heritage

508. KALAGU – KIZE. NANIKILA BHUCHELE BHUJIKU, WELA NABHUGAYIWA:- SONDA.

Imbuki ya kalagu yiniyo yilolile sonda. Isonda jili ginhu jilabhangizu, ijo jigikalaga ng’wigulya. Ijoyi jigigelaga bhujiku, ulu wela jidigelaga. Hunagwene abhanhu bhagiganilaga giki, ‘nanikila bhuchele bhujiku, wela nabhugayiwa’ bhashosha, ‘Sonda’.

Ikalagu yiniyo igalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagahayoga kihamo ibhujiku, ulu bhalipanga imilimo ya ntondo iyahakaya yabho. Abhanhu bhenabho bhagabhejaga mahoya gabho genayo bhujiku kugiki, bhuli ng’wene apangilwe guja gujutumama nimo halebhe, ulu wela ubhujiku.

Ulu wela ubhujiku bhunubho, bhuli ng’wene agajaga uko opangilagwa nabhiye ibhujiku ni kaya yiniyo. Hunagwene abhanhu bhenabho, bhagikolaga ni sonda ijo jigigelaga bhujibu iki nabho bhagahoyaga bhujiku, ulu bhalipanga imilimo yabho iya ntondo. Ulu wela ubhujibu, bhagabalasanaga guja kumilimo yabho, guti ni sonda ijo jidigelaga ulu wela ubhujiku. Hunagwene abhanhu bhagiganilaga giki, ‘nanikila bhuchele bhujiku, wela nabhugayiwa’ bhashosha, ‘Sonda.’

Ikalagu yiniyo yalanga bhanhu  gugabhana milimo yabho ibhujiku halumo, kugiki ulu wela, bhuli ng’wene aje agagutumame chiza unimo uyo opangilagwa nabhiye ahakaya yiniyo. Ubhugabhanhi bho milimo yiniyo bhugubhambilija ijinagupandika matwajo mingi, agagujilanghanila ikaya jabho.

(Kutoka 12: 40-42; Mathayo 5: 13-16; Mathayo 10: 26-22).

KISWAHILI: KITENDAWILI   –   TEGA: NILIANIKA MCHELE USIKU, KUMEKUCHA NIKAUKOSA – NYOTA.

Chanzo cha kitendawili hicho chaangalia nyota. Nyota ni vitu vinavyometameta ambavyo huonekana juu angani wakati wa usiku. Usiku ukicha, huwa hazionekani. Ndiyo maana watu hutegeana kitendawili kwamba, ‘nimeanika mchele usiku, kumekucha nikaukosa’ na kujibu, ‘Nyota’.

Kitendawili hicho chalinganishwa kwa watu ambao huongea kwa pamoja nyakati za usiku, kila wanapopanga mgawanyo wa kazi zao za siku inayofuta. Watu hao huendesha maongezi yao usiku ili kila mmoja aweze kupangiwa majukumu ya kutekeleza siku ifuatayo, kwa ajili ya kuwawezesha wote kupata mafanikio mengi maishani mwao.

Hivyo, usiku ukicha, kila mmoja huenda kule alikopangiwa na kikao cha usiku. Ndio maana watu hao hufananishwa na nyota ambazo huonekana usiku, kwa vile wao huongea usiku wanapopanga kazi za kila mmoja zitakiwazo kutekelezwa siku inayofuta.

Usiku ukicha, wao hutawanyika kwenda kule ambako kila mmoja amepangiwa kwenda kufanyia kazi yake na kutoweka kama vile nyota ambazo huwa hazionekani usiku unapokucha. Ndiyo maana watu hutegeana kitendawili kwamba, ‘nimeanika mchele usiku, kumekucha nikaukosa’ na kujibu, ‘Nyota’.

Kitendawili hicho chafundisha watu kuwa na umoja wa kugawana majukumu yao nyakati za usiku, ili kila mmoja aweze kuyatekeleza vizuri na kwa wakati unaotakiwa. Mgawanyo huo wa kazi utawasaidia katika kupata mafanikio mengi yawawezeshayo kuziendesha vizuri familia zao.

(Kutoka 12: 40-42; Mathayo 5: 13-16; Mathayo 10: 26-22).

rice

ENGLISH: I HAVE A RIDDLE- LET IT COME: I PUT OUT RICE TO DRY LAST NIGHT, BUT IT WENT MISSING IN THE MORNING – STARS.

