Sukuma Proverbs

699. BUGALI WA HENAHA WA KUGULA IDAKO.

Yalihoyi kaya imo ya bhanhu bhabhili, ngosha na nkima. Ungosha wipunaga guja gungunda gujulima,  oneka unkima alizuga jiliwa ja guchala ukumilimo yabho, kugiki bhagalye kihamo. Aliyo lulu, unkima ng’wunuyo, okelejaga noyi bhuli lushiku uguchala ijiliwa jinijo.

Lushigu lumo, ungoshi agang’wila unke okwe, ‘intondo dugwipuna pye abhose dugalime mpaga ikanza ilebhe, hunadugushoka kaya gwiza gulya jiliwa. Unke okwe ashosha, ‘nahene dugwipuna dugalime ulu dushoka nagwiza nazuge ijiliwa dulya.’

Aho wela ubhujiku, bhagipuna diyu bhugalima mpaga lyushika ikanza ilebhe bhushoka kaya gwiza gulya jiliwa. Ungosha ung’wila unke, ‘zugaga lulu ijiliwa dulye.’ Unke ushosha, ‘nahene nazuge.’

Unkima ng’wunuyo, agandya guzuga hado hado nose ungosha, unoga ugwigasha. Umuja, ‘umukaya  ng’wabisha ijiliwa?’ Unke okwe ushosha, ‘degelaga.’ Ungosha agankomeleja, ‘kangilijaji uguzuga, nose gayusada amadako ugwishasha.’

Oganoga unke okwe obhisha ijiliwa na gujitenga, unkabhulisha ungoshi, ‘karibhu lulu dabisha ijiiwa.’ Ungoshi wiza ugulya aliyomba, ‘bugali wa henaha wa gugula idako.’ Ubhunubho huwandijo bho gutumimalwa go lusumo lunulo.

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli ngosha nulu ng’wimeji ulu nke okwe alikeleja gubisha jiliwa kunguno ya bhugokolo, nulu bhugulu bhokwe. Ugugula idako  yili guyomba: Ulilipa bho wiyumilija bho madako kunguyo ya gulindila jiliwa kuli kanza lilifu. Udulipaga hela aliyo ulilipa. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘bugali wa henaha wa kugula idako.’ Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 72.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na bhukamu bhutale ubho gubhambilija uguitumama chiza imilimo yabho, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi, umuwikaji bhobho.

“Dulidakilwa gutumama milimo ku bhukamu bhuli ikanza ilo dulibhatumamila abhigusu nulu ulu dulintumamila Sebha. UMulungu adatogishiyagwa nu munhu uyo agantumimalaga bho nduhu bhukamu nulu moyo go gutogwa.

Dudizubhiza  hagatigati umuguntumamila Sebha, aliyo dubhize moto, giki, duntogwe ku moyo gwise gose, masala gise gose, na nguzu jise jose. Hangi dulidakilwa gubhatumamila abhigisu bho bhukamu na moyo go bhutogwa gitumo agitila UYesu Kristo ng’winikili.” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 72.

Wakolosai 3:23-24.

Ufunuo 3:16.

Waebrania 6:12.

Waroma 12:11.

KISWAHILI: UGALI WA HAPA NI WA KUNUNUA TAKO.

Ilikuwepo familia moja yenye watu wawili, mme na mke. Mwanamume alikuwa alijilawa asubuhi na mapema kwenda kulima shambani, alimuacha mke wake akipika chakula cha kupeleka shambani ili wakale huko kwa pamoja. Lakini basi, mwanamke huyo, alikuwa akichelewa sana kila siku kupeleka chakula hicho.

Siku moja, mwanamume alimwambia mke wake, ‘kesho tutaamuka mapema wote twende shambani tukalime mpaka wakati fulani ndipo tutarudi nyumbani kuja kula chakula.’ Mke wake akajibu, ‘sawa tutaamuka mapema asubuhi tukalime tukirudi nitakuja kupika chakula tule.’

Kesho yake waliamuka asubuhi kwenda shambani kulima mpaka ukafika wakati fulani, wakarudi nyumbani kula chakula. Mwanamume alimwambia mke wake, ‘pika basi chakula tule.’ Mke wake akajibu, ‘sawa napika.’

Mwanamke huyo, alianza kupika pole pole, mwishowe mume wake, akashoka kukaa. Akamuuliza, ‘humo ndani mmeivisha chakula?’ Mke wake akajibu, ‘tumekaribia.’ Mume wake akamhimiza, ‘fanyeni haraka, mwishowe matako yameanza kuuma kukaa.’

Mwishowe mke wake aliivisha chakula, akakipeleka mezani na kumkaribisha mumewe akisema, ‘karibu basi tumeivisha chakula.’ Mume wake alinuka kwenda kula chakula mezani akisema, ‘ugali wa hapa ni wa kunulua tako.’ Huo ndiyo ukawa mwanzo wa kutumika kwa methali hiyo.

