Akahayile kenako, kalolile bhabhini bha mbina abho bhagitanagwa bhagoyangi. Abhabhini bhenabho, bhagafunyama nzoka ulu bhandya ugubhina mbina jabho. Abhanhu bhenabho, bhaga muchalo jilebhe bhugajifunya nzoka jabho jinijo, aliyo bhali hoyi bhanhu bhadadu duhu ahenaho.
Hunagwene abhanhu aho bhabhona chene bhagayomba giki, “bhagoyangi bhadina mbina ndo.” Ubhunubho huna bhub’iza wandijo bho kahayile kenako, kunguno, abhab’ini abhangi bhagafunyaga nzoka ulu bhanhu bhukwila aha mbina yiniyo.
Akahayile kenako, kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatumilaga nguzu ningi, ku jikolo jidoo, nulu umugutumama nimo ndoo, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, adulile nulu gubhucha ngong’ho gujupigila mhumbi, kunguno adadebhile ugulinganija ijilanga jakwe ni ndimu iyo aligibhulaga. Uweyi agatumamaga imilimo yakwe gitumo alitogelwa, kunguno ya wangu bhokwe bho gupelana, umuwikaji bhokwe.
Umunhu ng’wunuyo agikolaga na bhagoyangi abho bhagafunyaga nzoka ulu bhandya ugubhina nulu bhagab’iza bhalihoyi bhanhu bhatatu du hoyi, kunguno nuweyi agatumilaga nguzu ningi nulu alitumama nimo ndoo duhu. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “bhagoyangi bhadina mbina ndo.”
Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya gubhiza na masala ga gulinganija chiza imiliimo yabho, umukikalile kabho, kugiki bhadizumala nguzu jabho sagala, umuwikaji bhobho.
Mathayo 18:20.
Mathayo 13:31.
KISWAHILI: WAGOYANGI HAWA NA NGOMA NDOGO.
Msemo huo, ulianzia kwa wacheza ngoma wanaoitwa wagoyangi. Wagoyangi hayo ni wana mchezo wa ngoma ya kutumia nyoka. Watu hao, huwatoa hao nyoka wanapoanza tu kucheza. Hivyo, watu hao walifika kwenye kijiji kimoja, ambapo waliwatoa nje hao nyoka nje wakati watu waliokuwepo hapo walikuwa wawili tu.
Ndiyo maana watu walipoona hivyo, walisema, “wagoyangi hawana ngoma ndogo.” Huo ndiyo ukawa mwanzo wa msemo huo, kwa sababu wachezaji wa makundi wengine, husubiri mpaka wawepo watu wengi zaidi, ndipo hufikia hatua ya kuwatoa nje hayo nyoka.
Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hutumia nguvu kubwa kwenye kitu kidogo, katika maisha yake. Mtu huyo, aweza hata kuchukua bunduki kwenda kuulia panzi, kwa sababu yeye hajui kulinganisha silaha zake na kitu anachoenda kukiua, maishani makwe. Yeye hufanya kazi zake kwa kadiri anavyotaka, kwa sababu ya wepesi wake wa kukasilia.
Mtu huyo, hufanana na wagoyangi ambao hutoa nyoka nje kata kama kuna watu watatu tu kwenye ngoma yao, kwa sababu naye hutumia nguvu kubwa kwenye kazi ndogo, pia hukasilishwa hata na jambo dogo zaidi. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “wagoyangi hawana ngoma ndogo.”
Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuwa na akili ya kuwawezesha kutumia nguvu inayolingana na kazi wanazozifanya, katika maisha yao, ili wasizipoteze bure nguvu zao, maishani mwao.
Mathayo 18:20. “Kwa kuwa wanapokusanyika pamoja watu wawili au watatu kwa jina langu, mimi niko papo hapo pamoja nao.””
Mathayo 13:31. “Akawaambia mfano mwingine, akasema, “Ufalme wa Mbinguni ni kama punje ya haradali, ambayo mtu aliichukua akaipanda shambani mwake.””