Sukuma Proverbs

701. B’ULI HIWE B’UGIMBILIGWA.

Ulusumo lunulo, lyandija kuli ‘mayu uyo oshaga bhusiga hiwe. Umayu ng’wunuyo wilungujaga bho gwimba kugiki adule gwiyumilija umunimo gunuyo na gugutumama mpaga ha nhalikilo. Ugusha ahiwe jili ginhu ijo jidijinogu nu mayu agapandikaga bhukoyi. Aliyo kunguno ya matwajo ga nimo gokwe ayo galigelage ahanuma ya bhukoyi aliyumilija bho bhuyegi bho nduhu ugubhudilila ubhukoyi bhunubho.

Ulusumo lunulo lugatumilagwa kubhatinbwa ng’holo abhanhu abho bhali na makoye, nulu abhatumami kugiki bhikomeje umumakoye nulu umumilimo kunguno ubhukamu bhobho bhugubhiza bhuyegi ukubhoyi ahabhutongi na bhagulya matwajo ga nungula yabho.

Hangi ulusumo lunulo, lugatumilagwa kuli munhu uyo alikoyiwa na bhusatu bhulebhe. Ukuli munhu o mbika yiniyi ilidudaka gundilila umubhusatu bhokwe bho nduhu ugubhinzika moyo.’ Lolaga Kugundua Mbegu za Injili, ukurasa 12.

Ijitabho jinijo jigandikwa na Kamati ya Utafiti wa Utamaduni Bujora, ijojigahaririwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gutumama milimo bho wiyumilija na gubhatinbya ng’holo abhanhu bhabho, kugiki bhadule gutumama chiza imilimo yabho, na kupandika matwajo mingi, umuwikaji bhobho.

“Yadudaka ayise gwiyumilija umugunondela UYesu Kristo bho nduhu ugugwa ng’holo dikale na wisagiji bho gupandika matwajo ga nungula yise aho bhutongi. Dubhize guti mayu uyo oshaga bhusiga umo agiyumiligija bho bhuyegi na bho nduhu ugudilila ubhukoyi bhosebhose kunguno ya matwajo ga milimo yakwe ayo galigele aha bhutongi yaho.

Padre Emmanuli Makolo wi Jimbo lya Shinyaga, Tanzania agalwandika ulusumo lunulu: “Buli hiwe bukimbiligwa” umu kadi yakwe iya bhupadirisho. Giki, agagulenganija unimo go bhubadiri nu mayu uyo Alisha.” Lolaga Kugundua Mbegu ya Injili, 13.

Waroma 12:11.

Wagalatia 6:9.

Mathayo 24:13.

Yohane 16:21.

Ufunuo 2:10.

Luka 9:62.

KISWAHILI: ULIOKO KWENYE JIWE HUIMBIWA  (MSAGAJI HUJIFARIJI KWA KUIMBA).

Methali hiyo, ilianzia kwa ‘mama anayesaga mtama kwenye jiwe. Mama huyo hujifariji kwa kuimba aweze kuvumilia katika kazi hiyo na kuifanya mpaka mwisho. Kusaga kwenye jiwe ni jambo lisilo rahisi na mama huwa anapata masumbufu. Lakini kwa sababu ya matunda ya kazi yake yatakayopatikana baadaye huwa anajikaza kwa furaha bila kujali masumbufu hayo.

Methali hii hutumika kwa kuwatia moyo watu wenye shida au wafanyakazi ili wajitahidi katika shida au kazi, kwa sababu bidii yao itakuwa furaha kwao baadaye na watakula tunda la jasho lao.

Tena methali hiyo hutumika kwa mtu anayezidiwa na ugonjwa fulani. Kwa mtu wa namna hii inatupasa kumjali katika ugonjwa wake bila kukata tamaa.’ Rejea Kugundua Mbegu za Injili, ukurasa 12.

Kitabu hicho, kiliandikwa na Kamati ya Utafiti wa utamaduni Bujora, kilichohaririwa na watafiti: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1993.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kufanya kazi kwa uvumilivu na kuwatia moyo watu wao ili waweze kuyatekeleza majukumu yao vizuri na kupata mafanikio mengi, maishani mwao.

“Yatupasa sisi kupiga moyo konde katika kumfuata Yesu Kristo bila kukata tamaa tukiwa na tumaini la kupata matunda ya jasho letu hapo baadaye. Tuwe kama mama mwenye kusaga mtama anavyojikaza kwa furaha bila kujali masumbufu yoyote kwa sababu ya matunda ya kazi yake yatakayopatikana baadaye.

Padre Emmanueli Makolo wa Jimbo la Shinyanga, Tanzania aliandika methali hii: “Buli hiwe bukimbilagwa” kwenye kadi yake ya upadrisho. Yaani, alifananisha kazi ya upadre na kazi ya mama mwenye kusaga.’ Rejea Kugundua Mbegu ya Injili, ukurasa 13.

