stories

321. B’UTA B’UDIMANILE NA LUGE

Imbuki ya lusumo lunulo yingilile kub’uta na luge. Ub’uta nu luge jigikalaga kihamo jiidimile chiza. Jigikalaga bho gwiyambilija uguitumama imilimo yajo. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, b’uta b’udimanile na luge.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhitolile. Abhanhu bhenabho bhagikalaga kihamo umuwikaji bhobho, guti numo bhuli ub’uta nu luge. Bhose ungosha nu nkima bhagiyambilijaga uguitumama imilimo yabho. Abhoyi b’alumanile halumo umushigu ja b’ulamu bhobho. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘b’uta b’udimanile na luge.’

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu abho b’itolile higulya ya gwiidima bho gulumana chiza umuwikaji bhob’o, guti b’uta na luge, umo b’udimanilile. Akikalile kenako kagubhinha nguzu ja gwiyambilija umubhutumami bho milimo yabho.

Mwanzo 9:13-16.

Waefeso 5:31.

KISWAHILI: UPINDE HUSHIKAMANA NA UGWE/KAMBA YAKE

Chanzo cha methali hiyo chatokea kwenye upinde na kamba yake. Upinde na ugwe au kamba yake huwa zimeshikamana pamoja vizuri. Husaidiana katika kufanya kazi zote. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘upinde hushikamana na ugwe/kamba yake.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa watu waliooana. Watu hao huishi pamoja maishani mwao, kama ulivyo upinde na ugwe. Wote mume na mke husaidiana katika kufanya kazi zao. Huungana pamoja siku zote za maisha yao. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘upinde hushikamana na ugwe.’

Methali hiyo hufundisha watu wa ndoa juu ya kushikamana vizuri maishani mwao, kama upinde na ugwe, ushikamanavyo. Maisha hayo yatawapatia nguvu za kusaidiana katika utekelezaji wa majukumu yao.

Mwanzo 9:13-16.

Waefeso 5:31.

arrow

 

ENGLISH: THE BOW AND ITS STRING ARE FASTENED TOGETHER

The source of this proverb comes from the bow and its string. The bow and its string tend to fit together nicely and they function together. That is why people say, “a bow and its string are fastened together.”

The proverb is likened to married people. Married people live together just like a bow and its string.The couples live together and they support each other in life.That is why people say, “a bow and its string are fastened together.”

The proverb teaches couples about how to stick together in their lives like a bow and its string. This kind of life will give them the strength to help each other in fulfilling their responsibilities.

Genesis 9: 13-16.

Ephesians 5:31.

320. UDIZUNIDIMILA MUB’ANA B’A MBULI

Imbuki ya lusumo lunulo yingilile kuli ndimi o mbuli. Undimi ng’wunuyo agajikomanyaga imbuli inhale, na bhana bha mbuli heke. Bhuli jene agajidimaga heke ni jingi. Kuyiniyo lulu, imbuli inhale igalemaga ugudimilwa mub’ana bha mbuli, nulu igab’iza ilinamili gudoo na ginehe. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘udizunidimila mub’ana bhana bha mbuli.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo alidalahijiwa na bhiye kunguno ya mili gokwe gudoo, aliyo alimunhu ntale. Umunhu ng’wunuyo agalemaga ugusanjiwa mub’anigini. Hunagwene agayombaga giki, ‘udizunidimila mub’ana b’a mbuli.’

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya kuleka nhungwa ja kub’adalahija abhanhu, kugiki bhadule ugutumama milimo yabho chiza, mu kaya jabho.

Zaburi 31:18.

1 Petro 2:16-17.

KISWAHILI: USINICHUNGIE KWENYE WATOTO WA MBUZI

Chanzo cha methali hiyo chatokea kwa mchungaji wa mbuzi. Mchungaji huyo huwatenga mbuzi wakubwa na watoto wao, upande mwingine. Kila kundi hulichungia sehemu tofauti na lingine. Kwa hiyo basi, mbuzi mkubwa hukataa kuchungiwa kwenye kundi la watoto, hata kama atakuwa na umbo dogo namna gani. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘usinichungie kwenye kundi la watoto wa mbuzi.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu yule anayedharauliwa na wenzake kwa sababu ya umbo lake kuwa dogo, ijapokuwa yeye ni mkubwa kiumri. Mtu huyo hukataa kuchanganywa kwenye kundi la watoto, kwa kusema kwamba, ‘usinichungie kwenye watoto wa mbuzi.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuacha tabia ya kuwadharau watu maishani  mwao, ili waweze kufanya kazi vizuri, katika familia zao.

