Joe Healey

697. AHO UKALILAGA HAHO UKANYELAGA.

Aho kale olihoyi munhu uyo oliogaiwa jiliwa ahikanza lya nzala. Umunhu ng’wunuyo, ojaga agucholaga jiliwa uko usimizilaga. Lushigu lumo agajipandika ijiliwa ulya mpaga wiguta. Oho omala ugulya, aganyela haho olilaga ijiliwa jilinijo, adizukaga igiki alashoka hoyi alye hangi.  Hunagwene abhanhu bhagandya guyung’wila giki, ‘aho ukalilag haho ukanyelaga.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo okaribhushiyagwa chiza ha kaya ya ng’wa munhu. Ubhegejiyawa chiza guti ndugu ohakaya yiniyo, bhuyulya kihamo na gwendelea.

Aha ngelelo yaho, umunhu ng’wunuyo, ushiya nu mayu uoha kaya yiniyo, nulu, wibha ginhu hoyi, nulu wita jito jose jose ijo jidijawiza.’ Ugubhilitia ya bhubhi abhanhu bhenabho, yikolile na gunyela oholilaga, umunhu ng’wunuyo. Hunagwene abhanhu bhang’wilaga giki, ‘aho ukalilag haho ukanyelaga.’ Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 70.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na bhulumbi ukubhanhu abho bhalibhitila ya wiza, bho kuleka ugubhitila iyabhubhi, kugiki bhadule gwendelea gwiyambilija chiza, umuwikaj bhobho.

“Abhanhu abho dugabhitililaga yabhubhi bhali bhanhu abho dugikalaga kihamo nabho. Dugemele: ugushiya nu nkima o nzenganwa, gung’wibhila nwani, na gwendelea.

Hangi iyiniyo yili jigemelo ukubhumani wise nu Yesu Kristo uyo agadubokelaga kuwizang’holo na gwifunya gete kubhise guti nwani. Ningiki odutogwa, bho miito gise mabhi duganhemaga na gundalaha.

Hangi umusakramenti ya Ekaristia tugadumaga ugunkuja kunguno dugalyaga mili gokwe na gung’wa mininga gakwe bho nduhu ugwigelelwa. Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 71.

Zaburi 55:12-14.

Mathayo 26:49-50.

Yohone 13:21, 25-26.

1Wakorintho 11:27.

KISWAHILI: UNAPOKULA PAPO HAPO UNAPOKWENDA HAJA.

Hapo zamani alikuwepo mtu aliyekosa chakula wakati wa njaa. Mtu huyo, alienda kutafuta chakula kule alipotembelea. Siku moja alipata chakula, akala mpaka agatosheka. Alipomaliza kula, alijisaidia papo hapo alipolia chakula. Ndiyo maana watu wakaanza kumwambia, kwamba, ’unapokula papo hapo unakokwenda haja.’

 Methali hiyo hulinganisha kwa mtu yule ambaye amekaribishwa vizuri kwenye nyumba ya mtu. Akatendewa vizuri kama mmoja wa jamaa, wakila pamoja na kadhalika.

Mwishowe mtu huyo, huzini na mama wa kaya hiyo, au huiba au hutenda kitendo chote chote, ambacho si kizuri. Kuwafanyia ubaya watu hao, hufanana na kunyea pale alipolia chakula mtu huyo. Ndiyo maana watu humwambia mtu huyo, kwamba ‘unapokula papo hapo unapokwenda haja. Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 70.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na shukrani kwa watu wanaowatendea mema kwa kuacha kuwatendea mabaya, ili waweze kuendelea kusaidiana vizuri, katika maisha yao.

“Watu ambao tunawatendea mabaya ni watu (wale) ambao tunaokaa pamoja nao. Kwa mfano: Kuzini na bibi wa jirani, kumwibia rafiki, na kadhalika.

Tena hii ni mifano kwa uhusinano wetu na Yesu Kristo anayetupokea kwa ukarimu na kujitoa kwetu kabisa kama rafiki. Ijapokuwa ametupenda, kwa matendo yetu mabaya, huwa tunamkataa na kumdharau.

Tena katika sakramenti ya Ekaristi huwa tunashindwa kumheshimu kwa sababu tunakula mwili wake na kunywa damu yake bila kustahili.” Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 71.

Zaburi 55:12-14. “Kama aliyenitukana ni adui yangu ningevumilia, kama mtu mwovu angejiinua dhidi yangu, ningejificha asinione. Kumbe ni wewe, mwenzangu, mshiriki na rafiki yangu wa karibu, ambaye wakati fulani tulifurahia ushirika mzuri tulipokuwa tukienda katikati ya umati hekaluni mwa Mungu.”

Mathayo 26:49-50. “Mara akamjia Yesu na kumsalimu, “Salaam, Rabi!’’ Akambusu. Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya kile ulichokuja kufanya hapa.”

Yohane 13:21, 25-26. “Baada ya kusema haya, Yesu alifadhaika sana moyoni, akasema, ‘‘Amin, amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.’’ Yule mwanafunzi akiwa amemwegemea Yesu akamwuliza, ‘‘Bwana tuambie ni nani?’’   Yesu akajibu, ‘‘Ni yule nitakayempa hiki kipande cha mkate baada ya kukichovya kwenye bakuli.’’ Hivyo baada ya kukichovya kile kipande cha mkate, akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskariote.”

