myth

689. NG’HWI NINGI JIGANGALUCHAGA.

Ulusumo lunulo, lufumilile kulilomelele lya bhazugi bhahanimo nhebhe. Uumo obho agabhawila abhiye, ‘dujagi dugasene ng’hwi kunguno unimo gunuyu gulintale noyi.’ Umo obhiye ashosha, ‘jilihoyi ijo denhile iyigolo.’ Uweyi agayomba, ‘ijinijo jigushila hayo ijiliwa jidinapya. Igelelilwe dujijile ng’hwi ningi ijo jidulile gubhachiwa mpaga jujibisha ijiliwa ja ha nimo gunuyo.’

Bhagizunilija bhugenha ng’wi ningi ijo bhagajizugula mpaga bhujibisha ijiliwa ija ha nimo gobho gunuyo. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘ng’hwi ningi jigangaluchaga.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhali ni nikoye ilo bhalihaya bhalyinje umuwikaji bhobho. Abhanhu bhenabho, bhagatumilaga nzila ningi ijo jigikolanijiyagwa na ng’hwi ningi, ijagudula gujibisha ijiliwa jabho. Ugwangalucha go bhujiku ing’hwi jigubhakaga, yilingisilile gutumila nguzu na nzila ningi, ijagudula gulimala ilikoye linilo.

Abhanhu bhenabho, bhagatumilaga nzila ningi ijagudula dulyinja ilikoye ilya bhusatu bho corona. Bhagabhalanjaga abhichabho ahigulya ya gulunganija kihamo inguzu nu bhumani bhobho, ijina gujidilila inzila ijo abhatalaamu bha afya bhalibhalanga. Abhoyi bhagalunganaga halumo ijina gunomba Mulungu abhambilije ugulimala wangu ilikoye linilo. Hunagwene abhanhu bhenabho, bhagayombaga giki, ‘ng’hwi ningi jigangaluchaga.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gulungana halumo ijinagujidimila inzila ijo abhadaktari bhalibhalanga, ni jingi ijo jidulile gubhingija ilikoye guti linilo, ilya bhusatu bho corona, kugiki bhadule gumala wangu, na gwikala bho mholele, umuwikaji bhobho.

KISWAHILI: KUNI NYINGI HUKESHA.

Methali hiyo, ilitokea kwenye maongezi ya wapishi wa kwenye sherehe fulani. Mmoja wao, aliwaambia wenzake, ‘twendeni tukakate kuni kwa sababu sherehe hii, ni kubwa sana.’ Mmoja wale wenazake alijibu, ‘zipo zile tulizoleta jana.’ Yeye alisema, ‘hizo zitakwisha bila kukiivisha chakula hicho. Inafaa tuendee kuni nyingi za kutosha kuwashwa mpaga kukiivisha chakula cha kwenye sherehe hiyo.’

Walikubaliana wakaenda kuleka kuni nyingi walizozipikia mpaga wakakiivisha chakula cha kwenye sherehe hiyo. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘kuni nyingi hukesha.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa watu walio na tatizo wanalotaka kulitatua katika maisha yao. Watu hao, hutumia njia nyingi ambazo hufananishwa na kuni ziwezazo kuivisha chakula chao. Kukesha usiku mzima zikiwaka kuni hizo, humaanisha kutumia nguvu na njiza nyingi kutosha kulimaliza tatizo hizo.

Watu hao, hutumia njia nyingi za kuwawezesha kujikinga na tatizo kama hilo la ugonjwa wa corona. Wao huwafundisha wenzao namna za kuungana pamoja katika kuyafuata maelekezo yanayotolewa na watalaamu wa afya. Watu hao, huunganisha nguvu zao huku wakimuomba Mungu awasaidie katika kulimaliza haraka tatizo hilo. Ndiyo maana wao huwaambia watu kwamba, ‘kuni nyingi hukesha.’

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuunganisha nguvu na ufahamu wao, katika kuyafuata maelekezo ya madaktari, na mengine mengi ambayo yanaweza kuwaondolea tatizo hilo, la ugonjwa wa corona, ili waweze kuishi kwa furaha na amani, maishani mwao.

firewood3

firewood

ENGLISH: MANY PIECES OF FIREWOOD LIGHT THE WHOLE NIGHT.

The above proverb started from a conversation of cooks at a ceremony. One of them, says to her companions, ‘let us go to cut firewood because this celebration is so big.’ One of the others replies, ‘there are some that we brought yesterday.’ The other says, ‘those ones will get finished before the food is ready, we have to increase enough firewoods to cook nice meal for this ceremony.’

They agreed and went to pick up as many  fire woods as they can, which they used for cooking nice food for the ceremony. That is why people say that, ‘many fire-woods keep up burning for the whole night.’

This proverb is compared to people who have a problem that they want to solve in their lives. These people use a variety of ways in solving it, which are compared to many fire woods that spend the whole night burning. Keeping up all night burning the wood, means spending enough energy and knowledge in getting rid of their problems.

These people,  help others in using many ways for protecting themselves from various problems including the corona epidemic. They teach their fellows on how to get together  their strenghs enough to follow the instructions which have been provided to them by health professionals.

These people unite their efforts in using their talents as well as asking God for help in resolving  quickly the pandemic. That is why they tell people that, ‘many fire-woods keep up burning for the whole night.’

The proverb imparts in people an idea about putting together their efforts and understandings, for following doctors’ instructions, and many other ways that can remove the problem of corona virus, so that they can live happily and peacefully, in their lives.

