Sukuma Proverbs

691. NKUNGA LYOCHI.

Nkunga lyochi, luli lusumo ulo lwandija kuli munhu uyo ojaga ulilila jiliwa aha kaya iyo obhonaga lilizuka lyochi. Uweyi oli adalimaga aha kaya yakwe, kunguno ya gumalina guja ulya aho obhonaga lilizukila ilyochi linilo. Nose, abhanhu bhagandya guyung’watana giki, ‘Nkunga Lyochi.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo alingokolo ugutumama imilimo. Umunhu ng’wunuyo, atogilwe gulya jiliwa duhu bho nduhu ugujitumamila milimo ijo alijilya, kunguno ahikanza ilya gutumama milimo, uweyi agibhisaga halebhe, oyulola aho lilifumilila ilyochi.

Abhanhu bhagang’witanaga Nkunga Lyochi, bhogundalaha, kunguno ali munhu uyo agacholaga aha kaya iyo bhalizucha lyochi, odebha igiki bhalizuga jiliwa, oja hoyi gujulwa.

Uweyi ulu ubhona lyochi, agafumilaga wangu na kujulya aha kaya yiniyo. Hunagwene abhanhu bhagang’witanaga giki, ‘Nkunga Lyochi.’ Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, 60.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kuleka bhugokolo bho gutumama milimo, ibadala yaho, bhikomeje kuitumama chiza imilimo yao, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi, umukikalile kabho.

“Ubhugokolo bhudarahilwe na Bhasuguma. Hangi bhulemilwe nu Mulungu. Ubhugokolo mugutumama milimo yise iya bhuli lushugu, guti gulima, nulu, bhugokolo umumihayo ya moyo, guti, gukija gujusalila ulushigu ulo Jumapili, guleka gusalia aha kaya, guleka guntumamila Mulungu bho bhukamu, na yingi guti yiniyo, yilemilwe pye iyose.

 Hangi dudizubhiza bhanhu abho guhebhilwe na bhikumvi bho jiliwa nulu walwa. Uwikaji bhudi jiliwa duhu, bhubhitilile noyi. Bhuli munhu alina nhumbu ya gulya jiliwa. Dubhize na nzala ya gumbokela Sebha wise Yesu Kristo, umu Sakramenti ya Bhukaristia. Dubhize na nhumbu ya gulya jiliwa ja ng’wa Sebha. Dubhize na bhuyegi uludulimbokela umujigukulu jakwe. Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 60-61.

Mwanzo 25:34.

Waebrania 12:16.

2Wathesalinike 3:10.

Waroma 4:17.

Methali 28:19.

KISWAHILI: MVIZIA MOSHI AU MTU MWENYE KUANGALIA (KUTAFUTA) MOSHI.

Mvizia moshi ni methali ambayo ilianzia kwa mtu aliyekuwa anakula chakula kwenye familia za watu kwa kuvizia pale unapotakea moshi. Yeye alikuwa halimi au hafanyi kazi, kwenye familia yake, kwa sababu ya kuutumia muda wake huo, katika kuvizia familia inayopika chakula, kwa kuangalia pale unatopokea moshi. Mwishowe watu, walimgundua kuwa, anavizia chakula kwa kuangalia moshi, wakaanza kumuita, ‘mvizia moshi.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ni mzembe katika kufanya kazi. Mtu huyo, hupenda kula tu bila kukifanyia kazi kile anachokila, kwa sababu, wakati wa kufanya kazi, yeye hujificha mahali fulani ili kungojea moshi au kuvizia moshi unapotokea.

Watu humwita mvizia moshi, kama njia ya kuonesha dharau kwake, kwa sababu ni mtu anayetafuta familia ile ambayo inatoa moshi, na kufahamu kwamba wanapika chukula pale. Mtu huyo akiona moshi mara moja hujitokeza kwenye chakula. Ndiyo maana watu humuita ‘mvizia moshi.’ Rejea Kueneza Injili kwa Methali, 60.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuacha uzembe wa kufanya kazi, badaya yake, wajibidishe kuyatekeleza vizuri majukumu yao, ili waweze kupata mafanikio mengi, katika maisha yao.

“Uzembe umedharauliwa na Wasukuma. Tena umekataliwa na Mungu kama ni uzembe katika kufanya kazi yetu ya kila siku, kwa mfano kulima, au uzembe katika mambo ya kiroho, kwa mfano kutosali Jumapili, kutosali nyumbani, kutomtumikia Mungu kwa bidii, n.k.

Tena tusiwe watu ambao tunatawaliwa na tamaa ya chakula au pombe. Maisha si chakula tu, bali ni zaidi. Kila mtu ana haja ya kula chakula. Tuwe na njaa ya kumpokea Bwana Wetu Yesu Kristo katika sakramenti ya Ekaristi. Tuwe na haja ya kula chakula cha Bwana. Tuwe na furaha tunapokuwa kwenye karamu yake.” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 60-61.

Mwanzo 25:34. “Ndipo Yakobo akampa Esau mkate na ule mchuzi wa dengu. Akala na kunywa, kisha akainuka akaenda zake. Kwa hiyo Esau alidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.”

Waebrania 12:16. “Angalieni miongoni mwenu asiwepo mwasherati au mtu asiyemcha Mungu kama Esau, ambaye kwa ajili ya mlo mmoja aliuza haki ya uzaliwa wake wa kwanza.”

2Wathesalinike 3:10. “Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri ili kwamba: ‘‘Mtu ye yote asiyetaka kufanya kazi, wala asile.’’”

