myth

712. KUNTOJA NG’WANA WA NG’WIYO KUMILIWE.

“Idi ginhu ja gukamaja ugumona munhu nhebhe alifunya sabho ja guntoja ng’wana okwe. Jili ginhu ja kawaida duhu. Aliyo jili ginhu ja gukumya gumona umunhu alinfunija sabho ng’wana ong’wa ungi ja gutolela. Ugwita yawiza nulu ugungunana munhu uyo adio ludugu loko, igabhizaga guti gumiliwe; giki ili jidimu gete na bhanhu abha bhalita giki bhali bhagehu duhu.

Ulusumo lunulo lulidulanga giki ili jilidimu ugwifunya kulya bhabhu abho bhadi bhandugu. “Mininga gali madito kukila minzi.”” Lolaga Kugundua Mbegu za Injili, bhukurasa 63.

Ijitabho jinijo jigandikwa na Kamati ya Utafiti wa Utamaduni Bujora, ijojigahaririwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

“Ulu nkristo aliifunya kulwa munhu uyo adio ndugu, ubhutogwa bho ng’wa Mulungu bhushikanile gete umugati yakwe nu ung’wunuyo hunkristo unshikanu.

 Ikaya jise ija jikristo jidizubhiza kaya ijo jigacholaga solobho jajo duhu. Aliyo jibhize kaya ijo jigifunyaga gubhambilija abhangi abho bhadi bhandugu umu shida ja bhuli mbika.

Ugwifunya kulwa bhanhu bhose, nono abho bhadibhadugu bhise ili jidimu nghana. Ili kuti gumiliwe. Ugwikala jikristo guli nimo, na idi ligusha.

Umu kaya nu muwikaji bho jikristo ugwifunya jili ginhu ja kawaida, guti mayu uyoalifunya kulwa bhana, bhabyaji abho bhalifunya bho gubhalipila ada ja shule abhana. Giko na bhakristo, kaya na Jumuiya ndoo jidakililwe gwifunya noyi.” Lolaga Kugundua mbegu ja Injili, ukurasa 64.

Mambo ya Walawi 19:34.

Isaya 58:10.

Mathayo 5:46.

Mathayo 10:8.

KISWAHILI: KUMWOZA MTOTO WA MWENZAKO NI KUMEZA JIWE.

“Si jambo la kushangaza kumwona mtu fulani akitoa mahari kumwoza mwanaye. Ni jambo la kawaida tu. Lakini ni jambo la kustaajabisha kumwona mtu anayemtolea mahari mtoto wa mwingine. Kufanya wema au ufadhili kwa mtu asiye wa ukoo wako, huwa kama kumeza jiwe; yaani ni vigumu kweli na watu wanaofanya hivi ni wachache tu.

Methali hii inatufundisha kwamba ni vigumu kujitoa kwa ajili ya watu wasio ndugu. “Damu ni nzito kuliko maji.”” Rejea Kugundua Mbegu za Injili, ukurasa 63.

Kitabu hicho, kiliandikwa na Kamati ya Utafiti wa utamaduni Bujora, kilichohaririwa na watafiti: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

“Ikiwa mkristo anajitolea kwa ajili ya mtu asiye ndugu, upendo wa Mungu umekalimika kweli ndani yake na yeye ndiye mkristo kamili.

Familia zetu za kikristo zisiwe familia ambazo zinatafuta faida zao tu. Bali ziwe familia zinazojitolea kwa kuwasaidia wengine wasio ndugu katika shida mbalimbali.

Kujitolea kwa ajili ya watu wote, hasa wale wasio ndugu kwetu ni vigumu kweli. Ni kama kumeza jiwe. Kuishi kikristo ni kazi, na siyo mchezo.

Katika familia na maisha ya kikristo kujitoa ni kitu cha kawaida, k.m. mama anayejitoa kwa ajili ya watoto, wazazi ambao wanajitoa kwa kulipa ada za shule za watoto. Pia wakristo, familia na Jumuiya Ndogo Ndogo zinaitwa kujitoa zaidi.” Rejea Kugundua mbegu za Injili, ukurasa 64.

Mambo ya Walawi 19:34. “Mgeni anayeishi pamoja nawe ni lazima umtendee kama mmoja wa wazawa wa nchi yako. Mpende kama unavyojipenda mwenyewe, kwa maana ulikuwa mgeni katika nchi ya Misri. Mimi ndimi BWANA Mungu wako.”

Isaya 58:10. “nanyi kama mkimkunjulia mtu mwenye njaa nafsi zenu na kutosheleza mahitaji ya walioonewa, ndipo nuru yenu itakapong’aa gizani, nao usiku wenu utakuwa kama adhuhuri.”

Mathayo 5:46. “Kama mkiwapenda wale wanaowapenda tu, mtapata thawabu gani? Je, hata watoza ushuru hawafanyi hivyo?”

Mathayo 10:8. “Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo wachafu. Mmepata bure, toeni bure.”

stone1

lovely black marriage

bhitoji

 

ENGLISH: PAYING DOWRY FOR YOUR FELLOW’S SON IS LIKE SWALLOWING A STONE.

It is not strange to see someone paying dowry for his son, but it is not easy to see someone paying dowry for someone’s son. Sacrificing your wealth for someone else is hard. It is like swallowing a stone.

This proverb teaches us that it is difficult to make sacrifice for for people who are not your relative. “Blood is thicker than water” (Refer to Kugundua Mbegu za Injili, which means ‘Discovering the Seed of the Gospel,’ page 63). This book was written by the Bujora Cultural Research Committee, edited by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1993.

If a Christian offers himself for a non-brother, then the love of God is firmly rooted in him and he is a complete Christian.

Our Christian families should not be families that are only seeking their own advantage. Rather, be families dedicated to helping others who are not brothers in various situations.

