Sukuma Proverbs

752. GUB´ISA GO NVA GUGAFUMBULAGWA NG`HUNGULU.

Ulusumo lunulo, lulihoyela higulya ya masala ga nva ayo gagafumbulagwa na ng’hungulu. Inva ili na masala ayo gagikolaga hadoni na ga bhanhu kunguno igabhisaga inyama ulu uyisaga. Ulu yukuga nyama yulwa yiguta mpaga yuyisaja, igajagub´isa hanhu kugiki ilize yilwe hangi ulu yutubha.

Ing´hungulu nayo ili noni iyo ili na masala gagupadija aho yabhiyisilaga inva inyama yiniyo. Gashinaga lulu, ulu ub´isa umuna mva iyoyi igajaga yaginjaho yalila ha ng´wape, aho bhadulile nulu bhanhu bhuyibhona na gudebha igiki inva yaliyabhisa nyama. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “gub´isa go nva gugafumbulagwa ng`hungulu.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agitaga ginhu bho gwibhisa ijo jigamanyikaga aha numa yaho. Umunhu ung’wunuyo, alina nhungwa ja wiminholo ukubhiye, ijo jigampondaga soni ulu bhandebha bhiye. Uweyi agiganikaga giki alibhakelela abhangi aliyo gashinaga bhayidebhile iyo agiyitaga.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nhi nhungwa ja nva ija gubhisa nyama iyo igafumbulagwa na ng’hungulu, kunguno nuweyi agabhisaga ginhu ijo jigampondaga soni ulu jagiza kumanyika ukubhiye. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “gub´isa go nva gugafumbulagwa ng`hungulu.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kuleka nhungwa ja wiminholo umuwikaji bhobho, kugiki bhadule gwiyambilija chiza umubhutumami bho milimo yabho. Igelelilwe bhiyambilije kihamo umukikalile kabho, kugiki bhadule kupandika matwajo ga gujibheja chiza ikaya jabho.

Warumi 2:16.

1Wakorintho 14:25.

KISWAHILI: KUFICHA KWA MBWA HULIFICHULIWA KUNGULU.

Methali hiyo, huongelea juu ya  akili za mbwa ambazo hufichuliwa na kungulu. Mbwa ana akili ambayo hufanana kidogo na ile ya wanadamu kwa sababu yeye huficha  nyama anayoisaza. Hivyo, akiokota nyama na kuila mpaka akaisaza, huificha sehemu ili aje aile tena baadaye akijisikia njaa.

Kungulu naye ni ndege mwenye akili za kugundua pale alipoyificha mbwa yule ile nyama. Kumbe basi, mbwa akificha yenyewe huenda kuichukua ile nyama na na kuanza kuila mahali pa wazi. Ndiyo maana watu husema kwamba, “kuficha kwa mbwa hufichuliwa na kungulu.”

Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hutenda jambo fulani kwa kujificha ambalo hujulikana baadaye kwa wale aliowaficha. Mtu huyo, ana tabia ya uchoyo kwa wenzake, ambayo humfedhehesha kutokana na aibu anayoipata mbele ya wenzake baadaye siri yake kujulikana. Yeye hufikiri kwamba anawazidi ujanja wengine kumbe wanakielewa kile anachokifanya.

Mtu huyo, hufanana na akili ya mbwa ya kuficha nyama ambao ilifichuliwa na kungulu, kwa sababu naye huficha jambo fulani ambalo humuaibisha baada ya kujulikana kwa wenzake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “kuficha kwa mbwa hufichuliwa na kungulu.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuacha tabia ya uchoyo maishani mwao, ili waweze kusaidiana vizuri katika utekelezaji wa kazi zao. Wanatakiwa kuwa  na ushirikiano wa pamoja katika kutekeleza majukumu yao ili waweze kupata mafanikio ya kuziendeleza vizuri familia zao.

Warumi 2:16. “Hili litatukia siku hiyo Mungu atakapozihukumu siri za mioyo ya wanadamu kwa njia ya Yesu Kristo, kama isemavyo Injili yangu.”

1Wakorintho 14:25. “nazo siri za moyo wake zitawekwa wazi. Kwa hiyo ataanguka chini na kumwabudu Mungu akikiri, “Kweli Mungu yuko katikati yenu!””

crow kunguru

crow kunguru raven-

dog4

crow kunguru raven-1

ENGLISH: WHAT HAS BEEN HIDDEN BY A DOG IS USUALLY UNCOVERED BY A CROW.

