Kashinje Zacharia

420. UNENE NABHIZILE NTONGEJI O LUGENDO.

Imbuki ya lusumo lunulo yingilile kubhushikanu bho ng’wa munhu. Ubhushikanu bhunubho bhuli bho gubhatongela abhanhu.

Ubhutongeji bhunubho bhudulile gubhiza bho gulekelwa na bhanhu abho bhali bhatongeji, nulu bhogushila gucha abhantongeji, usaga weyi uyo alintali, umuchalo jinijo. Hunagwene umunhu ng’wunuyo agayombaga giki, ‘unene nabhizile ntongeji o lugendo.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo aimanile chiza imilimo yakwe iyagubhatongela abhanhu bhakwe bhenabho.

Umunhu ng’wunuyo alintongeji o bhanhu uyo agabhatongelaga bhobhutogwa bhutale. Uweyi agabhalangaga abhanhu bhakwe inzila ja gubhatumamila bho bhutogwa abhichabho. Hunagwene umunhu ng’wunuyo agayombaga giki, ‘unene nabhizile ntongeji o lugendo.’

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya gujimana inzila ja gubhatongela abhanhu bhabho bho bhutogwa bhutale, kugiki bhadule gwikala bho mholele, umuwikaji bhobho.

Matendo ya mitume 2: 14-22.

KISWAHILI: MIMI NIMEKUWA KIONGOZI WA SAFARI.

Chanzo cha methali hiyo chatokea kwenye ukomavu wa mtu katika makuzi yake. Ukomavu huo ni wa kuongoza watu kuyafikia malengo fulani.

Uongozi huo waweza kuwa wa kurithi, au wa kutokana na kufa kwa viongozi wote, akabaki yeye peke yake, ambaye ni mkubwa katika kijiji hicho. Ndiyo maana mtu huyo husema kwamba, ‘mimi nimekuwa kiongozi wa safari.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu yule ambaye anaelewa vizuri wajibu wake wa kuwaongoza wananchi wake. Mtu huyo ni kiongozi wa watu, ambaye huwaongoza watu kwa upendo mkubwa.

Yeye huwafundisha pia watu wake njia za kuwaongoza wenzao kwa upendo huo. Ndiyo maana mtu huyo husema kwamba, ‘mimi nimekuwa kiongozi wa safari.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuzielewa njia za kuwaongoza watu wao kwa upendo mkubwa, ili waweze kuishi kwa amani, maishani mwao.

Matendo ya mitume 2: 14-22.

people-leader

ENGLISH: I HAVE BEEN A LEADER OF THE JOURNEY.

The source of the above saying comes from one’s ability to demonstrate his/her capacity to lead others. His/her capacity is gauged based on how he/she can lead others to attain their desired goals in life. This leadership position can be through inheritance (after the death of the former leader) or by appointment. Such a person, after succeeding to lead his/her people in the right direction, he/she can say ‘I have been a leader of the journey.’

This saying can be compared to a person who understands his/her responsibilities to his/her citizens; leading people to the right direction. Such a leader leads his/her people with love and humility. He/she also teaches others how lead in a manner that can make them be loved by others as well.

The proverb teaches people to understand the ways of leading their people with great love. This will help them to have peace and love all the time.

Acts 2: 14-22.

 

419. BHANABHANE NAMTONGE KUNTI KULUGULU NG’WITUMBI GUGAPYAGA MANG’OMBE.

Imbuki ya lusumo lunulo yingilile kumahoya ga namhala na bhana bhakwe. Unamhala ng’wunuyo obhalomelaga abhana bhakwe higulya ya gubhatongela kulugulu, ukunti go gupandikila jikolo.

Unti gunuyo ilimbisila ya gwikala chiza na bhanhu. Uwikaji bhunubho bhuli bho gwilanga gutumama milimo na bhukamu bhatale. Hunagwene unamhala ng’wunuyo agayombaga giki, ‘bhana bhane namtonge kunti kulugulu ng’witumbi gugapyaga mang’ombe.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kubhabyaji abho bhagabhalanga bhana bhabho gwikala chiza na bhanhu, bho gutumama milimo na bhukamu bhutale.

