Kashinje Zacharia

683. NTEMI NYIA NA MBOZU.

Ulusumo lunulo, lwingila ku wikaji bho Ntemi o Jisuguma, uyo obhabokelaga abhanhu abho bhalemagwa na bhananzengo bhakwe. Munanzengo umo agamuja UNtemi, “ni bhuli ugabhabokelaga abhanhu abho bhali na kajile kabhi?” UNtemi aganshokeja, “unene nagalyaga na bhanhu bhose, abhawiza na bhabhubhi, kunguno abhenabho pye, bhali bhanhu bhane.” Hunagwene abhanhu bhagandya guyuyomba giki, ‘Ntemi nyia na mbozu.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhatongeji, nabho bhagabhabokelaga na gubhalisha bhanhu bha mbiga jose, bho nduhu ubhusolanya. Dugemele, umunhu uyo ali na bhusadu bho mbiji, “mbozu”, umunhu uyo ali nabhubhozu, umunhu uyo ali na nhungwa ja bhubhi, jilema, Namba (Malaya) na yingi guti yiniyo. Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa bho 44.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Abhanhu bhenabho, bhagabhalangaga abhanhu bhabho, inzila ja gubhabokela abhanhu bhose bho nduhu bhusolanya. Abhoyi bhagikolaga nu Ntemi uo Jisuguma uyo obhabokelaga pye abhanhu, kunguno nabhoyi bhagikalaga na bhanhu bhose, bhawiza  na bhabhubhi. Hunagwene abhanhu bhagandya guyuyomba giki, ‘Ntemi Nyia na Mbozu.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na wizang’holo bho gubhakaribhusha pye abhanhu bho nduhu, bhusolanya bho rangi, ikabhila nabho Lihanga.

Ahanaha Welelo bhulihoyi bhutemi bhubhili. UYesu Kristo, agayomba giki, “nali na nzala uganinha ijiliwa.’ Adayombile higulya ya bhanhu abho bhalibhitila ya bhubhi abhichabho, aliyo agayomba higulya ya bhanhu abho bhadabhadililaga nulu, bhadihoyi moyi, aliyo agayomba giki bhanhu abho bhadadililaga nulu abho bhagayombaga giki, bhadihoyi moyi, na gali makoye ukubhanhu.

Ishibhi idi gubhitila abhanhu yabhubhi duhu, aliyo ili gukija ugutimija iyo igelelilwe bhayitimije, na guyomba giki, bhadiho moyi umumakoye ga bhanhu. Dudizubhiza bhanhu abho dulichola solobho ise, aliyo ibhize solobho ya bhigisu.

Dubhize guti Ntemi Yesu Kristo, uyo agifunya kunguno ya bhigisu, nulu ng’wanishi ubhusolanya. Umuyiniyo, dugumanyika igiki, dulihoyi ng’hana UBhutemi bhotwe, duduleng’wa ahalushigu ulo Nhalikijo. Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 45.

Luka 14:13-14.

Methali 31:8-9.

Marko 10:45.

Mathayo 25:34-36.

Zaburi ya 23.

Yohane 10:11.

KISWAHILI: MTEMI HULA NA MWENYE KUOZA.

Methali hiyo, ilianzia kwenye maisha ya Mtemi wa Kisukuma aliyekuwa anawapokea watu waliokataliwa na wananchi wake. Mwananchi mmoja alimuuliza mtemi, ‘kwa nini unawapokea watu wenye tabia mbaya?’ Mtemi alijibu, ‘mimi hula na watu wote wabaya na wema, kwa sababu watu hao wote ni wangu.’ Ndiyo maana watu wakanza kusema kwamba, ‘mtemi hula na mwenye kuoza.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa viongozi na wale wanaowapokea na kuwalisha watu wa kila aina bila ubaguzi. Kwa mfano, mtu mwenye ugonjwa wa ukoma, “mbozu” yaani mtu mwenye hali ya kuoza, mtu mwenye sifa mbaya, kama vile kiwete, Malaya na kadhalika. Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 44.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Watu hao huwafundisha watu wao namna ya kuwakaribisha watu wote bila ubaguzi, kwa njia ya maisha yao. Wao wanafanana na Mtemi wa kisukuma aliyewapokea watu wote, kwa sababu nao pia huishi na watu wote, wema na wabaya. Ndiyo maana watu hao huwaambia watu kwamba, ‘Mtemi hula na mwenye kuoza.’

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na ukarimu wa kuwakaribisha watu wote bila ubaguzi. Kama ‘Mtemi wa Kisukuma”, Mungu ni Baba ambaye hana ubaguzi. Huwapenda na kuwalisha watu wote bila kujali rangi ya mtu au kabila au Taifa.

Hapa duniani kuna falme za aina mbili. Ufalme wa watu ambao wanajali au wanahusika na shida za watu. Yesu Kristo aliposema, “nilikuwa na njaa hukunipa chakula,” hakusema juu ya watu ambao wanawatendea wenzao vibaya, bali alisema juu ya watu ambao hawajali au hawahusiki na shida za watu.

Dhambi sio kuwatendea watu mabaya tu, bali ni kutotimiza wajibu wetu, kutojali na kutohusika na shida za watu. Tusiwe watu ambao tunatafuta faida yetu bali faida ya wenzetu.

Tuwe kama Mtemi Yesu Kristo aliyejitoa kwa ajili ya wenzetu, hata adui ubabuzi. Katika hili tutajulikana kwamba tumo kweli katika ufalme wake na hatutakataliwa siku ya mwisho. Rejea Kueneza Injili kwa Methali, 45.