This proverb, speaks of the minds of dogs that are exposed by crows. The dog has a mind that is a little similar to that of human beings because it hides the meat in leaves. So, when it picks up the meat and eats it, it hides the part of it so that it can eat again later when it is hungry.

The crow is also a clever bird that discovered where the dog had hidden the meat. However, a crow can take the meat and begin to eat it in an open area. That is why people say that “What has been hidden by the dog is revealed by a crow.”

The proverb above is likened with a man who does something secretly, but which latter on is known to those it had hidden been hidden from. Such person, however, has a greedy attitude toward his colleagues, which humiliates him due to the embarrassment he gets in front of his colleagues later when his secret is known. He thinks he is better than others, but they understand what he is doing.

Such man is like the dog that hid meat which, was exposed by the crow, because he too hides something that embarrasses him after it is known by his peers. That is why people tell him that, “what has been hidden by a dog is usually uncovered by a crow.”

This proverb teaches people about giving up habits of greed in their lives, so that they can help each other better in the execution of their duties. They need to be co-operative in carrying out their responsibilities so that they can achieve success for the good of their families.

Romans 2:16.

1Corinthians 14:25.

751. B´UB´I BHO JISINZA B´UDI BHO NSUJI.

Ulusumo lunulo lwingine kuli munhu uyo abhejaga jisinza. Ijisinza jinijo jidulile gubhiza jawiza nulu ja bhibhu, aluweyi agasaga mumo ali, kunguno adadulile ugwikola nhi chuma ijo ojibhejaga. Ulu jubhiza jibhi ijisinza, munho jilichene bho joyi idi giki uyo ojibheje ali ob’ub’i. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “b’ub’i bho jisinza b’udi bho nsuji.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agapandikaga ginhu jawiza ojikenagula, nulu uyo agapandikaga bhanhu bhawiza, aliyo uweyi agadumaga ugubhalangaha, umukikalile kakwe.

Umunhu ng’wunuyo, agajikenagulaga sagala ijikolo ijawiza kunguno ya nhungwa jakwe ijo jidijawiza. Uweyi hangi agabhapejaga abhanhu abho agikalaga nabho kunguno ya gubhitila ibhengwe abhanhu bhenabho.

 Abhanhu bhagang’wikolanijaga nu nsuji o jisinza uyo agajibheja chiza jasaja na b’ub’i bhojo duhu, kunguno nuweyi agapandikaga bhanhu abho bhalibhawiza, oduma ugwikala nabho chiza iki nhungwa jakwe jili jabhubhi. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “b’ub’i bho jisinza b’udi bho nsuji.”

Ulusumo lunulo lolanga bhanhu higulya ya gudebha gwikala na bhanhu bho gwiyambilija nabho, umukikalile kabho, kugiki bhadule gwikala bho mholele na bhanhu bhabho. Igelelilwe bhilange ugwitongela, bho gujilang’hana ijo bhali najo.

Mathayo 19:12.

KISWAHILI: UBAYA WA CHUMA SIO WA MTENGENEZAJI.

Methali hiyo, ilianzia kwa mtu yule aliyekuwa akitengeneza chuma. Chuma hicho, chaweza kuwa kizuri au kibaya, lakini yeye hubaki kama alivyo, kwa sababu hawezi kufanana na kile alichokitengeneza. Kikiwa kibaya maana yake kipo hivyo chenyewe, siyo kwamba mtengenezaji wake ni mbaya. Ndiyo maana watu husema kwamba, “ubaya wa chuma sio wa mtengenezaji.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hupata vitu vizuri, lakini hushindwa kuvitunza, kwa sababu ya uzembe au kutoelewa namna ya kuvitumia vizuri.  Hivyo yeye pia hupata watu wema lakini hushindwa kuishi nao kwa sababu ya tabia mbaya aliyo nayo, katika maisha yake.

Mtu huyo, hushindwa kuvitunza vitu vyake, kutokana na mwenendo wake wa kuviharibu kwenye matumizi yasiyofaa. Yeye pia, huwavuruga watu anaoishi nao kwa sababu ya tabia yake ya kuwadharau wenzake.

Watu humfananisha na mtu yule aliyekuwa akitengeneza chuma ambacho hubaki na ubaya wa chenyewe, siyo wake mtengenezaji, kwa sababu naye huwapata watu wenye tabia njema, lakini hushindwa kuishi nao vizuri. Ndio maana watu humwambia kwamba, “ubaya wa chuma sio wa mtengenezaji.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuelewa namna ya kuishi na watu kwa kusaidiana vizuri katika maisha yao, ili waweze kujiletea maendeleo mengi maishani mwao. Wanatakiwa kujifunza namna ya kuishi kwa kuongozana na watu wao.

