Fr. Zakaria Kashinje

1530. SUKUMA: UMOTO UYO GOBHACHA NZENGANWA GUDULILE GUBHACHA NUMBA YINGI.

Imbuki ya lusumo lunulo yinginile ku likujo lya bhikaji bha Afrika. Uloyi luhoyelile munhu uyo adadilile makoye ayo gayikenagulaga kaya yingi. Amakoye geneyo nose gagashiga na ha kaya yakwe kunguno ya guleka gugadilila aho galikubhangi. Hunagwene abhanhu bhaganhugula bho guyomba giki, “umoto uyo gobhacha nzenganwa gudulile gubhacha numba yingi.”

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo adadililaga makoye ga bhiye bho gwiganika giki, gadadulile ugunpandika uweyi, umuwikaji bhokwe bhunubho. Umunhu ng’wunuyo, agagabhonaga amakoye gabhiye olema ugwambilija josejose kunguno ya bhujidalonja bhokwe bhunubho, umukikalile kakwe. Aha ngelelo yabho, amakoye genayo gagashikaga nu kubhanhu bha ha kaya yakwe gayubhakoya mpaga oduma uguginja, kunguno ya bhujidalonja bhokwe bhunubho umuwikaji bhokwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo agaleka gugadilila makoye gabhiye mpaga nose kuyipandika ni ikaya yakwe, kunguno nuweyi agalemaga ugugadilila amakoye gabhiye mpaga nose gabhapandika na kubhakoya abhanhu bha ha kaya yakwe yiniyo, umuwikaji bhokwe bhunubho. Hunagwene abhanhu bhaganhugulaga bho guyomba giki, “umoto uyo gobhacha nzenganwa gudulile gubhacha numba yingi.”

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na witegeleja bho gudilila gwiyambilija gugamala wangu amakoye gabhichabho haho gatali ugukula, kugiki bhadule gwikala bho mholele umukaya jabho jinijo.

Wagalatia 6:2.

1Wakorintho 12:26.

Mithali 26:20.

Yakobo 3:5-6.

Mathayo 5:9.

SWAHILI: MOTO ULIOWASHA JIRANI HUWEZA KUWASHA NYUMBA NYINGINE.

Methali hiyo inatokana na hekima ya jadi za Kiafrika. Inazungumzia mtu aliyepuuza hatari, uovu, migogoro, au matatizo yaliyoathiri familia nyingine. Matatizo hayo yaliifikia pia familia yake kwa urahisi kwa sababu ya kuyapuuza. Kama vile moto unavyohama haraka kutoka nyumba moja hadi nyingine, matatizo katika jamii moja yanaweza kuathiri jamii nzima. Ndiyo maana watu walimwambia mtu huyo kwamba, “moto uliowasha nyumba ya jirani unaweza kuwasha nyumba nyingine.”

Methali hii hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hupuuza mateso, migogoro, au makosa yanayowapata wengine, akifikiri kwamba hayatamwathiri kamwe. Mtu huyo huona mgawanyiko, chuki, dhambi, ufisadi, au vurugu zikiongezeka karibu naye lakini hukataa kutenda lolote, kusaidia, kuomba, au kuwaonya wengine kwa sababu ya kutojali kwake. Mwishowe, shida hiyo hiyo iliwafikia wanafamilia wake kiasi cha kushindwa kuitatua katika maisha yake.

Mtu huyo hufanana na yule aliyepuuza matatizo ya wengine hadi kufikia hatua ya kuyaruhusu yawafikie watu wa familia yake, kwa sababu naye pia hupuuza mgawanyiko, mateso, na matatizo ambayo yanawaathiri wengine hadi baadaye, uharibifu huo huo huingia katika familia yake mwenyewe. Ndiyo maana watu humuonya kwa kusema kwamba, “moto uliowasha nyumba ya jirani unaweza kuwasha nyumba nyingine.”

