Imbuki ya lusumo lunulo ilolile jisumbwa ja ng’wa Mulungu. Ijisumbwa jinijo jili jabhuli mbika. Bhuli jene jili na wiza bhojo, ubho bhujikilile ijingi. Aliyo lulu gashinaga, jilihoyi ijawiza hangi kukila ni jinijo, ijo umunhu ujikumilijaga, giki jilijawiza kulilanija pye. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘jawiza jidamalagwa.’
Ulusumo lunulo lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agajidalahijaga ijo alinajo bho gujibhona giki angu jidijawiza, nulu jilijabhubhi, ulu ojibhona jingi ijo jilijawiza gukila ijo alinajo. Aliyo lulu umunhu ng’wunuyo aho ojibhonaga ijo alinajo ihaha, ojihayaga giki, jilijawiza gukila pye ijingi. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘jawiza jidamalagwa,’ kunguno uweyi wiganikaga giki, ojimala pye ugujibhona, ijawiza jinijo.
Ulusumo lunulo lolanga bhanhu gufula ijo bhalinajo umuwikaji bhobho, bho gujibhona giki jilijawiza, kunguno ijawiza jidamalagwa.
(Luka 12:16-21; Luka 16:19)’
KISWAHILI: VIZURI HAVIMALIZWI/WAZURI HAWAMALIZWI.
Chanzo cha methali hiyo chaangalia viumbe vya Mungu. Viumbe hivyo ni vingi, na pia ni vya kila aina. Kila kimoja kina uzuri wake uliotafauti na ule wa kingine. Lakini basi, vipo vilivyo vizuri zaidi ya vingine, ambavyo mtu alishaviona mara ya kwanza, na kudhani kwamba, hicho ni kizuri kuliko vyote. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘vizuri havimalizwi.’
Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu ambaye huvidharau vile alivyo navyo, baada ya kuviona vingine kuwa ni vizuri kuliko alivyo navyo. Lakini mtu huyo, alipoviona kwa mara ya kwanza vile alivyo navyo, alivifikiria kuwa ni vizuri kupita vyote, alivyoviona wakati huo. Yeye alifikiria kwamba, alivishamaliza kuviona vyote vilivyo vizuri, kumbe haikuwa hivyo. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘vizuri havimalizwi.’
Methali hiyo hufundisha watu kuridhika na vile walivyovichagua maishani mwao. Kuridhika huko, kutawawezesha watu hao, kuyaishi vizuri maisha yao waliyoyachagua, au kuishi kwa amani na wenza wao waliowachagua, maishani mwao, kwa sababu ‘vizuri havimalizwi, au wazuri hawamalizwi.’
(Luka 12:16-21; Luka 16:19).
ENGLISH: THAT WHICH IS GOOD IS NEVER FINISHED.
The origin of this proverb is God’s creations. They are many, and of all kinds. Each has its own unique beauty that is different from that of the other. But then, there are other things that are much better than that which is thought to be the best. That is why people say, ”what is good is never finished.”
The proverb is comparatively used to remind those who despise what they have after seeing other things or other people as better than what they have that “the good things/the beautiful ones are never finished”. But when these people first saw what they have, they thought that it was the best. They thought that they had finished seeing all that was good or beautiful, which wasn’t the case. That is why people say, ”what is good is never finished.”
The proverb teaches people about being content with the choices they make in their lives. That satisfaction, will allow them to live the life they have chosen, or to live in peace with the people they have chosen in their lives, because ”what is good is never finished.”
(Luke 12: 16-21; Luke 16:19)