myth

741. BHAGOYANGI BHADINA MBINA NDO.

Akahayile kenako, kalolile bhabhini bha mbina abho bhagitanagwa bhagoyangi. Abhabhini bhenabho, bhagafunyama nzoka ulu bhandya ugubhina mbina jabho. Abhanhu bhenabho, bhaga muchalo jilebhe bhugajifunya nzoka jabho jinijo, aliyo bhali hoyi bhanhu bhadadu duhu ahenaho.

Hunagwene abhanhu aho bhabhona chene bhagayomba giki, “bhagoyangi bhadina mbina ndo.” Ubhunubho huna bhub’iza wandijo bho kahayile kenako, kunguno, abhab’ini abhangi bhagafunyaga nzoka ulu bhanhu bhukwila aha mbina yiniyo.

Akahayile kenako, kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatumilaga nguzu ningi, ku jikolo jidoo, nulu umugutumama nimo ndoo, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, adulile nulu gubhucha ngong’ho gujupigila mhumbi, kunguno adadebhile ugulinganija ijilanga jakwe ni ndimu iyo aligibhulaga. Uweyi agatumamaga imilimo yakwe gitumo alitogelwa, kunguno ya wangu bhokwe bho gupelana, umuwikaji bhokwe.

Umunhu ng’wunuyo agikolaga na bhagoyangi abho bhagafunyaga nzoka ulu bhandya ugubhina nulu bhagab’iza bhalihoyi bhanhu bhatatu du hoyi, kunguno nuweyi agatumilaga nguzu ningi nulu alitumama nimo ndoo duhu. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki,  “bhagoyangi bhadina mbina ndo.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya gubhiza na masala ga gulinganija chiza imiliimo yabho, umukikalile kabho, kugiki bhadizumala nguzu jabho sagala, umuwikaji bhobho.

Mathayo 18:20.

Mathayo 13:31.

KISWAHILI: WAGOYANGI HAWA NA NGOMA NDOGO.

Msemo huo, ulianzia kwa wacheza ngoma wanaoitwa wagoyangi. Wagoyangi hayo ni wana mchezo wa ngoma ya kutumia nyoka. Watu hao, huwatoa hao nyoka wanapoanza tu kucheza. Hivyo, watu hao walifika kwenye kijiji kimoja, ambapo waliwatoa nje hao nyoka nje wakati watu waliokuwepo hapo walikuwa wawili tu.

Ndiyo maana watu walipoona hivyo, walisema, “wagoyangi hawana ngoma ndogo.” Huo ndiyo ukawa mwanzo wa msemo huo, kwa sababu wachezaji wa makundi wengine, husubiri mpaka wawepo watu wengi zaidi, ndipo hufikia hatua ya kuwatoa nje hayo nyoka.

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hutumia nguvu kubwa kwenye kitu kidogo, katika maisha yake. Mtu huyo, aweza hata kuchukua bunduki kwenda kuulia panzi, kwa sababu yeye hajui kulinganisha silaha zake na kitu anachoenda kukiua, maishani makwe.  Yeye hufanya kazi zake kwa kadiri anavyotaka, kwa sababu ya wepesi wake wa kukasilia.

Mtu huyo, hufanana na wagoyangi ambao hutoa nyoka nje kata kama kuna watu watatu tu kwenye ngoma yao, kwa sababu naye hutumia nguvu kubwa kwenye kazi ndogo, pia hukasilishwa hata na jambo dogo zaidi. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “wagoyangi hawana ngoma ndogo.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuwa na akili ya kuwawezesha kutumia nguvu inayolingana na kazi wanazozifanya, katika maisha yao, ili wasizipoteze bure nguvu zao, maishani mwao.

Mathayo 18:20. “Kwa kuwa wanapokusanyika pamoja watu wawili au watatu kwa jina langu, mimi niko papo hapo pamoja nao.””

