Kashinje Zacharia

703. KALAGU – KIZE. NG’HINGI YA KITIMBO UT’IMIGIJA MAMILA:- USO (SHINYANGA). NG’HINGI YA KITIMBO UT’IMIGIJA MAMILA:- SO. (MWANZA).

“Itendile igiki umubhuzengi bho numba ja kale, jigabhizaga na ng’ingi ningi. Imo ya ng’inghi jilijo igayidimilaga inumba ngima iyo yili ‘ng’hingi ya kitimbo,’ umujisuguma. Ing’hingi yiniyi iya jitimbo yili ya solobho noyi ukumhola bho numba nu ukumhola ya wikaji.

Giko numu wikaji bho kaya Ubhaba umyaji ali guti ng’hingi ya kitimbo, iki alolilwe weyi nabhose. Umu kajile kise abhingi, bhagamijaga mamila na gugabhila ha ginhu jose jose ijo jidina solobho, aliyo guli ngilo ugujibhila mamila iginhu ijo jili na solobho. Yijinijo higinhu, nulu munhu umo yigelelilwe witilwe gitumo yibhelelile ni likujo lyakwe.

Ulu undharaha so nunu mayu oko ntale oseose, yili guti gumigija mamila. Ikalagu yiniyi ilidulanga kubhakuja abhatale bhise.” Lolaga Kugundua Mbegu ya Injili, ukurasa 15.

Ijitabho jinijo jigandikwa na Kamati ya Utafiti wa Utamaduni Bujora, ijojigahaririwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

“UMulungu ali ng’hingi ya kitimbo ku jisumva jose. “Iki uweyi Ng’winikili huyo agabhinhaga abhanhu ubhupanda, agabhinhaga bhudula bho gweshema na gubhinha bhuli ginhu” (Matendo 17:25).

Kuyiniyo, igelelilwe dunhamye Mulungu gitumo ihayililwe. Ulu dunbyeda Mulungu, dulimila mamila. Miito gose agabhubhi gali guti mamila.

Umushandikwa Shela duliwilwa hape giki, UYesu Kristo hi “Liwe ilisolanyiwa na lya solobho nhale” (1Petro 2:4). Ee, umu wikaji wise, nani nulu kiyi jili ng’hingi ya kitimbo nulu liwe lya munsingi?

Ee, tulizunya igiki UYesu Kristo ng’winikili ali Sebha, wandijo na ngelelo, na wandijo bho wiza bhose? Guli mhayo go gupinihaja ugubhona giki nhangala ningi dudumanaga UYesu Kristo igiki ali nsingi go wikaji wise. Dugundalahaga na kumila mamila sagala duhu bho nduhu ugundilila. Jili ginhu ja gukumya gete.”

Lolaga Kugundua Mbegu ya Injili, ukurasa 16.

Kutoka 20:12.

Mithali 9:10.

Mathayo 2:42.

1Petro 2:4-5.

Mathayo 16:18.

KISWAHILI: NGUZO KUU YA NYUMBA HAIPENGEWI KAMASI:- BABA MZAZI.

“Ni dhahiri ya kwamba katika ujenzi wa nyumba zetu za jadi, huwa na nguzo nyingi. Moja ya nguzo hizi hutegemeza nyumba nzima ndiyo nguzo kuu, yaani kwa kisukuma: “ng’ingi ya kitimbo”. Nguzo hii kuu ni muhimu sana kwa usalama wa nyumba na kwa usalama wa wakazi.

Hali kadhalika, katika maisha ya familia baba mzazi ni kama nguzo kuu, kwani hutegemewa na wote. Katika mila zetu wengi hupenga kamasi na kupakaa kwenye kitu chochote tusichokithamini, lakini ni haramu kupakaa kamasi kwenye kitu chenye thamani. Ndivyo kitu au mtu anavyopaswa kutendewa kadiri ya stahili au heshima yake.

Ukimdharau baba au mama mkubwa yeyote, ni kama kumpaka kamasi. Kitendawili hiki kinatufundisha kuwaheshimu wakubwa wetu.” Rejea Kugundua Mbegu ya Injili, ukurasa 15.

Kitabu hicho, kiliandikwa na Kamati ya Utafiti wa utamaduni Bujora, kilichohaririwa na watafiti: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

“Mungu ni nguzo kuu ya viumbe vyote. “Kwa kuwa yeye Mwenyewe ndiye anayewapa watu uhai, anawawezesha kupumua na anawapa kila kitu” (Matendo 17:25).

Kwa hiyo, yatupata kumcha Mungu kadiri ya stahili yake. Tukimdharau Mungu, tunampaka kamasi. Matendo yote mabaya ni kama kamasi.

Katika maandiko Matakatifu tunaambiwa wazi kwamba Yesu Kristo ndiye “Jiwe teule na la thamani kubwa” (Petro 2:4). Je, katika maisha yetu, nani au nini ni nguzo kuu au jiwe la msingi?