1Wakorintho 11:27. “Kwa hiyo, mtu ye yote alaye mkate huo au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa na hatia ya dhambi juu ya mwili na damu ya Bwana.”

table food

tradition-

tradition1

ENGLISH: YOU DEFACATE WHERE YOU ATE FOOD FROM.

Once upon a time ago, there was a person who had no food during famine. One day this person travelled in search for food. He reached somewhere where he got food, ate it to his satisfaction. When he had satisfied with the food he defacate on that place. This is why people say ‘you defacate where you ate food from.’

 This saying can be compared to a person who is most welcomed in someone’s house. Such a person was well treated. Finally, instead of appreciating for the kindness, turns around the host by embarrassing him/her. This embarrassment can be stealing from his/her host or anything that disturbs their relationship (Refer to Kueneza Injili kwa Methali’ which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 70). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

This saying teaches people to be thankful to people who do good for them. They don’t have to return embarrassment for good things they have done to them.

The people we are abusing are the people we are living with. For example, committing adultery with a neighbor’s wife, robbing a friend, and so on.

Again these are examples of our association with Jesus Christ, who graciously accepts us and gives Himself completely as a friend. Although He loves us, by our evil deeds, we often reject and despise him.

And in the sacrament of the Eucharist we often fail to honor Him because we eat His flesh and drink His blood unworthily (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 71).

Psalm 55: 12-14. Matthew 26: 49-50. John 13:21, 25-26. 1 Corinthians 11:27.

696. NZUGA (NZUGILA) LUSEKO, NULU, NDEKA LUSEKO.

Aho kale olihoyi nkima umo uyo wikalaga ha chalo jilebhe. Lushigu lumo apandika ngeni uyo oliofumila kulipande lya kule. Ungeni  ng’wunuyo, oliotuubha noyi kunguno ya gusiminza lugendo lulihu.

Umayi ng’wunuyo, uyo oliombokela ungeni okwe, agandya mahoha higulya ya ginhu ja mbika ningi. Umumahoya genayo, ungenihwa omanaga wisekeleja bho nduhu ugunzugila ijiliwa ungeni okwe ng’wunuyo.

Nose ungeni ng’wunuyo, ubhona ubhujiku bhulingila bho nduhu uguzugilwa ijiliwa, ubadija giki, umayu uyo aliyitya wizang’holo bho golecha luseko lo hanze, gashinaga umugati ya ng’holo yakwe adahayile ungeni alye ijiliwa jakwe.

Ungeni ng’wunuyo, agagema gunhaga ung’wenyeji okwe, kugiki abhone niagushosha ginehe, bho guyomba, ‘mlihoyi unene nashoke kaya.’ Umayu uyo agashosha, ‘sawa dugwibhona lushiku lungi.’ Hunagwene abhanhu bhagandya guyung’witana umayu ng’wunuyo, giki ‘nzuga (nzugila) luseko.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agiyolechaga bho hanze giki ali ng’wizang’holo, aliyo umugati yakwe, ali ming’holo. Umunhu ng’wunuyo agamanaga useka na kuhoya kihamo nu ngeni bho nduhu ugunzugila ijiliwa.

Ulu munhu adatogilwe nulu adahayile ugugwitila ginhu jilebhe idilazima aguwile giki, nadagutogilwe au nadahayile; ugudula gudebha bho shitwa shakwe, guti numo agitila umayu uyo oliombokela ngeni. Hunagwene abhanhu bhagang’witanaga giki, ‘nzuga (nzugila) luseko.’ Lolaga kueneza Injili Kwa Methali, bhukurasa 66.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na wizang’holo bho ng’hana gufumila mu ng’holo jabho, gutinda ugubhiza bhibheleja giki wizang’holo, bho hanze duhu, aliyo bhiming’holo umumioyo yabho, kugiki bhadule gubhagola chiza abhageni bhabho, umuwikaji bhobho.

“Umuwikaji wise ubho ng’wa Kristo, amiito gali na solobho gukila imihayo. UYesu Kristo adayombile mihayo duhu bho nduhu miito. Aliyo wikalaga agubhitilaga ya wiza abhanhu mpaga uduchila ha nsalabha.

Ulu munhu adagutogilwe idilazima aguwile, “Nadagutogilwe” nulu “nadahayile.” Ugudula gumaga bho shitwa shakwe, guti nu kuli nkima uyo adazugaga jilila, aliyo guseka duhu.

Nulu ayise bhakristo ilijidamu noyi ugung’wila UYesu, “Nadagutogilwe”, nulu, nadahayile”. Aliyo dugampejaga bho miito gise mabhi. Dudanzugilaga UYesu Kristo, dugayombaga, “Sebha! Sebha! bho nduhu ugwikala gitumo bhuli ubhulangwa bhokwe.” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 66.

Yakobo 2:15-17.

1Yohane 3:18.

Mathayo 15:8.

Mathayo 7:21.

KISWAHLI: MPIKA KICHEKO.

