Joe Healey

559. LIMI BHADABHIMBELAGWA.

Imbuki ya kahayile kenako yingilile ku bhuli bho jiliwa ahikanza lya limi. Umunhu ulu ulya wiguta gete ahikanza linilo ilya limi, adiko ugubhimbelwa kunguno, adulile guja gujutumama milimo mpaka utubha. Umunhu ng’wunuyo agushoka ikaya otubhaga. Hunagwene, abhanhu bhagayombaga giki, ‘limi bhadabhimbelagwa.’

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agalitumilaga ilikanza ilya limi bho gutumama milimo chiza. Umunhu ng’wunuyo, agajitumilaga ijiliwa ijo ojilyaga bho gutumama milimo yakwe bho bhukamu bhutale, kugiki adule gupandika matwajo mingi ayo gadulile guyilang’hana chiza ikaya yakwe.Uweyi adebhile ugubhalanga abhanhu bhakwe gubhiza bhali kumilimo ahikanza lyabho ilya limi, bho gubhinha jigemelo ja wikaji na bhutumami bhokwe. Umunhu ng’wunuyo agifulaga ibhujiku, kugiki adule guyitumama chiza imilimo yakwe ahikanza ilya limi. Ulu wela ubhujiku, agalyaga wiguta, na kuja kumilimo yakwe, ogatumama mpaga utubha, na ogodoka. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘limi bhadabhimbelagwa.’

Akahayile kenako, kalanga bhanhu  gulitumila ilikanza ilya limi, bho gwigulambija gutumama milimo yabho, kugiki bhadule gupandika matwazo mingi, umuwikaji bhobho.

(Ufunuo 3:20-21).

KISWAHILI: MCHANA HAWAVIMBIWI.

Chanzo cha msemo huu chatokea katika ulaji wa chakula wakati wa mchana. Mtu akila sana chakula wakati wa mchana, havimbiwi kwa sababu aweza kwenda kufanya kazi mpaka akajisikia njaa. Mtu huyo atarudi nyumbani akijisikia njaa. Ndiyo maana watu husema kwamba ‘mchana hawavimbiwi.’

Msemo huu hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huutumia muda wake wa mchana kufanya kazi zake vizuri. Mtu huyo hukifanyia kazi chakula alichokula, kwa kuyatekeleza majukumu yake ambayo humpatia mafanikio ya kuitunza vizuri familia yake. Yeye anafahamu kuwafundisha watu wake kuwa kazini wakati huo wa mchana, kwa sababu ya yeye mwenyewe kuwa mfano wa kufanya kazi vizuri, maishani mwake. Mtu huyo hupumzika wakati wa usiku, ili aweze kuyatekeleza vizuri majukumu yake wakati mchana.

Usiku ukipambazuka, yeye hula chakula na kwenda kazini kwake, ambako hufanya kazi mpaka anajisikia njaa, ndipo hurudi nyumbani. Ndiyo maana watu husema kwamba ‘mchana hawavimbiwi.’

Msemo huu hufundisha watu kuutumia vizuri wakati wao wa mchana kwa kuyatekeleza vizuri majukumu yao, ili waweze kupata mafanikio makubwa maishani mwao.

(Ufunuo 3:20-21).

bhuli bho jiliwa

magwa limi

ENGLISH: THERE IS NO SUCH THING AS OVEREATING DURING DAY TIME.

The origin of this is eating habits during the day. If a person eats too much food during the day, they cannot said to have over eaten because they can go to work and work until they feel hungry. Tht person will come back home hungry. That is why people say, ‘there is no such thing as over eating during day time.’

The saying is used comparatively to refer to a person who spends most of his day working well. The person works and burns the food he/she eats, fulfilling his/her obligations and succeeds in takin good care of his/her family. Such a person knows how to teach others about being at work during the day time, because of himself/herself being the role model in his life. The person rests at night, so he can carry out his/her duties during the day.

In the morning, he/she eats food and goes to his/her place of work, where he/she works until he/she is hungry and then returns home. That is why people say,  Tthere is no such thing as over eating during day time.’

The saying teaches people o make the most of their day, by doing their jobs well so that they can get the most out of their lives.