Waroma 12:11. “Msiwe wavivu, bali mwe na bidii katika roho mkimtumikia Bwana.”

Wagalatia 6:9. “Hivyo, tusichoke katika kutenda mema, kwa kuwa tutavuna kwa wakati wake tusipokata tamaa.”

Mathayo 24:13. “Atakayemumilia mpaka mwisho, ataokoka.”

Yohane 16:21. “Mwanamke anapokuwa na utungu wa kuzaa huwa na maumivu kwa sababu saa yake imewadia. Lakini mtoto akiisha kuzaliwa, yule mwanamke husahau maumivu hayo kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtoto ulimwenguni.”

Ufunuo 2:10. “Usiogope mateso yatakayokupata. Nakuambia Shetani atawatia baadhi yenu gerezani ili kuwajaribu, nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Uwe mwaminifu, hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.”

Luka 9:62. “Yesu akamwambia, “Mtu ye yote atiaye mkono wake kulima, kisha akatazama nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu.””

stone-grinding.2

stone-grinding

 

ENGLISH: THE GRINDER OF SORGHUM SINGS TO COMFORT HERSELF.

This proverb comes from a woman who was singing while grinding sorghum. This woman was able to console herself through singing until she finishes grinding. That is why people came with the proverb ‘the grinder of sorghum sings to comfort herself’ to describe this situation. Grinding sorghum on the stone is not an easy task; it needs courage and perseverance.

This proverb is used to encourage distressed people or workers to work and be courageous enough in performing some tasks because they will benefit in future. Also this proverb can be used in the context of sickness where the sick person needs to tolerate without despair (Refer to Kugundua Mbegu za Injili, which means, ‘Discovering the Seed of the Gospel,’ page 12). This book was written by the Bujora Cultural Research Committee, edited by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1993.

This proverb teaches people to work patiently and inspires people to be courageous in their lives. Patience and courage will make people to be responsible in whatever they decide to do in life. “We need to be heartfelt in following Jesus Christ without giving up hope of finding the fruit of our sweat. May we be like the grinding woman who happily presses herself with no worries because of the fruit of her labour.

Fr. Emmanuel Makolo from Shinyanga diocess, Tanzania, wrote the same proverb in his sovernior . That is, he likened the work of a priest to the work of a grinding mother (See Gospel Seed Discoveries, page 13).

Romans 12:11. Galatians 6: 9. Matthew 24:13. John 16:21. Revelation 2:10.Luke 9:62.

700. BULUNGALEKELE! NI SHITAKONZAGWA? SHIKAKONZAGWA.

“Ulusumo lunulo, lugatumilwa na Nkwilima aho umayu bhukwi okwe ogakeleja ugubisha ijiliwa.

Unkwilima aginga guja gujungisha umayu bhukwi okwe. Ugansanga alimhola, aliyo alitumama nimo go gulinda noni. Aho bhamala ugwigisha Unkwilima agayomga: “Mayu, nagubhona, nashoke kaya lulu.” Umayu agalema: “Ubhebhe ulingeni one. Ududula ugushoka na nzala. Nambilijage ugulinda inoni, nagagwigile nhomba.”

Unkwilima agalekwa lulu mungunda alilinda noni. Ungikulu agaja kaya ugandya guzuga jiliwa tamu. Uchola nyama njumu, ilina lyayo, “ng’homele”. Uguzuga inyama injumu lulu igasolaga ikanza lilihu noyi. Gwandija usibhuche minzi na guyoja bho minzi ga moto. Huna uibudagule ibhize ndogoleku. Hunawandya uguizuga na minzi. Aminzi ulu gukama, ongeja mabhele. Amabhele ulu gukama ongeja maguta.

Ungikulu atali aguzugaga makubhi, Unkwilima ubhona giki odila. Wandya gunmela bho mbisila umayu bhukwi okwe. Ulu alijipuga inoni aliyosemba, “bulungakele”, giki, “udilaga ugubisha ijiliwa.”  Ungikulu wigwa iyoaliiyomba Unkwilima uyomba: “Unkwilima one wandya gunimela ihaha.” Aha nhalikilo agabisha ijiliwa. Unkwilima nang’hwe agikomeja kuyomba: “Bulungakele” (“milele”).

Unkwilima agakalibhushiwa lulu gwiza gulya. Ungikulu nang’hwe uja ugujulinda inoni, wandya gunshokeja bho mbisila. Agayomba: “Ni shitakonzagwa? Shikakonzagwa.” Ugukonza, iligwita nimo hado hado bho bhulingisiji na wangaliji.

Ulusumo lunulo, lulidulanga gwiyumilija mpaga ilikanza lishige. Hangi lulidulanga gutumama milimo na wangaliji.” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa, 73.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

“Ilidudaka gubhiza bhiyumilija ulu kinhu jilebhe jidujaga gitumo bhuli ubhutogwa wise. Bhuli ginhu jili ni kanza lyajo. Igelelilwe dutule uwikaji wise mumakono ga ng’wa Mulungu bho nduhu ugukoyakoya. Aliho kihamo na yise alitutongela mubhuli mhayo, agudinhila kuli kanza lwakwe gitumo bhuli ubhupangi bhokwe.