Methali hiyo huwapa watu mawazo kuhusu: kujaliana katika jamii kwa kutatua matatizo kabla hayajaenea, kuwasaidia majirani wakati wa shida, kuelewa kwamba mateso ya mtu mmoja yanaweza kuathiri kila mtu.

Pia inawakumbusha watu kuhusu wajibu wao wa kukuza amani, umoja, na uwajibikaji miongoni mwao.

Wagalatia 6:2. “Chukulianeni mizigo, na kwa njia hii mtatimiza sheria ya Kristo.” Mstari huu unawafundisha Wakristo kusaidiana kwa sababu matatizo yanayomhusu mwamini mmoja yanaweza pia kuathiri jamii nzima.

1Wakorintho 12:26. “Kiungo kimoja kikiteseka, vyote huumia pamoja nacho.” Mtume Paulo anaelezea kwamba waumini ni kama mwili mmoja. Maumivu au shida katika sehemu moja huathiri pia mtu mwingine.

Mithali 26:20. “Pasipo kuni moto huzimika; bila umbea ugomvi hupungua.” Mstari huu unafundisha kwamba migogoro midogo inaweza kukua kama moto ikiwa watu wataendelea kueneza chuki na mgawanyiko.

Yakobo 3:5-6. “Ulimi pia ni moto…” Yakobo analinganisha maneno ya uharibifu na moto ambao unaweza kuharibu maisha ya watu wengi ikiwa hautadhibitiwa.

Mathayo 5:9. “Heri wapatanishi; maana hao wataitwa wana wa Mungu.” Yesu anawafundisha waumini kuacha migogoro na kuleta amani kabla uharibifu haujaenea zaidi.

ENGLISH: A FIRE THAT STARTED IN A NEIGHBOR’S HOUSE CAN SET FIRE TO ANOTHER HOUSE.

This proverb comes from traditional African wisdom. It talks about a person who ignored danger, evil, conflict, or problems which affected another family. Those problems easily reached his family because of ignoring them. Just as fire moves quickly from one house to another, trouble in one community can affect the whole society. That is why people told him, “a fire that started in a neighbor’s house can set fire to another house.”

This proverb is compared to a person who ignores suffering, conflict, or wrongdoing happening to others, thinking that it will never affect him.  This person sees division, hatred, sin, corruption, or violence growing around him but refuses to act, help, pray, or warn others because of his less concern. In the end, the same trouble reached his family members to point of failing to solve it in his life.

This person resembles that person who ignored problems of others to the point of letting them reach his family, because of he ignores division, suffering, and other problems which affect others until later, the same destruction enters his own family. That is why people warn his by saying, “a fire that started in a neighbor’s house can set fire to another house.”

This proverb imparts in people ideas about: caring for one another in communities by solving problems before they spread, helping neighbors during times of trouble, understanding that the suffering of one person can affect everyone.

It also reminds people about their duty of promoting peace, unity, and responsibility among people.

Galatians 6:2. “Carry each other’s burdens, and in this way you will fulfill the law of Christ.” This verse teaches Christians to help one another because problems affecting one believer can also affect the whole community.

1Corinthians 12:26. “If one member suffers, all suffer together with it.” The Apostle Paul explains that believers are like one body. Pain or trouble in one part affects everyone else.

Proverbs 26:20. “Without wood a fire goes out; without a gossip a quarrel dies down.” This verse teaches that small conflicts can grow like fire if people continue spreading hatred and division.

James 3:5-6. “The tongue also is a fire…” James compares destructive words to fire that can destroy many lives if not controlled.

Matthew 5:9. “Blessed are the peacemakers, for they shall be called children of God.” Jesus teaches believers to stop conflict and bring peace before destruction spreads further.