(Revelation 3: 20-21).

558. BHUTEMI BHUDIINHAGWA KABHILI.

Imbuki ya kahayile kenako ilolile winhiwa bho ng’wa munhu bhutemi. Ubhutemi bhunubho bhobhizaga ikanza lya Ng’wana o Ntemi gwinhiwa bhutale bho h’ikulu. Umunhu ulu winhiwa bhutemi bhunubho mumho ukulaga, kunguno gwingila hikanza linilo abhanhu bhakwe bhagandyaga kung’witana giki uweyi ali Ntemi obho. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘bhutemi bhudiinhagwa kabhilli.’

Akahayile kenako, kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo wingilaga muwikaji bhupya bho gubhatijiwa. Umunhu ng’wunuyo obyalagwa bhupya bho gwingijiwa ishibhi jakwe gubhitila mubhubhatijiwa bhunubho. Uweyi agandyaga wikaji bhupya ubho gwikala kihamo na Yesu.

Umunhu ng’wunuyo agiikolaga n’uwinhiwa bho bhutemi, kunguno nang’hwe agalumanyiyagwa mubhutemi bho Ng’wa Yesu, uyo alitemi Ntale. Uweyi adabhatijiyagwa kabhili, kunguno ubhubhatijiwa bhugabhinhaga abhabhatijiwa lumenho ulo ludajimilaga. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘bhutemi bhudiinhagwa kabhilli.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu gudebha gubhatongela mukikalile kawiza abhanhu bhabho bho guwikalana ubhung’hana, kugiki bhadule gubhutumamila chiza na bho mholele ubhutale ubho bhalinabho umukaya jabho.

(Waefeso 4:4-6).

KISWAHILI: MTU HAPEWI UFALME MARA MBILI.

Chanzo cha msemo huu chaangalia upewaji wa ufalme kwa mtu. Ufalme huo huja  kwa mtoto wa mfalme ambaye hupewa ukuu wa Ikulu. Mtu huyo aliyepewa ufalme huwa mkuu kwa sababu watu wake huanza kumwita Mfalme wao, kuanzia wakati alipokabhidhiwa ufalme huo. Ndiyo maana watu husema  kwamba, ‘Mtu hapewi ufalme mara ya pili.’

Msemo huu hulinganishwa kwa mtu aliyeanza maisha mapya kwa kubatizwa. Mtu huyo huzaliwa upya kwa kuondolewa dhambi zake kupitia ubatizo huo. Yeye huanza maisha mapya ya kuungana na Yesu.Mtu huyo hufanana na aliyepewa ufalme, kwa sababu naye hushirikiswa ufalme wa Yesu ambaye ni Mfalme Mkuu. Yeye habatizwi mara ya pili, kwa sababu ubatizo huo humuwekea mbatizwa alama isiyofutika. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘Mtu hapewi ufalme mara ya pili.’

Msemo huu hufundisha watu kuelewa kuwaongoza  vizuri watu wao katika njia za haki, kwa kuuishi ukweli, ili waweze kuufanyia kazi vizuri na kwa amani ukuu walio nao katika familia zao.

(Waefeso 4:4-6).

swaziland warior

wigisha1

 

ENGLISH: KINGSHIP IS NOT BESTOWED TWICE.

The basis of this saying is bestowment of kingship. The kingship is given to crown prince. This man to whom the kingship is bestowed becomes great because his people begin to call him their King from the time of his coronation. That is why people say, Kingship is not bestowed twice.’

The saying is used comparatively with reference to someone who starts new life by following baptism. The person is born again through cleasing of his/her sins through that baptism. He/she begins a new life of union with Jesus. This person is like the heir apparent to the throne who has been bestowed with kingship, because he/she is associated with the Kingdom of Jesus, the great King. He/she is not baptized twice, because the baptism leaves an everlasting mark. That is why people say, ‘Kingship is not bestowed twice.’

The saying teaches people about understanding how to lead their people in the ways of justice, by living the truth, so that they can work well and peacefully on their greatness.

(Ephesians 4: 4-6).