Abhabyaji bhenabho, bhajidebhile inzila ja gujipandikila isabho, bho gutumama milimo ya bhuli lushugu. Hunagwene bhagabhawilaga abhana bhabho giki, ‘bhana bhane namtonge kunti kulugulu ng’witumbi gugapyaga mang’ombe.’

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya gubhalekela abhanhu bhabho, ilange lya gutumama milimo bho bhukamu bhutale, kugiki bhadule gupandika sabho ja gubhambilija umuwikaji bhobho.

Yohane 13:1-11.

KISWAHILI: WANANGU TWENDENI KWENYE MTI MLIMANI NG’WITUMBI UZAAO NG’OMBE.

Chanzo cha methali hiyo chatokea kwenye maongezi ya mzee na watoto wake. Mzee huyo alikuwa akiwasilimulia watoto wake hao juu ya kuwaongoza kwenye mti mlimani wa kupatia mali.

Mti huo ni fumbo la kuishi na watu vizuri. Maisha hayo ni ya kujifunza kufanya kazi kwa bidii kubwa. Ndiyo maana mzee huyo huwaambia watoto wake kwamba, ‘Wanangu twendeni kwenye mti mlimani uzaao ng’ombe.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa wazazi wale ambao huwafundisha watoto wao juu ya kuishi vizuri na watu. Maisha hayo ni kufanya kazi kwa bidii kubwa.

Wazazi hao wanazifahamu njia za kupatia mali kwa kufanya kazi za kila siku. Ndiyo maana wazazi hao huwaambia watoto wao kwamba, ‘wanangu twendeni kwenye mti mlimani uzaao ng’ombe.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuwaachia watu wao malezi ya kufanya kazi kwa bidii kubwa, ili waweze kupata mali za kuweza kuwasaidia, maishani mwao.

Yohane 13:1-11.

massai-tanzania

 

ENGLISH: MY CHILDREN LET ME LEAD YOU TO THE TREE THAT BEARS CATTLE IN THE MOUNTAIN.

The source of the above saying comes from the conversation between an old man and his children. The old man tells his children to go with him to the tree located in the mountain where they can get cows. The mountain tree is believed to be bearing cows.

The saying can be compared to those parents who teach their children how to live well. They encourage their children to be hard workers so that they can have good life in future. As a way to lead them to future better life, parents could use the saying ‘my children, ‘let me lead you to the tree that bears cattle in the Mountain.’

The proverb teaches people about working hard. Parents have to guide their children to walk the path of success.

John 13: 1-11.

418. IHAHA UBHUJIKU BHOLYAGA GUDULU.

Imbuki ya lusumo lunulo yilolile bhujiku ubho bhomalaga gulya gudulu. Ubhujiku bhunubho bhuli bho gupinihaja, kunguno ya gwigela mhayo uyo guli ntale, umuchalo jilebhe.

Umhayo gunuyo gugakumukaga noyi umuchalo ijo gwigelelaga, kunguno guli gugeni. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘ihaha ubhujiku bholyaga gudulu.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kubhanhu bha muchalo ijo jabhipaga, kunguno ya gwigela mhayo ntale, guti go gucha munhu uyo akumukile, umuchalo jinijo. Abhanhu bhenabho bhagapinihalaga kunguno ya kuchilwa nu munhu ng’wunuyo, uyo aliowiza ukubhananzengo bhiye. Hunagwene abhanhu bhenabho bhagayombaga giki, ‘ihaha ubhujiku bholyaga gudulu.’

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya gubhitila ya wiza abhanhu na guilunguja halumo, umulikanza lya mayange.

Ufunuo 14:13.

