Justina

1529. SUKUMA: UYO ADIZUKAGA UKO OFUMILA, AGAJIMILAGA UKO AJILE.

Ulusumo lunulo lulolile likujo lya kihalile ka jiafrika. Abhanhu bhalangagwa gwizuka imbuki ya kaya jabho, kikalile, ni nhungwa ijawiza. Abhatale bhalibhamana igiki umunhu uyo agibhaga imbuki ya mizwi yakwe agajimilaga wangu umuwikaji bhokwe. Hunagwene bhagang’wilaga giki “uyo adizukaga uko ofumila, agajimilaga uko ajile.”

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agalekaga imbuki ya kikalile ka bhatale bhakwe nu bhulangwa ubho bhonkuja, umuwikaji bhokwe. Umunhu ng’wunuyo, alinanhinda ja gubhulema ubhushauli bho gwita mihayo ya sagala kunguno ya gubhudalahija ubhulangwa bho bhatale bhakwe umuwikaji bhokwe bhunubho. Uweyi agadumaga uguimala imilimo ya ha kaya yakwe kunguno ya guleka gubhudilila chiza ubhulangwa bho bhatale bhakwe, umukikalile kakwe kenako.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo agayibhaga imizwi ya bhatale bhakwe mpaka ojimila, kunguno nuweyi agabhudalahijaga ubhulangwa bho bhatale bhakwe mpaka oduma uguyimala chiza imilimo yakwe yiniyo, aha kaya yakwe, umuwikaji bhokwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “uyo adizukaga uko ofumila, agajimilaga uko ajile.”

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya: gwizuka isumo yabho, bho gubhakuja abhabyaji bhabho, kugiki bhadule gujilela chiza ikaya jabho, umuwikaji bhobho bhunubho.

Kumbukumbu la Torati 8:2.

Mithali 22:28.

Luka 15:17-18.

Zaburi 78:4.

Yeremia 6:16.

SWAHILI: ASIYEKUMBUKA ALIPOTOKA, HUPOTEA AENDAKO.

Methali hii inatokana na hekima ya kitamaduni ya Kiafrika. Katika jamii nyingi za Kiafrika, watu walifundishwa kukumbuka historia ya familia zao, utamaduni, mila, na maadili. Wazee waliamini kwamba mtu anayesahau mizizi yake hupoteza mwelekeo maishani kwa urahisi. Methali hiyo ilitumika sana kuwakumbusha vijana kuheshimu historia yao, wazazi, mila, na imani. Ndiyo maana wazee walimwambia yule anayesahau mizizi yake kwamba, “asiyekumbuka alipotoka, hupotea aendako.”

Methali hii hulinganishwa kwa mtu yule anayeacha mila zake kwa kupuuza ushauri mzuri kutoka kwa wazee ulioyaunda maisha yake. Mtu kama huyo huwa na kiburi kimpelekeacho kuwa na hali kuchanganyikiwa, au kufanya maamuzi mabaya kwa sababu hakumbuki tena msingi wa maisha yake. Yeye hushindwa kutimiza malengo yake katika familia yake kwa sababu ya kupuuza ushauri mzuri kutoka kwa wazee wake katika maisha yake.

Mtu huyu hufanana na yule mtu aliyesahau mizizi yake akapokea, kama msafiri anayetembea msituni bila kujua njia aliyotumia kuingia. Kwa kuwa amesahau njia aliyotoka, anapotea na hawezi kupata mwelekeo sahihi kwa urahisi. Ndiyo maana watu humuonya kwa kusema kwamba, “asiyekumbuka alipotoka, hupotea aendako.”

Methali hii huwafundisha watu kuhusu: kukumbuka asili na historia yao, kwa kuwaheshimu wazazi, wazee, na mila, kujifunza kutokana na uzoefu wa zamani, kubaki wanyenyekevu hata baada ya mafanikio, na kudumisha imani na maadili popote wanapokwenda, ili waweze kufanikiwa katika kuwalea wanafamilia wao, katika maisha yao.