Luka 14:13-14. “Bali ufanyapo karamu, waalike maskini, vilema na vipofu, nawe utabarikiwa kwa sababu hawa hawana uwezo wa kukulipa. Mungu atakulipa wakati wa ufufuo wa wenye haki.””

Methali 31:8-9. “Sema kwa ajili ya wale wasioweza kujisemea, kwa ajili ya haki za wote walioachwa ukiwa. Sema na uamue kwa haki, tetea haki za maskini na wahitaji.”

Marko 10:45. “Kwa kuwa hata Mwana wa Adamu hakuja kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai Wake kuwa ukombozi kwa ajili ya wengi.”

Mathayo 25:34-36. “Ndipo Mfalme atawaambia wale walioko upande wake wa kuume, ‘Njoni, ninyi mliobarikiwa na Baba yangu, urithini Ufalme ulioandaliwa kwa ajili yenu tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Kwa maana nilikuwa na njaa mkanipa chakula, nilikuwa na kiu mkaninywesha, nilikuwa mgeni mkanikaribisha, nilikuwa uchi mkanivika, nilikuwa mgonjwa mkanitunza, nami nilikuwa kifungoni mkaja kunitembelea.’”

Zaburi ya 23.1-6.  “BWANA ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu. Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, kando ya maji ya utulivu huniongoza, huihuisha nafsi yangu. Huniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. Naam, nijapopita katikati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya, kwa maana wewe upo pamoja nami, rungu yako na fimbo yako vyanifariji. Waandaa meza mbele yangu machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu,  kikombe changu kinafurika. Hakika wema na fadhili zitanifuata siku zote za maisha yangu, nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.”

Yohane 10:11. ‘‘Mimi ndimi Mchungaji Mwema. Mchungaji Mwema huutoa uhai Wake kwa ajili ya kondoo.”

king1

chief

king2

 

ENGLISH: THE CHIEF EATS WITH ALL PEOPLE.

This saying has its origin on the Sukuma chief who used to receive people who were refused by his citizens. One day, one of his citizens asked him: ‘Why do you receive even bad people?’ The chief replied, ‘I eat with all people; the bad and the good ones because they are all mine.’

This saying can be compared to leaders and those who receive and feed people of all kinds, for example, people with leprosy, lame, prostitutes, and so on (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs’, page 44). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

These people teach their fellows how to welcome all people in their lives.

This proverb teaches people about generosity of welcoming all people with impartiality. As the Sukuma chief, God is an impartial Father. People need to love and feed all people regardless of their race or ethnic or national origin.

There are two kingdoms on earth. A kingdom of people who care for or deal with people’s problems and another kingdom of people who are not concerned about people’s problem. When Jesus Christ said, “I was hungry and you did not give me food,” he was not talking about people who treat others badly, but rather about people who do not care about others or are not concerned about people’s problems.

Sin is not just doing wrong to people, but not fulfilling our responsibility, being careless and not dealing with people’s problems. We shouldn’t be the people we seek for our own benefit but the benefit of our fellow men.

Let us be like the Lord Jesus Christ who gave Himself for all. In this we shall be known that we are truly in His kingdom and will not be rejected on the last day (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 45).

Luke 14: 13-14. Proverbs 31: 8-9. Mark 10:45. Matthew 25: 34-36. Psalm 23. John 10:11.

682. KULYA N’GWA MPANGA TUKIKALAGA HA NGEGU (LUGEGU).

Ulusumo lunulo, lofumila mulyimbo lya Nhingi, Shagembe, uyo agang’wimbila nywani okwe, Nchimani:

“Unene naduduja uguleka ugung’wa uwalwa, Nchimani ng’wana o ng’wa Mulola, muna Kadoto. UMulungu adina mahoya ulu uhaya gugusola. Bhabehi ugulya ng’wa mpanga dugikala ha ngegu. Abho mtogilwe gubyaja sabho na ng’wisabhe guti ng’walagana nu Mulungu. Bhabehi! Nalimuwila, gulya ng’wa mpanga dugikalaga ha ngegu.” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 42.

 Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagatumilaga chiza ijiliwa ijo bhinhiwa nu Mulungu. Giko, abhoyi bhadebhile igiki, bhinhiwa jiliwa na Mulungu, ijo igelelilwe bhajilye haho bhatali bhapanga.

Bhalihoyi bhanhu bhamo abho bhalemile ugulya, nulu, ugujitumila isabho ijaha welelo. Abhanhu bha mbika jinijo, bhadina masala, dugemele, umunhu alina ng’ombe nyingi, aliyo abhana bhakwe na nke okwe, bhagazwalaga sagala sagala.

Hangi, bhadina bhulalo bhusoga. Ulu umo obho usada bhalemile ujinga ng’ombe bhang’wambilije. Hunagwene abho bhadebhile isolobho ya gujitumila chiza isabho jinijo, bhagabhawilaga abhanhu bhenabho, giki, ‘kulya ng’wa mpanga tukikalaga ha ngegu (lugegu).’ Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ubhukurasa bho 42.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu giki, idina solobho uguleka ugulya ijiliwa nulu, uguleka ujitumila isabho ijo bhinhiwa nu Mulungu. “Giko ugukija ugulya ijiliwa ijo dalekelwa nu Yesu Kristo, idina solobho.

UYesu Kristo ng’winikili, agadukomelejaga gulya mili gokwe na gung’wa milinga gakwe, mu Sakramenti ya Ekaristi Nhagatifu. Ulu dutali aha welelo igubhiza mhayo go nyabuli ulu dukija gulya umili gokwe nu gung’wa amilinga gakwe, iki “kulya ng’wa mpanga tukikalaga ha ngegu (lugegu).