Je, tunaamini kwamba Yesu Kristo mwenyewe ndiye Bwana, mwanzo na mwisho, na chimbuko la mema yote? Ni jambo la kusikitisha kuona kwamba mara nyingi hatumtambui Yesu Kristo kuwa msingi wa maisha yetu. Tunamdharau na kumpaka kamasi ovyo tu bila kumjali. Ni jambo la ajabu kweli.” Rejea Kugundua Mbegu ya Injili, ukurasa 16.

Kutoka 20:12. “Waheshimu baba yako na mama yako, ili upate kuishi siku nyingi katika nchi anayokupa BWANA Mungu wako.”

Mithali 9:10. “Kumcha BWANA ni mwanzo wa hekima na kumjua Mtakatifu ni ufahamu.”

Mathayo 21:42. “Yesu akawaambia, “Je, hamjasoma katika maandiko kwamba:  “Lile jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni, Bwana ndiye aliyefanya jambo hili, nalo ni la ajabu machoni petu?’”

1Petro 2:4-5. “Mwendeeni Yeye aliye Jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu bali kwa Mungu ni teule na la thamani Kwake. Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa kuwa nyumba ya Roho, mpate kuwa ukuhani mtakatifu, mkitoa dhabihu za kiroho zinazokubaliwa na Mungu kwa njia ya Yesu Kristo”

Mathayo 16:18. “Nami nakuambia, wewe ndiwe Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu, hata malango ya kuzimu hayataweza kulishinda.”

posit

father-son

village

 

ENGLISH: I HAVE A RIDDLE- LET COME, THE CENTRAL POLE OF THE HOUSE IS NOT SMEARD WITH MUCUS: FATHER.

In the construction of traditional houses, there are many poles but one of them is considered central; the main pole. This central pole is very important in the life of the whole house.

Likewise, in the family the father is the central pole of the family. The whole family depends on him. It is uncultured if someone can smear his/her mucus on something of great value. If one can do so then he/she is regarded as someone who doesn’t respect himself/herself and others as well.

Similarly, if someone can despise his/her father then it is like smearing mucus on him. This riddle teaches people to respect their parents (Refer to Kugundua Mbegu za Injili, which means, ‘Discovering the Seed of the Gospel,’ page 15). This book was written by the Bujora Cultural Research Committee, edited by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1993.

“God is the ultimate pillar of all creations. “For He Himself gives to men life, allow them to breath and give them everything ” (Acts 17:25).

Thus, we have to fear God. If we disrespect God, we rub Him mucus. All bad deeds are like mucus.

In the Holy Scriptures we are clearly told that Jesus Christ is the “chosen and precious stone” (1Peter 2: 4). In our life, who or what is the main pole or cornerstone?

Do we believe that Jesus Christ Himself is Lord, beginning and end, and the source of all good? It is sad to see that we often do not recognize Jesus Christ as the foundation of our lives. We despise Him and rub Him with the mucus without care. It’s really astonishing (See ‘Discovering the Gospel Seed,’ page 16).

Exodus 20:12. Proverbs 9:10. Matthew 2:42. 1 Peter 2: 4-5. Matthew 16:18.

702. MPANGA WA KUSHA NA KWANZULA.

Ulusumo lunulo lwandija kuli munhu uyo wiyumilijaga gutumama nimo go gusha mpaga ugumala. Dugemele: umayu uyo alushaga bhusiga adulile guguleka unimo gokwe, kunguno ndebhe na ubhutula ubhusiga hanhelo, “kwanzula”. Aliyo agwiza agumalije.

Ulusumo lunulo lugatumilagwa kuli munhu uyo ali na wiyumilija umumilimo. Umunhu umpanga, uyo adinsadu, adadulile uguguleka unimo go gusha na guguleka sagala. Aliyo agiyumilijaga mpaga gushile.” Hunagwene abhanhu bhagang’witanaga giki, ‘mpanga wa kusha na kwangula.’ Lolaga kugundua mbegu ya Injili, ukurasa 12-13.

Ijitabho jinijo jigandikwa na Kamati ya Utafiti wa Utamaduni Bujora, ijojigahaririwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gutumama milimo mpaga guyimala umulikanza ilobhalibhapanga, kugiki bhadule kupandika matwajo mingi, umuwikaji bhobho.

Ulusumo lunulo, hangi, ‘lulidulanga higulya ya bhatizimu. Idina solobho ugubhatijiwa na gushoka nyuma hangi. Umayu uyo oshaga bhusiga, uluwitanwa ku nimo gungi, otulaga ubhusiga lwande, “kwanzula”. Aliyo kuli kanza duhu, hanuma yaho, agwiza ugugumalija unimo gokwe. Adadulile uguguleka unimo gokwe sagala. Uluuduma ugugumala unimo gokwe agusekwa na bhanhu. Gitumo UYesu agayombela ahigulya ya munhu uyo ohayaga guzenga nnala aliyo agaduma ugumalija abhanhu bhuyomba, “Umunhu uyu agandya guzenga aliyo adamalile” (Luka 14:29-30).