Methali huwafundisha watu kwamba, mtu anayekumbuka asili yake atakuwa na hekima, mwongozo, na utulivu maishani.

Kumbukumbu la Torati 8:2. “Kumbuka jinsi Bwana, Mungu wako, alivyokuongoza njia yote jangwani miaka hii arobaini.” Mstari huu unawafundisha watu kutosahau mahali ambapo Mungu amewaleta kutoka.

Mithali 22:28. “Usiondoe mawe ya mpaka wa zamani yaliyowekwa na mababu zako.” Hii inawakumbusha watu kuheshimu misingi na mila zilizorithiwa na mababu zao.

Luka 15:17-18. Mwana mpotevu alikumbuka nyumba ya baba yake baada ya kupotea katika maisha ya dhambi. Kukumbuka nyumba yake kulimsaidia kurudi kwenye njia sahihi.

Zaburi 78:4. “Tutawaambia kizazi kijacho matendo ya sifa ya Bwana.” Mstari huu unawahimiza watu kukumbuka na kuhifadhi historia na imani yao.

Yeremia 6:16. “Simama kwenye makutano ya barabara mkaone; uliza njia za kale, uliza njia iliyo njema iko wapi, na uifuate.” Hii inawafundisha watu kufuata njia nzuri na hekima ya zamani.

ENGLISH: HE WHO DOES NOT REMEMBER WHERE HE COMES FROM, HE GETS LOST WHERE HE GOES.

This proverb originates from traditional African wisdom. In many African communities, people were taught to remember their family background, culture, traditions, and values. Elders believed that a person who forgets his roots easily loses direction in life. The proverb was commonly used to remind young people to respect their history, parents, customs, and faith. That is why the elders told the one who forgets his roots “he who does not remember where he comes from, he gets lost where he goes.”

This proverb is compared to a person who abandons his traditions, ignores good advice from elders, and forgets the struggles that shaped his life. Such a person may become proud, confused, or make wrong decisions because he no longer remembers the foundation of his life. He fails to actualize his goals at his family because of ignoring good advice from elders in his life.

This person resembles the traveler who walks into a forest without knowing the path he used to enter. Since he has forgotten the way he came from, he becomes lost and cannot easily find the right direction. That is why people warm him saying “he who does not remember where he comes from, he gets lost where he goes.”

This proverb teaches people about: remembering their roots and background, by respecting parents, elders, and traditions, learning from past experiences, staying humble even after success, and keeping faith and moral values wherever the go, so that they be successfully in nurturing their family members, in their lives.

The proverb teaches that a person who remembers his origin will have wisdom, direction, and stability in life.

Deuteronomy 8:2. “Remember how the Lord your God led you all the way in the wilderness these forty years.” This verse teaches people not to forget where God has brought them from.

Proverbs 22:28. “Do not move the ancient boundary stones set up by your ancestors.” This reminds people to respect the foundations and traditions handed down by their forefathers.

Luke 15:17-18. The prodigal son remembered his father’s house after getting lost in sinful living. Remembering his home helped him return to the right path.

Psalm 78:4. “We will tell the next generation the praiseworthy deeds of the Lord.” This verse encourages people to remember and preserve their history and faith.

Jeremiah 6:16. “Stand at the crossroads and look; ask for the ancient paths, ask where the good way is, and walk in it.” This teaches people to follow the good paths and wisdom from the past.

1528. SUKUMA: NZILAMAKA IGANJIMIJAGA UNSIMINZI.

Ulusumo lunulo lufumilile kulikujo lya kale ilya Africa. Ikale abhasiminzi wasiminzaga bho magulu bhalibhitila mumapolu, mabhonde na mumachalo bho mduhu ramani. Abhanhu bhenabho bhashikaga aha nzilamaka bhajimija ijilunga. Hunagwene bhagayomba giki, “njilamaka iganjimijaga unsiminzi.”