Volunteering for all people, especially those who are not our relatives, is really hard. It’s like swallowing a stone, but we need to abide by God’s commandments that we have to love and help each other in solving problems.

In Christian life, giving is a common practice, for example, helping widows, paying school fees, etc. Christians, families, and small christian communities are called upon to make a greater commitment on helping the needy people (See ‘Discovering Gospel Seeds,’ page 64).

Leviticus 19:34. Isaiah 58:10. Matthew 5:46. Matthew 10: 8.

711. MASABHO MABHONWA BHUPANGA BHULAMBU.

“Ulusumo lunulu lugatumikaga ahikanza munhu ojimijaga sabho jakwe ijo ojipandikila kuluyilo. Jigemelo: Gwibhilwa ng’ombe. Agazunyaga gujimija sabho kukila bhupanga bhokwe aliyomba: “Masabho mabhonwa bhupanga bhulambu.” Isabho jili ndogu. Ubhupanga bhuli na solobho kukila sabho. Umunhu uyo ocha adadulile guchola sabho hangi.” Lolaga Kugundua Mbegu za Injili, bhukurasa 61.

Ijitabho jinijo jigandikwa na Kamati ya Utafiti wa Utamaduni Bujora, ijojigahaririwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agadililaga bhupanga kukila sabho, umuwikaji bhokwe. Umunhu ng’wunuyo, agabhalangaga na bhiye inzila jagubhulonja ubhupanga bho bhanhu bhabho, kukila umobhagajilongejaga isabho jabho. Hunagwene umunhu ng’wunuyo, agabhawilaga abhanhu giki, “masabho mabhonwa bhupanga bhulambu.”

 “Umuwikaji wise ubhupanga bho mili bhuli ginhu ja solobho ubhodubhutogilwe na dugabhulang’hanaga kuliko maginhu gose. Hangi dugatumilaga bhuli nzila bhudizujimila nulu bhudizukenaguka.

UYesu Kristo agiza ahasi adinhe bhupanga, idibhupanga bho mili, aliyo bhupanga bho ng’wa Mulungu ng’winikili. (Lolaga Yohane 10:10). UBhupanga bhunubhu bhugigelaga bho gunzunya Yesu Kristo uyo otung’wa na Mulungu B’ab’a (lolaga Yohane 3:16). Yilihoyi solobho ki uguyipandika pye uyamusi na gubhugaiwa ubhupanga ubho bhugigelaga bhule bho guzunya? Nulu yili na solobho ki ugwikomanya nu Mulungu?

Ulusumo lunulu lodulanga gubhudilila ubhupanga ubho bhulunga kele ubhobhudashilaga kukila gugadilila maginhu gamusi ayo gadalamaga (Lolaga 2Kor. 4:18). Hangi lodulanga gubhulang’hana ubhupanga wise ubho mili, na guiliga yose iyoidulile gubhubhipya ubhupanga bhunubho.” Lolaga Kugundua Mbegu za Injili, 62.

Mathayo 19:16.

Marko 8:36.

Yohane 3:16.

Yohane 6:27.

Yohane 10:10.

KISWAHILI: BORA UHAI KULIKO MALI.

“Methali hii hutumika wakati mtu apotezapo mali yake aliyoichuma kwa jasho. Kwa mfano: Kuibiwa ng’ombe. Akakubali kupoteza mali kuliko maisha yake akisema: “Bora uhai kuliko mali iwezayo kupatikana tena.” Mali ni rahisi. Uhai ni bora kuliko mali. Mtu aliyekufa hawezi kutafuta mali tena.” Rejea Kugundua Mbegu za Injili, ukurasa 61.

Kitabu hicho, kiliandikwa na Kamati ya Utafiti wa utamaduni Bujora, kilichohaririwa na watafiti: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu yule anayejali zaidi uhai wa watu kuliko mali, katika maisha yake. Mtu huyo hufundisha pia wenzake namna ya kuthamini zaidi uhai wa watu wao, kuliko wanavyothamini mali zao. Ndiyo maana mtu huyo huwaambia watu kwamba, “Bora uhai kuliko mali iwezayo kupatikana tena.”

“Katika maisha yetu uzima wa kimwili ni jambo muhimu ambao tunaupenda na kuutunza kuliko mambo yote. Tena tunatumia kila njia usipotee au usiharibike.

Yesu Kristo alikuja hapa duniani atupe uzima, siyo uzima wa kimwili, bali uzima wa Mungu mwenyewe. (Tazama Yohane 10:10). Uzima huu unapatikana kwa kumwamini Yesu Kristo aliyetumwa na Mungu baba (tazama Yohane 3:16). Kuna faida gani kupata ulimwengu wote na kukosa uzima unaopatikana bure kwa imani? Au kuna faida gani kujitenga na Mungu?

Methali hii yatufundisha kuzingatia uzima wa milele unaodumu kuliko kuzingatia mambo yasiyodumu (Taz. 2Kor. 4:18). Tena yatufundisha kutunza uzima wetu wa kimwili, na kuepuka yote yanayoweza kuuharibu uzima ule.” Rejea Kugundua Mbegu za Injili, ukurasa 62.

Mathayo 19:16. “Mtu mmoja akamjia Yesu na kumwuliza, “Mwalimu mwema, nifanye jambo gani jema ili nipate uzima wa milele?””

Marko 8:36. “Mtu atafaidiwa nini kama akiupata ulimwengu wote lakini akaipoteza nafsi yake?”

Yohane 3:16. “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.”

Yohane 6:27. “Msishughulikie chakula kiharibikacho, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele, ambacho Mwana wa Adamu atawapa. Yeye ndiye ambaye Mungu Baba amemtia muhuri.”

Yohane 10:10. “Mwivi huja ili aibe, kuua na kuangamiza. Mimi nimekuja ili wapate uzima kisha wawe nao tele.”

masai1

nsabhi masai

bhatalii bha bhuganda

ENGLISH: LIFE IS BETTER THAN WEALTH.

