Kashinje Zacharia

728. NAMUGI ADAB´IHAJA.

Akahayile kenako, kalolile munhu uyo alintale, nulu uyo ali namugi aha kaya yakwe. Olihoyi namhala umo uyo adimaga mitugo na bhana bhakwe. Lushigu lumo agajimija ng’ombe ubhabhuja abhana bhakwe, “nani uijimijije ing’ombe?” ung’wana ushosha, “ima lulu.” Unamhala ubhawila, “jaji mugaichole mpaga muyibhone.” Aho bhagaibhona bhudebha igiki unamhala huyo aijimija ng’ombe yiniyo, bhuyomba giki, “namugi adab’ihaja.”

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatumilaga bhutale bhokwe bho gubhaluhya abhanhu bhakwe. Umunhu ng’wunuyo, agabhutumilaga ubhutale bhunubho bho gubhubhisa ubhunhana, kunguno ya kulang’hana ikujo lwakwe. Uweyi agitaga giko bho gubhasayila salaga abhanhu bhakwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nu namhala uyo agajimija ng’ombe ubhasayila na gubhaluhya abhana bhakwe, kunguno nu weyi agabhaluhyaga abhanhu bhakwe bho gubhubhisa ubhung’hana. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “namugi agab’ihaga.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya gubhutumila chiza ubhutale bhobho, kugiki abhanhu bhabho bhadule gwikala na mholele ya gubhambilija guitumama chiza imilimo yabho. Abhanhu bhenabho igelelilwe bhabhize ni kujo kubhanhu bhose.

Zaburi 2:1-12.

Waebrania 6.1-4.

Ayubu 32:6b-7.

KISWAHILI: MZEE WA FAMILIA HAKOSEI.

Msemo huo, huangalia mtu yule ambaye ni mwenye madaraka au baba wa familia. Alikuwepo mzee mmoja aliyekuwa anachunga mifugo na watoto wake. Siku moja, alipoteza ng’ombe akawauliza watoto wake, “nani amepoteza ng’ombe?” Mmoja wa watoto akajibu, “simfahamu?” Akawambia, “nendeni mukamtafute mpaka mmuone.” Walipomuona waligundua kwamba, baba yao ndiye aliyempotea huyo ng’ombe, wakasema, “mzee wa familia hakosei.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huyatumia madaraka yake kwa kuwakandamiza watu wake. Mtu huyo, hutumia madaraka au nafasi yake hiyo katika kuuficha ukweli, kwa lengo la kulinda heshima yake mbele ya watu. Yeye huwalaimu hovyo watu wake.

Mtu huyo, hufanana na mzee mwenye watoto aliyepoteza ng’ombe akawasingizia watoto wake, kwa sababu naye huitumia nafasi yake ya ukubwa katika kuwakadamiza wale walioko chini yake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba,  “mzee wa familia hakosei.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuitumia vizuri nafasi yao ya uongozi, ili waweze kuishi kwa amani ya kuwezesha kuyatekeleza vizuri majukumu yao. Watu hao, wanatakiwa kuwa na heshima kwa watu wote wanaoishi nao.

Zaburi 2:1-12. “Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na mataifa kula njama bure? Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya BWANA na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake. Wanasema, ‘‘Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.’’ Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau. Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema, “Nimemweka Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.’’ Nitatangaza amri ya BWANA : yeye aliniambia, “Wewe ni mwanangu, leo nimekuwa Baba yako. Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa mali yako. Utawatawala kwa fimbo ya kifalme ya chumana kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.’’ Kwa hiyo, ninyi wafalme, iweni na hekima, mwonyeke, enyi watawala wa dunia. Mtumikieni BWANA kwa hofu na mshangilieni kwa kutetemeka. Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.”

