Joe Healey

682. KULYA N’GWA MPANGA TUKIKALAGA HA NGEGU (LUGEGU).

Ulusumo lunulo, lofumila mulyimbo lya Nhingi, Shagembe, uyo agang’wimbila nywani okwe, Nchimani:

“Unene naduduja uguleka ugung’wa uwalwa, Nchimani ng’wana o ng’wa Mulola, muna Kadoto. UMulungu adina mahoya ulu uhaya gugusola. Bhabehi ugulya ng’wa mpanga dugikala ha ngegu. Abho mtogilwe gubyaja sabho na ng’wisabhe guti ng’walagana nu Mulungu. Bhabehi! Nalimuwila, gulya ng’wa mpanga dugikalaga ha ngegu.” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 42.

 Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagatumilaga chiza ijiliwa ijo bhinhiwa nu Mulungu. Giko, abhoyi bhadebhile igiki, bhinhiwa jiliwa na Mulungu, ijo igelelilwe bhajilye haho bhatali bhapanga.

Bhalihoyi bhanhu bhamo abho bhalemile ugulya, nulu, ugujitumila isabho ijaha welelo. Abhanhu bha mbika jinijo, bhadina masala, dugemele, umunhu alina ng’ombe nyingi, aliyo abhana bhakwe na nke okwe, bhagazwalaga sagala sagala.

Hangi, bhadina bhulalo bhusoga. Ulu umo obho usada bhalemile ujinga ng’ombe bhang’wambilije. Hunagwene abho bhadebhile isolobho ya gujitumila chiza isabho jinijo, bhagabhawilaga abhanhu bhenabho, giki, ‘kulya ng’wa mpanga tukikalaga ha ngegu (lugegu).’ Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ubhukurasa bho 42.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu giki, idina solobho uguleka ugulya ijiliwa nulu, uguleka ujitumila isabho ijo bhinhiwa nu Mulungu. “Giko ugukija ugulya ijiliwa ijo dalekelwa nu Yesu Kristo, idina solobho.

UYesu Kristo ng’winikili, agadukomelejaga gulya mili gokwe na gung’wa milinga gakwe, mu Sakramenti ya Ekaristi Nhagatifu. Ulu dutali aha welelo igubhiza mhayo go nyabuli ulu dukija gulya umili gokwe nu gung’wa amilinga gakwe, iki “kulya ng’wa mpanga tukikalaga ha ngegu (lugegu).

Hangi ijililwa iji jidaliyagwa na bhanhu abho bhacha, ukwene huguhaya, abhanhu abho bhali mushibhi, ijoyi jigaliyagwa na bhanhu abho bhali na mioyo yape na guzunya…Ulu duli mushibhi igelelilwe dulumbwe ishibhi haho dutali ugubhokela Ekaristi. Ee, ugalyaga bho nduhu ugukalabha amakono?” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ubhukurasa bho 43.

Mhubiri 5:18-19.

Zaburi 128:1-2.

Mathayo 26:26-28.

Yohane 6: 52-53.

KISWAHILI: MWENYE KULA NI MTU HAI TUNAKAA UKINGONI.

Methali hiyo, imetokea kwenye wimbo wa Manju Shagembe aliyemwimbia rafiki yake Nchimani:

“Mimi siwezi kuacha kunywa pombe, Nchimani bin Mulola, wa Kadoto. Mungu hana maongezi kama akitaka kukuchukua. Jamani kula tukingalia hai, kwani, huwa tunakaa ukingoni. Mnaopenda kuzalisha mali na mtajirike kama mna mapatano na Mungu. Jamani! Nawaambieni, kula tungali hai kwani tunakaa ukingoni.” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 42.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo hulinganishwa kwa watu wanaotumia vizuri chakula ambacho wamepewa na Mungu. Hivyo, wanafahamu kwamba, wamegawiwa chakula na Mungu ambacho ni lazima wakile wakati wangali wazima.

Wako baadhi ya watu ambao hawataki kula au kutumia mali ya hapa duniani. Watu wa namna hiyo hawana akili, kwa mfano, mtu ana ng’ombe wengi, lakini watoto wake na mke wake huvaa ovyo ovyo.

Tena hawana mahali pazuri pa kulala. Ikiwa mmoja wao amepatwa na ugonjwa hataki kuuza ng’ombe amsaidie. Ndiyo maana wale wanafahamu umuhimu wa kuvitumia vizuri mali walivyo navyo, huwaambia watu hao kwamba, ‘mwenye kula ni mtu hai, tunakaa ukingoni.’ Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa, 42.

Methali hiyo, huwafundisha watu kwamba, haina maana kutokula chakula au kutokutumia mali ambazo wamepewa na Mungu. “Vile vile kutokula chakula tulichoachiwa na Yesu Kristo pia, haina maana.

Yesu Kristo mwenyewe hutuhimiza kula mwili wake na kunywa damu yake katika Sakramenti ya Ekaristi Takatifu. Ikiwa bado tupo hapa duniani litakuwa jambo la kipumbavu tusipokula mwili wake na kunywa damu yake kwa kuwa. “Mwenye kula ni mtu hai, tunakaa ukingoni.”

Tena chakula hiki hakiwezi kuliwa na watu ambao wamekufa, yaani watu ambao wamo katika hali ya dhambi, bali huliwa na watu wenye mioyo safi na imani…Ikiwa tumo katika hali ya dhambi yatupata kuungama kabla ya kupokea Ekaristi. Je, hula bila kunawa mikono?” Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 43.

Mhubiri 5:18-19. “Ndipo nikatambua kwamba ni vema na sahihi kwa mtu kula na kunywa na kutosheka katika kazi yake ngumu chini ya jua katika siku chache za maisha yake Mungu alizompa, kwa maana hili ndilo fungu lake. Zaidi ya yote, Mungu anapompa mtu ye yote utajiri na milki, humwezesha kuvifurahia, kukubali fungu lake na kuwa na furaha katika kazi yake, hii ni karama ya Mungu.”

Zaburi 128:1-2. “Heri ni wale wote wamchao BWANA, waendao katika njia zake. Utakula matunda ya kazi yako, Baraka na mafanikio vitakuwa vyako.”

Mathayo 26:26-28. “Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, ‘‘Twaeni, mle, huu ndio mwili wangu.’’Kisha akachukua kikombe, akashukuru, akawapa akisema, ‘‘Kunyweni nyote katika kikombe hiki. Hii ndiyo damu yangu ya agano, ile imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.”

Yohane 6: 52-53. “Ndipo Wayahudi wakaanza kuhojiana vikali wao kwa wao wakisema, “Mtu huyu awezaje kutupatia mwili wake tuule?’’ Hivyo Yesu akawaambia, “Amini, amini, nawaambia, msipoula mwili wa Mwana wa Adamu na kuinywa damu Yake, hamna uzima ndani yenu.”

africa uganda

food5

ENGLISH: OUR DAYS TO LIVE ON EARTH ARE NUMBERED, EATING IS IMPORANT.