688. MASHIGA NILI, NULU, MAHIGA NILI.

Ulusumo lunulo, lwandija kumahoya ga bhanhu bhabhili ayo gahoyela mashiga. Uumo agamuuja ung’wiye, ‘amashiga ni kiyi?” Ung’wiye aganshokeja aliyomba, ‘amashiga gali mawe, nulu, madafari adatu ayo gagatumilagwa gujidimila ijisema ija guzugila ahaliko. Ahasi yago, gugabhachiyagwa moto umung’hwi ijo jigasolelagwa moyi. Umoto gunuyo gugagasebhyaga amashiga genayo.

Aliyo lulu, amashiga genayo gagabhizaga manilizu, ulugudubhachiyagwa umoto. Hunagwene abhanhu, ulu bhubhona kaya iduzugaga jiliwa, bhagayombaga giki, ‘mashiga nili, nulu, mahida nili.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa ku kaya iyo idabokelaga chiza abhageni na kubhalisha jiliwa, kunguno abhahenaho, bhadina bhutogwa, nulu, ikaya yiniyo idina jiliwa.

Amashiga ayo gali mawe adatu gagatumamilagwa gudima nungu, nulu fulila, aha liko, gagikalaga manilizu kunguno bhadazugaga ijiliwa ahakaya yiniyo. Hunagwene abhanhu, bhagayiwilaga ikaya yiniyo giki, mashiga nili, nulu, mahiga nili. Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa bho 58.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na wizang’holo bho gubhakaribhusha abhageni aha kaya jabho, kugiki bhadule gujipandika imbango ijo jigigelaga kunguno ya gubhagola chiza abhanhu bhenabho, umuwikaji bhobho.

“Ugubhakaribhusha abhageni bho wizang’holo umu kaya jise, guli nimo gwize ayise abho duganhondejaga Yesu Kristo. Ishibhi idigwita yabhubhi duhu, aliyo hangi nu kuleka gubhitila yawiza abhigisu, guleka uguitumama imilimo yise, na guleka gubhadilila abho bhali na makoye gabho. Ukuhani nu Nawi bhadang’witilile yabhubhi uyo oliotulwa na manyami, aliyo bhagamitilia bho nhudu ugundilila. Bhaditile lyose lyose. Lolaga Kueneza Injili Kwa Methali, bhukurasa, 58.

Mambo ya Walawi 19:34.

Luka 10:31-33.

Waroma 15:7.

Waebrania 13:2.

Mwanzo 18:1-8.

1Wafalme 17:10-16.

Mathayo 25:31-46.

KISWAHILI: MAFIGA BARIDI.

Methali hiyo ilianzia kwenye maongezi ya watu wawili juu ya kazi ya mafika. Mmoja alimuuliza mwenzake, ‘mafiga ni nini?’ Mwenzake alimjibu akisema, ‘mafiga ni mawawe, au matofari matatu yanayotumika katika kushikilia chombo cha kupikia. Chini ya mafiga hayo huwekwa kuni ambazo huwashwa moto unaoleta joto kwenye mafiga hayo. Mafiga hayo huwa baridi kama watu hawapiki chakula.’ Ndiyo maana watu kama wakiona chakula hakipikwi kwenye familia fulani, husema, ‘mafiga baridi.’

Methali hiyo hulinganishwa kwenye familia au kaya ile ambayo haipokei vizuri wageni na kuwalisha chakula, kwa kuwa hawana mapendo au kaya hiyo haina chakula.

Mafiga ambayo ni mawe matatu yatumikayo kutelekea chungu au sufuria jikoni, hukaa baridi kwa sababu hawapiki chakula. Ndiyo maana watu huiambia familia hiyo kwamba, ‘mafiga baridi.’ Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 58.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuwa na ukarimu wa kuwakaribisha wageni katika familia zao, ili waweze kupata Baraka zitokanazo na kuwatunza watu hao, katika maisha yao.

 “Kuwakaribisha wageni kwa ukarimu kwenye kaya zetu ni wajibu wetu sisi tunaomfuata Yesu Kristo. Dhambi sio kutenda mabaya tu, bali pia ni kutowatendea mema wenzetu, kutotimiza wajibu wetu, na kutohusika na shida zao. Kuhani na Mlawi hawakumtendea vibaya yule aliyepigwa na majambazi, bali walipita bila kujali. Hawakutenda lo lote.” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 58.

Mambo ya Walawi 19:34. “Mgeni anayeishi pamoja nawe ni lazima umtendee kama mmoja wa wazawa wa nchi yako. Mpende kama unavyojipenda mwenyewe, kwa maana ulikuwa mgeni katika nchi ya Misri. Mimi ndimi BWANA Mungu wako.”

Luka 10:31-33. “Kwa bahati nzuri kuhani mmoja alikuwa anapitia njia ile, alipomwona huyo mtu, akapita upande mwingine wa barabara, akamwacha hapo hapo. Vivyo hivyo Mlawi mmoja naye alipofika mahali pale, alimwona, akapita upande mwingine wa barabara, akamwcha hapo hapo. ‘‘Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa akisafiri kupitia njia hiyo alipomwona, alimhurumia,”

Waroma 15:7. “Karibishaneni ninyi kwa ninyi kama Kristo alivyowakaribisha ninyi ili kumletea Mungu utukufu.”

Waebrania 13:2. “Msisahau kuwakaribisha wageni, kwa kuwa kwa kufanya hivyo, watu wengine waliwakaribisha malaika pasipo kujua.”

