mother tongue

694. WASANGA NTEMI WABHITA.

Ulusumo lunulo, lwandija kuli munhu uyo agabhasanga abhiye bhamalaga ugulya ijiliwa. Umunhu ng’wunuyo, agawilwa giki, ‘wasanga Ntemi wabhita.’ Ukwene, huguhaya giki, wasanga bhamalaga ugulya.

“Ikale untemi uluubhasanga abhanhu bhalihalibhilimga, nulu ha nimo, bhimilaga na gungisha. Aliyo untemi ulubhasanga bhalilya, goli ng’wiko ugwimila na gungisha. Ulunibhangisha niobhaobhalemeja na gubhawila: “Unene nadalang’hanalaga ubhupanga wing’we, ubhugali hugabhulang’hanaga ubhupanga wing’we; hangi bhugalang’hanaga ubhupanga bhone. Unene nadi ntemi wing’we. Ijiliwa, nulu ubhugali hu ntemi wing’we. Idichiza ugunkuja ntemi gulebha ijiliwa.”

Mpaga lelo uluubhasanga bhanhu bhalilya guling’wiko ugwigisha, kunguno bhalihoya na ntemi obho. Ulubhumala ugulya bhagatulaga magofi kugiki bhize gwinja jiseme, mumho giki, untemi omalaga gubhita. Bhamalaga ugulya.” Hunagwene abhanhu bhagandya guyuyomba ukuli munhu uyo osangaga abhiye bhamalaga ugulya, giki, ‘wasanga ntemi wabhita.’ Lolaga kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 64.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gudebha solobho ya jiliwa bhogolecha ikujo, kunguno hijene hijo jigadinhaga nguzu ja gwendelea gwikala na guitumama chiza imilimo yise.

“Umuwikaji bho munhu ijiliwa nulu ubhugali hi ginhu ja solobho noyi. Ubhugali hu ntemi wise kunguno agadulang’hanijaga ubhupanga wise.

Hangi UMhayo go ng’wa Sebha guli jiliwa ijojigadinhaga bhupanga bho ng’wa Mulungu ng’winikili ubho bhudakenagukaga.

ISakramenti iya Ekaristi jili jiliwa ng’hana na ja solobho noyi ijojibhugalang’hanaga na gubhujamya ubhupanga ubho bhuli bho ng’wa Mulungu umugati yise. “Uyo agulyaga mili gone na gun’gwa mininga gane, agikalaga mugati yane nu nene mugati yakwe.” (Yohana 6:56).

Uluushiga Mukanisa ugunsanga Untemi oko UYesu Kristo, alimo umu shimile sha Ngate umugati ya Tabarnakulo. Adingaga, nulu adabhitaga. Uguzunya gwise ugojigatoliki guliduwila na guduhagigish’ija giki, UYesu Kristo alimo nhana umu shimile sha ngate umu Sakramenti ya Ekaristia. Kuyiniyo, igeleliwe gunamya na gunkuja umu Sakramenti yiniyi Uweyi uyo Ali Ntemi wise bho guntulila mgofi.” Lolaga, Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 65.

Kumbukumbu 8:3.

Yeremia 15:16.

Yohane 4:34.

Yohane 6:11-15.

Yohane 6:51, 57.

Mathayo 6:11.

KISWAHILI: UMEKUTA MTEMI AMEPITA.

Methali hiyo ilianzia kwa mtu aliyewakuwa wenzie wamekwisha kula chakula. Mtu huyo, aliambiwa na wenzake hao kwamba, “umekuta mtemi amepita,” Maana yake, amewakuta wamemaliza kula.

“Zamani mtemi akiwakuta watu kwenye mkutano au kazini, walisimama na kumsalimu. Lakini akiwakuta wanakula, ilikuwa mwiko kusimama na kumsalimu. Kama wangelimsalimu, angeliwakataza na kuwaambia: “Mimi situnzi maisha yenu, ugali hutunza maisha yenu; tena hutunza maisha yangu. Mimi si mtemi wenu. Chakula au ugali ni mtemi wenu. Si vizuri kumtukuza mtemi kuliko chakula.”

Mpaka leo ukiwakuta watu wanakula ni mwiko kusalimiana, kwa maana wanaongea na mtemi wao. Wakimaliza kula wanapiga makofi ili waje kuondoa vyombo, maana yake mtemi amekwisha pita. Wamemaliza kula.” Ndiyo maana watu walianza kusema kwa mtu aliyewakuta wamekula, kwamba, ‘umekuta mtemi amepita.’ Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 64.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kutambua umuhimu wa chakula kwa kuonesha heshima kwa sababu, hicho ndicho kinachowapatia uhai, na nguvu za kuendelea kuishi na kufanya kazi zao vizuri.

“Katika maisha ya mtu chakula au ugali ni kitu muhimu sana. Ugali ni mtemi wetu kwa kuwa unatutunzia uzima wetu.

Tena Neno la Bwana ni chakula ambacho kinatupa uzima wa Mungu ndani yetu, uzima wa Mungu mwenyewe usioharibika.

Sakramenti ya Ekaristi ni chakula kweli na cha maana sana kinachotunza na kuimarisha uzima ule wa Mungu ndani yetu. “Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, akaa ndani yangu nami ndani yake.” (Yohane 6:56).