This saying comes from Manju Shagembe’s song who was singing to his friend Nchimani:

“I cannot stop drinking alcohol, Nchimani, Mulola’son’son, of Kadoto. God has no negotiation if He wants to take you. Eat while still alive, for we are always on the brink. You who want to produce wealth and get rich as if you have agreement with God. Hello! I tell you, “Eating is life to human being” (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 42). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

This saying can be compared to those people who make good use of the food given to them by God. Such people have food that can make them eat throughout their life on earth. This saying also can be compared to someone who has enough riches but does not spend it well for the benefit of his/her children as a result, they can end up dying poorly. In such a scenario of not spending well the riches one has, one can experience things such as failing to have a good place to sleep, and not attending well family members when have problems. That is why those who are aware of the importance of using the resources they  tell those people, ‘The days to live on earth are numbered, eating is important’ (Refer to ‘Gospel Spelling in Proverbs,’ page 42).

This saying teaches people to spend well what they have managed to get in their lives. For Christians, not eating food Jesus left us with is none sense; it makes us die a satanic death.

Jesus Christ Himself urges us to eat His flesh and drink His blood in the Sacrament of the Holy Eucharist. If we are still here on earth it would be foolish for us not to eat His body and drink His blood. “Eating is life to human being who live on the brink.”

And this food cannot be eaten by people who are dead, that is, people who are in a state of sin, but is eaten by people who have a pure heart and faith. Do you eat without washing your hands? ” (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 43).

Ecclesiastes 5:18-19  “ This is what I have observed to be good: that it is appropriate for a person to eat, to drink and to find satisfaction in their toilsome labour under the sun during the few days of life God has given him –this is their lot. Moroever, when God gives someone wealth and possessions, and the ability to enjoy them, to accept their lot be happy in their toil –this is a gift of God.”

Psalm: 128:1-2 “ Blessed are all who fear the LORD, who walk in obedience to him. You will eat the fruit of your of your labour; blessings and prosperity will be yours.”

Matthew 26:26-28 “ While they were eating Jesus took bread, and when he had given thanks, he broke it and gave it to his deciples, saying, ‘take and eat; this is my body.’ The he took a cup, and when he had given thanks, he gave it to them, saying ‘Drink from it, all of you. This is my blood of the covenant, which is poured out for many for the forgiveness of sins.”

John 6: 52-53 “ Then the Jews began to argue sharply among themselves, ‘How can this man give us his flesh to eat?’ Jesus said to them, ‘very truly I tell you, unless you eat the flesh of the son of Man and drink his blood, you have no life in you.’”

681. ISUMBI LILI MU NDA.

Ulusumo lunulo, lwingilile ku mahoya ga bhageni na bhanikili kaya yiniyo. Uumo o bhanikili kaya agabhasumbila abhageni aliyomba, ‘makaribhu ng’wigashe mumasumbi.’ Uweyi agashosha, ‘umunhu adadulile gwigasha hisumbi ulu adina bhisagilwa bho gupandika jiliwa.’ Nang’hwe agashosha, ‘guli gonghana ubho nduhu jiliwa umu nda, ugwikala hoyi idinasolobho.’ Hunagwene abhanhu bhagandya guyuyomba giki, ‘isumbi lili mu nda.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatumamaga milimo na wisagilwa bho gupandika matwajo mingi, umuwikaji bhokwe. Umunhu adadulile gwita nimo uyo gudina solobho.

Isolobho yiniyo, bhuli wisagilwa ng’wa munhu uyo alizunya gwigasha hisumbi kunguno ya kumana igiki agupandikia jiliwa. Giko lulu, umunhu ulu ugaiwa ijiliwa, ihingi, agingaga haho na haho, kunguno adalazunya ugwigasha bho nduhu gulya aho kaya yiniyo. Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ubhukurasa 40.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Umunhu ng’wunuyo agatumamaga milimo yakwe bho bhukamu ubho bhudulile gumpandikila matwajo mingi, umuwikaji bhokwe, ayo gagikolanijiyagwa na jiliwa. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘isumbi lili mu nda.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kubhiza na wizagilwa bho gubhambilija ijinagongeja bhukamu bho gutumama milimo yabho chiza, kugiki bhadule kupandika matwajo mingi, umuwikaji bhobho.

Ijina moyo, dulidakilwa gwikala wikaji bho nyazunya aise bhazunya bha ng’wa Yesu Kristo, na gunondela weyi, bho gubhiza na bhisagilwa bhutale giki dulapandika bhupanga ubho bhudashilaga.

Ulu dubhiza dudina wisagilwa bho gupandika bhupanga ubho bhudashilaga, munho ugunondela gwise UYesu Kristo, gugubhiza gudina solobho, nulu nimo go bhule duhu. Kuti numo Untume Paulo aliyombela, ‘ulu Yesu Kristo adajukile, uguzunya gwise guli bhule.’

Ulu munhu agazunya gwiyumilija gwikala hizumbi, bho gwigasha ahisumbi linilo, ali na wisagiji bho gupandika jiliwa, nayise bhazunya igelelilwe gwiyumilija, guja kwikelesia, bhuli lushugu ulo Mfungo, kunguno dumanile igiki dugulwa Jiliwa na Sebha, na gulangwa Mhayo go ng’wa Mulungu, uyo gugailishaga imioyo yise.

Aliyo uwiza bho jizunya, (guti bhutumami ukubhangi, bhugubhiza bhulihoyi bhuying’wene, na bhutumami bho nduhu gulindila gulipwa) bhuli na solobho nhale gukila ulusumo ulo Jisuguma. Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa bho 40-41,

Yohane 6: 26-27.

Luka 2:25-32.

Marko 10:29-30.

2Timotheo 4:6-8.

KISWAHILI: KITI KIMO TUMBONI.

Methali hiyo ilianzia kwenye maongozi ya watu wageni na wanafamilia. Mmoja ya wanafamilia aliwakaribisha wageni akisema, ‘karibuni mketi kwenye kiti.’ Mmoja wa wageni alijibu, ‘mtu hawezi kuketi kitini isipokuwa ana tumaini la kupata chakula.’ Yeye akajibu, ‘ni kweli kiti bila chakula kwenye tumbo hakina maana.’ Ndiyo maana watu wakaanza kusema kwamba, ‘kiti kimo tumboni.’

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu anayefanya kazi kwa kutumaini kupata mafanikio mengi kwenye kazi yake hiyo. Mtu hawezi kufanya kazi bila kuwa na faida. Faida hiyo ni kama matumaini ya mtu anayekubali kuketi kwenye kiti kwa sababu ya kuelewa kwamba atapata chakula.