Mwanzo 18:1-8. “BWANA akamtokea Abrahamu karibu na mialoni ya Mamre wakati alipokuwa ameketi kwenye ingilio la hema lake wakati wa adhuhuri. Abrahamu akainua macho akaona watu watatu wamesimama karibu naye. Alipowaona, aliharakisha kutoka kwenye ingilio la hema lake kuwalaki na kuwasujudia hadi nchi.  Akasema, “Kama nimepata kibali machoni penu, ee bwana wangu, usimpite mtumishi wako. Acha yaletwe maji kidogo, kisha ninyi  nyote mnawe miguu yenu na mpumzike chini ya mti huu. Niruhusuni niwapatie chakula kidogo mle, ili mpate nguvu mwendelee na safari yenu, kwa kuwa mmekuja kwa mtumishi wenu.’’ Nao wakamjibu, “Vema sana, fanya kama unavyosema.’’

 Hivyo Abrahamu akaharakisha akaingia hemani kwa Sara. Akasema, “Chukua vipimo vitatu vya unga laini haraka, ukande na uoke mikate.”   Kisha akakimbia kwenda kwenye kundi  akachagua ndama mzuri, laini na akampa mtumishi, ambaye aliharakisha kumtayarisha. Kisha akaleta jibini, maziwa na nyama ya yule ndama iliyoandaliwa, akaviweka mbele ya wageni. Walipokuwa wakila, alisimama karibu nao chini ya mti.”

1Wafalme 17:10-16. “Hivyo akaenda Sarepta. Alipofika kwenye lango la mji, mjane alikuwa huko akiokota kuni. Akamwita na kumwomba, “Naomba uniletee maji kidogo kwenye gudulia ili niweze kunywa.’’ Alipokuwa anakwenda kumletea, akamwita akasema, “Tafadhali niletee pia kipande cha mkate.” Akamjibu, ‘Hakika kama BWANA wako aishivyo, sina mkate wo wote, isipokuwa konzi ya unga kwenye gudulia na mafuta kidogo kwenye chupa. Ninakusanya kuni chache nipeleke nyumbani na nikapike chakula kwa ajili yangu na mwanangu, ili kwamba tule kiishe tukafe.’’ Eliya akamwambia, “Usiogope. Nenda nyumbani ukafanye kama ulivyosema. Lakini kwanza unifanyizie mimi mkate mdogo kutoka vile ulivyonavyo kisha uniletee na ndipo utayarishe cho chote kwa ajili yako na mwanao. Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo BWANA, Mungu wa Israeli: “Lile gudulia la unga halitakwisha wala ile chupa ya mafuta haitakauka hadi siku ile BWANA atakapoleta mvua juu ya nchi.’’ Akaondoka na kufanya kama Eliya alivyomwambia. Kwa hiyo kukawa na chakula kila siku kwa ajili ya Eliya, yule mwanamke na jamaa yake. Kwa kuwa lile gudulia la unga halikwisha na ile chupa ya mafuta haikukauka, sawasawa na lile neno la BWANA alilosema Eliya.  ”

Mathayo 25:31-46. Hukumu ya mwisho. “Mwana wa Adamu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote watakatifu pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti cha enzi cha utukufu wake. Mataifa yote watakusanyika mbele zake, naye atawatenga kama mchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi. Atawaweka kondoo upande wake wa kuume na mbuzi upande wake wa kushoto.

“Ndipo Mfalme atawaambia wale walioko upande wake wa kuume, ‘Njoni, ninyi mliobarikiwa na Baba yangu, urithini Ufalme ulioandaliwa kwa ajili yenu tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Kwa maana nilikuwa na njaa mkanipa chakula, nilikuwa na kiu mkaninywesha, nilikuwa mgeni mkanikaribisha, nilikuwa uchi mkanivika, nilikuwa mgonjwa mkanitunza, nami nilikuwa kifungoni mkaja kunitembelea.’

“Ndipo wale wenye haki watakapomjibu wakisema, ‘Bwana, ni lini tulikuona una njaa tukakulisha au ukiwa na kiu tukakunywesha? Lini tulikuona ukiwa mgeni tukakukaribisha au ukiwa uchi tukakuvika? Tena ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa tukakutunza au ukiwa kifungoni tukakutembelea?’ 

“Naye Mfalme atawajibu, ‘Amin, amin ninawaambia, kwa jinsi mlimvyotendea mmojawapo wa hawa ndugu Zangu walio wadogo, mlinitendea Mimi.’ “Kisha atawaambia wale walio upande Wake wa kushoto, ‘Ondokeni kwangu, ninyi mliolaaniwa, nendeni kwenye moto wa milele alioandaliwa kwa ajili ya ibilisi na malaika zake. Kwa maana nilikuwa na njaa hamkunipa chakula, nilikuwa na kiu hamkuninywesha, nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha, nilikuwa uchi hamkunivika, nilikuwa mgonjwa hamkunitunza na nilikuwa gerezani nanyi hamkuja kunitembelea.’

“Ndipo wao pia watajibu, ‘Bwana ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, au ukiwa mgeni au uchi , au ukiwa mgonjwa na kifungoni na hatukukuhudumia?’ “Naye atawajibu, ‘Amin, amin nawaambia, kwa jinsi ambavyo hamkumtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, hamkunitendea mimi.’ “Ndipo hawa watakapoingia kwenye  adhabu ya milele, lakini wale wenye haki wataingia katika uzima wa milele.’’”

cooking-pot-

cooking

cooking1

ENGLISH: COLD THREE COOKING STONES.

 The proverb started in a two-person conversation about the work of the three cooking stones. One asked the other, ‘What are the three cooking stones?’  The other answered, ‘these are the three stones, or bricks which are used in holding the cooking tool.’

The cooking pot sits on those three stones in the traditional African fireplace. These three cooking stones of equal size and placement easily support the clay or metal cooking pot. They are positioned very carefully. 

