Folklore

667. SHIHILE/JIPILE SHITABHELAGA NDA.

Imbuki ya lusuno lunulo, yilolile jiliwa jizugile ijo jidatumlaga Nda ya ng’wa munhu uyo ojilyaga. Ijiliwa jinijo, jidikalaga wikanza ilihu umunda ya ng’wa munhu uyo ojilyaga, kunguno jigafuma wangu guti minzi. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘shihile/jipile shitabhelaga Nda.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo ali nevi, nulu ng’wii o walwa, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, adulile nulu gujimalila ihela jakwe bho gujigulila walwa bho gung’wa, kunguno ya bhulevi bhokwe bhunubho. Uweyi adatumamaga chiza imilimo ya ha ng’wakwe, kunguno ya gwikala aguyungaga sagala mumawalwa.

Umunhu ng’wunuyo, agakoyiyagwa na nzala akaya yakwe, kunguno ya kugaiyawa ijiliwa aha ng’wakwe henaho. Uweyi agikomejaga gung’wa walwa duhu bho nduhu guidilila ikaya yakwe yiniyo.

Giko lulu, ulu udahilwa uwalwa bhunubho na gwinhilijiwa, agayombaga giki, ‘bhudabhelaga Nda,’ kunguno ulu ubhung’wa agwikala ikanza iguhi, wandya gusubhala. Hunagwene agayombaga giki, ‘shihile/jipile shitabhelaga Nda.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya guleka bhulevi bho gung’wa walwa umukikalile kabho, kugiki bhadule gwigulambija gutumama milimo iyo idulile gubhapandikalila matwajo gagujibheja chiza ikaya jabho, umuwikaji bhobho.

Marko 7:14.

Yohana 2:1-12.

KISWAHILI: VILIVYOIVA HAVIPASUI TUMBO.

Chanzo cha methali hiyo, chaangalia chakula kilichoiva ambacho hakipasui tumbo la mlaji wake. Chakula hicho, hakikai kwa muda mrefu tumboni mwa mtu yule aliyevila, kwa sababu huwa vinatoka kama maji. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘vilivyoiva havipasui tumbo.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ni mlevi wa pombe, katika maisha yake. Mtu huyo, huweza hata kuzimalizia pesa zake kwa kuzinunulia pombe za kunywa, kwa sababu ya ulevi wake huo. Yeye hafanyi vizuri kazi za nyumbani kwake, kwa sababu ya kutumia muda wake kuzurura hovyo kwenye vilabu vya pombe.

Mtu huyo, husumbuliwa na jaa kwenye familia yake kwa sababu ya kukosa chakula. Yeye huendelea kunywa pombe bila kuijali familia yake hiyo, katika maisha yake.

Hivyo, yeye akichotewa pombe hiyo, na kupewa husema kwamba, ‘haupasui tumbo,’ kwa sababu akiinywa hubaki tumboni kwa muda mfupi, na kuanza kutoka kwa njia ya mkojo. Ndiyo maana yeye husema kwamba, ‘vilivyoiva havipasui tumbo.’

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuacha ulevi wa kunywa pombe, katika maisha yao, ili waweze kujibidisha kufanya kazi zinazoweza kuwapatia mafanikio ya kuziendeleza vizuri familia zao, maishani mwao.

Marko 7:14.

Yohana 2:1-12.

food4

food-3

food tamarind

ENGLISH: COOKED FOOD WILL NEVER CAUSE THE STOMACH TO BURST.

The source of this proverb is food and its eater. The food when eaten, it does not stay long in the eater’s stomach rather it is taken out in a different form through the process of excretion. This is why people came with this proverb that ‘cooked food will never cause the stomach to burst.’

This proverb can be compared to an alcoholic person who spends much of his/her money on alcohol. This person can fail to do most of his/her activities and eventually can suffer from famine. When asked why spending much time in alcohol he/she can say that he/she won’t be affected by it because finally it goes out of his/her stomach.

The proverb teaches people about avoiding taking much alcohol in their lives. Rather, people have to commit themselves to activities that can make them successful in life.

