Kashinje Zacharia

650. BHEJAGI NGATA NIGO GULI NDITO.

Imbuki ya lusumo lunulo, yingilile kubhubheja bho ngata ya gubhukija nigo ndito. Ingata yiniyo, igambilijaga ugugukikija ntwe kugiki gudizubhunwa nu nigo gunuyo, kunguno gulintale. Hunagwene abhanhu ulubhuhaya gubhucha nigo uyo guli ndito bhagikomelejaga gubheja ngata bho guyomba giki, ‘bhejagi ngata nigo guli ndito.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agibhegelejaga chiza ulu  alihaya gwita nimo uyo guli ndito. Umunhu ng’wunuyo, ulu uhaya gutumama nimo uyo guli ndito, agajikumingaga pye ijitumamalo ja nimo gunuyo, kugiki adule gugumala chiza.

Uweyi agikolaga nu munhu uyo agabhejaga ngata ulu ohaya gubhucha nigo ndito, kunguno nu weyi agibhegelejaga bho gujikuminga pye ijitumamilo ja nimo uyo ulihaya gugutumama.

Umunhu ng’wunuyo, agabhakomelejaga na bhiye kugiki nabho bhadule gwibhegeleja chiza haho bhatali uguitumama imilimo yabho. Hunagwene agabhawilaga abhiye bhenabho giki, ‘bhejagi ngata nigo guli ndito.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya ya gwibhegeleja chiza haho bhatali uguyandya imilimo yabho, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi, ijinabhutumami bho milimo yabho yiniyo, umuwikaji bhobho.

Mathayo 26:36-46.

Mathayo 11:18.

Waefeso 6:10.

Marko 8:34.

KISWAHILI: TENGENEZENI NZINGA MZIGO NI MZITO.

Chanzo cha methali hiyo, chatokea kwenye utengenezaji wa Nzinga ya kubebea mzigo mzito. Nzinga hiyo, husaidia katika kukizuia kichwa kupata maumivu ya mzigo huo, kwa sababu ya ukubwa na uzito wake. Ndiyo maana watu wakitaka kubeba mzigo mzito husema kwamba, ‘tengenezeni Nzinga mzigo ni mzito.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hujiandaa vizuri anapotaka kufanya kazi ambazo ni mzito, katika maisha yake. Mtu huyo, huvikusanya vifaa vyote vinavyohitajika katika utekelezaji wa kazi anayotaka kuifanya, ili aweze kuitekeleza vizuri kazi yake hiyo.

Yeye hufanana na mtu yule ambaye hutengeneza nzinga ya kubebea mzigo mzito anaotaka kuubeba, kwa sababu naye hujiandaa vizuri, kwa kuvikusanya vifaa vile vyote vinavyohitajika katika utekelezaji wa kazi zake.

Mtu huyo, huwahimiza pia wenzake ili nao waweze kujiandaa vizuri kila wanapotaka kuyatekeleza majukumu yao, maishani mwao. Ndiyo maana huwaambia wenzake hao kwamba, ‘tengenezeni Nzinga mzigo ni mzito.’

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kufanya maandalizi ya kina, kila wanapotaka kuyatekeleza majukumu yao, ili waweze kupata mafanikio mengi katika kazi zao, maishani mwao.

Mathayo 26:36-46.

Mathayo 11:18.

Waefeso 6:10.

Marko 8:34.

kaniki1

ngata

nkima o benin

 

ENGLISH: PRAPARE A ROUND HEAD PAD, THE LUGGAGE IS HEAVY TO CARRY.

The source of this saying is a luggage one has to carry on his/her head. In order to carry this luggage, one has to prepare himself/herself by having a round head pad in order to prevent direct pain that the luggage can inflict on the head of the one carrying it. This is why people came with the saying that ‘prepare a round pad, the luggage is heavy to carry’ to communicate preparedness in carrying out some duties.

This saying can be compared to a person who prepares well for the difficult task ahead of him/her. This person can gather all what is needed to make sure that he/she fulfills his/her ambition. This person is like the one who prepares a round head pad ready to undertake the duties ahead of him/her. Such a person teaches others the importance of preparing themselves in carrying out their responsibilities.

The saying teaches people how to prepare themselves before they embark on the actual performance of their duties. Preparedness can make someone have achievements in life.

Matthew 26: 36-46, Matthew 11:18, Ephesians 6:10, Mark 8:34.