Waroma 14:17. “Kwa maana Ufalme wa Mungu si kula na kunywa, bali ni haki, amani na furaha katika Roho Mtakatifu.”

Methali 28:19. “Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha.”

smoke1

smoke2

ENGLISH: HE WHO WAITS TO SEE WHERE THE SMOKE COMES FROM.

This saying comes from someone who is fond of eating food from other people’s homes. This person does not work in his/her farm to get food but he/she just stays home looking for where the smoke comes from and follow it because he/she knows that he/she can get food. When this happened, people labeled him/her as someone who is pushed by smoke thus coming with the saying that ‘he who waits to see where the smoke comes from.’

This saying can be compared to a person who is negligent in working. This person likes eating without working out what he/she eats. When others are working in their farms he/she hides himself/herself, waiting to see where the smoke comes from. People, as a way of despising such behaviour, can call such a person as someone who looks where the smoke comes from. He/she easily associates smoke and food ‘Refer to ‘Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ ukurasa wa 60). This book was written by searchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

The proverb teaches people to stop negligence and, on the other hand, make a commitment to carry out their responsibilities so that they can achieve more in their lives.

“Negligence is discouraged by the Sukuma people. God also, through holy scriptures, discouraged negligence in, for example, gardening, or spiritual neglect; not praying on Sunday, not praying at home, not serving God diligently, etc.

And we must not be people who are ruled by a desire for food or alcohol. Life is not just food, but more than food. Everyone has a need to eat food. May we be hungry to receive Our Lord Jesus Christ in the sacrament of the Eucharist. We need to eat the Lord’s Supper. Have joy while we’re at his banquet ” (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ pages 60-61).

Genesis 25:34. Hebrews 12:16. 2Thessalonians 3:10. Romans 4:17. Proverbs 28:19.

690. SEKELA MIDEKO.

Sekela mideko luli lusumo ulo lulingisilile kuli munhu uyo agayegelaga aha gulya jiliwa, kulebha ugujichola. Galihoyi mahoya ga bhanhu bhabhili, uungi atogilwe ugutumama imilimo, uungi adatogilwe. Uyo atogilwe ugutumama imilimo akayomba, ‘tujage dugatumame milimo kunguno ilikanza lyashigaga.’ Uyo adayitogilwe imilimo agashosha bhobhuzongu aliyomba, ‘naduduja ugujutumama imilimo, kunguno naliigwa shibhi.’

Uyo aitogilwe imilimo agang’wila, ‘bhasi, dujage gugalwe jiliwa kugiki umili goko gupandike nguzu chiza.’ Uweyi agashosha kubhuyegi ukunu alimila, ‘nahene dujage.’ Hunagwene abhanhu bhagandya guyung’witana giki, ‘sekela mideko.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo alingokolo umugutumama imilimo. Umunhu ng’wunuyo, atogilwe gulya jiliwa duhu bho nduhu ugujitumamila milimo ijo alijilya. Abhanhu bhagang’witanaga sekala mideko bhogundalaha, kunguno ali munhu uyo agasekaga ahikanza lya gulya jiliwa, aliyo ahikanza ilya gutumama milimo, agasunduhalaga. Hunagwene abhanhu bhagang’witanaga giki, ‘sekela mideko.’ Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, 60.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kuleka bhugokolo bho gutumama milimo, ibadala yaho, bhikomeje kuitumama chiza imilimo yao, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi umuwikaji bhobho.

“Ubhugokolo bhudarahilwe na Bhasuguma. Hangi bhulemilwe nu Mulungu. Ulu bhugokolo mugutumama milimo yise iya bhuli lushugu, guti gulima, nulu, bhugokolo umumihayo ya moyo, guti, gukija gujusalila ulushigu ulo Jumapili, guleka gusalia aha kaya, guleka guntumamila Mulungu bho bhukamu, na yingi guti yiniyo, yilemilwe pye iyose.

 Hangi dudizubhiza bhanhu abho guhebhilwe na bhikumvi bho jiliwa nulu walwa. Uwikaji bhudi jiliwa duhu, bhubhitilile noyi. Bhuli munhu alina nhumbu ya gulya jiliwa. Dubhize na nzala ya gumbokela Sebha wise Yesu Kristo, umu Sakramenti ya Bhukaristia. Dubhize na nhumbu ya gulya jiliwa ja ng’wa Sebha. Dubhize na bhuyegi uludulimbokela umujigukulu jakwe. Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 60-61.

Mwanzo 25:34.

Waebrania 12:16.

2Wathesalinike 3:10.

Waroma 4:17.

Methali 28:19.

KISWAHILI: MCHEKEA CHAKULA.

Mchekea chakula ni methali ambayo humaanisha mtu anayefurahia kula chakula, kuliko kukitafuta. Kulikuwa na maongezi ya watu wawili, mmoja anapenda kufanya kazi mwingine hapendi. Anayependa kufanya kazi alisema, ‘twende tukafanye kazi kwa sababu wakati umefika.’ Asiyependa kufanya kazi, alijibu kwa unyonge akisema, ‘siwezi kwenda kufanya kazi kwa sababu najisikia vibaya.’

Mpenda kazi akamwambia, ‘basi twende tukale chakula ili mwili wako upate nguvu vizuri.’ Yeye alijiku kwa furaha huku akiwa amesimama, ‘sawa twende.’ Ndiyo maana watu wakaanza kumuita, ‘mchekea chakula.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ni mzembe katika kufanya kazi. Yeye anapenda kula tu bila kukifanyia kazi kile anachokila. Watu humwita mchekea chakula kama njia ya kuonesha dharau kwake, kwa sababu ni mtu anayecheka wakati wa kula, lakini wakati wa kazi husikitika. Ndiyo maana watu humuita ‘Mchekea chakula.’ Rejea Kueneza Injili kwa Methali, 60.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuacha uzembe wa kufanya kazi, badala yake, waongeze bidii ya kuyatekeleza vizuri majukumu yao, ili waweze kupata mafanikio mengi, maishani mwao.