Hangi ijililwa iji jidaliyagwa na bhanhu abho bhacha, ukwene huguhaya, abhanhu abho bhali mushibhi, ijoyi jigaliyagwa na bhanhu abho bhali na mioyo yape na guzunya…Ulu duli mushibhi igelelilwe dulumbwe ishibhi haho dutali ugubhokela Ekaristi. Ee, ugalyaga bho nduhu ugukalabha amakono?” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ubhukurasa bho 43.

Mhubiri 5:18-19.

Zaburi 128:1-2.

Mathayo 26:26-28.

Yohane 6: 52-53.

KISWAHILI: MWENYE KULA NI MTU HAI TUNAKAA UKINGONI.

Methali hiyo, imetokea kwenye wimbo wa Manju Shagembe aliyemwimbia rafiki yake Nchimani:

“Mimi siwezi kuacha kunywa pombe, Nchimani bin Mulola, wa Kadoto. Mungu hana maongezi kama akitaka kukuchukua. Jamani kula tukingalia hai, kwani, huwa tunakaa ukingoni. Mnaopenda kuzalisha mali na mtajirike kama mna mapatano na Mungu. Jamani! Nawaambieni, kula tungali hai kwani tunakaa ukingoni.” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 42.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo hulinganishwa kwa watu wanaotumia vizuri chakula ambacho wamepewa na Mungu. Hivyo, wanafahamu kwamba, wamegawiwa chakula na Mungu ambacho ni lazima wakile wakati wangali wazima.

Wako baadhi ya watu ambao hawataki kula au kutumia mali ya hapa duniani. Watu wa namna hiyo hawana akili, kwa mfano, mtu ana ng’ombe wengi, lakini watoto wake na mke wake huvaa ovyo ovyo.

Tena hawana mahali pazuri pa kulala. Ikiwa mmoja wao amepatwa na ugonjwa hataki kuuza ng’ombe amsaidie. Ndiyo maana wale wanafahamu umuhimu wa kuvitumia vizuri mali walivyo navyo, huwaambia watu hao kwamba, ‘mwenye kula ni mtu hai, tunakaa ukingoni.’ Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa, 42.

Methali hiyo, huwafundisha watu kwamba, haina maana kutokula chakula au kutokutumia mali ambazo wamepewa na Mungu. “Vile vile kutokula chakula tulichoachiwa na Yesu Kristo pia, haina maana.

Yesu Kristo mwenyewe hutuhimiza kula mwili wake na kunywa damu yake katika Sakramenti ya Ekaristi Takatifu. Ikiwa bado tupo hapa duniani litakuwa jambo la kipumbavu tusipokula mwili wake na kunywa damu yake kwa kuwa. “Mwenye kula ni mtu hai, tunakaa ukingoni.”

Tena chakula hiki hakiwezi kuliwa na watu ambao wamekufa, yaani watu ambao wamo katika hali ya dhambi, bali huliwa na watu wenye mioyo safi na imani…Ikiwa tumo katika hali ya dhambi yatupata kuungama kabla ya kupokea Ekaristi. Je, hula bila kunawa mikono?” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 43.

Mhubiri 5:18-19. “Ndipo nikatambua kwamba ni vema na sahihi kwa mtu kula na kunywa na kutosheka katika kazi yake ngumu chini ya jua katika siku chache za maisha yake Mungu alizompa, kwa maana hili ndilo fungu lake. Zaidi ya yote, Mungu anapompa mtu ye yote utajiri na milki, humwezesha kuvifurahia, kukubali fungu lake na kuwa na furaha katika kazi yake, hii ni karama ya Mungu.”

Zaburi 128:1-2. “Heri ni wale wote wamchao BWANA, waendao katika njia zake. Utakula matunda ya kazi yako, Baraka na mafanikio vitakuwa vyako.”

Mathayo 26:26-28. “Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, ‘‘Twaeni, mle, huu ndio mwili wangu.’’Kisha akachukua kikombe, akashukuru, akawapa akisema, ‘‘Kunyweni nyote katika kikombe hiki. Hii ndiyo damu yangu ya agano, ile imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.”

Yohane 6: 52-53. “Ndipo Wayahudi wakaanza kuhojiana vikali wao kwa wao wakisema, “Mtu huyu awezaje kutupatia mwili wake tuule?’’ Hivyo Yesu akawaambia, “Amini, amini, nawaambia, msipoula mwili wa Mwana wa Adamu na kuinywa damu Yake, hamna uzima ndani yenu.”

africa uganda

food5

ENGLISH: OUR DAYS TO LIVE ON EARTH ARE NUMBERED, EATING IS IMPORANT.

This saying comes from Manju Shagembe’s song who was singing to his friend Nchimani:

“I cannot stop drinking alcohol, Nchimani, Mulola’son’son, of Kadoto. God has no negotiation if He wants to take you. Eat while still alive, for we are always on the brink. You who want to produce wealth and get rich as if you have agreement with God. Hello! I tell you, “Eating is life to human being” (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 42). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

This saying can be compared to those people who make good use of the food given to them by God. Such people have food that can make them eat throughout their life on earth. This saying also can be compared to someone who has enough riches but does not spend it well for the benefit of his/her children as a result, they can end up dying poorly. In such a scenario of not spending well the riches one has, one can experience things such as failing to have a good place to sleep, and not attending well family members when have problems. That is why those who are aware of the importance of using the resources they  tell those people, ‘The days to live on earth are numbered, eating is important’ (Refer to ‘Gospel Spelling in Proverbs,’ page 42).