1528. SUKUMA: NZILAMAKA IGANJIMIJAGA UNSIMINZI.

Ulusumo lunulo lufumilile kulikujo lya kale ilya Africa. Ikale abhasiminzi wasiminzaga bho magulu bhalibhitila mumapolu, mabhonde na mumachalo bho mduhu ramani. Abhanhu bhenabho bhashikaga aha nzilamaka bhajimija ijilunga. Hunagwene bhagayomba giki, “njilamaka iganjimijaga unsiminzi.”

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agabhonaga wiza wingi oduma uguchagula nulu jimo umuwikaji bhokwe bhunubho. Umunhu ng’wunuyo, agadumaga uguchagula josejose ulu ubhonaga majikolo mingi agawiza kunguno ya gugawila bhumani wikujo lya kikalile kiza umuwikaji bhokwe bhunubho. Uweyi agajimijaga ijilunga ja guitongela chiza ikaya yakwe kunguno ya gugaiwa bhulangwa bho guchagula chiza, umuwikaji bhokwe bhunubho.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nabhasiminzi bha mumapoli abho bhagajimija ijilunga, kunguno nuweyi agajimijaga amasala ga guchagula chiza mpaga oduma uguitongela chiza ikaya yakwe ulu obhonaga majikolo mingi agawiza, umuwikaji bhokwe bhunubho. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki “njizamaka iganjimijaga unsiminzi.”

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na witegeleja bho guchagula gwikala chiza ulubhabhonaga majikolo mingi agawiza, kugiki bhadule kupandika matwajo mingi umukaya yabho jinijo, umuwikaji bhobho bhunubho.

Mithali 3:5–6.

Mathayo 7:13–14.

Yakobo 1:5.

1Wakorintho 14:33.

SWAHILI: NJIA PANDA HUMCHANGANYA MSAFIRI.

Methali hii inatokana na hekima ya jadi ya Kiafrika na pia inaakisiwa katika tamaduni nyingi kote ulimwenguni. Zamani, wasafiri walisafiri kwa miguu kupitia misitu, mabonde, na vijiji bila ramani. Walipofika kwenye barabara nyingi zinazovuka yaani njia panda, waliweza kuchanganyikiwa kwa urahisi na kupoteza mwelekeo. Kwa hivyo methali hiyo iliundwa ili kuwafundisha watu umuhimu wa hekima, mwongozo, na kufanya maamuzi yaliyo wazi maishani mwao. Ndiyo maana walisema kwamba, “njia panda humchanganya msafiri.”

Methali hii hulinganishwa kwa mtu yule hukabiliwa na chaguzi nyingi maishani na hajui ni njia gani ya kufuata maishani mwake. Mtu kama huyo huweza kuchanganyikiwa kwa sababu ya maoni mengi, vishawishi, au fursa nyingi maishani. Yeye hupoteza mwelekeo wa kuongoza familia yake vizuri kwa sababu ya kukosa hekima, mwongozo, na uwezo wa kufanya maamuzi mazuri maishani mwake.

Mtu huyu hufanana na wale watu waliokosa mwongozo na hekima sahihi hadi kufikia hatua ya kupoteza mwelekeo wao kwa sababu naye pia hufuata maelekezo mengi kwa wakati mmoja na hatimaye hupoteza umakini katika kuongoza familia yake hiyo maishani mwake. Kama vile msafiri anavyoweza kupotea kwenye njia panda, mtu asiye na kusudi wazi anaweza kupotea kiroho, kimaadili, au kijamii maishani mwake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “njia panda humchanganya msafiri.”

Methali hii huwafundisha watu kuhusu: umuhimu wa hekima katika kufanya maamuzi, kutafuta mwongozo kabla ya kuchagua njia, kubaki makini maishani, kuepuka mkanganyiko unaosababishwa na mawazo mengi yanayokinzana, na kuamini uongozi na mwelekeo mzuri. Inawakumbusha watu kwamba maisha yana njia nyingi, na chaguo baya zaweza kusababisha matatizo huku chaguo za busara zikiongoza kwenye mafanikio na amani maishani mwao.