“Uzembe umedharauliwa na Wasukuma. Tena umekataliwa na Mungu kama ni uzembe katika kufanya kazi yetu ya kila siku, kwa mfano kulima, au uzembe katika mambo ya kiroho, kwa mfano kutosali Jumapili, kutosali nyumbani, kutomtumikia Mungu kwa bidii, n.k.

Tena tusiwe watu ambao tunatawaliwa na tamaa ya chakula au pombe. Maisha si chakula tu, bali ni zaidi. Kila mtu ana haja ya kula chakula. Tuwe na njaa ya kumpokea Bwana Wetu Yesu Kristo katika sakramenti ya Ekaristi. Tuwe na haja ya kula chakula cha Bwana. Tuwe na furaha tunapokuwa kwenye karamu yake.” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 60-61.

Mwanzo 25:34. “Ndipo Yakobo akampa Esau mkate na ule mchuzi wa dengu. Akala na kunywa, kisha akainuka akaenda zake. Kwa hiyo Esau alidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.”

Waebrania 12:16. “Angalieni miongoni mwenu asiwepo mwasherati au mtu asiyemcha Mungu kama Esau, ambaye kwa ajili ya mlo mmoja aliuza haki ya uzaliwa wake wa kwanza.”

2Wathesalinike 3:10. “Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri ili kwamba: ‘‘Mtu ye yote asiyetaka kufanya kazi, wala asile.’’”

Waroma 14:17. “Kwa maana Ufalme wa Mungu si kula na kunywa, bali ni haki, amani na furaha katika Roho Mtakatifu.”

Methali 28:19. “Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha.”

laugh

laugh children

ENGLISH: LAUGHING FOR FOOD.

This saying comes from someone who enjoys eating food rather working for it. One day, two people were in conversation, one of them was fond of working while the other one not. In the course of conversation one of them said ‘Let’s go to work because the time has come.’ The other fellow who doesn’t like to work replied saying ‘I can’t go to work because I feel bad.’ The one who likes to work, later, told his/her fellow workmate that ‘let’s go eat some food so that your body can be healthy.’ The statement on going to eat was received with the greatest joy, ‘let’s go.’

This saying can be compared to a person who doesn’t like working. This person likes to eat without working for what he/she eats. People can ridicule him/her as someone who laughs whenever he/she sees food but feels bad whenever the question of working is mentioned (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 60). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

The saying teaches people to stop negligence and, instead, increase the effort to carry out their responsibilities so that they can achieve more in their lives.

The Sukuma people tend to hate negligence. God also hates negligence manifested in, for example, not farming, not praying, not attending Sunday church services, not diligently serving God, etc. We must not be people who are ruled by a desire for food or alcohol. Life is not just food, but more than food. Everyone has a need to eat food. May we be hungry to receive Our Lord Jesus Christ in the sacrament of the Eucharist. We need to eat the Lord’s Supper. Have joy while we’re at his banquet (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 60-61).

Genesis 25:34. Hebrews 12:16. 2Thessalonians 3:10. Romans 4:17. Proverbs 28:19.

689. NG’HWI NINGI JIGANGALUCHAGA.

Ulusumo lunulo, lufumilile kulilomelele lya bhazugi bhahanimo nhebhe. Uumo obho agabhawila abhiye, ‘dujagi dugasene ng’hwi kunguno unimo gunuyu gulintale noyi.’ Umo obhiye ashosha, ‘jilihoyi ijo denhile iyigolo.’ Uweyi agayomba, ‘ijinijo jigushila hayo ijiliwa jidinapya. Igelelilwe dujijile ng’hwi ningi ijo jidulile gubhachiwa mpaga jujibisha ijiliwa ja ha nimo gunuyo.’

Bhagizunilija bhugenha ng’wi ningi ijo bhagajizugula mpaga bhujibisha ijiliwa ija ha nimo gobho gunuyo. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘ng’hwi ningi jigangaluchaga.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhali ni nikoye ilo bhalihaya bhalyinje umuwikaji bhobho. Abhanhu bhenabho, bhagatumilaga nzila ningi ijo jigikolanijiyagwa na ng’hwi ningi, ijagudula gujibisha ijiliwa jabho. Ugwangalucha go bhujiku ing’hwi jigubhakaga, yilingisilile gutumila nguzu na nzila ningi, ijagudula gulimala ilikoye linilo.

Abhanhu bhenabho, bhagatumilaga nzila ningi ijagudula dulyinja ilikoye ilya bhusatu bho corona. Bhagabhalanjaga abhichabho ahigulya ya gulunganija kihamo inguzu nu bhumani bhobho, ijina gujidilila inzila ijo abhatalaamu bha afya bhalibhalanga. Abhoyi bhagalunganaga halumo ijina gunomba Mulungu abhambilije ugulimala wangu ilikoye linilo. Hunagwene abhanhu bhenabho, bhagayombaga giki, ‘ng’hwi ningi jigangaluchaga.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gulungana halumo ijinagujidimila inzila ijo abhadaktari bhalibhalanga, ni jingi ijo jidulile gubhingija ilikoye guti linilo, ilya bhusatu bho corona, kugiki bhadule gumala wangu, na gwikala bho mholele, umuwikaji bhobho.