Hangi, umuguntumamila Mulungu ilidudaka gubhiza na bhutaratibhu, wangaliji, na bhushikanu.” Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 74.

Mhubiri 3:1.

Wagalatia 4:4-5.

Luka 2:25-26.

Yakobo 5:10-11.

2Petro 1:10-11.

KISWAHILI: MILELE! SIYO LAZIMA KUFUATA UTARATIBU CHAKULA KIPIKWE VIZURI? NI LAZIMA KUFUATA UTARATIBU CHAKULA KIPIKWE VIZURI.

“Methali hii ilitumiwa na Mkwilima alipokawia mama mkwe kuivisha chakula.

Mkwilima aliondoka kwenda kumsalimu mama mkwe. Akamkuta mzima, lakini alikuwa na kazi ya kulinda ndege. Walipomaliza kusalimiana Mkwilima akasema: “Mama, nimekuona, nirudi sasa nyumbani.” Mama akataa: “Wewe ni mgeni wangu. Huwezi kurudi na njaa. Unisaidie kulinda ndege, nikupikie uji.”

Basi Mkwilima akaachwa shambani analinda ndege. Mzee akaenda nyumbani kwanza kupika chakula. Akatafuta nyama kavu, jina lake “ng’homele”. Basi kupika nyama kavu inakuchukua muda mrefu sana. Kwanza uchemshe maji na kuiosha kwa maji ya moto. Halafu kuipondaponda iwe laini. Sasa unaanza kupika na maji. Maji yakikauka unaongeza maziwa. Maziwa yakikauka unaongeza mafuta.

Mzee bado akipika mboga, Mkwilima akaona kwamba anakawia. Akaanza kumtania kwa fumbo mama mkwe. Anapowafukuza ndege anasema, “bulungakele”, yaani “umekawia kuivisha chakula.” Mzee anasikia anayosema Mkwilima akanena: “Mkwilima wangu ameanza kunitania sasa.” Mwisho akaivisha chakula. Mkwilima naye anazidi kusema: “Bulungakele” (“milele”).

Basi Mkwilima alikaribishwa kuja kula. Mzee naye akaenda kulinda ndege, akaanza kumjibu kwa fumbo. Akasema: “Ni shitakonzagwa? Shikakonzagwa.” Kukonza, maana yake, ni kufanya kazi pole pole kwa utaratibu na kwa uangalifu.

Methali hii inatufundisha kuvumilia mpaka wakati umefika. Tena inafundisha kufanya kazi kwa uangalifu.” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 73.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

“Inatupasa kuwa wavumilivu ikiwa jambo fulani haliendi kama yalivyo mapenzi yetu. Kila jambo lina wakati wake. Yatubidi kuweka maisha mikononi mwa Mungu bila kuhangaika. Yumo pamoja nasi akituongoza katika kila neno, atatufanikisha wakati wake kadiri ya mpango wake.

Tena, katika kumtumikia Mungu inatupasa kuwa na utaratibu, uangalifu na ukamilifu.” Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 74.

Mhubiri 3:1. “Kuna wakati kwa ajili ya kila jambo, nayo majira kwa kila tendo chini ya mbingu:”

Wagalatia 4:4-5. “Lakini ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe, ambaye alizaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria, kusudi awakomboe wale waliokuwa chini ya sheria, ili tupate kupokea zile haki kamili za kufanywa watoto wa Mungu.”

Luka 2:25-26. “Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake. Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.”

Yakobo 5:10-11. “Ndugu zangu, waangalieni manabii walionena kwa Jina la Bwana, ili kuwa mfano wa uvumilivu katika kukabiliana na mateso. Kama mnavyojua, tunawahesabu kuwa wamebarikiwa wale waliovumilia. Mmesikia habari za uvumilivu wake Ayubu na mmeona kile ambacho hatimaye Bwana alimtendea. Bwana ni mwingi wa huruma naye aliyejaa rehema.”

2Petro 1:10-11. “Kwa hiyo, ndugu zangu, fanyeni bidii zaidi kuuthibitisha wito wenu na uteule wenu, kwa maana mkifanya hivyo, hamtajikwaa kamwe. Kwa njia hii, mtajaliwa kwa ukarimu mwingi kuingia katika Ufalme wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo.”

nkima o ghana1

ghana man

african-millet-field

ENGLISH: “PERPETUAL! IS IT NOT NECESSARY TO FOLLOW RULES FOR COOKING FOOD CAREFULLY? IT IS NECESSARY TO FOLLOW RULES FOR COOKING FOOD WELL.”