Hivyo mtu akikosa chakula huondoka mara moja kwa sababu hatakubali kukaa bila kula kwenye familia hiyo. Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 40.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Mtu huyo hufanya kazi zake kwa bidii ya kumwezesha kupata mafanikio yanayofananishwa na chakula. Ndiyo maana watu husemwa kwamba, ‘kiti kimo tumboni.’

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na matumaini ya kumwezesha kuongeza bidii katika kuyatekeleza vizuri majukumu yao, ili waweze kupata mafanikio ya kutosha kuyandesha vizuri maisha yao.

Kiroho, tunahitaji kuishi maisha ya Kikristo na kumfuata Yesu Kristo, kwa kuwa tuna tumaini la kwamba tutatunukiwa uzima wa milele. Ikiwa hatuna tumaini la kuupata uzima huo wa milele, kumfuata Yesu Kristo hakuna maana, au ni kazi bure tu. Kama Mtakatifu Paulo aliyosema, “ikiwa Yesu Kristo hakufufuka imani yetu ni bure.”

Kama mtu aliyekubali kuvumilia kukaa kitini kuwa ana tumaini la kupata chakula, ndiyo sisi waamini yatupata kuvumilia kwenda Kanisani kila Jumapili kwa sababu tuna hakika kwamba tutakula chakula cha Bwana, na kufundishwa Neno la Mungu linalotulisha mioyo yetu.

Lakini ubora wa ukristo (kama huduma kwa wengine, kutakuwa na ubinafsi na huduma bila kutumaini malipo) unaleta maana kubwa zaidi kuliko methali hii ya Kisukuma. Rejea Kueneza Injili Kwa Methali, ukurasa 40-41.

Yohane 6: 26-27. “Yesu akawajibu, “Amini, amini nawaambia, ninyi hamnitafuti kwa kuwa mliona ishara na miujiza, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba. Msishughulikie chakula kiharibikacho, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele, ambacho Mwana wa Adamu atawapa. Yeye ndiye ambaye Mungu Baba amemtia muhuri.’”

Luka 2:25-32. “Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake. Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.

Simeoni akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria, ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake  na kumsifu Mungu, akisema: “Bwana Mungu Mwenyezi, maana macho yangu yameuona wokovu    Wako,  ulioweka tayari machoni pa watu wote, nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu Mataifa na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.””

Marko 10:29-30. “Yesu akasema, “Amini, nawaambia, hakuna mtu ye yote aliyeacha nyumba, ndugu waume, au ndugu wake, mama, baba, watoto au mashamba kwa ajili Yangu na kwa ajili ya Injili, ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu, nyumba, ndugu waume, ndugu wake, mama, baba, watoto, mashamba pamoja na mateso kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao.”

2Timotheo 4:6-8. “Kwa maana mimi sasa ni tayari kumiminwa kama sadaka ya kinywaji, nayo saa yangu ya kuondoka imetimia. Nimevipiga vita vizuri, mashindano nimeyamaliza, imani nimelinda. Sasa nimewekewa taji ya haki ambayo Bwana, mwamuzi wa haki, atanitunukia siku ile, wala si mimi tu, bali pia wote ambao wamengoja kwa shauku kuja Kwake.”

 

chair1

marriage1

marriage

ENGLISH: A SEAT WITHOUT FOOD IS NOTHING.

This saying comes from the conversation between visitors and the host family. One of the family members welcomed the guests saying, ‘welcome and have a seat’ then the visitor replied saying that ‘a seat without food is nothing.’

The saying can be compared to a person who works with hopes to gain something in his/her work. One cannot work without knowing how much will he/she going to benefit from that work. That benefit is like the prospects that can make someone agree to sit on a chair. When a visitor doesn’t see any sign of getting food, he/she can leave the house (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 40.) This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

People can work hard in order to achieve food-related successes.

This saying teaches people about how to increase their efficiency in performing their tasks. This can make them to be successful in their lives.

Spiritually, we need to live the Christian life and follow Jesus Christ, for we have the hope of being blessed with eternal life. If we have no hope of attaining that eternal life, following Jesus Christ is useless, or even futile. As St. Paul puts it, “if Jesus Christ had not risen, our faith would be in vain.”

As someone who has agreed to stay in the chair having the hope of finding food, then we believers have endured going to church every Sunday because we are confident that we will eat the Lord’s Supper, and be taught the Word of God that warms our hearts.

But the quality of Christianity (as a service to others, it is special because it is a service without hope of reward) makes much more sense than this Sukuma proverb (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 40-41)

John 6: 26-27. Luke 2: 25-32. Mark 10: 29-30. 2Timothy 4: 6-8.

680. DESHI AKALEKA JULALA.

Deshi lili lina na noni iyo ikagalyaga miswa ijo jigitanagwa kidetemela mbula. Lushigu lumo, uDeshi agaja aha jigulu aha tuzengile utujidetemela mbula tunuto.

Aho oshika hoyi, agajibhona jilifuma imoimo umulipundu. Bhuli yene iyo yafumaga, UDeshi uyitulaga munomo. Agendelea gwita giko ku likanza lilihu. Iki imiswa jigendelea gufuma duhu kulikanza lilihu, UDeshi agiguta na guduma ugujimila, nose imiswa jigaikindika gung’wiyungulila na gubhita umumiso gakwe.

UDeshi agandya guhaya, “ingaji, nose muliningilila mumiso.” Agashoka na gujileka jilifuma. Hunagwene abhanhu bhagandya guyuyomba ulu bhalya jiliwa bhiguta na gujileka, giki, ‘Deshi agaleka julala.’

Intondo yahoo, UDeshi agaja hangi, mujigulu atubhile na ukunhu alimba. “itagi kiti igolo, itagi kiti igolo.” Ahikanza lya mhindi agimbaga giki, “Mukutudisha, mukutudisha.” Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 38.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagalyaga jiliwa mpaga bhiguta na guleka, umukikalile kabho. Abhanhu bhenabho, ulu bhalya mpaka bhiguta, bhagaluyombaga ulusumo lunulo guti nzila ya goyela gujilya ijijiwa jinijo, iki bhajidumaga ugujimala, giki, ‘Deshi agaleka julala.’

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gubhiza na jipimilo ja gwiyangula gujileka ijojabhalemelaga. Hangi, lobhalanga abhanhu bhenabho, gubhiza na wizang’holo bho gubhakaribhusha abhageni na gubhalila bho gubhinha jiliwa, kugiki abhanhu bhenabho, bhadule gulya na kupandika nguzu ja gwikomeja guminza chiza, umulugendo lobho.

Igelelilwe gubhitila yawiza abhigisu. Bhuli ikanza ilo dulibhitila ya wiza abhigizu, dugung’witilaga Yesu Kristo iya wiza yiniyo. UYesu obhitilaga yawiza abhanhu, umuwikaji bhokwe.