Methali hiyo, hulinganishwa kwa bwana au mtani ikiwa mke wake anachelewa kuivisha chakula kwa sababu ya uvivu au ujeuri wake. Kununua tako ni kusema: Unalipa kwa maumivu ya matako kwa sababu ya kusubiri chakula kwa muda mrefu. Hulipi pesa lakini unalipa. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘ugali wa hapa ni wa kunulua tako.’ Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 72.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methail hiyo, hufundisha watu juu ya kuyatekeleza majukumu yao kwa bidii kubwa, ili waweze kupata mafanikio mengi zaidi katika maisha yao.

“Yatupasa kufanya kazi kwa bidii kila tunapowatumikia wenzetu au tunapomtukika Bwana. Mungu hapendezwi na mtu anayemtumikia bila bidii au moyo wa kupenda. Tusiwe vuguvugu katika kumtumikia Bwana, bali tuwe moto, yaani tumpende kwa moyo wetu wote, akili zetu zote na nguvu zetu zote. Tena yatupasa kuwatumikia wenzetu kwa bidii na moyo wa upendo kama alivyofanya Yesu Kristo mwenyewe.’ Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 72.

Wakolosai 3:23-24. “Lo lote mfanyalo, fanyeni kwa moyo kama watu wanaomtumikia Bwana na si wanadamu. Kwa kuwa mnajua kwamba mtapokea urithi wenu kutoka kwa Bwana kuwa thawabu yenu”

Ufunuo 3:16. “Hivyo kwa kuwa u uvuguvugu, kwamba wewe si baridi wala si moto, nitakutapika utoke kinywani Mwangu.”

Waebrania 6:11-12. “Nasi twataka kila mmoja wenu aonyeshe bidii iyo hiyo ili mpate kujua uhakika kamili wa lile tumaini mpaka mwisho, ili msije mkawa wavivu, bali mpate kuwaiga wale ambao kwa imani na saburi hurithi zile ahadi.”

Waroma 12:11. “Msiwe wavivu, bali mwe na bidii katika roho mkimtumikia Bwana.”

ghana1

ghana child-

food1

 

ENGLISH: UGALI IN THIS HOUSE IS BOUGHT THROUGH YOUR BUTTOCKS.

There was one family with two people, husband and wife. The man would wake up very early in the morning going to the farm. And the woman could delay a bit because she has to cook some meal and carry it with her to the farm and eat with her husband. But this woman used to be late everyday to bring food for the man.

One day the man told his wife that all of them have to leave home very early in the morning without carrying food and that, food will be eaten when they come back from the farm. The wife agreed with the man and left for the farm. When they came back from the farm, the woman went to the kitchen and spent a lot of hours cooking the food until the man became tired of waiting for food. The man kept on asking for food and the woman could reply, wait; it will be done soon.

The man waited until his buttocks began to pain for too much sitting. When the food was ready, the man was invited to eat and he said ‘ugali in this house is bought through your buttocks.’ This marked the beginning of this saying.

This saying can be compared to a person who is lazy or cruel in his/her life. Such a person will not help others easily during distress times. People of this nature will enjoy seeing others suffer (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 72). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications Ndanda – Peramiho, 1984.

This saying teaches people how to carry out their tasks with great effort so that they can achieve more success in their lives.

We must work hard every time we serve our fellowmen or when we serve the Lord. God is displeased with someone who serves Him with little effort. Let us not be slothful in serving the Lord, but zelous, loving Him with all our heart, mind, and strength. We must serve our fellow men with as much zeal and love as Jesus Christ Himself (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 72).

Colossians 3: 23-24. Revelation 3:16. Hebrews 6:12. Romans 12:11.

698. AHO UKADAHILAGA NA HAHO BUNYELO.

Ikale olihoyi munhu uyo olimulugendo lo guja halebhe. Aliyo lulu, umunhu ng’wunuyo, agakolwa nota noyi. Ukubahati ya wiza, agashiga mumongo umo agadula gukumba lyinzi ung’wa aminzi mpaga ufula inota yakwe.

Oho omala ugung’wa aminzi gaha lyinzi lunulo, aganyela mumo lyinzi  lunulo, ulo odahilaga aminzi genayo, adizukaga igiki alakolwa nota hangi wiza gung’wa minzi hoyi.  Hunagwene abhanhu bhagandya guyung’wila giki, ‘aho ukadahilaga na haho bhunyelo.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo okaribhushiyagwa chiza ha kaya ya ng’wa munhu. Ubhegejiyawa chiza guti ndugu ohakaya yiniyo, bhuyulya kihamo na gwendelea.

Aha ngelelo yaho, umunhu ng’wunuyo, ushiya nu mayu uoha kaya yiniyo, nulu, wibha ginhu hoyi, nulu wita jito jose jose ijo jidijawiza.’ Ugubhilitia ya bhubhi abhanhu bhenabho, yikolile na gunyela oho agadahilaga minzi, umunhu ng’wunuyo. Hunagwene abhanhu bhang’wilaga giki, ‘aho ukadahilaga na haho bhunyelo.’ Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 70.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na bhulumbi ukubhanhu abho bhalibhitila ya wiza, bho kuleka ugubhitila iyabhubhi, kugiki bhadule gwendelea gwiyambilija chiza, umuwikaj bhobho.