KISWAHILI: KUNI NYINGI HUKESHA.

Methali hiyo, ilitokea kwenye maongezi ya wapishi wa kwenye sherehe fulani. Mmoja wao, aliwaambia wenzake, ‘twendeni tukakate kuni kwa sababu sherehe hii, ni kubwa sana.’ Mmoja wale wenazake alijibu, ‘zipo zile tulizoleta jana.’ Yeye alisema, ‘hizo zitakwisha bila kukiivisha chakula hicho. Inafaa tuendee kuni nyingi za kutosha kuwashwa mpaga kukiivisha chakula cha kwenye sherehe hiyo.’

Walikubaliana wakaenda kuleka kuni nyingi walizozipikia mpaga wakakiivisha chakula cha kwenye sherehe hiyo. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘kuni nyingi hukesha.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa watu walio na tatizo wanalotaka kulitatua katika maisha yao. Watu hao, hutumia njia nyingi ambazo hufananishwa na kuni ziwezazo kuivisha chakula chao. Kukesha usiku mzima zikiwaka kuni hizo, humaanisha kutumia nguvu na njiza nyingi kutosha kulimaliza tatizo hizo.

Watu hao, hutumia njia nyingi za kuwawezesha kujikinga na tatizo kama hilo la ugonjwa wa corona. Wao huwafundisha wenzao namna za kuungana pamoja katika kuyafuata maelekezo yanayotolewa na watalaamu wa afya. Watu hao, huunganisha nguvu zao huku wakimuomba Mungu awasaidie katika kulimaliza haraka tatizo hilo. Ndiyo maana wao huwaambia watu kwamba, ‘kuni nyingi hukesha.’

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuunganisha nguvu na ufahamu wao, katika kuyafuata maelekezo ya madaktari, na mengine mengi ambayo yanaweza kuwaondolea tatizo hilo, la ugonjwa wa corona, ili waweze kuishi kwa furaha na amani, maishani mwao.

firewood3

firewood

ENGLISH: MANY PIECES OF FIREWOOD LIGHT THE WHOLE NIGHT.

The above proverb started from a conversation of cooks at a ceremony. One of them, says to her companions, ‘let us go to cut firewood because this celebration is so big.’ One of the others replies, ‘there are some that we brought yesterday.’ The other says, ‘those ones will get finished before the food is ready, we have to increase enough firewoods to cook nice meal for this ceremony.’

They agreed and went to pick up as many  fire woods as they can, which they used for cooking nice food for the ceremony. That is why people say that, ‘many fire-woods keep up burning for the whole night.’

This proverb is compared to people who have a problem that they want to solve in their lives. These people use a variety of ways in solving it, which are compared to many fire woods that spend the whole night burning. Keeping up all night burning the wood, means spending enough energy and knowledge in getting rid of their problems.

These people,  help others in using many ways for protecting themselves from various problems including the corona epidemic. They teach their fellows on how to get together  their strenghs enough to follow the instructions which have been provided to them by health professionals.

These people unite their efforts in using their talents as well as asking God for help in resolving  quickly the pandemic. That is why they tell people that, ‘many fire-woods keep up burning for the whole night.’

The proverb imparts in people an idea about putting together their efforts and understandings, for following doctors’ instructions, and many other ways that can remove the problem of corona virus, so that they can live happily and peacefully, in their lives.

688. MASHIGA NILI, NULU, MAHIGA NILI.

Ulusumo lunulo, lwandija kumahoya ga bhanhu bhabhili ayo gahoyela mashiga. Uumo agamuuja ung’wiye, ‘amashiga ni kiyi?” Ung’wiye aganshokeja aliyomba, ‘amashiga gali mawe, nulu, madafari adatu ayo gagatumilagwa gujidimila ijisema ija guzugila ahaliko. Ahasi yago, gugabhachiyagwa moto umung’hwi ijo jigasolelagwa moyi. Umoto gunuyo gugagasebhyaga amashiga genayo.

Aliyo lulu, amashiga genayo gagabhizaga manilizu, ulugudubhachiyagwa umoto. Hunagwene abhanhu, ulu bhubhona kaya iduzugaga jiliwa, bhagayombaga giki, ‘mashiga nili, nulu, mahida nili.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa ku kaya iyo idabokelaga chiza abhageni na kubhalisha jiliwa, kunguno abhahenaho, bhadina bhutogwa, nulu, ikaya yiniyo idina jiliwa.

Amashiga ayo gali mawe adatu gagatumamilagwa gudima nungu, nulu fulila, aha liko, gagikalaga manilizu kunguno bhadazugaga ijiliwa ahakaya yiniyo. Hunagwene abhanhu, bhagayiwilaga ikaya yiniyo giki, mashiga nili, nulu, mahiga nili. Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa bho 58.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na wizang’holo bho gubhakaribhusha abhageni aha kaya jabho, kugiki bhadule gujipandika imbango ijo jigigelaga kunguno ya gubhagola chiza abhanhu bhenabho, umuwikaji bhobho.

“Ugubhakaribhusha abhageni bho wizang’holo umu kaya jise, guli nimo gwize ayise abho duganhondejaga Yesu Kristo. Ishibhi idigwita yabhubhi duhu, aliyo hangi nu kuleka gubhitila yawiza abhigisu, guleka uguitumama imilimo yise, na guleka gubhadilila abho bhali na makoye gabho. Ukuhani nu Nawi bhadang’witilile yabhubhi uyo oliotulwa na manyami, aliyo bhagamitilia bho nhudu ugundilila. Bhaditile lyose lyose. Lolaga Kueneza Injili Kwa Methali, bhukurasa, 58.

