Joe Healey

424. MASALA GADIYONGEJIYAGWA.

Imbuki ya kahahyile kenako yilolile masala ga bhanhu. Amasala genayo  gagabhizaga gali mtwe go ng’wa munhu, ayo gagatulagwa moyi na Nsumbi okwe umunhu ng’wunuyo. Kuyiniyo lulu, ulu munhu ukenya mhayo nebhe, abhanhu bhaganhugulaga kugiki wilange.

Aliyo, ulu ukenye hangi umunhu ng’wunuyo, mumho amasala gakwe gagelelile henaho, bhadikomile ugung’ongegeja. Hunagwene abhanhu bhagayongaba giki, ‘masala gadiyongejiyagwa.’

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agamanaga ukenye mara hingi, umuwikaji bhokwe. Umunhu ng’wunuyo, agabhakoyaga abhiye kunguno ya masala gakwe genayo, ayo gagang’wenhelejaga gwita ya bhubhi. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘masala gadiyongejiyagwa.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya gubhiza na wiyumija bho gudula gubhambilija ugwikala na bhanhu bha mbika ningi, kunguno, a‘masala gadiyongejiyagwa,’ bhuli ng’wene umo winhilwa, agusaga ni giko.

Mithali 19:25.

KISWAHILI: AKILI HAZIONGEZEANWI.

Chanzo cha msemo huo chaangalia akili za mtu. Akili hizo huwa kichwani mwake mtu alizopewa na Muumba wake. Kwa hiyo basi, mtu akikosea neno fulani, huonywa na wenzake ili ajifunze.

Lakini akikosea tena mtu huyo maana yake, akili zake hunesha kwamba, zimekomea hapo, wao hawawezi kuziongeza. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘akili haziongezeanwi.’

Msemo huo hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hukosea mara kwa mara, maishani mwake. Mtu huyo huwasumbua wenzake kwa sababu ya akili zake hizo, ambazo humsababisha kutendo maovu. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘akili haziongezeanwi.’

Msemo huo hufundisha watu juu ya kuwa na uvumilivu wa kuwasaidia katika kuishi na wenzao wenye tabia tofauti na wao, ili waweze kuwa pamoja, kwa sababu ‘akili haziongezeanwi.’

Mithali 19:25.

black-woman1

 

ENGLISH: INTELLIGENCIES DO NOT ADD TO EACH OTHER.

The essence of the above saying looks at one’s intelligence.  Intelligence is considered to be in one’s head as given by his/her Creator. If someone fails to do something someone else can help to correct it with the aim of making him/her learn. But, if it happens that that person keeps on repeating the same mistake then the conclusion is that his/her intelligence ends up there. He/she cannot stretch it further. That is why people can describe this scenario using the saying that ‘intelligencies do not add to each other.’

The saying can be compared to a person who repeatedly makes mistakes in his/her life. Such a person can bother others who witness those mistakes. He/she appears to justify that his/her capacity in thinking has ended and no one can add more to what he/she has in mind.

The saying teaches people about having patience in living with others with different capacities and personalities.

Proverbs 19:25.

423. UBHEBHE ULIKALEMEJI.

Imbuki ya lusumo lunulo yingilile kubhulemeji bho ng’wa munhu nebhe. Umunhu ng’wunuyo ulu utung’wa guja gujutumama nimo nebhe, agalemaga.

Uweyi adahamagwa na bhiye umuwikaji bhokwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, ‘ubhebhe ulikalemeji.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo obhalemela abhabyaji bhakwe. Umunhu ng’wunuyo adabhigwaga abhabyaji bhakwe bhenabho, ulu bhang’wila mhayo nebhe. Ulu bhanhugula higulya ya guleka ginhu jilebhe, uweyi agalemaga. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, ‘ubhebhe ulikalemeji.’

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya kubhakuja bhabyaji bhao, kugiki bhadule gupandika wikaji bho shigu ningi ukuwelelo, na bhuyeji bhutale ung’wigulu.

Mithali 19:13.

KISWAHILI: WEWE NI YULE ALIYESHINDIKANA.

Chanzo cha methali hiyo chatokea kwenye hali ya kushindikana kwa mtu fulani. Mtu huyo akitumwa kwenda kufanya kazi fulani hukataa.

Yeye hukataa kuonywa na wenzake maishani mwake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, ‘wewe ni yule aliyeshindikana.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ameshindikana kwa wazazi wake. Mtu huyo hawasikilizi wazazi wake, wakimwambia kufanya kitu fulani. Wakimuonya juu ya kuacha kufanya jambo fulani, yeye hukataa. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, ‘wewe ni yule aliyeshindikana.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuwaheshimu wazazi wao, ili waweze kuishi siku nyingi hapa duniani, na heri Mbinguni.

