Riddles

88. Jigano Ja Ntemi

Collected by: Don Sybertz,

With special thanks to Rev Joe Healey  (African proverbs,Sayings and stories)

Aho kale oliho Ntemi nkumuku noi. Uyo olintongeji o wiza noi na makujo mingi. Aho lwabhita ikanza itale lwa bhutongeji bhokwe, igigela nzala umu si yakwe na lwande lo bhuzenganwa na si yakwe.

Nzala yiniyo igasola ikanza lwa miaka idatu na nusu. Bhanhu bhagayanga na gukoya noi ung’wibala lwakwe, bhangi bhagacha na nzala. Untemi agakoiwa noi na bhanhu, giki adubhakoyakoyelaga abhanhu ku lwande lo nzala na gubhenhela mbula. Ikale yalibhizile untemi lazima weng’nhe mbula.

Bhanhu bhagayomba giki, Untemi ulu adabhingije umu makoye ga nzala na gubhenhela mbula, bhaguntula mpaga ache. Untemi aho wigwa ubhulalamiki bhingi bho bhanhu, agiyangula gutoloka guja ng’wibolu, gugapela makoye mingi umu si yakwe.

Ugonghana agatoroka uja ng’wipolu uko bhanhu bhatiho, ugibhanda mumi milima. Agikala kunuko miaka idatu na nusu. Wikala agulwaga matunda ga ng’wipolu. Mbula igatula aho yabhita miaka idatu na nusu.

Aho otoroka bhanhu bhagapandika noi ijiliwa na bhagayega noi, mpaga bhita npango gogunchola untemi obho, aliyo bhadampandikile gete.

Yubhiza abhanasi umu si yakwe, bhuja ng’wipolu kubhulingi bho ndimu. Bhaginga chalo jinane guja ng’wipolu. Kwikanza lya shigu mpungati, ukwene guhaya, nyuma imo.

Bhagalinga ukunuko kwipolu mpaga lushigu lo gatandatu dilu saa nne. Aho bhashiga ukunima nhihu uko oliwibhisa untemi obho, bhagagunyamanija unima, untemi nanghwe oliwiyanikija mulimi ku nguno ya mbeho.

Itukio la gafula (Nhanga) jigasalambana munima, na abhalingi bhusalambana, mpaga nsumba umo ufuada nhanga na mbwa jakwe ibhili.

Bhogafula umona untemi, wimila, alina hali ya nyahabhi, nzwili jakwe jabhiza ndihu, na hangi obhipa mako na mywenda ya mako noi.

Unsumba ugubhona hali yiniyo agiganika giki obhona ng’wengeleji. Unsumba agapela nhambo noi, agikindika uching’wa linti munda, ubhula bhufuma.

Unsumba agalila na gulija ng’wano. Aho bhigwa abhiye bhagiganika giki odimagwa na shimba.  Nanghwe Untemi agashiga agakumya na guhaya, “Napelaga makoye nu kunu ganipandika hangi.”

Bhagamuja na adamile ugogwita. Bhanhu bhagashiga na gumuja unsumba ng’wenuyu witaga kii? Untemi agahaya, “Nu nene onibhonaga ogoha ku gafula ku nguno ya hali yane umo nalibhizila o mako, nzwili na mpaga mywenda yane yabhipa mako.

Bhanhu bhagamuja, “Ntemi wizaga nanali ukunu?” Untemi ushosha ku bhupina, “Niza kale, nina miaka idatu na nusu.” Bhagamuja hangi, “Wizaga gwita kiyi?” Untemi uhaya, “Nagatoroka aho gigela makoye uko kaya niza gwibhisa kunu mapolu.”

Kiswahili: Hadithi Ya Mtemi (Mfalme)

Hapo zamani kulikuwako na mtemi maarufu sana. Ambaye alikuwa kiongozi safi sana na hekima nyingi. Baada ya muda mrefu wa uongozi wake, ilitokea njaa katika nchi yake na pande za jirani mwa nchi yake.

Njaa hii ilichukua muda wa miaka mitatu na nusu. Watu waliyumba sana katika eneo lake, wengine walikufa na njaa. Mtemi alisumbuliwa sana na watu, kwamba hawashughulikii watu hao kwa upande wa njaa na kuwaletea mvua. Zamani ilikuwa Mtemi lazima awe mleta mvua.