“Abhanhu abho dugabhitililaga yabhubhi bhali bhanhu abho dugikalaga kihamo nabho. Dugemele: ugushiya nu nkima o nzenganwa, gung’wibhila nwani, na gwendelea.

Hangi iyiniyo yili jigemelo ukubhumani wise nu Yesu Kristo uyo agadubokelaga kuwizang’holo na gwifunya gete kubhise guti nwani. Ningiki odutogwa, bho miito gise mabhi duganhemaga na gundalaha.

Hangi umusakramenti ya Ekaristia tugadumaga ugunkuja kunguno dugalyaga mili gokwe na gung’wa mininga gakwe bho nduhu ugwigelelwa. Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 71.

Zaburi 55:12-14.

Mathayo 26:49-50.

Yohone 13:21, 25-26.

1Wakorintho 11:27.

UCHOTEAPO NDIPO UNAPONYEA.

Zamani alikuwepo mtu mmoja aliyekuwa katika safari yake ya kwenda sehemu fulani. Lakini basi mtu huyo, alijisikia kiu kali sana. Kwa bahati nzuri, alifika mtoni ambamo alifaulu kuchimba kisima akanywa maji mpaka akakidhi kiu yake.

Alipomaliza kunywa maji ya kwenye kisima hicho, alinyea kwenye kisima hicho alimoyachotea maji hayo, bila kukumbuka kwamba atajisikia kiu tena na kurudi pale kung’wa maji. Ndiyo maana watu wakaanza kumwambia kwamba, ‘uchoteapo ndipo unaponyea.’

Methali hiyo hulinganisha kwa mtu yule ambaye amekaribishwa vizuri kwenye nyumba ya mtu. Akatendewa vizuri kama mmoja wa jamaa, wakila pamoja na kadhalika.

Mwishowe mtu huyo, huzini na mama wa kaya hiyo, au huiba au hutenda kitendo chote chote, ambacho si kizuri. Kuwafanyia ubaya watu hao, hufanana na kunyea pale achoteapo maji mtu huyo. Ndiyo maana watu humwambia mtu huyo, kwamba ‘uchoteapo ndipo unaponyea.’. Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 70.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na shukrani kwa watu wanaowatendea mema kwa kuacha kuwatendea mabaya, ili waweze kuendelea kusaidiana vizuri, katika maisha yao.

“Watu ambao tunawatendea mabaya ni watu (wale) ambao tunaokaa pamoja nao. Kwa mfano: Kuzini na bibi wa jirani, kumwibia rafiki, na kadhalika.

Tena hii ni mifano kwa uhusinano wetu na Yesu Kristo anayetupokea kwa ukarimu na kujitoa kwetu kabisa kama rafiki. Ijapokuwa ametupenda, kwa matendo yetu mabaya, huwa tunamkataa na kumdharau.

Tena katika sakramenti ya Ekaristi huwa tunashindwa kumheshimu kwa sababu tunakula mwili wake na kunywa damu yake bila kustahili.” Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 71.

Zaburi 55:12-14. “Kama aliyenitukana ni adui yangu ningevumilia, kama mtu mwovu angejiinua dhidi yangu, ningejificha asinione. Kumbe ni wewe, mwenzangu, mshiriki na rafiki yangu wa karibu, ambaye wakati fulani tulifurahia ushirika mzuri tulipokuwa tukienda katikati ya umati hekaluni mwa Mungu.”

Mathayo 26:49-50. “Mara akamjia Yesu na kumsalimu, “Salaam, Rabi!’’ Akambusu. Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya kile ulichokuja kufanya hapa.”

Yohane 13:21, 25-26. “Baada ya kusema haya, Yesu alifadhaika sana moyoni, akasema, ‘‘Amin, amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.’’ Yule mwanafunzi akiwa amemwegemea Yesu akamwuliza, ‘‘Bwana tuambie ni nani?’’   Yesu akajibu, ‘‘Ni yule nitakayempa hiki kipande cha mkate baada ya kukichovya kwenye bakuli.’’ Hivyo baada ya kukichovya kile kipande cha mkate, akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskariote.”

1Wakorintho 11:27. “Kwa hiyo, mtu ye yote alaye mkate huo au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa na hatia ya dhambi juu ya mwili na damu ya Bwana.”

drinking water

water-fetchers.1

water-fetchers

 

ENGLISH: YOU DEFACATE WHERE YOU FETCH WATER FROM.

Once upon a time ago, there was a man who was travelling to a certain place. This man reached a point when he was feeling thirsty. To quinch his thirsty, he went to a waterlogged place and dag a small hole where he can get water to drink. When he drank water to his satisfaction, he never thought of wanting water again. He defecated in the water and left. This is where the saying ‘you defacate where you fetch water from’ came from.

This saying can be compared to a person who is well received by his/her host but, instead of appreciating him/her for the kindness, he/she turns around abusing him/her. The abuse can be like committing adultery with the wife/husband of the host, stealing some of the host’s properties, etc. (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 70). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

This saying teaches people to be thankful to people who do good to them. People should stop doing evils in order to have good life and good relationship with others.