557. KALAGU – KIZE: MULULO GO MHELA – MPELO GO NZOKA.

Imbuki ya kalagu yiniyo yilolile nzoka. Inzoka aha yub’itila igamanyikaga, kunguno ya mpelo goyo. Umpelo gunuyo guli jimanyikijo ja nzoka. Hunagwene abhanhu bhagiganilaga giki, ‘mululo go mhela’ bhashosha, ‘Mpelo go nzoka.’

Ikalagu yiniyo igalengajiyagwa kuli munhu uyo agitaga ya bhubhi umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo alina nhungwa ja gwibhonela bhanhu na gwituula bhumani bho gubhadalaha abhiye umumahoya gakwe. Uweyi agiikolaga n’umpelo go nzoka, kunguno n’uweyi agitaga ya bhubhi iyo igamanyichaga ukubhanhu. Umunhu ng’wunuyo agagayiyagwa abhanhu bhaguhoya nang’hwe, kunguno bhajidebhile inhungwa jakwe igiki jili jabhubhi. Hunagwene abhanhu bhanebho bhagiganilaga giki, ‘mululo go mhela’ bhashosha, ‘Mpelo go nzoka.’

Ikalagu yiniyo, yalanga bhanhu guleka nhungwa ja bhubhi na gubhadebha abhichacho bho gulola nhungwa jabho, kugiki bhadule gwikala bho mholele na bhichabho umuwikaji bhobho. Yigelelilwe bhuli ng’wene abhize nzugulu matu umukikale kakwe.

(Ufunuo 14:13; Ufunuo 12:13-17; Mthayo 7:15-20; Luka 6:43-45).

KISWAHILI: KITENDAWILI  – TEGA: MBURUTO WA KIFARU – ALAMA YA MPITO WA NYOKA.

Chanzo cha kitendawili hiki chaangalia alama ya nyota alimopitia. Nyoka huacha alama inayomtambulisha kila anapopitia. Alama hiyo humwezesha kila anayeiona kuelewa kuwa amepita nyoka, kwa sababu alama hiyo huonesha umbo lake lilivyo. Ndiyo maana watu hutegeana kitendawili kwamba, ‘mburuto wa kifaru‘ na kujibu ‘Alama ya mpito wa nyoka’.

Kitendawili hiki, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hutenda maovu katika maisha yake. Mtu huyo ana tabia ya kuonea wenzake na kujidai kujua zaidi kuliko wenzake katika maongezi yake. Yeye hufanana na alama ya mpito wa nyoka, kwa sababu hufanya maovu ambayo humtambulisha kwa watu kuwa ndiye aliyeyatenda. Mtu huyo hukosa hata watu wa kuongea naye, kwa sababu watu wanaifahamu tabia yake ilivyo mbaya. Ndiyo maana watu hutegeana kitendawili kwamba ‘mburuto wa kifaru’ na kujibu, ‘Alama ya mpito wa nyoka.’

Kitendawili hiki, hufundisha watu kuacha tabia mbaya na kuwafahamu wenzao kwa kuangalia matendo yao maishani, ili waweze kuishi kwa amani na wenzao maishani. Yafaa kila mmoja awe mwangalifu kwa mwenzake.

(Ufunuo 14:13; Ufunuo 12:13-17; Mathayo 7:15-20; Luka 6:43-45).

nzoka

nzoka1

ENGLISH: I HAVE A RIDDLE – LET IT COME: A RHINO’S TRACE – THE TRACE OF A SERPENT.

The foundation of this riddle is a trace of a snake. The snake leaves a mark that identifies its passage. The mark enables everyone who sees it to understand that a serpent passed, because the mark shows the true nature of the snake. That’s why people pose a riddle, ‘a rhino’s trace’ and repond, ‘The trace of serpent.’

The riddle is used comparatively to refer to a person who does evil in his/her life. The person has a tendency of bullying others and is a much-know in his/her talks. He/she resembles the trace of a serpent, because he/she does evil that identifies him/her as the doer. This person doesn’t get people to talk to, because people know his/her bad behavior. That’s why people pose a riddle, ‘a rhino’s trace’ and repond, ‘The trace of serpent.’

