions. That’s why people pose a riddle, ‘If you don’t use your thumb he won’t work’ and respond. ‘A phone.’

This riddle teaches people about understanding how to lead their people, by assigning responsibilities to fulfil, so that they can achieve more in their lives.

(Exodus 20:12; Matthew 4: 18-22; Proverbs 4: 1-4).