The people we are abusing are the people we are living with. For example, committing adultery with a neighbor’s wife, robbing a friend, and so on.

Again these are examples of our association with Jesus Christ, who graciously accepts us and gives Himself completely as a friend. Although He loves us, by our evil deeds, we often reject and despise Him.

And in the sacrament of the Eucharist we often fail to honor Him because we eat His flesh and drink His blood unworthily (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 71).

Psalm 55: 12-14. Matthew 26: 49-50. John 13:21, 25-26. 1 Corinthians 11:27.

697. AHO UKALILAGA HAHO UKANYELAGA.

Aho kale olihoyi munhu uyo oliogaiwa jiliwa ahikanza lya nzala. Umunhu ng’wunuyo, ojaga agucholaga jiliwa uko usimizilaga. Lushigu lumo agajipandika ijiliwa ulya mpaga wiguta. Oho omala ugulya, aganyela haho olilaga ijiliwa jilinijo, adizukaga igiki alashoka hoyi alye hangi.  Hunagwene abhanhu bhagandya guyung’wila giki, ‘aho ukalilag haho ukanyelaga.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo okaribhushiyagwa chiza ha kaya ya ng’wa munhu. Ubhegejiyawa chiza guti ndugu ohakaya yiniyo, bhuyulya kihamo na gwendelea.

Aha ngelelo yaho, umunhu ng’wunuyo, ushiya nu mayu uoha kaya yiniyo, nulu, wibha ginhu hoyi, nulu wita jito jose jose ijo jidijawiza.’ Ugubhilitia ya bhubhi abhanhu bhenabho, yikolile na gunyela oholilaga, umunhu ng’wunuyo. Hunagwene abhanhu bhang’wilaga giki, ‘aho ukalilag haho ukanyelaga.’ Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 70.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na bhulumbi ukubhanhu abho bhalibhitila ya wiza, bho kuleka ugubhitila iyabhubhi, kugiki bhadule gwendelea gwiyambilija chiza, umuwikaj bhobho.

“Abhanhu abho dugabhitililaga yabhubhi bhali bhanhu abho dugikalaga kihamo nabho. Dugemele: ugushiya nu nkima o nzenganwa, gung’wibhila nwani, na gwendelea.

Hangi iyiniyo yili jigemelo ukubhumani wise nu Yesu Kristo uyo agadubokelaga kuwizang’holo na gwifunya gete kubhise guti nwani. Ningiki odutogwa, bho miito gise mabhi duganhemaga na gundalaha.

Hangi umusakramenti ya Ekaristia tugadumaga ugunkuja kunguno dugalyaga mili gokwe na gung’wa mininga gakwe bho nduhu ugwigelelwa. Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 71.

Zaburi 55:12-14.

Mathayo 26:49-50.

Yohone 13:21, 25-26.

1Wakorintho 11:27.

KISWAHILI: UNAPOKULA PAPO HAPO UNAPOKWENDA HAJA.

Hapo zamani alikuwepo mtu aliyekosa chakula wakati wa njaa. Mtu huyo, alienda kutafuta chakula kule alipotembelea. Siku moja alipata chakula, akala mpaka agatosheka. Alipomaliza kula, alijisaidia papo hapo alipolia chakula. Ndiyo maana watu wakaanza kumwambia, kwamba, ’unapokula papo hapo unakokwenda haja.’

 Methali hiyo hulinganisha kwa mtu yule ambaye amekaribishwa vizuri kwenye nyumba ya mtu. Akatendewa vizuri kama mmoja wa jamaa, wakila pamoja na kadhalika.

Mwishowe mtu huyo, huzini na mama wa kaya hiyo, au huiba au hutenda kitendo chote chote, ambacho si kizuri. Kuwafanyia ubaya watu hao, hufanana na kunyea pale alipolia chakula mtu huyo. Ndiyo maana watu humwambia mtu huyo, kwamba ‘unapokula papo hapo unapokwenda haja. Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 70.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na shukrani kwa watu wanaowatendea mema kwa kuacha kuwatendea mabaya, ili waweze kuendelea kusaidiana vizuri, katika maisha yao.

“Watu ambao tunawatendea mabaya ni watu (wale) ambao tunaokaa pamoja nao. Kwa mfano: Kuzini na bibi wa jirani, kumwibia rafiki, na kadhalika.

Tena hii ni mifano kwa uhusinano wetu na Yesu Kristo anayetupokea kwa ukarimu na kujitoa kwetu kabisa kama rafiki. Ijapokuwa ametupenda, kwa matendo yetu mabaya, huwa tunamkataa na kumdharau.

Tena katika sakramenti ya Ekaristi huwa tunashindwa kumheshimu kwa sababu tunakula mwili wake na kunywa damu yake bila kustahili.” Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 71.