Ukifika kanisani utamkuta mtemi wako Yesu Kristo yumo katika maumbo ya mkate ndani ya Tabernakulo. Haondoki au kupita. Imani yetu ya kikatoliki yatujulisha na kutuhakikishia kwamba Yesu Kristo yumo kweli katika maumbo ya mkate katika sakramenti ya Ekaristi. Kwa hiyo yatupasa kumwabudu na kumtukuza katika sakramenti hii yeye aliye mtemi wetu kwa kumpigia makofi.” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 65.

Kumbukumbu 8:3. “Alikudhili na kukufanya uone njaa kisha akulishe kwa mana, ambayo wewe wala baba zako hamkuijua, awafundishe kuwa mwanadamu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila neno litokalo katika kinywa cha BWANA.”

Yeremia 15:16. “Maneno yako yalipokuja, niliyala, yakawa shangwe yangu na furaha ya moyo wangu, kwa kuwa nimeitwa kwa jina lako, Ee BWANA Mungu, Mungu Mwenye Nguvu.”

Yohane 4:34. “Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma na kuikamilisha kazi yake.”

Yohane 6:11-15. “Ndipo Yesu akachukua ile mikate, akamshukuru Mungu na kuwagawia wale watu waliokuwa wamekaa kwa kiasi walichohitaji. Akafanya vivyo hivyo na wale samaki. Kila mtu akapata kadri alivyotaka. Watu wote walipokwisha kula na kushiba, akawaambia wanafunzi wake, “Kusanyeni vipande vilivyobaki vya ile mikate, kisipotee cho chote.’’ Hivyo wakavikusanya wakajaza vikapu kumi na viwili kwa vipande vilivyobaki vya ile mikate mitano na samaki wale wawili wadogo.

Baada ya watu kuona mwujiza ule Yesu aliofanya, walianza kusema, “Hakika huyu ndiye Nabii ajaye ulimwenguni!’’ Yesu akijua kwamba walitaka kuja kumfanya awe mfalme wao, kwa nguvu, akajitenga nao akaenda milimani peke Yake.”

Yohane 6:50- 57. “Lakini hapa kuna mkate utokao mbinguni, ambao mtu ye yote akiula, hatakufa. Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu ye yote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.’’

Ndipo Wayahudi wakaanza kuhojiana vikali wao kwa wao wakisema, “Mtu huyu awezaje kutupatia mwili wake tuule?’’ Hivyo Yesu akawaambia, “Amin, amin, nawaambia, msipoula mwili wa Mwana wa Adamu na kuinywa damu Yake, hamna uzima ndani yenu.

Mtu ye yote aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele. Nami nitamfufua siku ya mwisho. Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli. Ye yote alaye mwili wangu na kunywa damu yangu, atakaa ndani yangu nami nitakaa ndani yake. Kama vile Baba aliye hai alivyonituma Mimi, na kama nami ninavyoishi kwa sababu ya Baba, hivyo anilaye mimi ataishi kwa sababu yangu.”

Mathayo 6:11. “Utupe leo chakula chetu tunachohitaji.”

food6

ntemi zulu-kingdom-

child eating food

ENGLISH: YOU HAVE FOUND THE CHIEF GONE.

This proverb has its origin from someone who found his fellows had finished eating food. To report to him that they had already eaten food, they told him that “you found the chief gone” meaning that they had finished eating food.

“In the past when the chief walked in for meeting or any business, people around him were to stand up and greet him as a sign of respect. But if the chief reaches a certain place and finds people eating, he was not allowed to stop them from eating. Even if people can stand to greet him he could stop them saying that food keeps peoples’ lives but the chief does not. He (chief) also respects food because it gives him life. Until today, when people are eating they don’t have to speak to each other because they are busy with their chief, food. When they finish eating, they clap hands as a sign of calling the one responsible to collect the vessels used for eating. This is the time one can say ‘the chief has gone’ (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 64). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

The proverb teaches people to recognize the importance of food by showing respect because that is what gives them life and the power to continue living and doing their jobs.

In a person’s life food is the most important thing. Food is our chief in that it gives us life.

Again the Word of the Lord is the food that gives us the life of God in us, the life of God Himself who is immortal.

The sacrament of the Eucharist is a true and very important food that sustains and enhances the life of God in us. “Whoever eats my flesh and drinks my blood dwells in me and I in him” (John 6:56).

When you get to the church you will find your Lord Jesus Christ in the form of bread in the Tabernacle. He does not go away or pass away. Our Catholic faith informs us and assures us that Jesus Christ is indeed in the form of bread in the sacrament of Eucharist. Therefore, we must worship and glorify Him through this sacrament (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 65).

Deuteronomy 8: 3. Jeremiah 15:16. John 4:34. John 6: 11-15. John 6:51, 57. Matthew 6:11.

693. KUGULU KULI NG’OMBE IDAKO ILALIJA.

Ulusumo lunulo, lwingilile muwikaji bho bhanhu bhabhili, abho bhikalaga heke bhuli ng’wene. Uumo olatogilwe kusiminza, uungi olatogilwe gwigasha ha kaya.

Uyo olatogilwe gusiminza, agayela ugapandika milimo, umubhuyeji bhokwe bhunubho. Imilimo yiniyo, igang’wambilija gupandika ng’ombe na sabho ningi. Umunhu ng’wunuyo, agasabha noyi kunguno ya ng’ombe yakwe yiniyo, gwendelea gubyala mpaga nose, ubhiza nsabhi ntale, umuwikaji bhokwe.