Hapo zamani alikuwepo mama mmoja aliyeishi katika kijiji fulani. Siku moja alitembelewa na mgeni aliyetoka sehemu za mbali. Mgeni huyo alishikwa na njaa kwa sababu ya kusafiri safari ndefu.

Mama huyo alimpokea mgeni wake wakaanza maongezi yaliyohusu mambo mbalimbali. Katika maongezi hao, mwenyeji wake alikuwa akicheka sana bila kumpikia chakula mgeni wake huyo.

Mwishowe yule mgeni akaona usiku unaingia bila kupikiwa chakula, akagundua kwamba, mama yule anajifanya mkarimu kwa kuonesha kicheko cha nje, kumbe ndani ya moyo wake hataki mgeni huyo ale chakula chake.

Mgeni huyo, aliamua kujaribu kumuaga mwenyeji wake, ili aone kama atakubali au la, kwa kusema, ‘kwa heri mimi narudi nyumbani.’ Mama yule alijibu, ‘sawa tutaonana siku nyingine.” Ndiyo maana watu wakaanza kumuita mama yule, ‘mpika kicheko.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu anayejionesha kwa nje kuwa ni mkarimu, lakini kwa ndani ni mchoyo. Mtu huyo, huwa anacheka na kuzungumumza pamoja na mgeni, bila kumpikia chakula.

Ikiwa mtu hakupendi au hataki kukufanyia jambo fulani si lazima akuambie sikupendi au sitaki; utaweza kujua kwa vitendo vyake, kama alivyofanya yule mama aliyepokea mgeni. Ndiyo maana watu humuita mtu huyo huwa ni ‘mpika kicheko.’ Rejea kueneza Injili kwa methali, ukurasa 66.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na ukarimu wa kweli kutoka mioyoni mwao, badala ya kuwa wanafiki, ambao huuonesha ukarimu kwa nje tu, lakini kwa ndani ni wachoyo, ili waweze kuwatunza vizuri wageni wao, katika maisha yao.

“Katika maisha yetu ya Kikristo matendo yana maana kuliko maneno. Yesu Kristo hakusema maneno tu bila matendo. Bali alikuwa akiwatendea mema watu mpaka katufia msalabani.

Ikiwa mtu hakupendi si lazima akuambie, “Sikupendi” au “sitaki”. Utaweza kujua kwa matendo yake. Kama kwa mwanamke asiyepika chakula, ila kucheka tu. Hata sisi wakristo ni vigumu sana kumwambia Yesu, “Sikupendi”, au “sitaki”. Lakini huwa tunamfukuza kwa matendo yetu mabaya. Hatumpikii Yesu Kristo, tukisema “Bwana! Bwana!”, bila kuishi kadiri ya mafundisho yake.” Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 66.

Yakobo 2:15-17. “Ikiwa ndugu yako au dada hana mavazi wala chakula, mmoja wenu akamwambia, ‘‘Enenda zako kwa amani, ukaote moto na kushiba,’’ pasipo kumpatia yale mahitaji ya mwili aliyopungukiwa, yafaa nini? Vivyo hivyo, imani peke yake kama haikuambatana na matendo, imekufa.”

1Yohane 3:18. “Watoto wangu wadogo, tusipende kwa maneno au kwa ulimi bali kwa tendo na katika kweli.”

Mathayo 15:8. “‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.”

Mathayo 7:21. “Si kila mtu aniambiaye, ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa Mbinguni bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.”

african happy women

adult2

adults

 

ENGLISH: A COOK OF LAUGHTER.

Once upon a time ago there was a woman who lived in a certain village. One day this woman was visited by visitor and this visitor had walked for a long distance and she needed food. The host received her visitor and began conversation on different issues. The host could burst into laughter most of the time. She never thought of cooking for her guest. When the night was about to fall, the guest suggested to leave and the host replied , ‘Good luck, we will meet sometime.’ This why people began calling this host woman as someone who cook laughter.

This saying can be compared to a person who outwardly displays a generous heart, but inwardly, he/she is greedy. These are the people who will laugh and talk without thinking of cooking for their visitors.

If someone doesn’t like you or doesn’t want to do something for you, they don’t have to tell you ‘I don’t like you or I don’t want you;’ you will know by their actions. That’s why people call this host a ‘cook of laughter.’ (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 66). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

The saying teaches people to be genuinely generous from their heart, rather than hypocrites. In so doing, they can take good care of their guests in their lives.

“In our Christian life actions are more meaningful than words. Jesus Christ didn’t just say words without actions. But he was doing good to the people until He died on the cross.

If someone doesn’t love you he/she doesn’t have to tell you, “I don’t like you” or “I don’t want you”. You will know by their actions. As for a woman who does not cook food, only to laugh, even we Christians are very hard to say to Jesus, “I don’t love you”, or “I don’t want you”. But we usually expel Him through our evil deeds. We deny Jesus Christ by saying, “Lord! Lord! ”, without living up to His teachings (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 66).

James 2: 15-17. 1 John 3:18. Matthew 15: 8. Matthew 7:21.

695. WABYALILWA HIKULU.

Ulusumo lunulo, lwandija kubhanhu abho bhagankaribhusha ng’wichabho uyo agabhasanga bhalilya jiliwa bho gung’wila giki, ‘wabyalilwa hikulu.’ Mumho giki, wabyalilwa ha kaya iyo ili najiliwa, nulu hakaya ya ntemi.