Mathayo 13:31. “Akawaambia mfano mwingine, akasema, “Ufalme wa Mbinguni ni kama punje ya haradali, ambayo mtu aliichukua akaipanda shambani mwake.””

wagoyangi africa

south-africa2

wagoyangi samburu

740. LYAB´IMBILILE HAB´I.

Ulusumo lunulo, lwingilile kuli munhu uyo agab’imbila lib’ute, kulwande lo mili gokwe ulo adadulile uguloyomba sagala. Ilib’ite linilo, lyalib’imbilile kulwande lo mbisila yakwe. Uweyi agacha soni uguyomba hab’utongi bho bhanhu aho lib’ilimbile. Hunagwene agayomba bho mbisila giki, “lyab’imbilile hab’i.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo opandikile ikoye itale umuwikaji bhokwe, ilo adadulile ugulimala ubho gutumila nguzu yakwe duhu. Umunhu ng’wunuyo, agalombaga wambilijiwa bho gufumila kubhiye na kuli Mulungu uyo adulile gung’wingija wangu ilikoye linilo. Uweyi adebhile igiki uwambilijiwa bhunubho, bhudulile gulimala ilikoye lyakwe linilo.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo oliob’imbila lib’ute litale kulipande lya mili gokwe ilo agabhona soni uguliyomba sagala, kunguyo nuweyi ligankoyaga mpaka olomba wambilijiliwa, bho dugula gulyinja ilikoye lwakwe linilo. Hunagwene nang’hwe agabhawila abhanhu giki, “lyab’imbilile hab’i.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gub’iza na masala ga gwiyumilija umumakoye ayo bhalinago, na gulomba wambilijiwa bho gugamala wangu amakoye genayo, kugiki bhadule gwikala chiza na bho mholele na bhichabho, umuwikaji bhobho.

1Wakorintho 12:20-31.

KISWAHILI: LIMEVIMBIA PABAYA.

Methali hiyo, ilianzia kwa mtu aliyevimba jipu katika sehemu ya mwili wake ambayo hawezi kuitaja hovyo, kwa sababu ya kuona aibu. Jipu hilo, lilivimbia kwenye sehemu zake za siri. Yeye hujikia aibu kuitaja mbele za watu sehemu hiyo. Ndiyo maana yeye huitaja kwa mafumbo akisema, “limevimbia pabaya.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule aliyepata tatizo kubwa maishani mwake, ambalo hawezi kulitatua kwa kutumia uwezo wake tu. Mtu huyo huomba msaada kutoka kwa wezake na kwa Mungu awezaye kumtatulia tatizo hilo. Yeye anaelewa kwamba, msaada huo unaweza kulitatua kwa haraka tatizo lake hilo.

Mtu huyo hufanana na yule aliyevimba jipu kwenye sehemu zake za siri akashindwa kuitaja mbele za watu sehemu hiyo kutokana na kuona aibu, kwa sababu naye alishindwa kulitatua tatizo lake hilo mpaka akaomba msaada kutoka kwa wenzake na kwa Mungu mwenye uwezo wa kulitatua tatizo hilo kwa haraka. Ndiyo maana naye alisema kwamba, “limevimbia pabaya.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na akili ya kuvumilia matatizo na kuomba msaada wa kuweza kuyatatua, ili waweze kuishi vizuri na kwa amani na wenzao, maishani mwao.

1Wakorintho 12:20-31. “Kama ulivyo, kuna viungo vingi, lakini mwili ni mmoja. Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sina haja nawe!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sina haja na ninyi!” Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana. Navyo vile viungo vya mwili tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee. Wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa, ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane usawa kila kimoja na mwenzake. Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho, kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho. Sasa ninyi ni mwili wa Kristo na kila mmoja wenu ni kiungo. Mungu ameweka katika kanisa, kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za masaidiano, karama za maongozi, aina mbalimbali za lugha. Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanafanya miujiza? Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri? Basi tamanini sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.”

malawi1

malawi3

malawi4

ENGLISH: I HAVE AN ABCESS SWOLLEN AT A BAD PLACE.