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agabhonaga wiza wingi oduma uguchagula nulu jimo umuwikaji bhokwe bhunubho. Umunhu ng’wunuyo, agadumaga uguchagula josejose ulu ubhonaga majikolo mingi agawiza kunguno ya gugawila bhumani wikujo lya kikalile kiza umuwikaji bhokwe bhunubho. Uweyi agajimijaga ijilunga ja guitongela chiza ikaya yakwe kunguno ya gugaiwa bhulangwa bho guchagula chiza, umuwikaji bhokwe bhunubho.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nabhasiminzi bha mumapoli abho bhagajimija ijilunga, kunguno nuweyi agajimijaga amasala ga guchagula chiza mpaga oduma uguitongela chiza ikaya yakwe ulu obhonaga majikolo mingi agawiza, umuwikaji bhokwe bhunubho. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki “njizamaka iganjimijaga unsiminzi.”

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na witegeleja bho guchagula gwikala chiza ulubhabhonaga majikolo mingi agawiza, kugiki bhadule kupandika matwajo mingi umukaya yabho jinijo, umuwikaji bhobho bhunubho.

Mithali 3:5–6.

Mathayo 7:13–14.

Yakobo 1:5.

1Wakorintho 14:33.

SWAHILI: NJIA PANDA HUMCHANGANYA MSAFIRI.

Methali hii inatokana na hekima ya jadi ya Kiafrika na pia inaakisiwa katika tamaduni nyingi kote ulimwenguni. Zamani, wasafiri walisafiri kwa miguu kupitia misitu, mabonde, na vijiji bila ramani. Walipofika kwenye barabara nyingi zinazovuka yaani njia panda, waliweza kuchanganyikiwa kwa urahisi na kupoteza mwelekeo. Kwa hivyo methali hiyo iliundwa ili kuwafundisha watu umuhimu wa hekima, mwongozo, na kufanya maamuzi yaliyo wazi maishani mwao. Ndiyo maana walisema kwamba, “njia panda humchanganya msafiri.”

Methali hii hulinganishwa kwa mtu yule hukabiliwa na chaguzi nyingi maishani na hajui ni njia gani ya kufuata maishani mwake. Mtu kama huyo huweza kuchanganyikiwa kwa sababu ya maoni mengi, vishawishi, au fursa nyingi maishani. Yeye hupoteza mwelekeo wa kuongoza familia yake vizuri kwa sababu ya kukosa hekima, mwongozo, na uwezo wa kufanya maamuzi mazuri maishani mwake.

Mtu huyu hufanana na wale watu waliokosa mwongozo na hekima sahihi hadi kufikia hatua ya kupoteza mwelekeo wao kwa sababu naye pia hufuata maelekezo mengi kwa wakati mmoja na hatimaye hupoteza umakini katika kuongoza familia yake hiyo maishani mwake. Kama vile msafiri anavyoweza kupotea kwenye njia panda, mtu asiye na kusudi wazi anaweza kupotea kiroho, kimaadili, au kijamii maishani mwake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “njia panda humchanganya msafiri.”

Methali hii huwafundisha watu kuhusu: umuhimu wa hekima katika kufanya maamuzi, kutafuta mwongozo kabla ya kuchagua njia, kubaki makini maishani, kuepuka mkanganyiko unaosababishwa na mawazo mengi yanayokinzana, na kuamini uongozi na mwelekeo mzuri. Inawakumbusha watu kwamba maisha yana njia nyingi, na chaguo baya zaweza kusababisha matatizo huku chaguo za busara zikiongoza kwenye mafanikio na amani maishani mwao.

Mithali 3:5–6. “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe; katika njia zako zote mtii, naye atanyosha mapito yako.” Mstari huu unafundisha kwamba Mungu hutoa mwongozo wakati barabara za maisha zinaonekana kuchanganyikiwa.

Mathayo 7:13–14. “Ingieni kwa kupitia mlango mwembamba… mlango ni mdogo, na njia nyembamba iendayo uzimani.” Yesu anafundisha kwamba kuna njia nyingi maishani, lakini njia sahihi tu ndiyo inayoongoza kwenye uzima wa milele.