Ung’wiye uyo olatogilwe gwigasha hakaya, agamala ijiliwa uyukoyiwa na nzala nhali, ahakaya yake yiniyo. Wiyangula guja gujulomba wambilijiwa ukuli ng’wiye, unsabhi ng’wunuyo.

Ahogambilijiwa bho gwinhiwa jiliwa nu ng’wiye ng’wunuyo, agadebha igiki ubhusiminzi bhuli na solobho nhale, gutinda uwigashi bho aha kaya, ubho bhugenhaga makoye ga nzala. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘Kugulu kuli Ng’ombe idako ilalija.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagasusanyaga ugutumama imilimo. Umunhu ulu wigasha duhu adupandika josejose. Ulu uhaya gupandika ililazima wimile asiminze guja gujuchola. Uluuleka uguchola agulalila. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘Kugulu kuli Ng’ombe idako ilalija.’ Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa bho 62.’

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gugatumila amakanza gabho mugwigulambija gutumama milimo, kugiki bhadule gupandika jiliwa, jiswalo na bhulalo, umuwikaji bhobho.

 “Dulidakiwa dutumame milimo yise ya bhuli lushigu bho bhukamu. Unimo jiliginhu ijojigatulilagwa ikujo na gusungulilwa lubhango nu Mulungu. Ulu dulitumama milimo dulishugulika kihamo nu Mulungu umumilimo yakwe ya gubhumba. Kuyiniyo, imilimo jiliginhu ja solobho noyi umuwikaji bho bhanhu.

Giko dulidakilwa guchola jiliwa ijo jidakenakuguka, ijene hubhupanda ubho ng’wa Mulungu ubho bhugigelaga umu gunzunya Yesu Kristo.

Idinatosha, duchole hangi ijiliwa ija ng’hana ijoduling’hiwa umu Sakramenti ya Bhukaristia.” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, 62-63.

Methali 28:19.

Methali 20:13.

1Wathesalonike 4:11.

Yohane 6:27.

KISWAHILI: MGUU NI NG’OMBE TAKO NI JAA.

Methali hiyo, ilitokea kwenye maisha ya watu wawili waliokuwa na mapendelo tofauti. Mmoja alipenda kutembea, mwingine alipenda kukaa nyumbani.

Yule aliyependa kutembea alifanikiwa kupata kazi katika kutembea kwake. Kazi hiyo, ilimwezesha kupata ng’ombe na mali zingine, katika maisha yake. Kupitia ng’ombe huyo, alifanikiwa kuwa tajiri mkubwa baada ya ng’ombe kuendelea kuzaana zaidi na zaidi.

Yule aliyependa kukaa nyumbani aliishiwa chakula, akawa anasumbuliwa na tatizo la njaa kali katika familia yake. Ikabidi yeye aende kuomba msaada kwa yule tajiri, aliyependa kutembea. Baada ya kupatiwa msaada huo kwa kupewa chakula, alielewa kuwa, kumbe kupembea kunafaida ikiwemo hiyo ya kupata mafanikio hayo, kuliko kukaa nyumbani, ambako kunaleta tatizo la njaa. Ndiyo maana watu wakaanza kusema kwamba, ‘mguu ni ng’ombe, tako ni njaa.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa watu wale ambao wanajishauri kufanya kazi. Mtu akikaa tu hatapata chochote. Akitaka kupata lazima asimame atembee kwenda kutafuta. Asipotafuta atalala akiwa na njaa. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘mguu ni ng’ombe tako ni njaa.’ Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 62.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuutumia muda wao katika kujibidisha kufanya kazi zao za kila siku, ili waweze kujipatia chakula, nguo na malazi, katika maisha yao.

“Yatupasa kufanya kazi zetu za kila siku kwa bidii. Kazi ni jambo linaloheshimiwa na kubarikiwa na Mungu. Tunapofanya kazi tunashughulika na Mungu katika kazi yake ya kuumba. Kwa hiyo, kazi ni kitu cha maana sana katika maisha ya watu.

Vile vile yatupasa kutafuta chakula kisichoharibika, yaani uzima wa Mungu unaopatikana kwa kumwamini Yesu Kristo.

Isitoshe tutafute tena chakula cha kweli tunachopewa katika Sakramenti ya Ekaristi.” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, 62-63.

Methali 28:19. “Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele,  bali afuataye mambo ya upuzi atakuwa na  umaskini wa kumtosha.”

Methali 20:13. “Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.”

1Wathesalonike 4:11. “Jitahidini kuishi maisha ya utulivu, kila mtu akijishughulisha na mambo yake mwenyewe na kufanya kazi kwa mikono yake, kama vile tulivyowaagiza pale awali.”

Yohane 6:27. “Msishughulikie chakula kiharibikacho, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele, ambacho Mwana wa Adamu atawapa. Yeye ndiye ambaye Mungu Baba amemtia muhuri.””

man-traditional one

cows-

nkima6

 

ENGLISH: HE WHO MOVES AROUND WILL GET GOD’S PROVIDENCE, HE WHO STAYS HOME WILL DIE OF HUNGER.

This provrb comes from two individuals with different tastes in life. One of them likes so much moving around while the other one likes staying home. The one who was moving around succeeded to get something that helped him to get more wealth; cows that kept on reproducing to fill his kraal. And the one who used to stay home suffered of hunger in his family. As a result, he had to go beg from his fellow. After managing to get food from his fellow who was moving around, he said ‘he who moves around will get God’s providence, he who stays home will die of hunger’ and that came to be a proverb to warn lazy people.