649. LIMI LITABEHAGA BHUGOLO.

Imbuki ya lusumo lunulo, ilolile bhutumami bho limi. Ilimi linilo, ligatumamaga bho gutima pye amakanza, kunguno lidalindanaga lulu kiyi.  Ilyoyi ligenhaga isana ukubhose abho bhalilibhona bho nduhu ugwima, kunguno litiho nulu gwilendeja gubeha bhugolo. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘limi lidabehaga bhugolo.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatumamaga milimo bho bhukamu ahikanza lya milimo linilo, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agigulambijaga uguitumama imilimo yakwe yiniyo, kunguno adebhile igiki Ilimi lidalindanaga, iki ilyoyi lidabehaga nulu bhugolo. Uweyi agabhakomelejaga abhanhu bhakwe gwanguha kuja gujutumama milimo bho gumisha dilu, kugiki bhadule guitumama hatale imilimo yiniyo, hayo bhutali ugwila ubhujiku.

Umunhu ng’wunuyo, agapandika matwajo mingi ahakaya yakwe, kunguno ya gwigulambija gutumama milimo yakwe chiza ahikanza ilya limi. Uweyi agabhalanjaga abhiye ahigulya ya guitumama imilimo yabho, bho bhukamu bhutale ahikanza ilya milimo linilo. Hunagwene agabhakomelejaga gubhuka kuja kujutumama bho gubhawila giki, ‘limi lidabehaga bhugolo.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gwigulambija guitumama imilimo yabho ahikanza ilya milimo, na gubhakomeleja abhichabho gwanguha gujuitumama imilimo yiniyo, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi, umuwikaji bhobho.

Marko 13:33-37.

1 Wathesalonike 5:5-6.

Mathayo 6:34.

Luka 17:20-21.

2 Wakorintho 6:2.

2 Petro 3:8-9.

Yohana 9:4.

Wagalatia 6:9.

KISWAHILI: JUA HALIVUTI UGOLO.

Chanzo cha methali hiyo, chaangalia utendaji kazi wa Jua. Jua hilo, hufanya kazi ya kutoa mwanga muda wote, kwa sababu halisubiri chochote. Lenyewe huendelea kutoa mwanza wake bila kusimama, kwa sababu halivuti wala ugolo. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘Jua halivuti ugolo.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hutumia muda wake kwa hufanya kazi kwa bidii kubwa, katika maisha yake. Mtu huyo, hujibidisha kuyatekeleza majukumu yakwe hayo,  kwa sababu anaelewa kwamba, Jua halisuburi, kwa vile halivuti wala ugolo. Yeye huwahimiza watu wake kuwahi kwenda kufanya kazi, ili waweze kufanya kazi kubwa mpaga kufikia  wakati ule unapoingia usiku.

Mtu huyo, hupata mafanikio mengi kwenye familia yake, kwa sababu ya kujibidisha kwake, kuyatelekeza vizuri majukumu yake wakati wa kazi. Yeye huwafundisha wenzake juu ya kuutumia muda wao kwa kufanya kazi zao kwa bidii kubwa. Ndiyo maana yeye huwahimiza watu wake hao, kuwahi kwenda kazini kwa kusema kwamba, ‘Jua halivuti ugolo.’

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuutumia muda wao kwa kujibidisha kuyatekeleza majukumu yao, na kuwahimiza wenzao, kuwahi kwenda kazini, ili waweze kupata mafanikio mengi, maishani mwao.

Marko 13:33-37.

1 Wathesalonike 5:5-6.

Mathayo 6:34.

Luka 17:20-21.

2 Wakorintho 6:2.

2 Petro 3:8-9.

Yohana 9:4.

Wagalatia 6:9.

limi5

limi6

limi4

bhalimi1

 

ENGLISH: THE SUN DOES NOT SMOKE TOBACCO.

The source of this saying is the sun and its function. One of the central functions of the sun is to provide light. It does so tirelessly. It will never delay waiting for someone rather it works non-stop in its function. This is why people came with the saying that ‘The sun does not smoke tobacco’ to mean that the sun is busy all the time. It doesn’t delay like the way someone can do because of having other issues to deal with before embarking on his/her journey.

This saying can be compared to a person who spends his/her time working hard in his/her life. This person knows the value of time and he/she would struggle to make sure that he/she follows it well without any delay. Such a person encourages others to work hard in order to have great achievements in their lives.

This saying teaches people to spend their time well by fulfilling their responsibilities without wasting time for nothing. In so doing, they can have success in life.

Mark 13: 33-37,1Thessalonians 5: 5-6, Matthew 6:34, Luke 17: 20-21, 2Corinthians 6: 2, 2Peter 3: 8-9

      John 9: 4, Galatians 6: 9.