The origin of this riddle relates to the stars. Stars are twinkling objects that appear in the sky at night. When it dawns, they become invisible. That is why people pose a riddle, ‘I put out rice to dry last night, but it went missing in the morning’ and respond, ‘stars’.

The riddle is comparatively used with reference to people who talk together at night times as they plan their day-to-day work assignments. These people hold their conversations at night times so that each one can be assigned the tasks to perform the following day to enable them all achieve more in life.

So, when it dawns, everyone disappears and goes to their duty post assigned to them last night. That is why such people are like the stars that appear at night, because they carry out their planning talks at night times as they plan each other’s tasks to perform when it dawns.

When it dawns, they disperse to each one’s duty post as assigned such that they are invisible at home, just like what stars do when it dawns. That is why people pose a riddle that ‘I put out rice to dry last night, but it went missing in the morning’ and reply, ’Stars’.

This riddle teaches people to be united in sharing their responsibilities at night, so that everyone can carry out the tasks at the right time. This division of labour will help them in achieving their plans and recording notable successes, which in turn enables them to manage their families well as they deserve.

(Exodus 12: 40-42; Matthew 5: 13-16; Matthew 10: 26-22).

507. SHINGWAGULAMIWA.

Imbuki ya kahayile kenako yilolile Ntale uyo agalamiwagwa na bhanhu. Ung’wenuyo hu Mulungu ng’winikili, unduja o jose, kunguno ali weyi ing’wene; nduhu unamiwa ungi. Hunagwene agitanagwa, ‘Shingwagulamiwa,’ kunguno atiho ungi uogunshigila.

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agawikalanaga chiza ubhuzunya bhokwe ukuli Mulungu. Umunhu ng’wunuyo, agajitumilaga ijinhilwa jakwe, bho gubhambilija abhanhu ijinagwikala bho gunamywa UMulungu, kunguno uweyi hu Unsumbi obho.

Umunhu ng’wunuyo abhudebhile ubhudula bho ng’wa Mulungu, ubho bhugubhinha masala, na nguzu abhanhu bhose, kugiki bhadule gumana weyi umubhutumami bho milimo yabho. Uwikaji bhokwe bhunubho bhugabhalanjaga abhanhu gunzunya na gunamya Mulungu, kunguno Ung’wene huShingwagulamiwa.

Akahayile kenako kalanga bhanhu  gunzunya na gunhamya Mulungu, kugiki bhadule gupandika mbango ja gwikala bho mholele na bhichabho umuwikaji bhobho.

(Kutoka 20:1-6; Wafilipi 2:1-11; Waebrania 1:1-4; Luka 4:4-8).

KISWAHILI: MWABUDIWA.

Chanzo cha msemo huu chaangalia Mkuu ambaye huabudiwa na watu. Huyo ndiye Mungu mwenyezi, ambaye ni Muweza wa yote, kwa sababu ni Yeye pekee anayestahili kuabudiwa, na hakuna mwingine. Ndiyo maana Yeye huitwa ‘Mwadudiwa.’

Msemo huou hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huiishi vizuri imani yake kwa Mungu. Mtu huyo, hutumia vipaji vyake kwa kuwasaidia watu katika kuishi kwa kumwabudu Mungu, kwa sababu Yeye ndiye Muumba wao.

Mtu huyo anauelewa uwezo wa Mungu katika kuwapa akili na nguvu watu wote ili waweze kumjua Yeye katika utekelezaji wa kazi zao. Maisha yake mtu huyo huwafundisha wenzake kumwamini na kumwabudu Mungu, kwa sababu Yeye ndiye ‘Mwabudiwa.’

Msemo huu hufundisha watu kumwamini na kumwabudu Mungu, ili waweze kupata baraka za kuishi kwa amani na wenzao siku zote za maisha yao.

(Kutoka 20:1-6; Wafilipi 2:1-11; Waebrania 1:1-4; Luka 4:4-8).

mountain-church

 

ENGLISH: THE ADORABLE.

The origin of this saying relates to the Mighty who is worshiped by people. He is God the Almighty, because He alone is worthy of adoration, and there is no other. That is why He is called ‘the Adorable.’

The saying is used comparatively to adorn a person who lives well with faith in God. That person uses his or her talents to help others live a God fearing life, because He is their Creator.

Such a person understands the power of God in giving all people wisdom and strength so that they may know Him in the performance of their duties. Through his or her life, that person teaches others about believing in and worshiping God, because He is the ‘the Adorable.’

