“Itendile igiki umubhuzengi bho numba ja kale, jigabhizaga na ng’ingi ningi. Imo ya ng’inghi jilijo igayidimilaga inumba ngima iyo yili ‘ng’hingi ya kitimbo,’ umujisuguma. Ing’hingi yiniyi iya jitimbo yili ya solobho noyi ukumhola bho numba nu ukumhola ya wikaji.
Giko numu wikaji bho kaya Ubhaba umyaji ali guti ng’hingi ya kitimbo, iki alolilwe weyi nabhose. Umu kajile kise abhingi, bhagamijaga mamila na gugabhila ha ginhu jose jose ijo jidina solobho, aliyo guli ngilo ugujibhila mamila iginhu ijo jili na solobho. Yijinijo higinhu, nulu munhu umo yigelelilwe witilwe gitumo yibhelelile ni likujo lyakwe.
Ulu undharaha so nunu mayu oko ntale oseose, yili guti gumigija mamila. Ikalagu yiniyi ilidulanga kubhakuja abhatale bhise.” Lolaga Kugundua Mbegu ya Injili, ukurasa 15.
Ijitabho jinijo jigandikwa na Kamati ya Utafiti wa Utamaduni Bujora, ijojigahaririwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.
“UMulungu ali ng’hingi ya kitimbo ku jisumva jose. “Iki uweyi Ng’winikili huyo agabhinhaga abhanhu ubhupanda, agabhinhaga bhudula bho gweshema na gubhinha bhuli ginhu” (Matendo 17:25).
Kuyiniyo, igelelilwe dunhamye Mulungu gitumo ihayililwe. Ulu dunbyeda Mulungu, dulimila mamila. Miito gose agabhubhi gali guti mamila.
Umushandikwa Shela duliwilwa hape giki, UYesu Kristo hi “Liwe ilisolanyiwa na lya solobho nhale” (1Petro 2:4). Ee, umu wikaji wise, nani nulu kiyi jili ng’hingi ya kitimbo nulu liwe lya munsingi?
Ee, tulizunya igiki UYesu Kristo ng’winikili ali Sebha, wandijo na ngelelo, na wandijo bho wiza bhose? Guli mhayo go gupinihaja ugubhona giki nhangala ningi dudumanaga UYesu Kristo igiki ali nsingi go wikaji wise. Dugundalahaga na kumila mamila sagala duhu bho nduhu ugundilila. Jili ginhu ja gukumya gete.”
Lolaga Kugundua Mbegu ya Injili, ukurasa 16.
Kutoka 20:12.
Mithali 9:10.
Mathayo 2:42.
1Petro 2:4-5.
Mathayo 16:18.
KISWAHILI: NGUZO KUU YA NYUMBA HAIPENGEWI KAMASI:- BABA MZAZI.
“Ni dhahiri ya kwamba katika ujenzi wa nyumba zetu za jadi, huwa na nguzo nyingi. Moja ya nguzo hizi hutegemeza nyumba nzima ndiyo nguzo kuu, yaani kwa kisukuma: “ng’ingi ya kitimbo”. Nguzo hii kuu ni muhimu sana kwa usalama wa nyumba na kwa usalama wa wakazi.
Hali kadhalika, katika maisha ya familia baba mzazi ni kama nguzo kuu, kwani hutegemewa na wote. Katika mila zetu wengi hupenga kamasi na kupakaa kwenye kitu chochote tusichokithamini, lakini ni haramu kupakaa kamasi kwenye kitu chenye thamani. Ndivyo kitu au mtu anavyopaswa kutendewa kadiri ya stahili au heshima yake.
Ukimdharau baba au mama mkubwa yeyote, ni kama kumpaka kamasi. Kitendawili hiki kinatufundisha kuwaheshimu wakubwa wetu.” Rejea Kugundua Mbegu ya Injili, ukurasa 15.