This saying was used by a son-in-law when his mother-in-law cooked him food. One day the son-in-law went to visit his mother-in-law. By the time the man reached the place, she was busy chasing birds that were eating her cereals in the farm. When they had finished greeting  the son-in-law said: “Mama, I have seen you, and now I would like to leave for home. The mother-in-law refused saying: “You are my guest. You can’t go back hungry. Help me chasing the birds, and I cook you some food. ” The mother-in-law began the process of making her food. She took dried meat and cooked it (the process which took quiet a long time), she then boiled the meat, washed it, and pounded the meat in order to make it soft then final cooking. When cooking water dried, she added milk and finally fat (after the milk has dried).

After she had finished with meat, she began working on vegetables for her son-in-law to have delicious food. These processes made the man see his mother-in-law as someone who is very slow in her doings. He jokingly began talking to his mother-in-law in parables: “ bulungakele ,” that is, “you are late for food.” When the mother-in-law heard what the son-in-law said, she said to herself: “My son-in-law has started to joke me now.” The man kept on saying, bulungakele, “that is, you are late for food.” Thereafter, the food was brought, the man began eating the food and his mother-in-law took turn to chase birds in the farm.

In the same way, the mother-in-law began joking the son-in-law in parables: “perpetual! Is it not necessary to follow rules for cooking food carefully? It is necessary to follow rules for cooking food well.”

This proverb teaches us to persevere until the time has come. It also teaches us to be smart (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 73). This book was written by researchers: Dr. Donald Sybertz, M.M., and Joseph Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

We have to be patient if something doesn’t work out as we wish. Every thing has its time. We have to put life in God’s hands without worry. He is with us guiding us in every word, and He will fulfill His promises according to His plan.

Also, in serving God we must be orderly, careful and thorough (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 74).

Ecclesiastes 3: 1. Galatians 4: 4-5. Luke 2: 25-26. James 5: 10-11. 2 Peter 1: 10-11.

699. BUGALI WA HENAHA WA KUGULA IDAKO.

Yalihoyi kaya imo ya bhanhu bhabhili, ngosha na nkima. Ungosha wipunaga guja gungunda gujulima,  oneka unkima alizuga jiliwa ja guchala ukumilimo yabho, kugiki bhagalye kihamo. Aliyo lulu, unkima ng’wunuyo, okelejaga noyi bhuli lushiku uguchala ijiliwa jinijo.

Lushigu lumo, ungoshi agang’wila unke okwe, ‘intondo dugwipuna pye abhose dugalime mpaga ikanza ilebhe, hunadugushoka kaya gwiza gulya jiliwa. Unke okwe ashosha, ‘nahene dugwipuna dugalime ulu dushoka nagwiza nazuge ijiliwa dulya.’

Aho wela ubhujiku, bhagipuna diyu bhugalima mpaga lyushika ikanza ilebhe bhushoka kaya gwiza gulya jiliwa. Ungosha ung’wila unke, ‘zugaga lulu ijiliwa dulye.’ Unke ushosha, ‘nahene nazuge.’

Unkima ng’wunuyo, agandya guzuga hado hado nose ungosha, unoga ugwigasha. Umuja, ‘umukaya  ng’wabisha ijiliwa?’ Unke okwe ushosha, ‘degelaga.’ Ungosha agankomeleja, ‘kangilijaji uguzuga, nose gayusada amadako ugwishasha.’

Oganoga unke okwe obhisha ijiliwa na gujitenga, unkabhulisha ungoshi, ‘karibhu lulu dabisha ijiiwa.’ Ungoshi wiza ugulya aliyomba, ‘bugali wa henaha wa gugula idako.’ Ubhunubho huwandijo bho gutumimalwa go lusumo lunulo.

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli ngosha nulu ng’wimeji ulu nke okwe alikeleja gubisha jiliwa kunguno ya bhugokolo, nulu bhugulu bhokwe. Ugugula idako  yili guyomba: Ulilipa bho wiyumilija bho madako kunguyo ya gulindila jiliwa kuli kanza lilifu. Udulipaga hela aliyo ulilipa. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘bugali wa henaha wa kugula idako.’ Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 72.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na bhukamu bhutale ubho gubhambilija uguitumama chiza imilimo yabho, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi, umuwikaji bhobho.

“Dulidakilwa gutumama milimo ku bhukamu bhuli ikanza ilo dulibhatumamila abhigusu nulu ulu dulintumamila Sebha. UMulungu adatogishiyagwa nu munhu uyo agantumimalaga bho nduhu bhukamu nulu moyo go gutogwa.

Dudizubhiza  hagatigati umuguntumamila Sebha, aliyo dubhize moto, giki, duntogwe ku moyo gwise gose, masala gise gose, na nguzu jise jose. Hangi dulidakilwa gubhatumamila abhigisu bho bhukamu na moyo go bhutogwa gitumo agitila UYesu Kristo ng’winikili.” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 72.

Wakolosai 3:23-24.

