Songs

107. NTUNGILIJA NA NG’WANA WA JING’WENG’WE

Collected by: Don Sybertz,

With special thanks to Rev Joe Healey  (African proverbs,Sayings and stories)

Olaliho  ngosha umo uyo witanagwa Ntungilija kunguno oladalemaga ugub’ambilija b’iye. Lushiku lumo Ntungilija agab’uka gujuyela ng’wipolu. Aho oshika ukwenuko agamanhya na kana kali Shing’weng’we, kung’wila giki, “B’ageshi Ntungilija, unene aho nabyalwa, abhabyaji bhane bhakanileka sagala. Nduhu nulu numba, kulwa yeniyo lulu nalilomba unizengele nulu kakulyandi unitule moyi naguluhaga noi ulunili. Ntungilija wita gitumo kana kali Shing’weng’we kagang’wilila.

Aho kana kalishing’weng’we kikala shigu ng’ehu duhu ung’widulyandi, gumadika, gung’wila hangi, Ntungilija, akazengele iluli pye nung’wene kokala. Aho kokala umunumba kung’wila, “ntungilija namanile giki ulintungilija, nane naduhayaga gugukoya. Nalulu giki bhageshi Ntungilija, jaga kumalugulu uganikob’ele ipilinga ilitale gete. Ung’wenumo lulu nadugukoya.”

Ntungilija agandya lugendo loguja kumapolu gujuchob’a lipilinga ilitale. Mpaga ugalala guko, upandika ilipilinga. Ntondo yene ushoga dilu ukawila akana ka Shing’weng’we giki, “opandikaga ilipilinga.” Nab’ub’uka pye bhajile gujulilola ilipilinga. Aho bhashiga, akana ka Shing’weng’we kingila ung’wipilinga. Kuligemela gwigasha moyi, kigelelwa.

Aho kigelwa kung’wila Ntungilija giki, “Ntungilija, aliyo nalina mhayo gumo uyo nalitogwa naguwile.”  Ntungilija uhaya,  “Niwilage duhu bhageshi.” Kana ka Shing’weng’we kung’wila Ntungilija. “Aliyo lulu bhageshi Ntungilija nalitogwa nagulye, kunguno ukuwelelo kulikuduhu.” Ntungilija nang’hwe agasunduhala sana uhaya, “hali bhuli bhageshi unilye, pye iyose iyo yawiza nagwitilile?”

Nako akana ka Shing’weng’we kushosha, “Ulu uduzunyaga iyo naliguwila jaga nahene ugab’ab’uje ab’aduguyo,  b’asumba b’iyo nu nkima oko ulu giki aliho Ntungilija ukunu kuwelelo. Ujidutoloka uje ilali kunguno nagumanile pye nab’aduguyo ji nammanile.”

Nang’hwe agaja kujub’ab’uja. Aho oshiga nagub’awila, nabho bhakakumya b’uhaya, pye imihayo iyose iyo ong’witilile ung’wana Oshing’weng’we yaya nagugulumba, ii! Gushinaga ukunu kuwelelo adiko Ntungilija.

Nang’hwe agaja kuli nke gujunaga giki, ashoganye aje agaliwe na Lishing’weng’we, ili lidi kana hangi kunguno lyakulile na lyab’izile Lishing’weng’we.

Nang’hwe unke uhaya giki anshindikile agilolele umo agumililagwa. Nabho bhabhili b’andya lugendo loguja kumalugulu. Aho b’ashiga, kana  ka Shing’weng’we bhukasanga kakulile, lyab’izile Lishing’weng’we. Nalyo ligamuja unkima “wizilaga ki ub’eb’e ukunu?” Nang’hwe ushosha. “Nizaga  kung’wilolela ungoshi wane umo ulimilila.” Nang’hwe Shing’weng’we uhaya, “Ingaga aha unene nadaguhayile ub’eb’e shogaga kaya.”

Nang’hwe nkima ushosha, “nadudula ugushoga ugukaya ing’wene kunguno inzila iyo dab’itilile ili na mashinhu mingi noi. Mayoka, Mashimba na angi mingi duhu, galihoi.”