This saying has its origin on losing wealth one has accumulated for a long time. One can lose wealth through being stolen, burnt by fire and other calamities. When this happens, as a way to comfort oneself, one can come up with this saying that ‘life is better than wealth.’ As long as one is still alive, he/she can look for more wealth but it is impossible for someone dead to look for properties (Refer to Kugundua Mbegu za Injili, which means ‘Discovering the Seed of the Gospel,’ page 61).

This book was written by the Bujora Cultural Research Committee, edited by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1993.

This saying can be compared to a person who cares more about human life than material things. The person also teaches his/her colleagues how to value other people’s lives more than they value their property.

In our lives, physical well-being is the most important thing than anything else. We have to protect our life so that it doesn’t get lost or destroyed.

Jesus Christ came to earth to give us life, not physical life, but the life of God himself (See John 10:10). This life is obtained by believing in Jesus Christ sent by God the Father (see John 3:16). What good is it to gain the whole world and to lose  etenarl? Or what are the benefits of separating yourself from God?

This saying teaches us to focus on eternal life rather than perishable things (cf. 2 Cor. 4:18). It also teaches us how to take care of our physical well-being, and to avoid anything that might destroy that life (See ‘Discovering Gospel Seeds,’ page 62).

Matthew 19:16. Mark 8:36. John 3:16. John 6:27. John 10:10.

710. NYAMA YAWIZA KUKILA NYAMA YOSE ILI KINEHE? NA NYAMA YABHUBHI KUKILA NYAMA YOSE ILI KINEHE?

“Bhugigela wihalaliki bho bhanhu bhabhili higulya ya libhujo ili: Inyama ya wiza kukila nyama yose ili kinehe? Na Nyama yabhubhi kukila nyama yose ili kinehe? Abhanhu abhabhili bhenabho bhagigasha, bhuhoya na gukengela aliyo adadulile nulu umo ugupandika ilishosho ilya gunfuja ung’wiye. Uumo o bhanhu abhabhili bhenabho witanagwa Ivigiri. Aho bhamala uwihalaliki bhunubho, uIvigiri agaja gujichobhela milimo. Ugajiliwa nimo go bhuzugi na munhu umo nkumuku uyo olinsabhi gete gete.

Lushigu lumo unsabhi ng’wunuyo agenhelwa mhola giki abhabyaji bhakwe bhalihaya gwiza aha kaya yakwe bhangishe. Agang’witana UIvirigi bhiinhe miganiko umo bhalabhasumbilile abhabyaji bhenabho. Bhagiyangula giki ulushugu ulo gubhabokela abhabyaji, abhanwani bha nsabhi ng’wunuyo nibhabhilingwa kugiki ulushigu lunulo lubhize lushigu lo gwizukwa na bhanhu bhingi umo ilidulikanila. Lulu, ulushugu ulo gushiga abhabyaji na bhanwani lugashika.

Unsabhi ung’witana untumami okwe uIvigiri ung’wila, “Jaga kuligulilu. Nalihaya ugule inyama iyawiza kulebha jose, iki ilelo abhabyaji na bhanwani bhane bhagulya henaha. Ilelo luli lushigu lo gwizukwa.”

UIvigiri uwizuka ubhihalaliki ubho bhugigela aho bhali nu nwani okwe ubho bhuli: “Inyama yawiza kukila nyama yose ili kinehe? Na Nyama yabhubhi kukila nyama yose ili kinehe?”

Agaja muligulilu alibhuja niogula nyama ki, luguku, jigubha, mhigo, matima nulu mbazu? Wiyangula gugula lulimi. Uluchala kaya nagwandya guluzuga. Unsabhi unsanga na gung’wila ashoke hangi ukuligulilu agagule nyama iyabhubhi kukila jose ayizuge lwande niyo ili yawiza kukila jose.

UIvigiri agaja hangi ukwigulilu wiyangula gugula lulimi hangi. Ushoka wangu na guluzuga ululimi ulo kabhili ahalwande lungi nulo gwandya. Imhindi abhabyaji na bhanwani bha nsabhi bhaganguha ugushika, bhubhakaribhusha chiza.

Unsabhi unhadika uIvigiri ayenhe gwandya inyama iyawiza kukila yose. Aho lyabhita ikanza bhandya gulya. Aho bhalilya unsabhi agankumilija uIvigiri giki oli nzugi mmani uyo agadula guzuga jiliwa jawiza.

Ahanuma ya yiniyo, unsabhi unhadika uIvigiri wenhe inyama iyo yiliyabhubhi kukila yose. UIvigiri agalwenha ululimi ulo kabhili, ulu tuula aha meza na guja kuliko haho na haho.

Unsabhi ahoyilingula inyama yiniyo bho witegeleja agabhulucha giki idabhizile heke nulu hadoo niyo yali ya gwandya. Aganondeja uIvigiri ukuliko na gung’wila Ivigiri bho bhukali, “Ivigiri, nayombaga wenhe nyama yabhubhi kukila nyama yose. Udigwaga?” Ivigiri agashosha, “Ng’hana iyo niyenhaga ihaha hiyene inyama iyabhubhi kukila yose.”

Unsabhi wingililwa bhupelanu bhukali na bho nduhu ugudilila abhageni agandukila uIvigiri aliyomba, “Nhala ntale ebhe! Udadulile ugumana ginhu. Nalinagutumaga ugenhe nyama ja mbika ibhili: imo yabhiza kukila yose na yingi yabhubhi kukila yose. Ukubhuhala bhoko wenhaga mbika imo duhu ya nyama. Onipondaga soni habhutongi ya bhabyaji bhane na bhanwani bhane. Kwingila haha yiniyi nagulechaga unimo. Ingaga! Jaga lyako.”

