Folklore

543. SUHA YA BHUKI IDAMALAGA BHUNONU.

Imbuki ya kahayile kenako, yilolile bhuki. Ubhuki bhunubho bhuli bhunonu noyi, nulu bhugatulwa musuha, isuha yiniyo igunona nayo, kunguno ubhuki bhugamililaga umugati yayo. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘suha ya bhuki idamalaga bhunonu.’

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo alina nhungwa ja wiza umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo agayombaga mihayo ya wiza, kunguno yigenhaga mholele ya gwitogwa na bhiye umumahoya gakwe.

Imihayo yakwe yiniyo igabhizaga minonu guti bhuki, kunguno idasukaga ukubhadegeleki bhayo. Abhanhu bhagikalaga na ng’humbu ya gundegeleka umunhu ng’wunuyo, kugiki bhadule guyimana iyo aliiyombaga. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, ‘suha ya bhuki idamalaga bhunonu.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu gubhiza na nhungwa ja wiza umukikalile kabho, kugiki bhadule gwikala bho mholele na bhichabho umuwikaji bhobho.

(1Wakorintho 16:13-14; Zaburi 119:89-91).

KISWAHILI: KIBUYU CHA ASALI HAKIISHIWI UTAMU.

Chanzo cha msemo huu chaangalia uwekaji wa asali kwenye kibuyu. Asali ni tamu sana, hata ukiiweka kwenye kibuyu, utamu wake utabakia humo kwa sababu huwa inang’ang’ania ndani yake. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘kibuyu cha asali hakiishiwi utamu.’

Msemo huu hulinganishwa kwa mtu yule ambaye, ni mwenye tabia njema katika maisha yake. Mtu huyo huongea maneno mazuri yenye amani na upendo kwa wenzake katika maongezi yake.

Maneno hayo huwa matamu kama asali, kwa sababu huwa hayaishiwi utamu wake kwa wasikilizaji wake. Watu huwa na hamu ya kuendelea kumsikiliza mtu huyo, ili waweze kuyaelewa yale anayoyaongea. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, ‘kibuyu cha asali hakiishiwi utamu.’

Msemo huu hufundisha watu kuwa na tabia njema katika namna yao ya kuishi kwao, ili waweze kuishi kwa amani na wenzao maishani mwao.

(1Wakorintho 16:13-14; Zaburi 119:89-91).

honey-bhuki

ENGLISH: A HONEYCALABASH NEVER LACKS SWEETNESS.

The origin of this saying is storage of honey in a calabash. Honey is very sweet, even if you put it in a syrup, its sweetness will remain there because it sticks in it. That is why people say, ‘Honeycalabash never lacks sweetness.’

The saying is used comparatively to refer to any person with good character in life. That person speaks sweet words of peace and love to his/her fellows in his/her conversation. These words are as sweet as honey, because they are not confined to their audience. People are eager to keep listening to that person, so they can understand what he or she is saying. That is why people tell him, ‘Honeycalabash never lacks sweetness.’

The saying teaches people to be good in their ways of living, so that they can live in harmony with others.

(1Corinthians 16: 13-14; Psalm 119: 89-91).

542. LUGENGO LO SHIMBA YOMBO MUNZENGO.

Imbuki ya kahayile kenako yilolile shimba. Ishimba ili ndimu iyo iling’hali noyi umukikalile kayo. Iyoyi uluyingila mulugali gwikolela jiliwa, igabhizaga yombo nhale umuchalo jinijo, kunguno ya makanji gayo. Igikindikaga nulu mulugutu yapula ng’ombe. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki ‘lugendo lo shimba yombo munzengo.’

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agabhizaga nsambo umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo agabhinzaga milyango ya bhanhu, wingila gwibha sabho jabho. Uweyi ulu wibha jikolo ja bhanhu, yigabhizaga yombo umunzengo, guti ni shimba iyo igenhaga yombo bho gupula mitugo ja bhanhu umuchalo. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘lugendo lo shimba yombo munzengo.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu guleka kajile kawibhi umukikalile kabho, kugiki bhadizenha yombo umunzengo gobho umuwikaji bhobho.

(Matendo ya Mitume 9:19-25; Mithali 4:10-18).

KISWAHILI: SAFARI YA SIMBA KELELE KIJIJINI.

Chanzo cha msemo huu chaangalia simba. Simba ni mnyamapori ambaye ni mkali sana maishani mwake. Yeye akiingia kwenye zizi kujitafutia chakula, husababisha kelele kubwa kwenye kijiji hicho, kwa sababu ya hali yake hiyo ya kutisha. Mnyama huyo hurukia hata zizini na kuchukua ng’ombe. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘safari ya simba kelele kijijini.’