Underneath or between them firewoods are put, which are set on fire. The three stones need each other; they work together. If one takes away one stone and the pot falls down. They however, get cold if people don’t cook food. That’s why when people discover that food is not cooked at a particular family, they say, ‘cold three cooking stones.’

The balance between their standing close together yet apart is a symbol of community life. This is one the Sukuma Proverb that is used to teach about the values of unity, community and working together.

It is found in the Small Christian Communities (SCCs) Book: During a SCC Workshop a very effective teaching on of unity and working together is to demonstrate African proverb.

It has the following teachings:

  1.   A creative way of teaching the importance of SCCs is to describe the three cooking stones on which SCCs are “cooked” as spiritual values, acts of mercy, and concrete projects.
  2.   The metaphor of the one cooking pot and three stones can be used in different ways to describe the Catholic Church.  That is, one church but three parts: priests, religious and laity.
  3.   The image of the cooking pot and the three stones is an important analogy for the Trinity: that is one God and three Divine Persons, namely Father, Son and the Holy Spirit.
  4.   A Sukuma, Tanzania proverb:  The three stones that support the cooking pot are cold (literally mafiga baridi in Swahili) means that there is no fire and thus no food is being cooked, which is a sign of the lack of hospitality, welcome and love. 

The cold stones are a sign of the lack of good relationships within the home itself and with people living outside. Three-cooking stones used for holding a pot or kitchen pan, stay cool because they do not cook food. That is why people tell such family, ‘cold three cooking stones.’ Refer to ‘Kueneza Injili kwa Methali’; which can be literally translated as ‘Spreading the Gospel through Proverbs, page 58.

Such book was written by researchers who are: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Joseph Healey M.M., published by Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

The proverb teaches people about generosity of welcoming strangers into their families, so that they can receive the blessings that come from caring for them, in their lives.

 “The generous hospitality of our families is the responsibility of those who follow Jesus Christ. Sin is not only doing wrong, but also not doing good to others, not fulfilling our obligations, and not dealing with their problems. The priest and the Levite did not harm the victim, but they passed away regardless. They did nothing. ” Refer to “Kueneza Injili kwa Methali” which means, ‘Spreading the Gospel through Proverbs’, page 58.

Leviticus 19:34.

Luke 10: 31-33.

Romans 15: 7.

Hebrews 13: 2.

Genesis 18: 1-8.

1Kings 17: 10-16.

Matthew 25: 31-46.

684. CHUGA JA NKOGO (IPANDO LYA NGOGO) ITABHANYA BHALOSO. NULU “NUNDI GWANGOKO ITABHANYA BHALOSO.”

Ulusumo lunulo, lwingilile kuli munhu uyo alinhaku ogulya nyama. Alihoyi namhala umo uyo oli adina mino. Uweyi  oliatogilwe gulya nyama ja nofu. Lushigu lumo agalomba nyama kubhiye, aliyomba, ‘ninhagi inyama nalye.’  Abhiye bhang’winha bhaliyomba, ‘solaga yiyi.’

Gashinaga inyama iyo bhagang’winha lyali pando lya ngoko, lulu, nundi go ngoko. Ohayugema ugugulya gunemela kulwa bhudamu bhogo.  Hunagwene abhanhu bhenabho, bhagandya guyuyomba giki, ‘chuga ja ngoko (ipando lya ngoko) itabhanya bhaloso.’ Nulu ‘Nundi go ngoko itabhanya bhaloso.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo alina wikumvi bho gulya nyama nsoga bhuli makanza. Umunhu ng’wunuyo, ulu ugayiwa inyama ija jofu agagemaga yoseyose. Uluwinhiwa gugulu go ngoko aguduma ugugubhinza na agukoyakoya noyi ugugudakuna.

Uweyi agikiloaga nu ngosha uyo alina wikumvi bho guja kuli nkima uyo aliowiza. Nang’hwe ulu ugaiwa agakoya koyaga noyi, guti nu ni ogugulu go ngoko. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘chuga ja ngoko (ipando lya ngoko) itabhanya bhaloso.’ Nulu ‘Nundi go ngoko itabhanya bhaloso.’ Lolaga kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 50.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya guleka bhulaku, nulu wikumvi bho gwita yabhubhi, umuwikaji bhobho, kugiki bhadule gwikala bho mholele na bhichabho, umukikalile kabho.

Yilijidamu noyi ukubhanhu abho bhagatongelagwa na wikumvi bho gwita mihayo ya bhubhi aha welelo, ugugaluka. Ukwene hu guleka uwikaji bho gwita iyabhubhi na gwingila muwikaji bhupya ubho gwita ya wiza. (Matayo 19:23-26).

Umuwikaji wise dulilomba wambilijiwa bho ng’wa Mulungu na jinhilwa ja ng’wa Moyo Ng’wela, kunguno ubho nguzu jise bhung’wene, dududula ugwita josejose. Ulu dunomba Mulungu bho guzunya dugubhedecha, iki ayo gadadulikanile ukubhanhu, gadulikanile ukuli Mulungu. Rejea Kueneza Injili Kwa Methali, bhukurasa bho 50.

Matendo ya mitume 24:24-25.

Marko 10:22.

Marko 4:19.

Tito 2:12.

KISWAHILI: KIKWATO CHA KUKU HUWAHANGAISHA WENYE TAMAA (WANAOPENDA KULA NYAMA KILA WAKATI).

Methali hiyo, yatokea kwa mtu yule ambaye ni mlafi wa kula nyama. Alikuwepo mzee mmoja ambaye hakuwa na meno. Yeye alipenda kula nyama ya minofu. Siku moja aliomba nyama kwa wenzake akisema, ‘nipeni nyama nile.’ Wenzake hao, walimpatia wakisema, ‘chukua hii.’