UIvigiri agahaya gwitetea hadoo. Agabhawila abhabyaji na bhanwani bha nsabhi giki “guli go nhana gete igiki inyama iyawiza kukila yose luli lulimi: iki ulu ubhiza na lulimi lowiza udulile gubhiza na bhabyaji abho bhagutogilwe, na bhanwani bhingi, majikolo mingi aga solobho nu bhebhe ng’winikili ugubhiza munhu ogukumilijiwa. Ichene, ulutumile chiza duhu, ululimi loko ufunye ilaka lyawiza.

Ukulwande ulungi,”  agendelea uIvigiri guyomba, “Ululimi ludulile gubhiza nyama yabhubhi kukila yose umusi; kunguno ulu uli ni laka lyabhubhi ugalutumilaga ululimi loko gudukila bhanhu, guyomba bhulomo lomo, gulisanya bhanhu na gusiga, lulu ugulwita ululimi loko guti wandijo bho gwiduma na bhabyaji bhako, bhanwani bhako mpaga ugubhiza munhu o sagala gete.”

Abhageni bhagabhona inguno ya ndimi ijibhili jinijo ijoagajibheja uIvigiri na aho bhiganika noyi bhagazunya giki olinikujo.” Lolaga Kugundua Mbegu za Injili, bhukurasa 50-51.

Ijitabho jinijo jigandikwa na Kamati ya Utafiti wa Utamaduni Bujora, ijojigahaririwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

“Gutumo dasomelaga umu lugano lyise, ululimi luli ginhu ijo jidulile gutumilwa ku nzila ibhili: Ku nzila yawiza na ku nzila yabhubhi. Ululimi lunulo ulo lugankujaga mulungu gunkumilija na gunamya ludulile gugaluka na gutumilwa bho gundukila na gundalaha. Ululimi lunulo ulo lugabhejaga widebhi wiza na bhanhu ludulile hangi gutumilwa bho gubhubomola uwidebhi bhunubho.

Dunombe Mulungu B’ab’a nema ya giki bhuli mhayo uyo duliguyomba duguyombe ku likujo lya lina lyakwe, nulu bho gubheja widebhi wiza na bhanhu.

Umukaya jise bhuli hoyi wasa bho heke bhuli ikanza ubho gunkuja Mulungu na gubheja bhumo bho gulutumila ululimi chiza.” Lolaga Kugundua Mbegu za Injili, ukurasa 52.

Zaburi 35:28.

Luka 1:64.

Waefeso 4:29.

1Petro 3:10.

KISWAHILI: IPI NYAMA NZURI KUPITA ZOTE NA IPI NYAMA MBAYA KUPITA ZOTE?

“Ulizuka ubishi kati ya watu wawili kuhusu swali hili: ni ipi nyama nzuri kupita zote na ipi nyama mbaya kupita zote? Watu hao wawili walikaa, wakajadili na kuchunguza lakini hata mmoja hakuweza kupata jibu lililomridhisha mwenzake. Mmoja wa watu hawa wawili aliitwa Ivigiri. Baada ya ubishi ule, Ivigiri akaenda kujitafutia kazi. Akaajiriwa kazi ya upishi na mtu mmoja maarufu ambaye alikuwa tajiri kweli kweli.

Siku moja yule tajiri akaletewa habari kwamba wazazi wake walitaka kuja nyumbani kwake wamsalimu. Akamwita Ivigiri washauriane jinsi ya kuwakaribisha wale wazazi. Walionelea kuwa siku ya kuwapokea wazazi, marafiki wa yule tajiri wangealikwa ili siku hiyo ipate kuwa siku ya kukumbukwa na watu wengi itakavyowezekana. Basi, siku ya kufika wazazi na marafiki ikawadia.

Tajiri akamwita mtumishi wake Ivigiri akamwambia, “Nenda sokoni. Nataka ununue nyama nzuri na safi kushinda zote, maana leo wazazi na rafiki zangu watakula hapa. Leo ni siku ya kukumbukwa.”

Ivigiri akakumbuka ubishi aliowahi kuwa nao baina yake mwenyewe na rafiki zake, nao ni: “Ipi nyama nzuri kupita zote na ipi nyama mbaya kupita zote?” Akaelekea sokoni akijiuliza angenunua nyama ya namna gani, nundu, kidari, figo, maini au mbavu? Akakata shauri kununua ulimi. Akaupeleka nyumbani na kuanza kuupika. Tajiri akamwendea na kumwambia arudi tena sokoni anunua nyama mbaya kushinda zote aipike mbali na ile nyama nzuri kupita zote.

Ivigiri akaelekea tena sokoni akakata shauri kununua tena ulimi. Akarudi mapema na kuupika ulimi wa pili kando ya ule wa kwanza. Jioni wazazi na warafiki wa tajiri wakawasili, wakakaribishwa vizuri.

Tajiri akamwamuru Ivigiri alete kwanza nyama nzuri kushinda zote. Baada  ya muda wakaanza kula. Walipokuwa wakila tajiri akamsifu Ivigiri kwamba alikuwa mpishi hodari aliyeweza kupika chakula safi. Baadaye tajiri akamwamuru Ivigiri alete ile nyama mbaya kushinda zote. Ivigiri kauleta tena ulimi wa pili, kauweka mezani na kuelekea jikoni mara moja.

Tajiri alipokagua nyama ile kwa makini aligundua kuwa haikuwa tofauti hata kidogo na ile ya kwanza. Akamfuata Ivigiri jikoni na kumwambia Ivigiri kwa hasira, “Ivigiri, nimesema lete nyama mbaya kushinda zote. Husikii?” Ivigiri akajibu, “Hakika niliyoleta sasa hii ndiyo nyama mbaya kushinda zote.”