Mithali 19:13.

lady

kids3

 

ENGLISH: YOU ARE A FAILED PERSON.

The source of this saying is someone’s failure to achieve his/her expectations in life. That person tends to refuse doing something when asked to do so. Due to his/her behaviour of disobeying his/her elders he/she can be warned by the saying that ‘you’re a failed person.’

This saying can be compared to a person who refuses to obey the teachings of his/her parents. Such a person does not listern to his/her parents who tell him/her how to approach life. Eventually, parents can give give up leaving him/her to face the consequences of his/her disobedience.

The proverb teaches people to respect their parents so that they can live longer and be blessed in Heaven.

Proverbs 19:13.

422. NAKAKUMBULAGA AKANIGO KANE.

Imbuki ya kahayile kenako yingilile kubhukumbuji bho nigo gokwe, umunhu nebhe. Ubhukumbuji bho nigo gunuyo, bhuli bho ng’wa munhu uyo oya kale ugugubhona unigo gokwe gunuyo. Hunagwene umunhu ng’wunuyo agayombaga giki, ‘nakakumbulaga akanigo kane.’

Akahahile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo alintonda ng’wiye ginhu guti hela, bhusiga, nulu ng’wenda uyo ogulanda. Umunhu ng’wunuyo agayombaga giko, kubho guntonda ung’wiye anshokeje iginhu jakwe jinijo, kunguno ya gudila ugujishosha ukuli weyi. Hunagwene umunhu ng’wunuyo, agayombaga giki, ‘nakakumbulaga akanigo kane.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya gushosha wangu iginhu ijo bhalanda ukubhinikili, kugiki.bhadule gwikala halumo bho bhutogwa na bhichabho, umuwikaji bhobho.

Mithali 11:24.

Mithali 12:9.

KISWAHILI: LETA ULE MZIGO NIMEUKUMBUKA.

Chanzo cha msemo huo chatokea kwenye ukumbukaji wa mzigo wake mtu fulani. Ukumbukaji wa mzigo huo, ni wa mtu ambaye hajauona mzigo wake huo tangu siku nyingi. Ndiyo maana mtu huyo husema kwamba, ‘leta ule mzigo nimeukumbuka.’

Msemo huo hulinganishwa kwa mtu yule ambaye anamdai mwenzake kitu kama hela, mtama, au nguo aliyoazima. Mtu huyo husema hivyo kama njia ya kumdai mwenzake huyo amrudishie deni lake, kwa sababu ya kuchelewa kulirudisha kwake. Ndiyo maana mtu huyo husema kwamba, ‘leta ule mzigo nimeukumbuka.’

Msemo huo hufundisha watu juu ya kurudisha haraka kitu walichokopa kwa wenyewe, ili waweze kuishi katika umoja na wenzao, maishani mwao.

Mithali 11:24.

Mithali 12:9.

basket

luggage

 

ENGLISH: BRING MY LUGGAGE, I HAVE REMEMBERED IT.

The source of the above saying comes from the memory of someone whose property was borrowed by someone else. It might have taken quiet sometime without returning it. This is why the owner of the property can use the saying ‘bring my luggage, I have remembered it’ to communicate his/her need to getting back his/her property.

The saying can be compared to a person who demands for his/her property such as money, sorghum, or clothes from someone else. The debtor is forced to pay it back.

The saying teaches people about repaying their debts in order to create a ground for unity and cooperation in the society.

Proverbs 11:24.

Proverbs 12: 9.

421. NILINDAGI NAGAPONYE NIGO.

Imbuki ya kahayile kenako yingilile kubhuponya bho nigo go bhanhu. Olihoyi munhu uyo oliotung’wa guchala ginhu halebhe. Umunhu ng’wunuyo oli nabhiye umulugendo lunulo. Aho oshiga uko kaya iyo oguchalaga unigo gunuyo, agabhawila abhiye giki, ‘nilindagi nagaponye nigo.’

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatimijaga chiza, imilimo iyo utung’wa na bhiye guitumama. Umunhu ng’wunuyo agabhambilijaga abhanhu, ukunhu alikihamo na bhiye abho alinabho. Hunagwene agayombaga giki, ‘nilindagi nagaponye nigo.’

Akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya gujishisha chiza imhola ijo bhatung’wa gujichala halebhe, kugiki bhadule gwiyambilija halumo na bhichabho, umuwikaji bhobho.

Zaburi 43:3.

Mathayo 11:28.

KISWAHILI: NINGOJENI NIKATUPE MZIGO.

