heritage

743. OBHUKIJAGA MULI PUNDUKILE.

Olihoyi munhu uyo oliabhuchije jiliwa ja guchala hanhu. Aliyo lulu, ijiliwa jinijo jamanaga jugeha duhu, umu lugendo lokwe. Nose uibhuja bhung’wene, “ni bhuli unigo gone guli geha chiniki?”  Munhu umo uyo alihanuma yakwe ujibhona ijiliwa ijo jidikaga umunzila, ung’wila, “obhukikaja mulipundukile.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatumamaga nimo uyo gudina na solobho yose yose, umuwikaji bhokwe. Umunhu ng’winuyo agajimijaga makanza gakwe bho nduhu solobho, ukunhu alijimala sagala ni nguzu jakwe. Uweyi agamalaga nguzu jakwe bho nduhu gupandika solobho yose yose.

Umunhu ng’wunuyo, agatumamaga nimo uyo gudikilile nu munhu uyo obhukijaga jiliwa jakwe muli ginhu ilo lipundukile, kunguno nuweyi agatumamaga nimo uyo gudina solobho, umukikalile kakwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga umunhu ng’wunuyo giki, “obhukikaja mulipundukile.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kuleka gutumama milimo iyo idina solobho yose yose, kunguno munho bhagujimija makanza gabho sagala. Gashinaga lulu, igelelilwe bhaisolanye imilimo iyo idulile gubhenhela solobho ningi, hunabhayitumame lulu iyiniyo, umuwikaji bhobho.

Hagai 1:6.

Mhubiri 2:11.

Isaya 49:4.

Yeremia 12:13.

Luka 17:10.

1 Wathesalonike 3:5.

Tito 3:9.

Luka 10:38-42.

Luka 16:16-20.

KISWAHILI: UMEBEBEA KWENYE CHOMBO KILICHOTOBOKA.

Alikuwepo mtu aliyebeba chakula akikipeleka sehemu fulani. Lakini, chakula hicho kilikuwa kikizidi kupungua tu katika safari yake hiyo. Mwishowe akaanza kujiuliza mwenyewe, “kwa nini mzigo wangu unazidi kupungua?” Mtu mmoja aliyekuwepo nyuma yake akakiona chakula hicho kilichokuwa kikimwagika, akamwambia, “umebebea kwenye chombo kilichotoboka.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hufanya kazi isiyo na faida yoyote, katika maisha yake. Mtu huyo, hupoteza wakati wake bure, huku akizimaliza hovyo nguvu zake hizo. Yeye huzimaliza nguvu zake hizo kwa kuifanya kazi hiyo kwa muda mrefu na bila faida yoyote.

Mtu huyo, hufananishwa na yule aliyebebea chakula chake kwenye chombo kilichotoboka, kwa sababu naye hufanya kazi isiyo na faida, katika utendaji wake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “umebebea kwenye chombo kilichotoboka.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuacha kupoteza muda wao katika kufanya kazi isiyo na faida yoyote, maishani mwao. Kumbe basi, wanatakiwa kuzifanyia utafiti kazi zao, ili waweze kuzichagua na kuzitekeleza zile zinazowaletea faida katika kuziendeleza familia zao, maishani mwao.

Hagai 1:6. “Mmepanda vingi, lakini mmevuna haba. Mnakula lakini hamshibi, mnakunywa, lakini hamtosheki. Mnavaa nguo, lakini hamsikii joto. Mnapata mishahara, lakini inatoweka kama imewekwa kwenye mfuko uliotoboka toboka.”

Mhubiri 2:11. “Hata hivyo nilipokuja kuangalia yote ambayo mikono yangu ilikuwa imefanya na yale niliyotaabika kukamilisha, kila kitu kilikuwa ni ubatili, ni kukimbizaupepo, hapakuwa na faida yo yote chini ya jua.”

Isaya 49:4. “Lakini nilisema, “Nimetumika bure, nimetumia nguvu zangu bure bila faida. Hata hivyo linalonistahili liko mkononi mwa BWANA, nayo ijara yangu iko kwa Mungu wangu.””

Yeremia 12:13. “Watapanda ngano lakini watavuna miiba, watajitaabisha lakini hawatafaidi cho chote Kwa hiyo beba aibu ya mavuno yako kwa sababu ya hasira kali ya BWANA Mungu.’’”