“Ikale ulu munhu winhiwa bhutemi nu ubhutemi bhokwe bhubhiza na nzala agupejiwa umubhutemi, nu ulu ijiliwa jubhiza ja shili na ndulu, na gwendelea, ntemi ng’winuyo witanagwa ntemi obhakima. Ulu jiliwa ja bhusiga bhingi, agwitanwa ntemi o “Bhagosha”.

Ulu bhanhu bhumala ugulya bhagatulaga magofi guti numo bhitila ikale abho bhangishaga untemi, mumho giki, bhagasunde ijiliwa, kunguno utemi omalaga gubhita. Bhamalaga ugulya.” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, 64.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na wizang’holo bho gubhakaribhusha abhanhu aha jiliwa jabho, kunguno ijiliwa jili na solobho umugubhulang’hana ubhupanga bho bhanhu bhose.

“Umuwikaji bho munhu ijiliwa nulu ubhugali hi ginhu ja solobho noyi. Ubhugali hu ntemi wise kunguno agadulang’hanijaga ubhupanga wise.

Hangi UMhayo go ng’wa Sebha guli jiliwa ijojigadinhaga bhupanga bho ng’wa Mulungu ng’winikili ubho bhudakenagukaga.

ISakramenti iya Ekaristi jili jiliwa ng’hana na ja solobho noyi ijojibhugalang’hanaga na gubhujamya ubhupanga ubho bhuli bho ng’wa Mulungu umugati yise. “Uyo agulyaga mili gone na gun’gwa mininga gane, agikalaga mugati yane nu nene mugati yakwe.” (Yohana 6:56).

Uluushiga Mukanisa ugunsanga Untemi oko UYesu Kristo, alimo umu shimile sha Ngate umugati ya Tabarnakulo. Adingaga, nulu adabhitaga. Uguzunya gwise ugojigatoliki guliduwila na guduhagigish’ija giki, UYesu Kristo alimo nhana umu shimile sha ngate umu Sakramenti ya Ekaristia. Kuyiniyo, igeleliwe gunamya na gunkuja umu Sakramenti yiniyi Uweyi uyo Ali Ntemi wise bho guntulila mgofi.” Lolaga, Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 65.

Kumbukumbu 8:3.

Yeremia 15:16.

Yohane 4:34.

Yohane 6:11-15.

Yohane 6:51, 57.

Mathayo 6:11.

KISWAHILI: UMEZALIWA IKULUNI.

Methali hiyo, ilianzia kwa watu waliomkaribisha mwenzao aliyewakuta wakila chakula kwa kumwambia kwamba, ‘umezaliwa ikuluni.’ Maana yake amezaliwa kwenye kaya yenye chakula, au kaya ya mtemi.’

“Zamani ikiwa mtu amepewa utemi, na utawala wake ukawa na njaa, atafukuzwa katika utemi, na kama mavuno yatakuwa ya kunde, choroko, na kadhalika, mtemi huyo huitwa mtemi wa wanawake. Kama mavuno ya mtama ni tele, huitwa mtemi wa “Bagosha” wanaume.

Ikiwa watu wamekwisha kula huwa wanapiga makofi kama walivyofanya zamani wakimsalimu mtemi, maana yake wachukue vyombo, kwa kuwa mtemi amekwisha pita. Wamemaliza kula.” Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 64.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na ukarimu wa kuwakaribisha watu kwenye chakula chao, kwa sababu chakula ni muhimu katika kutunza uzima wa mwanadamu wote.

“Katika maisha ya mtu chakula au ugali ni kitu muhimu sana. Ugali ni mtemi wetu kwa kuwa unatutunzia uzima wetu.

Tena Neno la Bwana ni chakula ambacho kinatupa uzima wa Mungu ndani yetu, uzima wa Mungu mwenyewe usioharibika.

Sakramenti ya Ekaristi ni chakula kweli na cha maana sana kinachotunza na kuimarisha uzima ule wa Mungu ndani yetu. “Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, akaa ndani yangu nami ndani yake.” (Yohane 6:56).

Ukifika kanisani utamkuta mtemi wako Yesu Kristo yumo katika maumbo ya mkate ndani ya Tabernakulo. Haondoki au kupita. Imani yetu ya kikatoliki yatujulisha na kutuhakikishia kwamba Yesu Kristo yumo kweli katika maumbo ya mkate katika sakramenti ya Ekaristi. Kwa hiyo yatupasa kumwabudu na kumtukuza katika sakramenti hii yeye aliye mtemi wetu kwa kumpigia makofi.” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 65.

Kumbukumbu 8:3. “Alikudhili na kukufanya uone njaa kisha akulishe kwa mana, ambayo wewe wala baba zako hamkuijua, awafundishe kuwa mwanadamu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila neno litokalo katika kinywa cha BWANA.”

Yeremia 15:16. “Maneno yako yalipokuja, niliyala, yakawa shangwe yangu na furaha ya moyo wangu, kwa kuwa nimeitwa kwa jina lako, Ee BWANA Mungu, Mungu Mwenye Nguvu.”