Mithali 3:5–6. “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe; katika njia zako zote mtii, naye atanyosha mapito yako.” Mstari huu unafundisha kwamba Mungu hutoa mwongozo wakati barabara za maisha zinaonekana kuchanganyikiwa.

Mathayo 7:13–14. “Ingieni kwa kupitia mlango mwembamba… mlango ni mdogo, na njia nyembamba iendayo uzimani.” Yesu anafundisha kwamba kuna njia nyingi maishani, lakini njia sahihi tu ndiyo inayoongoza kwenye uzima wa milele.

Yakobo 1:5. “Lakini mtu yeyote kati yenu akipungukiwa na hekima, na amwombe Mungu, awapaye wote kwa ukarimu.” Watu wanapokabiliwa na maamuzi yanayochanganya, wanapaswa kutafuta hekima kutoka kwa Mungu.

1Wakorintho 14:33. “Maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani.” Mungu anatamani watu wake watembee katika uwazi, amani, na mwelekeo sahihi badala ya mkanganyiko.

Methali “njia panda humchanganya msafiri” hufundisha kwamba maisha yamejaa chaguzi na njia panda. Bila hekima, mwongozo, na imani katika Mungu, mtu anaweza kupoteza mwelekeo kwa urahisi. Watu wenye busara hutafuta ushauri, huomba uelewa, na kwa uangalifu.

ENGLISH: “INTERSECTION OF ROADS CONFUSES THE TRAVELER.”

This proverb comes from traditional African wisdom and is also reflected in many cultures around the world. In ancient times, travelers journeyed on foot through forests, valleys, and villages without maps. When they reached many crossing roads, they could easily become confused and lose direction. The proverb was therefore created to teach people the importance of wisdom, guidance, and clear decision-making in life. That is why they said, “Intersection of roads confuses the traveler.”

This proverb is compared to a person who faces many choices in life and does not know which path to follow in life. Such a person may become confused because of too many opinions, temptations, or opportunities. He loses direction of leading well his family because of lacking wisdom, guidance, and clear decision-making in life.

This person resembles those people who lacked proper guidance and wisdom to the point of losing their directions because he also follows many directions at the same time and finally loses focus in leading his family in life.

Just as a traveler can become lost at roads intersection, a person without clear purpose can become lost spiritually, morally, or socially. That is why people tell him that, “Intersection of roads confuses the traveler.”

This proverb teaches people about: the importance of wisdom in making decisions, seeking guidance before choosing a path, remaining focused in life, avoiding confusion caused by many conflicting ideas, and trusting good leadership and direction. It reminds people that life has many crossroads, and wrong choices can lead to trouble while wise choices lead to success and peace.

Proverbs 3:5–6. “Trust in the Lord with all your heart and lean not on your own understanding; in all your ways submit to Him, and He will make your paths straight.” This verse teaches that God gives direction when life’s roads seem confusing.

Matthew 7:13–14. “Enter through the narrow gate… small is the gate and narrow the road that leads to life.” Jesus teaches that there are many paths in life, but only the right path leads to eternal life.

James 1:5. “If any of you lacks wisdom, you should ask God, who gives generously to all.” When people face confusing decisions, they should seek wisdom from God.

1Corinthians 14:33.“For God is not a God of confusion but of peace.” God desires His people to walk in clarity, peace, and right direction rather than confusion.

The proverb “intersections of roads confuse the traveler” teaches that life is full of choices and crossroads. Without wisdom, guidance, and faith in God, a person can easily lose direction. Wise people seek counsel, pray for understanding, and carefully.