Zaburi 55:12-14. “Kama aliyenitukana ni adui yangu ningevumilia, kama mtu mwovu angejiinua dhidi yangu, ningejificha asinione. Kumbe ni wewe, mwenzangu, mshiriki na rafiki yangu wa karibu, ambaye wakati fulani tulifurahia ushirika mzuri tulipokuwa tukienda katikati ya umati hekaluni mwa Mungu.”

Mathayo 26:49-50. “Mara akamjia Yesu na kumsalimu, “Salaam, Rabi!’’ Akambusu. Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya kile ulichokuja kufanya hapa.”

Yohane 13:21, 25-26. “Baada ya kusema haya, Yesu alifadhaika sana moyoni, akasema, ‘‘Amin, amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.’’ Yule mwanafunzi akiwa amemwegemea Yesu akamwuliza, ‘‘Bwana tuambie ni nani?’’   Yesu akajibu, ‘‘Ni yule nitakayempa hiki kipande cha mkate baada ya kukichovya kwenye bakuli.’’ Hivyo baada ya kukichovya kile kipande cha mkate, akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskariote.”

1Wakorintho 11:27. “Kwa hiyo, mtu ye yote alaye mkate huo au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa na hatia ya dhambi juu ya mwili na damu ya Bwana.”

table food

tradition-

tradition1

ENGLISH: YOU DEFACATE WHERE YOU ATE FOOD FROM.

Once upon a time ago, there was a person who had no food during famine. One day this person travelled in search for food. He reached somewhere where he got food, ate it to his satisfaction. When he had satisfied with the food he defacate on that place. This is why people say ‘you defacate where you ate food from.’

 This saying can be compared to a person who is most welcomed in someone’s house. Such a person was well treated. Finally, instead of appreciating for the kindness, turns around the host by embarrassing him/her. This embarrassment can be stealing from his/her host or anything that disturbs their relationship (Refer to Kueneza Injili kwa Methali’ which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 70). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

This saying teaches people to be thankful to people who do good for them. They don’t have to return embarrassment for good things they have done to them.

The people we are abusing are the people we are living with. For example, committing adultery with a neighbor’s wife, robbing a friend, and so on.

Again these are examples of our association with Jesus Christ, who graciously accepts us and gives Himself completely as a friend. Although He loves us, by our evil deeds, we often reject and despise him.

And in the sacrament of the Eucharist we often fail to honor Him because we eat His flesh and drink His blood unworthily (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 71).

Psalm 55: 12-14. Matthew 26: 49-50. John 13:21, 25-26. 1 Corinthians 11:27.

696. NZUGA (NZUGILA) LUSEKO, NULU, NDEKA LUSEKO.

Aho kale olihoyi nkima umo uyo wikalaga ha chalo jilebhe. Lushigu lumo apandika ngeni uyo oliofumila kulipande lya kule. Ungeni  ng’wunuyo, oliotuubha noyi kunguno ya gusiminza lugendo lulihu.

Umayi ng’wunuyo, uyo oliombokela ungeni okwe, agandya mahoha higulya ya ginhu ja mbika ningi. Umumahoya genayo, ungenihwa omanaga wisekeleja bho nduhu ugunzugila ijiliwa ungeni okwe ng’wunuyo.

Nose ungeni ng’wunuyo, ubhona ubhujiku bhulingila bho nduhu uguzugilwa ijiliwa, ubadija giki, umayu uyo aliyitya wizang’holo bho golecha luseko lo hanze, gashinaga umugati ya ng’holo yakwe adahayile ungeni alye ijiliwa jakwe.

Ungeni ng’wunuyo, agagema gunhaga ung’wenyeji okwe, kugiki abhone niagushosha ginehe, bho guyomba, ‘mlihoyi unene nashoke kaya.’ Umayu uyo agashosha, ‘sawa dugwibhona lushiku lungi.’ Hunagwene abhanhu bhagandya guyung’witana umayu ng’wunuyo, giki ‘nzuga (nzugila) luseko.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agiyolechaga bho hanze giki ali ng’wizang’holo, aliyo umugati yakwe, ali ming’holo. Umunhu ng’wunuyo agamanaga useka na kuhoya kihamo nu ngeni bho nduhu ugunzugila ijiliwa.

Ulu munhu adatogilwe nulu adahayile ugugwitila ginhu jilebhe idilazima aguwile giki, nadagutogilwe au nadahayile; ugudula gudebha bho shitwa shakwe, guti numo agitila umayu uyo oliombokela ngeni. Hunagwene abhanhu bhagang’witanaga giki, ‘nzuga (nzugila) luseko.’ Lolaga kueneza Injili Kwa Methali, bhukurasa 66.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na wizang’holo bho ng’hana gufumila mu ng’holo jabho, gutinda ugubhiza bhibheleja giki wizang’holo, bho hanze duhu, aliyo bhiming’holo umumioyo yabho, kugiki bhadule gubhagola chiza abhageni bhabho, umuwikaji bhobho.

“Umuwikaji wise ubho ng’wa Kristo, amiito gali na solobho gukila imihayo. UYesu Kristo adayombile mihayo duhu bho nduhu miito. Aliyo wikalaga agubhitilaga ya wiza abhanhu mpaga uduchila ha nsalabha.