Watu walisema Mtemi asipowashughulikia kwenye tatizo la njaa na kuwaletea mvua, watampiga mpaka kufa. Mtemi aliposikia malalamiko mengi ya watu, aliamua kutoroka kwenda porini, kuyakimbia matatizo mengi katika nchi yake.

Kweli alitoroka akaenda porini kusiko na watu,  akajificha kwenye milima. Alikaa huko miaka mitatu na nusu. Alikuwa  anakula matunda ya porini. Mvua ilinyesha baada ya kupita miaka mitatu na nusu. Alipotoroka watu walipata sana chakula na kufurahi sana, hata wakafanya mpango wa kumtafuta  Mtemi wao na wasimpate kabisa.

Ikawa wananchi katika nchi yake,  walikwenda porini kwa mawindo ya wanyama. Waliondoka vijiji vinane kwenda porini. Kwa muda wa siku saba, yaani wiki moja.

 Waliwinda huko porini hata siku ya Jumamosi asubuhi kama saa nne. Walifika kwenye mlima mrefu, alikojificha Mtemi wao. Waliuzingira mlima, Mtemi naye alikuwa amejianika kwenye jua kwa ajili ya baridi.

Tukio la ghafula (Kanga) walisambaa kwenye mlima, na wawindaji walisambaa, hata kijana mmoja alifuata kanga na mbwa wake wawili. Ghafula akamwona Mtemi, akasimama, akiwa na hali duni, nywele zake zimekuwa ndefu, na tena chafu na nguo chafu sana.

 Kijana kuona hali hiyo alidhani ameona kivuli. Kijana akakimbia mbio sana, akaruka akachomwa mti tumboni na utumbo ukatoka. Kijana akalia na kupiga yowe. Waliposikia wenzake walidhani ameshikwa na Simba.  Na mtemi alifika akashangaa na kusema, “Nimekimbia matatizo na huku yamenikuta tena.”

Wakamwuliza na asijue la kufanya. Watu walifika wakamwuliza huyu kijana amefanya nini? Mtemi  akasema,  “Ni mimi ameniona  ghafula akaogopa kwa sababu ya hali yangu nilivyokuwa mchafu, nywele na hata nguo zangu na hali ya uchafu.

Watu walimwuliza,  “Mtemi umekuja lini huku?”  Mtemi akajibu kwa huzuni,  “Nimekuja zamani, nina miaka mitatu na nusu.” Waliuliza tena, “Umekuja kufanya nini? Mtemi alisema, “Nilitoroka  baada ya kutokea matatizo huko nyumbani na kujificha huku maporini.”

african-chief

ENGLISH: THE STORY OF THE CHIEF.

Once upon a time, there was a very famous chief who was a very good leader with a lot of wisdom. After a long time of his leadership, there was famine outbreak in his country and the surrounding neighbouring countries.

This famine took about three and a half years. People suffered from it very much in that area.Many died of famine. The chief was very troubled by the people.They complained that he did not deal with the people on matters of famine.They looked at him as a person who had failed to bring rain. Formerly, the chief was considered to be the one who brings rain.

The people said that if the chief could not deal with the problem of famine and bring rain, they would kill him. When the chief heard people’s complaints, he decided to escape and went to the wilderness, running away the problems in his country.

He went to settle in the wilderness where there were no people.He hid himself in the mountains. He stayed there for three and a half years. He was eating only wild fruits. Finally, back in the village, it rained heavily. One day, the people of his land went to the wilderness to hunt preys. They passed eight villages and as they moved to the wilderness. They spent seven days on the way.

 They were hunting in the wilderness one Saturday morning at around ten o’clock. They came to a high mountain where their chief himself was hiding. As they hunted, they encircled the mountain.Meanwhile,the chief was enjoying  the sun for it was winter.

All of a sudden,Guinea fowls spread in different parts of the mountain.The hunters also scattered.Among the hunters, a young man was running after guinea fowls. This young man had his two hunting dogs. Suddenly he saw the chief, standing.He was in a poor condition.His hair was long and dirty.The clothes were also dirty.

As the young man saw the situation, he thought he was seeing a shadow. The young man ran very fast, trying to save his life. As he ran,a dry tree branch hit him in the stomach. He was badly injured. In fact, intestines came out. The young man screamed madly. When other hunters heard,they  thought he was being attackedby a lion. As hunters were looking at their fellow hunter who was in agony, the chief also came to the scene. Hewas surprised and he said, “I have run  away from trouble and I now have found it again.”