Tajiri akaingiwa na hasira kali na bila kujali wageni alimtukana Ivigiri akisema, “Mjinga mkubwa we! Huwezi kuelewa kitu. Nilikuagiza ulete nyama za aina mbili: moja nzuri kupita zote na nyingine mbaya kushinda zote. Kwa upumbavu wako umeleta aina moja tu ya nyama. Umeniaibisha mbele ya wazazi wangu na marafiki wangu. Toka sasa hivi nimekuachisha kazi. Ondoka! Nenda zako.”

Ivigiri akataka kujitetea kidogo. Akawaambia wazazi na marafiki wa tajiri kuwa “ni kweli kabisa kwamba nyama nzuri kuliko zote ni ulimi: maana ukiwa na ulimi mzuri unaweza kuwa na wazazi wanaokupenda, marafiki wengi, vitu vingi vya thamani na wewe mwenyewe utakuwa mtu anayesifiwa. Mradi tu uutumie ulimi wako utoe kauli nzuri.

Kwa upande mwingine,” akaendelea Ivigiri kusema, “Ulimi unaweza kuwa nyama mbaya kushinda zote duniani; kwa sababu kama ukiwa na kauli mbaya ukautumia ulimi wako kutukana watu, kusema uongo, kuchonganisha watu na kusengenya, basi utaufanya ulimi wako kama chanzo cha kukosana na wazazi wako, rafiki zako hata ukawa mtu ovyo kabisa.”

Wageni waliona maana ya ndimi zile mbili alizotayarisha Ivigiri na baada ya kufikiri sana wakakubali kuwa alikuwa na hekima.” Rejea Kugundua Mbegu za Injili, ukurasa 50-51.

Kitabu hicho, kiliandikwa na Kamati ya Utafiti wa utamaduni Bujora, kilichohaririwa na watafiti: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

“Kama tulivyosoma katika hadithi yetu, ulimi ni kitu ambacho kinaweza kutumika kwa njia mbili: Kwa njia nzuri na kwa njia mbaya. Ulimi ule ule unaomtukuza Mungu kumsifu na kumwabudu unaweza kugeuka na kutumika kwa kumtukana au kumdharau. Ulimi ule ule unaojenga uhusiano mwema na watu unaweza tena kutumika kwa kubomoa uhusiano huo.

Tumwombe Mungu Baba neema ya kwamba kila neno tusemalo lisemwe kwa utukufu wa jina lake, au kwa kujenga uhusiano mwema na watu.

Katika familia zetu kuna nafasi maalum kila wakati kumtukuza Mungu na kujenga umoja kwa kutumia ulimi vizuri.” Rejea Kugundua Mbegu za Injili, ukurasa 52.

Zaburi 35:28. “Ulimi wangu utanena haki yako na sifa zako mchana kutwa.”

Luka 1:64. “Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.”

Waefeso 4:29. “Maneno mabaya yasitoke vinywani mwenu, bali yale yafaayo kwa ajili ya kuwajenga wengine kulingana na mahitaji yao, ili yawafae wale wasikiao.”

1Petro 3:10. “Kwa maana, “Ye yote apendaye uzima na kuona siku njema, basi auzuie ulimi wake usinene mabaya na midomo yake isiseme hila.”

tongues1

tongues grilled-meat

tongues

tongues3

 

ENGLISH: WHICH IS THE BEST MEAT AND WORST MEAT?

Once upon a time, there was a debate between two boys on which is the best meat and which one is the worst meat. They debated for quiet a long time without having an answer for that. One of these two debators was known by the name of Ivigiri. After their debate, Ivigiri left to look for job. Fortunate enough, he came to be employed by one of the rich person who employed Ivigiri as a cook.

One day the rich man told Ivigiri that his parents (the rich man’s parents) and friends will visit him and this rich person would like to make this day a remarkable day in his life. Therefore, he needs to have enough and delicious food to feed his parents and friends.

On the day the visitors came, Ivigiri was told by his boss to go buy the best meat for the guests. As Ivigiri was going to the marketplace to buy this meat, he kept on pondering himself, what is the best meat? He began recalling their earlier debate with his friend. Should he buy hump meat, brisket,kidney or rib? He finally decided to buy the cow’s tongue. He cooked the tongue. When his boss saw it, he appreciated but told him (Ivigiri) to go back to the marketplace and buy the worst meat and cook it separately. Ivigiri went to the market again and bought another piece of cow’s tongue and cooked as instructed by his boss.

 When the guests and Ivigiri’s boss had tasted the food, they appreciated Ivigiri’s art of cooking because it tasted so good. Later on the boss ordered Ivigiri to bring the worst food. Ivigiri brought the food and left for kitchen. The boss examined the meat considered to be the worst and he realized that it was the same as the first one.

He became so furious to the extent of shouting to Ivigiri: “Ivigiri, I said bring the worst meat. Don’t you hear? ” Ivigiri replied, “surely what I brought now is the worst meat of all.”

The rich man became very angry and he insulted Ivigiri saying, “Great fool! You can’t understand anything. I ordered you to bring two kinds of meat: the best and the worst meat. To your stupidity you have brought only one type of meat. You have humiliated me in front of my parents and friends. From now on be out of my house. “Get out!”

Ivigiri wanted to defend himself. He told his boss and the guests that “it is absolutely true that the best meat is the tongue: for if you have a good tongue you can have parents who love you, many friends, many valuable things and you will be the one to be praised. What matters is making use of the tongue in showing kindeness to others.

Continued Ivigiri, “the tongue can be the worst meat in the world; because if you have a bad language and  you use your tongue to curse people, to lie, to confuse and gossip, then you will make your tongue a source of confrontation with your parents, your friends to the point that you become a total nuisance. ”

The guests realized the meaning of the two languages manifested in the tongue. After a thorough thinking, theses guests acknowledged that Ivigiri was wise (Refer to Kugundua Mbegu za Injili, which means ‘Discovering the Seed of the Gospel,’ pages 50-51). This book was written by the Bujora Cultural Research Committee, edited by researchers: Patriarch Donald Sybertz, M.M., and Patriarch Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1993.