648. IGALASHU GASHI LYOCHI LYA NG´WISEGE LYAGUBEHA BHADAKI.

Imbuki ya kahayile kenako, yilolile igalashu. Iligalashu linilo, lili lisege ilo ligatumamilagwa mu gulibeha litumbati. Aliyo lulu, ilyochi lyalyo likab´izaga ikali gukila ilya mshigala. Hichene ligahayiyagwa giki, ‘Igalashu gashi lyochi lya ng’wisege lyagubeha bhadaki.’

Akahayile kenako, kagalenganijiyagwa  kuli munhu uyo agibhegelejaga chiza mpaka oitumama imilimo yakwe chiza, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agaitumamaga imilimo iyo ilidimu mpaga oyimala chiza kunguno, ya wibhegeleja bhokwe, haho atali uguyandya uguitumama imilimo yiniyo. Uweyi agajikumingaga pye ijitumamilo ijo jidulile ugumwambilija ijinagugumala wangu unimo gokwe gunuyo.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga ni igalashu, kunguno nuweyi alina bhudaki ubho uguitumama mpaga guimala imilimo yakwe yiniyo, umuwikaji bhokwe. Akikalile kakwe kagabhalanjaga abhiye inzila ja gwigulambija uguitumama imilimo yabho mpaga guimala chiza. Hunagwene abhanhu bhagang’witanaga giki, ‘Igalashu gashi lyochi lya ng’wisege lyagubeha bhadaki.’

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya gubhiza na bhukamu bho  gujikuminga pye ijitumamilo ja milimo yabho, haho bhatali uguyandya, na gwigulambija guitumama mpaga bhayimale chiza, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi, umuwikaji bhobho.

Luka 14:28-31.

Luka 4:1-5.

Mathayo 19:12.

KISWAHILI: IGALASHU KUMBE MOSHI WA KWENYE KIKO CHA KUVUTA WAKAKAMAVU.

Chanzo cha msemo huo, chaangalia igalashu. Igalashu hilo ni Kiko kinachotumiwa kuvitia tumbaku. Lakini moshi wake ni mkali kuliko ule wa sigara. Ndiyo maana watu husemwa kwamba, ‘Igalashu kumbe moshi wa kwenye Kiko cha kuvuta wakakamavu.’

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ana bidii ya kuzitekeleza vizuri kazi zake, katika maisha yake. Mtu huyo, hujiandaa vizuri kwa kuvikusanya vitendea kazi vinavyotakiwa katika utekelezaji wa kazi hiyo husika, kabla ya kuianza kuitekeleza. Yeye hujibidisha kuifanya kazi hiyo mpaka hufaulu kuimaliza, kwa sababu ya kufanya maandalizi mazuri kabla ya kuianza.

Mtu huyo, hufanana na wale wakakamavu, kwa sababu na yeye ni mkamavu katika utekelezaji wa majukumu yake, kwa vile hujibidisha kuzitekeleza kazi zake mpaka anafaulu kuzimalima vizuri.

Maisha yake, huwafundisha wenzake, juu ya kujibidisha kuyatekeleza majukumu yao hayo, mpaka kuyamaliza vizuri, maishani mwao. Ndiyo maana watu humuita kwamba, ‘Igalashu kumbe moshi wa kwenye Kiko cha kuvuta wakakamavu.’

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuwa na bidii ya kufanya maangalizi ya kuvikufanya vitendea kazi vyao, kabla ya kuanza kazi,  na kujibidisha kuzitekeleza mpaka kuzimaliza vizuri, ili waweze kupata mafanikio mengi, maishani mwao.

Luka 14:28-31.

Luka 4:1-5.

Mathayo 19:12.

isege6

isege10

isege9

 

ENGLISH: THE SMOKE FROM TOBACCO PIPE IS SMOKED BY BRAVE PEOPLE.

The source of this saying is tobacco pipe and its smoke. This tobacco pipe is said to produce bitter smoke when compared to that that comes from cigarattes. To be able to smoke one needs to be strong enough and courageous. This is why people came with this saying that ‘the smoke from tobacco pipe is smoked by brave people’ to communicate the bitterness of the smoke.

This saying can be compared to a person who has the ability to carry out his/her duties in his/her life. This person can prepare himself/herself well by gathering the necessary resources for the execution of his/her duties before commencing to carry it out. He/she takes care of the task until he/she finishes it. Such a person teaches others about responsibility and perseverance in life.

The saying teaches people how to be diligent in practicing their skills. They need to be tolerant in carrying out their duties in life.

Luke 14: 28-31, Luke 4: 1-5, Matthew 19:12.