This saying teaches people to spend well what they have managed to get in their lives. For Christians, not eating food Jesus left us with is none sense; it makes us die a satanic death.

Jesus Christ Himself urges us to eat His flesh and drink His blood in the Sacrament of the Holy Eucharist. If we are still here on earth it would be foolish for us not to eat His body and drink His blood. “Eating is life to human being who live on the brink.”

And this food cannot be eaten by people who are dead, that is, people who are in a state of sin, but is eaten by people who have a pure heart and faith. Do you eat without washing your hands? ” (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 43).

Ecclesiastes 5:18-19  “ This is what I have observed to be good: that it is appropriate for a person to eat, to drink and to find satisfaction in their toilsome labour under the sun during the few days of life God has given him –this is their lot. Moroever, when God gives someone wealth and possessions, and the ability to enjoy them, to accept their lot be happy in their toil –this is a gift of God.”

Psalm: 128:1-2 “ Blessed are all who fear the LORD, who walk in obedience to him. You will eat the fruit of your of your labour; blessings and prosperity will be yours.”

Matthew 26:26-28 “ While they were eating Jesus took bread, and when he had given thanks, he broke it and gave it to his deciples, saying, ‘take and eat; this is my body.’ The he took a cup, and when he had given thanks, he gave it to them, saying ‘Drink from it, all of you. This is my blood of the covenant, which is poured out for many for the forgiveness of sins.”

John 6: 52-53 “ Then the Jews began to argue sharply among themselves, ‘How can this man give us his flesh to eat?’ Jesus said to them, ‘very truly I tell you, unless you eat the flesh of the son of Man and drink his blood, you have no life in you.’”

681. ISUMBI LILI MU NDA.

Ulusumo lunulo, lwingilile ku mahoya ga bhageni na bhanikili kaya yiniyo. Uumo o bhanikili kaya agabhasumbila abhageni aliyomba, ‘makaribhu ng’wigashe mumasumbi.’ Uweyi agashosha, ‘umunhu adadulile gwigasha hisumbi ulu adina bhisagilwa bho gupandika jiliwa.’ Nang’hwe agashosha, ‘guli gonghana ubho nduhu jiliwa umu nda, ugwikala hoyi idinasolobho.’ Hunagwene abhanhu bhagandya guyuyomba giki, ‘isumbi lili mu nda.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatumamaga milimo na wisagilwa bho gupandika matwajo mingi, umuwikaji bhokwe. Umunhu adadulile gwita nimo uyo gudina solobho.

Isolobho yiniyo, bhuli wisagilwa ng’wa munhu uyo alizunya gwigasha hisumbi kunguno ya kumana igiki agupandikia jiliwa. Giko lulu, umunhu ulu ugaiwa ijiliwa, ihingi, agingaga haho na haho, kunguno adalazunya ugwigasha bho nduhu gulya aho kaya yiniyo. Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ubhukurasa 40.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Umunhu ng’wunuyo agatumamaga milimo yakwe bho bhukamu ubho bhudulile gumpandikila matwajo mingi, umuwikaji bhokwe, ayo gagikolanijiyagwa na jiliwa. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘isumbi lili mu nda.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kubhiza na wizagilwa bho gubhambilija ijinagongeja bhukamu bho gutumama milimo yabho chiza, kugiki bhadule kupandika matwajo mingi, umuwikaji bhobho.

Ijina moyo, dulidakilwa gwikala wikaji bho nyazunya aise bhazunya bha ng’wa Yesu Kristo, na gunondela weyi, bho gubhiza na bhisagilwa bhutale giki dulapandika bhupanga ubho bhudashilaga.

Ulu dubhiza dudina wisagilwa bho gupandika bhupanga ubho bhudashilaga, munho ugunondela gwise UYesu Kristo, gugubhiza gudina solobho, nulu nimo go bhule duhu. Kuti numo Untume Paulo aliyombela, ‘ulu Yesu Kristo adajukile, uguzunya gwise guli bhule.’

Ulu munhu agazunya gwiyumilija gwikala hizumbi, bho gwigasha ahisumbi linilo, ali na wisagiji bho gupandika jiliwa, nayise bhazunya igelelilwe gwiyumilija, guja kwikelesia, bhuli lushugu ulo Mfungo, kunguno dumanile igiki dugulwa Jiliwa na Sebha, na gulangwa Mhayo go ng’wa Mulungu, uyo gugailishaga imioyo yise.

Aliyo uwiza bho jizunya, (guti bhutumami ukubhangi, bhugubhiza bhulihoyi bhuying’wene, na bhutumami bho nduhu gulindila gulipwa) bhuli na solobho nhale gukila ulusumo ulo Jisuguma. Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa bho 40-41,

Yohane 6: 26-27.

Luka 2:25-32.

Marko 10:29-30.

2Timotheo 4:6-8.

KISWAHILI: KITI KIMO TUMBONI.

Methali hiyo ilianzia kwenye maongozi ya watu wageni na wanafamilia. Mmoja ya wanafamilia aliwakaribisha wageni akisema, ‘karibuni mketi kwenye kiti.’ Mmoja wa wageni alijibu, ‘mtu hawezi kuketi kitini isipokuwa ana tumaini la kupata chakula.’ Yeye akajibu, ‘ni kweli kiti bila chakula kwenye tumbo hakina maana.’ Ndiyo maana watu wakaanza kusema kwamba, ‘kiti kimo tumboni.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu anayefanya kazi kwa kutumaini kupata mafanikio mengi kwenye kazi yake hiyo. Mtu hawezi kufanya kazi bila kuwa na faida. Faida hiyo ni kama matumaini ya mtu anayekubali kuketi kwenye kiti kwa sababu ya kuelewa kwamba atapata chakula.