As we have read in our story, the tongue is something that can be used in two ways: for good and for bad. The same language that glorifies God and worships Him can be turned around and and be used to insult or discredit Him. The same language that builds a good relationship with people can also be used to break down that relationship.

May we ask God the Father for grace that every word we say be spoken in the glory of His name, or in building good relationship with the people.

In our families there is always a special opportunity to glorify God and build unity by using the tongue well (See ‘Discovering Gospel Seeds,’ page 52).

 Psalm 35:28. Luke 1:64. Ephesians 4:29. 1 Peter 3:10.

709. BHUJINGI WAKO NG’WANA INYAMI WALEMA KOYA.

“Umulyimbo linili ilya jisuguma Ningi umo Makwenu aganhugula ningi ng’wiye, Jibishi Ng’wana Inyami, ahigulya ya bhubhi bho kajile kakwe umuwikaji nono umubhujingi.

Ilyimbo linulo liligiki, “Ubhujingi bhoko nwani one Ng’wana Inyami walema koya. Nulu, duyombe ologelejiwa kubhujingi? Sengwa ishigu jako jilingehu, jidi kule makumi atano. Mujigila ugujikwa ndugu one, Ng’wana Inyami. Ugucha guti mva, iginhu jako ija bhujingi. Abhiyo hambohambo ng’ombe, ubhebhe isonga munhumbi. Sengwa lekaga ubhujingi bhoko, ishigu jako jidikule. Mujigila ugujikwa ndugu one, Ng’wana Inyami.” Lolaga Kugundua Mbegu za Injili, bhukurasa 46.

Ijitabho jinijo jigandikwa na Kamati ya Utafiti wa Utamaduni Bujora, ijojigahaririwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

“Gwandija kale Ikanisa igadulangaga gwikala jitakatifu na guduhugula ahigulya ya kajile akabhubhi umuwikaji. Ulushigu lo bhatizimu yise dugazunya gubhuzula ubhumunhu wise ubho kale kihamo na miito gabho gose agabhubhi na gunzwala Yesu Kristo.

 Hangi giki, jilihoyi iginhu ijingi ijabhubhi ijojigajilanijaga na bhujingi, dugemele guti bhusatu bho BHUKIMWI (AIDS) ubho bhugagubhinhyaga bhupanga.

Nono ishigu jiniji bhuli nyanda nulu ng’waniki, alanhale ubhupanga bhokwe jisoga na abhize na bhulumani bho mugati nu Mulungu. Na bhose bhizuke giki umo guli unpango go ng’wa Mulungu umu witoji ya jizunya, ali ngosha umo na nkima umo. Uguyela na ungi ili hanze ya npango go ng’wa Mulungu.”  Lolaga Kugundua Mbegu za Injili, bhukurasa 47.

Mathayo 5:27-28.

Mathayo 15:19.

1Wakorintho 6:18.

Wakolosai 3:8.

KISWAHILI: UASHERATI WAKO UMEZIDI RAFIKI YANGU MWANA INYAMI.

“Katika wimbo huu wa Kisukuma manju mmoja Makwenu anamwonya manju mwenzake, Jibishi mwana Inyami, kuhusu ubaya wa mwenendo wake maishani, hasa uasherati. Tafsiri ya wimbo huo kwa Kiswahili ni hii:

“Uhuni wako umezidi rafiki yangu, Mwana Inyami. Ama, tuseme umelogwa kwa hayo mambo ya kihuni? Sengwa siku zako chache, siyo mbali hamsini. Kaburini utazikwa ndugu yangu, Mwana Inyami. Utakufa kama mbwa, kwa mambo hayo ya kihuni. Wenzio bora ng’ombe, wewe mshale tumboni. Sengwa acha wako uhuni, siku zako siyo mbali. Kaburini utazikwa ndugu yangu, Mwana Inyami.” Rejea Kugundua Mbegu za Injili, ukurasa 46.

Kitabu hicho, kiliandikwa na Kamati ya Utafiti wa utamaduni Bujora, kilichohaririwa na watafiti: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

“Tangu zamani kanisa linatufundisha kuishi kitakatifu na kutuonya kuhusu mwenendo mbaya maishani. Siku ya ubatizo wetu tulikubali kuvua utu wetu wa kale pamoja na matendo yake yote mabaya na kumvaa Yesu Kristo.

Tena kuna mambo mengine mabaya yanayoambatana na uasherati, kwa mfamo, ugonjwa wa UKIMWI (AIDS) unaofupisha maisha.

Hasa siku hizi kila kijana achunge maisha yake vizuri na awe na uhusiano wa ndani na Mungu. Pia wote wakumbuke kwamba kadiri ya mpango wa Mungu katika ndoa ya Kikristo kuna mume mmoja na mke mmoja. Kutembea na mwingine ni nje ya mpango wake Mungu.” Rejea Kugundua Mbegu za Injili, ukurasa 47.

Mathayo 5:27-28. “Mmesikia kwamba ilinenwa, ‘Usizini’. Lakini mimi nawaambia: kwamba ye yote amtazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.”

Mathayo 15:19. “Kwa maana ndani ya moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na masingizio.”

1Wakorintho 6:18-20. “Ikimbieni zinaa. Dhambi nyingine zote atendazo mtu ziko nje ya mwili wake, lakini yeye aziniye hutenda dhambi ndani ya mwili wake mwenyewe. Je, hamjui ya kwamba miili yenu ni hekalu la Roho Mtakatifu, akaaye ndani yenu, ambaye mmepewa na Mungu? Ninyi si mali yenu wenyewe, kwa maana mmenunuliwa kwa gharama. Kwa hiyo mtukuzeni Mungu katika miili yenu na katika roho zenu ambazo ni mali ya Mungu.”