Yakobo 1:5. “Lakini mtu yeyote kati yenu akipungukiwa na hekima, na amwombe Mungu, awapaye wote kwa ukarimu.” Watu wanapokabiliwa na maamuzi yanayochanganya, wanapaswa kutafuta hekima kutoka kwa Mungu.

1Wakorintho 14:33. “Maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani.” Mungu anatamani watu wake watembee katika uwazi, amani, na mwelekeo sahihi badala ya mkanganyiko.

Methali “njia panda humchanganya msafiri” hufundisha kwamba maisha yamejaa chaguzi na njia panda. Bila hekima, mwongozo, na imani katika Mungu, mtu anaweza kupoteza mwelekeo kwa urahisi. Watu wenye busara hutafuta ushauri, huomba uelewa, na kwa uangalifu.

ENGLISH: “INTERSECTION OF ROADS CONFUSES THE TRAVELER.”

This proverb comes from traditional African wisdom and is also reflected in many cultures around the world. In ancient times, travelers journeyed on foot through forests, valleys, and villages without maps. When they reached many crossing roads, they could easily become confused and lose direction. The proverb was therefore created to teach people the importance of wisdom, guidance, and clear decision-making in life. That is why they said, “Intersection of roads confuses the traveler.”

This proverb is compared to a person who faces many choices in life and does not know which path to follow in life. Such a person may become confused because of too many opinions, temptations, or opportunities. He loses direction of leading well his family because of lacking wisdom, guidance, and clear decision-making in life.

This person resembles those people who lacked proper guidance and wisdom to the point of losing their directions because he also follows many directions at the same time and finally loses focus in leading his family in life.

Just as a traveler can become lost at roads intersection, a person without clear purpose can become lost spiritually, morally, or socially. That is why people tell him that, “Intersection of roads confuses the traveler.”

This proverb teaches people about: the importance of wisdom in making decisions, seeking guidance before choosing a path, remaining focused in life, avoiding confusion caused by many conflicting ideas, and trusting good leadership and direction. It reminds people that life has many crossroads, and wrong choices can lead to trouble while wise choices lead to success and peace.

Proverbs 3:5–6. “Trust in the Lord with all your heart and lean not on your own understanding; in all your ways submit to Him, and He will make your paths straight.” This verse teaches that God gives direction when life’s roads seem confusing.

Matthew 7:13–14. “Enter through the narrow gate… small is the gate and narrow the road that leads to life.” Jesus teaches that there are many paths in life, but only the right path leads to eternal life.

James 1:5. “If any of you lacks wisdom, you should ask God, who gives generously to all.” When people face confusing decisions, they should seek wisdom from God.

1Corinthians 14:33.“For God is not a God of confusion but of peace.” God desires His people to walk in clarity, peace, and right direction rather than confusion.

The proverb “intersections of roads confuse the traveler” teaches that life is full of choices and crossroads. Without wisdom, guidance, and faith in God, a person can easily lose direction. Wise people seek counsel, pray for understanding, and carefully.

850. NZUB’I ADAB’ITILAGA ILAMBO.

Ulusumo lunulo, lulilola nzub’i o shi, nulu ndilo uyo agaja ogazub’a bhuli hilambo lyene mpaga abhite hoyi, gujilola ishi. Unzub’i ng’wunuyo, agitaga giko kunguno ahayile apandike ndilo nyingi. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “nzub’i adab’itilaga ilambo.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agasulujaga jikolo jilebhe, uyo agab’itaga bhuli kaya yene, umubhusuluja bhokwe. Unsuluja ng’wunuyo, agajaga uliga bhuli aha kaya yene iyo aliyibhona ilugulile unyango, kunguno atogilwe amale gujijinja pye ijikolo ijo alijisuluja, umunimo gokwe gunuyo. Uweyi agapandikaga solobho mhale noyi umubhusuluja bhokwe bhunubho kunguno ya wikomeja bhokwe ubho gubhita bhuli kaya, umutumami bho milimo yakwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nu nzub’i o ndilo uyo agabhitaga bhuli ilambo, kunguno nu weyi agajaga ubhita bhuli kaya, umubhusuluja bhokwe bhunubho. Uweyi abhalangaga abhanhu bhakwe inzila ja guhoya na bhanhu bhingi umubhutumami bhobho, kugiki bhadule gupandika sabho ningi, umumilimo yabho. Hunagwene agabhawilaga abhanhu giki, “nzub’i adab’itilaga ilambo.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gwigulambija gubhutumila pye uwasa ubho bhali nabho umubhutumami bho milimo yabho, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi, umuwikaji bhobho.