They asked him not to know what to do. People came and asked what the boy had done? The Chief said, “I think after seeing me, the young man got shocked and started running. The young man may have been frightened by my dirt condition, hair and even my clothes and the general dirty condition in which I am.

The hunters asked him, “When did you come here?” The Chief replied sadly, “I have come a long time ago, I have been here for  three and a half years.” They asked again, “Why did you come here? The Chief said, “I escaped as there wasa problem in the home village which could endanger my life. So, I came to hide myself here in the forest.”

86. Bhuluguji bho Zahanati

Collected by: Don Sybertz,  

With special thanks to Rev Joe Healey  (African proverbs,Sayings and stories)

Ng’walimu Julius Nyerere, aho oliatali ali Rais o Tanzania. Lushigu lumo agabhilingwa gujulugula Zahanati munkoa gumo. Agashika Jumamos mhindi, agikala na bhatongeji bha hibala linilo.

Agalomba asome latibha ya bhuluguji. Ubhutaratibhu bholi giki:

Gubokela bhageni.

Lwimbo lwa Taifa.

Kwaya, michezo, n.k.

Hotubha ya ntale o mkoa n.k.

Agisoma pye ilatibha aliyo adabhonile moyi mhayo higulwa ya gunkuja Mulungu. Agabhalola kubhupelanu na guitantula ilatibha habhutongi yabho, agahaya, “Ying’we mmanile igiki unene nali nkristo Gatoliki, nalisoma misa bhuli lo jumapili. Nahanaha bhaliho bhakristo bhingi abho bhagasalilaga, nibhuli umulatibha ying’we bhutiho wasa bho gunkuja Mulungu, nulu gunhumbilija?

 Kiswahili: Uzinduzi Wa Zahanati

Mwalimu Julius Nyerere, alipokuwa bado Rais wa Tanzania. Siku moja alialikwa kufungua Zahanati katika mkoa fulani. Alifika Jumamosi jioni, akakaa na viongozi wa mahali hapo. Akaomba asome ratiba ya ufunguzi.

Utaratibu ulikuwa hivi:

Kupokea wageni.

Wimbo wa Taifa.

Kwaya, Michezo, n.k.

Hotuba ya mkuu wa mkoa n.k.

Akasoma ratiba yote lakini hakuona neno juu ya kumtukuza Mungu. Akawaangalia kwa hasira na kuichana ratiba mbele yao, akasema, “Ninyi mnajua kwamba mimi ni mkristu Mkatoliki, huwa nasali Misa kila Jumapili. Na hapa kuna wakristu wengi ambao wanasali, kwa nini katika ratiba yenu haipo nafasi ya kumtukuza Mungu, au kumshukuru?

pharmacist

English: Launching Of A Dispensary.

ENGLISH: THE LAUNCHING OF A DISPENSARY

When MwalimuJulius Nyerere was still the President of Tanzania, he was one day invited to launch a dispensary in a particular region. He arrived there on Saturday evening.He stayed with the local leaders of that place. He asked to be given the opening schedule.

The schedule read as follows:

Receiving visitors.

The National Anthem.

Choir, sports and games, etc.

The speech of the regional commissioner etc.

He read the whole schedule but he did not see anything about glorifying God. As reaction, he looked at them with anger and tore the schedule in front of them saying, “You know that I am a Catholic, I normally attend Mass every Sunday. And here there are many Christians who pray.Why is it that in your schedule there is no space for glorifying God, or for thanking Him?

85. Nsumba Nhabhi

Collected by: Don Sybertz,  

With special thanks to Rev Joe Healey  (African proverbs,Sayings and stories)

Ikanza lwa kale oliho Nsumba umo nzunya nhabhi. Wikalaga uzwala madaso na oliadina jilatu umumagulu. Abhiye bhalibhandalaha na gunseka noi. Hangi bhangemaga nyahala bhalihaya, “Bhebhe ulinzunya, ulu Mulungu agutogilwe, nibhuli adagulanghanaga na gukulinda? Adadulile gung’wila nulu munhu umo agwinhe ng’wenda nulu jilatu?”

Unsumba ng’wenuyo agayanga noi ukunu agwitaga jisoji alihaya, “Naliganika uMulungu agubhawilaga abhanhu, aliyo bhadandegelekaga.”

Kiswahili: Kijana Fukara

Enzi hizo alikuwapo kijana mmoja mkristu  fukara. Alikuwa anavaa matambara (yaani nguo chakavu) na hakuwa na viatu miguuni. Wenzake walimdharau na kumcheka sana.