Luka 17:10. “Vivyo hivyo nanyi mkiisha kufanya mliyoagizwa, semeni, ‘Sisi tu watumishi tusiostahili, tumefanya tu yale tuliyopaswa kufanya.”

1 Wathesalonike 3:5. “Kwa sababu hii nilipokuwa siwezi kuvumilia zaidi, nilimtuma mtu ili nipate habari za imani yenu. Niliogopa kwamba kwa njia fulani yule mjaribu asiwe amewajaribu, nasi tukawa tumejitaabisha bure.”

Tito 3:9. “Lakini jiepushe na maswali ya kipuzi, mambo ya koo, mabishano na ugomvi kuhusu sheria, kwa sababu haya hayana faida tena ni ubatili.”

Luka 10:38-42. “Ikawa Yesu na wanafunzi Wake walipokuwa wakienda Yerusalemu, akaingia kwenye kijiji kimoja ambapo mwanamke mmoja aliyeitwa Martha alimkaribisha nyumbani kwake. Martha alikuwa na mdogo wake aliyeitwa Maria, ambaye yeye aliketi chini miguuni mwa Yesu akisikiliza yale aliyokuwa akisema. Lakini Martha alikuwa akihangaika na maandalizi yote yaliyokuwa yafanyike. Martha akaja kwa Yesu na kumwuliza, “Bwana, hujali kwamba ndugu yangu ameniachia kazi zote mwenyewe? Basi mwambie anisaidie.” Lakini Bwana akamjibu, “Martha,Martha, mbona unasumbuka na kuhangaika na mengi? Lakini kunahitajika kitu kimoja tu. Maria amechagua kile kilicho bora, wala hakuna mtu atakayemwondolea.””

Luka 16:16-20. ‘‘Torati na manabii vilitumiwa mpaka kuja kwa Yohana Mbatizaji. Tangu wakati huo habari njema za Ufalme wa Mungu zinahubiriwa na kila mmoja hujiingiza kwa nguvu. Lakini ni rahisi zaidi mbingu na nchi kupita kuliko hata herufi moja kuondoka katika Sheria. “Mtu ye yote ampaye mkewe talaka na kumwoa mwanamke mwingine azini, naye mwanaume amwoaye mwanamke aliyetalikiwa azini.  ‘‘Palikuwa na mtu mmoja tajiri aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, ambaye aliishi kwa anasa, kila siku. Hapo penye mlango wake aliishi maskini mmoja, jina lake Lazaro, mwenye vidonda mwili mzima.”

water carrying africa

water carrying africa1

bhakima bha madagascar

ENGLISH: YOU HAVE CARRIED IT IN A LEAKY CONTAINER.

There was a man carrying food to a certain place. However, the food he was carrying went on diminishing as he was going. He began wondering by asking himself, “Why is my load becoming lighter?” A man behind him saw the spilled food and said, “You have carried it in a leaky container.”

This proverb is likened with a man who works in vain. Such man wastes his time, as well as his energy. He completes his task by working for a long time and to no avail.

Such person is likened with a person who carries his food in a leaky container. That is why, when making reference to such a person, people say to him, “You have carried it in a leaky container.”

This proverb teaches people how to stop wasting their time doing useless work. Therefore in order to succeed, they need to scrutinise what they are doing so that they can choose and implement those activities that can benefit them for the development of their families, in their lives.

Haggai 1: 6 Ecclesiastes 2:11. Isaiah 49: 4 Jeremiah 12:13. Luke 17:10. 1 Thessalonians 3: 5 Titus 3: 9. Luke 10: 38-42 Luke 16: 16-20.

742. UGUB´INAGA WISAGILILE ULU UKABHONILE UDUKALEKA.

Ulusumo lunulo, lulolile nguno ya ng’wa munhu uyo agub’inaga mbina. Inguno yakwe yiniyo igang’winhaga wisagizu bho gujipandika ijo ajihayile jinijo umubhutumami bhokwe.

Olihoyi munhu uyo ob’inaga mbina kunguno ya kuchola nyiye bhitole. Umunhu ng’wunuyo, agikomeja noyi ub’ina mbina yiniyo, mpaga nose umpandika ung’wiye bhitola, naoya lulu ugub’ina. Hungwene abhanhu bhang’wilaga giki, “ugub’inaga wisagilile ulu ukabhonile udukaleka.”