Yoshua Bin Sira 3:12-14. “Mwanangu, umsaidia baba yako katika uzee wake, wala usipate kumhuzunisha siku zote za maisha yake. Akiwa amepungukiwa na ufahamu umwie kwa upole, wala usimdharau iwapo wewe u mzima sana; kwa maana sadaka apewayo baba haitaswahauliwa, na badala ya dhambi itahesabiwa kwa kukuthibitisha; ”

Waebrania 6.1-4. “Kwa hiyo, tukiachana na mafundisho yale ya awali kuhusu Kristo na tusonge mbele ili tufikie utimilifu, si kuweka tena msingi wa mafundisho ya kuzitubia kazi zisizo na uhai na imani katika Mungu, yaani, mafundisho kuhusu mabatizo, kuwekea watu mikono, ufufuo wa wafu na hukumu ya milele. Mungu akitujalia tutafanya hivyo. Kwa kuwa ni vigumu kuwarejeza tena katika toba wale ambao wakati fulani walishapata nuru, ambao walishaonja kipawa cha mbinguni, ambao wamekwisha kushiriki katika Roho Mtakatifu.”

Ayubu 32:6b-7. “Mimi ni mdogo kwa umri, ninyi ni wazee, ndiyo sababu niliogopa, sikuthubutu kuwaambia kile ninachojua. Nilifikiri, ‘Yafaa umri useme, nao wingi wa miaka ungefundisha hekima.’”

hunters nature

familiy africa

ENGLISH: THE FATHER OF THE FAMILY DOES NOT MAKE MISTAKES.

This saying refers to the person who is in charge of something or the father of the family. There was an old man who was tending cattle and his children. One day, he lost a cow and asked his children, “Who has lost this cow?” One of the children replied, “I don’t know” He told them, “Go and look for her until you find her.” When they saw her, they realized that their father was the one who had lost the cow, and they said, “The father of the family does not make mistakes.

This saying is used to refer to a person who uses his power to oppress his people. That person uses his position to conceal the truth, with the aim of protecting his dignity before the public eye. He falsely accuses his people.

Such man is like the father who had children and lost his cattle, but never admitted that he had done so instead he shifted the blame to his children. That is why people have a saying, “The father of the family does not make mistakes”

This saying, teaches people how to make good use of their leadership position, so that they can live in peace to enable them to carry out their responsibilities effectively. Such people have to be respectful to all the people who live with them.

Psalm 2: 1-12, Joshua Bin Sira 3: 12-14, Hebrews 6.1-4, Job 32: 6b-7.

726. OB´IB´ILA MU MHAGALE.

726. OB´IB´ILA MU MHAGALE.

Ulusumo lunulo, lulolile bhub’ib’i bho mbiyu mu mhagale. Imhagale gali manumba ayo gatali ugushila uguzengwa. Olihoyi munhu uyo agab’ib’a mbiyu jakwe umu mhagale jinijo aliganika giki adulile gubisha jiliwa moyi. Aho oduma ugubhona solobho yose yose wibhuja, “nibhuli nagaiwa solobho yose yose umubhutumami bhone?” Abhiye bhung’wila giki, “ob’ib’ila mu mhagale.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agahoyelaga mihayo iyo itina solobho yose yose, umuwikaji bhokwe. Umunhu ng’wunuyo, agajimijaga makanza gakwe sagala, kunguno adapandikaga ginhu ijo jidulile gung’wambilija umuwikaji bhokwe. Uweyi agabhalendejaga na  bhiye bhaduma uguitumama imilimo yabho, kunguno ya guhoyela mihayo iyo idadulile ugubhambilija jose jose.

Umunhu ung’wunuyo, agikolaga nu uyo ob’ib’ila mbiyu jakwe mu mhagale, kunguno nang’hwe adapandikaga solobho yose yose, umuwikaji bhokwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “ob’ib’ila mu mhagale.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya guhoyela mihayo ya gubhambilija ugujibheja chiza ikaya jabho, kugiki bhadule gupandika solobho ya gubhulang’hana chiza ubhupanga bho bhanhu bhabho, umuwikaji bhobho

Mathayo 13:5-7.