Pia walimdhihaki wakisema, “wewe ni mkristu, kama Mungu anakupenda, kwa nini hakulindi na kukutunza? Hawezi kumwambia hata mtu mmoja akupe nguo au viatu? Kijana alihangaika mno na huku akitokwa na machozi akasema, “Nafikiri Mungu anawaambia watu, lakini hawamsikilizi.”

boy

ENGLISH: A POOR BOY

There was a poor young man who was Christian. He used to wear rags (tatters). He had no shoes either.  His friends despised him and laughed at him.

They also mocked him, saying, “You are a Christian.If God loves you, why does He not guard you and take care of you?  He can’t He even tell someone to give you clothes or shoes?” The boy was very grieved and he cried saying, “I think God tells people, but they don’t listen to him.”

84. Bhusimbi bho Lwinzi- Lung’wando na Ndimu

Collected by: Don Sybertz,  

With special thanks to Rev Joe Healey  (African proverbs,Sayings and stories)

Aho Kale, jaliho ndimu ningi. Imo yajo yali Lung’wando. Bhasi, bhagiigwa gusimba lwinzi la minzi. Aho bhandya ugusimba ulwinzi, Ulung’wando uhaya, “Bhabehi, igwigelelwa dulombe giki mbula ipandike gutula. Ulu idishena igubhiza bhule.” Ibhujiku Ulung’wando wiza agwimbaga;

“Oo ndemle bhamayu ndemle,” “Oo ndemle Lung’wando Lung’wando aliza.” Agahodisha aho lwinzi, alihaya, “Hodii.”

Lidakulile ikanza Ulung’wando wingila umuminzi, wandya goga. Aho omala, unya mashi mumo. Uja lokwe. Intondo yaho bhagasanga mashi umu lwinzi.

Bhiyangula guntuula mnambiti ubhiza nindi o lwinzi lwobho. Ubhujiku Ulung’wando agashika hangi na kunu alimba lwimbo lwakwe lwenilo. Agahodisha, Mbiti agatima tochi na kubhuja, “Bhebhe uli nani?” “Nene aha!”

“Bhebhe uli lung’wando idishene?” “Ehee, jiliho ki?” “Bhebhe lung’wando huna uyo agubhipyaga a minzi gise, enh?”

Ulung’wando agashosha, “Iiii! Unene nadagamanile aminzi ging’we. Unene ninaminzi gane ayo galimasoga noi. Dujage nagagwinhe!”

Imbiti yuhaya, “Haya dujage.” Bhasi, ulung’wando na mbiti bhuja.

Aho bhashika aha lwande fulani ulung’wando ung’wila umnambiti, “Nahene, ubhebhe ikalaga aha si, unene nalinhe ng’wigulwa.”

Ulung’wando agandya kung’wikija. Inhalikilo, mbiti agiyibha, wandya kuntunga lugoye. Aho omala ugwita chiniko, Ulung’wando agiponeja mugati ya lwinzi lwobho, wandya goga. Aho omala goga, unya mashi, na kuja lokwe. Intondo yaho diyu, bhagibhuja, “Ng’wigisu ojaga hei?”

Imbiti yushosha, “Naliho kunu bhabehi, natungagwa lugoye na lung’wando!” Ulushigu ulo lugafuada, bhuntuula grumati giki alinde ulwinzi lwobho.

Bhung’winha bhulangeti na tochi. Bhujiku ulung’wando agashiga na gatolo/gajisabho ako kina bhuki na kunu aliimba lyimbo lwakwe linilo. Aho omala ugupiga ihodi, grumati agikala sele.

Ulung’wando agingila na gwigasha hahigula ya ng’wa grumati. Aho grumati wibhakila, agabhuja, “Ulinani ubhebhe? “Nali nene Lung’wando!” “Ahaa! Gashanaga nu bhebhe lung’wando!”

Aheneho grumati ufula mhembe. Ndimu pye jiza na mapanga. Uluwang’wando agabhawila, “Unene nadadulile gubhulagwa na mapanga.” Bhasi ndimu jigantunga lugoye umnalung’wando na guntuma gujila moto.

Aho lidakulile ikanza, ingoye ijo bhalibhantungila jutinika, na lung’wando agatoloka na gwandya gupela ukunu aliimba.

Lung’wando kanyama kadoo, aliyo kanyama kabhalaganu,

Ulung’wando kanyama kadoo, aliyo kanyaga kabhalaganu.