Ulusumo lununo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatumamaga milimo yakwe na wisagizu bhutale bho gupandika matwajo mingi, umubhutumami bhokwe. Umunhu ng’wunuyo, agikomeja noyi uguitumama imilimo yakwe na bho bhukamu bhutale, kunguno amanile igiki agupandika ijo alijichola.

Uweyi agabhalanjaga na bhanhu bhakwe inzila ja gwikomeja uguitumama imilimo yabho na wisagizu bho gupandika matwajo mingi. Kunzila yiniyo, agapandika amatwajo mingi noyi, umuwikaji bhokwe, ayo gagenhagwa na uwisagizu bhokwe bhunubho, ubho bhugang’winaga nguzu ja gwikomeja kutumama milimo yakwe mpaka ojipandika ijo alijichola.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nu mini ombina uyo ob’inaga na wisagizu bhutale bho gupandika ng’wiye ogwitola nang’hwe mpaka nose umpandika, kunguno nuweyi agatumamaga milimo yakwe na wisagizu bhutale mpaka opandika matwajo mingi umuwikaji bhokwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki,  “ugub’inaga wisagilile ulu ukabhonile udukaleka.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gutumama milimo yabho na wisagizu bho gupandika matwajo mingi, umubhutumami bhobho, kugiki bhadule guitumama imilimo yabho na bhukamu bhutale mpaka bhapandika matwajo gagujibheja chiza ikaya jabho, umuwikaji bhobho.

Mathayo 13:45-46.

Mathayo 10:10.

Mithali 6:23.

1 Wakorintho 9:23-27.

1 Yohana 3:2-3.

Luka 18:28-29.

Sala ya gwisagila

Mathayo 19:27-29.

KISWAHILI: UNACHEZA KWA MATUMAINI KAMA UMEKAONA HUTAKAACHA.

Methali hiyo, huangalia lengo la mtu anayecheza ngoma. Lengo hilo, humpatia matumaini ya kukipata kile anachokitaka, katika utendaji wake wa kazi. Alikuwepo mtu mmoja ambaye alikuwa anacheza ngoma kwa lengo la kumpata mwenzake wa kuoana naye.

Mtu huyo, alijibidisha kucheza ngoma hiyo, mpaka mwishowe akafanikiwa kumpata mwenzi huyo wa maisha, wakaoana, ndipo alipoacha kucheza ngoma hizo. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “unacheza kwa matumaini kama umekaona hutakaacha.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hufanya kazi zake kwa matumaini makubwa ya kupata mafanikio mengi, katika utendaji wake. Mtu huyo, hujibidisha kuzitelekeza vizuri kazi zake hizo, na kwa bidii kubwa kwa sababu anayo matumaini makubwa ya kufanikiwa.

Yeye huwafundisha pia wenzake njia za kujibidisha katika utekelezaji wa majukumu yao, wakiwa na matumaini ya kufanikiwa zaidi. Kupitia njia hizo, yeye pia hupata mafanikio mengi katika maisha yake, yatokanayo na kuwa na matumaini makubwa ambayo humpatia nguvu za kuyatekeleza vizuri majukumu yakwe.

Mtu huyo, hufanana na mcheza ngoma aliyekuwa aliyecheza huku akiwa na matumaini makubwa ya kumpata mwenzi wake wa maisha mpaka akampata, kwa sababu naye huyatekeleza majukumu yake kwa matumaini makubwa ya kufanikiwa kuyafikia malengo yake, maishani mwake. Ndiyo maana watu, humwambia kwamba, “unacheza kwa matumaini kama umekaona hutakaacha.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuyatekeleza majukumu yao wakiwa na matumaini makubwa ya kufanikiwa katika utendaji wao, ili waweze kuongeza bidii ya kuwapatia mafanikio ya kuziendeleza vizuri familia zao, maishani mwao.

Mathayo 13:45-46. ‘‘Tena, Ufalme wa Mbinguni unafanana na mfanya biashara aliyekuwa akitafuta lulu safi. Alipoipata lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza vyote alivyokuwa navyo akainunua.”

Mathayo 10:10. “Msichukue mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala jozi ya pili ya viatu, wala fimbo, kwa maana mtenda kazi anastahili posho yake.”