KISWAHILI: ULIPANDIA KWENYE MAPAGALE.

Methali hiyo, huangalia usiaji wa mbegu kwenye mapagale. Mapagale ni majengo yale ambayo hayajaisha kujengwa. Alikuwepo mtu mmoja ambaye alisia mbegu kwenye mapagale akitumainia kupata mazao kutoka humo. Alipokosa kupata faida yoyote, alijiuliza, “kwa nini nimekosa faida yoyote kwenye utendaji wangu wa kazi?” Wenzake walimjibu kwamba, “ulipandia kwenye mapagale.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hutumia muda wake katika huongelea maneno yasiyo na faida yoyote kwenye maisha yake. Mtu huyo, huupoteza hovyo muda wake kwa sababu huwa hapati kitu kinachoweza kumsaidia katika maisha yake. Yeye huwachelewesha hata wenzake kufanya kazi zao kwa sababu ya kuendelea kuwaongelesha maneno yasiyoweza kuwasaidia chochote.

Mtu huyo, hulingana na mtu aliyepanda mbegu kwenye mapagale, kwa sababu naye hakuweza kupata faida yoyote, katika maisha yake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “ulipandia kwenye mapagale.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuutumia muda wao katika kuongelea maneno yawezayo kuwaletea mandeleo kwenye familia zao, ili waweze kupata faida ya kuyalinda na kuyaendeleza vizuri maisha yao.

Mathayo 13:5-7. “Nyingine zikaanguka sehemu yenye mawe, ambapo hapana udongo mwingi. Zikaota haraka kwa sababu udongo ulikuwa hauna kina. Lakini jua lilipozidi, mimea hiyo ilinyauka na kukauka kwa sababu mizizi yake haikuwa na kina. Mbegu nyingine zilianguka katikati ya miiba, miiba hiyo ikakua ikazisonga.”

planting nimi nkima

ENGLISH: YOU PLANTED YOUR SEED IN AN UNFINISHED HOUSE.

There was one man who sowed seeds in the fields, hoping to get some produce from it. When he did not get any benefit, he asked himself, “Why have I missed any benefit in my career?” His colleagues replied, “You planted seeds in an unfinished house.”

This proverb is likened with a man who spends his time by talking nonsense in his life. Such person wastes his time carelessly because he does not find anything that will help him in his life. He delays even his colleagues from doing their work because he continues to speak words that do not help them at all.

The man is like the one who sowed seed in an unfinished house, because he did not have the benefit of it in his life. That’s why people say to him, “you planted you see in an unfinished house.”

This proverb teaches people how to spend their time by talking about words that can bring development to their families, so that they can reap the benefits of protecting and improving their lives.

Matthew 13: 5-7.

725. MIBHI UNGI NU NG´HELEMBI UNGI (MIBHI UNGI NU NIMI UNGI).

Olihoyi munhu uyo agalima ngunda ntale na ujibhibha imbiyu chiza. Imbiyu jinijo aho ja jukula agailimila ingeze ya ngunda gunuyo mpaka uyimala. Oho japya ijiliwa jinijo ijamungunda gokwe gunuyo, agazumalika umunhu ng’wunuyo. Unhekela munhu ungi uyo agajihelemba ijiliwa jinijo na gwandya gujilya. Abhanhu aho bhabhona shene, bhuyomba giki, “mibhi ungi nu ng’helembi ungi (mibhi ungi nu nimi ungi).”

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agukoyakoyelaga ginhu jose jose umuwikaji bhokwe. Aliyo lulu ulu ugajipandika isabho ijagufumila umunimo gunuyo, agakijaga ugujitumamila hamo kunguno ya gwinga kuwelelo, nulu gusamijiwa kungi uko adikomile ugujiyegela ijo ujikoyelaga. Iginhu jinijo jigatumamilagwa na bhanhu bhangi abho bhadajikoyelile.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nu mibhi o mbiyu uyo agajikoyelaga ijikolo ijo adajitumilaga ulu japya, kunguno nu weyi agabhalekelaga bhanhu bhangi,  bhajitumamila abho bhadajikoyelile.  Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “mibhi ungi nu ng’helembi ungi (mibhi ungi nu nimi ungi).”