Ufunuo 3:16.

Waebrania 6:12.

Waroma 12:11.

KISWAHILI: UGALI WA HAPA NI WA KUNUNUA TAKO.

Ilikuwepo familia moja yenye watu wawili, mme na mke. Mwanamume alikuwa alijilawa asubuhi na mapema kwenda kulima shambani, alimuacha mke wake akipika chakula cha kupeleka shambani ili wakale huko kwa pamoja. Lakini basi, mwanamke huyo, alikuwa akichelewa sana kila siku kupeleka chakula hicho.

Siku moja, mwanamume alimwambia mke wake, ‘kesho tutaamuka mapema wote twende shambani tukalime mpaka wakati fulani ndipo tutarudi nyumbani kuja kula chakula.’ Mke wake akajibu, ‘sawa tutaamuka mapema asubuhi tukalime tukirudi nitakuja kupika chakula tule.’

Kesho yake waliamuka asubuhi kwenda shambani kulima mpaka ukafika wakati fulani, wakarudi nyumbani kula chakula. Mwanamume alimwambia mke wake, ‘pika basi chakula tule.’ Mke wake akajibu, ‘sawa napika.’

Mwanamke huyo, alianza kupika pole pole, mwishowe mume wake, akashoka kukaa. Akamuuliza, ‘humo ndani mmeivisha chakula?’ Mke wake akajibu, ‘tumekaribia.’ Mume wake akamhimiza, ‘fanyeni haraka, mwishowe matako yameanza kuuma kukaa.’

Mwishowe mke wake aliivisha chakula, akakipeleka mezani na kumkaribisha mumewe akisema, ‘karibu basi tumeivisha chakula.’ Mume wake alinuka kwenda kula chakula mezani akisema, ‘ugali wa hapa ni wa kunulua tako.’ Huo ndiyo ukawa mwanzo wa kutumika kwa methali hiyo.

Methali hiyo, hulinganishwa kwa bwana au mtani ikiwa mke wake anachelewa kuivisha chakula kwa sababu ya uvivu au ujeuri wake. Kununua tako ni kusema: Unalipa kwa maumivu ya matako kwa sababu ya kusubiri chakula kwa muda mrefu. Hulipi pesa lakini unalipa. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘ugali wa hapa ni wa kunulua tako.’ Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 72.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methail hiyo, hufundisha watu juu ya kuyatekeleza majukumu yao kwa bidii kubwa, ili waweze kupata mafanikio mengi zaidi katika maisha yao.

“Yatupasa kufanya kazi kwa bidii kila tunapowatumikia wenzetu au tunapomtukika Bwana. Mungu hapendezwi na mtu anayemtumikia bila bidii au moyo wa kupenda. Tusiwe vuguvugu katika kumtumikia Bwana, bali tuwe moto, yaani tumpende kwa moyo wetu wote, akili zetu zote na nguvu zetu zote. Tena yatupasa kuwatumikia wenzetu kwa bidii na moyo wa upendo kama alivyofanya Yesu Kristo mwenyewe.’ Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 72.

Wakolosai 3:23-24. “Lo lote mfanyalo, fanyeni kwa moyo kama watu wanaomtumikia Bwana na si wanadamu. Kwa kuwa mnajua kwamba mtapokea urithi wenu kutoka kwa Bwana kuwa thawabu yenu”

Ufunuo 3:16. “Hivyo kwa kuwa u uvuguvugu, kwamba wewe si baridi wala si moto, nitakutapika utoke kinywani Mwangu.”

Waebrania 6:11-12. “Nasi twataka kila mmoja wenu aonyeshe bidii iyo hiyo ili mpate kujua uhakika kamili wa lile tumaini mpaka mwisho, ili msije mkawa wavivu, bali mpate kuwaiga wale ambao kwa imani na saburi hurithi zile ahadi.”

Waroma 12:11. “Msiwe wavivu, bali mwe na bidii katika roho mkimtumikia Bwana.”

ghana1

ghana child-

food1

 

ENGLISH: UGALI IN THIS HOUSE IS BOUGHT THROUGH YOUR BUTTOCKS.

There was one family with two people, husband and wife. The man would wake up very early in the morning going to the farm. And the woman could delay a bit because she has to cook some meal and carry it with her to the farm and eat with her husband. But this woman used to be late everyday to bring food for the man.

One day the man told his wife that all of them have to leave home very early in the morning without carrying food and that, food will be eaten when they come back from the farm. The wife agreed with the man and left for the farm. When they came back from the farm, the woman went to the kitchen and spent a lot of hours cooking the food until the man became tired of waiting for food. The man kept on asking for food and the woman could reply, wait; it will be done soon.

The man waited until his buttocks began to pain for too much sitting. When the food was ready, the man was invited to eat and he said ‘ugali in this house is bought through your buttocks.’ This marked the beginning of this saying.