Nang’hwe uShing’weng’we ung’wila giki, agung’winha b’ugota bhogubhashogelegeja na gubhabhulaga abhanashinhu bhenabo. Shing’weng’we ung’wila giki, asole bhugota ulu umanhya na mashinu genayo, ubhutula ubhugota hajiganza na uhaya giki, ukunu alifula, “Muna Nzoka chaga.” Nang’hwe agucha  upandika nzila yagub’itila.

Nulu muna Shimba chaga. Aho nkima winhwa ubhugota, agabhutula hajiganza na kubhufula ukunu alihaya, “Nang’ho muna Shing’weng’we chaga.” Haho na haho Shing’weng’we agacha. Nang’hwe ntungilija bhushoka kung’wabho kihamo na nkima.

KISWAHILI: MKWELI NA MTOTO WA ZIMWI

Alikuwapo mwanamume mmoja aliyeitwa Ntungilija (mkweli) ambaye alikuwa mwaminifu. Huyo  alikuwa na tabia ya kuwasaidia wengine. Siku moja Ntungilija alikwenda porini akakutana na zimwi mtoto. Yule zimwi akamwambia ntugilija, “nilipozaliwa wazazi wangu waliniacha  ovyo. Sikujengewa nyumba, hivyo naomba unijengee nyumba kwani nateseka mno kwa baridi.”

Ntungilija akamjengea nyumba yule zimwi. Baada ya kuishi katika nyumba ile kwa siku chache, akajaa mle. Zimwi akamwendea tena Ntungilija na kumwambia,  aende kumjengea ghala. Ntungilija alifanya hivyo. Zimwi alimsifu Ntungilija  kwa uaminifu wake na moyo wa kupenda kuwasaidia wengine, na mle akajaa.

Siku nyingine akamtaka Ntungilija aende mlimani akamtafutie pango kubwa la kuishi ili asihangaike tena.

Ntungilija akaenda kulitafuta lile pango kubwa, akalipata na akarudi kumwarifu zimwi. Hapo wote wawili walikwenda hadi kwenye pango kuliangalia. Walipowasili kwenye pango, zimwi aliingia ndani na kumwambia Ntungilija, “kwa vile humu duniani sijaona kitu kingine ila wewe njoo hapa nikutafune.” Ntungilija akashikwa na huzuni sana akasema, “kwa nini rafiki yangu unataka kunila, kwani huna shukrani kwa mema yote haya niliyokutendea?”

Zimwi akajibu, “kama hukubali, nenda ukawaulize ndugu zako, rafiki zako na mke wako kama kuna mtu  ye yote mwaminifu huku duniani! Ila usinitoroke. Hata kama utanitoroka ninakujua nyumbani kwako!”

Ntungilija akaenda kuwauliza. Nao walishangaa, wakasema, “Ala! Mbona wewe umemtendea mambo mema mengi hivyo, amekushukuru?” Akamwendea mkewe na kumwambia “Napenda kukuaga nakwenda kuliwa na zimwi.” Mkewe akajibu, “Nitakusindikiza ili nikashuhudie jinsi utakavyomezwa.”

Mume na mke wakaanza safari ya kwenda kwa zimwi. Kwa sauti ya kutisha zimwi akamwuliza mwanamke, “Na wewe umekuja huku kufanya nini?” Mwanamke akajibu, “Nimekuja ili kushuhudia jinsi mume wangu utakavyommeza.”

“Toka hapa! Mimi sikutaki wewe mwanamke! Rudi nyumbani kwako.” Zimwi alimfukuza yule mwanamke. Mwanamke akajibu, “siwezi kurudi nyumbani peke yangu, kwa sababu njia tuliyopita ina wanyama wakali wengi mno. Kuna simba na majoka na wengine wengi.

Shing’weng’we alijibu, “Nitakupa dawa ya kuwafukuza wanyama hao wakali. Utaiweka kwenye kiganja na kuipuliza ukisema, “hata simba, majoka kufa na wewe utapata njia ya kupita.”

Mara alipokabidhiwa ile dawa akaiweka kiganjani,  akaipuiliza na kusema “wewe zimwi kufa!” Palepale zimwi akafa. Ntungilija na mkewe wakarudi salama nyumbani.

mummyafrica-3

 

THE TRULY ONE THE CHILD OF THE THING

There was a man named Ntungilija (which means ‘honest’ in English) who was very faithful. He had the habit of helping others. One day, Ntungilija went to the wilderness and met the young of the ogre. It said to him, “When I was born my parents left me with nothing. I do not have a house. So, I beg you to build me a house because I am suffering from cold.”