Giko nu munhu uyo obhatijiwa na gushoka numa adafaile umu Bhutemi bho ng’wa Mulungu, kunguno agagulekaga unimo gokwe sagala bho nduhu ugugumalija. Lolaga Kugundua mbegu ya Injili, ukurasa 13-14.

Waroma 12:11.

Wagalatia 6:9.

Mathayo 24:13.

Yohane 16:21.

Ufunuo 2:10.

Luka 9:62.

KISWAHILI: MZIMA WA KUFANYA KAZI MPAKA KUMALIZA.

Methali hiyo ilianzia kwa mtu anayevumilia kufanya kazi ya kusaga nafaka mpaka anaimaliza. Kwa mfano: mama mwenye kusaga mtama anaweza kuacha kazi yake, kwa sababu fulani na kuweka mtama pembeni, “kwanzula”. Lakini atakuja kuimalizia.

Methali hii hutumika kwa mtu mwenye bidii katika kazi. Mtu mzima, asiye mgonjwa, hawezi kuianza kazi ya kusaga na kuiacha ovyo. Bali anavumilia mpaka imalizike.” Ndiyo maana watu humuita ‘mzima wa kufanya kazi mpaka kumaliza.’ Rejea kugundua mbegu ya Injili, ukurasa 12-13.

Kitabu hicho, kiliandikwa na Kamati ya Utafiti wa utamaduni Bujora, kilichohaririwa na watafiti: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

Methali hiyo hutufundisha juu ya kujibidisha kufanya kazi mpaka kuzimaliza wakati tukiwa wazima, ili tuweze kupata mafanikio mengi, katika maisha yetu.

Methali hii pia ‘inafundisha kuhusu ubatizo. Haina maana kubatizwa na kurudi nyuma tena. Mama anayesaga mtama, kama akiitwa kwa kazi nyingine, anaweka mtama pembeni, “kwanzula”. Lakini kwa muda tu, baadaye atakuja kumaliza kazi yake. Hawezi kuiacha kazi yake ovyo. Akishindwa kumaliza kazi yake atachekwa na watu. Kama Yesu alivyosema kuhusu mtu mwenye kutaka kujenga mnara lakini akashindwa kumaliza watu wakasema, “Mtu huyu alianza kujenga lakini hakumaliza” (Luka 14:29-30).

Vile vile mtu yule aliyebatizwa na kurudi nyuma hafai kwa Ufalme wa Mungu kwa sababu anaiacha kazi yake ovyo bila kuimaliza. Rejea Kugundua mbegu ya Injili, ukurasa 13-14.

Waroma 12:11. “Msiwe wavivu, bali mwe na bidii katika roho mkimtumikia Bwana.”

Wagalatia 6:9. “Hivyo, tusichoke katika kutenda mema, kwa kuwa tutavuna kwa wakati wake tusipokata tamaa.”

Mathayo 24:13. “Atakayemumilia mpaka mwisho, ataokoka.”

Yohane 16:21. “Mwanamke anapokuwa na utungu wa kuzaa huwa na maumivu kwa sababu saa yake imewadia. Lakini mtoto akiisha kuzaliwa, yule mwanamke husahau maumivu hayo kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtoto ulimwenguni.”

Ufunuo 2:10. “Usiogope mateso yatakayokupata. Nakuambia Shetani atawatia baadhi yenu gerezani ili kuwajaribu, nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Uwe mwaminifu, hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.”

Luka 9:62. “Yesu akamwambia, “Mtu ye yote atiaye mkono wake kulima, kisha akatazama nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu.””

women-working

women working

women1

 

ENGLISH: HE/SHE IS HEALTHIER ENOUGH TO FINISH HIS/HER WORK.

This saying comes from someone who managed to grind her cereals until she finished them. A woman who is grinding her millet on a stone can be courageous enough; she can work until she finishes the millet she has arranged to grind. Even if it happens that someone interrupts her in her grinding, she will come back after that interruption and finish grinding her millet.

This saying can be compared to a person who is a hard worker. It can be likened to a person who feels sick but does not give up working (Refer to Kugundua Mbegu za Injili, which means ‘Discovering the Seed of the Gospel,’ pages 12-13). This book was written by the Bujora Cultural Research Committee, edited by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1993.

The proverb teaches us to work hard in order to achieve more in our lives.

This proverb also teaches people about baptism. It does not mean to be baptized and go back to sin again. A grinding mother, even if she is called for other tasks, can put her millet aside so that she continues with grinding when she comes back. She cannot give up her work. Failing to finish her job means she will be laughed at by people. As Jesus said, of a man who wanted to build a tower but could not finish, people said, “This man began to build but did not finish it ” (Luke 14: 29-30).

Likewise, the person who is baptized and goes back to sin is unfit for the Kingdom of God because he or she undermines the work of God (See ‘Discovering the Gospel Seed,’ pages 13-14).

Romans 12:11. Galatians 6: 9. Matthew 24:13. John 16:21. Revelation 2:10. Luke 9:62.