Mambo ya Walawi 19:34.

Luka 10:31-33.

Waroma 15:7.

Waebrania 13:2.

Mwanzo 18:1-8.

1Wafalme 17:10-16.

Mathayo 25:31-46.

KISWAHILI: MAFIGA BARIDI.

Methali hiyo ilianzia kwenye maongezi ya watu wawili juu ya kazi ya mafika. Mmoja alimuuliza mwenzake, ‘mafiga ni nini?’ Mwenzake alimjibu akisema, ‘mafiga ni mawawe, au matofari matatu yanayotumika katika kushikilia chombo cha kupikia. Chini ya mafiga hayo huwekwa kuni ambazo huwashwa moto unaoleta joto kwenye mafiga hayo. Mafiga hayo huwa baridi kama watu hawapiki chakula.’ Ndiyo maana watu kama wakiona chakula hakipikwi kwenye familia fulani, husema, ‘mafiga baridi.’

Methali hiyo hulinganishwa kwenye familia au kaya ile ambayo haipokei vizuri wageni na kuwalisha chakula, kwa kuwa hawana mapendo au kaya hiyo haina chakula.

Mafiga ambayo ni mawe matatu yatumikayo kutelekea chungu au sufuria jikoni, hukaa baridi kwa sababu hawapiki chakula. Ndiyo maana watu huiambia familia hiyo kwamba, ‘mafiga baridi.’ Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 58.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuwa na ukarimu wa kuwakaribisha wageni katika familia zao, ili waweze kupata Baraka zitokanazo na kuwatunza watu hao, katika maisha yao.

 “Kuwakaribisha wageni kwa ukarimu kwenye kaya zetu ni wajibu wetu sisi tunaomfuata Yesu Kristo. Dhambi sio kutenda mabaya tu, bali pia ni kutowatendea mema wenzetu, kutotimiza wajibu wetu, na kutohusika na shida zao. Kuhani na Mlawi hawakumtendea vibaya yule aliyepigwa na majambazi, bali walipita bila kujali. Hawakutenda lo lote.” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 58.

Mambo ya Walawi 19:34. “Mgeni anayeishi pamoja nawe ni lazima umtendee kama mmoja wa wazawa wa nchi yako. Mpende kama unavyojipenda mwenyewe, kwa maana ulikuwa mgeni katika nchi ya Misri. Mimi ndimi BWANA Mungu wako.”

Luka 10:31-33. “Kwa bahati nzuri kuhani mmoja alikuwa anapitia njia ile, alipomwona huyo mtu, akapita upande mwingine wa barabara, akamwacha hapo hapo. Vivyo hivyo Mlawi mmoja naye alipofika mahali pale, alimwona, akapita upande mwingine wa barabara, akamwcha hapo hapo. ‘‘Lakini Msamaria mmoja aliyekuwa akisafiri kupitia njia hiyo alipomwona, alimhurumia,”

Waroma 15:7. “Karibishaneni ninyi kwa ninyi kama Kristo alivyowakaribisha ninyi ili kumletea Mungu utukufu.”

Waebrania 13:2. “Msisahau kuwakaribisha wageni, kwa kuwa kwa kufanya hivyo, watu wengine waliwakaribisha malaika pasipo kujua.”

Mwanzo 18:1-8. “BWANA akamtokea Abrahamu karibu na mialoni ya Mamre wakati alipokuwa ameketi kwenye ingilio la hema lake wakati wa adhuhuri. Abrahamu akainua macho akaona watu watatu wamesimama karibu naye. Alipowaona, aliharakisha kutoka kwenye ingilio la hema lake kuwalaki na kuwasujudia hadi nchi.  Akasema, “Kama nimepata kibali machoni penu, ee bwana wangu, usimpite mtumishi wako. Acha yaletwe maji kidogo, kisha ninyi  nyote mnawe miguu yenu na mpumzike chini ya mti huu. Niruhusuni niwapatie chakula kidogo mle, ili mpate nguvu mwendelee na safari yenu, kwa kuwa mmekuja kwa mtumishi wenu.’’ Nao wakamjibu, “Vema sana, fanya kama unavyosema.’’

 Hivyo Abrahamu akaharakisha akaingia hemani kwa Sara. Akasema, “Chukua vipimo vitatu vya unga laini haraka, ukande na uoke mikate.”   Kisha akakimbia kwenda kwenye kundi  akachagua ndama mzuri, laini na akampa mtumishi, ambaye aliharakisha kumtayarisha. Kisha akaleta jibini, maziwa na nyama ya yule ndama iliyoandaliwa, akaviweka mbele ya wageni. Walipokuwa wakila, alisimama karibu nao chini ya mti.”

1Wafalme 17:10-16. “Hivyo akaenda Sarepta. Alipofika kwenye lango la mji, mjane alikuwa huko akiokota kuni. Akamwita na kumwomba, “Naomba uniletee maji kidogo kwenye gudulia ili niweze kunywa.’’ Alipokuwa anakwenda kumletea, akamwita akasema, “Tafadhali niletee pia kipande cha mkate.” Akamjibu, ‘Hakika kama BWANA wako aishivyo, sina mkate wo wote, isipokuwa konzi ya unga kwenye gudulia na mafuta kidogo kwenye chupa. Ninakusanya kuni chache nipeleke nyumbani na nikapike chakula kwa ajili yangu na mwanangu, ili kwamba tule kiishe tukafe.’’ Eliya akamwambia, “Usiogope. Nenda nyumbani ukafanye kama ulivyosema. Lakini kwanza unifanyizie mimi mkate mdogo kutoka vile ulivyonavyo kisha uniletee na ndipo utayarishe cho chote kwa ajili yako na mwanao. Kwa kuwa hivi ndivyo asemavyo BWANA, Mungu wa Israeli: “Lile gudulia la unga halitakwisha wala ile chupa ya mafuta haitakauka hadi siku ile BWANA atakapoleta mvua juu ya nchi.’’ Akaondoka na kufanya kama Eliya alivyomwambia. Kwa hiyo kukawa na chakula kila siku kwa ajili ya Eliya, yule mwanamke na jamaa yake. Kwa kuwa lile gudulia la unga halikwisha na ile chupa ya mafuta haikukauka, sawasawa na lile neno la BWANA alilosema Eliya.  ”