Luka 24:47.

Matendo ya mitume 1:8.

Warumi 10:18.

Marko 16:15-16.

KISWAHILI: MVUVI HAACHI KUPITIA BWAWANI.

Methali hiyo, humwangalia mvuvi wa samaki ambaye hupitia kwenye kila bwawa akitafuta samaki. Mvuvi huyo, hufanya hivyo kwa sababu anataka kupata mafanikio ya kuvua samaki wengi. Ndiyo maana watu husema kwamba, “mvuvi haachi kupitia bwawani.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huuza vitu fulani, kwa hupitia kwenye kila familia, katika uuzaji wa biashana yake. Mfanya biashana huyo, huenda akiingia kwenye kila familia ambayo anauona mlango wake uko wazi, kwa sababu anapenda kuuza vitu vyake vyote, katika biashara yake hiyo. Yeye hupata faida kubwa sana katika kazi yake hiyo, kwa sababu ya bidii yake ya kupitia kwenye kila familia, katika utekelezaji wa majukumu yake.

Mtu huyo, hufanana na yule mvuvi wa samaki aliyepitia kwenye kila bwawa, kwa sababu naye huenda akiingia kwenye kila familia, katika biashara yake hiyo. Yeye huwafundisha pia watu wake namna ya kuongea na watu wengi katika utekelezaji wa majukumu yao, ili waweze kupata mafanikio mengi, katika kazi zao. Ndiyo maana huwa anawaambia watu kwamba, “mvuvi haachi kupitia bwawani.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kujibidisha kuzitumia fursa zote walizo nazo, katika utekelezaji wa majukumu yao, ili waweze kupata mafanikio mengi, maishani mwao.

Luka 24:47.

Matendo ya mitume 1:8.

Warumi 10:18.

Marko 16:15-16.

fisherman-1

people-with fish

visser-fishing zanzibar

fishpond-

ENGLISH: THE FISHER-PERSON DOES NOT JUMP A FISHPOND (TRADITIONS ARE LIKE A  LAW).

This proverb focuses on a fisherman who goes through each pond in searching for fish. He does this because he wants to be successful in catching more fish. That is why people say that, “the fisher-person does not jump a fishpond.”

This proverb is compared to the man who sells certain things by passing through every family in his trade. Such trader enters at every family which he sees that its door is open, because he likes to sell all his goods. He gets a lot of benefits from his work, because of his persistence of passing through each family that can buy his goods.

This man is like the fisherman who passed through every pond, because he too goes into every family that can buy his goods. He also teaches his people on how to communicate with many people in fulfilling their duties, so that they may be more successful in their daily activities. That is why he often tells people that, “the fisher-person does not jump a fishpond (traditions are like a law).”

This proverb teaches people on how to strive to use all the opportunities which they have in fulfilling their daily responsibilities, so that they may have more successes in their families.

Luke 24:47.

Acts 1: 8.

Romans 10:18.

Mark 16: 15-16.

849. LWAKA LO NKE O MHIMBI GUBHISA SISA MU NGOBHO.

Imbuki ya lusumo lunulo, ingilile kuli munhu uyo oli na lwaka lo gulya jiliwa, umukikalile kakwe. Olihoyi nkima uyo oli nke o mhimbi. Unkima ng’wunuyo, aginhwa sisa uing’wa mpaka wiguta iyingi uyibhisa mu ng’wenda gokwe.