Wakolosai 3:8. “Lakini sasa yawekeni mbali nanyi mambo kama haya yote, yaani: Hasira, ghadhabu, uovu, masingizio na lugha chafu kutoka midomoni mwenu.”

singing flutes music sound

AFRICAN DANGIN GROUP

 

people singing

 

ENGLISH: YOUR FORNICATION BEHAVIOUR MY FRIEND INYAMI’S SON IS TOO MUCH.

This saying comes from one of the Sukuma song where a singer, Makwenu, warns his fellow singer Inyami’s son about his evil deeds; being a fornicator. The song goes as follows:

Your fornication is too much my friend  Inyami’s son. Are you bewitched? Stay away from your fornication, you have few days to live on eath, not more than fifty from now. You will soon be buried my brother, Inyami’s son. You will die like a dog, with those evil things (Refer to Kugundua Mbegu za Injili, which means ‘Discovering the Seed of the Gospel,’ page 46).

This book was written by the Bujora Cultural Research Committee, edited by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1993.

The church has long taught us to live holy and has warned us about the bad ways of life. On the day of our baptism we agreed to strip off our old personality with all its evil deeds and put on Jesus Christ.

There are also other negative consequences associated with fornication, such as AIDS.

Every young man should look at his life well and have a close relationship with God. All should also remember that, according to God’s plan, for Christians, marriage has to do with one man, one woman. Having extramarital relationship is not God’s plan (See ‘Discovering Gospel Seeds,’ page 47).

Matthew 5: 27-28. Matthew 15:19. 1 Corinthians 6:18. Colossians 3: 8.

708. KALAGU – KIZE. LINSHISHI LYA HA NG’WANE LWAGWA MANEFUNEFU. NULU NG’WANA AKULIYOBA:- NONO JA NG’WA MAYU.

Ikalagu yiniyi igalenganijiyagwa na linti lya nshishi ilo lilina bhushishi wingi nu mayu myaji uyo alonghya ng’wana okwe. Guti umo ligabyalilaga noyi ilinshishi bhushishi ubho mpaga bhugaginamyaga amatambi galyo, mpaga giki ung’wana agadulaga ugubhuyobha ubhushishi bholyo.

Giko umayu umyaji umo agang’ongheja na gunanhana ung’wana okwe. Ikalagu yiniyi ilidolekeja bhutogwa bho ng’wa mayu ukuli ng’wana okwe.” Lolaga Kugundua Mbegu za Injili, ukurasa 43.

Ijitabho jinijo jigandikwa na Kamati ya Utafiti wa Utamaduni Bujora, ijojigahaririwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

“Ikalagu yiniyi ilidulanga guti umo umayu myaji atogelilwe ugunhanghana na gunhisha ung’wana okwe. Makanza gose umoyo gokwe ugojimayu guling’waje ukuli ng’wana okwe oseose.

 Ubhutogwa bho ng’wa Mulungu ukubhise nghangala ningi umu Biblia bhugalinganijiyagwa na bhutogwa bho ng’wa mayu umyaji ukuli ng’wana okwe. UMulungu adutogilwe guti mayu umyaji umo antogelilwe ung’wana okwe. (Lolaga Isaya 49:14-15).

Umukabhila ya Bhamasai bhagang’witanaga UMulungu kulina lya ng’wa “Mayu  uyo agonghyaga.” Hangi ilikanisa Alimayu wise. “Ulududuzunyaga ikigi Ikanisa alimayu wise nu Mulungu dudula uguyomba giki ali B’ab’a” (Mt. Augustino).

Uludulema ugulikumilija ilikanisa dulilema ugunkumilija UMulungu B’ab’a (lolaga Luka 10:16). IKanisa ali mayu uyo adutogilwe na agadulanghanaga ayise bhana bhakwe bho nduhu bhukomanya nulu bhubhaguzi. Makanza gose umoyo gokwe ugojimayu goling’waje uku bhana bhakwe. IKanisa ali mayu wise uyo agadubyalaga umuSakramenti ya bhatizimu (Lwinze lo bhatizimu hi nhumbi ya Kanisa), uyo agadulishaga na gudung’wisha umu Sakramenti ya Ekaristi.

Hangi UBikira Maria ali mayu. Ali mayu o ng’wa Yesu na mayu wise guti umo dulisomela umu Injili ya ng’wa Yohane (lolaga Yohane 19:26-27). Uweyi hu mayu uo Kanisa, hu mili gokwe UYesu Kristo.  Guti nu mayu myaji umo agalumilagwa bhusungu mpaga ung’wana abyalwe, giko nu mayu wise u Bikira Maria agadubhonelaga bhupina ayise bhana bhakwe mpaga UKristo ashikane umugati yise.” Lolaga Kugundua Mbegu za Injili, ukurasa 44.

Isaya 49:15-16.

Isaya 66:12-13.

Zaburi 133:2.

Wagalatia 4:26-27.

Luka 10:16.

KISWAHILI: KITENDAWILI   –   TEGA.

MKWAJU WANGU UMEJAA KOCHOKOCHO. HATA MTOTO ANAWEZA KUCHUMA:- MATITI YA MAMA.

Kitendawili hiki kinafananisha mti wa mkwaju wenye matunda mengi na mama mzazi anayemnyonyesha mtoto wake. Kama mkwaju ukizaa sana, matawi huinama kiasi kwamba hata mtoto aweza kuchuma matunda yake.

Ndivyo mama mzazi anavyomnyonyesha na kumtunza mtoto wake. Kitendawili hiki kinatuonesha upendo wa mama kwa mtoto wake. Rejea Kugundua Mbegu za Injili, ukurasa 43.