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya gwitolea gubhatumamila bhichabho umuwikaji bhobho, kugiki bhadue gupandika matwajo mingi, ayo gadulile gujibheja chiza ikaya jabho. Igelelilwe bhajileke inhungwa jagwiiganika bhoyi duhu, umuwikaji bhobho.

Waefeso 5:32.

Yohana 3:25.

Yahana 4:37-38.

1 Wakorintho 3:6-9.

Luka 10:2.

Wagalatia 6:7-9.

 

MPANDAJI MWINGINE NA MVUNAJI MWINGINE (MPANDAJI MWINGINE NA MLIMAJI MWINGINE.

Alikuwepo mtu mmoja aliyelima shamba kubwa, akamwaga mbegu vizuri. Zilipoota mbegu hizo aliipalilia palizi mpaka akaimaliza. Yalipoiva mazao yake, mtu huyo alifariki dunia. Akamwachia mtu mwingine ambaye aliyavuna mazao hayo na kuanza kuyatumia. Watu walipoona vivyo, walisema kwamba, “mpandaji mwingine na mvunaji mwingine (mpandaji mwingine na mlimaji mwengine).”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huhangaika kuifanya kazi fulani ambayo matunda yake hushindwa kuyafaidi, maishani mwake. Mtu huyo, hufanya kazi kwa bidii sana mpaka akafikia hatua ya kuanza kuyatumia matunda ya kazi yake hiyo. Lakini kabla ya kuanza kuyatumia matunda hayo, mtu huyo, ama hufariki dunia au huhamishwa na kupelekwa sehemu ambayo hushindwa kuyafaidi matunda ya kazi yake hiyo aliyoihangaikia.

Mtu huyo hufanana na mpandaji wa mbegu katika shamba ambaye alilitunza shamba lake mpaka apata mavuno mengi ambayo aliwaachia wengine wakayafaidi, kwa sababu naye huyu aliwaachiwa wengine wakafaidi matunda ya kazi hiyo, aliyoihangaikia. Ndiyo maana watu husema kwamba, “mpandaji mwingine na mvunaji mwingine (mpandaji mwingine na mlimaji mwingine).”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kujitolea kufanya kazi kwa ajili ya wenzao maishani mwao, ili waweze kupata mafanikio mengi zaidi yawezayo kuziendeleza vizuri familia zao.

Waefeso 5:32. “Siri hii ni kubwa, bali mimi nanena kuhusu Kristo na Kanisa.”

Yohana 3:25. “Mashindano yakazuka kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi mmoja kuhusu suala la desturi ya kunawa.”

Yahana 4:37-38. “Hivyo kule kusema, ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna,’ ni kweli kabisa. Niliwatuma mkavune mazao ambayo hamkupanda, wengine walifanya kazi ngumu, nanyi mmevuna faida ya taabu yao.”

1 Wakorintho 3:6-9. “Mimi nilipanda mbegu, Apolo akatia maji, lakini Mungu ndiye aliyekuza. Hivyo mwenye kupanda mbegu na mwenye kutia maji si kitu, bali Mungu peke Yake ndiye akuzaye. Apandaye mbegu ni sawa na yule atiaye maji. Kila mmoja atalipwa kulingana na kazi yake. Sisi ni watenda kazi pamoja na Mungu, ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu.”

Luka 10:2. “Akawaambia, “Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache. Kwa hiyo mwombeni Bwana wa mavuno, awapeleke watenda kazi katika shamba lake.”

