Imbuki ya kahayile kenaka ilolile nyama na nkila go ntugo uyo munhu ob’ilisaga kuli munhu nebhe. Ing’ombe iyo munhu ob’ilisilagwa ulu yucha, inyama yayo agalyaga umilisilwa, ilikunza nu nkila agachalilagwa ung’winikili mitugo. Hunagwene umilisi ng’wunuyo agabhab’awilaga abhanhu abho aliob’ab’ilisila giki, ‘mulalye inyama alunkila muladenhele.’
Akahayile kenaka kagalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagikalaga na bhutungilija bho gwilang’hanija sabho. Abhanhu bhenabho bhagajigolaga chiza isabho ja bhanhu abho bhabhab’ilisila. Hunagwene abhenikili ng’ombe jinijo bhagabhawilaga abhanhu bhenabho giki, ‘mulalye inyama alunkila muladenhele.’
Ulusumo lunulo lolanga bhanhu gubhiza bhatungilija umubhulang’hani bho jikolo ja bhanhu. Ubhutungilija bhunubho bhugubhambilija abhanhu bhenabho ugwikala bho mholele na bhichabho, umuwikaji bhobho.
(Mwanzo 42:16 – 17).
KISWAHILI: MKILA NYAMA MKIA MTATULETEA.
Chanzo cha methali hiyo chaangalia nyama na mkia wa mfugo ambao mtu aliukabidhi kwa mtu fulani, kwa ajili ya kuutunza. Ng’ombe aliyepewa mtu kumtunza akifa, nyama yake huliwa na mtunzaji wa ng’ombe huyo. Mkia wake pamoja na ngozi yake hupelekwa kwa mwenye ng’ombe kama ushahidi wa kufa kwa ng’ombe huyo. Ndiyo maana mwenye mali au mmiliki wa ng’ombe humwambia yule aliyempatia ng’ombe ili awatunze kwamba, ‘mkila nyama mkia mtatuletea.’
Methali hiyo hulinganishwa kwa watu walio waaminifu katika utunzaji wa mali za watu wengine. Watu hao huitunza vizuri mali hiyo ya watu waliowakabidhi. Ndiyo maana wale waliowapatia mali hiyo huwaambia watu hao kwamba, ‘mkila nyama mkia mtatuletea.’
Methali hiyo hufundisha watu kuwa waaminifu katika utunzaji wa mali za watu wengine. Uaminifu huo utawasaidia watu hao katika kuishi kwa amani na wenzao maishani mwao.
(Mwanzo 42:16 – 17).
ENGLISH: WHEN YOU EAT THE MEAT BRING US THE TAIL.
The origin of saying is meat and tail of a domesticated animal such as a cow that someone hands over to someone for the purpose of allowing the other person keep it. When such animal dies, its meat is eaten by the keeper, but the skin and the tail are taken to the owner of the livestock as proof of its death. That is why the owner of the herd tells the keeper that, ‘when you eat the meat, bring us the tail.’
The saying is used comparatively to commend people who are honest in other people’s property management. These people take good care of the property entrusted to them. That is why, when a cow dies, the owner tells those people that, ‘when you eat the meat bring us the tail.’’
The proverb teaches people to be honest in the management of other people’s property. That trust will help those people to live peacefully with their fellows.
(Genesis 42:16 – 17).