Mithali 6:23. “Kwa maana maagizo haya ni taa, mafundisho haya ni mwanga na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,”

1Wakorintho 9:23-27. “Nafanya haya yote kwa ajili ya Injili, ili nipate kushiriki baraka zake. Je, hamjui kwamba katika mashindano ya mbio wote wanaoshindana hukimbia, lakini ni mmoja wao tu apewaye tuzo? Kwa hiyo kimbieni katika mashindano kwa jinsi ambavyo mtapata tuzo. Kila mmoja anayeshiriki katika mashindano hufanya mazoezi makali. Wao hufanya hivyo ili wapokee taji isiyodumu, lakini sisi tunafanya hivyo ili kupata taji idumuyo milele. Kwa hiyo mimi sikimbii kama mtu akimbiaye bila lengo, sipigani kama mtu anayepiga hewa, la, bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha ili nikishawahubiria wengine, mimi nisiwe mtu wa kukataliwa.”

1 Yohana 3:2-3. “Wapenzi, sasa tu watoto wa Mungu, lakini bado haijadhihirika tutakavyokuwa, lakini twajua ya kwamba, Yeye atakapodhihirishwa, tutafanana naye, kwa maana tutamwona kama alivyo. Kila mmoja mwenye matumaini haya katika Yeye hujitakasa, kama vile Yeye alivyo mtakatifu.”

Luka 18:28-29. “Ndipo Petro akasema, “Tazama, tumeacha vyote tulivyokuwanavyo tukakufuata!” Yesu akajibu, “Amin nawaambia, hakuna hata mmoja aliyeacha nyumba yake, au mke, au ndugu, au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu”

Sala ya matumaini

Mathayo 19:27-29. “Ndipo Petro akamjibu, ‘‘Tazama, sisi tumeacha kila kitu na kukufuata, tutapata nini basi?’’ Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia , wakati wa kufanywa upya vitu vyote, wakati mwana wa Adamu atakapoketi kwenye kiti chake cha utukufu cha enzi, ninyi mliomfuata pia mtaketi katika viti vya enzi kumi na viwili, mkiyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli. Kila mmoja aliyeacha nyumba au ndugu zake wa kiume au wa kike au baba au mama au watoto au mashamba kwa ajili Yangu, atapokea mara mia zaidi ya hayo na ataurithi uzima wa milele.”

man dance botswana

dancers

people-

ENGLISH: YOU DANCE WITH A GOAL TO ACHIEVE.

This proverb focuses on the goal of the dancer. The goal that gives him some hope of achieving what he wants, in his career. There was one man who was dancing with the intention of finding a mate to marry him.

He danced until he finally managed to find the life partner. They got married, and then he stopped dancing. Of such a person, people woud “You dance with a goal to achieve, unless you realise it, you will not stop.”

This proverb is likened with a man who performs his duties with high hopes of achieving great success. Such person never loses hope because he expects to achieve something great.

He also teaches his colleagues how to work hard when discharging their duties. Through these means, he realises many successes in life, because he has high anticipations something that gives him strength to carry out his responsibilities effectively.

The above man is like the dancer who played with high expectations of finding his life partner until he found her. He succeeded because he fulfilled his responsibilities with the great hope of achieving his goal. That’s why, when people people make reference to people like that they would say, “You dance with a goal to achieve, unless you realise it, you will not stop.”

This proverb teaches people on how to fulfill their responsibilities with high anticipations of succeeding

Matthew 13: 45-46 Matthew 10:10 Proverbs 6:23. 1 Corinthians 9: 23-27 1 John 3: 2-3. Luke 18: 28-29 Prayer of hope, Matthew 19: 27-29.

741. BHAGOYANGI BHADINA MBINA NDO.

Akahayile kenako, kalolile bhabhini bha mbina abho bhagitanagwa bhagoyangi. Abhabhini bhenabho, bhagafunyama nzoka ulu bhandya ugubhina mbina jabho. Abhanhu bhenabho, bhaga muchalo jilebhe bhugajifunya nzoka jabho jinijo, aliyo bhali hoyi bhanhu bhadadu duhu ahenaho.