Zaburi 31:18.

1 Petro 2:16-17.

goats

 

ENGLISH: NEVER PASTURE ME AMONG SMALL GOATS/GOAT’S KIDS

The source of this proverb is a person who pastures goats. The person who tends goats usually separates kids from old goats. Each group is pastured separately. So, an old goat will refuse to be pastured in the same group as kids no matter how small it is in shape.That is why people say, ‘never pasture me among goat’s kids.’

The proverb is analogized to an adult person who is despised by his/her peers because of being small in appearance. The person usually refuses to be treated as a child by saying, “never pasture me among goat’s kids.”

The proverb teaches people to stop the habit of despising other people in their lives.

Psalm 31:18.

1 Peter 2: 16-17

319. LELO YA CHIMA NKUNDI

Imbuki ya lusumo lunulo, yingilile kunkundi uyo gochimagwa ginhu guminyiwa hatale. Unkundi gunuyo gugolechaga b’uminyiwa bho ng’wa munhu uyo ang’wisanije. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘lelo yachima nkundi.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo alioludugu, uyo wenhaga mamihayo matale. Abhaduguye b’agasatagwa noyi, kunguno ya gulombwa gufunya nsango kugiki bhabhone guimala imahayo yiniyo. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘lelo yachima nkundi.’

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya guleka gwita mamihayo gabhub’i kubhichabho, kunguno amamihayo genayo, gagachimaga nkundi, ukumioyo ya bhichabho bhenabho.

Wagalatia 6:10.

KISWAHILI: LEO IMECHOMA KITOVU

Chanzo cha methali hiyo chatokea kwenye kitovu kilichochomwa kitu fulani kikaumia sana. Kitovu hicho, huonesha jeraha la mauvumi ambalo mtu huyo amelipata kutoka kwa yule amtegemeae, au ameumizwa mtu wa karibu naye. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘leo imechoma kitovu.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu ambaye ameleta matatizo kwa ndugu zake. Ndugu zake mtu huyo huumia sana, kwa sababu ya kuwaletea shida ya kutakiwa kuchanga mali zikiwemo pesa, kwa lengo la kuyatatua matatizo hayo. Ndiyo maana watu husema, ‘leo imechoma kitovu.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuacha kuwaletea matatizo ndugu zao, au wenzao, kwa sababu, matatizo hayo huchoma vitovu vya mioyo ya wenzao hao, kwa maana ya kuwaumiza sana.

Wagalatia 6:10.

vintage

 

ENGLISH: THE NAVEL HAS BEEN STABBED TODAY

This proverb comes from a person whose navel has been stubbed badly. The navel represents injury caused by a closely-related person. That is why people say, “the navel has been stubbed today.” The proverb is compared to a person who has caused serious problems to his/her relatives. The relatives of that person suffer because of being asked to pay money or something else in order to resolve the problem their relative caused to them. That is why people say, “the navel has been stubbed today.”

The proverb warns people against causing problems to their brothers or their people because problems cause pain to people.

Galatians 6:10.

318. FUGO NHALE IDAMALAGA NGUKULU

Imbuki ya lusumo lunulo, yilolile nkukulu ijo jisagilile, mu fugo ya guzugila b’ugali. Ifugo yiniyo igab’izaga na masagilwa ga jiliwa ukusi yayo ijo bhagajilekelaga abhali bha jiliwa jinijo. Amalekelwa genayo hayo gagitanagwa ngukulu. Ingululu jinijo jigadamilaga hasi ya fugo yiniyo. Kuyiniyo lulu, umunhu uyo alasange jashilaga ijiliwa, adulile nulu gupala ngukulu ulya. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘fugo nhale idamalaga ngukulu.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo alinsab’i o mitugo, nulu o jose jose. Unsab’i ng’wunuyo nulu jigacha imitugo, jidushila pye, kunguno jigigelaga nulu ngehu ijagupila. Umunhu ng’wunuyo, agab’izaga na ginhu ja gufunya ukub’iye guti jikolo nulu miganiko ayo gadulile gubhambilija abhiye bhenabho. Hunawene abhanhu ulu bhalinomba ginhu bhagayombaga giki, ‘fugo nhale idamalaga ngukulu.’

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya gubhiza b’izanholo ukubhanhu abho bhali na makoye. Uwizanholo b’unubho, bhugubhambilija abhanhu bhenabho ijinakupandika nzila ja guginja amakoye genayo.

Yohane 6:13.