Ijinagongeja, ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya Ng’wa Yesu uyo agabhalishaga jiliwa, ijo jili mili na mininga gakwe, umu Isakramenti lya Ekaristi Nhagatifu.

Undimi untengeke agabhalishaga abhanhu jiliwa, bho gubhalanga Mhayo go Mulungu, uyo gugabhinhaga bhupanga. UYesu Kristo, hung’wene uyo ali ‘ha ng’wa Lutubhila gule.’ Ukwene huguhaya giki, ahali Uweyi bhagatubhilaga kule. Uyo agajaga kuli Weyi adubhona inzala. Uyo alinzunya Weyi, adiigwa inota gete. Rejea Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 39.

Isaya 25:6.

Ezekekieli 34: 1-2.

Marko 6:41-44.

Yohane 10:9-10.

Yakoko 2:15-17.

Luka 10:30-37.

Mathayo 25:31-46.

KISWAHILI: DESHI ALIAKA KUMBIKUMBI WAKARUKA.

Deshi ni jina la ndege ambaye hula jamii ya kumbikumbi wadogo (kidetemela mbula). Siku moja Deshi alikwenda kwenye kuchuguu (nyumba ya kidetemela mbula).

Alipofika hapo, alikuta kumbikumbi wanatoka mmoja mmoja shimoni. Kila kilichotoka Deshi alikiweka mdomoni. Akaendelea kufanya hivi kwa muda mrefu. Kwa vile waliendelea kutoka tu kwa muda mrefu, Deshi alishiba na kushindwa kuwameza, hata wakawa wanaruka kumzunguka na kupita machoni pake.

Deshi alianza kusema, ‘Ondokeni, mwishowe mtaniingia machoni.” Alirudi na kuwaacha kumbikumbi hao, wanatoka. Ndiyo maana watu wakaanza kusema wanaposhiba chakula na kukiacha, kwamba, ‘Deshi aliacha kumbikumbi wakaruka.”

Kesho yake, Deshi alikwenda tena kwenye kichuguu akiwa na njaa akiimba. “itagi kiti igolo, itagi kiti igolo” (fanyeni kama jana, fanyeni kama jana”). Wakati wa jioni huwa anaimba hivi, “Mukutudisha, mukutudisha” (mtatuingia machoni, mtatuingia machoni”). Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 38.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hulinganishwa kwa watu waliokula chakula mpaga wakashiba na kusaza, katika maisha yao. Watu hao, wanapokula mpaka kutosheka, huisema methali hiyo kama njia ya kuacha kula chakula, kwa vile wameshindwa kukimaliza, kwamba, ‘Deshi aliacha kumbikumbi wakaruka.’

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuwa na kiasi katika maisha, kwa maana ya kuamua kuacha kula chakula, baada ya kutosheka. Pia huwafundisha watu hao, kuwa na ukarimu wa kuwakaribisha wageni na kuwaandalia chakula, ili wageni hao waweze kula na kupata nguzu za kuwawezesha kuendelea vizuri na safari yao.

Yatupata kuwatendea wenzetu mema. Kila tunapomtendea mwenzetu mema tunamtendea mema Yesu Kristo. Kila tunapokosa kumtendea mwenzetu mema, tunakosa kumtendea Yesu Kristo mema hayo. Yesu alikuwa mtu aliyetenda wema kwa wengine.

Zaidi ya hayo, methali hiyo, yatufundisha juu ya Yesu Kristo anayetulisha na kutushibisha chakula, yaani mwili na damu yake katika Sakramenti ya Ekaristi Takatifu.

Mchungaji mwema huwalisha watu chakula, yaani huwafundisha neno la Mungu linalowapatia watu wokovu. Yesu Kristo ndiye “lutubhila kule,” yaani kwake njaa iko mbali. Anayekwenda kwake hataona njaa. Anayemwamini Yeye hataona kiu kamwe. Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 39.

Isaya 25:6. “Na katika mlima huu Bwana wa Majeshi atawafanyia mataifa yote karamu ya vitu vinono, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, karamu ya vinono vilivyojaa mafuta, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, iliyochujwa sana.”

Ezekekieli 34: 1-2. “Neno la Bwana likanijia kusema, mwanadamu, toa unabii juu ya wachungaji wa Israeli, toa unabii, uwaambie, naam hao wachungaji Bwana Mungu asema hivi, ole wao wachungaji wa Israeli wanaojilisha wenyewe. Je, wachungaji kuwalisha kondoo?”

Marko 6:41-44. “Kisha Yesu akatwa ile mikate mitano na wale sakaki wawili akatazama juu mbinguni akamshukuru Mungu, akaimeja mikate, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu na wale samaki wawili pia. Akawagawia wote, watu wote wakala wakashiba wakaokota mabaki ya mikate na samaki pia, wakaja vikapu kumi na viwili.”

Yohane 10:9-10. “Mimi ni mlango. Anayeingia kwa kupitia kwangu ataokolewa; ataingia na kutoka, na atapata malisho.”

Yakoko 2:15-17. “Tuseme kaka au dada hana nguo au chakula. Yafaa kitu gani ninyi kuwaambia hao: Nendeni salama, mkaote moto na kushiba bila kuwapatia mahitaji yao ya maisha?”

Luka 10:30-37. “Mfano wa Msamalia Mwema.”

Mathayo 25:31-46. “Hukumu ya Mwisho.”

bird eating insects

ants1

ants

 

ENGLISH: DESHI LEFT THEM TO FLY.

Deshi is the name of a bird that feeds on flying ants. One day deshi went to the anthill where flying ants live. When it got there, it found that the flying ants were coming out of their hole. What deshi did is setting its mouth closer to the entry of the hole so that the flying ants can enter straight into deshi’s mouth. It ate the flying ants to its satisfaction. Later on, because of satisfaction, the flying ants began flying around to surround deshi and, at this time, deshi had no any appetite to continue eating them. When the flying ants were doing so, deshi told them: “Get out, and finally you will enter our eyes.” He went back and left them, and they left to their hole. That is why people, when have eaten to their satisfaction, say “deshi left them to fly.”

The next day, deshi went back to the anthill while singing: “Itagi giti igolo, itagi git igolo” (do as you did yesterday, do as you did yesterday ). While the day before, it was singing “you will enter our eyes, you will enter our eyes” (Refer to Kueneza Injili kwa Methali’ which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 38). This book was written by researchers: Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

This proverb can be compared to greedy people who will tend to eat food to their satisfaction and later on begin to abuse it.

The proverb also teaches people to do good to fellows. Whenever we do good to one another, we do good to Jesus Christ. Whenever we fail to do good to one another, we fail to do good to Jesus Christ. Jesus was a man who did good to others.

Further, the proverb teaches us about Jesus Christ who nourishes and satisfies us with food, that is, his flesh and blood in the Sacrament of the Holy Eucharist.