This proverb can be compared to people who work hard to achieve success in life. If a person does not struggle, there is a danger of affecting the entire family because they can run shortage of food any time (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 62). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

The proverb teaches people to spend their time working hard in their daily activities so that they can provide food, clothing and shelter to their families.

We must work hard in our daily lives. Work is something that God respects and blesses. As we work we are dealing with God in His creative work. Therefore, work is the most important thing in people’s lives.

We must also seek for the imperishable food, the life of God, through the faith of Jesus Christ.

Let us also seek the true food given to us in the Eucharist (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ 62-63).

Proverbs 28:19. Proverbs 20:13. 1Thessalonians 4:11. John 6:27.

690. SEKELA MIDEKO.

Sekela mideko luli lusumo ulo lulingisilile kuli munhu uyo agayegelaga aha gulya jiliwa, kulebha ugujichola. Galihoyi mahoya ga bhanhu bhabhili, uungi atogilwe ugutumama imilimo, uungi adatogilwe. Uyo atogilwe ugutumama imilimo akayomba, ‘tujage dugatumame milimo kunguno ilikanza lyashigaga.’ Uyo adayitogilwe imilimo agashosha bhobhuzongu aliyomba, ‘naduduja ugujutumama imilimo, kunguno naliigwa shibhi.’

Uyo aitogilwe imilimo agang’wila, ‘bhasi, dujage gugalwe jiliwa kugiki umili goko gupandike nguzu chiza.’ Uweyi agashosha kubhuyegi ukunu alimila, ‘nahene dujage.’ Hunagwene abhanhu bhagandya guyung’witana giki, ‘sekela mideko.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo alingokolo umugutumama imilimo. Umunhu ng’wunuyo, atogilwe gulya jiliwa duhu bho nduhu ugujitumamila milimo ijo alijilya. Abhanhu bhagang’witanaga sekala mideko bhogundalaha, kunguno ali munhu uyo agasekaga ahikanza lya gulya jiliwa, aliyo ahikanza ilya gutumama milimo, agasunduhalaga. Hunagwene abhanhu bhagang’witanaga giki, ‘sekela mideko.’ Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, 60.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kuleka bhugokolo bho gutumama milimo, ibadala yaho, bhikomeje kuitumama chiza imilimo yao, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi umuwikaji bhobho.

“Ubhugokolo bhudarahilwe na Bhasuguma. Hangi bhulemilwe nu Mulungu. Ulu bhugokolo mugutumama milimo yise iya bhuli lushugu, guti gulima, nulu, bhugokolo umumihayo ya moyo, guti, gukija gujusalila ulushigu ulo Jumapili, guleka gusalia aha kaya, guleka guntumamila Mulungu bho bhukamu, na yingi guti yiniyo, yilemilwe pye iyose.

 Hangi dudizubhiza bhanhu abho guhebhilwe na bhikumvi bho jiliwa nulu walwa. Uwikaji bhudi jiliwa duhu, bhubhitilile noyi. Bhuli munhu alina nhumbu ya gulya jiliwa. Dubhize na nzala ya gumbokela Sebha wise Yesu Kristo, umu Sakramenti ya Bhukaristia. Dubhize na nhumbu ya gulya jiliwa ja ng’wa Sebha. Dubhize na bhuyegi uludulimbokela umujigukulu jakwe. Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 60-61.

Mwanzo 25:34.

Waebrania 12:16.

2Wathesalinike 3:10.

Waroma 4:17.

Methali 28:19.

KISWAHILI: MCHEKEA CHAKULA.

Mchekea chakula ni methali ambayo humaanisha mtu anayefurahia kula chakula, kuliko kukitafuta. Kulikuwa na maongezi ya watu wawili, mmoja anapenda kufanya kazi mwingine hapendi. Anayependa kufanya kazi alisema, ‘twende tukafanye kazi kwa sababu wakati umefika.’ Asiyependa kufanya kazi, alijibu kwa unyonge akisema, ‘siwezi kwenda kufanya kazi kwa sababu najisikia vibaya.’

Mpenda kazi akamwambia, ‘basi twende tukale chakula ili mwili wako upate nguvu vizuri.’ Yeye alijiku kwa furaha huku akiwa amesimama, ‘sawa twende.’ Ndiyo maana watu wakaanza kumuita, ‘mchekea chakula.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ni mzembe katika kufanya kazi. Yeye anapenda kula tu bila kukifanyia kazi kile anachokila. Watu humwita mchekea chakula kama njia ya kuonesha dharau kwake, kwa sababu ni mtu anayecheka wakati wa kula, lakini wakati wa kazi husikitika. Ndiyo maana watu humuita ‘Mchekea chakula.’ Rejea Kueneza Injili kwa Methali, 60.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuacha uzembe wa kufanya kazi, badala yake, waongeze bidii ya kuyatekeleza vizuri majukumu yao, ili waweze kupata mafanikio mengi, maishani mwao.

“Uzembe umedharauliwa na Wasukuma. Tena umekataliwa na Mungu kama ni uzembe katika kufanya kazi yetu ya kila siku, kwa mfano kulima, au uzembe katika mambo ya kiroho, kwa mfano kutosali Jumapili, kutosali nyumbani, kutomtumikia Mungu kwa bidii, n.k.