Mathayo 19:12. “Kwa maana wengine ni matoashi kwa sababu wamezaliwa hivyo, wengine wamefanywa matoashi na wanadamu na wengine wamejifanya matoashi kwa ajili ya Ufalme wa Mbinguni. Yeye awezaye kulipokea neno hili na alipokee.”

craftsman iron

hot-iron-

hammer iron

ENGLISH: THE USELESSNESS OF AN IRON SHOULD NOT BE BLAMED ON THE MANUFACTURER.

This proverb began with the man who was manufacturing irons. The manufactured iron may be good or bad, but the manufacturer remains as he is, because he cannot match what he made. If the manufactured iron is bad that means it is so in its own right not that its manufacturer is bad. That is why people say, “The uselessness of an iron should not be blamed on the manufacturer.”

The proverb is likened with a person who finds good things, but fails to take care of them, because of negligence or a lack of understanding on how to use them properly. So he also finds good people but fails to live with them because of the bad behaviour he has.

That person as result fails to take care of his or her belongings, due to his or her tendency to waste them due to his improper usage. He, too, disturbs the people he lives with because of his contemptuous behaviour.

People liken him with a man who used to make irons, this is because he also finds people with good character, but he fails to live well with them. That is why people say to him, “The uselessness of an iron should not be blamed on the manufacturer.”

This proverb teaches people how to understand ways of living with people by helping each other well in their lives so as to progress in their lives. They need to learn how to live in harmony with their people.

Matthew 19:12.

 

750. UBHIPE B´EB`E NTOJI, NTOLWA ATI NA MHAYO.

Ulusumo lunulo lwingine kuli munhu uyo ocholaga nhola. Uweyi omanaga uja agubhuja kubhanhu kugiki bhang’olekeja unkima uyo ali owiza. Umunhu ng’wunuyo abhabhujaga bhanhu, “ali ng’wanani unkima uyo aliowiza nagantole umuchalo jiniji?” Munhu umo aganshokeja, “alihoyi akaya iyaho.” Uweyi agabhuja hangi, “unkima ng’wunuyo alina nhungwa jawiza ahene?” Abhiye bhung’wila, “ubhipe b’eb’e ntoji, ntolwa ati na mihayo.”

Ulusumo lunulo, lugelenganijiyagwa kuli munhu uyo agapandikaga ginhu jawiza ojikenagula, nulu uyo agapandikaga bhanhu bhawiza, aliyo uweyi adamanile ugubhalangaha abhanhu bhakwe bhenabho, umukikalile kakwe.

Umunhu ng’wunuyo, agajikenagulaga sagala ijikolo ijawiza kunguno ya nhungwa jakwe ijo jidijawiza. Uweyi hangi agabhasalambanyaga abhanhu abho agikalaga nabho, kunguno ya gubhitila ibhengwe umukikalile kakwe.

 Abhanhu bhagang’wikolanijaga nuyo ocholaga kutola umpandika unkima uowiza, bhusaga ubhubhi gwigela kuliweyi duhu, kunguno nuweyi agapandika bhanhu abho bhalibhawiza, obhasambaja kubhitila ku nhungwa jakwe ijo jili jabhubhi. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “ubhipe b’eb’e ntoji ntolwa ati na mhayo.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gub’iza na nhungwa ja bhutogwa bho gubhambilija gwikala chiza na bhanhu, umukaya jabho, kugiki bhadule gwikala bho mholele na bhanhu bhabho. Igeleliwa bhilange ugwikala chiza, bho gujilang’hana ijo bhali najo.

Mathayo 19:12.

KISWAHILI: UWE MBAYA WEWE MWOAJI, MWOLEWA HANA NENO.

Methali hiyo ilianzia kwa mtu yule ambaye alikuwa akitafuta mwanamke wa kuoa. Mtu huyo, katika kutafuta kwake alikuwa akiuliza watu ili wamuoneshe aliko mwanamke ambaye ni mzuri. Aliuza watu, “yuko kwa nani mwanamke ambaye ni mzuri nimuoe kwenye kijiji hiki?” Mwenyeji mmoja akamjibu, “yuko kwenye familia yile.” Yeye akazidi kuuliza, “mwanamke yule anatabia njema?” Watu wakamjibu, “uwe mbaya wewe mwoaji, mwolewa hana neno.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hupata vitu vizuri, lakini hushindwa kuvitunza, au hupata watu wema lakini hushindwa kuishi nao kwa sababu ya tabia yake mbaya, katika maisha yake.

