Sukuma Proverbs

325. NOMBA GULYA ADAB’ONELAGWA MHAYO

Imbuki ya lusumo lunulo yingilile kubhulombi bho jiliwa. Unombi ojiliwa ng’wunuyo, agabhizaga atub’ile. Agabhonaga giki, ilichiza ugulomba ijiliwa jinijo ukubhanhu abho bhalinajo, gutimda kujisola bho nduhu uguzunulijwa na bhanikili jiliwa. Unombi o jiliwa ulu ojipandika ijo alilomba agajilyaga na b’uyegi, kunguno adiho guhayiwa giki ohub’aga. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘nomba gulya adabhonelagwa mhayo.’

Usulumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo adatogilwe gusola sabho jabhanhu bho nduhu ugulomba. Umunhu ng’wunuyo agatumilaga makanza gakwe bho gujilomba ijiliwa jinijo, kunguno adebhile igiki, ‘nomba gulya adabhonelagwa mhayo.’

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya kuleka gusola sabho ja bhanhu bho nduhu ugulomba, kugiki bhadule gwikala bho mholele na bhichabho, umuwikaji bhobho.

Mathayo 7:7.

KISWAHILI: MUOMBA KULA HAONEWI NENO

Chanzo cha methali hiyo chatokea kwenye uombaji wa chakula. Muombaji huyo wa chakula huwa ameshikwa njaa. Huona kwamba ni vizuri kuomba badala ya kuchukua bila kuruhusiwa na wenye chakula hicho. Muombaji huyo wa chakula hukila kwa furaha akikipata chakula hicho alichokiomba, kwa sababu hawezi kufikiliwa kwamba amekosea. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘muomba kula honewi neno.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu yule asiyependa kuchukua mali za watu bila kuomba. Mtu huyo hutumia mda wake katika kuomba chakula hicho, kwa sababu, aelewa kwamba, ‘muomba kula haonewi neno.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuacha kuchukua mali za watu bila kuomba, ili waweze kuishi kwa amani na wenzao, maishani mwao.

Mathayo 7:7.

poverty

ENGLISH: ONE WHO BEGS FOOD HAS NO FAULT

This proverb rises from a person who begs for food. The person who begs for food is always hungry. Such a person finds it good to beg rather than taking food without permission from owners. When he/she is given the food, this person eats it happily because he/she cannot be accused of having done something wrong.That is why people say, “he who begs for food has no fault.”

The proverb is likened to someone who does not want to take others’ properties without asking. Such a person spends his/her time begging for food because he/she understands that, “he who begs for food has no fault.”

The proverb teaches people to stop taking others’ possessions without permission in order to live peacefully with neighbours.

Matthew 7: 7.

324. NKULU ADALYAGA

Imbuki ya lusumo lunulo yingilile mub’utuuji bho jikolo jigehu mulijisema litale. Ijikolo jinijo jigusaga numo jilili duhu, jidikomile gukwila jokale umujiseme jinijo, nulu gugeha. Untuuji ojo agujisanga gitumo ojituulila jilihoyi. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘nkulu adalyaga.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kubhanhu abho b’agatuulaga sabho jabho mujikolo jitale ja gudula gujilang’hana chiza, nulu jigikala moyi bho makanza malihu jidujimila. Abhanhu bhenabho bhagajisangaga isabho jabho jilihoyi gitumo bhajituulila, kunguno b’adebhile igiki, ‘nkulu adalyaga.’

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya gulanghana chiza isabho jabho bho gujituula mubenki iyo idulile gujilanghana chiza.

Zaburi 78:70-72.

1Samweli 16:7.

KISWAHILI: MKUBWA HALI

Chanzo cha methali hiyo chatokea kwenye uwekaji wa vitu vichache kwenye chombo kikubwa. Kitu hicho hubakia kama kilivyo tu, hakiwezi kuongezeka kikalingana na chombo hicho, wala kupungua. Mwekaji wa kitu hicho huvikuta kama kilivyokuwa wakati akikiweka pale. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘mkubwa hali.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa watu wale wawekao mali zao kwenye kitu kikubwa ambacho chaweza kutunza mali hizo kwa usalama, hata kama zitakaa kwa mda mrefu, hazitapotea. Watu hao huzikuta mali zao zikiwa salama kama walivyoziweka, kwa sababu wafahamu kwamba, ‘mkubwa hali.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kutunza vizuri mali zao kwa kuziweka kwenye mabenki yawezayo kuzitunza vizuri.