Msemo huu hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ni jambazi katika maisha yake. Mtu huyo huvunja milango ya watu na kuingia kuiba mali zao, maishani mwake.

Yeye akiiba vitu vya watu, husababisha kelele kijijini, kama simba aletavyo kelele anapochukua ng’ombe kijijini. Ndiyo maana watu husema, ‘safari ya simba kelele kijijini.’

Msemo huu hufundisha watu kuacha mwenendo wa wizi, katika maisha yao, ili wasisababishe kelele katika vijiji vyao, maishani mwao.

(Matendo ya Mitume 9:19-25; Mithali 4:10-18).

shimba

ENGLISH: A LION’S TRIP IS A COMMOTION IN THE VILLAGE.

The origin of this saying is a lion. The lion is the most fierce animal in its life. When it goes to hunt, it causes a lot of commotion in the village, because of its scary condition. The animal even jumps into barns and takes livestock. That is why people say, ‘a lion’s trip is a commotion in the village.’

The saying is used comparatively to refer to any who is a gangster in his/her life. The person breaks into people’s properties and steal belongings. When he/she steals people’s belongings, they cause a commotion in the village, just as when the lion visits a village a takeslivestock. That is why people say, ‘a lion’s trip is a commotion in the village.’

The saying teaches people refrain from the practice of robbery, so as not to cause commotion in their villages.

(Acts 9: 19-25; Proverbs 4: 10-18).

541. ULU ULI DIDI IYO ULAIPANDIKE UGWIMALA BHEBHE NG’WINIKILI.

Imbuki ya kahayile kenako yilolile mafumilo ga ng’wa didi. Udidi jilijisumva ijo jili na nhinda ya gulema gwigwa mihayo ya wiza iyo jigawilagwa na bhichajo. Ijoyi jigacholaga ndebho bho gubhikolosha abhangi umukikajile kajo. Uwikolosha bhunubho bhugajenhelejaga guminyiwa nabho jigabhikoloshaga. Hunagwene abhanhu bhagajiwilaga giki ‘ulu uli didi iyo ulaipandike ugwimala bhebhe ng’winikili.’

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo alinchoji o ndebho uumukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo agabhikobyaga abhiye bho gubhitila mihayo ya bhubhi.  Uweyi agikalaga upandika mamihayo ng’hangala nyingi, kunguno ya bhudidi bhokwe ubho bhugabhenhelejaga na bhiye gupandika makoye umuwikaji bhobho.

Umunhu ng’wunuyo agabhizaga alemile uguhang’wa na bhiye. Abhanhu abho bhagang’hamaga olema ugubhazunilija bhaganekaga wibhegeje weyi ulu opandikaga makoye, kunguno obhanoja. Hunagwene abhanhu bhenabho bhagang’wilaga giki, ‘ulu uli didi iyo ulaipandike ugwimala bhebhe ng’winikili.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu guleka bhuchoji bho ndebho, nulu wikomya ukubhichabho, kugiki bhadule gwikala bho gujilanija chiza na bhichabho umuwikaji bhobho.

(Yoshua Bin Sira 27:25-27; Yoshua Bin Sira 32:18-19; Zaburi 7:16-17).

KISWAHILI: UKIWA MTUKUTU YATAKAYOKUPATA UTAYAMALIZA MWENYEWE.

Chanzo cha msemo huu chaangalia matokeo ya asiyesikia. Asiyesikia ni kiumbe chenye kiburi cha kukataa kusikia maneno yaliyo mema yatokayo kwa wenzake. Kiumbe hicho ni kitukutu kwa kuwa hutafuta uchokozi kwa wenzake kinapoishi. Uchokozi huo hukisababishia kuumizwa na wale kinaowachokoza. Ndiyo maana watu hukiambia kwamba, ‘ukiwa mtukutu yatakayokupata utayamaliza wewe mwenyewe.’

Msemo huu hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hutafuta uchokozi katika maisha yake. Mtu huyo huwachokoza wenzake kwa kuwatendea maovu. Yeye hupata matatizo mara nyingi, kwa sababu ya kiburi chake ambacho pia huwasababishia wenzake kuingia kwenye matatizo. Mtu huyo huwa hataki kuonywa na wenzake. Watu wanaomuonya na kuwakatalia, humuacha ajitatulie mwenyewe matatizo aliojiletea, kwa sababu ya yeye kuwachosha watu hao. Ndiyo maana wao humwambia kwamba, ‘ukiwa mtukutu yatakayokupata utayamaliza wewe mwenyewe.’