Kitabu hicho, kiliandikwa na Kamati ya Utafiti wa utamaduni Bujora, kilichohaririwa na watafiti: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.
“Mungu ni nguzo kuu ya viumbe vyote. “Kwa kuwa yeye Mwenyewe ndiye anayewapa watu uhai, anawawezesha kupumua na anawapa kila kitu” (Matendo 17:25).
Kwa hiyo, yatupata kumcha Mungu kadiri ya stahili yake. Tukimdharau Mungu, tunampaka kamasi. Matendo yote mabaya ni kama kamasi.
Katika maandiko Matakatifu tunaambiwa wazi kwamba Yesu Kristo ndiye “Jiwe teule na la thamani kubwa” (Petro 2:4). Je, katika maisha yetu, nani au nini ni nguzo kuu au jiwe la msingi?
Je, tunaamini kwamba Yesu Kristo mwenyewe ndiye Bwana, mwanzo na mwisho, na chimbuko la mema yote? Ni jambo la kusikitisha kuona kwamba mara nyingi hatumtambui Yesu Kristo kuwa msingi wa maisha yetu. Tunamdharau na kumpaka kamasi ovyo tu bila kumjali. Ni jambo la ajabu kweli.” Rejea Kugundua Mbegu ya Injili, ukurasa 16.
Kutoka 20:12. “Waheshimu baba yako na mama yako, ili upate kuishi siku nyingi katika nchi anayokupa BWANA Mungu wako.”
Mithali 9:10. “Kumcha BWANA ni mwanzo wa hekima na kumjua Mtakatifu ni ufahamu.”
Mathayo 21:42. “Yesu akawaambia, “Je, hamjasoma katika maandiko kwamba: “Lile jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni, Bwana ndiye aliyefanya jambo hili, nalo ni la ajabu machoni petu?’”
1Petro 2:4-5. “Mwendeeni Yeye aliye Jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu bali kwa Mungu ni teule na la thamani Kwake. Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa kuwa nyumba ya Roho, mpate kuwa ukuhani mtakatifu, mkitoa dhabihu za kiroho zinazokubaliwa na Mungu kwa njia ya Yesu Kristo”
Mathayo 16:18. “Nami nakuambia, wewe ndiwe Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu, hata malango ya kuzimu hayataweza kulishinda.”
ENGLISH: I HAVE A RIDDLE- LET COME, THE CENTRAL POLE OF THE HOUSE IS NOT SMEARD WITH MUCUS: FATHER.
In the construction of traditional houses, there are many poles but one of them is considered central; the main pole. This central pole is very important in the life of the whole house.
Likewise, in the family the father is the central pole of the family. The whole family depends on him. It is uncultured if someone can smear his/her mucus on something of great value. If one can do so then he/she is regarded as someone who doesn’t respect himself/herself and others as well.
Similarly, if someone can despise his/her father then it is like smearing mucus on him. This riddle teaches people to respect their parents (Refer to Kugundua Mbegu za Injili, which means, ‘Discovering the Seed of the Gospel,’ page 15). This book was written by the Bujora Cultural Research Committee, edited by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1993.
“God is the ultimate pillar of all creations. “For He Himself gives to men life, allow them to breath and give them everything ” (Acts 17:25).
Thus, we have to fear God. If we disrespect God, we rub Him mucus. All bad deeds are like mucus.
In the Holy Scriptures we are clearly told that Jesus Christ is the “chosen and precious stone” (1Peter 2: 4). In our life, who or what is the main pole or cornerstone?
Do we believe that Jesus Christ Himself is Lord, beginning and end, and the source of all good? It is sad to see that we often do not recognize Jesus Christ as the foundation of our lives. We despise Him and rub Him with the mucus without care. It’s really astonishing (See ‘Discovering the Gospel Seed,’ page 16).
Exodus 20:12. Proverbs 9:10. Matthew 2:42. 1 Peter 2: 4-5. Matthew 16:18.