Hunagwene abhanhu aho bhabhona chene bhagayomba giki, “bhagoyangi bhadina mbina ndo.” Ubhunubho huna bhub’iza wandijo bho kahayile kenako, kunguno, abhab’ini abhangi bhagafunyaga nzoka ulu bhanhu bhukwila aha mbina yiniyo.

Akahayile kenako, kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatumilaga nguzu ningi, ku jikolo jidoo, nulu umugutumama nimo ndoo, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, adulile nulu gubhucha ngong’ho gujupigila mhumbi, kunguno adadebhile ugulinganija ijilanga jakwe ni ndimu iyo aligibhulaga. Uweyi agatumamaga imilimo yakwe gitumo alitogelwa, kunguno ya wangu bhokwe bho gupelana, umuwikaji bhokwe.

Umunhu ng’wunuyo agikolaga na bhagoyangi abho bhagafunyaga nzoka ulu bhandya ugubhina nulu bhagab’iza bhalihoyi bhanhu bhatatu du hoyi, kunguno nuweyi agatumilaga nguzu ningi nulu alitumama nimo ndoo duhu. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki,  “bhagoyangi bhadina mbina ndo.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya gubhiza na masala ga gulinganija chiza imiliimo yabho, umukikalile kabho, kugiki bhadizumala nguzu jabho sagala, umuwikaji bhobho.

Mathayo 18:20.

Mathayo 13:31.

KISWAHILI: WAGOYANGI HAWA NA NGOMA NDOGO.

Msemo huo, ulianzia kwa wacheza ngoma wanaoitwa wagoyangi. Wagoyangi hayo ni wana mchezo wa ngoma ya kutumia nyoka. Watu hao, huwatoa hao nyoka wanapoanza tu kucheza. Hivyo, watu hao walifika kwenye kijiji kimoja, ambapo waliwatoa nje hao nyoka nje wakati watu waliokuwepo hapo walikuwa wawili tu.

Ndiyo maana watu walipoona hivyo, walisema, “wagoyangi hawana ngoma ndogo.” Huo ndiyo ukawa mwanzo wa msemo huo, kwa sababu wachezaji wa makundi wengine, husubiri mpaka wawepo watu wengi zaidi, ndipo hufikia hatua ya kuwatoa nje hayo nyoka.

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hutumia nguvu kubwa kwenye kitu kidogo, katika maisha yake. Mtu huyo, aweza hata kuchukua bunduki kwenda kuulia panzi, kwa sababu yeye hajui kulinganisha silaha zake na kitu anachoenda kukiua, maishani makwe.  Yeye hufanya kazi zake kwa kadiri anavyotaka, kwa sababu ya wepesi wake wa kukasilia.

Mtu huyo, hufanana na wagoyangi ambao hutoa nyoka nje kata kama kuna watu watatu tu kwenye ngoma yao, kwa sababu naye hutumia nguvu kubwa kwenye kazi ndogo, pia hukasilishwa hata na jambo dogo zaidi. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “wagoyangi hawana ngoma ndogo.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuwa na akili ya kuwawezesha kutumia nguvu inayolingana na kazi wanazozifanya, katika maisha yao, ili wasizipoteze bure nguvu zao, maishani mwao.

Mathayo 18:20. “Kwa kuwa wanapokusanyika pamoja watu wawili au watatu kwa jina langu, mimi niko papo hapo pamoja nao.””

Mathayo 13:31. “Akawaambia mfano mwingine, akasema, “Ufalme wa Mbinguni ni kama punje ya haradali, ambayo mtu aliichukua akaipanda shambani mwake.””