Mathayo 25:31-46. Hukumu ya mwisho. “Mwana wa Adamu atakapokuja katika utukufu wake na malaika wote watakatifu pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti cha enzi cha utukufu wake. Mataifa yote watakusanyika mbele zake, naye atawatenga kama mchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi. Atawaweka kondoo upande wake wa kuume na mbuzi upande wake wa kushoto.

“Ndipo Mfalme atawaambia wale walioko upande wake wa kuume, ‘Njoni, ninyi mliobarikiwa na Baba yangu, urithini Ufalme ulioandaliwa kwa ajili yenu tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Kwa maana nilikuwa na njaa mkanipa chakula, nilikuwa na kiu mkaninywesha, nilikuwa mgeni mkanikaribisha, nilikuwa uchi mkanivika, nilikuwa mgonjwa mkanitunza, nami nilikuwa kifungoni mkaja kunitembelea.’

“Ndipo wale wenye haki watakapomjibu wakisema, ‘Bwana, ni lini tulikuona una njaa tukakulisha au ukiwa na kiu tukakunywesha? Lini tulikuona ukiwa mgeni tukakukaribisha au ukiwa uchi tukakuvika? Tena ni lini tulikuona ukiwa mgonjwa tukakutunza au ukiwa kifungoni tukakutembelea?’ 

“Naye Mfalme atawajibu, ‘Amin, amin ninawaambia, kwa jinsi mlimvyotendea mmojawapo wa hawa ndugu Zangu walio wadogo, mlinitendea Mimi.’ “Kisha atawaambia wale walio upande Wake wa kushoto, ‘Ondokeni kwangu, ninyi mliolaaniwa, nendeni kwenye moto wa milele alioandaliwa kwa ajili ya ibilisi na malaika zake. Kwa maana nilikuwa na njaa hamkunipa chakula, nilikuwa na kiu hamkuninywesha, nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha, nilikuwa uchi hamkunivika, nilikuwa mgonjwa hamkunitunza na nilikuwa gerezani nanyi hamkuja kunitembelea.’

“Ndipo wao pia watajibu, ‘Bwana ni lini tulikuona ukiwa na njaa au kiu, au ukiwa mgeni au uchi , au ukiwa mgonjwa na kifungoni na hatukukuhudumia?’ “Naye atawajibu, ‘Amin, amin nawaambia, kwa jinsi ambavyo hamkumtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu walio wadogo, hamkunitendea mimi.’ “Ndipo hawa watakapoingia kwenye  adhabu ya milele, lakini wale wenye haki wataingia katika uzima wa milele.’’”

cooking-pot-

cooking

cooking1

ENGLISH: COLD THREE COOKING STONES.

 The proverb started in a two-person conversation about the work of the three cooking stones. One asked the other, ‘What are the three cooking stones?’  The other answered, ‘these are the three stones, or bricks which are used in holding the cooking tool.’

The cooking pot sits on those three stones in the traditional African fireplace. These three cooking stones of equal size and placement easily support the clay or metal cooking pot. They are positioned very carefully. 

Underneath or between them firewoods are put, which are set on fire. The three stones need each other; they work together. If one takes away one stone and the pot falls down. They however, get cold if people don’t cook food. That’s why when people discover that food is not cooked at a particular family, they say, ‘cold three cooking stones.’

The balance between their standing close together yet apart is a symbol of community life. This is one the Sukuma Proverb that is used to teach about the values of unity, community and working together.

It is found in the Small Christian Communities (SCCs) Book: During a SCC Workshop a very effective teaching on of unity and working together is to demonstrate African proverb.

It has the following teachings:

  1.   A creative way of teaching the importance of SCCs is to describe the three cooking stones on which SCCs are “cooked” as spiritual values, acts of mercy, and concrete projects.
  2.   The metaphor of the one cooking pot and three stones can be used in different ways to describe the Catholic Church.  That is, one church but three parts: priests, religious and laity.
  3.   The image of the cooking pot and the three stones is an important analogy for the Trinity: that is one God and three Divine Persons, namely Father, Son and the Holy Spirit.
  4.   A Sukuma, Tanzania proverb:  The three stones that support the cooking pot are cold (literally mafiga baridi in Swahili) means that there is no fire and thus no food is being cooked, which is a sign of the lack of hospitality, welcome and love. 

The cold stones are a sign of the lack of good relationships within the home itself and with people living outside. Three-cooking stones used for holding a pot or kitchen pan, stay cool because they do not cook food. That is why people tell such family, ‘cold three cooking stones.’ Refer to ‘Kueneza Injili kwa Methali’; which can be literally translated as ‘Spreading the Gospel through Proverbs, page 58.

Such book was written by researchers who are: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Joseph Healey M.M., published by Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

The proverb teaches people about generosity of welcoming strangers into their families, so that they can receive the blessings that come from caring for them, in their lives.

