Imbuki ya kahayile kenako yingilile kubhugemelwa bho ng’wa munhu guching’wa ichimu. Ilichimu linilo jiliginhu jugi ijo jidulile gunhemaja munhu. Kuyiniyo lulu, ulu munhu unkanga ng’wiye bho gungemela gunchima ichimu, uyo aligemelwa, adulile gugwa guti giki ochimagwa nili lichimu liniyo.
Gashinaga lulu, ulu munhu ungemela ng’wiye ichimu idi giki onchimaga, onkanga duhu kugiki, ogohe. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘gugemelwa ichimu idi guching’wa.’
Akahayike kenako kagalenganijiyagwa kubhanhu abho bhalib’ob’a bha gutumama milimo iyo ilimidimu, aliyo lulu imilimo yiniyo idulile gubhinja bhanhu mumakoye. Abhanhu bhenabho bhagawilagwa giki, imilimo yiniyo idadulile gubhabhulaga, kunguno, ugugemelwa ichimu idi kung’wa.
Akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya kuleka bhob’a bho uguitumama imilimo iyo ilimidumu, kunguno imilimo yiniyo idulile gub’inja bhichab’o mumakoye. Yigelelilwe abhanhu bhongeje bhukamu bho guitumama na bhuyegi imilimo yiniyo kugiki, bhadule gujib’eja chiza ikaya jabho.
Yohane 18:10-11.
1 Wakorintho 10:13.
KISWAHILI: KUJARIBIWA MKUKI SIO KUCHOMWA
Chanzo cha msemo huo chatokea kwenye tukio la mtu kujaribiwa kuchomwa mkuki. Mkuki ni kitu chenye ncha kali kiwezacho kumdhuru mtu. Kwa hiyo mtu akimtishia mwenzake kwa kumchoma mkuki, aliyetishiwa aweza hata kudondoka akidhani kwamba, amechomwa mkuki.
Kumbe basi, mtu akimjaribia mwenzake kumchoma mkuki huo, sio kwamba, amemchoma, bali amemtishia tu ili agope. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘kujaribiwa mkuki sio kuchomwa.’
Msemo huo hulinganishwa kwa watu ambao wana uoga wa kuzifanya kazi zile zilizongumu, lakini kazi hizo, zaweza kuwaokoa wenzao kutoka kwenye matatizo. Watu hao huambiwa kwamba, kazi hizo haziwezi kuwaua, kwa sababu ‘kujaribiwa mkuki sio kuchomwa.’
Msemo huo hufundisha watu juu ya kuacha uoga wa kuzifanya kazi zilizongumu, kwa sababu kazi hizo zaweza kuwaokoa wenzao kutoka kwenye matatizo. Hivyo, yafaa watu hao waongeze bidii ya kufanya kazi hizo, kwa furaha ili waweze kuziendeleza vizuri familia zao.
Yohane 18:10-11.
1Wakorintho 10:13.
ENGLISH: BEING TESTED BY SPEAR DOESN’T MEAN YOU HAVE BEEN PIERCED.
The source of the above saying comes from an incident of someone trying to brandish a spear. The spear is a sharp knot that can hurt a person. So, if a person threatens a fellow by stabbing him/her with a spear, the threatened person may even fall, thinking that he/she is being stabbed.
A person can pretend to be piercing someone but that doesn’t make this another person to be pierced. Rather, threatening him/her. This is why people say, ‘being tested by spear doesn’t mean that you have been pierced.’
The saying can be comparable to people who are afraid to do hard works, without knowing that those tasks can save others from trouble. These people are told that, those jobs can’t kill them, because ‘being tested by spear does’t mean that you have been pierced.’
The saying teaches people to break the fear of doing hard work because those tasks can save others from trouble. Therefore, it is important for these individuals to increase their efforts in such activities in order to create a better ground for future success in life.
John 18: 10-11.
1 Corinthians 10:13.
Msemo huu Ni muhimu katika maisha yetu ya kila siku, Kwani unatuimarisha na kutupa nguvu. Magumu tunayokutana nayo katika mahangaiko yetu kamwe yasitufanye tukakata tamaa, yanakuja ili kutuimarisha.
LikeLike