The saying teaches people to believe in and worship God, so that they can have the blessings of living in peace with others, all the days of their lives.

(Exodus 20: 1-6; Philippians 2: 1-11; Hebrews 1: 1-4; Luke 4: 4-8).

506. KALAGU – KIZE. NG’WIMEJI ONE NGINU NO, DINGILI DINGILI MUMHO WIGUSHA:- BOLI.

Imbuki ya kalagu yiniyo yilolile ginhu ijo jigitanagwa boli. Iboli lili liginhu libhilingu. Ulu lyushindilwa mpaga lyokala myuyi, ligidamagukaga ulu lyatalijiwa hasi lyita, ‘dingili dingili’. Hunagwene abhanhu bhagiganilaga gigi, ‘ng’wimeji one nginu no, dingili dingili mumho wigusha’ bhashosha, ‘Boli.’

Ikalagu yiniyo igalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagatumilaga solobho ya wimeji bhobho, bho gubhalunguja abhichabho abho bhali mumayange. Abhanhu bhenabho bhagadulaga nulu gubhasesha abhanhu abho bhali na mayange.

Abhanhu bhenabho, bhagabhutumilaga uwimeji bhobho bho gubhambilija abhichabho uguitumama na bhuyegi imilimo yabho. Akikalile kabho kenako kagabhalunguja abhichabho abho bhali mumayange na gubhinha nguzu ja kuitumama milimo yabho bhobhuyegi. Hunagwene abhanhu bhagiganilaga giki, ‘ng’wimeji one nginu no, dingili dingili mumho wigusha’ bhashosha, ‘Boli.’

Ikalagu yiniyo yalanga bhanhu gubhutumila uwimeji bhobho bho gwilunguja ahikanza lya mayange, na gwikomeleja gutumama milimo yabho bhobhuyegi, kugiki bhadule gujibheja chiza ikaya jabho.

(Waefeso 4:1-7; 2Wakorintho 2:1-3; Mathayo 10:16-22; 1Wakorintho 9:22-23).

KISWAHILI: KITENDAWILI  –  TEGA: MTANI WANGU NI MNENE MNO DINGILIDINGILI NDIKO KUCHEZA KWAKE – MPIRA.

Chanzo cha kitendawili hiki chaangalia kitu kiitwacho mpira. Kwa kawaida, mpira ni mkubwa, sawa na kitu kinene na ni wa mviringo. Ukijazwa upepo na kuachiwa chini, hudundadunda pale chini ukitoa sauti ya ‘dingilidingili’. Ndiyo maana watu hutegeana kitendawili kwamba, ‘mtani wangu mnene mno dingilidingili ndiko kucheza kwake’ na kujibu, ‘mpira’

Kitendawili hicho chaangalia watu wale ambao huutumia utani wao kwa faida ya kuwafariji wenzao walio katika matatizo mbalimbali. Watu hao wenye utani huweza hata kuwachekesha watu hao walio katika matatizo.

Watu hao huutumia utani wao kwa kuwasaidia wenzao katika kuyatekeleza vizuri majukumu yao. Maisha yao huwafariji wenzao walioko kwenye matatizo mbalimbali, kwa kuwapatia furaha ya kuzitekeleza kazi zao. Ndiyo maana watu hutegeana kitendawili kwamba, ‘mtani wangu ni mnene mno, dingilidingili ndiko kucheza kwake’ na kujibu, ‘Mpira’.

Kitendawili hicho hufundisha watu kuutumia utani wao katika kufarijiana wakati wa shida, na kuhimizana kufanya kazi katika kuyatekeleza kwa furaha majukumu yao ya kila siku, ili waweze kuziendeleza vizuri familia zao.

(Waefeso 4:1-7; 2Wakorintho 2:1-3; Mathayo 10:16-22; 1Wakorintho 9:22-23).

 

soccer-ball.png

african-players

ENGLISH: I HAVE A RIDDLE – LET IT COME: MY JOKER IS TOO FAT, THUMP-RINGING IS HOW HE PLAYS – A BALL.

The origin of this riddle is something called a ball. A ball is usually big and round. When pressurised and released to the ground, it bounces and makes a tump ringing sound. That is why people pose ariddle that, ‘my joker is too fat, thump-ringing is how he plays and reply, ‘A ball.’

The riddle is used with reference to those people who use their jokes for the benefit of others in various problems. Such people may even make fun of their people in difficult situations.