 “The generous hospitality of our families is the responsibility of those who follow Jesus Christ. Sin is not only doing wrong, but also not doing good to others, not fulfilling our obligations, and not dealing with their problems. The priest and the Levite did not harm the victim, but they passed away regardless. They did nothing. ” Refer to “Kueneza Injili kwa Methali” which means, ‘Spreading the Gospel through Proverbs’, page 58.

Leviticus 19:34.

Luke 10: 31-33.

Romans 15: 7.

Hebrews 13: 2.

Genesis 18: 1-8.

1Kings 17: 10-16.

Matthew 25: 31-46.

687. UYO UKALYAGA NAG’HWE ALAKUBHULAGA.

Ulusumo lunulo, lufumilile kumahoya ga bhanhu abho bhagiganikaga giki, abhanhu abhadibha namhala, ulu bhacha, bhagabhulagagwa na bhanhu abho bhagalyaga nabho. Uumo agayomba, ‘UMulungu adasolaga abhadoni, kunguno uweyi agasolaga bhanamhala na bhagigulu abho bhalimala ilikanza lya gwikala umusi munumu.’

Ung’wiye agabhuja, “ni bhule na bhayanda kihamo na bhanike bhagachaga bhabhaleka bhakuji?” Uweyi agashosha, ‘abhenabho bhagabhulagagwa na bhichabho, abho bhagikalaga nabho.’ Hunagwene  abhanhu bhagayombaga giki, ‘uyo ukalyaga nang’we alagubhulaga.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa ku bhanhu abho bhali na bhobha bho gulogwa, nulu abho bhagitilagwa yabhubhi na bhanhu abho bhali hakaya yabho. Abhoyi bhagiganikaga giki, abhanhu bhagibhulagaga bhoyi bhinikili. Abhanhu bhenabho, ulu ucha nyanda, nulu ng’waniki, bhagayombaga giki, ‘dugibhulagaga yise bhinikili UMulungu adahayile.’

Aliyo ulu ucha nkuji, abhoyi bhagayombaga giki, ‘adalogilwe, aliyo osolagwa na Mulungu.’ Uwikaji bho bhanhu bhenabho, nulu munhu agacha bho gung’wishiwa sumu, bhagiganikaga giki ologagwa. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘uyo ukalyaga nang’hwe alagubhulaga.’ Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 56.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kuleka bhobha bho gulogwa kunguno, ubhobha bhunubho, bhugenhaga widumi ubho gwenheleja nulu gubhabhulaga abhichabho abho bhadinabhuhubhi.

“Bhuli munhu uyo adantogagwa ndugu okwe alimhulagi. Uweyi adina bhupanga umugati yakwe, guti umo dulisomela umu nyalubha ya ng’wa Mt. Yohane. Giko uludubhatogwa abhigisu dabhitaga gufuma mulufu na gwingila mubhupanga.

Dudulile gwibhuja giki, ubhulogi bhulihoyi nulu ginehe? Dudulile guhaya giki: ubhulogi bhadiho aliyo ushetani alihoyi. Abhalogi bhadiho, aliyo umumiganiko ga ng’wa munhu uyo agogohaga abhalogi bhalihoyu ukuliweyi.”

Gashinaga ubhobha bho bhulogi bhugigelaga mu gugikija gwitogwa yise kubhayise. Ulu yise bhose ditogilwe guti umo ubhulangwa bhokwe UYesu Kristo, adiho munhu nulu umo alogoha gulogwa.

Ayise dugabhizaga bhakali ugugabhinza amalagilo ga ng’wa Mulungu. Aliyo dugogohaga gulogwa na gucha. Ilihambohambo dubhize bhakali gucha, hangi dubhize na bhobha bho gwita shibhi guti UYesu umo amooyombela: “Mdizubhogoha abho bhagabhulagaga mili, aliyo bhadadulile guibhulaga inholo. Ilihambohambo gung’wogoha uyo adulile gujikenagula jose mili kihamo ni nholo mumoto.”

Ahenaha ugung’ogoha Mulungu ilinabhulingisilo bho gunhang’wa. UMulungu wise alio mholele, adi obhobha. Ubhobha bhudafumaga kuli Mulungu aliyo kuli shetani. “Aho bhulihoyi bhutogwa bhudiho ubhobha; kunguno ubhutogwa ubhushikanile bhugabhupejaga ubhobha pye ubhose. Bhasi, umunhu uyo alina bhobha, adinashigana umubhutogwa,” (1Yohane 4:18). Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 57.

Mambo ya Walawi 19:31.

Wagalatia 5:19-20.

1Yohane 3:14-15.

Mathayo 5:21.

Mathayo 26:23, 50.

KISWAHILI: ANAYEKULA NAWE NDIYE ATAKAYEKUUA.

Methali hiyo, ilianzia kwenye maongezi ya watu wanaomini kwamba, vijana wanaokufa huuliwa na watu wanaokula nao. Mmoja alisema, ‘Mungu hachukui vijana, kwa sababu yeye huchukua wazee waliomaliza muda wao wa kuishi.’ 

Mwenzake aliuliza, “Mbona hata vijana hufa na kuwaacha wazee?”  Yeye alimjibu kwamba, “vijana huuliwa na watu wanaokula nao, ambao wanawafahamu vizuri.” Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘anayekula nawe ndiye atakayekuua.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa watu wale wanaoamani kulogwa au wale wanaotemdewa mabaya na watu walioko kwenye familia yao. Wenyewe wanaamini kwamba, watu huwa wanauana wenyewe. Watu hao, akifa kijana, husema kwamba, “tunajiua sisi wenyewe Mungu hataki.”