Chanzo cha msemo huo chatokea kwenye utupaji bha mzigo wa watu wa sehemu fulani. Alikuwepo mtu mmoja aliyetumwa kupeleka kitu fulani kwa watu. Mtu huyo alikuwa pamoja na wenzake, katika safari hiyo. Alipofika pale alipotumwa kuupeleka ule mzigo aliwaambia wenzake kwamba, ‘ningojeni nikatupe mzigo.’

Msemo huo hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hutimiza vizuri kazi aliyotumwa na wenzake kuifanya. Mtu huyo huwasaidia watu, huku akiwa pamoja na wenzake. Ndiyo maana mtu huyo huwaambia wenzake kwamba, ‘ningojeni nikatupe mzigo.’

Msemo huo hufundisha watu juu ya kufikisha vizuri ujumbe waliotumwa kuupeleka kwa watu, ili waweze kusaidiana katika kuutunza umoja huo, maishani mwao.

Zaburi 43:3.

Mathayo 11:28.

 

outdoors

carrying

 

ENGLISH: WAIT FOR I AM GOING TO THROW THE LUGGAGE.

The source of this saying comes from dumping someone’s luggage. There was a man who was asked to send a certain luggage to someone else. Such a man was with his friends walking towards that direction where he has to send the luggage. When he reached the destination, he told his friends that ‘wait for I am going to throw the luggage’ to mean handing over to the respective people.

The saying can be compared to a person who properly fulfills the tasks assigned to him/her by his/her colleagues.

The saying teaches people about effective communication by delivering the required information on time to the required people.

Psalm 43: 3.

Matthew 11:28.

420. UNENE NABHIZILE NTONGEJI O LUGENDO.

Imbuki ya lusumo lunulo yingilile kubhushikanu bho ng’wa munhu. Ubhushikanu bhunubho bhuli bho gubhatongela abhanhu.

Ubhutongeji bhunubho bhudulile gubhiza bho gulekelwa na bhanhu abho bhali bhatongeji, nulu bhogushila gucha abhantongeji, usaga weyi uyo alintali, umuchalo jinijo. Hunagwene umunhu ng’wunuyo agayombaga giki, ‘unene nabhizile ntongeji o lugendo.’

Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo aimanile chiza imilimo yakwe iyagubhatongela abhanhu bhakwe bhenabho.

Umunhu ng’wunuyo alintongeji o bhanhu uyo agabhatongelaga bhobhutogwa bhutale. Uweyi agabhalangaga abhanhu bhakwe inzila ja gubhatumamila bho bhutogwa abhichabho. Hunagwene umunhu ng’wunuyo agayombaga giki, ‘unene nabhizile ntongeji o lugendo.’

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya gujimana inzila ja gubhatongela abhanhu bhabho bho bhutogwa bhutale, kugiki bhadule gwikala bho mholele, umuwikaji bhobho.

Matendo ya mitume 2: 14-22.

KISWAHILI: MIMI NIMEKUWA KIONGOZI WA SAFARI.

Chanzo cha methali hiyo chatokea kwenye ukomavu wa mtu katika makuzi yake. Ukomavu huo ni wa kuongoza watu kuyafikia malengo fulani.

Uongozi huo waweza kuwa wa kurithi, au wa kutokana na kufa kwa viongozi wote, akabaki yeye peke yake, ambaye ni mkubwa katika kijiji hicho. Ndiyo maana mtu huyo husema kwamba, ‘mimi nimekuwa kiongozi wa safari.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu yule ambaye anaelewa vizuri wajibu wake wa kuwaongoza wananchi wake. Mtu huyo ni kiongozi wa watu, ambaye huwaongoza watu kwa upendo mkubwa.

Yeye huwafundisha pia watu wake njia za kuwaongoza wenzao kwa upendo huo. Ndiyo maana mtu huyo husema kwamba, ‘mimi nimekuwa kiongozi wa safari.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuzielewa njia za kuwaongoza watu wao kwa upendo mkubwa, ili waweze kuishi kwa amani, maishani mwao.

Matendo ya mitume 2: 14-22.

people-leader

ENGLISH: I HAVE BEEN A LEADER OF THE JOURNEY.

The source of the above saying comes from one’s ability to demonstrate his/her capacity to lead others. His/her capacity is gauged based on how he/she can lead others to attain their desired goals in life. This leadership position can be through inheritance (after the death of the former leader) or by appointment. Such a person, after succeeding to lead his/her people in the right direction, he/she can say ‘I have been a leader of the journey.’

This saying can be compared to a person who understands his/her responsibilities to his/her citizens; leading people to the right direction. Such a leader leads his/her people with love and humility. He/she also teaches others how lead in a manner that can make them be loved by others as well.

The proverb teaches people to understand the ways of leading their people with great love. This will help them to have peace and love all the time.

Acts 2: 14-22.