Imbuki ya lusumo lunulo ilolile ngegelehya iyogikikalaga muminzi, na bhahasha. Aliyo lulu ingegelehya yiniyo ilina magulu ayo gadulile nulu gupundula ginhu ijo jikolile na daladasi. Ulu yutulwa mub’ahasha mumho iguipundula duhu. Hunagwene abhanhu bhagahayaga giki, ‘b’ahasha ya ngegelehya igipundulaga yenikili.’
Ulusumo lunulo lugalenganijiyaga kuli munhu uyo agitaga yabhubhi umuchalo. Umunhu ng’wunuyo agamanyichaga ng’winikili gulwa gwiting’wa, nulu guhugana gokwe. Kihamo na gumanyika chiniko, umunhu ng’wunuyo agahalalikaga bho gulema giki aditile uwei ya wabhubhi yiniyo. Aliyo lulu, abhanhu abho bhalimhona bhalimana pye igiki, uwei huyo witaga iyabhu yiniyo. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘b’ahasha ya ngegelehya igipundulaga yenikili.’
Ulusumo lunulo lolanga bhanhu guleka gwita mihayo ya bhub’i kub’ichab’o. Akikalile kenako kagubhambilija ijinagubhiza na widohya bho gudula gwikala bho mholele na bhanhu umuwikaji b’ob’o.
KISWAHILI: BAHASHA YA KAA (WA MAJINI) HUJITOBOA YENYEWE.
Chanzo cha methali hiyo chaangalia kaa aishie majini, na bahasha. Lakini kaa huyo ana miguu ambayo huweza hata kutoboa vitu ambavyo hufanana na karatasi. Kwa hiyo, mtu akimweka kwenye bahasha ataitoboa tu. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘bahasha ya kaa hujitoboa yenyewe.’
Methali hiyo hulinganishwa kwa mtu yule atendaye maovu katika jamii. Mtu hiyo, hujulikana mwenyewe kutokana na wasi wasi wake, au hofu aliyo nayo. Pamoja na kuwa na wasi wasi au hofu hiyo, mtu huyo hubisha kwa kukataa kuwa yeye hajafanya uovu huo. Huyo ni mtu asiyetaka kukiri kosa lake ingawa kila mtu anajua kwamba mwenye kosa ni yeye.
Pamoja na kukataa kwake, watu wanaomtazama wote huelewa kuwa yeye ndiye aliyetenda uovu huo kutokana na wasi wasi wake alio nao. Kwa hiyo, mtu aliyetenda jambo baya hujibainisha mwenyewe kwa kubabaika kwake. Ndiyo maana watu husema kuwa, ‘bahasha ya kaa hujitoboa yenyewe.’
Methali hiyo hufundisha watu kuacha kutenda maovu katika jamii au kwa wenzao. Kuishi hivyo, kutawasaidia watu hao katika kujijengea unyenyekevu wa kuwawezesha kuishi kwa amani na wenzao, maishani mwao.
Luka 18:18-24.
ENGLISH: AN ENVELOPE WITH A CRAB PERFORATES ITSELF.
The origin of this proverb is a crab and an envelope. The crab has legs that can perforate such things as paper. So, if someone puts it in an envelope, it will simply perforate it. That is why people say, “An envelope with a crab perforates itself.”
The proverb is used comparatively to refer to any person who does evil in society. Such a person is easily identifieble because of his or her own anxiety and fears. Despite their anxiety and fears, the person denies committing the wrong. That is to say, such a person does not want to admit his or her mistake, even though it is obvious for everyone that he/she is wrong.
Despite his/her refusal, all observers understand that he/she committed the evil because he or she cannot hide the anxiety and fears. Therefore, a person who does wrong things will be easily identified because of his or her own anxiety and fears. That’s why people say, ‘An envelop with a crab perforates itself.’
This proverb teaches people to abandon evil deeds in the society or against their peers. Living free of evil deeds will help them to develop humility that can enable them to live in harmony with others throughout their lives.
Luke 18: 18-24.