Tena tusiwe watu ambao tunatawaliwa na tamaa ya chakula au pombe. Maisha si chakula tu, bali ni zaidi. Kila mtu ana haja ya kula chakula. Tuwe na njaa ya kumpokea Bwana Wetu Yesu Kristo katika sakramenti ya Ekaristi. Tuwe na haja ya kula chakula cha Bwana. Tuwe na furaha tunapokuwa kwenye karamu yake.” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 60-61.

Mwanzo 25:34. “Ndipo Yakobo akampa Esau mkate na ule mchuzi wa dengu. Akala na kunywa, kisha akainuka akaenda zake. Kwa hiyo Esau alidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.”

Waebrania 12:16. “Angalieni miongoni mwenu asiwepo mwasherati au mtu asiyemcha Mungu kama Esau, ambaye kwa ajili ya mlo mmoja aliuza haki ya uzaliwa wake wa kwanza.”

2Wathesalinike 3:10. “Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri ili kwamba: ‘‘Mtu ye yote asiyetaka kufanya kazi, wala asile.’’”

Waroma 14:17. “Kwa maana Ufalme wa Mungu si kula na kunywa, bali ni haki, amani na furaha katika Roho Mtakatifu.”

Methali 28:19. “Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha.”

laugh

laugh children

ENGLISH: LAUGHING FOR FOOD.

This saying comes from someone who enjoys eating food rather working for it. One day, two people were in conversation, one of them was fond of working while the other one not. In the course of conversation one of them said ‘Let’s go to work because the time has come.’ The other fellow who doesn’t like to work replied saying ‘I can’t go to work because I feel bad.’ The one who likes to work, later, told his/her fellow workmate that ‘let’s go eat some food so that your body can be healthy.’ The statement on going to eat was received with the greatest joy, ‘let’s go.’

This saying can be compared to a person who doesn’t like working. This person likes to eat without working for what he/she eats. People can ridicule him/her as someone who laughs whenever he/she sees food but feels bad whenever the question of working is mentioned (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 60). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

The saying teaches people to stop negligence and, instead, increase the effort to carry out their responsibilities so that they can achieve more in their lives.

The Sukuma people tend to hate negligence. God also hates negligence manifested in, for example, not farming, not praying, not attending Sunday church services, not diligently serving God, etc. We must not be people who are ruled by a desire for food or alcohol. Life is not just food, but more than food. Everyone has a need to eat food. May we be hungry to receive Our Lord Jesus Christ in the sacrament of the Eucharist. We need to eat the Lord’s Supper. Have joy while we’re at his banquet (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 60-61).

Genesis 25:34. Hebrews 12:16. 2Thessalonians 3:10. Romans 4:17. Proverbs 28:19.

689. NG’HWI NINGI JIGANGALUCHAGA.

Ulusumo lunulo, lufumilile kulilomelele lya bhazugi bhahanimo nhebhe. Uumo obho agabhawila abhiye, ‘dujagi dugasene ng’hwi kunguno unimo gunuyu gulintale noyi.’ Umo obhiye ashosha, ‘jilihoyi ijo denhile iyigolo.’ Uweyi agayomba, ‘ijinijo jigushila hayo ijiliwa jidinapya. Igelelilwe dujijile ng’hwi ningi ijo jidulile gubhachiwa mpaga jujibisha ijiliwa ja ha nimo gunuyo.’

Bhagizunilija bhugenha ng’wi ningi ijo bhagajizugula mpaga bhujibisha ijiliwa ija ha nimo gobho gunuyo. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘ng’hwi ningi jigangaluchaga.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhali ni nikoye ilo bhalihaya bhalyinje umuwikaji bhobho. Abhanhu bhenabho, bhagatumilaga nzila ningi ijo jigikolanijiyagwa na ng’hwi ningi, ijagudula gujibisha ijiliwa jabho. Ugwangalucha go bhujiku ing’hwi jigubhakaga, yilingisilile gutumila nguzu na nzila ningi, ijagudula gulimala ilikoye linilo.

Abhanhu bhenabho, bhagatumilaga nzila ningi ijagudula dulyinja ilikoye ilya bhusatu bho corona. Bhagabhalanjaga abhichabho ahigulya ya gulunganija kihamo inguzu nu bhumani bhobho, ijina gujidilila inzila ijo abhatalaamu bha afya bhalibhalanga. Abhoyi bhagalunganaga halumo ijina gunomba Mulungu abhambilije ugulimala wangu ilikoye linilo. Hunagwene abhanhu bhenabho, bhagayombaga giki, ‘ng’hwi ningi jigangaluchaga.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gulungana halumo ijinagujidimila inzila ijo abhadaktari bhalibhalanga, ni jingi ijo jidulile gubhingija ilikoye guti linilo, ilya bhusatu bho corona, kugiki bhadule gumala wangu, na gwikala bho mholele, umuwikaji bhobho.

KISWAHILI: KUNI NYINGI HUKESHA.

Methali hiyo, ilitokea kwenye maongezi ya wapishi wa kwenye sherehe fulani. Mmoja wao, aliwaambia wenzake, ‘twendeni tukakate kuni kwa sababu sherehe hii, ni kubwa sana.’ Mmoja wale wenazake alijibu, ‘zipo zile tulizoleta jana.’ Yeye alisema, ‘hizo zitakwisha bila kukiivisha chakula hicho. Inafaa tuendee kuni nyingi za kutosha kuwashwa mpaga kukiivisha chakula cha kwenye sherehe hiyo.’