This proverb began with a man who had a boil on a part of his body that he could not mention because he felt embarrassed to do so. For sure, this abscess was on his genitals. So he felt ashamed to mention it in public. That is why he spoke using a proverb saying that “I have an abscess swollen on a bad place.”

This proverb is likened with a man who has a serious problem in his life which he cannot solve by simply relying only on his own strengths. Such a person will have to ask for help from his peers and from God who can solve the problem. He understands that such support can quickly solve his problem.

This man is like the one who had a swollen boil on his genitals but failed to show it in public because he was ashamed. This person failed to solve his problem until he asked for help from his colleagues and from God who was able to solve it very quickly.

This proverb teaches people how to have stability to endure problems and ask for help to solve them, so that they can live peacefully with others.

1 Corinthians 12: 20-31.

739. IYIB´IMBILE NOMO IDULEMEJA B´IYE GUDIMA.

Ulusumo lunulo, lulolile ng’ombe iyo ibhimbilile nomo. Ing’ombe yiniyo, igadumaga ugulya amaswa kunguno ya bhubhimbi bho nomo goyo gunuyo. Olihoyi ndimi ong’ombe uyo agajilugalila pye mulugutu kunguno ya ing’ombe imo iyo yali ya bhimba nomo.

Ung’wiye ugamuuja, “nibhuli ojilugalilaga mulugutu ing’ombe aliyo ilimi lyakulaga?” Uweyi agashosha, “ilihoyi ng’ombe imo iyo yabhimbaga nomo idudula ugulya amaswa.” Ung’wiye unshokeja, “iyib’imbile nomo idulemeja b’iye gudima.” Ubhunubho nab’ib’iza wandijo bho gutumama go lusumo lunulo.

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagadumaga nulu gulya jiliwa, hamo nulu gutumama milimo yabho, kunguno ya ng’wichabho umo uyo agusataga. Abhanhu bhenabho, bhagasunduhalaga noyi mpaga bhaduma ugupandika ijiliwa ijo jigabhinaga nguzu ja gutumamila milimo yabho chiza.

Abhanhu bhenabho bhagikolaga nu munhu uyo agaleka ugujichala ing’ombe jakwe ukwidima kunguno ya ng’ombe yakwe imo iyo yaliyabhimba nomo, iki nabho bhagadumaga ugulya nulu gutumama milimo kunguno ya gusatilwa na munhu obho umo. Hunagwene abhanhu bhagabhawilaga giki, “iyib’imbile nomo idulemeja b’iye gudima.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kubhiza na wiyumilija bho gutumama milimo yabho, ulu bhalina makoye abhichacho, kugiki bhadule kupandika matwajo mingi ga gubhambilija ijinagubhulang’hana chiza ubhupanda bhobho.

Hangi lobhalanga abhanhu abho bhali na makoye kuleka ugubhamaja lubhango abhichabho, umubhasatu bhobho. Giko lulu, amakoye gabho, gadizubhiima lubhango abhichabho, umuwikaji bhobho.

Luka 15:25-31.

Zaburi 73:1-12.

Waefeso 2:4-10.

KISWAHILI: ALIYEVIMBA MDOMO HAWAZUII WANZAKE KULA MAJANI.

Methali hiyo huangalia ng’ombe aliyevimba mdomo. Ng’ombe huyo, hushindwa hata kula majani kwa sababu ya kuvimba mdomo wake. Alikuwepo mtu mmoja aliyekuwa mchungaji wa ng’ombe.

Mtu huyo aliwafungia zizini ng’ombe wote kwa sababu ya ng’ombe wake mmoja kuwa na tatizo la kuvimba mdomo wake. Mwenzake akamuuliza, “kwa nini hujawafungulia ng’ombe kwenda kuchunga hadi sasa?”