701. B’ULI HIWE B’UGIMBILIGWA.

Ulusumo lunulo, lyandija kuli ‘mayu uyo oshaga bhusiga hiwe. Umayu ng’wunuyo wilungujaga bho gwimba kugiki adule gwiyumilija umunimo gunuyo na gugutumama mpaga ha nhalikilo. Ugusha ahiwe jili ginhu ijo jidijinogu nu mayu agapandikaga bhukoyi. Aliyo kunguno ya matwajo ga nimo gokwe ayo galigelage ahanuma ya bhukoyi aliyumilija bho bhuyegi bho nduhu ugubhudilila ubhukoyi bhunubho.

Ulusumo lunulo lugatumilagwa kubhatinbwa ng’holo abhanhu abho bhali na makoye, nulu abhatumami kugiki bhikomeje umumakoye nulu umumilimo kunguno ubhukamu bhobho bhugubhiza bhuyegi ukubhoyi ahabhutongi na bhagulya matwajo ga nungula yabho.

Hangi ulusumo lunulo, lugatumilagwa kuli munhu uyo alikoyiwa na bhusatu bhulebhe. Ukuli munhu o mbika yiniyi ilidudaka gundilila umubhusatu bhokwe bho nduhu ugubhinzika moyo.’ Lolaga Kugundua Mbegu za Injili, ukurasa 12.

Ijitabho jinijo jigandikwa na Kamati ya Utafiti wa Utamaduni Bujora, ijojigahaririwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gutumama milimo bho wiyumilija na gubhatinbya ng’holo abhanhu bhabho, kugiki bhadule gutumama chiza imilimo yabho, na kupandika matwajo mingi, umuwikaji bhobho.

“Yadudaka ayise gwiyumilija umugunondela UYesu Kristo bho nduhu ugugwa ng’holo dikale na wisagiji bho gupandika matwajo ga nungula yise aho bhutongi. Dubhize guti mayu uyo oshaga bhusiga umo agiyumiligija bho bhuyegi na bho nduhu ugudilila ubhukoyi bhosebhose kunguno ya matwajo ga milimo yakwe ayo galigele aha bhutongi yaho.

Padre Emmanuli Makolo wi Jimbo lya Shinyaga, Tanzania agalwandika ulusumo lunulu: “Buli hiwe bukimbiligwa” umu kadi yakwe iya bhupadirisho. Giki, agagulenganija unimo go bhubadiri nu mayu uyo Alisha.” Lolaga Kugundua Mbegu ya Injili, 13.

Waroma 12:11.

Wagalatia 6:9.

Mathayo 24:13.

Yohane 16:21.

Ufunuo 2:10.

Luka 9:62.

KISWAHILI: ULIOKO KWENYE JIWE HUIMBIWA  (MSAGAJI HUJIFARIJI KWA KUIMBA).

Methali hiyo, ilianzia kwa ‘mama anayesaga mtama kwenye jiwe. Mama huyo hujifariji kwa kuimba aweze kuvumilia katika kazi hiyo na kuifanya mpaka mwisho. Kusaga kwenye jiwe ni jambo lisilo rahisi na mama huwa anapata masumbufu. Lakini kwa sababu ya matunda ya kazi yake yatakayopatikana baadaye huwa anajikaza kwa furaha bila kujali masumbufu hayo.

Methali hii hutumika kwa kuwatia moyo watu wenye shida au wafanyakazi ili wajitahidi katika shida au kazi, kwa sababu bidii yao itakuwa furaha kwao baadaye na watakula tunda la jasho lao.

Tena methali hiyo hutumika kwa mtu anayezidiwa na ugonjwa fulani. Kwa mtu wa namna hii inatupasa kumjali katika ugonjwa wake bila kukata tamaa.’ Rejea Kugundua Mbegu za Injili, ukurasa 12.

Kitabu hicho, kiliandikwa na Kamati ya Utafiti wa utamaduni Bujora, kilichohaririwa na watafiti: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kufanya kazi kwa uvumilivu na kuwatia moyo watu wao ili waweze kuyatekeleza majukumu yao vizuri na kupata mafanikio mengi, maishani mwao.

“Yatupasa sisi kupiga moyo konde katika kumfuata Yesu Kristo bila kukata tamaa tukiwa na tumaini la kupata matunda ya jasho letu hapo baadaye. Tuwe kama mama mwenye kusaga mtama anavyojikaza kwa furaha bila kujali masumbufu yoyote kwa sababu ya matunda ya kazi yake yatakayopatikana baadaye.

Padre Emmanueli Makolo wa Jimbo la Shinyanga, Tanzania aliandika methali hii: “Buli hiwe bukimbilagwa” kwenye kadi yake ya upadrisho. Yaani, alifananisha kazi ya upadre na kazi ya mama mwenye kusaga.’ Rejea Kugundua Mbegu ya Injili, ukurasa 13.

Waroma 12:11. “Msiwe wavivu, bali mwe na bidii katika roho mkimtumikia Bwana.”