Mtu huyo, hushindwa kuvitunza vitu vyake, kutokanam na mwenendo wake wa kuviharibu kwenye matumizi yasiyofaa. Yeye pia, huwasambalatisha watu anaoishi nao kwa sababu ya tabia yake ya kuwadharau wale anaoishi nao.

Watu humfananisha na mtu yule aliyekuwa akitatufa mwanamke mzuri wa kuoa, ambaye ubhaya ulibakia kwake tu, kwa sababu naye huwapata watu wenye tabia njema, lakini huwasambaza kwa kushindwa kuishi nao vizuri. Ndio maana watu humwambia, kwamba, “uwe mbaya wewe mwoaji, mwolewa hana neno.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na tabia zenye upendo wa kuishi na watu kwa amani, kwenye familia zao, ili waweze kusaidiana vizuri maishani mwao. Wanatakiwa kujifunza namna ya kuishi na watu wao, kwa kuvitunza vile walivyo navyo.

Mathayo 19:12. “Kwa maana wengine ni matoashi kwa sababu wamezaliwa hivyo, wengine wamefanywa matoashi na wanadamu na wengine wamejifanya matoashi kwa ajili ya Ufalme wa Mbinguni. Yeye awezaye kulipokea neno hili na alipokee.”

samburu-wedding

africa wedding

traditional-wedding

ENGLISH: THE WOMAN WHO WANTS TO MARRY YOU IS READY MAY BE YOU YOURSELF ARE NOT READY.

This proverb began with the man who was looking for a woman to marry. Such man, in his search, was asking people to show him where the best woman was. He sold his idea to the people, “Who is the best woman to marry in this village?” One host replied, “She is in that family.” He kept asking, “Is that a good woman?” The people answered him, “The woman who wants to marry you is ready may be you yourself are not ready.”

 This proverb is compared with a person who finds good things, but fails to take care of them, or finds good people but fails to live with them because of his bad behaviour in his life.

Such person, in turn, fails to take care of his or her belongings, due to his or her tendency to ruin them for improper use. He, too, stigmatizes the people he lives with because of his contempt for those around him.

People liken him with a man who wanted to marry a beautiful woman, but had a bad behaviour because he could find women of good character and fail to live with them well. That’s why people say to him, that, “The woman who wants to marry you is ready may be you yourself are not ready.”

This proverb teaches people to have habits of living peacefully with people in their families, so that they can help each other in their lives. They need to learn how to live with their people, by taking care of them as they are.

Matthew 19:12.

749. WELELO IDANAMHALAGA.

Ulusumo lunulo, lwingile kumahoya ga bhanhu higulya ng’wa Welelo. Umumahoya gabho genayo, munhu umo agayomba, “Welelo alina nguzu ijo jidashilaga makanza gose, kunguno agabhalang’hanaga bhose, bhanigini na bhakuji.” Ung’wiye agashosha, “inguzu ja ng’wa Welelo jidashilaga kunguno Uweyi adanamhalaga guti bhanhu abho bhagamalaga inguzu jabho ulu bhakula.” Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “Welelo idanamhalaga.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo abhumanile ubhudula bho ng’wa Welelo ubho gujilabhila chiza pye ijisumva jakwe. Umunhu ng’wunuyo, ang’wisanije Welelo umubhutumami bhokwe bhose, ubho bhugang’wenhelaga mafumilo mingi, umukikalile kakwe. Uweyi agabhalangaga abhanhu inzila ja gunsendamila Welelo umubhutumami bhobho, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi shiju jose.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga na bhanhu abho bhahoyelaga higulya ya nguzu ja ng’wa Welelo ijo jidashilaga, kunguno nuweyi, ang’winsanije Welelo umubhutumami bhokwe bhose. Hunagwene agabhawilaga abhanhu giki, “Welelo idanamhalaga.”

 Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gunzunya Welelo bho gung’wisanya weyi umubhutumami bhobho, kugiki bhadule kupandika matwajo mingi umumilimo yabho, shiku jose.

KISWAHILI: MUNGU HAZEEKI.