Msemo huu hufundisha watu kuacha kutafuta uchokozi kwa wenzao, ili waweze kuishi kwa kuelewana vizuri na watu wengine maishani.

(Yoshua Bin Sira 27:25-27; Yoshua Bin Sira 32:18-19; Zaburi 7:16-17).

ligusha na nzoka

pingu

 

ENGLISH: IF YOU ARE NAUGHTY, YOU WILL DEAL WITH WHATEVER BEFALLS YOU.

The origin of this saying is a person that is never told. Such a person refuses to listen to good advice from others. The person seeks out aggression from others by provoking them. The aggression, in turn, hurts the him/her and his/her company. That is why people tell him/her, ‘if you are naughty, you will deal with whatever befalls you.’

The saying is used comparatively to refer to a provocative person. The person annoys others by by provoking them and when they harm him they also do so to his/her companions. Such an individual often gets into trouble, because of his/her pride, which also causes his colleagues to get into troubles.

That person doesn’t want to be warned by his/her colleagues. Therefore they leave him alone to deal with whatever problem arising from his/her provocation to others. That is why they tell him/her, ‘if you are naughty, you will deal with whatever befalls you.’

This saying teaches people to refrain from aggression, so that they can live in harmony with other people in their lives.

(Joshua Bin Sira 27: 25-27; Joshua Bin Sira 32: 18-19; Psalm 7: 16-17.

540. LYAMOLOLO.

Imbuki ya kahayile kenaka yingilile kujisumva ijo jili na mololo umumili gojo. Amololo genayo gali malonda gapilile, ayo jagapandika ijisumva jinijo, kunguno ya nguzu jajo, ijo jidahebhagwa na oseose. Ijoyi jidulile gutumama milimo mingi bho nguzu mpaga guyimala. Hunagwene abhanhu bhagajitanaga giki, ‘lwamololo.’

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo ali na nguzu ja gutumama milimo yakwe chiza, mpaga guyimala. Umunhu ng’wunuyo, agigulyambijaga uguyitumama imilimo yiniyo, bho wangu wangu, na guyimala chiza aha kaya yakwe.

Uweyi agikolanijiyagwa ni lyamololo, kunguno nang’hwe ali na nguzu ja gudula gung’wenhela bhupandiki wingi umuwikaji bhokwe. Uwikaji bhokwe bhunubho, bhugabhambilijaga abhiye ugongeja bhukamu bho kutumama milimo yabho. Hunagwene abhanhu bhagang’witanaga giki, ‘lwamololo.’

Akahahile kenako kalanga bhanhu gongeja nguzu ja guitumama bho bhukama bhutale imilimo yabho, kugiki bhadule ugujibheja chiza ikaya jabho umuwikaji bhobho.

(Kutoka 2:11-15; Waamuzi 15:11-16; 1Wafalme 11: 15-16).

KISWAHILI: LENYE MAKOVU.

Chanzo cha msemo huu chaangalia kiumbe chenye makovu mwilini mwake. Makovu hayo ni madonda yaliyopona ambayo yalitokana na kiumbe hicho kuwa na nguvu za kutoshindwa na chochote. Kiumbe hicho kinaweza kufanya kazi nyingi mpaka kuzimaliza. Ndiyo maana watu hukiita ‘lenye makovu.’

Msemo huu hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ni mwenye nguvu za kufanya kazi vizuri mpaka kuzimaliza. Mtu huyo hujibidisha kuzitekeleza kazi zake hizo kwa haraka hadi kuzikamilisha. Yeye hufanana na dude lenye makovu, kwa sababu naye ana nguvu za kumwezesha kujiletea mafanikio mengi katika maisha yake. Maisha yake hayo huwasaidia pia wenzake katika kuongeza bidii za kuyatekeleza vizuri majukumu yao. Ndiyo maana watu humwita kwamba yeye ni ‘lenye makovu.’

Msemo huo hufundisha watu kuongeza nguvu za kuyatekeleza kwa bidii kubwa na vizuri majukumu yao, ili waweze kuziendeleza vizuri familia zao, maishani mwao.

(Kutoka 2:11-15; Waamuzi 15:11-16; 1Wafalme 11: 15-16).

mozambique-milimo

king-arthur-

 

ENGLISH: HE WHO IS FULL OF SCARS.

The origin of this saying is a creature with scars on his body. These scars are the healing wounds that resulted from the creature having the power to be invincible. The creature can do many tasks to complete it. That is why people call it ‘the one with scars.’

