Ulusumo lunulo, lwingila ku wikaji bho Ntemi o Jisuguma, uyo obhabokelaga abhanhu abho bhalemagwa na bhananzengo bhakwe. Munanzengo umo agamuja UNtemi, “ni bhuli ugabhabokelaga abhanhu abho bhali na kajile kabhi?” UNtemi aganshokeja, “unene nagalyaga na bhanhu bhose, abhawiza na bhabhubhi, kunguno abhenabho pye, bhali bhanhu bhane.” Hunagwene abhanhu bhagandya guyuyomba giki, ‘Ntemi nyia na mbozu.’
Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhatongeji, nabho bhagabhabokelaga na gubhalisha bhanhu bha mbiga jose, bho nduhu ubhusolanya. Dugemele, umunhu uyo ali na bhusadu bho mbiji, “mbozu”, umunhu uyo ali nabhubhozu, umunhu uyo ali na nhungwa ja bhubhi, jilema, Namba (Malaya) na yingi guti yiniyo. Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa bho 44.
Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.
Abhanhu bhenabho, bhagabhalangaga abhanhu bhabho, inzila ja gubhabokela abhanhu bhose bho nduhu bhusolanya. Abhoyi bhagikolaga nu Ntemi uo Jisuguma uyo obhabokelaga pye abhanhu, kunguno nabhoyi bhagikalaga na bhanhu bhose, bhawiza na bhabhubhi. Hunagwene abhanhu bhagandya guyuyomba giki, ‘Ntemi Nyia na Mbozu.’
Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na wizang’holo bho gubhakaribhusha pye abhanhu bho nduhu, bhusolanya bho rangi, ikabhila nabho Lihanga.
Ahanaha Welelo bhulihoyi bhutemi bhubhili. UYesu Kristo, agayomba giki, “nali na nzala uganinha ijiliwa.’ Adayombile higulya ya bhanhu abho bhalibhitila ya bhubhi abhichabho, aliyo agayomba higulya ya bhanhu abho bhadabhadililaga nulu, bhadihoyi moyi, aliyo agayomba giki bhanhu abho bhadadililaga nulu abho bhagayombaga giki, bhadihoyi moyi, na gali makoye ukubhanhu.
Ishibhi idi gubhitila abhanhu yabhubhi duhu, aliyo ili gukija ugutimija iyo igelelilwe bhayitimije, na guyomba giki, bhadiho moyi umumakoye ga bhanhu. Dudizubhiza bhanhu abho dulichola solobho ise, aliyo ibhize solobho ya bhigisu.
Dubhize guti Ntemi Yesu Kristo, uyo agifunya kunguno ya bhigisu, nulu ng’wanishi ubhusolanya. Umuyiniyo, dugumanyika igiki, dulihoyi ng’hana UBhutemi bhotwe, duduleng’wa ahalushigu ulo Nhalikijo. Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 45.
Luka 14:13-14.
Methali 31:8-9.
Marko 10:45.
Mathayo 25:34-36.
Zaburi ya 23.
Yohane 10:11.
KISWAHILI: MTEMI HULA NA MWENYE KUOZA.
Methali hiyo, ilianzia kwenye maisha ya Mtemi wa Kisukuma aliyekuwa anawapokea watu waliokataliwa na wananchi wake. Mwananchi mmoja alimuuliza mtemi, ‘kwa nini unawapokea watu wenye tabia mbaya?’ Mtemi alijibu, ‘mimi hula na watu wote wabaya na wema, kwa sababu watu hao wote ni wangu.’ Ndiyo maana watu wakanza kusema kwamba, ‘mtemi hula na mwenye kuoza.’
Methali hiyo, hulinganishwa kwa viongozi na wale wanaowapokea na kuwalisha watu wa kila aina bila ubaguzi. Kwa mfano, mtu mwenye ugonjwa wa ukoma, “mbozu” yaani mtu mwenye hali ya kuoza, mtu mwenye sifa mbaya, kama vile kiwete, Malaya na kadhalika. Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 44.
Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.
Watu hao huwafundisha watu wao namna ya kuwakaribisha watu wote bila ubaguzi, kwa njia ya maisha yao. Wao wanafanana na Mtemi wa kisukuma aliyewapokea watu wote, kwa sababu nao pia huishi na watu wote, wema na wabaya. Ndiyo maana watu hao huwaambia watu kwamba, ‘Mtemi hula na mwenye kuoza.’
Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na ukarimu wa kuwakaribisha watu wote bila ubaguzi. Kama ‘Mtemi wa Kisukuma”, Mungu ni Baba ambaye hana ubaguzi. Huwapenda na kuwalisha watu wote bila kujali rangi ya mtu au kabila au Taifa.
Hapa duniani kuna falme za aina mbili. Ufalme wa watu ambao wanajali au wanahusika na shida za watu. Yesu Kristo aliposema, “nilikuwa na njaa hukunipa chakula,” hakusema juu ya watu ambao wanawatendea wenzao vibaya, bali alisema juu ya watu ambao hawajali au hawahusiki na shida za watu.
Dhambi sio kuwatendea watu mabaya tu, bali ni kutotimiza wajibu wetu, kutojali na kutohusika na shida za watu. Tusiwe watu ambao tunatafuta faida yetu bali faida ya wenzetu.
Tuwe kama Mtemi Yesu Kristo aliyejitoa kwa ajili ya wenzetu, hata adui ubabuzi. Katika hili tutajulikana kwamba tumo kweli katika ufalme wake na hatutakataliwa siku ya mwisho. Rejea Kueneza Injili kwa Methali, 45.
Luka 14:13-14. “Bali ufanyapo karamu, waalike maskini, vilema na vipofu, nawe utabarikiwa kwa sababu hawa hawana uwezo wa kukulipa. Mungu atakulipa wakati wa ufufuo wa wenye haki.””
Methali 31:8-9. “Sema kwa ajili ya wale wasioweza kujisemea, kwa ajili ya haki za wote walioachwa ukiwa. Sema na uamue kwa haki, tetea haki za maskini na wahitaji.”
Marko 10:45. “Kwa kuwa hata Mwana wa Adamu hakuja kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai Wake kuwa ukombozi kwa ajili ya wengi.”
Mathayo 25:34-36. “Ndipo Mfalme atawaambia wale walioko upande wake wa kuume, ‘Njoni, ninyi mliobarikiwa na Baba yangu, urithini Ufalme ulioandaliwa kwa ajili yenu tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Kwa maana nilikuwa na njaa mkanipa chakula, nilikuwa na kiu mkaninywesha, nilikuwa mgeni mkanikaribisha, nilikuwa uchi mkanivika, nilikuwa mgonjwa mkanitunza, nami nilikuwa kifungoni mkaja kunitembelea.’”
Zaburi ya 23.1-6. “BWANA ndiye mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu. Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, kando ya maji ya utulivu huniongoza, huihuisha nafsi yangu. Huniongoza katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. Naam, nijapopita katikati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya, kwa maana wewe upo pamoja nami, rungu yako na fimbo yako vyanifariji. Waandaa meza mbele yangu machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, kikombe changu kinafurika. Hakika wema na fadhili zitanifuata siku zote za maisha yangu, nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.”
Yohane 10:11. ‘‘Mimi ndimi Mchungaji Mwema. Mchungaji Mwema huutoa uhai Wake kwa ajili ya kondoo.”
ENGLISH: THE CHIEF EATS WITH ALL PEOPLE.
This saying has its origin on the Sukuma chief who used to receive people who were refused by his citizens. One day, one of his citizens asked him: ‘Why do you receive even bad people?’ The chief replied, ‘I eat with all people; the bad and the good ones because they are all mine.’
This saying can be compared to leaders and those who receive and feed people of all kinds, for example, people with leprosy, lame, prostitutes, and so on (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs’, page 44). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.
These people teach their fellows how to welcome all people in their lives.
This proverb teaches people about generosity of welcoming all people with impartiality. As the Sukuma chief, God is an impartial Father. People need to love and feed all people regardless of their race or ethnic or national origin.
There are two kingdoms on earth. A kingdom of people who care for or deal with people’s problems and another kingdom of people who are not concerned about people’s problem. When Jesus Christ said, “I was hungry and you did not give me food,” he was not talking about people who treat others badly, but rather about people who do not care about others or are not concerned about people’s problems.
Sin is not just doing wrong to people, but not fulfilling our responsibility, being careless and not dealing with people’s problems. We shouldn’t be the people we seek for our own benefit but the benefit of our fellow men.
Let us be like the Lord Jesus Christ who gave Himself for all. In this we shall be known that we are truly in His kingdom and will not be rejected on the last day (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 45).
Luke 14: 13-14. Proverbs 31: 8-9. Mark 10:45. Matthew 25: 34-36. Psalm 23. John 10:11.