1527. SUKUMA: UBHULONGO BHULI MAGULU MAGUHI.

Ulusumo lunulo lwingile kuli mpeji o magulu maguhi uyo agagema gutoroka wangu uduma. Umunhu ng’wunuyo agandya gupela wangu, aliyo adasegendelile upandikwa. Hukwene huguhaya giki, ubhulongo bhudikalaga makanza malihu kunguno ubhunhana bhugabhupandikaga wangu. Hunagwene abhanhu bhagang’wila giki, “ubhulongo bhuli na magulu maguhi.”

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agabhalembaga abhangi kusolobho yakwe na nhinda jakwe, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agiganikaga giki ubhulongo bhunubho bhugumshisha kule aliyo lulu ubhunhana bhugang’olesha hape wangu, umuwikaji bhokwe. Uweyi agabhonaga soni ningi mpaga oduma uguilela ikaya yakwe yiniyo ulu bhobadijiwa ubhulongo bhokwe bhunubho, umukikalile kakwe kenako.

Umunhu ng’wunuyo agikolaga nu mpeji uo magulu maguhi uyo agagema gutoroka uduma, kunguno nuweyi agabhalembaga abhiye mpaga oduma uguyilema ikaya yakwe ulu bhobadijiwa ubhulongo bhokwe bhunubho, umuwikaji bhokwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “ubhulongo bhuli na magulu maguhi.”

Ulusumo lunulo lolanga abhanhu higulya ya guleka bhulongo bho guwikalana chiza ubhunhna, kugiki bhadule gujilela chiza ikaya jabho, umuwikaji bhobho bhunubho.

Luka 8:17.

Mithali 12:19.

Wakolosai 3:9.

Yohana 8:32.

Mithali 19:9.

SWAHILI: UONGO UNA MIGUU MIFUPI.

Methali hii inaweza kufuatiliwa hadi kwa mkimbiaji mwenye miguu mifupi ambaye alijaribu kumtoroka mtu haraka. Alianza mbio haraka, lakini hakuweza kwenda mbali kabla ya kukamatwa, akashindwa. Inamaanisha kwamba uongo haudumu kwa muda mrefu kwa sababu ukweli hatimaye humpata. Ndiyo maana watu humwambia kwamba “uongo una miguu mifupi.”

Methali hii hulinganishwa kwa mtu anayesema uongo ili kuwadanganya wengine kwa faida yake binafsi, ulinzi, au kiburi katika maisha yake. Mtu kama huyo hudhani uongo huo utampeleka mbali, lakini hivi karibuni ukweli humfichua. Yeye huona aibu hadi kufikia hatua ya kushindwa kuiongoza familia yake, pale uongo wake unapogunduliwa, katika maisha yake.

Mtu huyu hufanana na yule mkimbiaji mwenye miguu mifupi aliyejaribu kumtoroka mtu haraka akashindwa, kwa sababu naye pia huwadanganya wengine hadi kufikia hatua ya kuona aibu wakati wengine wanapoujua ukweli, katika maisha yake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba “uongo una miguu mifupi.”

Methali hii huwafundisha watu kuhusu: ukweli, hatari ya udanganyifu, uaminifu katika jamii, umuhimu wa kusema ukweli kila wakati na uhakika kwamba uwongo uliofichwa hatimaye utafichuliwa.

Luka 8:17 “Kwa maana hakuna kitu kilichofichwa ambacho hakitafichuliwa, wala hakuna kitu kilichofichwa ambacho hakitajulikana au kuwekwa wazi.”

Mithali 12:19 “Midomo ya kweli hudumu milele, lakini ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.”

Wakolosai 3:9 “Msiambiane uongo, kwa kuwa mmevua utu wenu wa zamani pamoja na matendo yake.”

Yohana 8:32 “Ndipo mtakapojua ukweli, nao ukweli utawaweka huru.”

Mithali 19:9 “Shahidi wa uongo hatakosa kuadhibiwa, na yeyote asemaye uongo ataangamia.”

ENGLISH PROVERB: A LIE HAS SHORT LEGS.