Yeye alijibu, “kuna ng’ombe mmoja amevimba mdomo, hivyo hawezi kula majani.” Mwenzake huyo akamjibu, “aliyevimba mdomo hawazuii wenzake kula majani.” Huo ndio ukawa mwanzo wa kutumika kwa methali hiyo.

Methali hiyo, hulinganishwa kwa watu wale ambao hushindwa hata kula au kufanya kazi zao, eti kwa sababu ya mtu mmoja kuugua, au kupata tatizo fulani. Watu hao, huhudhunika sana mpaka hufikia hatua ya kushindwa kujipatia mahitaji yao ya kila siku yakiwemo yale ya chakula, kwa sababu ya kuugua kwa mtu mwenzao. Wao hushindwa hata kufanya kazi za kuwapatia chakula, kwa sababu ya tatizo la mtu mmoja.

Watu hao, hufanana na mtu yule ambaye aliacha kuwafungulia ng’ombe wake kwenda malishoni kuchunga, eti kwa sababu ya ng’ombe mmoja kuvimba mdomo wake, kwa sababu na wao, hushindwa kuyatekeleza vizuri majukumu yao, kutokana na mmoja wao kupata tatizo fulani. Ndiyo maana watu huwaambia kwamba, “aliyevimba mdomo hawazuii wenzake kula majani.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na uvumilivu wa kuwawezesha kutimiza majukumu yao ya kuulinda na kuuendeleza uhai wao, hata kama kuna mmoja wao ambaye ana tatizo, ili waweze kujipatia mahitaji yao ya kila siku, maishani mwao.

Methali hiyo, pia huwafundisha watu wenye matatizo kutowafanya wenzao walio wazima, wakose raha au wahudhunike kipita kiasi kwa sababu ya kujidekeza kwao. Hivyo, matatizo yao yasiwazuie wengine kufurahi, maishani mwao.

Luka 15:25-31. “Wakati huo, yule mwana mkubwa alikuwa shambani. Alipokaribia nyumbani, akasikia sauti ya nyimbo na watu wakicheza. Akamwita mmoja wa watumishi na kumwuliza, ‘Kuna nini?’ Akamwambia, ‘Mdogo wako amekuja, naye baba yako amemchinja ndama aliyenona kwa sababu mwanawe amerudi nyumbani akiwasalama na mzima.’ Yule mwana mkubwa akakasirika, akakataa kuingia ndani. Basi baba yake akatoka nje na kumbembeleza. Lakini yeye akamjibu baba yake, ‘Tazama! Miaka yote hii nimekutumikia na hata siku moja sijaacha kutii amri zako, lakini hujanipa hata mwana mbuzi ili nifurahi na rafiki zangu. Lakini huyu mwanao ambaye ametapanya mali yako kwa makahaba aliporudi nyumbani, wewe umemchinjia ndama aliyenona!’

“Baba yake akamjibu, “ ‘Mwanangu, umekuwa nami sikuzote na vyote nilivyo navyo ni vyako. Lakini ilitubidi tufurahi na kushangilia kwa sababu huyu mdogo wako alikuwa amekufa na sasa yu hai, alikuwa amepotea naye amepatikana.’ ”

Zaburi 73:1-12. “Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi. Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza, nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama. Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu. Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu. Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo na wanadamu. Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri. Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, ubaya wa majivuno kutoka mioyoni mwao hauna kikomo. Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa. Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani. Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele. Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?’’ Hivi ndivyo walivyo waovu, sikuzote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.”

Waefeso 2:4-10. “Lakini Mungu, kwa upendo Wake mwingi kwetu sisi, ambaye ni mwingi wa rehema, hata tulipokuwa wafu kwa ajili ya makosa yetu, alitufanya tuwe hai pamoja na Kristo Yesu, yaani, mmeokolewa kwa neema. Mungu alitufufua pamoja na Kristo na kutuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho katika Kristo Yesu, ili katika ule ulimwengu ujao apate kuonyesha wingi wa neema Yake isiyopimika, iliyodhihirishwa kwetu kwa wema Wake ndani ya Kristo Yesu. Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani, wala hii si kwa matendo yenu mema. Hii ni zawadi kutoka kwa Mungu, si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu. Kwa maana sisi ni kazi ya mikono ya Mungu, tulioumbwa katika Kristo Yesu, ili tupate kutenda matendo mema, ambayo Mungu alitangulia kuyaandaa tupate kuishi katika hayo.”

cow-1

cow2

cows-

ENGLISH: A COW WITH A SWOLLEN MOUTH CANNOT PREVENT OTHERS FROM EATING GRASS.