Zaburi 78:70-72.

1Samweli 16:7.

treasure

 

ENGLISH: KEEP YOUR PROPERTIES/ ITEMS IN A BIG CONTAINER

This saying comes from a tendency of putting things in a big container. Things kept in a big container will not decrease or increase to fill the container. The owner of those things will find it intact.That is why people say, “keep your properties in a big container.”

The proverb is comparable to those people who put their belongings in a container that can hold them safely for a long time without losing them. These people find their properties intact.

The proverb teaches people how to take good care of their properties by putting them in banks that can take good care of them.

Psalm 78: 70-72.

1 Samuel 16: 7.

321. B’UTA B’UDIMANILE NA LUGE

Imbuki ya lusumo lunulo yingilile kub’uta na luge. Ub’uta nu luge jigikalaga kihamo jiidimile chiza. Jigikalaga bho gwiyambilija uguitumama imilimo yajo. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, b’uta b’udimanile na luge.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhitolile. Abhanhu bhenabho bhagikalaga kihamo umuwikaji bhobho, guti numo bhuli ub’uta nu luge. Bhose ungosha nu nkima bhagiyambilijaga uguitumama imilimo yabho. Abhoyi b’alumanile halumo umushigu ja b’ulamu bhobho. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘b’uta b’udimanile na luge.’

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu abho b’itolile higulya ya gwiidima bho gulumana chiza umuwikaji bhob’o, guti b’uta na luge, umo b’udimanilile. Akikalile kenako kagubhinha nguzu ja gwiyambilija umubhutumami bho milimo yabho.

Mwanzo 9:13-16.

Waefeso 5:31.

KISWAHILI: UPINDE HUSHIKAMANA NA UGWE/KAMBA YAKE

Chanzo cha methali hiyo chatokea kwenye upinde na kamba yake. Upinde na ugwe au kamba yake huwa zimeshikamana pamoja vizuri. Husaidiana katika kufanya kazi zote. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘upinde hushikamana na ugwe/kamba yake.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa watu waliooana. Watu hao huishi pamoja maishani mwao, kama ulivyo upinde na ugwe. Wote mume na mke husaidiana katika kufanya kazi zao. Huungana pamoja siku zote za maisha yao. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘upinde hushikamana na ugwe.’

Methali hiyo hufundisha watu wa ndoa juu ya kushikamana vizuri maishani mwao, kama upinde na ugwe, ushikamanavyo. Maisha hayo yatawapatia nguvu za kusaidiana katika utekelezaji wa majukumu yao.

Mwanzo 9:13-16.

Waefeso 5:31.

arrow

 

ENGLISH: THE BOW AND ITS STRING ARE FASTENED TOGETHER

The source of this proverb comes from the bow and its string. The bow and its string tend to fit together nicely and they function together. That is why people say, “a bow and its string are fastened together.”

The proverb is likened to married people. Married people live together just like a bow and its string.The couples live together and they support each other in life.That is why people say, “a bow and its string are fastened together.”

The proverb teaches couples about how to stick together in their lives like a bow and its string. This kind of life will give them the strength to help each other in fulfilling their responsibilities.

Genesis 9: 13-16.

Ephesians 5:31.

320. UDIZUNIDIMILA MUB’ANA B’A MBULI

Imbuki ya lusumo lunulo yingilile kuli ndimi o mbuli. Undimi ng’wunuyo agajikomanyaga imbuli inhale, na bhana bha mbuli heke. Bhuli jene agajidimaga heke ni jingi. Kuyiniyo lulu, imbuli inhale igalemaga ugudimilwa mub’ana bha mbuli, nulu igab’iza ilinamili gudoo na ginehe. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘udizunidimila mub’ana bhana bha mbuli.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo alidalahijiwa na bhiye kunguno ya mili gokwe gudoo, aliyo alimunhu ntale. Umunhu ng’wunuyo agalemaga ugusanjiwa mub’anigini. Hunagwene agayombaga giki, ‘udizunidimila mub’ana b’a mbuli.’