These people use their jokes to help their peers in fulfilling their responsibilities. Their lives give comfort to others who are in various forms of sufferings, giving them the joy of doing their work with happiness. That is why people pose a riddle, ‘My joker is too fat, thump-ringing is how he plays’ and reply, ‘a ball.’

This riddle teaches people to use their jokes in comforting one another in times of difficulty, and encouraging one another to work happily in their daily responsibilities, so that they can better the wellbeing of their families.

(Ephesians 4: 1-7; 2 Corinthians 2: 1-3; Matthew 10: 16-22; 1 Corinthians 9: 22-23).

505. KALAGU – KIZE. UKUNUMA NSULULU N’UKUBHUTONGI NSULULU:- LIWINGA.

Imbuki ya kalagu yiniyo yilolile wingi bho bhanhu ha liwinga. Ahawinga bhagikalaga bhalihoyi bhanhu bhingi abho bhayegile. Bhagimbaga na gutambila, ukunu bhali mbita nhale abho bhagamanaga bhuyunja na gutula mhundu. Hunagwene abhanhu bhagiganilaga giki, ‘ukunuma nsululu nukubhutongi nsululu’ bashosha giki ‘liwinga’.

Ikalagu yiniyo igalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagikalaga halumo bho ng’wigwano gutale. Abhanhu bhenabho bhagiyambilijaga kihamo umumakanza ga bhuyeji bhobho.

Abhoyi bhagikalaga nsululu guti go hawinga, kunguno na abhoyi bhagiyambilija bho bhuyeji umukikale kabho. Bhagabhalanjaga na bhichacho, gwiyambilija uguitumama imilimo yabho yiniyo. Hunagwene abhanhu bhagiganilaga giki, ‘ukunuma nsululu n’ukubhutongi nsululu’ bhashosha, ‘liwinga.’

Ikalagu yiniyo yalanga bhanhu  gutumama milimo yabho halumo, kugiki bhadule ugujibheja chiza ikaya jabho. Ubhulihamo bhunubho bhugubhambilija ijinagupandika matwayo mingi, umuwikaji bhobho na gwendelea guyega kihamo.

(Marko 10:1-10; Yohane 2:1-12; Mathayo 15:32-39).

KISWAHILI: KITENDAWILI  – TEGA: NYUMA MSURURU NA MBELE MSURURU – HARUSI.

Chanzo cha kitendawili hiki ni wingi wa watu harusini. Harusini mara nyingi huwa na watu wengi sana, ambao hufurahia kwa namna mbalimbali. Wengine huimba na kucheza, na wengine hupiga vigelegele huku wakitamba kwa namna mbalimbali, katika umati huo mkubwa. Ndiyo maana watu hutegeana kitendawili kwamba, ‘nyuma msururu na mbele msururu’ na kujibu, ‘Harusi’.

Kitendawili hicho chalinganishwa kwa watu wale ambao huishi katika umoja wa kuelewana kwa kiwango kikubwa. Watu hao husaidiana kwa pamoja katika kuyatekeleza majukumu yao ya kila siku, kwa furaha. Huendelea kuzijenga familia zao kwa ushirikiano mzuri.

Watu hao hulingana na msururu wa watu walioko kwenye harusi, kwa sababu ya umoja wao wa kusaidiana katika kuyatekeleza vizuri majukumu yao. Ndiyo maana watu hutegeana kitendawili kwamba, ‘nyuma msururu na mbele msururu’ na kujibu, ‘harusi.’

Kitendawili hicho chafundisha watu kufanya kazi zao kwa ushirikiano, ili waweze kuziendeleza vizuri familia zao. Ushirikiano huo utawasaidia katika kupata mafanikio mengi maishani mwao, na kuendelea kufurahi kwa pamoja pale wanapoishi.

(Marko 10:1-10; Yohane 2:1-12; Mathayo 15:32-39).

africa wedding

bhitoji

ENGLISH: I HAVE A RIDDLE – LET IT COME: THERE IS A QUEUE AT THE BACK AND AT THE FRONT – A WEDDING.

The origin of this riddle is the mass of people at a wedding. In most cases, there will be many people, who enjoy it in various ways. Some sing and ululate, while others clap and dance in different forms, in a large crowd. That’s why people pose a riddle that ‘there is a queue at the back and at the front’ and reply, ‘a wedding.’