wagoyangi africa

south-africa2

wagoyangi samburu

740. LYAB´IMBILILE HAB´I.

Ulusumo lunulo, lwingilile kuli munhu uyo agab’imbila lib’ute, kulwande lo mili gokwe ulo adadulile uguloyomba sagala. Ilib’ite linilo, lyalib’imbilile kulwande lo mbisila yakwe. Uweyi agacha soni uguyomba hab’utongi bho bhanhu aho lib’ilimbile. Hunagwene agayomba bho mbisila giki, “lyab’imbilile hab’i.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo opandikile ikoye itale umuwikaji bhokwe, ilo adadulile ugulimala ubho gutumila nguzu yakwe duhu. Umunhu ng’wunuyo, agalombaga wambilijiwa bho gufumila kubhiye na kuli Mulungu uyo adulile gung’wingija wangu ilikoye linilo. Uweyi adebhile igiki uwambilijiwa bhunubho, bhudulile gulimala ilikoye lyakwe linilo.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo oliob’imbila lib’ute litale kulipande lya mili gokwe ilo agabhona soni uguliyomba sagala, kunguyo nuweyi ligankoyaga mpaka olomba wambilijiliwa, bho dugula gulyinja ilikoye lwakwe linilo. Hunagwene nang’hwe agabhawila abhanhu giki, “lyab’imbilile hab’i.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gub’iza na masala ga gwiyumilija umumakoye ayo bhalinago, na gulomba wambilijiwa bho gugamala wangu amakoye genayo, kugiki bhadule gwikala chiza na bho mholele na bhichabho, umuwikaji bhobho.

1Wakorintho 12:20-31.

KISWAHILI: LIMEVIMBIA PABAYA.

Methali hiyo, ilianzia kwa mtu aliyevimba jipu katika sehemu ya mwili wake ambayo hawezi kuitaja hovyo, kwa sababu ya kuona aibu. Jipu hilo, lilivimbia kwenye sehemu zake za siri. Yeye hujikia aibu kuitaja mbele za watu sehemu hiyo. Ndiyo maana yeye huitaja kwa mafumbo akisema, “limevimbia pabaya.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule aliyepata tatizo kubwa maishani mwake, ambalo hawezi kulitatua kwa kutumia uwezo wake tu. Mtu huyo huomba msaada kutoka kwa wezake na kwa Mungu awezaye kumtatulia tatizo hilo. Yeye anaelewa kwamba, msaada huo unaweza kulitatua kwa haraka tatizo lake hilo.

Mtu huyo hufanana na yule aliyevimba jipu kwenye sehemu zake za siri akashindwa kuitaja mbele za watu sehemu hiyo kutokana na kuona aibu, kwa sababu naye alishindwa kulitatua tatizo lake hilo mpaka akaomba msaada kutoka kwa wenzake na kwa Mungu mwenye uwezo wa kulitatua tatizo hilo kwa haraka. Ndiyo maana naye alisema kwamba, “limevimbia pabaya.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na akili ya kuvumilia matatizo na kuomba msaada wa kuweza kuyatatua, ili waweze kuishi vizuri na kwa amani na wenzao, maishani mwao.

1Wakorintho 12:20-31. “Kama ulivyo, kuna viungo vingi, lakini mwili ni mmoja. Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sina haja nawe!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sina haja na ninyi!” Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana. Navyo vile viungo vya mwili tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee. Wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa, ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane usawa kila kimoja na mwenzake. Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho, kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho. Sasa ninyi ni mwili wa Kristo na kila mmoja wenu ni kiungo. Mungu ameweka katika kanisa, kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za masaidiano, karama za maongozi, aina mbalimbali za lugha. Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanafanya miujiza? Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri? Basi tamanini sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.”

malawi1

malawi3

malawi4

ENGLISH: I HAVE AN ABCESS SWOLLEN AT A BAD PLACE.

This proverb began with a man who had a boil on a part of his body that he could not mention because he felt embarrassed to do so. For sure, this abscess was on his genitals. So he felt ashamed to mention it in public. That is why he spoke using a proverb saying that “I have an abscess swollen on a bad place.”

This proverb is likened with a man who has a serious problem in his life which he cannot solve by simply relying only on his own strengths. Such a person will have to ask for help from his peers and from God who can solve the problem. He understands that such support can quickly solve his problem.

This man is like the one who had a swollen boil on his genitals but failed to show it in public because he was ashamed. This person failed to solve his problem until he asked for help from his colleagues and from God who was able to solve it very quickly.

This proverb teaches people how to have stability to endure problems and ask for help to solve them, so that they can live peacefully with others.

1 Corinthians 12: 20-31.

739. IYIB´IMBILE NOMO IDULEMEJA B´IYE GUDIMA.

Ulusumo lunulo, lulolile ng’ombe iyo ibhimbilile nomo. Ing’ombe yiniyo, igadumaga ugulya amaswa kunguno ya bhubhimbi bho nomo goyo gunuyo. Olihoyi ndimi ong’ombe uyo agajilugalila pye mulugutu kunguno ya ing’ombe imo iyo yali ya bhimba nomo.