Kumbe, hiyo nyama waliyompatia yilikuwa ya kwato la kuku, au mguu wa kuku. Alipojaribu kula ikamshinda, kwa sababu ya ugumu wake. Ndiyo maana watu wakaanza kusema kwamba, ‘kikwato cha kuku huwahangaisha wenye tamaa (wanaopenda kula nyama kila wakati).’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ni mwenye tamaa ya kula nyama nzuri kila wakati. Mtu huyo, akikosa nyama hiyo, huhangaika sana, kwa kujaribu kile anachokiona. Akipewa kwato au mguu wa kuku, hushindwa kuuvunja na huhangaika sana kuutafuna.

Yeye hufanana na mwanamume yule ambaye ni mwenye tamaa ya kwenda kwa mwanamke anayemuona kuwa ni mzuri. Naye akimkosa huhangaika sana katika maisha yake, kama mtu yule aliyeshindwa kula kikwato cha kuku. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘kikwato cha kuku huwahangaisha wenye tamaa (wanaopenda kula nyama kila wakati).’ Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 50.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuachana na tabia ya ulafi au tamaa ya kutenda maovu, maishani mwao, ili waweze kuishi kwa amani na wenzao, katika maisha yao.

Ni vigumu sana kwa watu wale ambao wanatawaliwa na tamaa za kufanya anasa za hapa duniani, kugeuka, yaani kuacha maisha ya namna hiyo na kuwa na maisha mapya (Mathayo 19:23-26).

Katika unyonge wetu tunahitaji msaada wa Mungu na vipawa vya Roho Mtakatifu, kwa kuwa kwa nguzu zetu hatuwezi kufanya lolote. Tukimwomba Mungu kwa imani tutafanikiwa kwa kuwa yasiyowezekana kwa mwanadamu, yawezekana kwa Mungu. Rejea Kueneza Injili Kwa Methali, bhukurasa bho 50.

Matendo ya mitume 24:24-25. “Baada ya siku kadhaa Feliksi alipokuja pamoja na Drusila mkewe, ambaye alikuwa Myahudi, alituma aitiwe Paulo na kumsikiliza alipokuwa akinena juu ya imani katika Yesu Kristo. Naye Paulo alipokuwa akinena juu ya haki kuwa na kiasi na juu ya hukumu ijayo, Feliksi aliingiwa na hofu na kusema, “Hiyo yatosha sasa! Waweza kuondoka. Nitakapokuwa na wasaa nitakuita.””

Marko 10:22. “Yule mtu aliposikia hayo, akasikitika sana, akaondoka kwa huzuni kwa sababu alikuwa na mali nyingi.”

Marko 4:19. “lakini masumbufu ya maisha haya, udanganyifu wa mali na tamaa ya mambo mengine huja na kulisonga lile neno na kulifanya lisizae.”

Tito 2:12. “Nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia, ili tupate kuishi maisha ya kiasi, ya haki na ya kumcha Mungu, katika ulimwengu huu wa sasa, huku.”

chicken-1

chicken2

chicken3

ENGLISH: CHICKEN LEGS PUNISHED THE GREEDY MEAT EATER.

This proverb comes from a greedy person. Some days back, there was a toothless old person who preferred eating boneless meat. One day he asked for meat from his friends. He said, ‘Give me some meat to eat.’

Instead of giving him boneless meat, they gave him chicken legs. He tried eating it but it was not easy to chew the bones. This is where the proverb ‘chicken legs punished the greedy meat eater’ came into being.

This proverb can be likened to a man who always want to eat good meat. Such a person will be uncomfortable if there is no meat to eat. This person can be compared to a man who always chase for beautiful ladies. At the end of the day, this man is likely to land on a difficult woman who will cause trouble to him (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 50). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

This proverb teaches people to break free from the desire to do evil things in life. This can make one to live in harmony with others in their lives.

It is very difficult for those people who are ruled by the lust of this world to turn around, to give up such a life and to have a new life (Matthew 19: 23-26).

In our weaknesses we need the help of God and the gifts of the Holy Spirit, for in our own strength we cannot do anything. If we ask God in faith we will succeed because whatever is impossible to man, it is possible with God (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 50).

Mark 10:22. Mark 4:19 .Titus 2:12.

681. ISUMBI LILI MU NDA.

Ulusumo lunulo, lwingilile ku mahoya ga bhageni na bhanikili kaya yiniyo. Uumo o bhanikili kaya agabhasumbila abhageni aliyomba, ‘makaribhu ng’wigashe mumasumbi.’ Uweyi agashosha, ‘umunhu adadulile gwigasha hisumbi ulu adina bhisagilwa bho gupandika jiliwa.’ Nang’hwe agashosha, ‘guli gonghana ubho nduhu jiliwa umu nda, ugwikala hoyi idinasolobho.’ Hunagwene abhanhu bhagandya guyuyomba giki, ‘isumbi lili mu nda.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatumamaga milimo na wisagilwa bho gupandika matwajo mingi, umuwikaji bhokwe. Umunhu adadulile gwita nimo uyo gudina solobho.

Isolobho yiniyo, bhuli wisagilwa ng’wa munhu uyo alizunya gwigasha hisumbi kunguno ya kumana igiki agupandikia jiliwa. Giko lulu, umunhu ulu ugaiwa ijiliwa, ihingi, agingaga haho na haho, kunguno adalazunya ugwigasha bho nduhu gulya aho kaya yiniyo. Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ubhukurasa 40.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Umunhu ng’wunuyo agatumamaga milimo yakwe bho bhukamu ubho bhudulile gumpandikila matwajo mingi, umuwikaji bhokwe, ayo gagikolanijiyagwa na jiliwa. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘isumbi lili mu nda.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kubhiza na wizagilwa bho gubhambilija ijinagongeja bhukamu bho gutumama milimo yabho chiza, kugiki bhadule kupandika matwajo mingi, umuwikaji bhobho.