Walikubaliana wakaenda kuleka kuni nyingi walizozipikia mpaga wakakiivisha chakula cha kwenye sherehe hiyo. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘kuni nyingi hukesha.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa watu walio na tatizo wanalotaka kulitatua katika maisha yao. Watu hao, hutumia njia nyingi ambazo hufananishwa na kuni ziwezazo kuivisha chakula chao. Kukesha usiku mzima zikiwaka kuni hizo, humaanisha kutumia nguvu na njiza nyingi kutosha kulimaliza tatizo hizo.

Watu hao, hutumia njia nyingi za kuwawezesha kujikinga na tatizo kama hilo la ugonjwa wa corona. Wao huwafundisha wenzao namna za kuungana pamoja katika kuyafuata maelekezo yanayotolewa na watalaamu wa afya. Watu hao, huunganisha nguvu zao huku wakimuomba Mungu awasaidie katika kulimaliza haraka tatizo hilo. Ndiyo maana wao huwaambia watu kwamba, ‘kuni nyingi hukesha.’

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuunganisha nguvu na ufahamu wao, katika kuyafuata maelekezo ya madaktari, na mengine mengi ambayo yanaweza kuwaondolea tatizo hilo, la ugonjwa wa corona, ili waweze kuishi kwa furaha na amani, maishani mwao.

firewood3

firewood

ENGLISH: MANY PIECES OF FIREWOOD LIGHT THE WHOLE NIGHT.

The above proverb started from a conversation of cooks at a ceremony. One of them, says to her companions, ‘let us go to cut firewood because this celebration is so big.’ One of the others replies, ‘there are some that we brought yesterday.’ The other says, ‘those ones will get finished before the food is ready, we have to increase enough firewoods to cook nice meal for this ceremony.’

They agreed and went to pick up as many  fire woods as they can, which they used for cooking nice food for the ceremony. That is why people say that, ‘many fire-woods keep up burning for the whole night.’

This proverb is compared to people who have a problem that they want to solve in their lives. These people use a variety of ways in solving it, which are compared to many fire woods that spend the whole night burning. Keeping up all night burning the wood, means spending enough energy and knowledge in getting rid of their problems.

These people,  help others in using many ways for protecting themselves from various problems including the corona epidemic. They teach their fellows on how to get together  their strenghs enough to follow the instructions which have been provided to them by health professionals.

These people unite their efforts in using their talents as well as asking God for help in resolving  quickly the pandemic. That is why they tell people that, ‘many fire-woods keep up burning for the whole night.’

The proverb imparts in people an idea about putting together their efforts and understandings, for following doctors’ instructions, and many other ways that can remove the problem of corona virus, so that they can live happily and peacefully, in their lives.

688. MASHIGA NILI, NULU, MAHIGA NILI.

Ulusumo lunulo, lwandija kumahoya ga bhanhu bhabhili ayo gahoyela mashiga. Uumo agamuuja ung’wiye, ‘amashiga ni kiyi?” Ung’wiye aganshokeja aliyomba, ‘amashiga gali mawe, nulu, madafari adatu ayo gagatumilagwa gujidimila ijisema ija guzugila ahaliko. Ahasi yago, gugabhachiyagwa moto umung’hwi ijo jigasolelagwa moyi. Umoto gunuyo gugagasebhyaga amashiga genayo.

Aliyo lulu, amashiga genayo gagabhizaga manilizu, ulugudubhachiyagwa umoto. Hunagwene abhanhu, ulu bhubhona kaya iduzugaga jiliwa, bhagayombaga giki, ‘mashiga nili, nulu, mahida nili.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa ku kaya iyo idabokelaga chiza abhageni na kubhalisha jiliwa, kunguno abhahenaho, bhadina bhutogwa, nulu, ikaya yiniyo idina jiliwa.

Amashiga ayo gali mawe adatu gagatumamilagwa gudima nungu, nulu fulila, aha liko, gagikalaga manilizu kunguno bhadazugaga ijiliwa ahakaya yiniyo. Hunagwene abhanhu, bhagayiwilaga ikaya yiniyo giki, mashiga nili, nulu, mahiga nili. Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa bho 58.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na wizang’holo bho gubhakaribhusha abhageni aha kaya jabho, kugiki bhadule gujipandika imbango ijo jigigelaga kunguno ya gubhagola chiza abhanhu bhenabho, umuwikaji bhobho.

“Ugubhakaribhusha abhageni bho wizang’holo umu kaya jise, guli nimo gwize ayise abho duganhondejaga Yesu Kristo. Ishibhi idigwita yabhubhi duhu, aliyo hangi nu kuleka gubhitila yawiza abhigisu, guleka uguitumama imilimo yise, na guleka gubhadilila abho bhali na makoye gabho. Ukuhani nu Nawi bhadang’witilile yabhubhi uyo oliotulwa na manyami, aliyo bhagamitilia bho nhudu ugundilila. Bhaditile lyose lyose. Lolaga Kueneza Injili Kwa Methali, bhukurasa, 58.

Mambo ya Walawi 19:34.

Luka 10:31-33.

Waroma 15:7.

Waebrania 13:2.

Mwanzo 18:1-8.

1Wafalme 17:10-16.

Mathayo 25:31-46.

KISWAHILI: MAFIGA BARIDI.

Methali hiyo ilianzia kwenye maongezi ya watu wawili juu ya kazi ya mafika. Mmoja alimuuliza mwenzake, ‘mafiga ni nini?’ Mwenzake alimjibu akisema, ‘mafiga ni mawawe, au matofari matatu yanayotumika katika kushikilia chombo cha kupikia. Chini ya mafiga hayo huwekwa kuni ambazo huwashwa moto unaoleta joto kwenye mafiga hayo. Mafiga hayo huwa baridi kama watu hawapiki chakula.’ Ndiyo maana watu kama wakiona chakula hakipikwi kwenye familia fulani, husema, ‘mafiga baridi.’