Yohane 4:34. “Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma na kuikamilisha kazi yake.”

Yohane 6:11-15. “Ndipo Yesu akachukua ile mikate, akamshukuru Mungu na kuwagawia wale watu waliokuwa wamekaa kwa kiasi walichohitaji. Akafanya vivyo hivyo na wale samaki. Kila mtu akapata kadri alivyotaka. Watu wote walipokwisha kula na kushiba, akawaambia wanafunzi wake, “Kusanyeni vipande vilivyobaki vya ile mikate, kisipotee cho chote.’’ Hivyo wakavikusanya wakajaza vikapu kumi na viwili kwa vipande vilivyobaki vya ile mikate mitano na samaki wale wawili wadogo.

Baada ya watu kuona mwujiza ule Yesu aliofanya, walianza kusema, “Hakika huyu ndiye Nabii ajaye ulimwenguni!’’ Yesu akijua kwamba walitaka kuja kumfanya awe mfalme wao, kwa nguvu, akajitenga nao akaenda milimani peke Yake.”

Yohane 6:50- 57. “Lakini hapa kuna mkate utokao mbinguni, ambao mtu ye yote akiula, hatakufa. Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu ye yote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.’’

Ndipo Wayahudi wakaanza kuhojiana vikali wao kwa wao wakisema, “Mtu huyu awezaje kutupatia mwili wake tuule?’’ Hivyo Yesu akawaambia, “Amin, amin, nawaambia, msipoula mwili wa Mwana wa Adamu na kuinywa damu Yake, hamna uzima ndani yenu.

Mtu ye yote aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele. Nami nitamfufua siku ya mwisho. Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli. Ye yote alaye mwili wangu na kunywa damu yangu, atakaa ndani yangu nami nitakaa ndani yake. Kama vile Baba aliye hai alivyonituma Mimi, na kama nami ninavyoishi kwa sababu ya Baba, hivyo anilaye mimi ataishi kwa sababu yangu.”

Mathayo 6:11. “Utupe leo chakula chetu tunachohitaji.”

food woman

food-5

food-4

 

ENGLISH: YOU WERE BORN IN PALACE.

This saying comes from a certain person who arrived at his fellow’s house and found them eating food. As a way to welcome him, they said ‘you were born in palace’ to mean the land of plenty and abundance; a house of the king. In the past, when someone is installed as a king in a certain area he was to ensure that his people do not suffer from hunger and if the harvest will be only crops such as cowpeas, groundnuts and other food crops, he was regarded as a king of women. But if people will manage to have good harvests of crops such as sorghum, he will be regarded as the king of men.

Kings, in the past, were highly respected. This is why people could stand and cheer him up by clapping hands when he passes around. The same to food, people will tend to clap hands when they finish eating, in the same way they used to cheer up their king. In this case, their clapping of hands means calling someone responsible to collect the vessels after they have finished eating. They clap hands to mean that the ‘king has already gone’ Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 64). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

This saying teaches people about the generosity of welcoming people to their food, because food is essential to the wellbeing of the human body and life in general.

“In a person’s life food is the most important thing. Food is our king in that it gives us life.

Again the Word of the Lord is the food that gives us the life of God in us, the life of God Himself who is immortal.

The sacrament of the Eucharist is a true and very important food that sustains and enhances the life of God in us. “Whoever eats my flesh and drinks my blood dwells in me and I in him” (John 6:56).

When you get to the church you will find your Lord Jesus Christ in the form of bread in the Tabernacle. He doesn’t leave. Our Catholic faith informs us and assures us that Jesus Christ is indeed in the form of bread in the sacrament of Eucharist. Therefore, we must worship and glorify in this sacrament. ” (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 65).

Deuteronomy 8: 3. Jeremiah 15:16. John 4:34. John 6: 11-15. John 6:51, 57. Matthew 6:11.

694. WASANGA NTEMI WABHITA.

Ulusumo lunulo, lwandija kuli munhu uyo agabhasanga abhiye bhamalaga ugulya ijiliwa. Umunhu ng’wunuyo, agawilwa giki, ‘wasanga Ntemi wabhita.’ Ukwene, huguhaya giki, wasanga bhamalaga ugulya.

“Ikale untemi uluubhasanga abhanhu bhalihalibhilimga, nulu ha nimo, bhimilaga na gungisha. Aliyo untemi ulubhasanga bhalilya, goli ng’wiko ugwimila na gungisha. Ulunibhangisha niobhaobhalemeja na gubhawila: “Unene nadalang’hanalaga ubhupanga wing’we, ubhugali hugabhulang’hanaga ubhupanga wing’we; hangi bhugalang’hanaga ubhupanga bhone. Unene nadi ntemi wing’we. Ijiliwa, nulu ubhugali hu ntemi wing’we. Idichiza ugunkuja ntemi gulebha ijiliwa.”

Mpaga lelo uluubhasanga bhanhu bhalilya guling’wiko ugwigisha, kunguno bhalihoya na ntemi obho. Ulubhumala ugulya bhagatulaga magofi kugiki bhize gwinja jiseme, mumho giki, untemi omalaga gubhita. Bhamalaga ugulya.” Hunagwene abhanhu bhagandya guyuyomba ukuli munhu uyo osangaga abhiye bhamalaga ugulya, giki, ‘wasanga ntemi wabhita.’ Lolaga kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 64.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gudebha solobho ya jiliwa bhogolecha ikujo, kunguno hijene hijo jigadinhaga nguzu ja gwendelea gwikala na guitumama chiza imilimo yise.