Methali hiyo, ilitokea kwenye maongezi ya watu waliokuwa wakiongelea juu ya Mungu. Mmoja wao, katika maongezi hayo, alisema, “Mungu ana nguvu ambazo haziishi wakati wote, kwa sababu Yeye huwalinda watu wote watoto na wazee.” Mwenzake alijibu, “nguvu za Mungu haziishi kwa sababu Yeye hazeeki kama wanadamu walivyo, ambao nguvu zao hupungua wanapozeeka.” Ndiyo maana watu husema kwamba, “Mungu hazeeki.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye anauelewa uwezo wa Mungu ambao huvilinda viumbe vyakwe vyote. Mtu huyo, humtegemea Mungu katika utekelezaji wa majukumu yake yote, ambaye humpatia mafanikio mengi, maishani mwake. Yeye huwafundisha pia wenzake namna ya kumtegemea Mungu katika kazi zao, ili waweze kupata mafanikio mengi, siku zote.

Mtu huyo, hufanana na wale watu waliokuwa wakiongelea juu ya uwezo wa Mungu ambao hauishi, kwa sababu naye, humtegemea Mungu katika utendaji wa kazi zake zote. Ndiyo maana huwaambia watu kwamba, “Mungu hazeeki.”

Methali hiyo, huwafundisha watu juu ya kumwamini Mungu kwa kumtegemea Yeye katika utekelezaji wa majukumu yao yote, ili waweze kupata mafanikio mengi katika kazi zao, maishani mwao.

Mwanzo 6:11-12. “Wakati huu dunia ilikuwa imejaa uharibifu na jeuri machoni pa Mungu. Mungu akaona jinsi dunia ilivyoharibika, kwa maana watu wote duniani walikuwa wameharibu njia zao.”

Mathayo 23:37-39. “Ee Yerusalemu, mnaowaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwenu! Mara ngapi nimetamani kuwakusanya watoto wako, kama vile kuku akusanyavyo vifaranga vyake chini ya mbawa zake, lakini hukutaka! Tazama nyumba yako imeachwa tupu na ukiwa. Kwa maana nawaambia, hamtaniona tena mpaka siku ile mtakaposema, ‘Amebarikiwa Yeye ajaye kwa Jina la Bwana.´”

Luka 13:34-35. “Ewe Yerusalemu, Yerusalemu, weweuwauaye manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetamani kuwakusanya watoto wako pamoja kama kuku akusanyavyo vifaranga vyake chini ya mbawa zake, lakini hamkutaka! Tazama nyumba yenu inaachwa ukiwa, ninawaambia hamtaniona tena mpaka wakati ule mtakaposema, “Amebarikiwa Yeye ajaye katika Jina la Bwana.’””

bhabhini bha benini

berber older

musicians-older

ENGLISH: GOD DOES NOT GROW OLD.

This saying came from the conversation of people who talked about God. In the conversation one of them said, “God has power that does not last forever, because He protects all people, young and old.” His companion replied, “The power of God exists because He does not grow old like the human race, whose vigour decreases with age.” That is why people say, “God does not grow old.”

This saying is likened with a man who understands the power of God that protects all his creatures. That person depends on God in discharging all of his responsibilities, he also teaches his fellow human beings on how to rely on God in what they are doing so that they can always be more successful.

That person is like those people who were talking about the inexhaustible power of God in whatever a human being does. That is why he tells people, “God does not grow old.”

This saying teaches people to trust in God by relying on Him in the discharge of all their responsibilities. By doing so, they are always more successful in what they are doing than those who do not.

Genesis 6: 11-12. Matthew 23: 37-39 Luke 13: 34-35.

748. SI IDAB´IPAGA.

Ulusumo lunulo, lulolile Si na bhubhipi bhoyo. Isi iyoyi igikalaga numo ili duhu, kunguno idagaluka ilihanga lyayo gitumo bhagalukilaga abhanhu bho gwingila mu bhusoga mpaga mu ilihanga lya bhubhi. Hunagwene abhanhu bhagayomgaga giki,  “Si idabhipaga.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo adebhile akakulile ka bhanhu, umuwikaji bhokwe. Abhanhu bhagingilaga mubhunigini ulu bhabyalwa. Ahikanza linilo bhagabhiza ni hanga lyawiza kunguno bhatali bhaniki nulu bhayanda. Aliyo lulu, ili hanga lyabho ligajaga lyubhipa ulu bhandya ugunamhala abhayanda, nulu ugugiguluha abhanike.

Gashinaga lulu, akakulile ka bhanhu kagingila kubhuyanda nulu kuwaniki, kaja mpaga kubhunamhala, nulu kubhugikulu, uko bhagabhipile abhanhu abho bhali bhasoga aho bhatali bhadoo.

