Oliho mayu umo uyo oshaga bhusiga, aliyo lulu oshelaga haluyaga. Ubhufu bhokwe bhomanaga bhuchalwa na luyaga. Aho omala ugusha wisanga bhoshilaga guchalwa na nyaga ubhufu bhoke. Aho obhugaiwa ubhufu agayomba, “nanoga bhure kunguno nu bhufu nagaiwa.” Abhiye bhung’wila giki, “oshela ha nyaga.”
Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatumamaga nimo uyo gudina na solobho yose yose. Umunhu ung’winuyo agajimijaga makanza gakwe bhure ukunhu alijimala sagala inguzu jakwe. Uweyi agamalaga nguzu jakwe bho nduhu gupandika solobho yose yose.
Umunhu ng’wunuyo, agatumamaga nimo uyo gudikilile na munhu uyo alishela bhusiga bhokwe ha nyaga aho bhugamanaga bhuchalwa ubhusu ubho alibhusha. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga umunhu ng’wunuyo giki, “oshela ha nyaga.”
Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kuleka gutumama milimo iyo idina solobho yose yose, kunguno bhagujimija makanza gabho sagala. Gashinaga lulu, igelelilwe bhaisolanye imilimo iyo idulile gubhenhela matwajo mingi, umuwikaji bhobho, hunabhayitumama lulu iyiniyo.
Mathayo 13:5-7.
Wagalatia 6:7-10.
KISWAHILI: UMESAGIA KWENYE UPEPO.
Alikuwepo mama mmoja ambaye alikuwa anasaga mtama, lakini alikuwa anasagia kwenye upepo. Unga wake ulikuwa ukichukuliwa na upepo. Alipomaliza kusaga akajikuta hana unga, akasema, “nimechoka bure na unga nimekosa.” Wenzake wakamwambia kwamba, “umesagia kwenye upepo.”
Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hufanya kazi isiyo na faida yoyote. Mtu huyo, hupoteza wakati wake bure huku akizimaliza hovyo nguvu zake hizo. Yeye huzimaliza nguvu zake hizo kwa kuifanya kazi hiyo kwa muda mrefu na bila faida yoyote.
Mtu huyo, hufanya kazi ambayo haiko tofauti na mtu aliyesagia mtama wake kwenye upepo ambao ulikuwa unauchukua unga wake aliokuwa akiusaga. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “umesagia kwenye upepo.”
Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuacha kupoteza muda wao katika kufanya kazi isiyo na faida yoyote maishani mwao. Kumbe basi, wanatakiwa kuzifanyia utafiti kazi zao, ili waweze kuzichagua na kuzitekeleza zile zinazowaletea faida katika kuziendeleza familia zao.
Mathayo 13:5-7. “Nyingine zikaanguka sehemu yenye mawe, ambapo hapana udongo mwingi. Zikaota haraka kwa sababu udongo ulikuwa hauna kina. Lakini jua lilipozidi, mimea hiyo ilinyauka na kukauka kwa sababu mizizi yake haikuwa na kina. Mbegu nyingine zilianguka katikati ya miiba, miiba hiyo ikakua ikazisonga.”
Wagalatia 6:7-10. “Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi. Kwa kuwa kile apandacho mtu ndicho atakachovuna. Apandaye kwa mwili, katika mwili wake, atavuna uharibifu, lakini yeye apandaye katika Roho, katika Roho atavuna uzima wa milele. Hivyo, tusichoke katika kutenda mema, kwa kuwa tutavuna kwa wakati wake tusipokata tamaa. Kwa hiyo, kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema, hasa wale wa jamaa ya waaminio.”
ENGLISH: YOU HAVE GROUND YOUR FLOUR WHILE FACING THE WIND.
There was a mother who was grinding millet on her grinding stone while facing the wind. Therefore, her flour was being carried away by the wind in the process.When she finished grinding, she found that she had no flour, and she said, “I am tired and I have no flour.” Her companions told her, didn’t you see? You were grinding while exposed to the wind” “
This proverb is likened with a person who works in vain. Such person wastes his time and energy by working without any benefit. He completes his task by working for a long time but to no avail.
The person who does such a job is like the one who grinds his millet while exposed to the wind that blows all the flour one is grinding. That is why people say, “You ground your millet while exposed to the wind.”
This proverb teaches people to stop wasting their time doing useless things in their lives. Therefore, they need to be discriminating in their practices by choosing only those activities that bring them benefits
Matthew 13: 5-7.Galatians 6: 7-10.