This proverb can be traced back to a runner with short legs who tried to escape from someone faster. He began the race quickly, but could not go far before being caught. It means that lies do not last long because the truth eventually catches up with them. That is why people say “a lie has short legs.”

This proverb is compared to a person who speaks falsehood to deceive others for personal gain, protection, or pride in his life. Such a person may think the lie will carry him far, but soon the truth exposes him. He is ashamed when his lie is discovered to the point of failing to lead his family, in his life.

This person resembles that runner with short legs who tried to escape from someone faster because he also lies others to the point of being ashamed when others know the truth, in his life. That is why people tell him “a lie has short legs.”

This proverb teaches people about: Honesty and truthfulness, the danger of deception, trustworthiness in society, the importance of speaking the truth always and the certainty that hidden lies will eventually be revealed

Luke 8:17 “For there is nothing hidden that will not be disclosed, and nothing concealed that will not be known or brought out into the open.”

Proverbs 12:19 “Truthful lips endure forever, but a lying tongue lasts only a moment.”

Colossians 3:9 “Do not lie to one another, since you have taken off your old self with its practices.”

John 8:32 “Then you will know the truth, and the truth will set you free.”

Proverbs 19:9 “A false witness will not go unpunished, and whoever pours out lies will perish.”

1525. SUKUMA: BHULANGWA BHO NDUHU JITO BHULI GUTI TALA IYO IDINA MAGUTA.

Ulusumo lunulo luhoyelile giki ubhumani ying’wene bhudatoshije mpaka wambilije bhanhu gwikala chiza. Umulikujo lya jiafrica, nono abhamuchalo, abhanhu bhanhiyagwa likujo bho gujilanija numo alibhutumamila ubhumani bhokwe ijinagubheja kaya iyalange lisoga, idi bho bhumani duhu.

Itala iyo idina mafuta idadulile gufunya lisana, giko lulu, nu bhumani ubho bhudina miito bhudadulile gwambilija bhanbhu gwikala chiza. Hunagwene abhanhu abhakikujo bhagayomba giki, “bhulangwa bho nduhu miito bhuli guti tala iyo idina maguta.”

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo wilanga mihayo mingi mushule, mukanika nulu mubhananzengo bhiye, aliyo lulu adumile uguitumamila umuwikaji bhokwe. Umunhu ng’wunuyo, agayombaga mihayo ikujo aliyo adikalaga muwikaji wikujo kunguno ya nhungwa jakwe gubhiza ja bhubhi, umukajile kakwe. Uweyi agadumaga uguyilela chiza ikaya yakwe kunguno ya nhungwa jakwe ijabhubhi jinijo, umukikalile kakwe kenako.

Umunhu ng’wunuyo agikolaga nuyo alinibala litale aliyo adalilimaga kunguno nuweyi alinabhumani bho mihayo mingi aliyo adabhutumamilaga umuwikaji bhokwe bhunubho. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “bhulangwa bho nduhu miito bhuli guti tala iyo idina maguta.”

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya solobho ya kubhutumamila chiza ubhulangwa ubho bhabhupandika kugiki bhadule gujilela chiza ikaya jabho jinijo, umuwikaji bhobho bhunubho.

Yakobo 1:22.

Mathayo 5:16.

Mhubiri 9:10.

Luka 11:33.

SWAHILI: ELIMU BILA MATENDO NI KAMA TAA ISIYO NA MAFUTA.

Methali hii huzungumzia kwamba maarifa pekee hayatoshi isipokuwa yaemetekelezwa. Katika hekima ya kitamaduni ya Kiafrika, haswa katika jamii nyingi za vijijini, watu walimthamini mtu si tu kwa kile alichokijua, bali pia kwa jinsi alivyotumia maarifa yake katika kuwasaidia wengine vya kutosha kuboresha maisha yao. Taa isiyo na mafuta haiwezi kutoa mwanga; vivyo hivyo, elimu isiyo na matendo haiwezi kuinufaisha jamii. Ndiyo maana wenye busara walisema “elimu bila matendo ni kama taa isiyo na mafuta.”