“Umuwikaji bho munhu ijiliwa nulu ubhugali hi ginhu ja solobho noyi. Ubhugali hu ntemi wise kunguno agadulang’hanijaga ubhupanga wise.

Hangi UMhayo go ng’wa Sebha guli jiliwa ijojigadinhaga bhupanga bho ng’wa Mulungu ng’winikili ubho bhudakenagukaga.

ISakramenti iya Ekaristi jili jiliwa ng’hana na ja solobho noyi ijojibhugalang’hanaga na gubhujamya ubhupanga ubho bhuli bho ng’wa Mulungu umugati yise. “Uyo agulyaga mili gone na gun’gwa mininga gane, agikalaga mugati yane nu nene mugati yakwe.” (Yohana 6:56).

Uluushiga Mukanisa ugunsanga Untemi oko UYesu Kristo, alimo umu shimile sha Ngate umugati ya Tabarnakulo. Adingaga, nulu adabhitaga. Uguzunya gwise ugojigatoliki guliduwila na guduhagigish’ija giki, UYesu Kristo alimo nhana umu shimile sha ngate umu Sakramenti ya Ekaristia. Kuyiniyo, igeleliwe gunamya na gunkuja umu Sakramenti yiniyi Uweyi uyo Ali Ntemi wise bho guntulila mgofi.” Lolaga, Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 65.

Kumbukumbu 8:3.

Yeremia 15:16.

Yohane 4:34.

Yohane 6:11-15.

Yohane 6:51, 57.

Mathayo 6:11.

KISWAHILI: UMEKUTA MTEMI AMEPITA.

Methali hiyo ilianzia kwa mtu aliyewakuwa wenzie wamekwisha kula chakula. Mtu huyo, aliambiwa na wenzake hao kwamba, “umekuta mtemi amepita,” Maana yake, amewakuta wamemaliza kula.

“Zamani mtemi akiwakuta watu kwenye mkutano au kazini, walisimama na kumsalimu. Lakini akiwakuta wanakula, ilikuwa mwiko kusimama na kumsalimu. Kama wangelimsalimu, angeliwakataza na kuwaambia: “Mimi situnzi maisha yenu, ugali hutunza maisha yenu; tena hutunza maisha yangu. Mimi si mtemi wenu. Chakula au ugali ni mtemi wenu. Si vizuri kumtukuza mtemi kuliko chakula.”

Mpaka leo ukiwakuta watu wanakula ni mwiko kusalimiana, kwa maana wanaongea na mtemi wao. Wakimaliza kula wanapiga makofi ili waje kuondoa vyombo, maana yake mtemi amekwisha pita. Wamemaliza kula.” Ndiyo maana watu walianza kusema kwa mtu aliyewakuta wamekula, kwamba, ‘umekuta mtemi amepita.’ Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 64.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kutambua umuhimu wa chakula kwa kuonesha heshima kwa sababu, hicho ndicho kinachowapatia uhai, na nguvu za kuendelea kuishi na kufanya kazi zao vizuri.

“Katika maisha ya mtu chakula au ugali ni kitu muhimu sana. Ugali ni mtemi wetu kwa kuwa unatutunzia uzima wetu.

Tena Neno la Bwana ni chakula ambacho kinatupa uzima wa Mungu ndani yetu, uzima wa Mungu mwenyewe usioharibika.

Sakramenti ya Ekaristi ni chakula kweli na cha maana sana kinachotunza na kuimarisha uzima ule wa Mungu ndani yetu. “Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, akaa ndani yangu nami ndani yake.” (Yohane 6:56).

Ukifika kanisani utamkuta mtemi wako Yesu Kristo yumo katika maumbo ya mkate ndani ya Tabernakulo. Haondoki au kupita. Imani yetu ya kikatoliki yatujulisha na kutuhakikishia kwamba Yesu Kristo yumo kweli katika maumbo ya mkate katika sakramenti ya Ekaristi. Kwa hiyo yatupasa kumwabudu na kumtukuza katika sakramenti hii yeye aliye mtemi wetu kwa kumpigia makofi.” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 65.

Kumbukumbu 8:3. “Alikudhili na kukufanya uone njaa kisha akulishe kwa mana, ambayo wewe wala baba zako hamkuijua, awafundishe kuwa mwanadamu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila neno litokalo katika kinywa cha BWANA.”

Yeremia 15:16. “Maneno yako yalipokuja, niliyala, yakawa shangwe yangu na furaha ya moyo wangu, kwa kuwa nimeitwa kwa jina lako, Ee BWANA Mungu, Mungu Mwenye Nguvu.”

Yohane 4:34. “Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma na kuikamilisha kazi yake.”