This riddle, teaches people to refrain from bad habits and get to know their peers through their actions, so that they can live in harmony with others. Everyone should be careful with one another.

(Revelation 14:13; Revelation 12: 13-17; Mathayo 7: 15-20; Luke 6: 43-45).

556. NANCHIMA UNG’WANA MHELA ILINDA.

Imbuki ya kahayile kenako ilolile bhuching’wa bho ng’wana o mhela iyo ilinda. Ubhuching’wa bhunubho bhuli bho guchima jisumva jibhili, kunguno uyo alinda, ibhize mhela nulu munhu, agabhizaga alina ng’wiye umugati yakwe. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘nanchima ung’wana mhela ilinda’.

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo alinsabhi o jikolo ja mbika ningi aha ng’wakwe. Umunhu ng’wunuyo agikalaga na sabho ningi ijo agajitumilaga nulu agalabhuka munhu ahakaya yakwe gumpija. Uweyi agajigufunyaga duhu, kunguno ojipandika ijikolo ijo jili jingi noyi umuwikaji bhokwe. Umunhu ng’wunuyo, agiikolaga nu munhu uyo  alinda, nulu ndimu iyo ilinda, kunguno n’uweyi alina sabho ijo agajitumilaga nulu kunchala ng’wiye uyo ominyikaga kusibhitali. Hunagwene abhanhu bhagayombaa giki, ‘nanchima ung’wana mhela ilinda.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu kubhiza na wisagizu bho gupandika jikolo bhuli ng’wene ijo alijichola umubhutumami bho milimo yakwe, kugiki bhadule gwikala bho mholele na bhichabho umukikalile kabho.

(Mathayo 7:7-8; Luka 11:9-10; Luka 11:13).

KISWAHILI: NIMEMCHOMA MWANA KIFARU ANA HIMILA.

Chanzo cha msemo huu chaangalia kuchomwa kwa  kifaru ambaye ana mimba. Kuchomwa huko kwa kifaru mwenye himila ni hali ya kuumizwa kwa viumbe wawili, kwa sababu mwenye himila, awe mwanadamu au mnyama, ana mtoto ndani ya tumbo lake. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘nimemchoma mwana kifaru ana himila.’

Msemo huu hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ni tajiri mwenye mali nyingi nyumbani kwake. Mtu huyo huzitumia mali zake hizo katika kutatua matatizo mbalimbali katika familia yake. Wingi wa mali hizo huweza kumsaidia hata mtu akiumia nyumbani kwake; huchukua mali hizo na kumuwahisha kwenye matibabu hospitalini. Mtu huyo hufanana na yule kiumbe mwenye himila aliyeumia, kwa sababu naye anazo mali ambazo huonekana anapozitumia wakati wa kutatua tatizo fulani katika familia yake. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘nimemchoma mwana kifaru ana himila.’

Msemo huu hufundisha watu kuwa na matumaini ya kupata mafanikio makubwa kila mmoja wao anayejibidisha kutafuta katika utekelezaji wa makukumu yake, ili aweze kuishi kwa amani na wenzake maishani.

(Mathayo 7:7-8; Luka 11:9-10; Luka 11:13).

nsabhi masai

mhela

ENGLISH: I HAVE STABED A BABY IN A PREGNANT RHINO.

The origin of this saying is stabbing of a baby in a pregnant creature. This is a traumatic experience for two beings, because a pregnant being, whether human or animal, has a baby inside her womb. That is why people say, ‘I have stabbed a baby in a pregnant rhino.’

The saying is used comparatively to refer to a rich person with many possessions in his home. The person uses his/her wealth to solve various problems in his/her family. The wealth can even help a person when he or she is injured to get treated in a hospital. This person is like a pregnant creature, because his/her wealth is useful in solving problems in his/her family. That is why people say, ‘I have stabbed a baby in a pregnant rhino.’

The saying teaches people to hope for the greatest success as long as they execute their responsibilities as they should, so that they can live in peace with their peers.

(Matthew 7: 7-8; Luke 11: 9-10).

