Folklore

538. KALAGU – KIZE: MUNHU ADINA NH’UNGWA NSOGA NA BHIYE – MHELA.

Imbuki ya kalagu yiniyo, ilolile ndimu iyo igitanagwa mhela. Imhela yili ndimu ng’hali noyi iyo itogilwe gwikala ying’wene na nkima oyo duhu. Iyoyi idina bhunwani na ndimu nyichayo. Hunagwene abhanhu bhagiganilaga giki, ‘munhu adina nhungwa nsoga na bhiye’ bhashosha, ‘Mhela.’

Ikalagu yiniyo igalenganijiyagwa kuli munhu uyo ali nkali noyi umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo adina bhunwani na bhiye umuwikaji bhokwe, kunguno ya bhukali bhokwe bhunubho.

Uweyi agabhabalasanyaga abhanhu bhakwe, kunguno ya kahoyele kakwe ako kali kabhukali bhuli ikanza. Abhanhu bhagang’ogohaga noyi, kunguno bhandebhile igiki adabhatogilwe abhiye. Uweyi witogilwe weyi bhung’wene duh, umukikalile kakwe. Hunagwene abhanhu bhagang’winataga giki, ‘munhu adina nhungwa nsoga na bhiye’.

Ikalagu yiniyo yalanga bhanhu kuleka nhungwa ja bhukali ubho bhudina solobho umuwikaji bhobho, kugiki bhadule gwikala bho witogwa na bhichabho.

(Yohana 1:11-12; Yohana 15:4-6; Yohana 17:22-25; Waebrania 10:37-38; 1Thimotheo 2:1-5).

KISWAHILI: KITENDAWILI – TEGA: MTU ASIYE NA TABIA NJEMA KWA WENZAKE – KIFARU.

Chanzo cha kitendawili hiki chaangalia myamapori anayeitwa kifaru. Myama huyo ni mkali sana na hupenda kuishi peke yake na mkewe tu. Mwenyewe hana urafiki na myama mwenzake. Ndiyo maana watu hutegeana kitendawili kwamba, ‘mtu asiye na tabia njema kwa wenzake’ na kujibu, ‘Kifaru.’

Kitendawili hiki hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ni mkali wa hovyo katika maisha yake. Mtu huyo hana urafiki na wenzake anapoishi, kwa sababu ya ukali wake huo. Yeye huwasambaratisha watu wake, kwa sababu ya namna yake hiyo ya kuongea, ambayo hutawaliwa na ukali usio na maana yoyote. Watu humwogopa sana mtu huyo, kwa sababu wanamfahamu kwamba hana upendo kwa wenzake. Yeye hujipenda mwenyewe tu katika maisha yake. Ndiyo maana watu humwita kwamba ni ‘mtu asiye na tabia njema kwa wenzake’.

Kitendawili hiki hufundisha watu kuacha tabia za kuwa na ukali usio na maana katika maisha yao, ili waweze kuishi kwa upendo na wenzao maishani mwao.

(Yohana 1:11-12; Yohana 15:4-6; Yohana 17:22-25; Waebrania 10:37-38; 1Thimotheo 2:1-5).

black-rhinoceros

southern-white-rhinoceros

 

ENGLISH: I HAVE A RIDDLE – LET IT COME: A PERSON WHO IS UNKIND TO COLLEAGUES – A RHINOCEROS.

The origin of this riddle is wild animal called rhinoceros. The beast is very fierce and likes to live alone with his wife only. He has no friendship with his fellow animals. That is why people pose a riddle, ‘a person who is unkind to colleagues‘ and respond, ‘A rhinoceros.’

This riddle is used compared to refer to a person who is unnecessarily strict and harsh in his/her life. The person has no friends because of their harshness.

Because of his/her unnecessary harshness, his/her people do not always stay at home as they disperse to different places. People are very afraid of that person, because they know that he/she does not love other people as he/she only loves himself/herself. That is why people call him, ‘a person who is unkind to colleagues’.

This riddle teaches people to refrain from unreasonable extremism in their lives, so that they can live in love with their peers.

(John 1: 11-12; John 15: 4-6; John 17: 22-25; Hebrews 10: 37-38; 1Timothy 2: 1-5).