This proverb focuses on a cow with a swollen mouth. Such a cow is unable to eat grass because of the swelling on its mouth. There was a man who was a herdsman.

The man locked all the cows in the cow shed because one of his cows had a swollen mouth therefore it was unable to eat grass. Seeing that he had locked all of his cattle in the shed, his companion asked him, “Why haven’t you allowed the cattle to go to graze up to this moment?”

He replied, “One cow has a swollen mouth, so she can’t eat grass.” His companion replied, “”a swollen mouth of one cow cannot prevent others from eating grass.” That was the beginning of the proverb.

The proverb is likened with a person who loses his ability to eat or work, perhaps because of a physical ailment or a malady. When it happens that their fellow is sick these, people are so depressed that they fail to provide for their daily needs, including food, because of the illness of a fellow human being.

These people are like the man who stopped taking his cattle to the grazing place because one of the cows had a swollen mouth which was preventing her from eating. That is why people tell the people with such a character, “a cow with a swollen mouth cannot prevent others from eating grass.”

This proverb teaches people about patience that will enable them to fulfill their responsibilities enough to protect and sustain their lives, even if one of them has a problem.

This proverb also teaches people who have problems not to make their peers miserable, uncomfortable or overwhelmed with their self-esteem. Thus, their problems should not prevent others from enjoying life.

Luke 15: 25-31.

Psalm 73: 1-12.

Ephesians 2: 4-10.

738. SHAKUBHIMBYA NTWE ULASHIBHONA.

Ulusumo lunulo, lulolile ginhu ja gubhimbya ntwe go ng’wa munhu nhebhe ijo alijibhona aha shigu jahabhutongi. Olihoyi munhu umo uyo agantuma ng’wiye guja gujugusa jiseme aliyomba, “jaga ugaguse ijisema ja gulila jiliwa.” Uweyi agalema aliyomba, “unene nadujaga ugujugusa ijiseme jinijo.” Ung’wiye agashosha, “shagubhimbya ntwe ulashibhona.”

Ulusumo lunulo, lugaganijiyagwa kuli munhu nambu uyo agapandikaga makoye, umuwikaji bhokwe. Umunhu ng’wunuyo, alina nhinda ja gulema gwigwa iya guwilwa na bhiye, kunguno ya gubhadalaha abho agikalaga nabho. Uweyi agisangaga opandikaga makoye, kunguno ya bhulambu bhokwe bhunubho, umukikalile kakwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo agalema gutumama nimo go gugusa jiseme aho atung’wa nung’wiye, kunguno nuweyi alinambu uyo agapandikaga makoye ga gwenhwa na bhulambu bhokwe bhunubho, umuwikaji bhokwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “shagubhimbya ntwe ulashibhona.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kuleka bhulanbu, bho gulema gutung’wa na bhichabho, umukikalile kabho, kugiki bhadule gwigulambija gutumama milimo ya gubhapandikila matwajo mingi, umuwikaji bhobho.

Yeremia 49:16.

Mathayo 23:33.

Ezekieli 7:24.

Yeremia 50:32.

KISWAHILI: UTAKIONA KILICHOKUVIMBISHA KICHWA.