Ntungulija built the house for the ogre as requested. After living in the house for a few days, the ogre had become so big that it made the house full. The young ogre came back to Ntungilija and told him to go and build him a bigger houe. Ntungilija did it.The ogre praised him for his loyalty and a willingness to help others. The ogre kept expanding. As a result, this other house was also full.

One day, the ogre asked Ntungilija to go to the mountains and find a great cave for it to live.

He went to look for the big cave as requested.  He found it and came but to inform the ogre. Both the ogre and Ntungilija went up to the cave to examine the cave. When they came to the cave, the ogre came in and told Ntungilija, “Since here on earth I have not seen anything else but you come here so that I eat you” Ntungilija was very sad and said, “Why do you my friend want to eat me? Don’t you have thanks for all this good I have done to you?”

The ogre replied, “If you don’t agree with me, go and ask your relatives, friends and wife if anyone is honest here on the earth! Don’t leave me. Even if you run away I know you in your home!”

Ntungilija went to ask them. And they were marveled, saying, “Aha! Why have you done such good things to it, thank you?” He went to his wife and told her, “I am going to be eaten by the ogre.” His wife replied, “I will accompany you just to witness you being swallowed by the ogre.”

The husband and wife set out the journey to the cave. In a frightening voice, the ogre asked the woman, “And what have you come here for?” The woman replied, “I have come to witness how you will swallow my husband.”

“Get out of here! I didn’t want you woman! Return to your home.” The ogre ordered the woman. The woman replied, “I can’t go home alone because the way we have gone through has many wild animals. There are lions and dragon and many others.”

The ogre replied, “I will give you some medicine to drive those wild animals. You will put it on the palm of your hand and blow it out, saying, “Let the lions die and you will find a way to pass.”

As soon as she was given the medicine and put it in her hand’s palm, she turned to it blew the medicine saying, “You ogre die!” Immediately the ogre died. Ntungilija and his wife went home safely.

106. Jigano Ja Ng’wa bahati

Collected by: Don Sybertz, Scanned by: Cephas Yao Agbemenu

With special thanks to Rev Joe Healey (African proverbs,Sayings and stories)

Waliho nkima uyo walina ng’wana umo. Lushiku lumo ng’wana ng’wenuyo akamisha nsati. Nina akanaja ng’wana mu kaya, uja kujukobha bhugota halinzenganwa.

Guko atali kwinhwa bhugota, wahayimanila ubhona numba yakwe ilibhaka moto. Nkima ng’wenuyo upela wangu wangu kuja ko. Aho washika wingila mu kaya na kunsomba ng’wana wakwe. Umandila ha shikubha atizupya moto. Aliyo unina upya pye umili, wita malonda kufumila ku magulu kushika kuntwe.

Aho wapila usaga na malanda mili pye. Ihanga lyakwe lyubhipa no. Ng’wana ng’wenuyo witanagwa Bahati. Aho wakula uyuja kujigusha na bhana bhiye, bhalinseka na bhaling’wila giki, “Limayu lyako libhi no, lilini hanga litilyawiza. Utubhonaga bhamayu bhise umo bhali bhusheku.

Bahati aho wawilwa chene, wandya kundalaha unina. Lushigu lumo akamuja unina, “Iki bhuli mayu uti ni hanga lya wiza? Bhuli mili gwako guli na malanda pye? Kufumila kuntwe kushika kumagulu?” Nina akansombolela umo yali, “Ng’wana wane aho utali ndo, numba ikapya moto. Nu bhebhe walulalile mumo, nakingila mukaya kukusola nukubhandila ha shikubha utizupya moto. Hi chene ulinibhona nalina malanda pye umili. Iki bhebhe nakutogilwe.”

Bahati aho wigwa giko akayegano, akamana giki, mayu wane wa ng’hana. Uyubhawila na bhiye, “Lolagi mayu umo anitogelilwe, abhakilile na bhamayu bhing’we.” Kufumila lushiku lwene, walatalekaga kunumbilija nina. Na akanela chiza no umu bhugikulu wakwe.