Mark 7:14. John 2: 1-12.

666. NG´WIZA ADAGAYIYAGWA JIKA.

Imbuki ya lusumo lunulo, yilolile jika ja ng’wa munhu uyo owiza. Umunhu ng’wunuyo, ali na nhungwa jawiza, nuweyi ali owiza umukikalile kabho. Aliyo lulu, bhalihoyi nabho bhagidumaga nawe, abho bhadantogagwa hamo kunguno ya bhukali bhokwe. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘ng’wiza adagayiyagwa jika.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agajikalana inhungwa ijawiza, aliyo lulu, alina bhanhu abho bhagamonelaga jika, umuwikaji bhokwe. Umunhu ng’wunuyo, agitaga iyawiza ukubhiye, bho bhutogwa ubho bhuli bho nghana umu ng’holo yakwe.

Uweyi agiyumilijaga uguitumama imilimo yakwe bho wigulambija bhutale, umukikalile kakwe. Gashinaga, umunhu nulu agab´iza o wiza aliyo jigwigela duhu ijika ija guleka guntogwa abhangi.

Umunhu ng’wunuyo, alijigemelo ja gwikala na bhanhu chiza ukubhiye, kunguno ya kikalile kakwe kenako, ako kagolechaga wiyumilija ahikanza lya gubyedwa na bhanhu abho bhagamhonelaga jika. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, ‘ng’wiza adagayiyagwa jika.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na wiyumilija bho gujikalana inhungwa ijawiza, umuwikaji bhobho, kugiki bhadule gupandika matwajo agagujibheja chiza ikaya jabho, umukikalile kabho.

Mithali (Hekima) 2:1ª, 12-22.

KISWAHILI: MZURI HAKOSI KASORO.

Chanzo cha methali hiyo, chaangalia kasoro ya mtu yule ambaye ni mzuri. Mtu huyo, ana sura nzuri na tabia njema, lakini basi, kuna baadhi ya watu wanaokosana naye, ambao humuona kuwa ana kasoro ya ukali. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘mzuri hakosi kasoro.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huyaishi maadili yaliyomema, lakini baadhi ya watu humuona kuwa ana kasoro, maishani mwake. Mtu huyo hutenda wema unaotoka ndani ya moyo wake ambao una upendo wa kweli.

Yeye huvumilia katika utekelezaji wa majukumu yake, ambayo huyakamilisha kwa bidii kubwa, katika maisha yake. Pamoja na yeye kuwa na tabia hiyo njema, baadhi ya watu hutafuta kasoro ya kuwafanya wasimpende.

Mtu huyo, ni mfano wa kuigwa na wenzake katika kuishi vizuri na watu, kwa sababu ya mwenendo wake ambao huonesha uvumilivu hata wakati ule anapodharauliwa na watu wanaongalia kasoro yake, badala ya wema wake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, ‘mzuri hakosi kasoro.’

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na uvumilivu wa kuendelea kuyaishi maadili yaliyo mema, katika maisha yao, ili waweze kupata mafanikio ya kuziendeleza vyema familia zao, maishani mwao.

Mithali (Hekima) 2:1ª, 12-22.

kind one

kind one1

kind one2

 

ENGLISH: NO ONE IS PERFECT.

The source of this proverb is the faults that can bee seen in someone assumed to be perfect in his/her doings. There are people in the society who are considered to be perfectionists. Such people are likely to fall in danger of being scrutinized by others to see how they can commit mistakes. When they spot even a single mistake in him/her they will publicize it in order for people to know the other side of that particular person. This is why people came with the proverb ‘no one is perfect’ to describe this scenario.

 This proverb can be compared to someone who lives a good life. Such a person is likely to be looked at by others in relation to how he/she can commit mistakes. A person of this nature can be very organized in his/her duties despite others looking for his/her flaws. He/she appears to be a role model to others because of the way he/she is patient in his/her execution of duties.

This proverb teaches people to have patience in life and continue living the right values in their lives. In so doing, they will be successful in improving their families in their lives.