Yohane 6:11-15. “Ndipo Yesu akachukua ile mikate, akamshukuru Mungu na kuwagawia wale watu waliokuwa wamekaa kwa kiasi walichohitaji. Akafanya vivyo hivyo na wale samaki. Kila mtu akapata kadri alivyotaka. Watu wote walipokwisha kula na kushiba, akawaambia wanafunzi wake, “Kusanyeni vipande vilivyobaki vya ile mikate, kisipotee cho chote.’’ Hivyo wakavikusanya wakajaza vikapu kumi na viwili kwa vipande vilivyobaki vya ile mikate mitano na samaki wale wawili wadogo.

Baada ya watu kuona mwujiza ule Yesu aliofanya, walianza kusema, “Hakika huyu ndiye Nabii ajaye ulimwenguni!’’ Yesu akijua kwamba walitaka kuja kumfanya awe mfalme wao, kwa nguvu, akajitenga nao akaenda milimani peke Yake.”

Yohane 6:50- 57. “Lakini hapa kuna mkate utokao mbinguni, ambao mtu ye yote akiula, hatakufa. Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu ye yote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.’’

Ndipo Wayahudi wakaanza kuhojiana vikali wao kwa wao wakisema, “Mtu huyu awezaje kutupatia mwili wake tuule?’’ Hivyo Yesu akawaambia, “Amin, amin, nawaambia, msipoula mwili wa Mwana wa Adamu na kuinywa damu Yake, hamna uzima ndani yenu.

Mtu ye yote aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele. Nami nitamfufua siku ya mwisho. Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli. Ye yote alaye mwili wangu na kunywa damu yangu, atakaa ndani yangu nami nitakaa ndani yake. Kama vile Baba aliye hai alivyonituma Mimi, na kama nami ninavyoishi kwa sababu ya Baba, hivyo anilaye mimi ataishi kwa sababu yangu.”

Mathayo 6:11. “Utupe leo chakula chetu tunachohitaji.”

food6

ntemi zulu-kingdom-

child eating food

ENGLISH: YOU HAVE FOUND THE CHIEF GONE.

This proverb has its origin from someone who found his fellows had finished eating food. To report to him that they had already eaten food, they told him that “you found the chief gone” meaning that they had finished eating food.

“In the past when the chief walked in for meeting or any business, people around him were to stand up and greet him as a sign of respect. But if the chief reaches a certain place and finds people eating, he was not allowed to stop them from eating. Even if people can stand to greet him he could stop them saying that food keeps peoples’ lives but the chief does not. He (chief) also respects food because it gives him life. Until today, when people are eating they don’t have to speak to each other because they are busy with their chief, food. When they finish eating, they clap hands as a sign of calling the one responsible to collect the vessels used for eating. This is the time one can say ‘the chief has gone’ (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 64). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

The proverb teaches people to recognize the importance of food by showing respect because that is what gives them life and the power to continue living and doing their jobs.

In a person’s life food is the most important thing. Food is our chief in that it gives us life.

Again the Word of the Lord is the food that gives us the life of God in us, the life of God Himself who is immortal.

The sacrament of the Eucharist is a true and very important food that sustains and enhances the life of God in us. “Whoever eats my flesh and drinks my blood dwells in me and I in him” (John 6:56).

When you get to the church you will find your Lord Jesus Christ in the form of bread in the Tabernacle. He does not go away or pass away. Our Catholic faith informs us and assures us that Jesus Christ is indeed in the form of bread in the sacrament of Eucharist. Therefore, we must worship and glorify Him through this sacrament (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 65).

Deuteronomy 8: 3. Jeremiah 15:16. John 4:34. John 6: 11-15. John 6:51, 57. Matthew 6:11.

693. KUGULU KULI NG’OMBE IDAKO ILALIJA.

Ulusumo lunulo, lwingilile muwikaji bho bhanhu bhabhili, abho bhikalaga heke bhuli ng’wene. Uumo olatogilwe kusiminza, uungi olatogilwe gwigasha ha kaya.

Uyo olatogilwe gusiminza, agayela ugapandika milimo, umubhuyeji bhokwe bhunubho. Imilimo yiniyo, igang’wambilija gupandika ng’ombe na sabho ningi. Umunhu ng’wunuyo, agasabha noyi kunguno ya ng’ombe yakwe yiniyo, gwendelea gubyala mpaga nose, ubhiza nsabhi ntale, umuwikaji bhokwe.

Ung’wiye uyo olatogilwe gwigasha hakaya, agamala ijiliwa uyukoyiwa na nzala nhali, ahakaya yake yiniyo. Wiyangula guja gujulomba wambilijiwa ukuli ng’wiye, unsabhi ng’wunuyo.

Ahogambilijiwa bho gwinhiwa jiliwa nu ng’wiye ng’wunuyo, agadebha igiki ubhusiminzi bhuli na solobho nhale, gutinda uwigashi bho aha kaya, ubho bhugenhaga makoye ga nzala. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘Kugulu kuli Ng’ombe idako ilalija.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagasusanyaga ugutumama imilimo. Umunhu ulu wigasha duhu adupandika josejose. Ulu uhaya gupandika ililazima wimile asiminze guja gujuchola. Uluuleka uguchola agulalila. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘Kugulu kuli Ng’ombe idako ilalija.’ Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa bho 62.’

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gugatumila amakanza gabho mugwigulambija gutumama milimo, kugiki bhadule gupandika jiliwa, jiswalo na bhulalo, umuwikaji bhobho.