537. KALAGU – KIZE: OZWALA NHANZO ILALI – NZOKA.

Imbuki ya kalagu yiniyo ilolile nzoka. Inzoka yiniyo, igikalaga numo ili duhu pye amakanza. Iyoyi idagalukaga nulu hado umukikalile kayo. Iki yiikolile pye umili goyo, igikolaga n’umunhu uyo azwalile ng’hanjo. Hunagwene abhanhu bhagiganilaga giki, ‘ozwala nhanjo ilali’ bhashosha, ‘Nzoka.’

Ikalagu yiniyo igalenganijiyagwa kuli munhu uyo obhatijiwa winhiwa ng’wenda gope. Umunhu ng’wunuyo, aginhagwa nimo go gugulang’hana ung’wenda gunuyo, mpaga agushishe ng’wigulu guligope chiniko.

Uweyi agikomeja ugwikala chiza na bhanhu, kunguno idakililwe agulang’hane umoyo gokwe gubhize gope shigu jose, mpaga agushime kuli Mulungu guli gutinumo gogejiwa ahabhubhatijiwa bhokwe. Hunagwene umunhu ng’wunuyo agabhaganilaga abhanhu giki, ‘ozwala ng’hanjo ilali’ bhashosha, ‘Nzoka.’

Ikalagu yiniyo yalanga bhabhatijiwa guhandatila gwikala muli Yesu bho gubhitila yawiza abhichabho umukikalile kabho, kugiki bhadule guishisha kuli Mulungu, imyoyo yabho yili yape chiniko.

(Marko 14:50-52; Luka 11:35-36).

KISWAHILI: KITENDAWILI    –    TEGA: KAVAA KANZU MILELE – NYOKA.

Chanzo cha kitendawili hiki chaangalia nyoka. Nyoka huwa kama alivyo wakati wote. Yeye habadilishi vazi hata kidogo maishani mwake. Hivyo, mwili wake wote hufanana na mtu aliyevaa kanzu. Ndiyo maana watu hutegeana kitendawili kwamba, ‘kavaa kanzu milele’ na kujibu, ‘Nyoka.’

Kitendawili hicho hulinganishwa kwa mtu aliyebatizwa na kupewa nguo nyeupe. Mtu huyo hupewa jukumu la kuitunza nguo hiyo, mpaga aifikishe kwa Mungu ikiwa nyeupe hivyo.

Mbatizwa huyo huendelea kuongeza bidii ya kuishi vizuri na watu, kwa sababu anatakiwa kuutunza moyo wake ili undelee kuwa safi siku zote, hadi aufikishe kwa Mungu ukiwa kama ulivyosafishwa siku ya ubatizo wake. Ndiyo maana mtu huyo huwategea watu kitendawili kwamba ‘kavaa kanzu kimoja’ nao hujibu, ‘Nyoka.’

Kitendawili hicho hufundisha watu kushikamana na Yesu maishani mwao, kwa kuwatendea mema wenzao ili waweze kuzifikisha roho zao kwa Mungu, zikiwa safi.

(Marko 14:50-52; Luka 11:35-36).

green-tree-python

basilisk-rattlesnake

ENGLISH: I HAVE A RIDDLE – LET IT COME: HE ALWAYS WEARS A ROBE – A SNAKE.

The origin of this riddle is snake. A snake is always as it is. It never changes garment (skin) in its life. Thus, its body resembles a person wearing a robe. That is why people answer ‘a snake’ to the riddle ‘He always wears a robe’.

This riddle, is used comparatively to a person baptized and given a white garment. The person is entrusted with the care of the garment, bringing it to God, as white as it were during baptism.

The baptismal candidate continues increasingly puts more efforts to live harmoniously with other people, because he/she must keep his heart clean and holy as it were cleansed during baptism until he/she meets God. That is why he/she puts up a riddle, ‘he always wears a robe’ and people reply, ‘a snake.’

This riddle teaches people about being connected to Jesus in their lives, by doing good to others, so that they can bring their souls to God as clean as they were during baptism.

(Mark 14: 50-52. Luke 11: 35-36).