Ijina moyo, dulidakilwa gwikala wikaji bho nyazunya aise bhazunya bha ng’wa Yesu Kristo, na gunondela weyi, bho gubhiza na bhisagilwa bhutale giki dulapandika bhupanga ubho bhudashilaga.

Ulu dubhiza dudina wisagilwa bho gupandika bhupanga ubho bhudashilaga, munho ugunondela gwise UYesu Kristo, gugubhiza gudina solobho, nulu nimo go bhule duhu. Kuti numo Untume Paulo aliyombela, ‘ulu Yesu Kristo adajukile, uguzunya gwise guli bhule.’

Ulu munhu agazunya gwiyumilija gwikala hizumbi, bho gwigasha ahisumbi linilo, ali na wisagiji bho gupandika jiliwa, nayise bhazunya igelelilwe gwiyumilija, guja kwikelesia, bhuli lushugu ulo Mfungo, kunguno dumanile igiki dugulwa Jiliwa na Sebha, na gulangwa Mhayo go ng’wa Mulungu, uyo gugailishaga imioyo yise.

Aliyo uwiza bho jizunya, (guti bhutumami ukubhangi, bhugubhiza bhulihoyi bhuying’wene, na bhutumami bho nduhu gulindila gulipwa) bhuli na solobho nhale gukila ulusumo ulo Jisuguma. Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa bho 40-41,

Yohane 6: 26-27.

Luka 2:25-32.

Marko 10:29-30.

2Timotheo 4:6-8.

KISWAHILI: KITI KIMO TUMBONI.

Methali hiyo ilianzia kwenye maongozi ya watu wageni na wanafamilia. Mmoja ya wanafamilia aliwakaribisha wageni akisema, ‘karibuni mketi kwenye kiti.’ Mmoja wa wageni alijibu, ‘mtu hawezi kuketi kitini isipokuwa ana tumaini la kupata chakula.’ Yeye akajibu, ‘ni kweli kiti bila chakula kwenye tumbo hakina maana.’ Ndiyo maana watu wakaanza kusema kwamba, ‘kiti kimo tumboni.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu anayefanya kazi kwa kutumaini kupata mafanikio mengi kwenye kazi yake hiyo. Mtu hawezi kufanya kazi bila kuwa na faida. Faida hiyo ni kama matumaini ya mtu anayekubali kuketi kwenye kiti kwa sababu ya kuelewa kwamba atapata chakula.

Hivyo mtu akikosa chakula huondoka mara moja kwa sababu hatakubali kukaa bila kula kwenye familia hiyo. Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 40.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Mtu huyo hufanya kazi zake kwa bidii ya kumwezesha kupata mafanikio yanayofananishwa na chakula. Ndiyo maana watu husemwa kwamba, ‘kiti kimo tumboni.’

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na matumaini ya kumwezesha kuongeza bidii katika kuyatekeleza vizuri majukumu yao, ili waweze kupata mafanikio ya kutosha kuyandesha vizuri maisha yao.

Kiroho, tunahitaji kuishi maisha ya Kikristo na kumfuata Yesu Kristo, kwa kuwa tuna tumaini la kwamba tutatunukiwa uzima wa milele. Ikiwa hatuna tumaini la kuupata uzima huo wa milele, kumfuata Yesu Kristo hakuna maana, au ni kazi bure tu. Kama Mtakatifu Paulo aliyosema, “ikiwa Yesu Kristo hakufufuka imani yetu ni bure.”

Kama mtu aliyekubali kuvumilia kukaa kitini kuwa ana tumaini la kupata chakula, ndiyo sisi waamini yatupata kuvumilia kwenda Kanisani kila Jumapili kwa sababu tuna hakika kwamba tutakula chakula cha Bwana, na kufundishwa Neno la Mungu linalotulisha mioyo yetu.

Lakini ubora wa ukristo (kama huduma kwa wengine, kutakuwa na ubinafsi na huduma bila kutumaini malipo) unaleta maana kubwa zaidi kuliko methali hii ya Kisukuma. Rejea Kueneza Injili Kwa Methali, ukurasa 40-41.

Yohane 6: 26-27. “Yesu akawajibu, “Amini, amini nawaambia, ninyi hamnitafuti kwa kuwa mliona ishara na miujiza, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba. Msishughulikie chakula kiharibikacho, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele, ambacho Mwana wa Adamu atawapa. Yeye ndiye ambaye Mungu Baba amemtia muhuri.’”

Luka 2:25-32. “Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake. Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.

Simeoni akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria, ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake  na kumsifu Mungu, akisema: “Bwana Mungu Mwenyezi, maana macho yangu yameuona wokovu    Wako,  ulioweka tayari machoni pa watu wote, nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu Mataifa na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.””

Marko 10:29-30. “Yesu akasema, “Amini, nawaambia, hakuna mtu ye yote aliyeacha nyumba, ndugu waume, au ndugu wake, mama, baba, watoto au mashamba kwa ajili Yangu na kwa ajili ya Injili, ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu, nyumba, ndugu waume, ndugu wake, mama, baba, watoto, mashamba pamoja na mateso kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao.”