647. IBHEGEJAGI GUTI NG’WANA O MBATA.

Mbuki ya kahayile kenako, ifumilile ku bhulekanija bho mbata ijinagubhelela abhana bhayo. Imbata yiniyo, idalelaga chiza abhana bhayo, na hangi idabhacholelaga ijiliwa, kunguno igikalaga idililile yoyi duhu. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘ibhegejagi guti bhana bha mbata.’

Akahayile kaneko, kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo adabhadililile chiza abhana bhakwe, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo adabhacholelaga ijiliwa abhana bhakwe bhenabho, kunguno ya gwikala widililile weyi duhu, umukikalile kakwe. Uweyi adabhalelaga bho gubhalanga ilange lya wiza abhana bhakwe bhenabho.

Umunhu ng’wunuyo, akikolaga ni mbata yiniyo iyo igabhalekanijaga abhana bhayo, kunguno nu weyi adabhalelaga chiza abhana bhakwe, iki agidililaga weyi duhu, umuwikaji bhokwe. Nuweyi adabhacholelaga ijiliwa abhana bhakwe bhenabho, guti ni mbata yiniyo. Hunagwene abhanhu bhagabhawilaga abhana bhakwe bhenabho giki, ‘ibhegejagi guti bhana bha mbata.’

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya gubhalelaga chiza na gubhacholela jiliwa abhana bhabho, kugiki bhadule kubhiza ni lange lya gwikala chiza na bhichabho, na guitumama milimo yabho chiza, umukikalile kabho.

2 Wakorintho 11:8-9.

Matendo 6:1.

1 Wathesalonike 3:6.

Mathayo 15:26.

KISWAHILI: JITEGEMEENI KAMA MTOTO WA BATA.

Chanzo cha msemo huo, chatokea kwenye utelekezaji wa bata katika kuwalea watoto wake. Bata huyo, hawalei vizuri watoto wake hao. Yeye pia hawatafutii chakula, kwa sababu ya kujijali yeye mwenyewe tu, katika maisha yake. Ndiyo maana watu huambiana kwamba, ‘jigetemeeni kama mtoto wa bata.’

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hawajali vizuri watoto wake, katika maisha yake. Mtu huyo, hawapatii malezi mema watoto wake hao. Yeye pia hawatafutii chakula, kwa sababu ya kujijali mwenyewe zaidi kuliko watoto wake hao, katika maisha yake.  

Mtu huyo, hufanana na Bata huyo atelekezaye watoto wake, kwa sabahu naye hawajali watoto wake kwa kuwalea katika maadili mema. Yeye pia hawatafutii chakula watoto wake hao kwa sababu ya kujijali yeye zaidi kuliko watoto wake, maishani mwake. Ndiyo maana watu huwaambia watoto wake hao kwamba, ‘jigetemeeni kama mtoto wa bata.’

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuwalea vizuri na kuwatafutia chakula watoto wao, ili waweze kupata malezi mema ya kuishi vizuri na kujibidisha kufanya kazi zao vizuri, katika maisha yao.

2 Wakorintho 11:8-9.

Matendo 6:1.

1 Wathesalonike 3:6.

Mathayo 15:26.

mbata8

mbata6

mbata2

ENGLISH: BE SELF-INDEPENDENT LIKE THE DUCK’S CHICKS.

The source of the saying is the chick of duck. Unlike hen, ducks tend to let their chicks free to look for their food. Duck’s chicks are made to struggle on their own without a help from their mothers. This is why people came up with this saying that ‘be self-independent like the duck’s chicks to imply dependence and personal struggle in achieving success in life.

This saying can be compared to a person who does not care well for his/her children in his/her life. Such a person does not provide food for his/her children thus letting them to suffer without any help. The person of this nature cares for himself/herself and ignores others.

The saying teaches people about how to properly nurture and feed their children so that they can have a good upbringing.

2 Corinthians 11: 8-9, Acts 6: 1, 1Thessalonians 3: 6, Matthew 15:26.

646. KALAGU – KIZE. BHANHYA BHAMILENGANILO:- MASHIGA.

Imbuki ya kalagu yiniyo, yingilile kukalenginilile ka wiyambilija bho katumamile ka mashiga. Amashiga genayo, gali mawe nulu madafali adatu ayo gagikalaga galenganilile chiza, kugiki gadule gudimila nungu, nulu sufulila iyaguzugila ijiliwa.

Ubhulenganiji bhogo bhunubho, bhulolile bhutale, nulu bhudoni ubho bhulinganilile.  Agoyi gagikolanijiyagwa na bhaniki, kunguno nabho bhagazugaga jiliwa aha kaya. Hunagwene abhanhu bhagiganilaga giki, ‘bhanhya bhamilenganilo:- Mashiga.’