The good shepherd feeds the people, that is, teaches them the word of God for salvation. In Jesus Christ hunger is far away. Whoever goes to Him will not be hungry. He who believes in Him will never feel thirsty (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 39).

Isaiah 25: 6. Ezekiel 34: 1-2. Mark 6: 41-44. John 10: 9-10. James 2: 15-17. Luke 10: 30-37. Matthew 25: 31-46.

679. HA NG’WA LUTUBHILA KULE.

Bhalihoyi bhanhu bhabhili abho bhalimugendo lo guja halebhe,  ukunhu bhalilomela. Aliyo abhanhu bhenabho, bhalibhatuubha noyi. Uumo obho agang’wila ung’wiye, ‘dugupandikila heyi ijiliwa?’ Ung’wiye agashosha, ‘dujage aha kaya iyaho.’ Nang’hwe agashosha, ‘nahene dujage.’

Aho bhashika aha kaya yiniyo, bhagazugilwa jiliwa ijo bhagajilya mpaga bhujileka. Uumo uyomba, ‘ulu uliha kaya yiniyo, udiyigwa nzala.’ Nu ng’wiye ushosha, ‘ng’hana, kunguno aho dali kule ni kaya yiniyi, dali dutubhile noyi.’ Hunagwene abhanhu bhagandya guyuyomba ulu kaya yubhazugila jiliwa ja gulya na gujileka, giki, ‘ha ng’wa lutubhila kule.’

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agabhabokelaga chiza abhageni na kubhalisha jiliwa bho wizang’holo.’ Giko lulu, ulu ulinang’hwe umunhu ung’unuyo, udutubha, kunguyo uweyi ali ‘ha ng’wa lutubhila kule.’ Rejea Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa bho 38.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kubhiza na wizang’holo bho gubhakaribhusha bhageni na kubhabhegeja jiliwa, kugiki bhadule gulya na kupandika nguzu ya gusimiza mpaga gushika uko bhajile, umulugendo lobho chiza.

Igelelilwe gubhitila yawiza abhigisu. Bhuli ikanza ilo dulibhitila ya wiza abhigizu, dugung’witilaga Yesu Kristo iya wiza yiniyo. UYesu obhitilaga yawiza abhanhu, umuwikaji bhokwe.

Ijinagongeja, ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya Ng’wa Yesu uyo agabhalishaga jiliwa, ijo jili mili na mininga gakwe, umu Isakramenti lya Ekaristi Nhagatifu.

Undimi untengeke agabhalishaga abhanhu jiliwa, bho gubhalanga Mhayo go Mulungu, uyo gugabhinhaga bhupanga. UYesu Kristo, hung’wene uyo ali ‘ha ng’wa Lutubhila gule.’ Ukwene huguhaya giki, ahali Uweyi bhagatubhilaga kule. Uyo agajaga kuli Weyi adubhona inzala. Uyo alinzunya Weyi, adiigwa inota gete. Rejea Kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 39.

Isaya 25:6.

Ezekekieli 34: 1-2.

Marko 6:41-44.

Yohane 10:9-10.

Yakoko 2:15-17.

Luka 10:30-37.

Mathayo 25:31-46.

KISWAHILI: KWAKE NJAA IKO MBALI.

Kulikuwa na watu wawili waliokuwa safarini kuelekea sehemu fulani. Lakini watu hao walijisikia njaa sana. Mmoja akamuuliza mwenzake, ‘tutapata wapi chakula?’ Mwenzake akajibu, twende kwenye familia ile pale.’ Naye akajibu, ‘sawa twende.’

Walipofika kwenye familia hiyo, walipikiwa chakula ambacho walikila mpaga wakatosheka na kukiacha. Mmoja akasema, ‘ukiwa kwenye familia hii, huwezi kujisikia njaa.’ Naye mwenzake akasema, ‘kweli kwa sababu tulipokuwa mbali na hapa tulijisikia njaa sana.’ Ndiyo maana watu wakaanza kusema kwenye familia ile waliokula chakula na kusaza kwamba, ‘kwake njaa iko mbali.’

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye anawapokea wageni na kuwalisha chakula kwa ukarimu. Hivyo ukiwa naye mtu huyo, huwezi kujisikia njaa, yaani ‘kwake nja iko mbali.’ Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 38.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo hufundisha watu juu ya kuwa na ukarimu wa kuwakaribisha wageni na kuwaandalia chakula, ili wageni hao waweze kula na kupata nguzu za kuwawezesha kuendelea na safari yao vizuri.

Yatupata kuwatendea wenzetu mema. Kila tunapomtendea mwenzetu mema tunamtendea mema Yesu Kristo. Kila tunapokosa kumtendea mwenzetu mema, tunakosa kumtendea Yesu Kristo mema hayo. Yesu alikuwa mtu aliyetenda wema kwa wengine.

Zaidi ya hayo, methali hiyo, yatufundisha juu ya Yesu Kristo anayetulisha na kutushibisha chakula, yaani mwili na damu yake katika Sakramenti ya Ekaristi Takatifu.

Mchungaji mwema huwalisha watu chakula, yaani huwafundisha neno la Mungu linalowapatia watu wokovu. Yesu Kristo ndiye “lutubhila kule,” yaani kwake njaa iko mbali. Anayekwenda kwake hataona njaa. Anayemwamini Yeye hataona kiu kamwe. Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 39.

Isaya 25:6. “Na katika mlima huu Bwana wa Majeshi atawafanyia mataifa yote karamu ya vitu vinono, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, karamu ya vinono vilivyojaa mafuta, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, iliyochujwa sana.”

Ezekekieli 34: 1-2. “Neno la Bwana likanijia kusema, mwanadamu, toa unabii juu ya wachungaji wa Israeli, toa unabii, uwaambie, naam hao wachungaji Bwana Mungu asema hivi, ole wao wachungaji wa Israeli wanaojilisha wenyewe. Je, wachungaji kuwalisha kondoo?”

Marko 6:41-44. “Kisha Yesu akatwa ile mikate mitano na wale sakaki wawili akatazama juu mbinguni akamshukuru Mungu, akaimeja mikate, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu na wale samaki wawili pia. Akawagawia wote, watu wote wakala wakashiba wakaokota mabaki ya mikate na samaki pia, wakaja vikapu kumi na viwili.”

Yohane 10:9-10. “Mimi ni mlango. Anayeingia kwa kupitia kwangu ataokolewa; ataingia na kutoka, na atapata malisho.”

Yakoko 2:15-17. “Tuseme kaka au dada hana nguo au chakula. Yafaa kitu gani ninyi kuwaambia hao: Nendeni salama, mkaote moto na kushiba bila kuwapatia mahitaji yao ya maisha?”

Luka 10:30-37. “Mfano wa Msamalia Mwema.”