Kitabu hicho, kiliandikwa na Kamati ya Utafiti wa utamaduni Bujora, kilichohaririwa na watafiti: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

“Kitendawili hiki kinafundisha kama mama mzazi anavyopenda kumtunza na kumlisha mtoto wake. Daima moyo wake wa kimama uko wazi kwa mtoto wake yeyote.

Upendo wa Mungu kwetu sisi mara nyingi katika Biblia unalinganishwa na upendo wa mama mzazi kwa mtoto wake. Mungu anatupenda kama mama mzazi anavyompenda mtoto wake. (Tazama Isaya 49:14-15).

Katika lugha yao Wamaasai wanamwita Mungu kwa jina la “Mama Anyonyaye.” Tena kanisa ni Mama Yetu. “Tusipokubali kuwa kanisa ni mama yetu hata Mungu hatuwezi kusema kwamba ni Baba” (Mt. Agustino).

“Tukikataa kulisifu kanisa tunakataa kumsifu Mungu Baba (tazama Luka 10:16). Kanisa ni mama anayetupenda na kutulinda sisi watoto wake bila ugaguzi. Daima moyo wake wa kimama uko wazi kwa watoto wake. Kanisa ni mama yetu anayetuzaa katika Sakramenti ya Ubatizo (Kisima cha ubatizo ni tumbo la kanisa), anayetulisha na kutunywesha katika Sakramenti ya Ekaristi.

Pia Bikira Maria ni mama. Ni mama wa Yesu na Mama yetu kama tulivyosoma katika Injili ya Yohane (tazama Yohane 19:26-27). Yeye ndiye mama wa kanisa, yaani mwili wake Yesu Kristo. Kama mama mzazi anavyoona uchungu mpaka mtoto azaliwe, vilevile Mama yetu Bikira Maria anavyotuonea uchungu sisi watoto wake mpaka Kristo akamilike ndani yetu.” Rejea Kugundua Mbegu za Injili, ukurasa 44.

Isaya 49:15-16. ““Je, mama aweza kumsahau mtoto aliyeko matitini mwake akinyonya?  Wala asiwe na huruma juu ya mtoto aliyemzaa?  Ingawa anaweza kusahau, Mimi sitakusahau wewe! Tazama, nimekuchora kama muhuri katika    vitanga vya mikono yangu, kuta zako zi mbele yangu daima.”

Isaya 66:12-13. “Kwa kuwa hili ndilo asemalo BWANA: “Nitamwongezea amani kama mto, nao utajiri wa mataifa kama kijito kifurikacho, utanyonya na kuchukuliwa mikononi mwake na kuchezeshwa magotini pake. Kama mama anavyomfariji mtoto wake, ndivyo nitakavyokufariji wewe, nawe utafarijiwa huko Yerusalemu.””

Zaburi 133:2. “Ni kama mafuta ya thamani yaliyomiminwa kichwani,   yakitiririka kwenye ndevu, yakitiririka kwenye ndevu za Aroni, mpaka kwenye upindo wa mavazi yake.”

Wagalatia 4:26-27. “Lakini Yerusalemu wa juu ni huru, nayo ndiye mama yetu. Kwa maana imeandikwa: “Furahi, wewe uliyetasa wewe usiyezaa, paza sauti, imba kwa furaha, wewe usiyepatwa na utungu, kwa maana watoto wa mwanamke aliyeachwa ni wengi kuliko watoto wa yule aliye na mume.’’”

Luka 10:16. ““Yeye awasikilizaye ninyi, anisikiliza Mimi, naye awakataaye ninyi, amenikataa Mimi. Lakini yeye anikataaye Mimi amkataa Yeye aliyenituma.””

woman breatfeeding

child mozambican-women-

nkima o benin

 

nkima wina ng'wana o namibia

 

ENGLISH: I HAVE A RIDDLE – LET IT COME

MY TAMARIND TREE HAS  MANY FRUITS TO THE EXTENT OF MAKING CHILDREN PICK ITS FRUITS WITH EASY-  MOTHER’S BREASTS.

This riddle comes from the fruit-bearing tree with the name tamarind. This tamarind tree is likened to a mother bcause of sharing the attribute of bearing fruits, something sweet for others to consume. In this tree, as its fruits develop, its branches become weak and begin bending down. They can bend down to the extent of making even young children to pick its fruits with easy. This scenario of a tamarind tree is compared to that of a woman who breastfeed her baby. This riddle shows us the mother’s love for her child (Refer to Kugundua Mbegu za Injili, which means ‘Discovering the Seed of the Gospel,’ page 43).

This book was written by the Bujora Cultural Research Committee, edited by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1993.

This riddle teaches us to love and care for our chidren. The mother’s heart is always open to any of her children.

God’s love for us, as indicated in the Bible, is often compared to the love of a parent for a child. God loves us just as a loving mother loves her child (See Isaiah 49: 14-15).

In their language, the Maasai call God by the name of ” Breastfeeding Mother” to compare God with a breastfeeding mother. Again the church is Our Mother. “Unless we acknowledge that the church is our mother, God will not be our Father” (St. Augustine).

If we refuse to praise the church we refuse to praise God the Father (see Luke 10:16). The Church is a mother who loves and protects us her children without exception. The mother’s heart is always open to her children. The Church is our mother; giving birth to the Sacrament of Baptism (The Source of Baptism is the womb of the church), nourishing us in the Eucharist.

The Virgin Mary is also a mother. She is the mother of Jesus and our Mother as we have read in the Gospel of John (see John 19: 26-27). She is the mother of the church, the body of Jesus Christ. Just as a mother feels the pain until the baby is born, so does the Virgin Mary suffered for us children until Christ is completed in us (See ‘Discovering Gospel Seeds,’ page 44).

Isaiah 49: 15-16. Isaiah 66: 12-13. Psalm 133: 2. Galatians 4: 26-27. Luke 10:16.