This riddle is use in comparison to refer to those people who live in unity and great harmony. These people help each other in fulfilling their daily tasks happily together. They continue to build their families cooperatively.

These people are, in fact, like a queue of people at a wedding, because of their unity in helping each other in fulfilling their responsibilities. That is why people pose a riddle that ‘there is a queue at the back and at the front’ and reply, ‘a wedding.’

This riddle teaches people about working together, so that they can better their families. Such cooperation will help them achieve notable success in their lives, and continue to enjoy their common life.

(Mark 10: 1-10; John 2: 1-12; Matthew 15: 32-39).

504. LYABHUMENDE GITI LIJISINZA.

Imbuki ya kahayile kenako yilolile ginhu ijo jigitanagwa jisinza. Ijisinza nulu jigasimbilwa hasi, uyo agulimaga agujipunila jitali jilijidimu, giti numo jalili aha gwandya.  Ijoyi nulu jigagwila gutu, jigikalaga jidimu duhu, jidagalukaga. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘lyabhumende giti lijisinza.’

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo adatinginyiyagwa sagala, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agimaga ha bhung’hana ilali, bho pye amakanza. Uweyi alemile ugusegeja nulu ugusegejiwa ahabhung’hana bhunubho.

Umunhu ng’wunuyo alinshikanu ijinaguwikalana ubhung’hana bhunubho. Hunagwene agalenganijiyagwa na jisinza ijo jilijidimu bho pye amakanza, kunguno nang’hwe, alindimu ugubhuleka ubhung’hana bhunubho, umukikalile kakwe. Uweyi adebhile ugubhalanga na bhiye ugubhumana ubhung’hana bhunubho, nuguwikalana. Hunagwene abhanhu bhaganyombaga giki ‘lyabhumende giti lijisinza.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu gubhumana ubhung’hana na gubhiza bhashikanu ijinaguwikalana ubhunghana bhunubho, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi umuwikaji bhobho.

(Mathayo 7:24-27; Mathayo 16:13-20; 1Petro 4:12-19).

KISWAHILI: NI IMARA KAMA CHUMA.

Chanzo cha msemo huu, chaangalia kitu ambacho huitwa chuma. Chuma hicho, hata kikichimbiwa chini, alimaye pale kilipochimbiwa atakikuta kikiwa imara kama kilivyokuwa mwanzoni. Chenyewe, hata kikipata kutu, huendelea kuwa kigumu tu; hakigeuki kuwa kilaini. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘ni imara kama chuma.’

Msemo huu hulinganishwa kwa mtu yule asiyetetereka ovyo maishani mwake. Mtu huyo husimama imara katika ukweli wakati wote. Yeye hukataa kuyumbishwa wala kuondolewa kwenye ukweli huo.

Mtu huyo alishaimarika katika kuuishi ukweli huo, hadi kufikia hatua ya kuwa mfano wa kuigwa na wenzake. Ndiyo maana yeye hulinganishwa na chuma kilivyo madhubuti muda wote, kwa sababu naye ni mgumu kuuacha ukweli huo maishani mwake.

Yeye anafahamu pia kuwafundisha wenzake kuuelewa ukweli na kuuishi katika maisha yao ya kila siku. Ndiyo maana watu humsema kwamba ‘ni imara kama chuma.’

Msemo huo hufundisha watu kuufahamu na kuuishi ukweli kwa ukamilifu, ili waweze kupata mafanikio mengi maishani mwao.

(Mathayo 7:24-27; Mathayo 16:13-20; 1Petro 4:12-19).

chuma

ENGLISH: IT IS ‘AS STRONG AS IRON’.

The origin of this saying is something called iron. Even when it is burried, someone will eventually find it as strong as it was in the beginning when one digs it out. Even if it gets rusty, it just remains strong; it does not turn out to be soft. That’s why people say, ‘As strong as iron.’

The saying is used comparatively to refer to a person who is not swayed in life as regards truth. That person always stands firm on the truth. He refuses to be swayed or shaken from that truth.

Such a person is steadfast in living the truth, to the point of being a role model to others. That is why he is compared to a hard metal that remains so at all timse, because he/she too is hard to let go of the truth in his life.

He also knows how to teach others about understanding the truth and living it in their daily lives. That is why people describe such a person, ‘As strong as iron.’

The saying teaches people about understanding and living the truth to the fullest so that they can adequately succeed in their lives.

(Matthew 7: 24-27. Matthew 16: 13-20. 1Peter 4: 12-19).