 Kiswahili: Uchimbaji Wa Kisima-Sungura Na Wanyama

Hapo zamani, kulikuwa na wanyama wengi. Mmoja wa wanyama hao alikuwa Sungura. Basi walikubaliana kuchimba kisima cha maji. Walipoanza kuchimba kisima, Sungura akasema, “Jamani, itafaa tuombe ili mvua ipate kunyesha. Vinginevyo itakuwa ni bure.” Usiku Sungura akaja akiimba;

“Oo ndemle wakina mama ndemle,

“Oo ndemle Sungura Sungura anakuja.”

Akapiga hodi pale kisimani, akisema, “Hodii!”

Mara Sungura akaingia katika kisima, akaanza kuoga, alipomaliza, akanya mavi humo humo. Akaenda zake. Kesho yake walikuta mavi katika kisima. Wakaamua kumweka Fisi kuwa mlinzi wa kisima chao. Usiku Sungura alifika tena na huku akiimba wimbo wake ule ule. Alipobisha hodi, Fisi akamulika tochi na kuuliza, “Wewe ni nani?”

“Mimi hapa!”

“Wewe ni Sungura sivyo?”

“Ndiyo, kulikoni?”

“Wewe Sungura ndiye unayechafua maji yetu, enh?”

Sungura akajibu, “Iiii! Mimi sichezei maji yenu. Mimi nina maji yangu ambayo ni safi sana. Twende nikakupe!”

Fisi akasema, “Haya twende.” Basi, Sungura na Fisi wakaenda. Walipofika mahali fulani Sungura akamwambia Fisi,  “Haya, wewe kaa chini na mimi nipande juu.”  Sungura akaanza kumdondoshea.

Mwisho, Fisi akajisahau, akaanza kumfunga kamba. Alipomaliza kufanya hayo, Sungura alijitumbukiza ndani ya kisima chao, akaanza kuoga. Kisha kuoga, akanya mavi, na akaenda zake. Kesho yake asubuhi, walijiuliza, “Mwenzetu amekwenda wapi?”

Fisi akajibu, “Niko huku jamani, nimefungwa kamba na Sungura!”  Siku iliyofuata, wakamweka Kobe ili alinde kisima chao. Walimkabidhi blanketi na tochi.

 Usiku Sungura akaja na kibuyu chenye asali na huku akiimba wimbo wake uleule. Baada ya kupiga hodi, Kobe akakaa kimya. Sungura akaingia na kukaa juu ya gamba la Kobe. Hapo Kobe akastuka, akauliza,  “Nani wewe?”

“Ni mimi Sungura!”

“Ahaa! Kumbe ni wewe Sungura!”

Hapo Kobe akapiga filimbi. Wanyama wote wakaja na mapanga. Sungura akawaambia, “Mimi siwezi kuuawa kwa mapanga.” Basi wanyama wakamfunga kamba Sungura na kumtupa kwenye moto. Mara kamba  walizomfunga zikakatika, na Sungura alichupa na kuanza kukimbia huku akiimba;

        “Sungura kanyama kadogo, lakini kanyama kajanja,

        “Sungura kanyama kadogo, lakini kanyama kajanja.

idyll

ENGLISH: THE WELLS  OF ANIMALS

In the past, there were many animals. One of these animals was Hare. Then all the animals agreed to dig a water well. When they started digging a well, Hare said, “Colleagues, we would have to ask for rain instead of digging a well. Otherwise it will be useless.” At night,Hare maliciously came to the well singing:

“Oo ndemle wakina mama ndemle,” (ooh ndemle mothers ndemle),

“Oo ndemle Sungura Sungura anakuja.”(Ooh ndemle Hare is coming).

He asked for permission of entrance to  the well, saying, “Hodi!” (a word used when asking people for permission to enter).

When the Hare got into the well, he began to wash his body.When he finished drinking and washing, he defecated  in it. Then, he went away. The following day,the  animals found the stool in the well. They decided to make Hyena  the guard of their well. At night,Hare came again and sang his same song. When he approached the well, Hyena switched on his torch and asked, “Who are you?”

“Here I am!”

“You are a Hare,are’nt you?”

“Yes, what is the matter?”

“You Hare is the one who spoils our water, right?”

The Harere plied, “Oh! I don’t spoil your water. I have my water which is very clean. Let us go so that I can give you the water!”

Hyena agreed, “Let’s go.” So, Hare and Hyena went. After a short while, the hare said to Hyena, “Well, you sit down and I will give you the water.” The Hare started to drop water at Hyena.