Ikalagu yiniyo, igalenganijiyagwa kubhanhu abho bhalina ng’wigwano go gwiyambilija uguitumama imilimo yabho, umuwikaji bhobho. Abhanhu bhenabho, bhali na bhutogwa ubho bhugabhalumanyaga kihamo, umukikalile kabho. Abhoyi bhagapandikaga matwajo mingi, umumilimo yabho guti numo gagajisijaga ijiliwa amashiga genayo.

Abhanhu bhenabho, bhagikolaga na mashiga, kunguno nabho bhali na ng’wigwano go gwiyambilija halumo uguitumama chiza imilimo yabho, umukikalile kabho.

Abhoyi bhagalangaga na bhichabho, ahigulya ya gubhiza na bhutogwa bho gwiyambilija halumo ijinaguitumama chiza imilimo yabho yiniyo, umuwikaji bhobho. Hunagwene abhanhu bhenabho, bhagabhaganilaga abhichabho giki, ‘bhanhya bhamilenganilo:- Mashiga.’

Ikalagu yiniyo, yalanga bhanhu higulya ya gubhiza na ng’wigwano go gwiyambilija halumo uguitumama na bhutogwa imilimo yabho, kugiki bhadule gupandika matwaho mingi, umuwikaji bhobho.

Mathayo 28:16-20. Jiligemelo ja Utatu Mtakatifu.

KISWAHILI: KITENDAWILI – TEGA:-

WASICHANA WANAOLINGANA:- MAFIGA.

Chanzo cha kitendawili hicho, chatokea kwenye ulinganifu wa mafiga katika kusaidiana kufanya kazi. Mafiga hayo, ni mawe au matofali matatu yanayolingana vizuri, kiasi cha kutosha kukishikilia chungu au chombo cha kupikia chakula. Yenyewe huwa yamelingana kwa maana kwa kuwa na ukubwa unaoendana, au kama ni madogo, yote yawe udogo unaolingana.

Mafiga hayo, hufananishwa na wasichana kwa sababu nao hufanya kazi za kupika chakula katika familia.  Yenyewe, huacha nafasi katikati ambapo huwekwa kuni zinawashwa moto na kuendelea kuchochewa mpaka chakula kinaifa vizuri. Ndiyo maana watu huhadithiana kwamba, ‘washichana wanaolingana:-  Mafiga.’

Kitendawili hicho, hulinganishwa kwa watu wale ambao wana uelewano wa kusaidiana katika kufanya kazi zao. Watu hao, wana upendo ambao huwaunganisha pamoja, maishani mwao. Wao hupata mafanikio mengi katika utekelezaji wa majukumu yao, kama yanavyoivisha chakula Mafiga hayo.

Watu hao, hufanana na mafiga, kwa sababu nao, wana uelewano wa kusaidiana pamoja katika utekelezaji wa majukumu yao, maishani mwao. Wao huwafundisha pia wenzao, juu ya kuwa na upendo huo wa kusaidiana pamoja katika kuzitekeleza vizuri kazi zao. Ndiyo maana watu hao, huwahadithia wenzao kwamba, ‘washichana wanaolingana:-  Mafiga.’

Kitendawili hicho, hufundisha watu juu ya kuwa na ushirikiano wa kusaidiana pamoja katika utekelezaji wa majukumu yao, ili waweze kupata mafanikio mengi, maishani mwao.

Mathayo 28:16-20. Ni mfano wa Utatu Mtakatifu.

cooking1

mashiga1

mashiga

nzugi

ENGLISH: I HAVE A RIDDLE – LET IT COME.

THREE GIRLS OF SIMILAR ATTRIBUTES – THREE COOKING STONES.

The source of this riddle is the cooking stones. These stones always appear in the kitchen and one of their central functions is to hold a cooking pot or saucepan when cooking. These three cooking stones are characterized by having similar attributes; they have similar size and height in order to facilitate easy holding of the pot or saucepan.

The three stones are always arranged in such a way that they leave a space between them where one can make fire. This is why people came with this riddle ‘three girls of similar attributes – cooking stones’ to communicate the resemblance of cooking stones.

This riddle can be compared to people who tend to help each other in doing something. Such peple tend to regard themselves as one solid unit who can work together in order to achieve something of great impact to the society. These people also teach others about the need for helping each other in doing their jobs well.

This riddle teaches people about how to work together to help each other in fulfilling their responsibilities so that they can achieve more in their lives.

Matthew 28: 16-20. It is an example of the Holy Trinity.