Proverbs (Wisdom) 2: 1ª, 12-22.

665. NULU UGABHELA NO BHADUGUTOGWA BHOSE.

Imbuki ya lusumo lunulo, yilolile wikaji bho wiza na bhanhu. Uwikaji bhunubho, bhuli bho ng’wa munhu uyo ali na nhungwa jawiza, uyo bhadantogagwa abha nhungwa jabhubhi, umukikalile kabho. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘nulu ugabhela no bhadugutogwa bhose.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo alina wiyumilija bho gujikalana inhungwa ijawiza, umuwikaji bhokwe. Umunhu ng’wunuyo, adebhile uguita iyawiza ukubhiye, bho bhutogwa ubho bhuli bho nghana umu ng’holo yakwe. Uweyi agiyumilijaga uguitumama imilimo yakwe bho wigulambija bhutale, umukikalile kakwe.

Umunhu ng’wunuyo, alijigemelo ja gwikala na bhanhu chiza ukubhiye, kunguno ya kikalile kakwe kenako, ako kagolechaga wiyumilija ahikanza lya gubyedwa na bhanhu abho bhali nhungwa ja bhubhi. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, ‘nulu ugabhela no bhadugutogwa bhose.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na wiyumilija bho gujikalana inhungwa ijawiza, umukikalile kabho, kugiki bhadule gupandika matwajo agagujibheja chiza ikaya jabho, umuwikaji bhobho.

Mithali (Hekima) 2:1ª, 12-22.

KISWAHILI: HATA UKIWA MZURI MNO HAWATAKUPENDA WOTE.

Chanzo cha methali hiyo, chaangalia namna ya kuishi vyema na watu. Maisha hayo, ni ya mtu mwenye tabia njema, ambaye watu walio na tabia mbaya humchukia, maishani mwao. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘hata ukiwa mzuri mno hawakakupenda wote.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule aliye na uvumilivu wa kuyaishi maadili yaliyomema, maishani mwake. Mtu huyo, anafahamu kutenda wema unaotoka ndani ya moyo wake ambao una upendo wa kweli. Yeye huvumilia katika utekelezaji wa majukumu yake, ambayo huyakamilisha kwa bidii kubwa, katika maisha yake.

Mtu huyo, ni mfano wa kuigwa na wenzake katika kuishi vizuri na watu, kwa sababu ya mwenendo wake ambao huonesha uvumilivu wakati anapodharauliwa na watu walio na nia mbaya. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, ‘hata ukiwa mzuri mno hawakakupenda wote.’

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na uvumilivu wa kuendelea kuyaishi maadili yaliyo mema, katika maisha yao, ili waweze kupata mafanikio ya kuziendeleza vyema familia zao, maishani mwao.

Mithali (Hekima) 2:1ª, 12-22.

good people

good people.jpg1

good people.jpg2

 

ENGLISH: YOUR BEAUTY DOES NOT MEAN TO BE LOVED BY ALL PEOPLE.

The source of this saying is the way to live with people. Under normal circumstances in life, good people tend to be hated by the bad ones. This is why people came with this saying that ‘your beauty does not mean to be loved by all people.’

This saying can be compared to a person who has the patience to live the good values ​​in his/her life. This person knows how to do good things from his/her heart. Such a person can tend to complete his/her tasks within the given time. In so doing, these people become role models to others who would wish to be the same as them. In contrast, the bad ones will hate them and do whatever means possible to blackmail them.

This saying teaches people to have the patience to continue living the right values in their lives. In doing so they can become very successful in improving their families in their lives.

Proverbs (Wisdom) 2: 1ª, 12-22.

664. KUBHELA KUBHO.

Imbuki ya lusumo lunulo, yilolile bhubheja bho ginhu kubhanhu bhalebhe. Ubhubheja bhunubho, bhuli bho kulwande lobho duhu, kunguno abhoyi bhahayile giki, imisoga ibhize kubhoyi duhu, abhangi bhayigayilwe. Hunagwene abhanhu bhagabhawilaga giki bha ‘kubhela kubho.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhahayile bhapandike bhoyi duhu, umuwikaji bhobho. Abhanhu bhenabho, bhalina wilu bhogutumama milimo yabho iyo idulile gubhambilija ugupandika matwajo mengi abhoyi, kunguno bhadatogilwe igiki bhagapandike, abhichabho. Abhoyi ulubhigwa giki bhapandikaga ginhu jawiza abhichabho, bhagakolagwa, kunguno ya wilu bhobho bhunubho.