Ulu munhu adagutogilwe idilazima aguwile, “Nadagutogilwe” nulu “nadahayile.” Ugudula gumaga bho shitwa shakwe, guti nu kuli nkima uyo adazugaga jilila, aliyo guseka duhu.

Nulu ayise bhakristo ilijidamu noyi ugung’wila UYesu, “Nadagutogilwe”, nulu, nadahayile”. Aliyo dugampejaga bho miito gise mabhi. Dudanzugilaga UYesu Kristo, dugayombaga, “Sebha! Sebha! bho nduhu ugwikala gitumo bhuli ubhulangwa bhokwe.” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 66.

Yakobo 2:15-17.

1Yohane 3:18.

Mathayo 15:8.

Mathayo 7:21.

KISWAHLI: MPIKA KICHEKO.

Hapo zamani alikuwepo mama mmoja aliyeishi katika kijiji fulani. Siku moja alitembelewa na mgeni aliyetoka sehemu za mbali. Mgeni huyo alishikwa na njaa kwa sababu ya kusafiri safari ndefu.

Mama huyo alimpokea mgeni wake wakaanza maongezi yaliyohusu mambo mbalimbali. Katika maongezi hao, mwenyeji wake alikuwa akicheka sana bila kumpikia chakula mgeni wake huyo.

Mwishowe yule mgeni akaona usiku unaingia bila kupikiwa chakula, akagundua kwamba, mama yule anajifanya mkarimu kwa kuonesha kicheko cha nje, kumbe ndani ya moyo wake hataki mgeni huyo ale chakula chake.

Mgeni huyo, aliamua kujaribu kumuaga mwenyeji wake, ili aone kama atakubali au la, kwa kusema, ‘kwa heri mimi narudi nyumbani.’ Mama yule alijibu, ‘sawa tutaonana siku nyingine.” Ndiyo maana watu wakaanza kumuita mama yule, ‘mpika kicheko.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu anayejionesha kwa nje kuwa ni mkarimu, lakini kwa ndani ni mchoyo. Mtu huyo, huwa anacheka na kuzungumumza pamoja na mgeni, bila kumpikia chakula.

Ikiwa mtu hakupendi au hataki kukufanyia jambo fulani si lazima akuambie sikupendi au sitaki; utaweza kujua kwa vitendo vyake, kama alivyofanya yule mama aliyepokea mgeni. Ndiyo maana watu humuita mtu huyo huwa ni ‘mpika kicheko.’ Rejea kueneza Injili kwa methali, ukurasa 66.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na ukarimu wa kweli kutoka mioyoni mwao, badala ya kuwa wanafiki, ambao huuonesha ukarimu kwa nje tu, lakini kwa ndani ni wachoyo, ili waweze kuwatunza vizuri wageni wao, katika maisha yao.

“Katika maisha yetu ya Kikristo matendo yana maana kuliko maneno. Yesu Kristo hakusema maneno tu bila matendo. Bali alikuwa akiwatendea mema watu mpaka katufia msalabani.

Ikiwa mtu hakupendi si lazima akuambie, “Sikupendi” au “sitaki”. Utaweza kujua kwa matendo yake. Kama kwa mwanamke asiyepika chakula, ila kucheka tu. Hata sisi wakristo ni vigumu sana kumwambia Yesu, “Sikupendi”, au “sitaki”. Lakini huwa tunamfukuza kwa matendo yetu mabaya. Hatumpikii Yesu Kristo, tukisema “Bwana! Bwana!”, bila kuishi kadiri ya mafundisho yake.” Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 66.

Yakobo 2:15-17. “Ikiwa ndugu yako au dada hana mavazi wala chakula, mmoja wenu akamwambia, ‘‘Enenda zako kwa amani, ukaote moto na kushiba,’’ pasipo kumpatia yale mahitaji ya mwili aliyopungukiwa, yafaa nini? Vivyo hivyo, imani peke yake kama haikuambatana na matendo, imekufa.”

1Yohane 3:18. “Watoto wangu wadogo, tusipende kwa maneno au kwa ulimi bali kwa tendo na katika kweli.”

Mathayo 15:8. “‘Watu hawa huniheshimu kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.”

Mathayo 7:21. “Si kila mtu aniambiaye, ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa Mbinguni bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.”

african happy women

adult2

adults

 

ENGLISH: A COOK OF LAUGHTER.

Once upon a time ago there was a woman who lived in a certain village. One day this woman was visited by visitor and this visitor had walked for a long distance and she needed food. The host received her visitor and began conversation on different issues. The host could burst into laughter most of the time. She never thought of cooking for her guest. When the night was about to fall, the guest suggested to leave and the host replied , ‘Good luck, we will meet sometime.’ This why people began calling this host woman as someone who cook laughter.

This saying can be compared to a person who outwardly displays a generous heart, but inwardly, he/she is greedy. These are the people who will laugh and talk without thinking of cooking for their visitors.