536. NATENG’WA NHELEKELE.

Imbuki ya kahayile kenako yilolile bhuteng’wa bho ng’helekele. Ubhuteng’wa bho ng’helekele bhunubho bhuli bhuwilwa bho mihayo iyo iliyambisila. Umunhu uyo owilagwa imihayo yiniyo, agadumaga uguyelelwa chiza. Hunagwene agayombaga giki, ‘nateng’wa ng’helekele.’

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agahoyaga na bhanhu bho nduhu uguiyomba hape imihayo yakwe. Umunhu ng’wunuyo agatumilaga mihayo ya mbisila umumahoya gakwe na bhanhu.

Abhanhu abho agahoyaga nabho bhagadumaga uguyidebha imihayo iyo agabhawilaga umunhu ng’wunuyo. Ulu bhamuja ubhulingisilo bho mihayo yakwe, uweyi agabhashokeja bho mbisila. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘nateng’wa ng’helekele.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu gubhawila abhichabho hape imihayo yabho, kugiki bhadule guyelelwa imihayo yiniyo, na guitumila chiza ijinagubheja ikaya jabho.

(Luka 8:16-17; Mathayo 5:14-16).

KISWAHILI: NIMEAMBIWA KIMAFUMBO.

Chanzo cha msemo huu chaangalia uambiwaji wa kitu kwa mafumbo. Uambiwaji huo ni wa kuambiwa maneno yenye mafumbo ambayo maana yake haiko wazi. Mtu aliyefumbiwa hushindwa kuuelewa ujumbe anaoambiwa na mwenzake huyo. Ndiyo maana husema kwamba, ‘nimeambiwa kimafumbo.’

Msemo huu hulinganishwa kwa mtu yule ambaye haongei na watu waziwazi. Mtu huyo hutumia maneno yenye mafumbo katika maongezi yake na wenzake, hali ambayo huwapa ugumu wa kumwelewa vizuri. Watu anaoongea nao hushindwa kuelewa maana ya maneno anayotumia katika maongezi yake. Wakimuuzila maswali kuhusu maana ya yale maneno yake aliyowaambia, yeye huwajibu kwa mafumbo, hali ambayo huongeza ugumu zaidi kwao. Ndiyo maana watu hao husema kwamba, ‘nimeambiwa kimafumbo.’

Msemo huu hufundisha watu kuongea na wenzao, kwa kutumia maneno yaliyo wazi, ili waweze kuuelewa vizuri ujumbe uliomo kwenye maneno hayo na kuufanyia kazi katika kuziendeleza familia zao.

(Luka 8:16-17; Mathayo 5:14-16).

mahoya

meeting-

ENGLISH: I HAVE BEEN TOLD IN PARABLES.

The origin of this saying is parables. A person who speaks in parables is usually not understood because the words he/she uses are considered vague by listeners. As such they fail to understand the message that person is telling them. That is why they say, ‘I have been told in parables.’

The saying is used comparatively to refer to a person who does not speak to people clearly. The person uses idiomatic expressions in his/her conversation with colleagues, which makes it difficult to clearly understand him or her.

The listeners fail to understand the meaning of the idiomatic expressions he/she uses in his/her conversation. When they ask questions about the meaning of such expressions, the person answers them in parables, which further complicates the matter. That is why those people say, ‘I have been told in parables.’

This saying teaches people about being clear when talking to others so that the listeners can better understand the message and work it out in the development of their families.

(Luke 8: 16-17; Matthew 5: 14-16).

535. GONBITYA MABHUGA NAGUYUNGAGWA NONI.

Imbuki ya kahayile kenako ilolile bhubhiti bho mumbuga bho ng’wa munhu uyo oyungagwa noni. Umunhu uyo alibhita mumbuga nhale aganogaga noyi, kunguno ya gusiminza lugendo lulihu, niyo aliyiyene.

Umunhu ng’wung’wunuyo agajibhonaga inoni yabhiza guti jiling’wiyungulila weyi, kunguno ya bhuyiyene bhokwe. Hunagwene umunhu ng’wunuyo agayombaga giki, ‘gombitya mabhuga naguyungagwa noni.’