Ung’wiye ugamuuja, “nibhuli ojilugalilaga mulugutu ing’ombe aliyo ilimi lyakulaga?” Uweyi agashosha, “ilihoyi ng’ombe imo iyo yabhimbaga nomo idudula ugulya amaswa.” Ung’wiye unshokeja, “iyib’imbile nomo idulemeja b’iye gudima.” Ubhunubho nab’ib’iza wandijo bho gutumama go lusumo lunulo.

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagadumaga nulu gulya jiliwa, hamo nulu gutumama milimo yabho, kunguno ya ng’wichabho umo uyo agusataga. Abhanhu bhenabho, bhagasunduhalaga noyi mpaga bhaduma ugupandika ijiliwa ijo jigabhinaga nguzu ja gutumamila milimo yabho chiza.

Abhanhu bhenabho bhagikolaga nu munhu uyo agaleka ugujichala ing’ombe jakwe ukwidima kunguno ya ng’ombe yakwe imo iyo yaliyabhimba nomo, iki nabho bhagadumaga ugulya nulu gutumama milimo kunguno ya gusatilwa na munhu obho umo. Hunagwene abhanhu bhagabhawilaga giki, “iyib’imbile nomo idulemeja b’iye gudima.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kubhiza na wiyumilija bho gutumama milimo yabho, ulu bhalina makoye abhichacho, kugiki bhadule kupandika matwajo mingi ga gubhambilija ijinagubhulang’hana chiza ubhupanda bhobho.

Hangi lobhalanga abhanhu abho bhali na makoye kuleka ugubhamaja lubhango abhichabho, umubhasatu bhobho. Giko lulu, amakoye gabho, gadizubhiima lubhango abhichabho, umuwikaji bhobho.

Luka 15:25-31.

Zaburi 73:1-12.

Waefeso 2:4-10.

KISWAHILI: ALIYEVIMBA MDOMO HAWAZUII WANZAKE KULA MAJANI.

Methali hiyo huangalia ng’ombe aliyevimba mdomo. Ng’ombe huyo, hushindwa hata kula majani kwa sababu ya kuvimba mdomo wake. Alikuwepo mtu mmoja aliyekuwa mchungaji wa ng’ombe.

Mtu huyo aliwafungia zizini ng’ombe wote kwa sababu ya ng’ombe wake mmoja kuwa na tatizo la kuvimba mdomo wake. Mwenzake akamuuliza, “kwa nini hujawafungulia ng’ombe kwenda kuchunga hadi sasa?”

Yeye alijibu, “kuna ng’ombe mmoja amevimba mdomo, hivyo hawezi kula majani.” Mwenzake huyo akamjibu, “aliyevimba mdomo hawazuii wenzake kula majani.” Huo ndio ukawa mwanzo wa kutumika kwa methali hiyo.

Methali hiyo, hulinganishwa kwa watu wale ambao hushindwa hata kula au kufanya kazi zao, eti kwa sababu ya mtu mmoja kuugua, au kupata tatizo fulani. Watu hao, huhudhunika sana mpaka hufikia hatua ya kushindwa kujipatia mahitaji yao ya kila siku yakiwemo yale ya chakula, kwa sababu ya kuugua kwa mtu mwenzao. Wao hushindwa hata kufanya kazi za kuwapatia chakula, kwa sababu ya tatizo la mtu mmoja.

Watu hao, hufanana na mtu yule ambaye aliacha kuwafungulia ng’ombe wake kwenda malishoni kuchunga, eti kwa sababu ya ng’ombe mmoja kuvimba mdomo wake, kwa sababu na wao, hushindwa kuyatekeleza vizuri majukumu yao, kutokana na mmoja wao kupata tatizo fulani. Ndiyo maana watu huwaambia kwamba, “aliyevimba mdomo hawazuii wenzake kula majani.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na uvumilivu wa kuwawezesha kutimiza majukumu yao ya kuulinda na kuuendeleza uhai wao, hata kama kuna mmoja wao ambaye ana tatizo, ili waweze kujipatia mahitaji yao ya kila siku, maishani mwao.