Aliyo lulu, iki isisa jili ndoto ung’wenda gokwe gugalob’a minzi mpaka umanyika igiki wayib’isaga mu ng’wenda gokwe. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “lwaka lo nke o mhimbi gubhisa sisa mu ngobho.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo alina lwaka lo bhulaku bho gulya majiliwa, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agikalaga na bhulaku bhutale ubho gulya jiliwa ukunhu adubhiganikaga abhiye, iki agimanaga ng’winikili duhu, kunguno ya bhukalu bhokwe bhunubho ubho nduhu ugubhizuka bhiye. Uweyi agikalaga ulya jiliwa mpaga wiguta na gulisaja bho nduhu ugubhadilila abhiye, aliyo bhalinanuka na nzala aha kaya yake henaho.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nu nke o  mhimbi uyo agabhisa sisa mu ng’wenda mpaga umanyika aho yagudotya ung’wenda gunuyo, kunguno nu weyi alinaku ogulya majiliwa bho nduhu ugubhadilila abhiye abho bhali na nzala, umukikalile kakwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “lwaka lo nke o mhimbi gubhisa sisa mu ngobho.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya guleka bhulaku bho gulya majiliwa ukunhu bhadubhadililaga abhichabho, kugiki bhadule gugabhana chiza ijiliwa ijo bhalijipandika, umuwikaji bhobho.

2 Samweli 12:4-6.

2Samweli 12:9-10.

Zaburi 55:11.

Zaburi 78:18.

KISWAHILI: TAMAA YA MKE WA PIMBI KUFICHA CHICHA KWENYE NGUO.

Chanzo cha methali hiyo, kilianzia kwa mtu yule ambaye alikuwa na tamaa ya ulafi wa kula chakula, katika maisha yake. Olikuwepo mwanzamke aliyekuwa mke wa Pinbi. Mwanamke huyo, alipewa chicha akanywa mpaka akashiba na kuificha kwenye nguo yake ile iliyobaki.

Lakini kwa vile chicha hiyo ni mbichi nguo yake ililowa maji mpaka akajulikana kwa watu kuwa alikuwa ameificha chicha hiyo kwenye nguo yake. Ndiyo maana watu walisema kwamba, “tamaa ya mke wa pimbi kuficha chicha kwenye nguo.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ana tamaa kubwa ya kula chakula, katika maisha yake. Mtu huyo, huwa ana ulafi wa kula chakula kwa kujifikiria yeye mwenyewe tu bila kuwajali wenzake, kwa sababu ya kutaka afaidike yeye peke yake.  Yeye huwa anakula chakula mpaka anasaza bila kuwajali wenzake wanaokosa chakula kwenye familia yake.

Mtu huyo, hufanana na mke wa Pimbi aliyeficha chicha kwenye nguo yake mpaka nguo hiyo ikalowana maji, kwa sababu naye ana ulafi wa kula chakula bila kuwajali wenzake walio na njaa, katika maisha yake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “tamaa ya mke wa pimbi kuficha chicha kwenye nguo.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuacha tamaa ya ulafi wa kula chakula bila kuwajali wenzao, ili waweze kugawana vizuri chakula wanachopata, maishani mwao.

2Samweli 12:4-6.

2Samweli 12:9-10.

Zaburi 55:11.

Zaburi 78:18.

black-girl

ethiopia-wine

hammer-

ENGLISH: PIMBI’S WIFE’S DESIRE TO HIDE DRINKS IN CLOTHES.

The origin of the proverb can be traced back from a woman who was greedy for eating food in life. There was a woman who was Pinbi’s wife. She was given a drink and drank until she was full and hid the remaining of it in her clothes.

But since such drink was raw her clothes became wet until it became known to the people of that area. That is why people said, “pimbi’s wife’s desire to hide drinks in clothes.”

This proverb is compared to a person who has a strong desire to eat, in life. Such person is obsessed with eating food without considering others because such desire for only benefiting him/herself. He/she often eats food to the point of stopping caring about his/her fellow food in the family.

This man is like the wife of Pimbi who hid drink in her clothes until the garment was wet, because he/she too is greedy enough to eat food without caring for others who are hungry in life. That is why people say to him/her that, “Pimbi’s wife’s desire to hide drinks in clothes.”