KISWAHILI: SASA USIKU UMEKULA GUDULU (SASA USIKU NI MBAYA).

Chanzo cha methali hiyo chaangalia usiku ule uliokula gudulu. Maana yake huo ni usiku mbaya. Usiku huo ni wa kusikitisha kwa sababu ya kutokea kwa tukio ambalo ni kubwa kwenye kijiji fulani.

Tukio hilo laweza kuwa la kushangaza kwa sababu ni tukio geni katika maeneo hayo. Ndiyo maana watu husema kwamba ‘sasa usiku umekula gudulu.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa watu wale ambao kijiji chao kimepata msiba wa kufiwa na kiongozi aliyesifika sana. Tukio hilo ni kubwa katika kijiji hicho. Watu hao husikitika kwa sababu kiongozi huyo alikuwa anawaongaza watu kwa upendo. Ndiyo maana watu hao husema kwamba, ‘sasa usiku umekula gudulu, maana yake usiku umekuwa mbaya.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuwatendea mema watu wao, na kufarijiana pamoja wakati wa misiba, maishani mwao.

Ufunuo 14:13.

night one

night2

 

ENGLISH: NOW THE NIGHT HAS BEEN BAD.

The source of the above saying is the night that ruined the life of people in a certain village. In that night, a certain sad event happened. In commemorating that night, people can say ‘the night has been bad.’

The saying can be compared to villages that happened to experience some traumatic events such as losing some important figures (for example, well-known leaders) which can shock the entire village. Villagers can be saddened by the event and, in summarizing the night that their beloved leader passed on, they can use the saying that ‘the night was bad.’

The proverb teaches people to do good to their people. They need to comfort each other during disasters in order to have a happy life all the time.

Revelation 14:13.

417. UBHUYEGI BHO WINGA BHUGALUKA GUBIZA JIGANO.

Imbuki ya kahayile kenako yingilile kubhanhu abho bhalihawinga. Ulu gwigela mhayo go gukamaja hoyi, guti ntolwa guja gujilekeleja na ugapulwa na ngosha ungi, ubhuyegi bhugashilaga. Hunagwene abhanhu bhagayomgaga giki, ‘ubhuyegi bho winga bhugaluka gubhiza jigano.’

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agayegaga ogita na mihayo ya soni, umuwikaji bhokwe. Umunhu ng’wunuyo adulile nulu gulya jiliwa wiguta mpaga wandya gubhasondagula abhanhu bhakwe. Hunagwene abhanhu bhenabho bhagayomgaga giki ‘ubhuyegi bho winga bhugaluka gubhiza jigano.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya kuleka gwita mihayo ya guponda soni abhanhu, umuwikaji bhobho, kugiki bhadule gwikala na bhuyegi bhobho, shigu jose.

Matendo ya mitume 9:1-9.

KISWAHILI: FURAHA YA HARUSI IMEGEUKA KUWA HADITHI.

Chanzo cha msemo huo chatokea kwa watu walioko kwenye sherehe ya harusi.  Likitokea tukio la kushangaza, kama vile bibi harusi kwenda kujisaidia na kutoroshwa na mwanaume mwingine, furaha yile waliyokuwa nayo watu huisha. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘furaha ya harusi imegeuka kuwa hadithi.’

Msemo huo hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hufurahi mpaka kufikia hatua ya kufanya vitendo vya aibu mbele ya watu aishio nao.

Mtu huyo aweza hata kula chakula akashiba na kuanza kuwasimanga watu wake. Ndiyo maana watu hao husema kwamba, ‘furaha ya harusi imegeuka kuwa hadithi.’

Msemo huo hufundisha watu juu ya kuacha kusema maneno ya kuwaibisha watu, maishani mwao, ili waweze kuishi kwa furaha na wenzao siku zote.

Matendo ya mitume 9:1-9.

active couple

escape

 

ENGLISH: THE WEDDING HAPPINESS HAS TURNED INTO A STORY.