Hadithi  Ya Mtoto Bahati

Alikuwepo mama mmoja, aliyekuwa na mtoto mmoja. Siku moja mtoto huyo aliamka mgonjwa. Mama alimlaza mtoto ndani ya nyumba. Alikwenda kutafuta dawa kwa jirani, kabla hajapewa dawa alishitukia akaona nyumba yake inawaka moto. Mwanamke huyo akakimbia haraka haraka kwenda huko. Alipofika akaingia ndani na kumchukua mtoto wake. Alimkumbatia kifuani ili asiungue na moto.

Lakini mama yake aliungua mwili wote, alipata madonda kutoka miguuni hadi kichwani. Alipopona akabaki na makovu mwili wote. Sura yake ikaharibika mno. mtoto huyo alikuwa anaitwa Bahati. Alipokua alikuwa anakwenda kucheza na watoto wenzake. Huku wakimcheka na kumwambia kwamba, “Mama yako ni mbaya mno, ana sura isiyo nzuri, huwaoni mama zetu walivyo laini.”  Bahati alivyoambiwa hivyo, akaanza kumdharau mama yake.

Siku moja akamwuliza mama yake, “Kwa nini  mama huna sura nzuri?, Kwa nini mwili wako una makovu wote? Kutoka kichwani hadi miguuni?”  Mama yake alimweleza jinsi ilivyokuwa. “Mtoto wangu ulipokuwa bado mdogo, nyumba iliungua moto, na wewe ulikuwa umelala humo. Niliingia ndani nikakuchukua nikakukumbatia kifuani. Ndivyo unavyoniona kuwa nina makovu mwili wote. Kwa kuwa wewe ninakupenda mno.”

Bahati aliposikia hivyo alifurahi mno akajua hivi,  Mama yangu ni wa kweli akawa anawaambia na wenzake, “Angalieni  Mama anavyonipenda, anawazidi hata mama zenu.”  Tokea siku hiyo  alikuwa haachi kumshukuru mama yake.  Na alimlea vizuri mno katika uzee wake.

ice-cream-

ENGLISH: BAHATI’S STORY

There was one woman who had one child. One day, the child woke up sick. The mother laid her on the bed inside the house. Then she went to her neighbour’s house to ask for a medicine. Before the woman was given the medicine, she saw her house burning.

She hurriedly returned home. When she arrived there, she went inside and took out her baby. She put her in her bosom so that she couldn’t get burnt.

But various parts of the woman’s body got burnt. After the wounds had healed, she had scars all over her body. Her face had been badly damaged.

The child was given the name Bahati. As Bahati was growing up, she used to play with her fellow children. Her friends laughed at her and often said to her, “Your mother is so ugly, she has bad skin, but each of our mothers has smooth skin.” As a result, she began looking down upon her mother.

One day, she asked, “Mother, why don’t you have beautiful skin? Why are there many scars on your body?” Her mother said to her, “When you were still young, the house went up in flames and you were inside, sleeping,” she said. “I went into it and carried you in my chest. Various parts of my body got burnt. That is the source of all the scars you see on my body. I did it because I love you very much.”

After hearing the story, Bahati became very happy. One day, as she was playing with her friends, she said to them, “My mother loves me very much. She loves me more than your mothers do you.” And she took good care of her mother in her old age.

105. Wikumbwa bhugabhulagaga

Collected by: Don Sybertz,

With special thanks to Rev Joe Healey  (African proverbs,Sayings and stories)

Oliho munhu umo, mu chalo jilebhe uyo otegaga  ndimu bho gutumila waya. Lushugu lumo uningi ng’wunuyo agasanga yapujiyagwa mhala na yaliyamala gucha.

Aho waitaligulila uwaya ubho bholibhoibhulaga, aha mhelo yaho agagabhona mashi madoto ga mbogo. Uningi ng’wunuyo agaileka imhala yakwe, na wandya gugalondeja amabhondo ga mbogo.

 Ubhulingisilo bhokwe bholi giki, ulu niodula guipandika niwandya guipeja, na ku namna yose iki mbogo nayo umo ili nhali, ni yanondeja na gumpeja.

Uningi ng’wunuyo agiyamini giki agupela lugendo lukali giki mpaga imbogo nidadulile ugumpandika. Huna niobhita ahenaho aha ntego gokwe, ku giki ndimu yiniyo uluyashiga aha ntego gokwe niyapujiwa.