Wagalatia 6:9. “Hivyo, tusichoke katika kutenda mema, kwa kuwa tutavuna kwa wakati wake tusipokata tamaa.”

Mathayo 24:13. “Atakayemumilia mpaka mwisho, ataokoka.”

Yohane 16:21. “Mwanamke anapokuwa na utungu wa kuzaa huwa na maumivu kwa sababu saa yake imewadia. Lakini mtoto akiisha kuzaliwa, yule mwanamke husahau maumivu hayo kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtoto ulimwenguni.”

Ufunuo 2:10. “Usiogope mateso yatakayokupata. Nakuambia Shetani atawatia baadhi yenu gerezani ili kuwajaribu, nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Uwe mwaminifu, hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.”

Luka 9:62. “Yesu akamwambia, “Mtu ye yote atiaye mkono wake kulima, kisha akatazama nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu.””

stone-grinding.2

stone-grinding

 

ENGLISH: THE GRINDER OF SORGHUM SINGS TO COMFORT HERSELF.

This proverb comes from a woman who was singing while grinding sorghum. This woman was able to console herself through singing until she finishes grinding. That is why people came with the proverb ‘the grinder of sorghum sings to comfort herself’ to describe this situation. Grinding sorghum on the stone is not an easy task; it needs courage and perseverance.

This proverb is used to encourage distressed people or workers to work and be courageous enough in performing some tasks because they will benefit in future. Also this proverb can be used in the context of sickness where the sick person needs to tolerate without despair (Refer to Kugundua Mbegu za Injili, which means, ‘Discovering the Seed of the Gospel,’ page 12). This book was written by the Bujora Cultural Research Committee, edited by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1993.

This proverb teaches people to work patiently and inspires people to be courageous in their lives. Patience and courage will make people to be responsible in whatever they decide to do in life. “We need to be heartfelt in following Jesus Christ without giving up hope of finding the fruit of our sweat. May we be like the grinding woman who happily presses herself with no worries because of the fruit of her labour.

Fr. Emmanuel Makolo from Shinyanga diocess, Tanzania, wrote the same proverb in his sovernior . That is, he likened the work of a priest to the work of a grinding mother (See Gospel Seed Discoveries, page 13).

Romans 12:11. Galatians 6: 9. Matthew 24:13. John 16:21. Revelation 2:10.Luke 9:62.

700. BULUNGALEKELE! NI SHITAKONZAGWA? SHIKAKONZAGWA.

“Ulusumo lunulo, lugatumilwa na Nkwilima aho umayu bhukwi okwe ogakeleja ugubisha ijiliwa.

Unkwilima aginga guja gujungisha umayu bhukwi okwe. Ugansanga alimhola, aliyo alitumama nimo go gulinda noni. Aho bhamala ugwigisha Unkwilima agayomga: “Mayu, nagubhona, nashoke kaya lulu.” Umayu agalema: “Ubhebhe ulingeni one. Ududula ugushoka na nzala. Nambilijage ugulinda inoni, nagagwigile nhomba.”

Unkwilima agalekwa lulu mungunda alilinda noni. Ungikulu agaja kaya ugandya guzuga jiliwa tamu. Uchola nyama njumu, ilina lyayo, “ng’homele”. Uguzuga inyama injumu lulu igasolaga ikanza lilihu noyi. Gwandija usibhuche minzi na guyoja bho minzi ga moto. Huna uibudagule ibhize ndogoleku. Hunawandya uguizuga na minzi. Aminzi ulu gukama, ongeja mabhele. Amabhele ulu gukama ongeja maguta.

Ungikulu atali aguzugaga makubhi, Unkwilima ubhona giki odila. Wandya gunmela bho mbisila umayu bhukwi okwe. Ulu alijipuga inoni aliyosemba, “bulungakele”, giki, “udilaga ugubisha ijiliwa.”  Ungikulu wigwa iyoaliiyomba Unkwilima uyomba: “Unkwilima one wandya gunimela ihaha.” Aha nhalikilo agabisha ijiliwa. Unkwilima nang’hwe agikomeja kuyomba: “Bulungakele” (“milele”).

Unkwilima agakalibhushiwa lulu gwiza gulya. Ungikulu nang’hwe uja ugujulinda inoni, wandya gunshokeja bho mbisila. Agayomba: “Ni shitakonzagwa? Shikakonzagwa.” Ugukonza, iligwita nimo hado hado bho bhulingisiji na wangaliji.

Ulusumo lunulo, lulidulanga gwiyumilija mpaga ilikanza lishige. Hangi lulidulanga gutumama milimo na wangaliji.” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa, 73.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

“Ilidudaka gubhiza bhiyumilija ulu kinhu jilebhe jidujaga gitumo bhuli ubhutogwa wise. Bhuli ginhu jili ni kanza lyajo. Igelelilwe dutule uwikaji wise mumakono ga ng’wa Mulungu bho nduhu ugukoyakoya. Aliho kihamo na yise alitutongela mubhuli mhayo, agudinhila kuli kanza lwakwe gitumo bhuli ubhupangi bhokwe.