This saying can be compared to a person who is lazy or cruel in his/her life. Such a person will not help others easily during distress times. People of this nature will enjoy seeing others suffer (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 72). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications Ndanda – Peramiho, 1984.

This saying teaches people how to carry out their tasks with great effort so that they can achieve more success in their lives.

We must work hard every time we serve our fellowmen or when we serve the Lord. God is displeased with someone who serves Him with little effort. Let us not be slothful in serving the Lord, but zelous, loving Him with all our heart, mind, and strength. We must serve our fellow men with as much zeal and love as Jesus Christ Himself (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 72).

Colossians 3: 23-24. Revelation 3:16. Hebrews 6:12. Romans 12:11.

698. AHO UKADAHILAGA NA HAHO BUNYELO.

Ikale olihoyi munhu uyo olimulugendo lo guja halebhe. Aliyo lulu, umunhu ng’wunuyo, agakolwa nota noyi. Ukubahati ya wiza, agashiga mumongo umo agadula gukumba lyinzi ung’wa aminzi mpaga ufula inota yakwe.

Oho omala ugung’wa aminzi gaha lyinzi lunulo, aganyela mumo lyinzi  lunulo, ulo odahilaga aminzi genayo, adizukaga igiki alakolwa nota hangi wiza gung’wa minzi hoyi.  Hunagwene abhanhu bhagandya guyung’wila giki, ‘aho ukadahilaga na haho bhunyelo.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo okaribhushiyagwa chiza ha kaya ya ng’wa munhu. Ubhegejiyawa chiza guti ndugu ohakaya yiniyo, bhuyulya kihamo na gwendelea.

Aha ngelelo yaho, umunhu ng’wunuyo, ushiya nu mayu uoha kaya yiniyo, nulu, wibha ginhu hoyi, nulu wita jito jose jose ijo jidijawiza.’ Ugubhilitia ya bhubhi abhanhu bhenabho, yikolile na gunyela oho agadahilaga minzi, umunhu ng’wunuyo. Hunagwene abhanhu bhang’wilaga giki, ‘aho ukadahilaga na haho bhunyelo.’ Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 70.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na bhulumbi ukubhanhu abho bhalibhitila ya wiza, bho kuleka ugubhitila iyabhubhi, kugiki bhadule gwendelea gwiyambilija chiza, umuwikaj bhobho.

“Abhanhu abho dugabhitililaga yabhubhi bhali bhanhu abho dugikalaga kihamo nabho. Dugemele: ugushiya nu nkima o nzenganwa, gung’wibhila nwani, na gwendelea.

Hangi iyiniyo yili jigemelo ukubhumani wise nu Yesu Kristo uyo agadubokelaga kuwizang’holo na gwifunya gete kubhise guti nwani. Ningiki odutogwa, bho miito gise mabhi duganhemaga na gundalaha.

Hangi umusakramenti ya Ekaristia tugadumaga ugunkuja kunguno dugalyaga mili gokwe na gung’wa mininga gakwe bho nduhu ugwigelelwa. Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 71.

Zaburi 55:12-14.

Mathayo 26:49-50.

Yohone 13:21, 25-26.

1Wakorintho 11:27.

UCHOTEAPO NDIPO UNAPONYEA.

Zamani alikuwepo mtu mmoja aliyekuwa katika safari yake ya kwenda sehemu fulani. Lakini basi mtu huyo, alijisikia kiu kali sana. Kwa bahati nzuri, alifika mtoni ambamo alifaulu kuchimba kisima akanywa maji mpaka akakidhi kiu yake.

Alipomaliza kunywa maji ya kwenye kisima hicho, alinyea kwenye kisima hicho alimoyachotea maji hayo, bila kukumbuka kwamba atajisikia kiu tena na kurudi pale kung’wa maji. Ndiyo maana watu wakaanza kumwambia kwamba, ‘uchoteapo ndipo unaponyea.’

Methali hiyo hulinganisha kwa mtu yule ambaye amekaribishwa vizuri kwenye nyumba ya mtu. Akatendewa vizuri kama mmoja wa jamaa, wakila pamoja na kadhalika.

Mwishowe mtu huyo, huzini na mama wa kaya hiyo, au huiba au hutenda kitendo chote chote, ambacho si kizuri. Kuwafanyia ubaya watu hao, hufanana na kunyea pale achoteapo maji mtu huyo. Ndiyo maana watu humwambia mtu huyo, kwamba ‘uchoteapo ndipo unaponyea.’. Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 70.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na shukrani kwa watu wanaowatendea mema kwa kuacha kuwatendea mabaya, ili waweze kuendelea kusaidiana vizuri, katika maisha yao.

“Watu ambao tunawatendea mabaya ni watu (wale) ambao tunaokaa pamoja nao. Kwa mfano: Kuzini na bibi wa jirani, kumwibia rafiki, na kadhalika.