The source of the above saying comes from the wedding ceremony. During wedding ceremony we expect most of the people to be in a jovial mood. But, it may happen that the bride leaves the stage for a short call then instead elopes for another man thus causing the entire ceremony turn into a traumatic story. When it happens so, people can say ‘the wedding happiness has turned into a story.’

This saying can be compared to a person who enjoys something to the point of committing acts of shame in the eyes of other people around that place. This person, because of extreme joy, may overfeed thus, instead of making people continue enjoying the event they end up getting a new and tragic story of someone who suffers from overfeeding.

The saying teaches people to stop making derogatory remarks. This will enable them to have good life people around them.

Acts 9: 1-9.

416. ILAMBO LYAKAMA.

Imbuki ya kahayile kenako yingilile kubhukami bho lilambo. Ubhukami bhunubho bhugenhega maluho ukujisumva ijo jigikalaga umu lilambo linilo.

Ijisumva jinijo jilikihamo na: bhudagala, ndilo, danga, ng’wina na jingi ningi, ijo jigikilaga umu lilambo linilo. Hunagwene abhanhu ulu bhugabhona amaluho ga jisumva jinijo, bhagayombaga giki, ‘ilambo lyakama.’

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kubhanhu abho bhalina nsabhi obho uyo bhang’wisanije. Abhanhu bhenabho bhangema uweyi guti bhupelelo bhobho, ulu umunhu alina makoye.

Ulu ucha unsabhi ng’wunuyo bhagagayiyagwa umunhu uogubhagunana. Abhoyi bhagabhizaga guti ni jisumva ija ng’wilambo ilo lyakama linilo, kunguno nabho bhagaluhaga noyi. Hunagwene abhanhu bhenabho bhagayombaga giki, ‘ilambo lyakama.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya guyitumama imilimo iyo bhayidulile, ulu bhaligunanwa na munhu nebhe, kugiki bhadizuluha ahikanza lyaguhayiwa uwambilijiwa bhunubho.

Luka 12:15-21.

KISWAHILI: BWAWA LIMEKAUKA.

Chanzo cha msemo huo chatokea kwenye ukaukaji wa Bwawa. Ukaukaji huo huleta mateso kwa viumbe waishio ndani ya Bwawa hilo.

Viumbe hayo ni pamoja na dagaa, samaki, vyura, na vingine vingi viishivyo kwenye Bwana hilo. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘Bwawa limekauka.’

Msemo huo hulinganishwa kwa watu wale ambao wana tajiri wanayemtegemea. Watu hao humfikiria tajiri huyo kama kimbilio lao la kuwasaidia katika kutatua shida zao.

Tajiri huyo akifa, watu hao hukosa mtu wa kuwasaidia katika matatizo yao. Wao hufanana na viumbe waliokuwepo kwenye Bwawa lililokauka, kwa sababu nao hupata mateso ya kukosa msaada maishani mwao. Ndiyo maana watu hao husema kwamba, ‘Bwawa limekauka.’

Msemo huo hufundisha watu juu ya kuzifanya kazi zile wanazoweza kwa ajili kujipatia mahitaji yao, wakati wanapata msaada fulani, ili wasihangaike watakapo ukosa msaada huo.

Luka 12:15-21.

dry pond

animal dry

 

ENGLISH: THE POOL IS DRY.

The source of the above saying comes from the dried pool that was a source of life of acquatic organisms such as frogs, fish, etc. The drying of the pool means death to these organisms.

This saying can be compared to rich people who tend to help others to make their ends meet. If it happens that the rich person dies or runs bankrupt it means that those who depend on him/her suffer miserably. That is why those people say ‘the pool is dry’ to communicate the suffering they undergo after their benefactor having either died or run bankrupt.

The saying teaches people to do their jobs they can for their own needs. They should’t depend so much on fellow human beings rather be independent. In so doing, they won’t have worries in life.

Luke 12: 15-21.