KISWAHILI: CHUNGU KUKUBWA HAKIMALIZI UKOKO

Chanzo cha methali hiyo chaangalia chungu cha kupikia ugali, chenye ukoko. Chungu hicho huwa na mabaki ya chakula ndani yake kwa chini, ambayo hubakishwa na walaji wa chakula hicho. Mabaki hayo hung’ang’ania chini ambayo huitwa ukoko. Ukoko huo huwa mgumu kutolewa ndani ya chungu hicho. Kwa hiyo basi, mtu atakayekuta chakula kimeliwa, huweza kukwangua walau ukoko huo na kula. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘chungu kikubwa hakimalizi ukoko.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu ambaye ni tajiri wa mifugo au wa kitu chochote kile. Mtu huyo huwa na kitu cha kutoa kwa wenzake wanaomuomba kama vile mali, au mawazo yawezayo kuwasaidia wenzake hao. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘chungu kikubwa hakimalizi ukoko.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuwa na ukarimu wa kuwasaidia wenye shida mbalimbali. Ukarimu huo, utawasaidia watu hao katika kupata njia za kuyatatulia matatizo hayo.

Yohane 6:13.

camping-cooker

 

ENGLISH: A BIG POT IS NOT WITHOUT CRUST

The source of this proverb is a big pot. A big pot always has crust at the base left by people who ate the food. The crust sticks below the base of the pot and it is difficult to remove it. Therefore, a person who finds the food has been eaten may scrape the crust and eat. That is why people say, “a big pot is not without crust.”

The proverb is analogized to someone who has many livestocks or anything else. Even if all the livestocks die, such a person will have few left behind. The person usually has something to give to those who approach him/her for help.That is why people say, “a big pot is not without crust.”

This proverb teaches people about being generous to other people with problems. Such generosity will help them to find ways to solve their problems.

John 6:13.

316. SHIMBA NG´OSHA IDAGAIYAGWA B´UYENZE

Imbuki ya lusumo lunulo ilolile shimba iyo iling´osha. Ishimba yiniyo, igikalaga na jimanikijo jayo, ijo jigitanagwa b´uyenze. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ´shimba ng´osha idagaiyagwa b´uyenze.´

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu ngosha, uyo amanyikile chene bho guilang´hana chiza ikaya yakwe. Ubhulang´hani bho kaya yakwe, umunhu ng´wunuyo, wikolile na b´uyenze bho guimanyikija ishimba yiniyo, igiki iling’osha. Umunhu ng´wunuyo agabhalangaga abhanhu bhakwe inzila ja gwikala chiza na bhichabho. Hunagwene abhanhu bhayombaga giki, ´shimba ng´osha idagaiyagwa b´uyenze.´

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya gudilila milimo yabho, bho gwikala chiza na bhichabho. Uwikaji bhunubho, bhubhamanyiche ikigi, abhoyi bhali bhanhu bha nhungwa ja wiza, umukikalile kabho.

Mithali 30:30.

Ufunuo 5:5.

KISWAHILI: SIMBA DUME HAKOSI SHALUBU

Chanzo cha methali hiyo chatokea kwenye simba dume. Simba huyo huwa na alama ya kumtambulisha kuwa yeye ni dume, iitwayo shalubu. Kila simba dume anashalubu. Ndiyo maana watu husema kwamba, ´simba dume hakosi shalubu.´

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu mwanaume ajulikanaye hivyo kwa kuitunza vizuri familia yake. Utunzaji huo wa familia yake, hufanana na shalubu la yule simba, limtambulishalo kuwa yeye ni dume. Mtu huyo huwafundisha  pia watu wake namna ya kuishi vizuri na watu. Ndiyo maana watu husema kwamba, ´simba dume hakosi shalubu.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kujali kazi zao kwa kuishi vizuri na wenzao. Maisha hayo, yatawatambulisha, maishani mwao, kuwa wao ni binadamu wenye tabia njema.

Mithali 30:30.

Ufunuo 5:5.

lion1

lion

 

ENGLISH: A MALE LION IS NOT WITHOUT MANE

The source of this proverb is the lione’s mane. The lion’s mane is one of the features used to identify a male lion. Every male lion has it. That is why people say, “a male lion is not without mane.”

The proverb is likened to a man who is known for taking good care of his family. The care of his family is like the lion’s mane; it identifies him as a real man. Such a person also teaches his people how to live well with other people. That is why people say, “a male lion is not without mane.”

The proverb teaches people about caring for their jobs and living well with their people. Such kind of life will make them to be identified as good people.

Proverbs 30:30.

Revelation 5: 5.