Tena hii ni mifano kwa uhusinano wetu na Yesu Kristo anayetupokea kwa ukarimu na kujitoa kwetu kabisa kama rafiki. Ijapokuwa ametupenda, kwa matendo yetu mabaya, huwa tunamkataa na kumdharau.

Tena katika sakramenti ya Ekaristi huwa tunashindwa kumheshimu kwa sababu tunakula mwili wake na kunywa damu yake bila kustahili.” Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 71.

Zaburi 55:12-14. “Kama aliyenitukana ni adui yangu ningevumilia, kama mtu mwovu angejiinua dhidi yangu, ningejificha asinione. Kumbe ni wewe, mwenzangu, mshiriki na rafiki yangu wa karibu, ambaye wakati fulani tulifurahia ushirika mzuri tulipokuwa tukienda katikati ya umati hekaluni mwa Mungu.”

Mathayo 26:49-50. “Mara akamjia Yesu na kumsalimu, “Salaam, Rabi!’’ Akambusu. Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya kile ulichokuja kufanya hapa.”

Yohane 13:21, 25-26. “Baada ya kusema haya, Yesu alifadhaika sana moyoni, akasema, ‘‘Amin, amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.’’ Yule mwanafunzi akiwa amemwegemea Yesu akamwuliza, ‘‘Bwana tuambie ni nani?’’   Yesu akajibu, ‘‘Ni yule nitakayempa hiki kipande cha mkate baada ya kukichovya kwenye bakuli.’’ Hivyo baada ya kukichovya kile kipande cha mkate, akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskariote.”

1Wakorintho 11:27. “Kwa hiyo, mtu ye yote alaye mkate huo au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa na hatia ya dhambi juu ya mwili na damu ya Bwana.”

drinking water

water-fetchers.1

water-fetchers

 

ENGLISH: YOU DEFACATE WHERE YOU FETCH WATER FROM.

Once upon a time ago, there was a man who was travelling to a certain place. This man reached a point when he was feeling thirsty. To quinch his thirsty, he went to a waterlogged place and dag a small hole where he can get water to drink. When he drank water to his satisfaction, he never thought of wanting water again. He defecated in the water and left. This is where the saying ‘you defacate where you fetch water from’ came from.

This saying can be compared to a person who is well received by his/her host but, instead of appreciating him/her for the kindness, he/she turns around abusing him/her. The abuse can be like committing adultery with the wife/husband of the host, stealing some of the host’s properties, etc. (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 70). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

This saying teaches people to be thankful to people who do good to them. People should stop doing evils in order to have good life and good relationship with others.

The people we are abusing are the people we are living with. For example, committing adultery with a neighbor’s wife, robbing a friend, and so on.

Again these are examples of our association with Jesus Christ, who graciously accepts us and gives Himself completely as a friend. Although He loves us, by our evil deeds, we often reject and despise Him.

And in the sacrament of the Eucharist we often fail to honor Him because we eat His flesh and drink His blood unworthily (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 71).

Psalm 55: 12-14. Matthew 26: 49-50. John 13:21, 25-26. 1 Corinthians 11:27.

697. AHO UKALILAGA HAHO UKANYELAGA.

Aho kale olihoyi munhu uyo oliogaiwa jiliwa ahikanza lya nzala. Umunhu ng’wunuyo, ojaga agucholaga jiliwa uko usimizilaga. Lushigu lumo agajipandika ijiliwa ulya mpaga wiguta. Oho omala ugulya, aganyela haho olilaga ijiliwa jilinijo, adizukaga igiki alashoka hoyi alye hangi.  Hunagwene abhanhu bhagandya guyung’wila giki, ‘aho ukalilag haho ukanyelaga.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo okaribhushiyagwa chiza ha kaya ya ng’wa munhu. Ubhegejiyawa chiza guti ndugu ohakaya yiniyo, bhuyulya kihamo na gwendelea.

Aha ngelelo yaho, umunhu ng’wunuyo, ushiya nu mayu uoha kaya yiniyo, nulu, wibha ginhu hoyi, nulu wita jito jose jose ijo jidijawiza.’ Ugubhilitia ya bhubhi abhanhu bhenabho, yikolile na gunyela oholilaga, umunhu ng’wunuyo. Hunagwene abhanhu bhang’wilaga giki, ‘aho ukalilag haho ukanyelaga.’ Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 70.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na bhulumbi ukubhanhu abho bhalibhitila ya wiza, bho kuleka ugubhitila iyabhubhi, kugiki bhadule gwendelea gwiyambilija chiza, umuwikaj bhobho.

“Abhanhu abho dugabhitililaga yabhubhi bhali bhanhu abho dugikalaga kihamo nabho. Dugemele: ugushiya nu nkima o nzenganwa, gung’wibhila nwani, na gwendelea.

Hangi iyiniyo yili jigemelo ukubhumani wise nu Yesu Kristo uyo agadubokelaga kuwizang’holo na gwifunya gete kubhise guti nwani. Ningiki odutogwa, bho miito gise mabhi duganhemaga na gundalaha.