Mathayo 25:31-46. “Hukumu ya Mwisho.”

rich one

cow2

 

ENGLISH: IN THIS FAMILY YOU CANNOT SUFFER FROM HUNGER.

There were two people traveling to a certain place. It reached a point when these two travelers felt hungry and they were in need of food. One of them asked the other, ‘Where can we get food?’ The other replied, let’s go to the family over there. ‘ When they arrived at that particular family, they were given food and ate to their satisfaction. After eating, the travellers said that, in ‘this family you cannot suffer from hunger.’

This saying can be compared to a kind person who welcomes others during needy times. This person is generous enough to others and he/she would not like seeing others suffer because of lacking something in life (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 38). This book was written by Fr. Donald Sybertz, M.M., and Fr. Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

The saying teaches people about the generosity and hospitality. People have to be kind to others in their lives. When we do good to others it means we are doing good to Jesus Christ. Whenever we fail to do good to one another, we fail to do good to Jesus Christ. Jesus was a man who did good to others.

Furthermore, the saying teaches us about Jesus Christ who nourishes and satisfies us with food, that is, his flesh and blood in the Sacrament of the Holy Eucharist.

The good shepherd feeds the people, that is, teaches them the word of God for salvation. In Jesus Christ there is no hunger. Whoever goes to Him will not be hungry. He who believes in Him will never feel thirsty (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 39).

Isaiah 25: 6. Ezekiel 34: 1-2. Mark 6: 41-44. John 10: 9-10. James 2: 15-17. Luke 10: 30-37. Matthew 25: 31-46.

678. NZONELI YABHULIGA NG’WAGALA. NULU, BHALEKAGI BHAKWILE AGABHENHELEJA ABHANA NG’WAGALA GUKINDWA.

Aho kale olihoyi nkima umo nsuguma, agatolwa na Mmasai. Unkuluye o nkima ng’wunuyo, alintemi o Ng’wagala. UNtemi ng’wunuyo, agang’winha uilumbuye, ng’ombe ja guja najo.

Ing’ombe jinijo, jigandya guyibyala noyi. Aha nghalikilo, igiza nzala iyo igajibhulaga pye ing’ombe jinijo, kunguno ya gugahiwa maswa. Abhana wa jimasai bhagizuka guja kuli mami obho. Bhagayomba, “dudizucha na nzala. Ilihambohambo duje kuli mami, kunguno isabho ijo alinajo umami jilijise.” (jise na Mami, Ishilina mami shise.”

Aho bhashiga ukulima mami obho, bhagang’wila giki, “Ing’ombe jashilile, dugabhilage hangi jingi mami.” Umami obho ulina bhana abho bhagalema bhaliyomba, “mudinhiwa hangi.” Bhubhuja, “Ni bhuli dudizinhiwa hangi?” Bhushokejiwa, “Ijo ng’winhiwa igwandya ditoshije, mududula gulomba igele lingi hangi. Ulu mulibhona giki mugucha na nzala ili hambohambo gwikala na yise.”

Abhipwa bha Ntemi bhagabhashokeja abhana bha Ntemi, “Ni bhuli mulidulemeja, ninga jili jing’we bhung’wene nayi? Ing’ombe ja henaha jili ja ng’wa mami, jidi jing’we; huna guhaya ija ng’wa mami, jili jise.” (Sha ng’wa mami shise).

Bhendelea gulema giki bhadujichala. “Kunguno muliyomba jili jing’we na mami wing’we, gemagi ugujitula ulu ning’we muli bhagosha ng’hana.” Abhoyi bhagashosha, “Ilelo dudina mhayo, dugujizila lushugu lungi.”

Aho jabhita shigu ningi bhagigela bhamulani bhabhili bha jimasai bhalipela, bhubhegela abhana Ng’wagala, bhubhakanga gubhachima machimu. Abhanhu wa Ng’wagala bhunchalila imhola untali obho uobhulugu. Bhagamuja, “Dubhatule masonga?” Uweyi agabhadalaha ubhalemeja, aliwawila, “bhalekagi bhakwile tamu, bhakwilikanike (b’izonele).”

Abhamulani bhajimasai bhagita giko nhangala idatu, untali o bhulugu uo Ng’wagala omanaga ubhadalaha abhamasai na gubhawila abhanhu bhakwe, “bhalekagi bhakwilikanike.”

Ulukangala ulo kane, bhagiza bhamasai pye bhandya bhulugu limo na limo. Abhamasai bhagabhalemela abhanhu bha Ng’wagala umubhulugu bhunubho, na gujisola pye ing’ombe. Bhaganekelela ng’ombe ngehu duhu, umami obho ja gulya, bhaliyomba, “ulu nioli nduhu umami nidudalekelile nulu ingehu jinijo.”

Giko lulu, gwingile ikanza linilo mpaga lelo abhanhu ulu bhumala amakubhi, lulu masangu, mandege nulu numbu, bhagayombaga, “Nzoneli” nulu “yabhulaga Ng’wagala.” Ukwene huguhaya giki, dongejaji, dudiniguta. Ulu nkima uyomba giki, gashilaga amakubhi, hamo ung’winikili kaya adulile guyomba giki, “Andi nagula makubhi mingi, gajaga heyi pye agose?”

Ikale inzoneli igabhulaga Ng’wagala, aliyo ilelo idulile gubhulaga kaya. Hunagwene abhanhu bhagandya guyuyomba giki, ‘Nzoneli yabhulaga Ng’wagala.’ Lolaga Kueneza Injili kwa Methali, ubhukurasa bho 31-32.

Ijitabho jinijo jigandikwa na bhakengeji bha: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na guchapishiwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagiyibhaga ugubhalela gwingila habhudoni abhana bhabho, nose bhagadumaga ugubhalela, nulu ugubhakuja chiza, umuwikaji bhobho.

Abhanhu abha bhalihaya gwita nimo nhebhe, wadakililwe gwanguha ugugwita unimo gunuyo, kutinda ugulindila ikanza lingi mpaga nose lyubhita ilikanza ilo lililyawiza ilya gugutumama na gugumala chiza unimo gobho.

Abhabyaji bhadakililwe kubhalanga ikujo abhanhu bhabho, gwingila haho bhatale bhadoo. Bhadizulindila mpaga bhabhize matale, kunguno gugubhiza guti nimo gunogu ukubhoyi. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘Nzoneli yabhulaga Ng’wagala.’ Lolaga kueneza Injili kwa Methali, ubhukurasa bho 32.

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya guitumama wangu imilimo yabho gwandija hayo wandijo bhoyo mpaka guimala chiza, umuwikaji bhobho, kugiki bhadule kupandika matwajo mingi, umukikalile kabho.

Ukulwande ulo Ekaristia, inzoneli ili na bhulingisilo bho gulya jiliwa ja Ng’wa Sebha nhangala ningi, kugiki tupandika nema ya bhukindi. Bhugadukamilishaga na gudugalucha dubhize guti Sebha wise Yesu Kristo.