555. UYO AGAFUGAGA MABHELE NGOKO JIDINAHILA ADALALAGA.

Imbuki ya lusumo lunulo yingilile kubhufugi bho mabhele. Amabhele  genayo, gagafugagwa nulu gagasegesagwa mpaga gapya chiza. Aliyo lulu, ulu galisegeswa chiniko gagamalaga likanza lilihu gagufugagwa, nulu gagusegesagwa huna gapya. Ulu gupya gagisungulaga amaguta gabhiza galihigulya amabhele gasaga hasi. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘uyo agufugaga mabhele ngoko jidinahila adalalaga.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo olagana, uyo atogilwe gwigusha n’ung’wiye uyo bhitolile nawe bhujiku pe. Umunhu ng’wunuyo agadumamaga ugutumama imilimo yakwe ulu wela ubhujiku, kunguno ya gwikala na tulo ningi iyo adaimalile ibhujiku. Uweyi agikolaga n’unsegesi o mabhele uyo adalalaga kunguno ya gugwandya unimo guniyo ngoko jidinahila, kulwakubhiza n’uweyi igigushashaga n’uyo bhitolile nawe bhujiku pe. Umunhu ng’wunuyo agikalaga agutindilaga ilimi, kunguno adalalile ibhujiku. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, ‘uyo agufugaga mabhele ngoko jidinahila adalalaga.’

Ulusumo lunuyo lolanga bhanhu gubhiza n’ikanza lya gwibhegeleja uigutumama imilimo yabho iyo igabhapandikalaga jililwa, kugiki bhadule gwinja makoye ga nzala aha kaya jabho.

(Marko 13:36-37).

KISWAHILI: ACHEKECHAYE MAZIWA KABLA YA JOGOO KUWIKA HUWA HALALI.

Chanzo cha methali hii chatokea kwenye uchekechaji wa maziwa. Maziwa huchekechwa kwa muda mrefu sana ndipo yaive. Kuiva kwake ni kufikia hatua ya kujitenga mafuta kuwa juu ya maziwa. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘achekechaye maziwa kabla ya jogoo kuwika huwa halali.’

Methali hii hulinganishwa kwa mwana ndoa ambaye hucheza na mwenzi wake usiku kucha. Mtu huyo hushindwa kufanya kazi kesho yake, kwa sababu ya kuwa na usingizi mwingi ambao hakuumaliza vizuri usiku uliopita. Yeye hufanana na yule anayechekecha maziwa kabla ya jogoo kuwika maana hufanya kazi hiyo usiku kucha bila kulala, kwa sababu naye hucheza na mwenzake wa ndoa usiku kucha, hali ambayo hunfanya aonekane mchovu wakati wa mchana. Mtu huyo hushinda kutwa nzima akisinzia kwa sababu ya kutolala vizuri usiku uliopita. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, ‘achekechaye maziwa kabla ya jogoo kuwika huwa halali.’

Methali hii hufundisha watu kutenga muda wa maandalizi yatakayowawezesha kuyatekeleza vizuri majukumu yao yanayowawezesha kupata chakula, ili waweze kupata mafanikio mengi katika kuzijenga vizuri familia zao. Muda wa maandalizi hayo utawawezesha kuondoa tatizo la njaa kwenye familia zao.

(Marko 13:36-37).

nhungulume2

african-couple

 

ENGLISH: HE WHO SHAKES MILK BEFORE COCKCROW NEVER SLEEPS.

The origin of this proverb is the act of shaking curdled milk to separate it from fat. This is done for a relatively very long time until the fat comes on top of the milk. That is why people say, ‘He who shakes milk before cockcrow never sleeps.’

The proverb is used comparatively to warn a married person who plays with his/her spouse all night long to desist from that behavior, because that person would always be unable to work the next day due to lots of sleep from the previous night. That person is like the one who shakes milk before cockcrow who does that all night without sleeping as he/she, too, plays with his/her spouse all night, which makes him/ look tired in during daytime. That person succumbs to sleeping all day because of not sleeping well the night before. That is why people tell him/her, ‘He who shakes milk before cockcrow never sleeps.’

The proverb teaches people to set aside time to prepare for their activities that bring food on the table, so that they can be more successful in building better families. Preparations will allow them to eliminate the problem of hunger in their families.

(Mark 13: 36-37).