Hangi umusakramenti ya Ekaristia tugadumaga ugunkuja kunguno dugalyaga mili gokwe na gung’wa mininga gakwe bho nduhu ugwigelelwa. Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 71.

Zaburi 55:12-14.

Mathayo 26:49-50.

Yohone 13:21, 25-26.

1Wakorintho 11:27.

KISWAHILI: UNAPOKULA PAPO HAPO UNAPOKWENDA HAJA.

Hapo zamani alikuwepo mtu aliyekosa chakula wakati wa njaa. Mtu huyo, alienda kutafuta chakula kule alipotembelea. Siku moja alipata chakula, akala mpaka agatosheka. Alipomaliza kula, alijisaidia papo hapo alipolia chakula. Ndiyo maana watu wakaanza kumwambia, kwamba, ’unapokula papo hapo unakokwenda haja.’

 Methali hiyo hulinganisha kwa mtu yule ambaye amekaribishwa vizuri kwenye nyumba ya mtu. Akatendewa vizuri kama mmoja wa jamaa, wakila pamoja na kadhalika.

Mwishowe mtu huyo, huzini na mama wa kaya hiyo, au huiba au hutenda kitendo chote chote, ambacho si kizuri. Kuwafanyia ubaya watu hao, hufanana na kunyea pale alipolia chakula mtu huyo. Ndiyo maana watu humwambia mtu huyo, kwamba ‘unapokula papo hapo unapokwenda haja. Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 70.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na shukrani kwa watu wanaowatendea mema kwa kuacha kuwatendea mabaya, ili waweze kuendelea kusaidiana vizuri, katika maisha yao.

“Watu ambao tunawatendea mabaya ni watu (wale) ambao tunaokaa pamoja nao. Kwa mfano: Kuzini na bibi wa jirani, kumwibia rafiki, na kadhalika.

Tena hii ni mifano kwa uhusinano wetu na Yesu Kristo anayetupokea kwa ukarimu na kujitoa kwetu kabisa kama rafiki. Ijapokuwa ametupenda, kwa matendo yetu mabaya, huwa tunamkataa na kumdharau.

Tena katika sakramenti ya Ekaristi huwa tunashindwa kumheshimu kwa sababu tunakula mwili wake na kunywa damu yake bila kustahili.” Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 71.

Zaburi 55:12-14. “Kama aliyenitukana ni adui yangu ningevumilia, kama mtu mwovu angejiinua dhidi yangu, ningejificha asinione. Kumbe ni wewe, mwenzangu, mshiriki na rafiki yangu wa karibu, ambaye wakati fulani tulifurahia ushirika mzuri tulipokuwa tukienda katikati ya umati hekaluni mwa Mungu.”

Mathayo 26:49-50. “Mara akamjia Yesu na kumsalimu, “Salaam, Rabi!’’ Akambusu. Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya kile ulichokuja kufanya hapa.”

Yohane 13:21, 25-26. “Baada ya kusema haya, Yesu alifadhaika sana moyoni, akasema, ‘‘Amin, amin, nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.’’ Yule mwanafunzi akiwa amemwegemea Yesu akamwuliza, ‘‘Bwana tuambie ni nani?’’   Yesu akajibu, ‘‘Ni yule nitakayempa hiki kipande cha mkate baada ya kukichovya kwenye bakuli.’’ Hivyo baada ya kukichovya kile kipande cha mkate, akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskariote.”

1Wakorintho 11:27. “Kwa hiyo, mtu ye yote alaye mkate huo au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa na hatia ya dhambi juu ya mwili na damu ya Bwana.”

table food

tradition-

tradition1

ENGLISH: YOU DEFACATE WHERE YOU ATE FOOD FROM.

Once upon a time ago, there was a person who had no food during famine. One day this person travelled in search for food. He reached somewhere where he got food, ate it to his satisfaction. When he had satisfied with the food he defacate on that place. This is why people say ‘you defacate where you ate food from.’

 This saying can be compared to a person who is most welcomed in someone’s house. Such a person was well treated. Finally, instead of appreciating for the kindness, turns around the host by embarrassing him/her. This embarrassment can be stealing from his/her host or anything that disturbs their relationship (Refer to Kueneza Injili kwa Methali’ which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 70). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

This saying teaches people to be thankful to people who do good for them. They don’t have to return embarrassment for good things they have done to them.

The people we are abusing are the people we are living with. For example, committing adultery with a neighbor’s wife, robbing a friend, and so on.

Again these are examples of our association with Jesus Christ, who graciously accepts us and gives Himself completely as a friend. Although He loves us, by our evil deeds, we often reject and despise him.

And in the sacrament of the Eucharist we often fail to honor Him because we eat His flesh and drink His blood unworthily (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 71).

Psalm 55: 12-14. Matthew 26: 49-50. John 13:21, 25-26. 1 Corinthians 11:27.