If someone doesn’t like you or doesn’t want to do something for you, they don’t have to tell you ‘I don’t like you or I don’t want you;’ you will know by their actions. That’s why people call this host a ‘cook of laughter.’ (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 66). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

The saying teaches people to be genuinely generous from their heart, rather than hypocrites. In so doing, they can take good care of their guests in their lives.

“In our Christian life actions are more meaningful than words. Jesus Christ didn’t just say words without actions. But he was doing good to the people until He died on the cross.

If someone doesn’t love you he/she doesn’t have to tell you, “I don’t like you” or “I don’t want you”. You will know by their actions. As for a woman who does not cook food, only to laugh, even we Christians are very hard to say to Jesus, “I don’t love you”, or “I don’t want you”. But we usually expel Him through our evil deeds. We deny Jesus Christ by saying, “Lord! Lord! ”, without living up to His teachings (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 66).

James 2: 15-17. 1 John 3:18. Matthew 15: 8. Matthew 7:21.

695. WABYALILWA HIKULU.

Ulusumo lunulo, lwandija kubhanhu abho bhagankaribhusha ng’wichabho uyo agabhasanga bhalilya jiliwa bho gung’wila giki, ‘wabyalilwa hikulu.’ Mumho giki, wabyalilwa ha kaya iyo ili najiliwa, nulu hakaya ya ntemi.

“Ikale ulu munhu winhiwa bhutemi nu ubhutemi bhokwe bhubhiza na nzala agupejiwa umubhutemi, nu ulu ijiliwa jubhiza ja shili na ndulu, na gwendelea, ntemi ng’winuyo witanagwa ntemi obhakima. Ulu jiliwa ja bhusiga bhingi, agwitanwa ntemi o “Bhagosha”.

Ulu bhanhu bhumala ugulya bhagatulaga magofi guti numo bhitila ikale abho bhangishaga untemi, mumho giki, bhagasunde ijiliwa, kunguno utemi omalaga gubhita. Bhamalaga ugulya.” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, 64.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na wizang’holo bho gubhakaribhusha abhanhu aha jiliwa jabho, kunguno ijiliwa jili na solobho umugubhulang’hana ubhupanga bho bhanhu bhose.

“Umuwikaji bho munhu ijiliwa nulu ubhugali hi ginhu ja solobho noyi. Ubhugali hu ntemi wise kunguno agadulang’hanijaga ubhupanga wise.

Hangi UMhayo go ng’wa Sebha guli jiliwa ijojigadinhaga bhupanga bho ng’wa Mulungu ng’winikili ubho bhudakenagukaga.

ISakramenti iya Ekaristi jili jiliwa ng’hana na ja solobho noyi ijojibhugalang’hanaga na gubhujamya ubhupanga ubho bhuli bho ng’wa Mulungu umugati yise. “Uyo agulyaga mili gone na gun’gwa mininga gane, agikalaga mugati yane nu nene mugati yakwe.” (Yohana 6:56).

Uluushiga Mukanisa ugunsanga Untemi oko UYesu Kristo, alimo umu shimile sha Ngate umugati ya Tabarnakulo. Adingaga, nulu adabhitaga. Uguzunya gwise ugojigatoliki guliduwila na guduhagigish’ija giki, UYesu Kristo alimo nhana umu shimile sha ngate umu Sakramenti ya Ekaristia. Kuyiniyo, igeleliwe gunamya na gunkuja umu Sakramenti yiniyi Uweyi uyo Ali Ntemi wise bho guntulila mgofi.” Lolaga, Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 65.

Kumbukumbu 8:3.

Yeremia 15:16.

Yohane 4:34.

Yohane 6:11-15.

Yohane 6:51, 57.

Mathayo 6:11.

KISWAHILI: UMEZALIWA IKULUNI.

Methali hiyo, ilianzia kwa watu waliomkaribisha mwenzao aliyewakuta wakila chakula kwa kumwambia kwamba, ‘umezaliwa ikuluni.’ Maana yake amezaliwa kwenye kaya yenye chakula, au kaya ya mtemi.’

“Zamani ikiwa mtu amepewa utemi, na utawala wake ukawa na njaa, atafukuzwa katika utemi, na kama mavuno yatakuwa ya kunde, choroko, na kadhalika, mtemi huyo huitwa mtemi wa wanawake. Kama mavuno ya mtama ni tele, huitwa mtemi wa “Bagosha” wanaume.

Ikiwa watu wamekwisha kula huwa wanapiga makofi kama walivyofanya zamani wakimsalimu mtemi, maana yake wachukue vyombo, kwa kuwa mtemi amekwisha pita. Wamemaliza kula.” Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 64.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na ukarimu wa kuwakaribisha watu kwenye chakula chao, kwa sababu chakula ni muhimu katika kutunza uzima wa mwanadamu wote.

“Katika maisha ya mtu chakula au ugali ni kitu muhimu sana. Ugali ni mtemi wetu kwa kuwa unatutunzia uzima wetu.

Tena Neno la Bwana ni chakula ambacho kinatupa uzima wa Mungu ndani yetu, uzima wa Mungu mwenyewe usioharibika.