Methali hiyo hulinganishwa kwenye familia au kaya ile ambayo haipokei vizuri wageni na kuwalisha chakula, kwa kuwa hawana mapendo au kaya hiyo haina chakula.

Mafiga ambayo ni mawe matatu yatumikayo kutelekea chungu au sufuria jikoni, hukaa baridi kwa sababu hawapiki chakula. Ndiyo maana watu huiambia familia hiyo kwamba, ‘mafiga baridi.’ Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 58.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuwa na ukarimu wa kuwakaribisha wageni katika familia zao, ili waweze kupata Baraka zitokanazo na kuwatunza watu hao, katika maisha yao.

 “Kuwakaribisha wageni kwa ukarimu kwenye kaya zetu ni wajibu wetu sisi tunaomfuata Yesu Kristo. Dhambi sio kutenda mabaya tu, bali pia ni kutowatendea mema wenzetu, kutotimiza wajibu wetu, na kutohusika na shida zao. Kuhani na Mlawi hawakumtendea vibaya yule aliyepigwa na majambazi, bali walipita bila kujali. Hawakutenda lo lote.” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 58.

Mambo ya Walawi 19:34. “Mgeni anayeishi pamoja nawe ni lazima umtendee kama mmoja wa wazawa wa nchi yako. Mpende kama unavyojipenda mwenyewe, kwa maana ulikuwa mgeni katika nchi ya Misri. Mimi ndimi BWANA Mungu wako.”

Luka 10:31-33. “Kwa bahati nzuri kuhani mmoja alikuwa anapitia njia ile, alipomwona huyo mtu, akapita upande mwingine wa barabara, akamwacha hapo hapo. Vivyo hivyo Mlawi mmoja naye alipofika mahali pale, alimwona, akapita upande mwingine wa barabara, akamwcha hapo hapo. ‘‘Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa akisafiri kupitia njia hiyo alipomwona, alimhurumia,”

Waroma 15:7. “Karibishaneni ninyi kwa ninyi kama Kristo alivyowakaribisha ninyi ili kumletea Mungu utukufu.”

Waebrania 13:2. “Msisahau kuwakaribisha wageni, kwa kuwa kwa kufanya hivyo, watu wengine waliwakaribisha malaika pasipo kujua.”

Mwanzo 18:1-8. “BWANA akamtokea Abrahamu karibu na mialoni ya Mamre wakati alipokuwa ameketi kwenye ingilio la hema lake wakati wa adhuhuri. Abrahamu akainua macho akaona watu watatu wamesimama karibu naye. Alipowaona, aliharakisha kutoka kwenye ingilio la hema lake kuwalaki na kuwasujudia hadi nchi.  Akasema, “Kama nimepata kibali machoni penu, ee bwana wangu, usimpite mtumishi wako. Acha yaletwe maji kidogo, kisha ninyi  nyote mnawe miguu yenu na mpumzike chini ya mti huu. Niruhusuni niwapatie chakula kidogo mle, ili mpate nguvu mwendelee na safari yenu, kwa kuwa mmekuja kwa mtumishi wenu.’’ Nao wakamjibu, “Vema sana, fanya kama unavyosema.’’

 Hivyo Abrahamu akaharakisha akaingia hemani kwa Sara. Akasema, “Chukua vipimo vitatu vya unga laini haraka, ukande na uoke mikate.”   Kisha akakimbia kwenda kwenye kundi  akachagua ndama mzuri, laini na akampa mtumishi, ambaye aliharakisha kumtayarisha. Kisha akaleta jibini, maziwa na nyama ya yule ndama iliyoandaliwa, akaviweka mbele ya wageni. Walipokuwa wakila, alisimama karibu nao chini ya mti.”

1Wafalme 17:10-16. “Hivyo akaenda Sarepta. Alipofika kwenye lango la mji, mjane alikuwa huko akiokota kuni. Akamwita na kumwomba, “Naomba uniletee maji kidogo kwenye gudulia ili niweze kunywa.’’ Alipokuwa anakwenda kumletea, akamwita akasema, “Tafadhali niletee pia kipande cha mkate.” Akamjibu, ‘Hakika kama BWANA wako aishivyo, sina mkate wo wote, isipokuwa konzi ya unga kwenye gudulia na mafuta kidogo kwenye chupa. Ninakusanya kuni chache nipeleke nyumbani na nikapike chakula kwa ajili yangu na mwanangu, ili kwamba tule kiishe tukafe.’’ Eliya akamwambia, “Usiogope. Nenda nyumbani ukafanye kama ulivyosema. Lakini kwanza unifanyizie mimi mkate mdogo kutoka vile ulivyonavyo kisha uniletee na ndipo utayarishe cho chote kwa ajili yako na mwanao. Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo BWANA, Mungu wa Israeli: “Lile gudulia la unga halitakwisha wala ile chupa ya mafuta haitakauka hadi siku ile BWANA atakapoleta mvua juu ya nchi.’’ Akaondoka na kufanya kama Eliya alivyomwambia. Kwa hiyo kukawa na chakula kila siku kwa ajili ya Eliya, yule mwanamke na jamaa yake. Kwa kuwa lile gudulia la unga halikwisha na ile chupa ya mafuta haikukauka, sawasawa na lile neno la BWANA alilosema Eliya.  ”

Mathayo 25:31-46. Hukumu ya mwisho. “Mwana wa Adamu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote watakatifu pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti cha enzi cha utukufu wake. Mataifa yote watakusanyika mbele zake, naye atawatenga kama mchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi. Atawaweka kondoo upande wake wa kuume na mbuzi upande wake wa kushoto.