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu yule ambaye amejifunza mambo mengi shuleni, kanisani, au katika jamii, lakini anashindwa kutumia maarifa hayo katika maisha ya kila siku. Mtu kama huyo huzungumza kwa busara lakini haishi kwa busara kwa sababu ya mwenendo wake mbaya. Yeye hushindwa kuwalea vizuri wanafamilia wake kwa sababu ya kuzungumza kwa busara bila kuishi kwa busara katika maisha yake.

Mtu huyo hufanana na mtu yule ambaye anamiliki zana za kilimo lakini halimi kamwe ardhi, au mtu ambaye hubeba Biblia kila siku lakini halitii Neno la Mungu. Maarifa ya mtu huyo hayana maana bila ya kutekelezwa kwa matendo yaboreshayo maisha ya watu. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “elimu bila matendo ni kama taa isiyo na mafuta.”

Methali hii huwafundisha watu kuhusu: umuhimu wa kutumia elimu katika vitendo, kutumia hekima kuitumikia jamii, kuishi kulingana na kile ambacho mtu amejifunza, uwajibikaji na tabia njema na thamani ya maarifa ya vitendo maishani mwao, ili waweze kufanikiwa maishani mwao.

Yakobo 1:22. “Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, mkijidanganya nafsi zenu.”

Mathayo 5:16. “Nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema.”

Mhubiri 9:10. “Lolote mkono wako utakalopata kulifanya, lifanye kwa nguvu zako zote.”

Luka 11:33. “Hakuna mtu awashaye taa na kuificha.”

Mistari hii huonesha kwamba hekima na elimu ya kweli lazima izae matendo mema yanayowanufaisha wengine.

ENGLISH: EDUCATION WITHOUT ACTION IS LIKE A LAMP WITHOUT OIL.

This proverb talks about that knowledge alone is not enough unless it is put into practice. In traditional African wisdom, especially in many village communities, people valued a person not only for what he knew, but for how he used his knowledge to help others enough to improve their lives. A lamp without oil cannot produce light; likewise, education without action cannot benefit society. That is why the wise said “education without action is like a lamp without oil.”

This saying is compared to a person who has learned many things in school, church, or society, but fails to apply that knowledge in daily life. Such a person talks wisely but does not live wisely because of his wicked conduct. He fails to nurture well his family members because of speaking wisely without living wisely in his life.

This person resembles someone who owns farming tools but never cultivates the land, or a person who carries a Bible every day but never obeys the Word of God. Knowledge becomes useless when it is not practiced. That is why people tell him that, “education without action is like a lamp without oil.”

This proverb teaches people about: the importance of putting education into action, using wisdom to serve society, living according to what one has learned, responsibility and good character and the value of practical knowledge in life.

James 1:22. “But be ye doers of the word, and not hearers only, deceiving your own selves.”

Matthew 5:16. “Let your light so shine before men, that they may see your good works.”

Ecclesiastes 9:10.  “Whatever your hand finds to do, do it with all your might.”

Luke 11:33. “No one lights a lamp and hides it.”

These verses show that true wisdom and education must produce good actions that benefit others.