Methali hiyo, pia huwafundisha watu wenye matatizo kutowafanya wenzao walio wazima, wakose raha au wahudhunike kipita kiasi kwa sababu ya kujidekeza kwao. Hivyo, matatizo yao yasiwazuie wengine kufurahi, maishani mwao.

Luka 15:25-31. “Wakati huo, yule mwana mkubwa alikuwa shambani. Alipokaribia nyumbani, akasikia sauti ya nyimbo na watu wakicheza. Akamwita mmoja wa watumishi na kumwuliza, ‘Kuna nini?’ Akamwambia, ‘Mdogo wako amekuja, naye baba yako amemchinja ndama aliyenona kwa sababu mwanawe amerudi nyumbani akiwasalama na mzima.’ Yule mwana mkubwa akakasirika, akakataa kuingia ndani. Basi baba yake akatoka nje na kumbembeleza. Lakini yeye akamjibu baba yake, ‘Tazama! Miaka yote hii nimekutumikia na hata siku moja sijaacha kutii amri zako, lakini hujanipa hata mwana mbuzi ili nifurahi na rafiki zangu. Lakini huyu mwanao ambaye ametapanya mali yako kwa makahaba aliporudi nyumbani, wewe umemchinjia ndama aliyenona!’

“Baba yake akamjibu, “ ‘Mwanangu, umekuwa nami sikuzote na vyote nilivyo navyo ni vyako. Lakini ilitubidi tufurahi na kushangilia kwa sababu huyu mdogo wako alikuwa amekufa na sasa yu hai, alikuwa amepotea naye amepatikana.’ ”

Zaburi 73:1-12. “Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi. Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza, nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama. Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu. Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu. Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo na wanadamu. Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri. Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, ubaya wa majivuno kutoka mioyoni mwao hauna kikomo. Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa. Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani. Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele. Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?’’ Hivi ndivyo walivyo waovu, sikuzote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.”

Waefeso 2:4-10. “Lakini Mungu, kwa upendo Wake mwingi kwetu sisi, ambaye ni mwingi wa rehema, hata tulipokuwa wafu kwa ajili ya makosa yetu, alitufanya tuwe hai pamoja na Kristo Yesu, yaani, mmeokolewa kwa neema. Mungu alitufufua pamoja na Kristo na kutuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho katika Kristo Yesu, ili katika ule ulimwengu ujao apate kuonyesha wingi wa neema Yake isiyopimika, iliyodhihirishwa kwetu kwa wema Wake ndani ya Kristo Yesu. Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani, wala hii si kwa matendo yenu mema. Hii ni zawadi kutoka kwa Mungu, si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu. Kwa maana sisi ni kazi ya mikono ya Mungu, tulioumbwa katika Kristo Yesu, ili tupate kutenda matendo mema, ambayo Mungu alitangulia kuyaandaa tupate kuishi katika hayo.”

cow-1

cow2

cows-

ENGLISH: A COW WITH A SWOLLEN MOUTH CANNOT PREVENT OTHERS FROM EATING GRASS.

This proverb focuses on a cow with a swollen mouth. Such a cow is unable to eat grass because of the swelling on its mouth. There was a man who was a herdsman.

The man locked all the cows in the cow shed because one of his cows had a swollen mouth therefore it was unable to eat grass. Seeing that he had locked all of his cattle in the shed, his companion asked him, “Why haven’t you allowed the cattle to go to graze up to this moment?”

He replied, “One cow has a swollen mouth, so she can’t eat grass.” His companion replied, “”a swollen mouth of one cow cannot prevent others from eating grass.” That was the beginning of the proverb.

The proverb is likened with a person who loses his ability to eat or work, perhaps because of a physical ailment or a malady. When it happens that their fellow is sick these, people are so depressed that they fail to provide for their daily needs, including food, because of the illness of a fellow human being.

These people are like the man who stopped taking his cattle to the grazing place because one of the cows had a swollen mouth which was preventing her from eating. That is why people tell the people with such a character, “a cow with a swollen mouth cannot prevent others from eating grass.”

This proverb teaches people about patience that will enable them to fulfill their responsibilities enough to protect and sustain their lives, even if one of them has a problem.

This proverb also teaches people who have problems not to make their peers miserable, uncomfortable or overwhelmed with their self-esteem. Thus, their problems should not prevent others from enjoying life.

Luke 15: 25-31.

Psalm 73: 1-12.

Ephesians 2: 4-10.