UMu sala iyo odulanga UYesu Kristo, dulisalila, “Uding’hage ilelo ijiliwa jise ijo dulijilomba.” Dulilomba jiliwa ja Ng’wa Sebha bhuli likanza kugiki dupandika gushikanyiwa, idalingisilile gubokela Ubhukaresitia kamo duhu ukung’waka. Igelelilwe kulomba “nzoneli,” ukwene huguhaya, gulya mili gokwe nhangala ningi umo ilidulikanila.

Untali o bhulugu agigimba na kubhadalaha abhamasai, kunguno bhalibhagehu. Aha nhalikilo, abhana Ng’wagala bhagakindwa. Ugwigimba na bubhadalaha abhangi mpaga nu Mulungu Ng’winikili, bhuli wandijo wa shipi. UMulungu agabhichaga abho bhali na nhinda, na kubhaling’ha abhidohya. UYesu Kristo, agidohya. Kunguno yiniyo, UMulungu aganhinhya higulya gete. Ung’winha ilina ilo lilitale gukila pye amina.

Untongeji o Ng’wagala ulu niobhapeja aha lukangala ulo gwandya abhamasai, gukila gubhalindila bhakwile, abhanhu bha Ng’wagala ni bhabhukinda ubhulugu bhunubho.

Kuyiniyo lulu, UMulungu alihaya gudupija ihaha yiniyi. Dudizubhiza na mioyo midimu, dudizulindila mpaka ikanza libhite, kunguno ilikanza ili, ni lya bhupiji. Lolaga kueneza Injili kwa Methali, bhukurasa 32-33.

1Samweli 17:42-43.

Luka 19:44.

2 Wakorintho 6:2.

KISWAHILI: NYONGELA ILIUA NG’WAGALA.

AU WAACHENI WAONGEZEKE, ILIWAFANYA WATU WA NG’WAGALA WASHINDWE.

Hapo zamani mwanamke mmoja Msukuma aliolewa na Mmasai. Kaka yake, mwanamke huyo, alikuwa mtemi wa Ng’wagala. Mtemi huyo alimpa dada yake ng’ombe akaenda nao.

Ng’ombe wale aliopewa dada huyo wakazaana sana. Mwishowe, ilitokea njaa, na ng’ombe wote walikufa kwa kukosa majani.  Watoto wa Kimasai walikumbuka kwenda kwa mjomba wao. Wakasema; “Tusije tukafa na njaa. Afadhali twende kwa mjomba, maana mali alizo nazo mjomba ni zetu pia.” (Shise na Mami, Ishilina Mami shise).

Walipofika kwa mjomba wao wakamwambia, “Ng’ombe wamekwisha, utugawie tena wengine, Mjomba.” Lakini watoto wa mjomba wao walipinga ombi hilo, wakasema, “Hamtapewa tena.” Wakauliza, “Kwa nini tusipewe tena?” Wakajibiwa, “Wale mliopewa mara ya kwanza wanatosha, hamwezi kuomba fungu jingine tena. Kama mmeona mtakufa  na njaa ni vema kukaa nasi.”

Wapwa wa mtemi wakawajibu watoto wa mtemi, “Mbona mnazikataza, kwani ni zenu peke yenu? Ng’ombe za hapa ni za mjomba siyo zenu; ndiyo kusema za mjomba ni zetu.” (Sha ng’wa mami shise).

Wakaendelea kukataa kwamba hawatawapeleka. “Kwa sababu mnasema ni zenu na mjomba wenu. Jaribuni kuwaswaga kama ninyi ni wanaume kweli.” Basi, wakajibu, “Kwa leo hatuna neno, tutazijia siku nyingine.”

Baada ya siku si nyingi wakatokea Morani wawili wa Kimasai wakikimbia, wakawakaribia watu wa Ng’wagala, wakawatisha kuwachoma mikuki. Watu wa Ng’wagala wakampa taarifa mkubwa wao wa vita. Wakamuuliza, “Je, tuwapige mishale?” Naye aliwadharau akawakataza, akiwaambia, “Waacheni kwanza, waongezeke (b’izonele).”

Morani wa Kimasai walifanya hivyo mara tatu, mkubwa wa vita wa Ng’wagala akazidi kuwadharau waMasai hao, na kuwaambia watu wake. “Waacheni, weaongezeke.”

Kwa mara ya nne wakaja wamasai wote wakaanza mara moja vita. Wamasai hao, wakawalemea watu wa Ng’wagala katika vita hiyo na kuziteka nyara ng’ombe zote. Wakamwachia mjomba wao ng’ombe chache tu za kula, wakisema, “Kama mjomba asingekuwa hai tusingewaachia hata hizo chache.”

Hivyo, kutoka wakati ule mpaka leo watu wakimaliza mboga, au makande, au mahindi au viazi husema, “Nyongeza.” (Nzoneli) au “Iliua Ng’wagala” (yabhulaga Ng’wagala), yaani ndiyo kusema, tuongezeeni, hatujashiba. Kama mwanamke akisema kwamba mboga zimekwisha, pengine mwenye nyumba anaweza kukasirika, “Mbona nilinunua mboga nyingi, zimekwisha zote?”

Zamani nyongeza iliua Ng’wagala, lakini leo inaweza kuvunja mji. Ndiyo maana watu wakaanza kusema, ‘Nyongeza iliua Ng’wagala.’ Rejea Kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 31-32.

Kitabu hicho, kiliandikwa na watafiti ambao ni: Padri Donald Sybertz, M.M., na Padri Joseph Healey M.M., na kuchapishwa na Benedictine Pubhications Ndanda – Peramiho, 1984.

Methali hiyo, hulinganishwa kwa watu wale wanaojisahau kuwalea watoto wao mapema, mwishowe watoto hao hufikia hatua ya kushindikana kulelewa, maishani mwao.

Watu wanaotaka kufanya jambo fulani, wanatakiwa kuliwahi mapema, wasingojee muda huo mwafaka upite, wasije wakashindwa kama walivyoshindwa watu wa Ng’wagala, kwa sababu ya kungojea wakati huo, unaofaa mpaka ukapita.

Wazazi kwa mfano, wanatakiwa kuwafundisha adabu watoto wao tangu wakiwa wadogo. Wasingojee mpaka wamekuwa wakubwa, maana itakuwa si kazi rahisi kwao. Ndiyo maana watu walisema, ‘nyongeza iliua Ng’wagala.’ Rejea Kueneza Injili kwa  Methali, ukurasa 32.

Methali hiyo, hufundidha watu juu ya kuyatekeleza majukumu yao kwa kufanya maandalizi mapema, kuanzia mwanzoni kabla hawajachelewa, katika maisha yao, ili waweze kupata mafanikio mengi, maishani mwao.