This proverb teaches people about giving up the greed of eating food without caring for others in the family, so that they can nicely share the food which they get in their lives.

2 Samuel 12: 4-6.

2 Samuel 12: 9-10.

Psalm 55:11.

Psalm 78:18.

hilippians 2: 8-9.

848. NDA IDI NA NZUNAYE.

Inda ya ng’wa munhu ili imo duhu iyo igabokelaga ijiliwa ijo agajilyaga umunhu ng’wunuyo. Iyoyi igabhizaga idina ng’wichayo, kunguno ili ing’wene duhu, umukikalile kayo. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “nda idi na nzunaye.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agikalaga wimanile weyi ng’winikili duhu, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agabhizaga atogilwe gwinhiwa jikono na bhiye, aliyo lulu uweyi adabhagunanaga abhanhu abho bhali na makoye, nulu agabhiza ali na jikolo ja gudula gubhambilija, kunguno ya bhulaku na wiming’holo bhokwe bhunubho, umuwikaji bhokwe. Uweyi agadumaga nulu ugwikala na bhanhu bhingi aha kaya yakwe, kunguno ya gogohaya kumajiwa jiliwa jakwe, umukikalile kakwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga ni nda iyo igimanaga yoyi duhu, kunguno nuweyi agiinikaga weyi duhu, bho nduhu ugubhambilija abhiye, umuwikaji bhokwe bhunubho. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “nda idi na nzunaye.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gutumama milimo yabho bho bhukamu bhutale kugiki bhadule gupandika sabho ja gubhambilija gubhiza bhizang’holo bha gubhalisha abho bhali na nzala, umuwikaji bhobho.

2Timotheo 2:11.

Ufunuo 14:13.

1Wakorintho 9:25.

Wafilipi 2:8-9.

KISWAHILI: TUMBO HALINA MDOGO WAKE.

Tumbo la mtu ni moja tu ambalo hupokea chakula anachokila mtu huyo. Lenyewe huwa halina mwenzake kwa sababu liko peke yake muda wote. Ndiyo maana watu husema kwamba, “tumbo halina mdogo wake.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hujijali yeye mwenyewe tu, katika maisha yake. Mtu huyo, huwa anapenda kupewa vitu na wenzake, lakini yeye huwa hawasaidii watu walioko kwenye matatizo, hata kama ana vitu vya kumwezesha kufanya hivyo, kwa sababu ya ulafi na uchoyo wake huo, maishani mwake. Yeye hushindwa hata kuishi wa watu wengi kwenye familia yake, kwa sababu ya kuogopa kummalizia chakula chake, katika maisha yake.

Mtu huyo, hufanana na tumbo lile ambalo hujijali lenyewe tu, kwa sababu naye hujifikiria yeye mwenyewe tu, kwa kutowasaidia wenzake mali zake, maishani mwake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “tumbo halina mdogo wake.”

Methail hiyo, hufundisha watu juu ya kuyatekeleza majukumu yao kwa bidii kubwa ili waweze kupata mali za kuwakarimu wenzao walio na njaa, maishani mwao.

2Timotheo 2:11.

Ufunuo 14:13.

1Wakorintho 9:25.

Wafilipi 2:8-9.

hunger-

african-child-1

food-1-

 ENGLISH: THE STOMACH HAS NO YOUNG RELATIVE.

A person’s stomach is the only one that receives the food that such person eats. It has no partner because it is alone all the time. There is no one who can eat for someone else. That is why people say that, “the stomach has no young relative.”

This proverb is compared to a man who cares only for himself in his life. He is the person who likes to be given things by others, but he does not help the people who suffer from various problems even if he has things for doing so. He does so because of his greed in his life. He fails even to live with other people in his family because of such greed.

This person is like the stomach that cares only for itself, because he is also a self-centered one who does not help others in his life. That is why people tell him that, “the stomach has no young relative.”

This proverb imparts in people an idea on how to carry out their responsibilities with great diligence so that they can acquire plenty wealth for generously helping the starving people in their lifetime.

2 Timothy 2:11.

Revelation 14:13.

1 Corinthians 9:25.