Abhanhu bhanebho bhagamanaga bhuphipa hado hado nose mpaga bhazumalika, bhajikwa musi, iyo bhagaiyeka mumo ili duhu. Ukubhunamhala nulu ikubhugikulu ili kwihanga lyabhub’i. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “Si idab’ipaga.’

Ulusumo lunulo, lolanga abhanhu higulya ya gubhiza na bhutogwa bho bhugwikala na bhanhu bhose, umukikalile kabho kunguno bhuli ng’wene alab’ipa duhu ulu unamhala, nulu ulu ugiguluha, kugiki bhadule gwiyambilija chiza, umuwikaji bhobho.

Mwanzo 6:11-12.

Mathayo 23:37-39.

Luka 13:34-35.

KISWAHILI: ARDHI HAIHARIBIKI.

Methali hiyo, huangalia ardhi na uhalibikaji wake. Ardhi hiyo, huwa kama ilivyo siku zote kwa sababu yenyewe haibadiliki kama walivyo wanadamu. Uso wa ardhi haikui kama wanavyokuwa watu ambao huwa na sura nzuri wakati wakiwa kwenye rika la ujana wao ambao huharibika, na kuwa na muonekano mbaya wanapofikia kwenye rika lao la uzeeni. Ndiyo maana watu husema kwamba, “ardhi haiharibiki.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye anaelewa ukuaji wa watu katika maisha yake. Watu hao hutokea kwenye hali ya rika la uzuri ambalo ni la ujana, hadi kwenye rika lenye muoneno mbaya ambalo ni la uzeeni. Hivyo sura za watu huendelea kuwa mbaya kwa kadiri wanavyozidi kuzeeka, maishani mwao.

Kumbe basi, ukuaji wa watu huanzia kwenye kuzaliwa, kuelekea ujanani, hadi kwenye uzee kule ambako sura zao hubadilika na kuwa mbaya. Watu hao huendelea kuwa na sura mbaya, mpaka mwishoni hufariki dunia  na kuzika ndani ya arbhi ambayo hupaki kama ilivyo. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘ardhi haiharibiki.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na upendo wa kuishi na watu wote vizuri, katika maisha yao, kwa sababu kila mmoja ataonekana kuwa mbaya akifika kwenye rika la uzeeni, ili waweze kuishi kwa uelewano, maishani mwao.

Mwanzo 6:11-12. “Wakati huu dunia ilikuwa imejaa uharibifu na jeuri machoni pa Mungu. Mungu akaona jinsi dunia ilivyoharibika, kwa maana watu wote duniani walikuwa wameharibu njia zao.”

Mathayo 23:37-39. “Ee Yerusalemu, mnaowaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwenu! Mara ngapi nimetamani kuwakusanya watoto wako, kama vile kuku akusanyavyo vifaranga vyake chini ya mbawa zake, lakini hukutaka! Tazama nyumba yako imeachwa tupu na ukiwa. Kwa maana nawaambia, hamtaniona tena mpaka siku ile mtakaposema, ‘Amebarikiwa Yeye ajaye kwa Jina la Bwana.´”

Luka 13:34-35. “Ewe Yerusalemu, Yerusalemu, weweuwauaye manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetamani kuwakusanya watoto wako pamoja kama kuku akusanyavyo vifaranga vyake chini ya mbawa zake, lakini hamkutaka! Tazama nyumba yenu inaachwa ukiwa, ninawaambia hamtaniona tena mpaka wakati ule mtakaposema, “Amebarikiwa Yeye ajaye katika Jina la Bwana.’””

water-land

masaka-land

ghana-land

ENGLISH: THE EARTH DOES NOT ROT.

This saying looks at the Earth and its incorruptibility. This is because it is always the same; it does not change as humans do. The surface of the Earth does not grow old as do people who are in good shape when they are in their youth, but have a bad appearance when they get old. That is why people say that “the Earth does not rot.”

This saying is compared with a person who understands how times change when it comes to human beings’ life. People may be young, beautiful or handsome today, but they get old in course of time. So the appearance of people is not like that of the Earth which is more or less permanent as it continues to deteriorate as they get older.

 The human beings’ life extends from birth, through adolescence, into adulthood where their physical appearance changes. Over time, these people changes as they become old and therefore lose their good appearance. They keep on changing appearance wise until at last they die and are buried in the Earth which remains as it is. That is why people say, “The Earth does not rot.”

This saying teaches people how to live peacefully with all people because everyone will look bad when they reach old age. So no one is better than the other.

Genesis 6: 11-12. Matthew 23: 37-39 Luke 13: 34-35.