Kwa upande wa Ekaristi, nyongeza kuna maana ya kusema kula chakula cha Bwana kila mara kunatupa neema ya ushindi. Kunatukamilisha na kutugeuza kuwa kama Bwana wetu Yesu Kristo.

Katika sala aliyotufundisha Yesu Kristo, tunasali, “Utupe leo chakula chetu tunachohitaji.” Tunahitaji chakula cha Bwana kila wakati tupate kukamilika, haina maana ya Ekaristi mara moja tu kwa mwaka. Bali yatupasa kusema “nyongeza”, yaani, kula mwili wake mara nyingi kama iwezekanavyo.

Mkubwa wa vita alijivuna na kuwadharau wamasai kwa sababu walikuwa wachache. Mwishowe watu wa Ng’wagala wakashindwa. Kujivuna na kuwadharau wengine hata kumdharau Mungu mwenyewe, ni chanzo cha dhambi.

Mungu huwashusha wenye kiburi na kuwakweza wanyenyekevu. Yesu Kristo, alijinyenyekeza. Kwa sababu hiyo Mungu alimkweza juu kabisa. Akampa jina lililo kuu zaidi kuliko majina yote.

Kiongozi wa Ng’wagala angaliwafukuza wamasai mara moja, badala ya kungoja waongezeke, watu wa Ng’wagala hawangelishinda vita hiyo.

Kwa hiyo, Mungu anataka kutuokoa sasa hivi. Tusiwe na mioyo migumu na tusingojee mpaka wakati umepita, kwa sababu wakati hu ndio wakati wa wokovu. Rejea kueneza Injili kwa Methali, ukurasa 32-33.

1Samweli 17:42-43. “Hata Mfilisti alipomtazama huku na huku, akamwona Daudi, akamdharau, kwa kuwa ni kijana tu, mwekundu, tena ana sura nzuri. Mfilisti akamwambia Daudi, Je, mimi ni mbwa hata umenijia kwa fimbo? Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake.”

Marko 6:3. “Je, huyu si yule seremala Mwana wa Maria, na ndugu zake akina Yakobo, Yosefu, Yuda na Simoni? Je, dada zake si wanaishi hapa hapa kwetu?” Basi, wakawa na mashaka naye.”

Luka 19:44. “Watakuangamiza wewe na watoto wako, hawatakuachia hata jiwe likisimama juu ya jiwe jingine, kwa sababu hukuutambua ule wakati wa Mungu alipokujia kukuokoa.”

2Wakorintho 6:2. “Basi, sasa ndio wakati wa kufaa, sasa ndiyo siku ya wokovu!”

king-arthur-

masai2

masai1

nsabhi masai

 

ENGLISH: ADDITION KILLED NG’WALAGALA PEOPLE.

In the past, a sukuma woman married a maasai man. The brother of this woman was Ng’wagala’s Chief. When this woman was leaving for he husband, her brother gave her a cow as his present to her. This cow multiplied in numbers to the extent of having many cows in her shed. When famine attacked the village where the woman and her maasai husband live, all their cows died for lacking food, grass and therefore they ran out of cow. Seeing that they no longer have cows, the children of this women went back to their uncle seeking help to get some other cows. They said; “Lest we die of hunger. We should go to our uncle, because the property he owns is ours too. ”

When they arrived at their uncle’s place , they said to him, “The cows are gone. Give us some more others, Uncle.” But their uncle’s children opposed the request, saying, “You will not be given again.” They asked, “Why don’t we have them again?” They were answered, “Those first given are enough, you cannot ask for more cows. If you think of dying of hunger in your place, you better come and stay with us. ”

The children of the maasai asked the children of their uncle (the chief) , “Why do you refuse them? The cows here are uncle’s not yours and the uncle’s cows are ours too”.

They kept on refusing that they would not take them. They told them that if they believe that they have a share in those cows let them force to take, if they are really men. The maasai boys ended up saying that “Today we have no word, we will come again another day.”

After a few days, two maasai Morans arrived at Ng’wagala’s place and approached the Ng’wagala people and threatened to pierce them with spears. The people of Ng’wagala people gave their chief a report on their arrival. They asked their chief, “Shall we shoot them?” The chief refused from having any reaction to the masai men. The chief said, they are still very few, let them mobilize themselves into a bigger number.

The maasai Morans went back and increased the number of warriers three times. But when they came back to fight with Ng’wagala, he again told them to go back and mobilize because their number is not good enough to fight with the Ng’wagala chief.

Later, the maasai warriers came, fully equipped and they started the war against the Ng’wagala chief. The maasai warriers managed to defeat the Ng’wagala chief and captured all his cows. They left their uncle with only few cows for meat but the rest were taken to maasai land. Thus, from that time until today people tend to finish whatever they are doing or having fear that it might increase in number thus causing some more difficulties. They hold the saying that ‘addition killed Ng’wagala.’

In the past the addition killed Ng’wagala, but today it could break the family. That is why people began to say, ‘addition killed Ng’wagala’ (Refer to Kueneza Injili kwa Methali which means ‘Spreading the Gospel through Proverbs,’ page 31-32). This book was written by Dr. Donald Sybertz, M.M., and Joseph Healey M.M., and published by Benedictine Publications, Ndanda – Peramiho, 1984.

This saying can be compared to those who forget to bring up their children. Parents should not wait until they are older, for it will not be an easy task for them. That is why people said, ‘addition killed Ng’wagala’ (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 32). Failure to nurture children from their earlier stages can result into their failure in life. People need to go with time by using given opportunities effectively.

The proverb teaches people how to carry out their responsibilities by preparing well in advance, from the very beginning before it is too late. In so doing, they can achieve more in their lives.

For the Eucharist, in addition, it means that eating the Lord’s Supper always gives us the grace of victory. It completes and transforms us into the likeness of our Lord Jesus Christ.

In the prayer that Jesus Christ taught us, we pray, “Give us today our daily bread.” We need the Lord’s Supper every time we are to be complete, it does not mean eating the Eucharist only once a year. But we have to say “addition”, that is, eat His body as often as possible.

The great warrior boasted and despised the Maasai because they were few. Eventually, the Ng’wagala people were defeated. Pride and disrespect for others, even blaspheming God, is the source of sin.

God humbles whoever exalts himself and exalts whoever humbles himself. Jesus Christ was humble. For this reason, God exalted Him to the highest. He gave Him a name that was greater than any other name.

To win the war, the Ng’wagala leader was to immediately dismiss the maasai instead of waiting for the maasai warriers to increase in number.

So, God wants to save us right now. Let us not be stubborn and not wait until time has passed because this is the time of salvation (Refer to ‘Spreading the Gospel in Proverbs,’ page 32-33).

1Samuel 17:42-43. Luke19:44. 2 Corinthians 6:2