2Timotheo 4:6-8. “Kwa maana mimi sasa ni tayari kumiminwa kama sadaka ya kinywaji, nayo saa yangu ya kuondoka imetimia. Nimevipiga vita vizuri, mashindano nimeyamaliza, imani nimelinda. Sasa nimewekewa taji ya haki ambayo Bwana, mwamuzi wa haki, atanitunukia siku ile, wala si mimi tu, bali pia wote ambao wamengoja kwa shauku kuja Kwake.”

 

chair1

marriage1

marriage

ENGLISH: A SEAT WITHOUT FOOD IS NOTHING.

This saying comes from the conversation between visitors and the host family. One of the family members welcomed the guests saying, ‘welcome and have a seat’ then the visitor replied saying that ‘a seat without food is nothing.’

The saying can be compared to a person who works with hopes to gain something in his/her work. One cannot work without knowing how much will he/she going to benefit from that work. That benefit is like the prospects that can make someone agree to sit on a chair. When a visitor doesn’t see any sign of getting food, he/she can leave the house (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 40.) This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

People can work hard in order to achieve food-related successes.

This saying teaches people about how to increase their efficiency in performing their tasks. This can make them to be successful in their lives.

Spiritually, we need to live the Christian life and follow Jesus Christ, for we have the hope of being blessed with eternal life. If we have no hope of attaining that eternal life, following Jesus Christ is useless, or even futile. As St. Paul puts it, “if Jesus Christ had not risen, our faith would be in vain.”

As someone who has agreed to stay in the chair having the hope of finding food, then we believers have endured going to church every Sunday because we are confident that we will eat the Lord’s Supper, and be taught the Word of God that warms our hearts.

But the quality of Christianity (as a service to others, it is special because it is a service without hope of reward) makes much more sense than this Sukuma proverb (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 40-41)

John 6: 26-27. Luke 2: 25-32. Mark 10: 29-30. 2Timothy 4: 6-8.

680. DESHI AKALEKA JULALA.

Deshi lili lina na noni iyo ikagalyaga miswa ijo jigitanagwa kidetemela mbula. Lushigu lumo, uDeshi agaja aha jigulu aha tuzengile utujidetemela mbula tunuto.

Aho oshika hoyi, agajibhona jilifuma imoimo umulipundu. Bhuli yene iyo yafumaga, UDeshi uyitulaga munomo. Agendelea gwita giko ku likanza lilihu. Iki imiswa jigendelea gufuma duhu kulikanza lilihu, UDeshi agiguta na guduma ugujimila, nose imiswa jigaikindika gung’wiyungulila na gubhita umumiso gakwe.

UDeshi agandya guhaya, “ingaji, nose muliningilila mumiso.” Agashoka na gujileka jilifuma. Hunagwene abhanhu bhagandya guyuyomba ulu bhalya jiliwa bhiguta na gujileka, giki, ‘Deshi agaleka julala.’

Intondo yahoo, UDeshi agaja hangi, mujigulu atubhile na ukunhu alimba. “itagi kiti igolo, itagi kiti igolo.” Ahikanza lya mhindi agimbaga giki, “Mukutudisha, mukutudisha.” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 38.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagalyaga jiliwa mpaga bhiguta na guleka, umukikalile kabho. Abhanhu bhenabho, ulu bhalya mpaka bhiguta, bhagaluyombaga ulusumo lunulo guti nzila ya goyela gujilya ijijiwa jinijo, iki bhajidumaga ugujimala, giki, ‘Deshi agaleka julala.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na jipimilo ja gwiyangula gujileka ijojabhalemelaga. Hangi, lobhalanga abhanhu bhenabho, gubhiza na wizang’holo bho gubhakaribhusha abhageni na gubhalila bho gubhinha jiliwa, kugiki abhanhu bhenabho, bhadule gulya na kupandika nguzu ja gwikomeja guminza chiza, umulugendo lobho.

Igelelilwe gubhitila yawiza abhigisu. Bhuli ikanza ilo dulibhitila ya wiza abhigizu, dugung’witilaga Yesu Kristo iya wiza yiniyo. UYesu obhitilaga yawiza abhanhu, umuwikaji bhokwe.

Ijinagongeja, ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya Ng’wa Yesu uyo agabhalishaga jiliwa, ijo jili mili na mininga gakwe, umu Isakramenti lya Ekaristi Nhagatifu.

Undimi untengeke agabhalishaga abhanhu jiliwa, bho gubhalanga Mhayo go Mulungu, uyo gugabhinhaga bhupanga. UYesu Kristo, hung’wene uyo ali ‘ha ng’wa Lutubhila gule.’ Ukwene huguhaya giki, ahali Uweyi bhagatubhilaga kule. Uyo agajaga kuli Weyi adubhona inzala. Uyo alinzunya Weyi, adiigwa inota gete. Rejea Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 39.

Isaya 25:6.

Ezekekieli 34: 1-2.

Marko 6:41-44.

Yohane 10:9-10.

Yakoko 2:15-17.

Luka 10:30-37.

Mathayo 25:31-46.

KISWAHILI: DESHI ALIAKA KUMBIKUMBI WAKARUKA.

Deshi ni jina la ndege ambaye hula jamii ya kumbikumbi wadogo (kidetemela mbula). Siku moja Deshi alikwenda kwenye kuchuguu (nyumba ya kidetemela mbula).

Alipofika hapo, alikuta kumbikumbi wanatoka mmoja mmoja shimoni. Kila kilichotoka Deshi alikiweka mdomoni. Akaendelea kufanya hivi kwa muda mrefu. Kwa vile waliendelea kutoka tu kwa muda mrefu, Deshi alishiba na kushindwa kuwameza, hata wakawa wanaruka kumzunguka na kupita machoni pake.