Hivyo mtu akikosa chakula huondoka mara moja kwa sababu hatakubali kukaa bila kula kwenye familia hiyo. Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 40.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Mtu huyo hufanya kazi zake kwa bidii ya kumwezesha kupata mafanikio yanayofananishwa na chakula. Ndiyo maana watu husemwa kwamba, ‘kiti kimo tumboni.’

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na matumaini ya kumwezesha kuongeza bidii katika kuyatekeleza vizuri majukumu yao, ili waweze kupata mafanikio ya kutosha kuyandesha vizuri maisha yao.

Kiroho, tunahitaji kuishi maisha ya Kikristo na kumfuata Yesu Kristo, kwa kuwa tuna tumaini la kwamba tutatunukiwa uzima wa milele. Ikiwa hatuna tumaini la kuupata uzima huo wa milele, kumfuata Yesu Kristo hakuna maana, au ni kazi bure tu. Kama Mtakatifu Paulo aliyosema, “ikiwa Yesu Kristo hakufufuka imani yetu ni bure.”

Kama mtu aliyekubali kuvumilia kukaa kitini kuwa ana tumaini la kupata chakula, ndiyo sisi waamini yatupata kuvumilia kwenda Kanisani kila Jumapili kwa sababu tuna hakika kwamba tutakula chakula cha Bwana, na kufundishwa Neno la Mungu linalotulisha mioyo yetu.

Lakini ubora wa ukristo (kama huduma kwa wengine, kutakuwa na ubinafsi na huduma bila kutumaini malipo) unaleta maana kubwa zaidi kuliko methali hii ya Kisukuma. Rejea Kueneza Injili Kwa Methali, ukurasa 40-41.

Yohane 6: 26-27. “Yesu akawajibu, “Amini, amini nawaambia, ninyi hamnitafuti kwa kuwa mliona ishara na miujiza, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba. Msishughulikie chakula kiharibikacho, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele, ambacho Mwana wa Adamu atawapa. Yeye ndiye ambaye Mungu Baba amemtia muhuri.’”

Luka 2:25-32. “Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake. Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.

Simeoni akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria, ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake  na kumsifu Mungu, akisema: “Bwana Mungu Mwenyezi, maana macho yangu yameuona wokovu    Wako,  ulioweka tayari machoni pa watu wote, nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu Mataifa na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.””

Marko 10:29-30. “Yesu akasema, “Amini, nawaambia, hakuna mtu ye yote aliyeacha nyumba, ndugu waume, au ndugu wake, mama, baba, watoto au mashamba kwa ajili Yangu na kwa ajili ya Injili, ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu, nyumba, ndugu waume, ndugu wake, mama, baba, watoto, mashamba pamoja na mateso kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao.”

2Timotheo 4:6-8. “Kwa maana mimi sasa ni tayari kumiminwa kama sadaka ya kinywaji, nayo saa yangu ya kuondoka imetimia. Nimevipiga vita vizuri, mashindano nimeyamaliza, imani nimelinda. Sasa nimewekewa taji ya haki ambayo Bwana, mwamuzi wa haki, atanitunukia siku ile, wala si mimi tu, bali pia wote ambao wamengoja kwa shauku kuja Kwake.”

 

chair1

marriage1

marriage

ENGLISH: A SEAT WITHOUT FOOD IS NOTHING.

This saying comes from the conversation between visitors and the host family. One of the family members welcomed the guests saying, ‘welcome and have a seat’ then the visitor replied saying that ‘a seat without food is nothing.’

The saying can be compared to a person who works with hopes to gain something in his/her work. One cannot work without knowing how much will he/she going to benefit from that work. That benefit is like the prospects that can make someone agree to sit on a chair. When a visitor doesn’t see any sign of getting food, he/she can leave the house (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 40.) This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

People can work hard in order to achieve food-related successes.

This saying teaches people about how to increase their efficiency in performing their tasks. This can make them to be successful in their lives.

Spiritually, we need to live the Christian life and follow Jesus Christ, for we have the hope of being blessed with eternal life. If we have no hope of attaining that eternal life, following Jesus Christ is useless, or even futile. As St. Paul puts it, “if Jesus Christ had not risen, our faith would be in vain.”

As someone who has agreed to stay in the chair having the hope of finding food, then we believers have endured going to church every Sunday because we are confident that we will eat the Lord’s Supper, and be taught the Word of God that warms our hearts.

But the quality of Christianity (as a service to others, it is special because it is a service without hope of reward) makes much more sense than this Sukuma proverb (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 40-41)

John 6: 26-27. Luke 2: 25-32. Mark 10: 29-30. 2Timothy 4: 6-8.

680. DESHI AKALEKA JULALA.

Deshi lili lina na noni iyo ikagalyaga miswa ijo jigitanagwa kidetemela mbula. Lushigu lumo, uDeshi agaja aha jigulu aha tuzengile utujidetemela mbula tunuto.

Aho oshika hoyi, agajibhona jilifuma imoimo umulipundu. Bhuli yene iyo yafumaga, UDeshi uyitulaga munomo. Agendelea gwita giko ku likanza lilihu. Iki imiswa jigendelea gufuma duhu kulikanza lilihu, UDeshi agiguta na guduma ugujimila, nose imiswa jigaikindika gung’wiyungulila na gubhita umumiso gakwe.