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo wiyumilija kutumama milimo yakwe gwingila mubhuhabhi mpaga gubhiza nsabhi, uyo alinkumuku, guti ningi umuwikaji bhokwe. Umunhu ng’wunuyo wingila mumakoye guti ga bhuhabhi, utumama milimo guti gwimba, mpaga nose upandika sabho ningi, kunguno ya bhutumami bhokwe bhunubho. Uweyi agikolaga n’umunhu uyo omala gubhita mulibhuga litale, kunguno nang’hwe winga kufuma mubhuhabi mpaga ushika mubhusabhi. Umunhu ng’wunuyo agabhalanjaga n’abhiye inzila ijo ojibhitila mpaga ugingila umubhuhabhi bhunubho. Hunagwene agabhawilaga abhanhu giki, ‘gombitya mabhuga naguyungagwa noni.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu gwiyumilija gutumama milimo yabho bho bhukamu bhutale, kugiki bhadule kuginja amakoye agabhuhabhi, mpaka bhashike mugupandika sabho ningi umuwikaji bhobho.

(Mathayo 15:29-39; Marko 3:7-10).

KISWAHILI: NIMEPITA MBUGA NYINGI NIKIZONGWA NA NDEGE.

Chanzo cha msemo huu chaangalia upitaji wa mtu katika mbuga nyingi akizongwa na ndege. Mtu huyo alizipita mbuga hizo kubwa akizongwa na ndege kwa sababu ya kutembea mwendo mrefu akiwa peke yake.

Mtu huyo aliwaona ndege wengi walioonekana kama wanamzonga katika safari yake hiyo ndefu alipokuwa peke yake. Ndiyo maana mtu huyo, husema kwamba, ‘nimepita mbuga nyingi nikizongwa na ndege.’

Msemo huu hulinganishwa kwa mtu yule aliyevumilia kufanya kazi ngumu kuanzia kwenye umaskini hadi kufikia kuwa tajiri aliyesifika kama manju. Mtu huyo alitokea kwenye matatizo ya umaskini, akafanya kazi nyingi zikiwemo zile za kuimba, hadi akapata mali nyingi kwa sababu ya bidii yake ya kufanya kazi.

Yeye hufanana na mtu yule aliyevuka mbuga nyingi na kubwa, kwa sababu naye alitokea kwenye matatizo ya umaskini hadi kwenye utajiri kupitia utekelezaji wa majukumu yake.

 Mtu huyo huwafundisha pia wenzake  njia alizopitia mpaka akatoka kwenye umaskini. Ndiyo maana yeye huwambia watu kwamba ‘nimepita mbuga nyingi nikizongwa na ndege.’

Msemo huu hufundisha watu kuvumilia matatizo na kufanya kazi kwa bidii kubwa katika utekelezaji wa majukumu yao, ili waweze kuyatatua matatizo ya umaskini kwa kupata mali za kuwatosha kutumia katika maisha yao.

(Mathayo 15:29-39; Marko 3:7-10).

falcon-

mbuga

ENGLISH:  I HAVE PASSED THROUGH MANY PLAINS WITH BIRDS FLYING OVER.

The origin of this is the passing of a person through many terrains with birds flying over him/her. The person walks alone for a long time while birds a flying over his/her head as a symbol of sufferings.. That is why he/she says, ‘I have passed through many plains with birds flying over.’

The saying is used comparatively to refer to a person who endures hard work that helps him/her transform life from poverty to affluence. This person who transforms life from poverty to affluence must have done several jobs including singing, until he/she got rich due to hard work. He/she is like a person who crosses many plains with birds flying over,, working hard from poverty to affluence. This person also teaches other about the ways he/she went through poverty. That is why he/she tells people that, ‘I have passed through many plains with birds flying over.’

The saying teaches people about persevering in the execution of their duties so that they can solve the problems of poverty by finding enough resources to spend in their lives.

(Matthew 15: 29-39; Mark 3: 7-10).

534. NHALA AGALANGA BHATENGEKE.

Imbuki ya kahayile kenako ilolile bhuhala bho ng’wa munhu. Umunhu ung’hala agabholechaga ubhuhala bhokwe bho gubhitila nhungwa jakwe ijo jili jabhubhi. Umunhu ng’wunuyo agitaga mihayo ya bhubhi ukubhiye abho bhalibhatengeke.