Wagalatia 6:7-9. “Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi. Kwa kuwa kile apandacho mtu ndicho atakachovuna. Apandaye kwa mwili, katika mwili wake, atavuna uharibifu, lakini yeye apandaye katika Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele. Hivyo, tusichoke katika kutenda mema, kwa kuwa tutavuna kwa wakati wake tusipokata tamaa.”

nkima na milimo

ENGLISH: THE PLANTER IS NOT NECESSARILY THE REAPER

There was a man who plowed a great field and sowed good seeds. When the seeds sprouted, he weeded out the weed making his crops clean.  Unfortunately, when his crops ripened, the man died. He left his field to someone who harvested the crops and began to use them. When the people saw him they all said, “The planter is not necessarily the reaper.”

This proverb is likened with a man who struggles with a desire to accomplish something in his life. Such a man works very hard until he reaches the point where he begins to use the fruits of his labour. But before one begins to use the fruit, the person either dies or is transferred to a place where he is unable to enjoy the fruits of his labour.

 Such a man is like a man who sowed seed in his field, but he did not reap what he had sown. That is why people say, “The planter is not necessarily the reaper.”

This proverb teaches people about volunteering to work for others in their lives, so that they can achieve more success that can make their families live better life

Ephesians 5:32. John 3:25. John 4: 37-38. 1 Corinthians 3: 6-9. Luke 10: 2. Galatians 6: 7-9.

724. UGUKOYAGA NA TEMBE ING´OMBE JACHILULAGA.

Ulusumo lunulo, lwingila kuli munhu uyo ocholaga gupandika ng’ombe  mulugutu lo ng’ombe, umujigalalilaga. Umunumo jigalekaga tembe iyo adulile umunhu nulu gulibhila amagulu gakwe uyo wingila moyi.

Umunhu ng’wunuyo agayukoya ugugafunya amagulu gakwe kunguno ya gulibhila umutembe ija ng’ombe ijojalijachilulwa jugading’wa. Agang’wila ung’wiye uyo bhali nawe, “ahenaha jilihoyi ing’ombe ningi noyi kunguno itembe jiniji jiliningi mpaga nalikoya ugugafunya amagulu gane.” Ung’wiye aganshokeja aliyomba, “ugukoyaga na tembe ing’ombe jachilulaga.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatumamaga nimo uyo gudina na solobho yose yose. Umunhu ng’winuyo agajimijaga makanza gakwe bho nduhu solobho, ukunhu alijimala sagala ninguzu jakwe. Uweyi agamalaga nguzu jakwe bho nduhu gupandika solobho yose yose.

Umunhu ng’wunuyo, agatumamaga nimo uyo gudikilile nu munhu uyo agukoyelaga tembe ja ng’ombe umo jitiho ing’ombe jinijo. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga umunhu ng’wunuyo giki, “ugukoyaga na tembe ing’ombe jachilulaga.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kuleka gutumama milimo iyo idina solobho yose yose, kunguno bhagujimija makanza gabho sagala. Gashinaga lulu, igelelilwe bhaisolanye imilimo iyo idulile gubhenhela solobho ningi, umuwikaji bhobho, hunabhayitumama lulu iyiniyo.

Mathayo 13:5-7.

Wagalatia 6:7-10.

UNAHANGAIKA NA TOPE (KINYESI CHA NG’OMBE) NG’OMBE WAMEENDA MACHUNGANI.

Methali hiyo ilianzia kwa mtu aliyekuwa akitafuta kupata ng’ombe, akiwa ndani ya zizi la ng’ombe waliokuwa wameenda machungani. Kwenye zizi hilo, kulikuwepo na tope la kinyesi cha ng’ombe la kuzamisha miguu yake yule anayeingia

Mtu huyo, alianza kuhangaika kuitoa miguu yake kwenye matope hayo kwa sababu ilikuwa imezama kwenye zizi hilo la ng’ombe waliokuwa wameenda machungani. Alimwambia mwenzake, “hapa pana ng’ombe wengi sana kwa sababu ya kinyesi au tope hili kuwa jingi mpaka nahangaika kuitoa miguu yangu.” Mwenzake akamjibu akisema, “unahangaika na tope (kinyesi cha ng’ombe) ng’ombe wameenda machungani.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hufanya kazi isiyo na faida yoyote. Mtu huyo, hupoteza wakati wake bure, huku akizimaliza hovyo nguvu zake hizo. Yeye huzimaliza nguvu zake hizo kwa kuifanya kazi hiyo kwa muda mrefu na bila faida yoyote.