The saying is used comparatively to refer to any person who has the power to do jobs well and complete it on time. The person undertakes to carry out and complete his/her tasks quickly. He/she is like a creature full of scars, because he also has the power to work bring about notable successes in his life. His own life also helps other to work harder  in fulfilling their roles. That is why people call him ‘he who is full of scars.’

The saying teaches people to maximize effort to carry out their hard work and responsibilities, so that they can better support their families.

(Exodus 2: 11-15; Judges 15: 11-16; 1Kings 11: 15-16).

539. KALAGU – KIZE: MUNHU OKAYA NHALE – MHULI.

Imbuki ya kalagu yiniyo ilolile bhutale na kikalile ka mhuli. Imhuli ili ndimu nhale ya ng’wipolu, iyo igasiminzaga hulimo na bhichayo. Ijoyi jigikilaga halumo pye n’ijibhyalilwe jayo. Hunagwene abhanhu bhagiganilaga giki, ‘munhu okaya nhale’ bhashosha, ‘Mhuli.’

Ikalagu yiniyo igalenganijiyagwa kuli munhu uyo aludebhile chiza uluganda lo hakaya yakwe. Umunhu ng’wunuyo agikalaga halumo n’uluganda lokwe lunulo, ulo bhanhu abho bagikalaga  ahakaya yakwe yiniyo.

Uweyi agikolaga n’imhuli yiniyo, iyo igikalaga halumo n’ijibhyalilwe jayo, kunguno nang’hwe agikalaga halumo na luganda lo bhanhu abha hakaya yakwe umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo agabhalanjaga na bhiye inzila ja gwikala bhitogilwe umuluganda lobho. Hunagwene abhanhu bhagiganilaga giki, ‘munhu okaya nhale’ bhashosha, ‘Mhuli.’

Ikalagu yiniyo yalanga bhanhu gubhiza na witogwa bho gwiyambilija gutumama milimo chiza umukikalile kabho, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi umuwikaji bhobho.

(Mwanzo 50:22-24; 2Mambo ya Nyakati 1:4-11).

KISWAHILI: KITENDAWILI   –  TEGA: MTU WA FAMILIA KUBWA –  TEMBO.

Chanzo cha kitendawili hiki chaangalia ukubwa na umoja wa tembo. Tembo ni myamapori mkubwa ambaye hutembea pamoja na wenzake. Yeye huishi na watoto wa uzao wake.  Ndiyo maana watu hutegeana kitendawili kwamba, ‘mtu wa familia kubwa’ na kujibu, ‘Tembo.’

Kitendawili hiki hulinganishwa kwa mtu yule ambaye anafahamu kuishi vizuri na kundi la watu walioko kwenye familia yake. Mtu huyo huishi kwa upendo wa kusaidiana na watu walioko kwenye familia yake hiyo. Yeye huuendeleza umoja wao vizuri. Mtu huyo hufanana na tembo anayeishi pamoja na kizazi chake, kwa sababu naye huishi vizuri na watu walioko kwenye familia yake maishani mwake. Yeye huwafundisha pia wenzake njia za kuishi kwa upendo wa kusaidiana vizuri katika maisha yao. Ndiyo maana watu hutegeana kitendawili kwamba, ‘mtu wa familia kubwa’ na kujibu, ‘Tembo.’

Kitendawili hicho, hufundisha watu  kuwa na upendo wa kusaidiana katika kuyatekeleza vizuri majukumu yao, ili waweze kupata mafanikio mengi, maishani mwao.

(Mwanzo 50:22-24; 2Mambo ya Nyakati 1:4-11).

elephant

elephant-

ENGLISH: I HAVE A RIDDLE – LET IT COME: A PERSON WITH A BIG HOUSEHOLD – AN ELEPHANT.

The origin of this riddle is the size and unity of elephants. The elephant is a large wild animal that walks with her/her family. He/she lives with his/her children’s children. That’s why people pose a riddle, A person with a big house hold’ and respond’ ‘An elephant.’

The riddle, is used comparatively to refer to any individual who knows how to live well with a group of people in his/her family. The person loves to help other people in his family to well promote their unity.

The person is like an elephant that lives with his/her family, because he also lives well with people in his/her family. He/she also teaches others to love and help one another. That’s why people pose a riddle, ‘A person with a big household’ and respond, ‘An elephant.’

This riddle teaches people to love and help each other in fulfilling their responsibilities, so that they can get the most out of their lives.

(Genesis 50: 22-24; 2 Chronicles 1: 4-11).