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya kuleka nhungwa ja kub’adalahija abhanhu, kugiki bhadule ugutumama milimo yabho chiza, mu kaya jabho.

Zaburi 31:18.

1 Petro 2:16-17.

KISWAHILI: USINICHUNGIE KWENYE WATOTO WA MBUZI

Chanzo cha methali hiyo chatokea kwa mchungaji wa mbuzi. Mchungaji huyo huwatenga mbuzi wakubwa na watoto wao, upande mwingine. Kila kundi hulichungia sehemu tofauti na lingine. Kwa hiyo basi, mbuzi mkubwa hukataa kuchungiwa kwenye kundi la watoto, hata kama atakuwa na umbo dogo namna gani. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘usinichungie kwenye kundi la watoto wa mbuzi.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu yule anayedharauliwa na wenzake kwa sababu ya umbo lake kuwa dogo, ijapokuwa yeye ni mkubwa kiumri. Mtu huyo hukataa kuchanganywa kwenye kundi la watoto, kwa kusema kwamba, ‘usinichungie kwenye watoto wa mbuzi.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuacha tabia ya kuwadharau watu maishani  mwao, ili waweze kufanya kazi vizuri, katika familia zao.

Zaburi 31:18.

1 Petro 2:16-17.

goats

 

ENGLISH: NEVER PASTURE ME AMONG SMALL GOATS/GOAT’S KIDS

The source of this proverb is a person who pastures goats. The person who tends goats usually separates kids from old goats. Each group is pastured separately. So, an old goat will refuse to be pastured in the same group as kids no matter how small it is in shape.That is why people say, ‘never pasture me among goat’s kids.’

The proverb is analogized to an adult person who is despised by his/her peers because of being small in appearance. The person usually refuses to be treated as a child by saying, “never pasture me among goat’s kids.”

The proverb teaches people to stop the habit of despising other people in their lives.

Psalm 31:18.

1 Peter 2: 16-17

319. LELO YA CHIMA NKUNDI

Imbuki ya lusumo lunulo, yingilile kunkundi uyo gochimagwa ginhu guminyiwa hatale. Unkundi gunuyo gugolechaga b’uminyiwa bho ng’wa munhu uyo ang’wisanije. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘lelo yachima nkundi.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo alioludugu, uyo wenhaga mamihayo matale. Abhaduguye b’agasatagwa noyi, kunguno ya gulombwa gufunya nsango kugiki bhabhone guimala imahayo yiniyo. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘lelo yachima nkundi.’

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya guleka gwita mamihayo gabhub’i kubhichabho, kunguno amamihayo genayo, gagachimaga nkundi, ukumioyo ya bhichabho bhenabho.

Wagalatia 6:10.

KISWAHILI: LEO IMECHOMA KITOVU

Chanzo cha methali hiyo chatokea kwenye kitovu kilichochomwa kitu fulani kikaumia sana. Kitovu hicho, huonesha jeraha la mauvumi ambalo mtu huyo amelipata kutoka kwa yule amtegemeae, au ameumizwa mtu wa karibu naye. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘leo imechoma kitovu.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu ambaye ameleta matatizo kwa ndugu zake. Ndugu zake mtu huyo huumia sana, kwa sababu ya kuwaletea shida ya kutakiwa kuchanga mali zikiwemo pesa, kwa lengo la kuyatatua matatizo hayo. Ndiyo maana watu husema, ‘leo imechoma kitovu.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuacha kuwaletea matatizo ndugu zao, au wenzao, kwa sababu, matatizo hayo huchoma vitovu vya mioyo ya wenzao hao, kwa maana ya kuwaumiza sana.

Wagalatia 6:10.

vintage

 

ENGLISH: THE NAVEL HAS BEEN STABBED TODAY

This proverb comes from a person whose navel has been stubbed badly. The navel represents injury caused by a closely-related person. That is why people say, “the navel has been stubbed today.” The proverb is compared to a person who has caused serious problems to his/her relatives. The relatives of that person suffer because of being asked to pay money or something else in order to resolve the problem their relative caused to them. That is why people say, “the navel has been stubbed today.”

The proverb warns people against causing problems to their brothers or their people because problems cause pain to people.

Galatians 6:10.