Abhanhu bhenabho, bhiyikolile nabho bhahayile giki, bhabheje bhoyi duhu, kunguno nabhoyi bhagakolagwa ulu bhapandika jawiza abhichabho, umukikalile kabho. Abhoyi bhagabhalanjaga bhugugu abhanhu bhabho, kunguno ya wilu bhobho bhunubho. Hunagwene abhanhu bhagabhawilaga giki bhatogilwe ‘kubhela kubho.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kuleka wilu bho gubhadakila abhichabho abho bhapandikaga jawiza, umuwikaji bhobho, kugiki bhadule gwikala bho mholele nabho, umukikalile kabho.

Luka 18:10-11.

Zaburi 73:1-4.

KISWAHILI: BORA KWAO.

Chanzo cha methali hiyo, chaangalia utengenezaji wa kitu kwa watu fulani. Utengenezaji huo, ni wa upande wao tu, kwa sababu wao wanataka mafanikio mengi yawe kwao, na wengine wayakose. Ndiyo maana watu hao hutaka hali iwe ‘bora kwao.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa watu wale ambao hutaka wapate wao tu, katika maisha yao. Watu hao, wana wivu wa kufanya kazi zile zinazoweza kuwasaidia kupata mafanikio wao, kwa sababu wao hawapendi wenzao, wafanikiwe. Hivyo wao wakisikia kwamba, wenzao wamepata mafanikio, huchukia mioyoni mwao, kutokana na wivu huo walio nao.

Watu hao, hufanana na wale watakao kupata mafanikio mengi wao tu, kwa sababu nao huchukia wanapofanikio wenzao, katika maisha yao. Wao huwafundisha watu wao kuwa na wivu huo, kwa sababu ya mifano yao wanayowaonesha. Ndiyo maana watu huwaambia kwamba wao hutaka hali iwe ‘bora kwao.’

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuacha wivu wa kuwachukia wenzao wanaopata mafanikio, katika maisha yao, ili waweze kuishi kwa amani na wenzao hao, maishani mwao.

Luka 18:10-11.

Zaburi 73:1-4.

egoism

selfish ones

selfish ones.jpg2ENGLISH: THE BEST IS FOR THEM.

The source of this saying is the production of a certain product to be used by a certain group of people. Those people would like to have that product for their own use because they want more success in life. This is why people can describe individuals with such a behaviour using the saying that ‘the best is for them.’

The saying can be compared to those people who want something for their own benefits without considering others. Those people are envious of doing tasks that can help them to achieve their success. In case they hear others to have achieved in their lives, they hate them out of jelous. They therefore teach people to be jelous in life.

This saying teaches people to give up the behaviour of being jelous rather they have to respect other peoples’ achievements and use them as challenges for their struggle in life.

Luke 18: 10-11. Psalm 73: 1-4.

663. WINGI BHO MIHAYO BHUDABHEJAGA KAYA.

Imbuki ya lusumo lunulo, yingilile kuwingi bho mihayo aha bhanhu bha hakaya ndebhe. Uwingi bho mihayo bhunubho, bhuli bho guduma ugwidegeleka chiza, kunguno bhuli ng’wene, agamagana uyomba mhayo gokwe. Imihayo yiniyo igabhejaga yombo ya guduma ugwiigwa chiza aha kaya yabho. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘wingi bho mihayo bhudabhejaga kaya.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa ku bhanhu abho bhagikalaga bhuyoga aha kaya yabho, umukikalile kabho. Abhanhu bhenabho, bhagituulaga bhumani bho bhuli ng’wene gulema ugwiigwa imihayo ya bhiye, kunguno ya guhaya adegelekwe weyi duhu. Abhoyi bhagadumaga nulu gutumama kihamo imilimo yabho, kunguno ya gubhiza bhuli ng’wene na nimo gokwe, uyo aligubhona gusoga, umumiganiko gakwe. Ikaya yiniyo nose igasalambanaga, kunguno ya bhuyogi bhunubho ubho guduma nulu gwiigwa.