UDeshi agandya guhaya, “ingaji, nose muliningilila mumiso.” Agashoka na gujileka jilifuma. Hunagwene abhanhu bhagandya guyuyomba ulu bhalya jiliwa bhiguta na gujileka, giki, ‘Deshi agaleka julala.’

Intondo yahoo, UDeshi agaja hangi, mujigulu atubhile na ukunhu alimba. “itagi kiti igolo, itagi kiti igolo.” Ahikanza lya mhindi agimbaga giki, “Mukutudisha, mukutudisha.” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 38.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagalyaga jiliwa mpaga bhiguta na guleka, umukikalile kabho. Abhanhu bhenabho, ulu bhalya mpaka bhiguta, bhagaluyombaga ulusumo lunulo guti nzila ya goyela gujilya ijijiwa jinijo, iki bhajidumaga ugujimala, giki, ‘Deshi agaleka julala.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na jipimilo ja gwiyangula gujileka ijojabhalemelaga. Hangi, lobhalanga abhanhu bhenabho, gubhiza na wizang’holo bho gubhakaribhusha abhageni na gubhalila bho gubhinha jiliwa, kugiki abhanhu bhenabho, bhadule gulya na kupandika nguzu ja gwikomeja guminza chiza, umulugendo lobho.

Igelelilwe gubhitila yawiza abhigisu. Bhuli ikanza ilo dulibhitila ya wiza abhigizu, dugung’witilaga Yesu Kristo iya wiza yiniyo. UYesu obhitilaga yawiza abhanhu, umuwikaji bhokwe.

Ijinagongeja, ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya Ng’wa Yesu uyo agabhalishaga jiliwa, ijo jili mili na mininga gakwe, umu Isakramenti lya Ekaristi Nhagatifu.

Undimi untengeke agabhalishaga abhanhu jiliwa, bho gubhalanga Mhayo go Mulungu, uyo gugabhinhaga bhupanga. UYesu Kristo, hung’wene uyo ali ‘ha ng’wa Lutubhila gule.’ Ukwene huguhaya giki, ahali Uweyi bhagatubhilaga kule. Uyo agajaga kuli Weyi adubhona inzala. Uyo alinzunya Weyi, adiigwa inota gete. Rejea Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 39.

Isaya 25:6.

Ezekekieli 34: 1-2.

Marko 6:41-44.

Yohane 10:9-10.

Yakoko 2:15-17.

Luka 10:30-37.

Mathayo 25:31-46.

KISWAHILI: DESHI ALIAKA KUMBIKUMBI WAKARUKA.

Deshi ni jina la ndege ambaye hula jamii ya kumbikumbi wadogo (kidetemela mbula). Siku moja Deshi alikwenda kwenye kuchuguu (nyumba ya kidetemela mbula).

Alipofika hapo, alikuta kumbikumbi wanatoka mmoja mmoja shimoni. Kila kilichotoka Deshi alikiweka mdomoni. Akaendelea kufanya hivi kwa muda mrefu. Kwa vile waliendelea kutoka tu kwa muda mrefu, Deshi alishiba na kushindwa kuwameza, hata wakawa wanaruka kumzunguka na kupita machoni pake.

Deshi alianza kusema, ‘Ondokeni, mwishowe mtaniingia machoni.” Alirudi na kuwaacha kumbikumbi hao, wanatoka. Ndiyo maana watu wakaanza kusema wanaposhiba chakula na kukiacha, kwamba, ‘Deshi aliacha kumbikumbi wakaruka.”

Kesho yake, Deshi alikwenda tena kwenye kichuguu akiwa na njaa akiimba. “itagi kiti igolo, itagi kiti igolo” (fanyeni kama jana, fanyeni kama jana”). Wakati wa jioni huwa anaimba hivi, “Mukutudisha, mukutudisha” (mtatuingia machoni, mtatuingia machoni”). Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 38.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hulinganishwa kwa watu waliokula chakula mpaga wakashiba na kusaza, katika maisha yao. Watu hao, wanapokula mpaka kutosheka, huisema methali hiyo kama njia ya kuacha kula chakula, kwa vile wameshindwa kukimaliza, kwamba, ‘Deshi aliacha kumbikumbi wakaruka.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuwa na kiasi katika maisha, kwa maana ya kuamua kuacha kula chakula, baada ya kutosheka. Pia huwafundisha watu hao, kuwa na ukarimu wa kuwakaribisha wageni na kuwaandalia chakula, ili wageni hao waweze kula na kupata nguzu za kuwawezesha kuendelea vizuri na safari yao.

Yatupata kuwatendea wenzetu mema. Kila tunapomtendea mwenzetu mema tunamtendea mema Yesu Kristo. Kila tunapokosa kumtendea mwenzetu mema, tunakosa kumtendea Yesu Kristo mema hayo. Yesu alikuwa mtu aliyetenda wema kwa wengine.

Zaidi ya hayo, methali hiyo, yatufundisha juu ya Yesu Kristo anayetulisha na kutushibisha chakula, yaani mwili na damu yake katika Sakramenti ya Ekaristi Takatifu.

Mchungaji mwema huwalisha watu chakula, yaani huwafundisha neno la Mungu linalowapatia watu wokovu. Yesu Kristo ndiye “lutubhila kule,” yaani kwake njaa iko mbali. Anayekwenda kwake hataona njaa. Anayemwamini Yeye hataona kiu kamwe. Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 39.