Mtu huyo, hufananishwa na mtu anayehangaika na kinyesi cha ng’ombe kilichoachwa zizini na ng’ombe walioenda kuchungwa. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “unahangaika na tope (kinyesi cha ng’ombe) ng’ombe wameenda machungani.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuacha kupoteza muda wao katika kufanya kazi isiyo na faida yoyote, maishani mwao. Kumbe basi, wanatakiwa kuzifanyia utafiti kazi zao, ili waweze kuzichagua na kuzitekeleza zile zinazowaletea faida katika kuziendeleza familia zao.

Mathayo 13:5-7. “Nyingine zikaanguka sehemu yenye mawe, ambapo hapana udongo mwingi. Zikaota haraka kwa sababu udongo ulikuwa hauna kina. Lakini jua lilipozidi, mimea hiyo ilinyauka na kukauka kwa sababu mizizi yake haikuwa na kina. Mbegu nyingine zilianguka katikati ya miiba, miiba hiyo ikakua ikazisonga.”

Wagalatia 6:7-10. “Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi. Kwa kuwa kile apandacho mtu ndicho atakachovuna. Apandaye kwa mwili, katika mwili wake, atavuna uharibifu, lakini yeye apandaye katika Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele. Hivyo, tusichoke katika kutenda mema, kwa kuwa tutavuna kwa wakati wake tusipokata tamaa. Kwa hiyo, kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema, hasa wale wa jamaa ya waaminio.”

cow2

ENGLISH: YOU ARE STRUGGLING TO FREE YOURSELF FROM THE COW DUNG BUT THE CATTLE HAVE GONE TO THE PASTURES

This proverb is tailored around a man who was looking for cattle, in a cowshed but the cattle were not there. They had gone to the pasture in the plains. They had left behind a mountain of fresh cow dung which made him stuck into it to the point of failing to get out of it

 Seeing that the cattle he was looking for were not there and having been stuck his feet being stuck in the mud, he began struggling to get them out of the fresh cow doing.  Seeing the amount of fresh dung, he told his colleague, “There must be many many cows in this shed because of the amount of cow dung I See. Look, this cowdung is so thick that I am not sure to get my feet out of it.” His companion replied, “You are so obsessed with the mere cow dung. Remember the cattle have gone to the pastures.”

This proverb is likened with a man who works in vain. Such man wastes his time as well as his energy.

 Someone who wastes his energy and time for nothing is likened with a man who is struggling to get out of fresh cowdung left in the cowshed by the cattle which have gone to pasture

This proverb teaches people to stop wasting their time by doing useless work, in their lives. Therefore, they need to choose and implement only those activities that can benefit them in the development of their families.

Matthew 13: 5-7 Galatians 6: 7-10.

723. OSHELA HA NYAGA.

Oliho mayu umo uyo oshaga bhusiga, aliyo lulu oshelaga haluyaga. Ubhufu bhokwe bhomanaga bhuchalwa na luyaga. Aho omala ugusha wisanga bhoshilaga guchalwa na nyaga ubhufu bhoke. Aho obhugaiwa ubhufu agayomba, “nanoga bhure kunguno nu bhufu nagaiwa.” Abhiye bhung’wila giki, “oshela ha nyaga.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatumamaga nimo uyo gudina na solobho yose yose. Umunhu ung’winuyo agajimijaga makanza gakwe bhure ukunhu alijimala sagala inguzu jakwe. Uweyi agamalaga nguzu jakwe bho nduhu gupandika solobho yose yose.