850. NZUB’I ADAB’ITILAGA ILAMBO.

Ulusumo lunulo, lulilola nzub’i o shi, nulu ndilo uyo agaja ogazub’a bhuli hilambo lyene mpaga abhite hoyi, gujilola ishi. Unzub’i ng’wunuyo, agitaga giko kunguno ahayile apandike ndilo nyingi. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “nzub’i adab’itilaga ilambo.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agasulujaga jikolo jilebhe, uyo agab’itaga bhuli kaya yene, umubhusuluja bhokwe. Unsuluja ng’wunuyo, agajaga uliga bhuli aha kaya yene iyo aliyibhona ilugulile unyango, kunguno atogilwe amale gujijinja pye ijikolo ijo alijisuluja, umunimo gokwe gunuyo. Uweyi agapandikaga solobho mhale noyi umubhusuluja bhokwe bhunubho kunguno ya wikomeja bhokwe ubho gubhita bhuli kaya, umutumami bho milimo yakwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nu nzub’i o ndilo uyo agabhitaga bhuli ilambo, kunguno nu weyi agajaga ubhita bhuli kaya, umubhusuluja bhokwe bhunubho. Uweyi abhalangaga abhanhu bhakwe inzila ja guhoya na bhanhu bhingi umubhutumami bhobho, kugiki bhadule gupandika sabho ningi, umumilimo yabho. Hunagwene agabhawilaga abhanhu giki, “nzub’i adab’itilaga ilambo.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gwigulambija gubhutumila pye uwasa ubho bhali nabho umubhutumami bho milimo yabho, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi, umuwikaji bhobho.

Luka 24:47.

Matendo ya mitume 1:8.

Warumi 10:18.

Marko 16:15-16.

KISWAHILI: MVUVI HAACHI KUPITIA BWAWANI.

Methali hiyo, humwangalia mvuvi wa samaki ambaye hupitia kwenye kila bwawa akitafuta samaki. Mvuvi huyo, hufanya hivyo kwa sababu anataka kupata mafanikio ya kuvua samaki wengi. Ndiyo maana watu husema kwamba, “mvuvi haachi kupitia bwawani.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huuza vitu fulani, kwa hupitia kwenye kila familia, katika uuzaji wa biashana yake. Mfanya biashana huyo, huenda akiingia kwenye kila familia ambayo anauona mlango wake uko wazi, kwa sababu anapenda kuuza vitu vyake vyote, katika biashara yake hiyo. Yeye hupata faida kubwa sana katika kazi yake hiyo, kwa sababu ya bidii yake ya kupitia kwenye kila familia, katika utekelezaji wa majukumu yake.

Mtu huyo, hufanana na yule mvuvi wa samaki aliyepitia kwenye kila bwawa, kwa sababu naye huenda akiingia kwenye kila familia, katika biashara yake hiyo. Yeye huwafundisha pia watu wake namna ya kuongea na watu wengi katika utekelezaji wa majukumu yao, ili waweze kupata mafanikio mengi, katika kazi zao. Ndiyo maana huwa anawaambia watu kwamba, “mvuvi haachi kupitia bwawani.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kujibidisha kuzitumia fursa zote walizo nazo, katika utekelezaji wa majukumu yao, ili waweze kupata mafanikio mengi, maishani mwao.

Luka 24:47.

Matendo ya mitume 1:8.

Warumi 10:18.

Marko 16:15-16.

fisherman-1

people-with fish

visser-fishing zanzibar

fishpond-

ENGLISH: THE FISHER-PERSON DOES NOT JUMP A FISHPOND (TRADITIONS ARE LIKE A  LAW).

This proverb focuses on a fisherman who goes through each pond in searching for fish. He does this because he wants to be successful in catching more fish. That is why people say that, “the fisher-person does not jump a fishpond.”

This proverb is compared to the man who sells certain things by passing through every family in his trade. Such trader enters at every family which he sees that its door is open, because he likes to sell all his goods. He gets a lot of benefits from his work, because of his persistence of passing through each family that can buy his goods.

This man is like the fisherman who passed through every pond, because he too goes into every family that can buy his goods. He also teaches his people on how to communicate with many people in fulfilling their duties, so that they may be more successful in their daily activities. That is why he often tells people that, “the fisher-person does not jump a fishpond (traditions are like a law).”

This proverb teaches people on how to strive to use all the opportunities which they have in fulfilling their daily responsibilities, so that they may have more successes in their families.

Luke 24:47.

Acts 1: 8.

Romans 10:18.

Mark 16: 15-16.