Aho oja lugendo luguhi, ohaimanila otung’wana bhilolile ni mbogo. Imbogo igandya gunkalihila uningi ng’wuniyo. Gashi uningi uyo aladabhejije imipango yakwe jisoga.

Aho obhona giki imbogo yabhunja bho wangu wangu, uningi agapelela mulinti ku giki ugulinhe apandike gupila. Imbogo igapelela wangu wangu na ku bhukali aho olili yugansanga alikoyakoya gulinha mulinti na gunshindika kule, aliyo idamulagile.

Bhasi, imbogo aho inga uningi widuta guja kaya bho nduhu gubhita gujusola untego gokwe, imhala. Aho jabhita shigu idatu, ihali yakwe yubhiza yabhipa noi, ulushugu ulo katano agazumalika musi.

Abha kale bhagahayaga giki, munhu ilinhadikija gurizika nijo uliojipandika, kukila gubhiza na wikumbwa bhutale. Uyo ahaile yose agagaiyagwa yose.

KISWAHILI: TAMAA HUUA

Kulikuwa na mtu mmoja katika kijiji fulani ambaye alikuwa akitega wanyama kwa kutumia nyaya. Siku moja mwindaji huyo alikuta amenasa paa na tayari amekwisha kufa. Baada ya kumfungua waya uliomuua, pembeni aliona kinyesi kibichi cha Nyati. Mwindaji huyo akamwacha paa wake pale na kuanza kufuata nyayo za Nyati.

Lengo lake lilikuwa kama angeweza kumkuta angeanza kumkimbiza, na kwa vyovyote vile naye nyati alivyo mkali angemfuata na kumkimbiza. Mwindaji alijiamini kuwa atakimbia mwendo kasi sana hata Nyati asingeweza kumkuta. Ndipo angepita pale kwenye mtego wake, ili Nyati yule atakapofika kwenye mtego wake ungemnasa.

Baada ya mwendo mfupi, ghafla akakutana na yule Nyati uso kwa uso. Nyati akaanza kumfokea yule mwindaji. Kumbe mwindaji huyo hakusuka mipango yake vizuri. Alipoona Nyati anamkimbiza kwa kasi, mwindaji alikimbilia kwenye mti ili akwee apate usalama. Nyati alikimbia kasi na kwa hasira hadi pale alipokumkuta anatapatapa kuukwea mti na kumsukumiza mbali, lakini hakuuawa. Basi,  Nyati aliondoka, naye mwindaji akajikokota kwenda nyumbani kwake bila hata ya kupita kuchukua windo lake, yaani Paa. Baada ya siku tatu hali yake ikawa mbaya zaidi, siku ya tano alifariki dunia.

Wahenga wanasema kuwa mtu anapaswa kuridhika na kile alichokipata kuliko kuwa na tamaa nyingi. Mtaka yote hukosa yote.

buffalo

ENGLISH: GREED KILLS

There was a man in a village who was trapping animals by using wires. One day, the hunter found that he had trapped an antelope which was already dead. After unlocking the deadly wire of the trap, he saw fresh stool of the buffalo. The hunter left his antelope there and began to follow the footsteps of the buffalo.

His aim was to make the buffalo run after him while he could be running towards the trap. He thought that the buffalo would eventually be caught in the trap. The trapper was confident that he would run faster than the buffalo.

Within a short distance, he met the buffalo face to face. The buffalo began to chase the hunter. It appears that the hunter underestimated the risk that was ahead of him. When he realized the buffalo ran faster that he estimated, the hunter ran to a tree to save his life. The buffalo reached him trying to climb the tree. The buffalo attacked him but he did not die.

Theafter, the buffalo left and the hunter went to home without even taking his meat of the antelope that he had trapped. After three days his condition worsened, and on the fifth day he died.

The sages have it that one should be satisfied with what he has earned and should not have have much desire. The one who wants all, misses all.

104. Wikumbwa/Bhulaku Bhubhi (Tamaa/Uroho Mbaya)

Collected by: Don Sybertz,

With special thanks to Rev Joe Healey  (African proverbs,Sayings and stories)

Aho kale agikala munhu umo lina lwakwe Lambwe. Munhu ng’wunuyo a-oliontola nkima o chalo ja kule. Yahaiyagwa giki u Lambwe adadulile ugupanke nkima ogutola umuchalo jakwe.