“Ndipo Mfalme atawaambia wale walioko upande wake wa kuume, ‘Njoni, ninyi mliobarikiwa na Baba yangu, urithini Ufalme ulioandaliwa kwa ajili yenu tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Kwa maana nilikuwa na njaa mkanipa chakula, nilikuwa na kiu mkaninywesha, nilikuwa mgeni mkanikaribisha, nilikuwa uchi mkanivika, nilikuwa mgonjwa mkanitunza, nami nilikuwa kifungoni mkaja kunitembelea.’

“Ndipo wale wenye haki watakapomjibu wakisema, ‘Bwana, ni lini tulikuona una njaa tukakulisha au ukiwa na kiu tukakunywesha? Lini tulikuona ukiwa mgeni tukakukaribisha au ukiwa uchi tukakuvika? Tena ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa tukakutunza au ukiwa kifungoni tukakutembelea?’ 

“Naye Mfalme atawajibu, ‘Amin, amin ninawaambia, kwa jinsi mlimvyotendea mmojawapo wa hawa ndugu Zangu walio wadogo, mlinitendea Mimi.’ “Kisha atawaambia wale walio upande Wake wa kushoto, ‘Ondokeni kwangu, ninyi mliolaaniwa, nendeni kwenye moto wa milele alioandaliwa kwa ajili ya ibilisi na malaika zake. Kwa maana nilikuwa na njaa hamkunipa chakula, nilikuwa na kiu hamkuninywesha, nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha, nilikuwa uchi hamkunivika, nilikuwa mgonjwa hamkunitunza na nilikuwa gerezani nanyi hamkuja kunitembelea.’

“Ndipo wao pia watajibu, ‘Bwana ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, au ukiwa mgeni au uchi , au ukiwa mgonjwa na kifungoni na hatukukuhudumia?’ “Naye atawajibu, ‘Amin, amin nawaambia, kwa jinsi ambavyo hamkumtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, hamkunitendea mimi.’ “Ndipo hawa watakapoingia kwenye  adhabu ya milele, lakini wale wenye haki wataingia katika uzima wa milele.’’”

cooking-pot-

cooking

cooking1

ENGLISH: COLD THREE COOKING STONES.

 The proverb started in a two-person conversation about the work of the three cooking stones. One asked the other, ‘What are the three cooking stones?’  The other answered, ‘these are the three stones, or bricks which are used in holding the cooking tool.’

The cooking pot sits on those three stones in the traditional African fireplace. These three cooking stones of equal size and placement easily support the clay or metal cooking pot. They are positioned very carefully. 

Underneath or between them firewoods are put, which are set on fire. The three stones need each other; they work together. If one takes away one stone and the pot falls down. They however, get cold if people don’t cook food. That’s why when people discover that food is not cooked at a particular family, they say, ‘cold three cooking stones.’

The balance between their standing close together yet apart is a symbol of community life. This is one the Sukuma Proverb that is used to teach about the values of unity, community and working together.

It is found in the Small Christian Communities (SCCs) Book: During a SCC Workshop a very effective teaching on of unity and working together is to demonstrate African proverb.

It has the following teachings:

  1.   A creative way of teaching the importance of SCCs is to describe the three cooking stones on which SCCs are “cooked” as spiritual values, acts of mercy, and concrete projects.
  2.   The metaphor of the one cooking pot and three stones can be used in different ways to describe the Catholic Church.  That is, one church but three parts: priests, religious and laity.
  3.   The image of the cooking pot and the three stones is an important analogy for the Trinity: that is one God and three Divine Persons, namely Father, Son and the Holy Spirit.
  4.   A Sukuma, Tanzania proverb:  The three stones that support the cooking pot are cold (literally mafiga baridi in Swahili) means that there is no fire and thus no food is being cooked, which is a sign of the lack of hospitality, welcome and love. 

The cold stones are a sign of the lack of good relationships within the home itself and with people living outside. Three-cooking stones used for holding a pot or kitchen pan, stay cool because they do not cook food. That is why people tell such family, ‘cold three cooking stones.’ Refer to ‘Kueneza Injili kwa Methali’; which can be literally translated as ‘Spreading the Gospel through Proverbs, page 58.

Such book was written by researchers who are: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Joseph Healey M.M., published by Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

The proverb teaches people about generosity of welcoming strangers into their families, so that they can receive the blessings that come from caring for them, in their lives.

 “The generous hospitality of our families is the responsibility of those who follow Jesus Christ. Sin is not only doing wrong, but also not doing good to others, not fulfilling our obligations, and not dealing with their problems. The priest and the Levite did not harm the victim, but they passed away regardless. They did nothing. ” Refer to “Kueneza Injili kwa Methali” which means, ‘Spreading the Gospel through Proverbs’, page 58.

Leviticus 19:34.

Luke 10: 31-33.

Romans 15: 7.

Hebrews 13: 2.

Genesis 18: 1-8.

1Kings 17: 10-16.

Matthew 25: 31-46.