 “Dulidakiwa dutumame milimo yise ya bhuli lushigu bho bhukamu. Unimo jiliginhu ijojigatulilagwa ikujo na gusungulilwa lubhango nu Mulungu. Ulu dulitumama milimo dulishugulika kihamo nu Mulungu umumilimo yakwe ya gubhumba. Kuyiniyo, imilimo jiliginhu ja solobho noyi umuwikaji bho bhanhu.

Giko dulidakilwa guchola jiliwa ijo jidakenakuguka, ijene hubhupanda ubho ng’wa Mulungu ubho bhugigelaga umu gunzunya Yesu Kristo.

Idinatosha, duchole hangi ijiliwa ija ng’hana ijoduling’hiwa umu Sakramenti ya Bhukaristia.” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, 62-63.

Methali 28:19.

Methali 20:13.

1Wathesalonike 4:11.

Yohane 6:27.

KISWAHILI: MGUU NI NG’OMBE TAKO NI JAA.

Methali hiyo, ilitokea kwenye maisha ya watu wawili waliokuwa na mapendelo tofauti. Mmoja alipenda kutembea, mwingine alipenda kukaa nyumbani.

Yule aliyependa kutembea alifanikiwa kupata kazi katika kutembea kwake. Kazi hiyo, ilimwezesha kupata ng’ombe na mali zingine, katika maisha yake. Kupitia ng’ombe huyo, alifanikiwa kuwa tajiri mkubwa baada ya ng’ombe kuendelea kuzaana zaidi na zaidi.

Yule aliyependa kukaa nyumbani aliishiwa chakula, akawa anasumbuliwa na tatizo la njaa kali katika familia yake. Ikabidi yeye aende kuomba msaada kwa yule tajiri, aliyependa kutembea. Baada ya kupatiwa msaada huo kwa kupewa chakula, alielewa kuwa, kumbe kupembea kunafaida ikiwemo hiyo ya kupata mafanikio hayo, kuliko kukaa nyumbani, ambako kunaleta tatizo la njaa. Ndiyo maana watu wakaanza kusema kwamba, ‘mguu ni ng’ombe, tako ni njaa.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa watu wale ambao wanajishauri kufanya kazi. Mtu akikaa tu hatapata chochote. Akitaka kupata lazima asimame atembee kwenda kutafuta. Asipotafuta atalala akiwa na njaa. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘mguu ni ng’ombe tako ni njaa.’ Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 62.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuutumia muda wao katika kujibidisha kufanya kazi zao za kila siku, ili waweze kujipatia chakula, nguo na malazi, katika maisha yao.

“Yatupasa kufanya kazi zetu za kila siku kwa bidii. Kazi ni jambo linaloheshimiwa na kubarikiwa na Mungu. Tunapofanya kazi tunashughulika na Mungu katika kazi yake ya kuumba. Kwa hiyo, kazi ni kitu cha maana sana katika maisha ya watu.

Vile vile yatupasa kutafuta chakula kisichoharibika, yaani uzima wa Mungu unaopatikana kwa kumwamini Yesu Kristo.

Isitoshe tutafute tena chakula cha kweli tunachopewa katika Sakramenti ya Ekaristi.” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, 62-63.

Methali 28:19. “Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele,  bali afuataye mambo ya upuzi atakuwa na  umaskini wa kumtosha.”

Methali 20:13. “Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.”

1Wathesalonike 4:11. “Jitahidini kuishi maisha ya utulivu, kila mtu akijishughulisha na mambo yake mwenyewe na kufanya kazi kwa mikono yake, kama vile tulivyowaagiza pale awali.”

Yohane 6:27. “Msishughulikie chakula kiharibikacho, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele, ambacho Mwana wa Adamu atawapa. Yeye ndiye ambaye Mungu Baba amemtia muhuri.””

man-traditional one

cows-

nkima6

 

ENGLISH: HE WHO MOVES AROUND WILL GET GOD’S PROVIDENCE, HE WHO STAYS HOME WILL DIE OF HUNGER.

This provrb comes from two individuals with different tastes in life. One of them likes so much moving around while the other one likes staying home. The one who was moving around succeeded to get something that helped him to get more wealth; cows that kept on reproducing to fill his kraal. And the one who used to stay home suffered of hunger in his family. As a result, he had to go beg from his fellow. After managing to get food from his fellow who was moving around, he said ‘he who moves around will get God’s providence, he who stays home will die of hunger’ and that came to be a proverb to warn lazy people.

This proverb can be compared to people who work hard to achieve success in life. If a person does not struggle, there is a danger of affecting the entire family because they can run shortage of food any time (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 62). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

The proverb teaches people to spend their time working hard in their daily activities so that they can provide food, clothing and shelter to their families.

We must work hard in our daily lives. Work is something that God respects and blesses. As we work we are dealing with God in His creative work. Therefore, work is the most important thing in people’s lives.

We must also seek for the imperishable food, the life of God, through the faith of Jesus Christ.

Let us also seek the true food given to us in the Eucharist (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ 62-63).

Proverbs 28:19. Proverbs 20:13. 1Thessalonians 4:11. John 6:27.