Sakramenti ya Ekaristi ni chakula kweli na cha maana sana kinachotunza na kuimarisha uzima ule wa Mungu ndani yetu. “Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, akaa ndani yangu nami ndani yake.” (Yohane 6:56).

Ukifika kanisani utamkuta mtemi wako Yesu Kristo yumo katika maumbo ya mkate ndani ya Tabernakulo. Haondoki au kupita. Imani yetu ya kikatoliki yatujulisha na kutuhakikishia kwamba Yesu Kristo yumo kweli katika maumbo ya mkate katika sakramenti ya Ekaristi. Kwa hiyo yatupasa kumwabudu na kumtukuza katika sakramenti hii yeye aliye mtemi wetu kwa kumpigia makofi.” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 65.

Kumbukumbu 8:3. “Alikudhili na kukufanya uone njaa kisha akulishe kwa mana, ambayo wewe wala baba zako hamkuijua, awafundishe kuwa mwanadamu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila neno litokalo katika kinywa cha BWANA.”

Yeremia 15:16. “Maneno yako yalipokuja, niliyala, yakawa shangwe yangu na furaha ya moyo wangu, kwa kuwa nimeitwa kwa jina lako, Ee BWANA Mungu, Mungu Mwenye Nguvu.”

Yohane 4:34. “Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma na kuikamilisha kazi yake.”

Yohane 6:11-15. “Ndipo Yesu akachukua ile mikate, akamshukuru Mungu na kuwagawia wale watu waliokuwa wamekaa kwa kiasi walichohitaji. Akafanya vivyo hivyo na wale samaki. Kila mtu akapata kadri alivyotaka. Watu wote walipokwisha kula na kushiba, akawaambia wanafunzi wake, “Kusanyeni vipande vilivyobaki vya ile mikate, kisipotee cho chote.’’ Hivyo wakavikusanya wakajaza vikapu kumi na viwili kwa vipande vilivyobaki vya ile mikate mitano na samaki wale wawili wadogo.

Baada ya watu kuona mwujiza ule Yesu aliofanya, walianza kusema, “Hakika huyu ndiye Nabii ajaye ulimwenguni!’’ Yesu akijua kwamba walitaka kuja kumfanya awe mfalme wao, kwa nguvu, akajitenga nao akaenda milimani peke Yake.”

Yohane 6:50- 57. “Lakini hapa kuna mkate utokao mbinguni, ambao mtu ye yote akiula, hatakufa. Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu ye yote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.’’

Ndipo Wayahudi wakaanza kuhojiana vikali wao kwa wao wakisema, “Mtu huyu awezaje kutupatia mwili wake tuule?’’ Hivyo Yesu akawaambia, “Amin, amin, nawaambia, msipoula mwili wa Mwana wa Adamu na kuinywa damu Yake, hamna uzima ndani yenu.

Mtu ye yote aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele. Nami nitamfufua siku ya mwisho. Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli. Ye yote alaye mwili wangu na kunywa damu yangu, atakaa ndani yangu nami nitakaa ndani yake. Kama vile Baba aliye hai alivyonituma Mimi, na kama nami ninavyoishi kwa sababu ya Baba, hivyo anilaye mimi ataishi kwa sababu yangu.”

Mathayo 6:11. “Utupe leo chakula chetu tunachohitaji.”

food woman

food-5

food-4

 

ENGLISH: YOU WERE BORN IN PALACE.

This saying comes from a certain person who arrived at his fellow’s house and found them eating food. As a way to welcome him, they said ‘you were born in palace’ to mean the land of plenty and abundance; a house of the king. In the past, when someone is installed as a king in a certain area he was to ensure that his people do not suffer from hunger and if the harvest will be only crops such as cowpeas, groundnuts and other food crops, he was regarded as a king of women. But if people will manage to have good harvests of crops such as sorghum, he will be regarded as the king of men.

Kings, in the past, were highly respected. This is why people could stand and cheer him up by clapping hands when he passes around. The same to food, people will tend to clap hands when they finish eating, in the same way they used to cheer up their king. In this case, their clapping of hands means calling someone responsible to collect the vessels after they have finished eating. They clap hands to mean that the ‘king has already gone’ Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 64). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

This saying teaches people about the generosity of welcoming people to their food, because food is essential to the wellbeing of the human body and life in general.

“In a person’s life food is the most important thing. Food is our king in that it gives us life.

Again the Word of the Lord is the food that gives us the life of God in us, the life of God Himself who is immortal.

The sacrament of the Eucharist is a true and very important food that sustains and enhances the life of God in us. “Whoever eats my flesh and drinks my blood dwells in me and I in him” (John 6:56).

When you get to the church you will find your Lord Jesus Christ in the form of bread in the Tabernacle. He doesn’t leave. Our Catholic faith informs us and assures us that Jesus Christ is indeed in the form of bread in the sacrament of Eucharist. Therefore, we must worship and glorify in this sacrament. ” (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 65).

Deuteronomy 8: 3. Jeremiah 15:16. John 4:34. John 6: 11-15. John 6:51, 57. Matthew 6:11.