Umunhu ng’wunuyo, agatumamaga nimo uyo gudikilile na munhu uyo alishela bhusiga bhokwe ha nyaga aho bhugamanaga bhuchalwa ubhusu ubho alibhusha. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga umunhu ng’wunuyo giki, “oshela ha nyaga.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kuleka gutumama milimo iyo idina solobho yose yose, kunguno bhagujimija makanza gabho sagala. Gashinaga lulu, igelelilwe bhaisolanye imilimo iyo idulile gubhenhela matwajo mingi, umuwikaji bhobho, hunabhayitumama lulu iyiniyo.

Mathayo 13:5-7.

Wagalatia 6:7-10.

KISWAHILI: UMESAGIA KWENYE UPEPO.

Alikuwepo mama mmoja ambaye alikuwa anasaga mtama, lakini alikuwa anasagia kwenye upepo. Unga wake ulikuwa ukichukuliwa na upepo. Alipomaliza kusaga akajikuta hana unga, akasema, “nimechoka bure na unga nimekosa.” Wenzake wakamwambia kwamba, “umesagia kwenye upepo.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hufanya kazi isiyo na faida yoyote. Mtu huyo, hupoteza wakati wake bure huku akizimaliza hovyo nguvu zake hizo. Yeye huzimaliza nguvu zake hizo kwa kuifanya kazi hiyo kwa muda mrefu na bila faida yoyote.

Mtu huyo, hufanya kazi ambayo haiko tofauti na mtu aliyesagia mtama wake kwenye upepo ambao ulikuwa unauchukua unga wake aliokuwa akiusaga. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “umesagia kwenye upepo.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuacha kupoteza muda wao katika kufanya kazi isiyo na faida yoyote maishani mwao. Kumbe basi, wanatakiwa kuzifanyia utafiti kazi zao, ili waweze kuzichagua na kuzitekeleza zile zinazowaletea faida katika kuziendeleza familia zao.

Mathayo 13:5-7. “Nyingine zikaanguka sehemu yenye mawe, ambapo hapana udongo mwingi. Zikaota haraka kwa sababu udongo ulikuwa hauna kina. Lakini jua lilipozidi, mimea hiyo ilinyauka na kukauka kwa sababu mizizi yake haikuwa na kina. Mbegu nyingine zilianguka katikati ya miiba, miiba hiyo ikakua ikazisonga.”

Wagalatia 6:7-10. “Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi. Kwa kuwa kile apandacho mtu ndicho atakachovuna. Apandaye kwa mwili, katika mwili wake, atavuna uharibifu, lakini yeye apandaye katika Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele. Hivyo, tusichoke katika kutenda mema, kwa kuwa tutavuna kwa wakati wake tusipokata tamaa. Kwa hiyo, kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema, hasa wale wa jamaa ya waaminio.”

mayu nshi

stone-grinding.1

ENGLISH: YOU HAVE GROUND YOUR FLOUR WHILE FACING THE WIND.

There was a mother who was grinding millet on her grinding stone while facing the wind. Therefore, her flour was being carried away by the wind in the process.When she finished grinding, she found that she had no flour, and she said, “I am tired and I have no flour.” Her companions told her, didn’t you see? You were grinding while exposed to the wind” “

This proverb is likened with a person who works in vain. Such person wastes his time and energy by working without any benefit. He completes his task by working for a long time but to no avail.

The person who does such a job is like the one who grinds his millet while exposed to the wind that blows all the flour one is grinding. That is why people say, “You ground your millet while exposed to the wind.”

This proverb teaches people to stop wasting their time doing useless things in their lives. Therefore, they need to be discriminating in their practices by choosing only those activities that bring them benefits

Matthew 13: 5-7.Galatians 6: 7-10.