Isaya 25:6. “Na katika mlima huu Bwana wa Majeshi atawafanyia mataifa yote karamu ya vitu vinono, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, karamu ya vinono vilivyojaa mafuta, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, iliyochujwa sana.”

Ezekekieli 34: 1-2. “Neno la Bwana likanijia kusema, mwanadamu, toa unabii juu ya wachungaji wa Israeli, toa unabii, uwaambie, naam hao wachungaji Bwana Mungu asema hivi, ole wao wachungaji wa Israeli wanaojilisha wenyewe. Je, wachungaji kuwalisha kondoo?”

Marko 6:41-44. “Kisha Yesu akatwa ile mikate mitano na wale sakaki wawili akatazama juu mbinguni akamshukuru Mungu, akaimeja mikate, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu na wale samaki wawili pia. Akawagawia wote, watu wote wakala wakashiba wakaokota mabaki ya mikate na samaki pia, wakaja vikapu kumi na viwili.”

Yohane 10:9-10. “Mimi ni mlango. Anayeingia kwa kupitia kwangu ataokolewa; ataingia na kutoka, na atapata malisho.”

Yakoko 2:15-17. “Tuseme kaka au dada hana nguo au chakula. Yafaa kitu gani ninyi kuwaambia hao: Nendeni salama, mkaote moto na kushiba bila kuwapatia mahitaji yao ya maisha?”

Luka 10:30-37. “Mfano wa Msamalia Mwema.”

Mathayo 25:31-46. “Hukumu ya Mwisho.”

bird eating insects

ants1

ants

 

ENGLISH: DESHI LEFT THEM TO FLY.

Deshi is the name of a bird that feeds on flying ants. One day deshi went to the anthill where flying ants live. When it got there, it found that the flying ants were coming out of their hole. What deshi did is setting its mouth closer to the entry of the hole so that the flying ants can enter straight into deshi’s mouth. It ate the flying ants to its satisfaction. Later on, because of satisfaction, the flying ants began flying around to surround deshi and, at this time, deshi had no any appetite to continue eating them. When the flying ants were doing so, deshi told them: “Get out, and finally you will enter our eyes.” He went back and left them, and they left to their hole. That is why people, when have eaten to their satisfaction, say “deshi left them to fly.”

The next day, deshi went back to the anthill while singing: “Itagi giti igolo, itagi git igolo” (do as you did yesterday, do as you did yesterday ). While the day before, it was singing “you will enter our eyes, you will enter our eyes” (Refer to Kueneza Injili kwa Methali’ which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 38). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

This proverb can be compared to greedy people who will tend to eat food to their satisfaction and later on begin to abuse it.

The proverb also teaches people to do good to fellows. Whenever we do good to one another, we do good to Jesus Christ. Whenever we fail to do good to one another, we fail to do good to Jesus Christ. Jesus was a man who did good to others.

Further, the proverb teaches us about Jesus Christ who nourishes and satisfies us with food, that is, his flesh and blood in the Sacrament of the Holy Eucharist.

The good shepherd feeds the people, that is, teaches them the word of God for salvation. In Jesus Christ hunger is far away. Whoever goes to Him will not be hungry. He who believes in Him will never feel thirsty (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 39).

Isaiah 25: 6. Ezekiel 34: 1-2. Mark 6: 41-44. John 10: 9-10. James 2: 15-17. Luke 10: 30-37. Matthew 25: 31-46.

679. HA NG’WA LUTUBHILA KULE.

Bhalihoyi bhanhu bhabhili abho bhalimugendo lo guja halebhe,  ukunhu bhalilomela. Aliyo abhanhu bhenabho, bhalibhatuubha noyi. Uumo obho agang’wila ung’wiye, ‘dugupandikila heyi ijiliwa?’ Ung’wiye agashosha, ‘dujage aha kaya iyaho.’ Nang’hwe agashosha, ‘nahene dujage.’

Aho bhashika aha kaya yiniyo, bhagazugilwa jiliwa ijo bhagajilya mpaga bhujileka. Uumo uyomba, ‘ulu uliha kaya yiniyo, udiyigwa nzala.’ Nu ng’wiye ushosha, ‘ng’hana, kunguno aho dali kule ni kaya yiniyi, dali dutubhile noyi.’ Hunagwene abhanhu bhagandya guyuyomba ulu kaya yubhazugila jiliwa ja gulya na gujileka, giki, ‘ha ng’wa lutubhila kule.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agabhabokelaga chiza abhageni na kubhalisha jiliwa bho wizang’holo.’ Giko lulu, ulu ulinang’hwe umunhu ung’unuyo, udutubha, kunguyo uweyi ali ‘ha ng’wa lutubhila kule.’ Rejea Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa bho 38.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kubhiza na wizang’holo bho gubhakaribhusha bhageni na kubhabhegeja jiliwa, kugiki bhadule gulya na kupandika nguzu ya gusimiza mpaga gushika uko bhajile, umulugendo lobho chiza.

Igelelilwe gubhitila yawiza abhigisu. Bhuli ikanza ilo dulibhitila ya wiza abhigizu, dugung’witilaga Yesu Kristo iya wiza yiniyo. UYesu obhitilaga yawiza abhanhu, umuwikaji bhokwe.

Ijinagongeja, ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya Ng’wa Yesu uyo agabhalishaga jiliwa, ijo jili mili na mininga gakwe, umu Isakramenti lya Ekaristi Nhagatifu.

Undimi untengeke agabhalishaga abhanhu jiliwa, bho gubhalanga Mhayo go Mulungu, uyo gugabhinhaga bhupanga. UYesu Kristo, hung’wene uyo ali ‘ha ng’wa Lutubhila gule.’ Ukwene huguhaya giki, ahali Uweyi bhagatubhilaga kule. Uyo agajaga kuli Weyi adubhona inzala. Uyo alinzunya Weyi, adiigwa inota gete. Rejea Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 39.