Deshi alianza kusema, ‘Ondokeni, mwishowe mtaniingia machoni.” Alirudi na kuwaacha kumbikumbi hao, wanatoka. Ndiyo maana watu wakaanza kusema wanaposhiba chakula na kukiacha, kwamba, ‘Deshi aliacha kumbikumbi wakaruka.”

Kesho yake, Deshi alikwenda tena kwenye kichuguu akiwa na njaa akiimba. “itagi kiti igolo, itagi kiti igolo” (fanyeni kama jana, fanyeni kama jana”). Wakati wa jioni huwa anaimba hivi, “Mukutudisha, mukutudisha” (mtatuingia machoni, mtatuingia machoni”). Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 38.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hulinganishwa kwa watu waliokula chakula mpaga wakashiba na kusaza, katika maisha yao. Watu hao, wanapokula mpaka kutosheka, huisema methali hiyo kama njia ya kuacha kula chakula, kwa vile wameshindwa kukimaliza, kwamba, ‘Deshi aliacha kumbikumbi wakaruka.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuwa na kiasi katika maisha, kwa maana ya kuamua kuacha kula chakula, baada ya kutosheka. Pia huwafundisha watu hao, kuwa na ukarimu wa kuwakaribisha wageni na kuwaandalia chakula, ili wageni hao waweze kula na kupata nguzu za kuwawezesha kuendelea vizuri na safari yao.

Yatupata kuwatendea wenzetu mema. Kila tunapomtendea mwenzetu mema tunamtendea mema Yesu Kristo. Kila tunapokosa kumtendea mwenzetu mema, tunakosa kumtendea Yesu Kristo mema hayo. Yesu alikuwa mtu aliyetenda wema kwa wengine.

Zaidi ya hayo, methali hiyo, yatufundisha juu ya Yesu Kristo anayetulisha na kutushibisha chakula, yaani mwili na damu yake katika Sakramenti ya Ekaristi Takatifu.

Mchungaji mwema huwalisha watu chakula, yaani huwafundisha neno la Mungu linalowapatia watu wokovu. Yesu Kristo ndiye “lutubhila kule,” yaani kwake njaa iko mbali. Anayekwenda kwake hataona njaa. Anayemwamini Yeye hataona kiu kamwe. Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 39.

Isaya 25:6. “Na katika mlima huu Bwana wa Majeshi atawafanyia mataifa yote karamu ya vitu vinono, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, karamu ya vinono vilivyojaa mafuta, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, iliyochujwa sana.”

Ezekekieli 34: 1-2. “Neno la Bwana likanijia kusema, mwanadamu, toa unabii juu ya wachungaji wa Israeli, toa unabii, uwaambie, naam hao wachungaji Bwana Mungu asema hivi, ole wao wachungaji wa Israeli wanaojilisha wenyewe. Je, wachungaji kuwalisha kondoo?”

Marko 6:41-44. “Kisha Yesu akatwa ile mikate mitano na wale sakaki wawili akatazama juu mbinguni akamshukuru Mungu, akaimeja mikate, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu na wale samaki wawili pia. Akawagawia wote, watu wote wakala wakashiba wakaokota mabaki ya mikate na samaki pia, wakaja vikapu kumi na viwili.”

Yohane 10:9-10. “Mimi ni mlango. Anayeingia kwa kupitia kwangu ataokolewa; ataingia na kutoka, na atapata malisho.”

Yakoko 2:15-17. “Tuseme kaka au dada hana nguo au chakula. Yafaa kitu gani ninyi kuwaambia hao: Nendeni salama, mkaote moto na kushiba bila kuwapatia mahitaji yao ya maisha?”

Luka 10:30-37. “Mfano wa Msamalia Mwema.”

Mathayo 25:31-46. “Hukumu ya Mwisho.”

bird eating insects

ants1

ants

 

ENGLISH: DESHI LEFT THEM TO FLY.

Deshi is the name of a bird that feeds on flying ants. One day deshi went to the anthill where flying ants live. When it got there, it found that the flying ants were coming out of their hole. What deshi did is setting its mouth closer to the entry of the hole so that the flying ants can enter straight into deshi’s mouth. It ate the flying ants to its satisfaction. Later on, because of satisfaction, the flying ants began flying around to surround deshi and, at this time, deshi had no any appetite to continue eating them. When the flying ants were doing so, deshi told them: “Get out, and finally you will enter our eyes.” He went back and left them, and they left to their hole. That is why people, when have eaten to their satisfaction, say “deshi left them to fly.”

The next day, deshi went back to the anthill while singing: “Itagi giti igolo, itagi git igolo” (do as you did yesterday, do as you did yesterday ). While the day before, it was singing “you will enter our eyes, you will enter our eyes” (Refer to Kueneza Injili kwa Methali’ which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 38). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

This proverb can be compared to greedy people who will tend to eat food to their satisfaction and later on begin to abuse it.

The proverb also teaches people to do good to fellows. Whenever we do good to one another, we do good to Jesus Christ. Whenever we fail to do good to one another, we fail to do good to Jesus Christ. Jesus was a man who did good to others.

Further, the proverb teaches us about Jesus Christ who nourishes and satisfies us with food, that is, his flesh and blood in the Sacrament of the Holy Eucharist.

The good shepherd feeds the people, that is, teaches them the word of God for salvation. In Jesus Christ hunger is far away. Whoever goes to Him will not be hungry. He who believes in Him will never feel thirsty (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 39).

Isaiah 25: 6. Ezekiel 34: 1-2. Mark 6: 41-44. John 10: 9-10. James 2: 15-17. Luke 10: 30-37. Matthew 25: 31-46.