Methali hiyo, huangalia kitu cha kuvimbisha kichwa cha mtu fulani ambacho yeye akiona kwenye siku za mbeleni. Alikuwepo mtu mmoja ambaye alimtuma mwenzake kwenda kuosha vyombo vya kulia chakula, akisema, “nenda ukaoshe vyombi vya kulia chakula.” Yeye alikataa akisema, “mimi siendi kuosha vyombo hivyo.” Mwenzake alimjibu, “utakiona kilichokuvimbisha kichwa.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu mwenye kiburi ambaye hupata matatizo, maishani mwake. Mtu huyo, huwa hasikii ya kuambiwa na wenzake, kwa sababu ya kuwadharau wenzake hao anaoishi nao. Yeye hujikuta amepata matatizo makubwa kwa sababu ya kiburi chake hicho.

Mtu huyo, hufanana na yule aliye kataa kuosha vyombo vya kulia chakula baada ya kutumwa na mwenzake, kwa sababu naye ana kiburi ambacho kumsababishia hupata matatizo. maishani mwake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “utakiona kilichokuvimbisha kichwa.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuacha kiburi, cha kukataa kutung’wa na wenzao, ili waweze kujibidisha kuyatekeleza vizuri majukumu yale yawapatiayo mafanikiyo mengi, maishani mwao.

Yeremia 49:16. “Vitisho vyako na kiburi cha moyo wako vimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba, wewe unayemiliki katika miinuko ya kilima. Ujapojenga kiota chako juu sana kama cha tai, kutoka huko nitakushusha chini,’’ asema BWANA.”

Mathayo 23:33. “Ninyi nyoka, ninyi uzao wa nyoka wenye sumu! Mtaiepukaje hukumu ya jehanam?”

Ezekieli 7:24. “Nitaleta taifa ovu kuliko yote ili kumiliki nyumba zao, nitakomesha kiburi cha wenye nguvu na mahali pao patakatifu patatiwa unajisi.”

Yeremia 50:32. “Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka wala hakuna ye yote atakayemuinua, nitawasha moto katika miji yake, utakaowateketeza wote wanaomzunguka.””

botswana1

women dance botswana

man dance botswana

ENGLISH: YOU WILL SEE WHAT INFLATES YOUR HEAD.

The above proverb looks at something that makes a person’s head swollen with pride. There was a man who was asked by his friend to wash the dishes, saying, “Go and wash the dishes.” However that person refused, saying, “I’m not going to wash the dishes.” His friend replied, “You will see what makes your head inflated.”

That proverb is likened with a haughty man who gets into trouble in his life. Such person does not listen to what his or her peers say, because he or she despises them. However, he finds himself into a lot of trouble because of his arrogance.

This person is like the one who refused to wash the dishes after being asked to by a colleague because he is full of pride that makes him get in trouble in his life. That is why, to such a person people say to, “You will see what makes your head inflated.”

This proverb teaches people to stop being arrogant, to refuse to be sent or instructed by others to do things so that they can strive to fulfill responsibilities that give them success in their lives.

Jeremiah 49:16.

Matthew 23:33.Ezekiel 7:24.

Jeremiah 50:32.

737. BHIMBA NTWE MASANGU GOKALE.

Ulusumo lunulo, lulolile bhubhimbi bho ntwe go ng’wa munhu nhebhe na masangu ayo gagokalaga umu ntwe gokwe gunuyo. Olihoyi munhu uyo agantuma ng’wiye gujutumama nimo nhebhe, aliyomba, “jaga ugatumame nimo ubhujiku welaga.” Uweyi agalema aliyomba, “unene nalemaga nadujaga ugujutumama unimo gunuyo.” Ung’wiye agashosha, “bhimba ntwe masangu gokale.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu nambu uyo agapandikaga makoye, umuwikaji bhokwe. Umunhu ng’wunuyo, adigwaga ya guwilwa na bhiye, kunguno ya gubhadalaha abho agikalaga nabho. Uweyi agisangaga opandikaga makoye, kunguno ya bhulambu bhokwe bhunubho, umukikalile kakwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nu bhubhinbi bho ntwe uyo gugokalaga masangu. Amasangu genayo agikolanijiyagwa na makoye ayo gagenhelejiyagwa na bhulambu bhokwe, kunguno nuweyi agapandikaga makoye ga gwenhwa na bhulambu bhunubho, umuwikaji bhokwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “bhimba ntwe masangu gokale.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kuleka bhulanbu, bho gulema gutung’wa na bhichabho umukikalile kabho, kugiki bhadule gwigulambija gutumama milimo ya gubhapandikila matwajo mingi, umuwikaji bhobho.