Kuyiniyo lulu, abhatengeke bhenabho bhagikalaga bhang’ogohile uweyi, kunguno ya kajile kakwe ako bhagilemejaga ugukigemeja umuwikaji bhobho. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘ng’hala agalanga bhatengeke.’

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo ogabhona amakoye ayo agapandikaga umunhu uyo aling’hala, mpaga gwiyangula gusaga mubhutengeke umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo agaidililaga chiza ikaya yakwe, kunguno adahayile abhanhu bhakwe bhapandike makoye guti nayo agapandikaga umunhu ung’hala ng’wunuyo umukikalile kakwe.

Kuyiniyo lulu, uweyi agadujaga ugubhalanja abhiye gwikala na nhungwa ja wiza bho gubhizukija amakoye ayo bhagagapandikaga abhanhu abho bhali na nhungwa ja bhubhi. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘ng’hala agalanga bhatengeke.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu  kuleka nhungwa ja bhubhi umukikale kabho, kugiki bhadule gwikala chiza na bhichabho umuwikaji bhobho.

(2Wathesalonike 3:13-15; Wagalatia 5:16-17; Wagalatia 5:22-23; 1Petro 3:17; 2Petro 3:17; Luka 2:34-36; Mithali 11:5-6; Mithali 11:19; Mithali 12:1-3).

KISWAHILI: MJINGA ALIFUNDISHA WEREVU.

Chanzo cha msemo huu chaangalia ujinga wa mtu fulani. Mtu huyo huonesha ujinga wake kwa kupitia tabia yake ambayo ni mbaya. Yeye hutenda matendo mabaya kwa wenzake ambao ni werevu.

 Kwa hiyo, watu walio werevu humwogopa mjinga huyo, kwa sababu ya mwenendo wake ambao watu hao hukatazana kuuiga maishani mwao. Ndiyo maana watu husema ‘mjinga alifundisha werevu.’

Msemo huu hulinganishwa kwa mtu yule aliyeyaona matatizo wanayoyapata wajinga maishani mwao, hadi akaamua kubaki katika werevu wake muda wa maisha yake. Mtu huyo, huijali vizuri familia yake, kwa sababu hataki watu wake wayapate matatizo yale wanayoyapata watu walio wajinga. Kwa hiyo basi, yeye huweza kuwafundisha wenzake  kuishi katika tabia njema kwa kuwakumbusha matatizo yale waliyo nayo wenye tabia mbaya katika maisha yao.  Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘mjinga alifundisha werevu.’

Msemo huu hufundisha watu kuacha tabia mbaya katika maisha yao, ili waweze kuishi vizuri na wenzao maishani.

(2Wathesalonike 3:13-15; Wagalatia 5:16-17; Wagalatia 5:22-23; 1Petro 3:17; 2Petro 3:17; Luka 2:34-36; Mithali 11:5-6; Mithali 11:19; Mithali 12:1-3).

ghana

fisherman-

ENGLISH: AN IMBECILE TAUGHT THE INTELLIGENT.

The origin of this saying is ignorance of someone. The ignorant person shows his/er ignorance through his evil behavior. He does evil deeds to his wise fellows. Therefore, the prudent are afraid of this imbecie, because of his/her conduct, which they have sworn not to imitate in their lives. That’s why people say ‘an imbecile taught the intelligent.’

The saying is used comparatively to refer to person who witnessed the plight of the imbecile in his/her life, so much that he/she decided to remain in control of his/her life. The person does take good care of his/her family, because he does not want his/her people to suffer the same problems that imbeciles experience.

Therefore, he or she can teach his or her colleagues about living a good life, by reminding them of the problems they have in their lives. That is why people say, ‘an imbecile taught the intelligent.’

The saying teaches people to refrain from bad habits in their lives, so that they can live well with their peers.

(2Thessalonians 3: 13-15; Galatians 5: 16-17; Galatians 5: 22-23; 1 Peter 3:17; 2 Peter 3:17; Luke 2: 34-36; Proverbs 11: 5-6; Proverbs 11:19; Proverbs 12: 1-3).