Hangi, umuguntumamila Mulungu ilidudaka gubhiza na bhutaratibhu, wangaliji, na bhushikanu.” Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 74.

Mhubiri 3:1.

Wagalatia 4:4-5.

Luka 2:25-26.

Yakobo 5:10-11.

2Petro 1:10-11.

KISWAHILI: MILELE! SIYO LAZIMA KUFUATA UTARATIBU CHAKULA KIPIKWE VIZURI? NI LAZIMA KUFUATA UTARATIBU CHAKULA KIPIKWE VIZURI.

“Methali hii ilitumiwa na Mkwilima alipokawia mama mkwe kuivisha chakula.

Mkwilima aliondoka kwenda kumsalimu mama mkwe. Akamkuta mzima, lakini alikuwa na kazi ya kulinda ndege. Walipomaliza kusalimiana Mkwilima akasema: “Mama, nimekuona, nirudi sasa nyumbani.” Mama akataa: “Wewe ni mgeni wangu. Huwezi kurudi na njaa. Unisaidie kulinda ndege, nikupikie uji.”

Basi Mkwilima akaachwa shambani analinda ndege. Mzee akaenda nyumbani kwanza kupika chakula. Akatafuta nyama kavu, jina lake “ng’homele”. Basi kupika nyama kavu inakuchukua muda mrefu sana. Kwanza uchemshe maji na kuiosha kwa maji ya moto. Halafu kuipondaponda iwe laini. Sasa unaanza kupika na maji. Maji yakikauka unaongeza maziwa. Maziwa yakikauka unaongeza mafuta.

Mzee bado akipika mboga, Mkwilima akaona kwamba anakawia. Akaanza kumtania kwa fumbo mama mkwe. Anapowafukuza ndege anasema, “bulungakele”, yaani “umekawia kuivisha chakula.” Mzee anasikia anayosema Mkwilima akanena: “Mkwilima wangu ameanza kunitania sasa.” Mwisho akaivisha chakula. Mkwilima naye anazidi kusema: “Bulungakele” (“milele”).

Basi Mkwilima alikaribishwa kuja kula. Mzee naye akaenda kulinda ndege, akaanza kumjibu kwa fumbo. Akasema: “Ni shitakonzagwa? Shikakonzagwa.” Kukonza, maana yake, ni kufanya kazi pole pole kwa utaratibu na kwa uangalifu.

Methali hii inatufundisha kuvumilia mpaka wakati umefika. Tena inafundisha kufanya kazi kwa uangalifu.” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 73.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

“Inatupasa kuwa wavumilivu ikiwa jambo fulani haliendi kama yalivyo mapenzi yetu. Kila jambo lina wakati wake. Yatubidi kuweka maisha mikononi mwa Mungu bila kuhangaika. Yumo pamoja nasi akituongoza katika kila neno, atatufanikisha wakati wake kadiri ya mpango wake.

Tena, katika kumtumikia Mungu inatupasa kuwa na utaratibu, uangalifu na ukamilifu.” Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 74.

Mhubiri 3:1. “Kuna wakati kwa ajili ya kila jambo, nayo majira kwa kila tendo chini ya mbingu:”

Wagalatia 4:4-5. “Lakini ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe, ambaye alizaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria, kusudi awakomboe wale waliokuwa chini ya sheria, ili tupate kupokea zile haki kamili za kufanywa watoto wa Mungu.”

Luka 2:25-26. “Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake. Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.”

Yakobo 5:10-11. “Ndugu zangu, waangalieni manabii walionena kwa Jina la Bwana, ili kuwa mfano wa uvumilivu katika kukabiliana na mateso. Kama mnavyojua, tunawahesabu kuwa wamebarikiwa wale waliovumilia. Mmesikia habari za uvumilivu wake Ayubu na mmeona kile ambacho hatimaye Bwana alimtendea. Bwana ni mwingi wa huruma naye aliyejaa rehema.”

2Petro 1:10-11. “Kwa hiyo, ndugu zangu, fanyeni bidii zaidi kuuthibitisha wito wenu na uteule wenu, kwa maana mkifanya hivyo, hamtajikwaa kamwe. Kwa njia hii, mtajaliwa kwa ukarimu mwingi kuingia katika Ufalme wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.”

nkima o ghana1

ghana man

african-millet-field

ENGLISH: “PERPETUAL! IS IT NOT NECESSARY TO FOLLOW RULES FOR COOKING FOOD CAREFULLY? IT IS NECESSARY TO FOLLOW RULES FOR COOKING FOOD WELL.”

This saying was used by a son-in-law when his mother-in-law cooked him food. One day the son-in-law went to visit his mother-in-law. By the time the man reached the place, she was busy chasing birds that were eating her cereals in the farm. When they had finished greeting  the son-in-law said: “Mama, I have seen you, and now I would like to leave for home. The mother-in-law refused saying: “You are my guest. You can’t go back hungry. Help me chasing the birds, and I cook you some food. ” The mother-in-law began the process of making her food. She took dried meat and cooked it (the process which took quiet a long time), she then boiled the meat, washed it, and pounded the meat in order to make it soft then final cooking. When cooking water dried, she added milk and finally fat (after the milk has dried).