Isaya 25:6.

Ezekekieli 34: 1-2.

Marko 6:41-44.

Yohane 10:9-10.

Yakoko 2:15-17.

Luka 10:30-37.

Mathayo 25:31-46.

KISWAHILI: KWAKE NJAA IKO MBALI.

Kulikuwa na watu wawili waliokuwa safarini kuelekea sehemu fulani. Lakini watu hao walijisikia njaa sana. Mmoja akamuuliza mwenzake, ‘tutapata wapi chakula?’ Mwenzake akajibu, twende kwenye familia ile pale.’ Naye akajibu, ‘sawa twende.’

Walipofika kwenye familia hiyo, walipikiwa chakula ambacho walikila mpaga wakatosheka na kukiacha. Mmoja akasema, ‘ukiwa kwenye familia hii, huwezi kujisikia njaa.’ Naye mwenzake akasema, ‘kweli kwa sababu tulipokuwa mbali na hapa tulijisikia njaa sana.’ Ndiyo maana watu wakaanza kusema kwenye familia ile waliokula chakula na kusaza kwamba, ‘kwake njaa iko mbali.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye anawapokea wageni na kuwalisha chakula kwa ukarimu. Hivyo ukiwa naye mtu huyo, huwezi kujisikia njaa, yaani ‘kwake nja iko mbali.’ Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 38.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuwa na ukarimu wa kuwakaribisha wageni na kuwaandalia chakula, ili wageni hao waweze kula na kupata nguzu za kuwawezesha kuendelea na safari yao vizuri.

Yatupata kuwatendea wenzetu mema. Kila tunapomtendea mwenzetu mema tunamtendea mema Yesu Kristo. Kila tunapokosa kumtendea mwenzetu mema, tunakosa kumtendea Yesu Kristo mema hayo. Yesu alikuwa mtu aliyetenda wema kwa wengine.

Zaidi ya hayo, methali hiyo, yatufundisha juu ya Yesu Kristo anayetulisha na kutushibisha chakula, yaani mwili na damu yake katika Sakramenti ya Ekaristi Takatifu.

Mchungaji mwema huwalisha watu chakula, yaani huwafundisha neno la Mungu linalowapatia watu wokovu. Yesu Kristo ndiye “lutubhila kule,” yaani kwake njaa iko mbali. Anayekwenda kwake hataona njaa. Anayemwamini Yeye hataona kiu kamwe. Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 39.

Isaya 25:6. “Na katika mlima huu Bwana wa Majeshi atawafanyia mataifa yote karamu ya vitu vinono, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, karamu ya vinono vilivyojaa mafuta, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, iliyochujwa sana.”

Ezekekieli 34: 1-2. “Neno la Bwana likanijia kusema, mwanadamu, toa unabii juu ya wachungaji wa Israeli, toa unabii, uwaambie, naam hao wachungaji Bwana Mungu asema hivi, ole wao wachungaji wa Israeli wanaojilisha wenyewe. Je, wachungaji kuwalisha kondoo?”

Marko 6:41-44. “Kisha Yesu akatwa ile mikate mitano na wale sakaki wawili akatazama juu mbinguni akamshukuru Mungu, akaimeja mikate, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu na wale samaki wawili pia. Akawagawia wote, watu wote wakala wakashiba wakaokota mabaki ya mikate na samaki pia, wakaja vikapu kumi na viwili.”

Yohane 10:9-10. “Mimi ni mlango. Anayeingia kwa kupitia kwangu ataokolewa; ataingia na kutoka, na atapata malisho.”

Yakoko 2:15-17. “Tuseme kaka au dada hana nguo au chakula. Yafaa kitu gani ninyi kuwaambia hao: Nendeni salama, mkaote moto na kushiba bila kuwapatia mahitaji yao ya maisha?”

Luka 10:30-37. “Mfano wa Msamalia Mwema.”

Mathayo 25:31-46. “Hukumu ya Mwisho.”

rich one

cow2

 

ENGLISH: IN THIS FAMILY YOU CANNOT SUFFER FROM HUNGER.

There were two people traveling to a certain place. It reached a point when these two travelers felt hungry and they were in need of food. One of them asked the other, ‘Where can we get food?’ The other replied, let’s go to the family over there. ‘ When they arrived at that particular family, they were given food and ate to their satisfaction. After eating, the travellers said that, in ‘this family you cannot suffer from hunger.’

This saying can be compared to a kind person who welcomes others during needy times. This person is generous enough to others and he/she would not like seeing others suffer because of lacking something in life (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 38). This book was written by Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

The saying teaches people about the generosity and hospitality. People have to be kind to others in their lives. When we do good to others it means we are doing good to Jesus Christ. Whenever we fail to do good to one another, we fail to do good to Jesus Christ. Jesus was a man who did good to others.

Furthermore, the saying teaches us about Jesus Christ who nourishes and satisfies us with food, that is, his flesh and blood in the Sacrament of the Holy Eucharist.

The good shepherd feeds the people, that is, teaches them the word of God for salvation. In Jesus Christ there is no hunger. Whoever goes to Him will not be hungry. He who believes in Him will never feel thirsty (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 39).

Isaiah 25: 6. Ezekiel 34: 1-2. Mark 6: 41-44. John 10: 9-10. James 2: 15-17. Luke 10: 30-37. Matthew 25: 31-46.