Finally, Hyena relaxed and Hare began to tie him with a string. When he finished doing that, the Hare plunged himself into the well and began to wash himself in it. After finishing this, he defecated in it, and went away. The following morning, they asked, “Where did our fellow go?”

Hyena answered, “I am here, I am tied with a rope by Hare!”

The next day, they made tortoise the new guard of their well. They handed him a blanket and a torch.

At night,Hare came with a honey calabash singing his own song. As he got closer to the well, Tortoise remained silent. Then Tortoise asked, “Who are you?”

“I am the Hare!”

“Ah! That is you Hare! ”

Then Tortoise immediately blew the whistle. All the animals came with swords. The Hare said to them, “I can’t be killed with the swords.” So the animals tied the rope to the Hare and threw him into the fire. In the blink of the eye, the string got loose and Hare escaped and started running while singing;

        “Harea small animal, but crafty,

        “Harea small, but very crafty.

 

83. Mbuki ya Bhulaga Numba: Mbuki-Wandijo wa Mihayo

Collected by: Don Sybertz,  

With special thanks to Rev Joe Healey  (African proverbs,Sayings and stories)

Waliho ngosha, akatojiwa na Ise. Aliyo walatantongilwe  unke. Akahadikijiwa Nuse, wiyumilija kwikala nang’hwe unkima ng’weji ngima.  Aho gwashila ung’weji uja kujudima ng’ombe  ha  ng’wabho bhuko wiza watungaga maswa.

Aho wiza lulu unke uhaya kung’wanukula  kanigo kenako. Ung’wila,  “Lekaga  kunanukula,  shilimo shikolo shitale.”   “Shikolo ki?”  “Ilimo mbuki  yane.”  Maswa aya gukatulwa  ha lugutu.

Aho wandya kushema,  unkima  nang’hwe uhaya,  “Nilole mbuki iyo yaluhayiwagwa.” Aho wadima maswa, alole ishilimo umugati,  ungosha walushemaga  wiponya  inhunda  ya mabhele ulila ng’hungu, “Wadima ha mbuki yane.”  Wandya lulu kuntula unke.  Ngosha uneka  unke, ushoka ku ng’wawe. Yubhiza lulu mbuki yabhulaga kaya.

Kiswahili: Kisa Kilichovunja Nyumba

Alikuwepo kijana mmoja aliozeshwa na baba yake. Lakini hakumpenda mke wake kwa vile alilazimishwa. Alivumilia kuishi na mke wake kwa muda wa mwezi mmoja. Lakini ulipomalizika muda huo, alikwenda kuchunga ng’ombe wa mkwewe.

Aliporudi kutoka huko, alifunga mzigo wa nyasi. Alipowasili nao pale nyumbani, mkewe alitaka kumpokea mzigo ule. Lakini alikataliwa, “Acha kunipokea kwani kuna kitu ndani.”  “Kuna kitu gani ndani?” mkewe aliuliza.

“Kuna mana.” Nyasi zile zikawekwa kando ya kizizi. Alipoanza kukamua, mwanamke naye akasema, “Ngoja niangalie mana ambayo imo ndani ya nyasi hizi.”

Alipoushika mzigo ili aangalie kilichomo ndani, mume aliyekuwa anakamua, chombo cha maziwa alikitupa, akalia kwa sauti kubwa na kusema, “Umeshika mana yangu.”  Hapo akaanza kumpiga mke wake na kumrudisha nyumbani kwa wazazi wake. Hicho ndicho kisa kilichovunja mji.

breakupENGLISH: AN INCIDENT THAT BROKE THE MARRIAGE

There was a young man whose father married him a wife. But he did not love his wife because he was married by force. He endured living with his wife for a month. But thereafter, he went to take care of his father-in-law’s cattle.

When he came back from there, he came with a load of grasses. When he arrived at his house, his wife wanted to  receive the load. But the husband rejected, “Do notcarryit  because there is something valuable inside.” “What is it that is inside?” His wife asked.

“There is manna.” Then that tuft of grasses was put near the cowshed. The husband was busy milking a cow.The woman wanted to use that opportunity and she said, “Let me look at the manna that is in this grass.”

When she was trying to do that, the man who was holding a milking container threw it and loudly shouted, “You are touching my manna.” He immediately began to beat his wife and that became the justification for sending his wifeback to her parents. That is the incident that broke the marriage.

divorce-2