Abhanhu bhenabho, bhagikolaga na bhanhu abho bhali na mihayo mingi aha kaya yabho, kunguno nabho bhali na mihayo mingi, iyo igabhenhelejaga guyoga aha kaya yabho yiniyo. Hunagwene abhanhu bhagabhawilaga giki, ‘wingi bho mihayo bhudabhejaga kaya.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na ng’wigwano go gwizunilija gutumama milimo yabho kihamo, kugiki bhadule gujibheja chiza kaya jabho, umukikalile kabho.

Daniel 3:8-18.

1 Wakorintho 13:1-8.

Zaburi 46:10.

Yohana 6:1-5.

Yakobo 1:19.

Mathayo 7:21.

Mathayo 11:28.

Yakobo 2:14.

Mathayo 28:20.

KISWAHILI: WINGI WA MANENO HAUTENGENEZI MJI.

Chanzo cha methali hiyo, chatokea kwenye wingi wa maneno ya watu walioko kwenye familia fulani. Wingi huo wa maneno ni wa kushindwa kusikilizana kwa sababu ya kila mmoja kuendelea kuongea neno lake. Maneno hayo huleta kelele ya kushindwa kuelewana vizuri. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘wingi wa maneno hautengenezi mji.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa watu wale ambao huwa wanazozana kila wakati kwenye familia yao, katika maisha yao. Watu hao, hujitia kujua zaidi kila mmoja kwa kukataa kuwasikiliza wenzake, kwa sababu ya kutaka asikilizwe yeye tu.

Wao hushindwa hata kufanya kazi kwa ushirikiano, kwa sababu ya kujikuta kila mmoja ana kazi yake mwenyewe, ambayo huiona kuwa ni ya maana kuliko zile wanazofanya wenzake. Mwishowe, familia hiyo husambalatika kwa sababu ya kelele hizo za kushindwa kuelewana.

Watu hao, hufanana na wale wenye maneno mengi kwenye familia yao, kwa sababu nao hawa, wana maneno mengi, ambayo husababisha wao kuzozana kwenye familia yao hiyo. Ndiyo maana watu huwaambia kwamba, ‘wingi wa maneno hautengenezi mji.’

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na uelewano wa kukubaliana kufanya kazi kwa umoja, ili waweze kupata mafanikio ya kutosha kuziendeleza vizuri familia zao, maishani mwao.

Daniel 3:8-18.

1 Wakorintho 13:1-8.

Zaburi 46:10.

Yohana 6:1-5.

Yakobo 1:19.

Mathayo 7:21.

Mathayo 11:28.

Yakobo 2:14.

Mathayo 28:20.

bhakima wa africa

zulu-youths war dance

ugulilu

 

ENGLISH: TOO MUCH WORDS DO NOT BUILD A FAMILY.

The source of this proverb is too much words that come from a certain family. When people in a family speak too much it becomes not easy to listern or understand each other. It rather leads to misunderstanding. People can describe this scenario using the proverb that ‘too much words do not build a family.’

This proverb can be compared to those people who are constantly in conflict in their families. Such people tend not to listern to others but to be listerned. They also fail to work together because each one of them will tend underrate the other’s work and consider his/hers to be more important than others. Eventualy, a family of this nature can easily disintegrate because of failing to have common goals. Some of them will appear to be more wordy and force to silence others.

This proverb teaches people about harmony by agreeing to work together. This can enable them to have success in life and take good care of their families.

Daniel 3: 8-18. 1 Corinthians 13: 1-8. Psalm 46:10. John 6: 1-5. James 1:19. Matthew 7:21. Matthew 11:28. James 2:14. Matthew 28:20.