Yeremia 49:16.

Mathayo 23:33.

Ezekieli 7:24.

Yeremia 50:32.

KISWAHILI: VIMBA KICHWA MAKANDE YAJAE.

Methali hiyo, huangalia uvimbaji wa kichwa cha mtu fulani na makande ambayo hujaa kwenye kichwa chake hicho. Alikuwepo mtu mmoja ambaye alimtuma mwenzake kwenda kufanya kazi fulani, akisema, “nenda ukafanye kazi kumekucha.” Yeye alikataa akisema, “mimi nimekataa siendi kufanya kazi hiyo.” Mwenzake akajibu, “vimba kichwa makande yajae.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu mwenye kiburi ambaye hupata matatizo maishani mwake. Mtu huyo, huwa hasikii ya kuambiwa na wenzake, kwa sababu ya kuwadharau wenzake hao anaoishi nao. Yeye hujikuta amepata matatizo makubwa kwa sababu ya kiburi chake hicho.

Mtu huyo, hulinganishwa na uvimbaji wa kichwa ambacho hujaa makande. Makande hayo hufananishwa na matatizo yaletwayo na kiburi chake hicho, kwa sababu naye hupata matatizo yasababishwayo na kiburi chake hicho. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “vimba kichwa makande yajae.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuacha kiburi, cha kukataa kutung’wa na wenzao, ili waweze kujibidisha kuyatekeleza vizuri majukumu yale yawapatiayo mafanikiyo mengi, maishani mwao.

Yeremia 49:16. “Vitisho vyako na kiburi cha moyo wako vimekudanganya, wewe unayeishi katika majabali ya miamba, wewe unayemiliki katika miinuko ya kilima. Ujapojenga kiota chako juu sana kama cha tai, kutoka huko nitakushusha chini,’’ asema BWANA.”

Mathayo 23:33. “Ninyi nyoka, ninyi uzao wa nyoka wenye sumu! Mtaiepukaje hukumu ya jehanam?”

Ezekieli 7:24. “Nitaleta taifa ovu kuliko yote ili kumiliki nyumba zao, nitakomesha kiburi cha wenye nguvu na mahali pao patakatifu patatiwa unajisi.”

Yeremia 50:32. “Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka wala hakuna ye yote atakayemuinua, nitawasha moto katika miji yake, utakaowateketeza wote wanaomzunguka.””

head

ENGLISH: A SWOLLEN HEAD THAT IS LIKE FULL ‘MAKANDE’ IN A POT.

This saying focuses on the proud person whose head is swollen with arrogance that he looks like a kind of food (makande) which keeps on swelling every time when water is added to it.

There was a man who was asked by his friend to do some work, who told him “Go and work because it is already dawn.” He refused, saying, “I’m not going to do that job.” His colleague replied, “You have a swollen head like ‘makande’ (food) full in the pot.”

This saying is likened with a haughty man who gets into trouble in his life. That person does not listen to what his or her peers say, because he or she despises those with whom he or she lives. He finds himself in a lot of troubles because of his arrogance.

The person, however, is likened to a swelling of the head that is filled with bruises. These are likened with the problems caused by his pride which makes him suffer. To such a person people would say, “you have a swollen head like makande’ (food) full in the pot.”

This saying teaches people to stop being arrogant, to refuse to be influenced by their peers, so that they can strive to fulfill the responsibilities that give them the most success in their lives.

Jeremiah 49:16. Matthew 23:33. Ezekiel 7:24. Jeremiah 50:32.