After she had finished with meat, she began working on vegetables for her son-in-law to have delicious food. These processes made the man see his mother-in-law as someone who is very slow in her doings. He jokingly began talking to his mother-in-law in parables: “ bulungakele ,” that is, “you are late for food.” When the mother-in-law heard what the son-in-law said, she said to herself: “My son-in-law has started to joke me now.” The man kept on saying, bulungakele, “that is, you are late for food.” Thereafter, the food was brought, the man began eating the food and his mother-in-law took turn to chase birds in the farm.

In the same way, the mother-in-law began joking the son-in-law in parables: “perpetual! Is it not necessary to follow rules for cooking food carefully? It is necessary to follow rules for cooking food well.”

This proverb teaches us to persevere until the time has come. It also teaches us to be smart (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 73). This book was written by researchers: Dr. Donald Sybertz, M.M., and Joseph Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

We have to be patient if something doesn’t work out as we wish. Every thing has its time. We have to put life in God’s hands without worry. He is with us guiding us in every word, and He will fulfill His promises according to His plan.

Also, in serving God we must be orderly, careful and thorough (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 74).

Ecclesiastes 3: 1. Galatians 4: 4-5. Luke 2: 25-26. James 5: 10-11. 2 Peter 1: 10-11.

699. BUGALI WA HENAHA WA KUGULA IDAKO.

Yalihoyi kaya imo ya bhanhu bhabhili, ngosha na nkima. Ungosha wipunaga guja gungunda gujulima,  oneka unkima alizuga jiliwa ja guchala ukumilimo yabho, kugiki bhagalye kihamo. Aliyo lulu, unkima ng’wunuyo, okelejaga noyi bhuli lushiku uguchala ijiliwa jinijo.

Lushigu lumo, ungoshi agang’wila unke okwe, ‘intondo dugwipuna pye abhose dugalime mpaga ikanza ilebhe, hunadugushoka kaya gwiza gulya jiliwa. Unke okwe ashosha, ‘nahene dugwipuna dugalime ulu dushoka nagwiza nazuge ijiliwa dulya.’

Aho wela ubhujiku, bhagipuna diyu bhugalima mpaga lyushika ikanza ilebhe bhushoka kaya gwiza gulya jiliwa. Ungosha ung’wila unke, ‘zugaga lulu ijiliwa dulye.’ Unke ushosha, ‘nahene nazuge.’

Unkima ng’wunuyo, agandya guzuga hado hado nose ungosha, unoga ugwigasha. Umuja, ‘umukaya  ng’wabisha ijiliwa?’ Unke okwe ushosha, ‘degelaga.’ Ungosha agankomeleja, ‘kangilijaji uguzuga, nose gayusada amadako ugwishasha.’

Oganoga unke okwe obhisha ijiliwa na gujitenga, unkabhulisha ungoshi, ‘karibhu lulu dabisha ijiiwa.’ Ungoshi wiza ugulya aliyomba, ‘bugali wa henaha wa gugula idako.’ Ubhunubho huwandijo bho gutumimalwa go lusumo lunulo.

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli ngosha nulu ng’wimeji ulu nke okwe alikeleja gubisha jiliwa kunguno ya bhugokolo, nulu bhugulu bhokwe. Ugugula idako  yili guyomba: Ulilipa bho wiyumilija bho madako kunguyo ya gulindila jiliwa kuli kanza lilifu. Udulipaga hela aliyo ulilipa. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘bugali wa henaha wa kugula idako.’ Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 72.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na bhukamu bhutale ubho gubhambilija uguitumama chiza imilimo yabho, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi, umuwikaji bhobho.

“Dulidakilwa gutumama milimo ku bhukamu bhuli ikanza ilo dulibhatumamila abhigusu nulu ulu dulintumamila Sebha. UMulungu adatogishiyagwa nu munhu uyo agantumimalaga bho nduhu bhukamu nulu moyo go gutogwa.

Dudizubhiza  hagatigati umuguntumamila Sebha, aliyo dubhize moto, giki, duntogwe ku moyo gwise gose, masala gise gose, na nguzu jise jose. Hangi dulidakilwa gubhatumamila abhigisu bho bhukamu na moyo go bhutogwa gitumo agitila UYesu Kristo ng’winikili.” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 72.

Wakolosai 3:23-24.

Ufunuo 3:16.

Waebrania 6:12.

Waroma 12:11.

KISWAHILI: UGALI WA HAPA NI WA KUNUNUA TAKO.

Ilikuwepo familia moja yenye watu wawili, mme na mke. Mwanamume alikuwa alijilawa asubuhi na mapema kwenda kulima shambani, alimuacha mke wake akipika chakula cha kupeleka shambani ili wakale huko kwa pamoja. Lakini basi, mwanamke huyo, alikuwa akichelewa sana kila siku kupeleka chakula hicho.