Lakini akifariki mzee, wao husema kwamba, “hakulogwa, bali amechukuliwa na Mungu.” Maisha ya watu hao, hata kama mtu akifariki kwa kupewa sumu, wao huamini kwamba amelogwa. Ndiyo maana huwa wanasema kwamba, ‘anayekula nawe ndiye atakayekuua.’ Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 56.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuacha hofu ya kuamini kulogwa kwa sababu hofu hiyo, huwajengea chuki ya kupelekea hata kuwaua wenzao wasio na hatia.

“Kila mtu asiyempenda ndugu yake ni mwuaji. Yeye hana uzima ndani yake, kama tunavyosoma katika waraka wa Mtakatifu Yohane.  Hivyo tukiwapenda wenzetu tumekwisha pita kutoka kifo na kuingia katika uzima.

Tunaweza kujiuliza kama uchawi upo au la. Tunaweza kujibu: Uchawi haupo, ila shetani yupo. Wachawi hawapo, isipokuwa katika mawazo ya mtu anayesadiki na anayeogopa kwake huyo wachawi wapo.”

Kumbe hofu ya uchawi inatokea kwa kutopendana sisi kwa sisi. Ikiwa sisi sote tunapendana kadiri ya mafundisho yake Yesu Kristo, hakuna mtu, hata mmoja atakayeogopa kulogwa.

Sisi huwa wakali kuvunja amri za Mungu. Lakini tunaogopa kulogwa na kufa. Ni afadhali tuwe wakali kufa, tena tuwe na hofu ya kutenda dhambi kama Yesu alivyosema: “Msiwaogope wale wauao mwili, lakini hawawezi kuiua roho. Afadhali kumwogopa yule awezaye kuangamiza mwili pamoja na roho motoni.”

Hapa kumwogopa Mungu, kuna maana ya kumcha. Mungu wetu ni Mungu wa amani, si wa hofu. Hofu haitoki kwa Mungu, bali kwa shetani. “Palipo na upendo hapana woga; naam; Upendo kamili hufukuza woga wote. Basi, mtu mwenye woga hajakamilika bado katika upendo.” (1Yohane 4:18). Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 57.

Mambo ya Walawi 19:31. ““Msiwaendee waaguzi, wala msitafute wapunga pepo, kwa maana vitawanajisi. Mimi ndimi BWANA Mungu wako.”

Wagalatia 5:19-20. “Basi matendo ya mwili ni dhahiri nayo ni haya: Uasherati, uchafu, ufisadi, kuabudu sanamu, kuamini uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi”

1Yohane 3:14-15. “Sisi tunajua ya kwamba tumepita kutoka mautini kuingia uzimani, kwa sababu tunawapenda ndugu. Kila asiyempenda ndugu yake akaa mautini. Ye yote amchukiaye ndugu yake ni mwuaji, nanyi mwajua ya kwamba mwuaji hana uzima wa milele ndani yake.”

Mathayo 5:21. “Mmesikia walivyoambiwa watu wa zamani kwamba, ‘Usiue, ye yote atakayeua atapasiwa hukumu.’”

Mathayo 26:23, 50. “Yesu akawaambia, ‘‘Yule aliyechovya mkono wake katika bakuli pamoja nami, ndiye atakayenisaliti.” “Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya kile ulichokuja kufanya hapa.”

children green

child2

 

ENGLISH: HE WHO KILLS YOU IS THE ONE YOU SHARE A PLATE WITH.

This proverb comes from a conversation of people who were arguing that teenegers cannot easily die but old people do. One of them said, ‘God does not take young people, because He takes only elders whose time to stay on eath is over. The other one asked, “Why do even young people die and leave the elders?” He replied that, “young people are killed by their fellow human beings. This response on why teenegars die brought about the proverb ‘he who kills you is the one you share a plate with.’

This proverb can be compared to those people who believe on witchcraft. They hold a belief that human beings kill fellow humans. When they hear that a young person has died, the comment from them can easily be, “We kill ourselves, God doesn’t want.” But, when an old person dies they say, “He/she was not bewitched, but taken by God.” There are times one can die of poison still such people will say he/she has been bewitched by his/her close relatives. That is why they often say, ‘He who kills you is the one you share the plate with’ (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 56). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

This proverb teaches people to stop being fearful in life. They don’t have to believe on witchcraft and people should not dare to impart fear to others because, in doing so, they can cause death.

Anyone who hates a brother or sister is a murderer, and you know that no murderer has eternal life residing in him, as we read in the epistle of St. John. So, having loved our fellows, we have passed from death unto life.

We may wonder if witchcraft exists or not. We can answer: Witchcraft does not exist, but Satan exists. Witches do not exist, except in the imagination of someone who believes and is afraid of them. ”

And the fear of witchcraft stems from not loving one another. If we all love one another, according to the teachings of Jesus Christ, no one will be afraid of being bewitched.

We are often in violation of God’s commandments. But we are scared of death. It is better for us to be fierce to die, and be afraid to sin as Jesus said: “Do not be afraid of those who kill the body but cannot kill the soul. Rather, be afraid of the one the one who can destroy both soul and body in hell.”

Here to fear God, it means to adore Him. Our God is a God of peace, not of fear. Fear comes not from God, but from Satan. “Where there is love there is no fear; yes; perfect love casts out all fear. Therefore, the man who fears is not made perfect in love ” (1 John 4:18) (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 57).

Leviticus 19:31. Galatians 5: 19-20. 1 John 3: 14-15. Matthew 5:21. Matthew 26:23, 50.