Siku moja, mwanamume alimwambia mke wake, ‘kesho tutaamuka mapema wote twende shambani tukalime mpaka wakati fulani ndipo tutarudi nyumbani kuja kula chakula.’ Mke wake akajibu, ‘sawa tutaamuka mapema asubuhi tukalime tukirudi nitakuja kupika chakula tule.’

Kesho yake waliamuka asubuhi kwenda shambani kulima mpaka ukafika wakati fulani, wakarudi nyumbani kula chakula. Mwanamume alimwambia mke wake, ‘pika basi chakula tule.’ Mke wake akajibu, ‘sawa napika.’

Mwanamke huyo, alianza kupika pole pole, mwishowe mume wake, akashoka kukaa. Akamuuliza, ‘humo ndani mmeivisha chakula?’ Mke wake akajibu, ‘tumekaribia.’ Mume wake akamhimiza, ‘fanyeni haraka, mwishowe matako yameanza kuuma kukaa.’

Mwishowe mke wake aliivisha chakula, akakipeleka mezani na kumkaribisha mumewe akisema, ‘karibu basi tumeivisha chakula.’ Mume wake alinuka kwenda kula chakula mezani akisema, ‘ugali wa hapa ni wa kunulua tako.’ Huo ndiyo ukawa mwanzo wa kutumika kwa methali hiyo.

Methali hiyo, hulinganishwa kwa bwana au mtani ikiwa mke wake anachelewa kuivisha chakula kwa sababu ya uvivu au ujeuri wake. Kununua tako ni kusema: Unalipa kwa maumivu ya matako kwa sababu ya kusubiri chakula kwa muda mrefu. Hulipi pesa lakini unalipa. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘ugali wa hapa ni wa kunulua tako.’ Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 72.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methail hiyo, hufundisha watu juu ya kuyatekeleza majukumu yao kwa bidii kubwa, ili waweze kupata mafanikio mengi zaidi katika maisha yao.

“Yatupasa kufanya kazi kwa bidii kila tunapowatumikia wenzetu au tunapomtukika Bwana. Mungu hapendezwi na mtu anayemtumikia bila bidii au moyo wa kupenda. Tusiwe vuguvugu katika kumtumikia Bwana, bali tuwe moto, yaani tumpende kwa moyo wetu wote, akili zetu zote na nguvu zetu zote. Tena yatupasa kuwatumikia wenzetu kwa bidii na moyo wa upendo kama alivyofanya Yesu Kristo mwenyewe.’ Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 72.

Wakolosai 3:23-24. “Lo lote mfanyalo, fanyeni kwa moyo kama watu wanaomtumikia Bwana na si wanadamu. Kwa kuwa mnajua kwamba mtapokea urithi wenu kutoka kwa Bwana kuwa thawabu yenu”

Ufunuo 3:16. “Hivyo kwa kuwa u uvuguvugu, kwamba wewe si baridi wala si moto, nitakutapika utoke kinywani Mwangu.”

Waebrania 6:11-12. “Nasi twataka kila mmoja wenu aonyeshe bidii iyo hiyo ili mpate kujua uhakika kamili wa lile tumaini mpaka mwisho, ili msije mkawa wavivu, bali mpate kuwaiga wale ambao kwa imani na saburi hurithi zile ahadi.”

Waroma 12:11. “Msiwe wavivu, bali mwe na bidii katika roho mkimtumikia Bwana.”

ghana1

ghana child-

food1

 

ENGLISH: UGALI IN THIS HOUSE IS BOUGHT THROUGH YOUR BUTTOCKS.

There was one family with two people, husband and wife. The man would wake up very early in the morning going to the farm. And the woman could delay a bit because she has to cook some meal and carry it with her to the farm and eat with her husband. But this woman used to be late everyday to bring food for the man.

One day the man told his wife that all of them have to leave home very early in the morning without carrying food and that, food will be eaten when they come back from the farm. The wife agreed with the man and left for the farm. When they came back from the farm, the woman went to the kitchen and spent a lot of hours cooking the food until the man became tired of waiting for food. The man kept on asking for food and the woman could reply, wait; it will be done soon.

The man waited until his buttocks began to pain for too much sitting. When the food was ready, the man was invited to eat and he said ‘ugali in this house is bought through your buttocks.’ This marked the beginning of this saying.

This saying can be compared to a person who is lazy or cruel in his/her life. Such a person will not help others easily during distress times. People of this nature will enjoy seeing others suffer (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 72). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications Ndanda – Peramiho, 1984.

This saying teaches people how to carry out their tasks with great effort so that they can achieve more success in their lives.

We must work hard every time we serve our fellowmen or when we serve the Lord. God is displeased with someone who serves Him with little effort. Let us not be slothful in serving the Lord, but zelous, loving Him with all our heart, mind, and strength. We must serve our fellow men with as much zeal and love as Jesus Christ Himself (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 72).

Colossians 3: 23-24. Revelation 3:16. Hebrews 6:12. Romans 12:11.