Olina jika jakwe. Oli atogilwe noi ugulwa nyama. Ulushugu ulo opandikaga nyama ohagigishaga igiki aliilya pye wei ng’winikili. Lambwe wiimililaga wei ahikanza ilizugwa inyama iniyo, ku giki adizigela munhu ose ose oguikumya nulu haho itali ugupya.

Makanza gose u Lambwe ozubhulaga inyama ijitinile manofu haho yandya gupya du wandya gujidakuna bho bhulaku bho gukumya. Abhabehi abho bhikalaga bhuzenganwa na bhabyaji bha ng’wa Lambwe bhagaduma gete ugung’wambilija unsumba ng’wunuyo.

Giko, inhungwa jakwe ijabhubhi jigamanyika bhuli kuli munhu uomu chalo jinijo. Mpaga oho okula wikoma gutola, bhuli ng’wenu uyo agang’wisonga agannema.

Aho obhumana ubhubhi bho nhungwa jakwe, agiyangula gujutola kuchalo ja bhuzenganwa. Gashi nu mu chalo ja bhuzenganwa inhungwa jakwe jali jimanyikile.

Lambwe iganhadikija gusunga lugengo lo guja kule uko agwigela giki ali ngeni gete. Agakoyakoya mpaga ku si ngeni ndebhe, uko agang’wisonga ng’waniki uyo witangwa Mugoli.

Ukubhu nghana Mugoli oli ng’waniki nsoga na o likujo na nhungwa ja wiza. Bhagizunilija gwitola. U Lambwe aho oshoka umu chalo jakwe kihamo na nke okwe u nsoga, gugabhibhakija bhanhu bhingi.

Olinduhu nulu umo umu chalo jakwe uyo wiganikaga giki u Lambwe niodula guntola nkima nsoga giti Mugoli! Wikaji bho ng’wa Lambwe na Mugoli bholi bhusoga na bhanhu bhagakumya pye.

Uwikumbwa bho ng’wa Lambwe ubho guhaya gulwa inyama yose bhugendelea. “Wifunya bhukindile bhusese”, Mugoli adadililile noi inhungwa ja ngoshi okwe kulwa nguno jalinduhu jika jingi umu witogwi bhobho.

Nose bhagapandika bhana bhadatu. Bhuli ng’wana ulu okula, oshiga bhukuji bhulebhe, ochalagwa gujumanyichiwa kuli guku obho. Unimo gogubhachala abhana bhanabho goli go ng’wa Lambwe.

Lambwe obhachala bho ndima abhana bhakwe ukuli nkwiye. Inzila ya guja kunuko igabhita ng’wipolu lya ndimu nhali. Lushigu lumo, Lambwe agaja gujubhagisha bhakwiye, aho oshika koi, agamana igiki ung’wana okwe uumo alianogile ugwikala aha kaya ya ng’wa guku na mama okwe. Agandya gulila. Lambwe agiyangula gushoka nawe.

Aganomba umayu bhukwi jiseme ja gubhukija jiliwa na jifaa jingi ja ng’wanokwe. Mayu bhukwi agamegelegeja bhuli ginhu. Lushigu lo kabhili dilu, Lambwe agandya lugendo lokwe ukunu amukije ung’wanokwe ku ngongo. Ali adibhile ugubhucha inhome, ichimu ni panga.

Aho oshika ung’wiporu linilo agigwa malaka ga noni jilimba ulu luli lumengho lwa giki jabhonaga ndimu. Agogoha noi mpaga wikumbwa gushoka uko ofumaga.

Kihamo ni yiniyo adashokile inuma, kulwa nguno ulugendo lokwe lolilomala mapande adatu ga lugendo, lyalilyasaga ipande limo du mpaga ashige ku kaya.

Agendelea na lugendo lokwe na ukunu inoni jinijo jilongeja guyoganya malaka. Aho olola lwande lumo lo nzila, agibhona Mboku ilalile. Ujipeja inoni jinijo, wiyegela ndimu yiniyo.

Igwandya wiganikaga giki imboku yiniyo yaliilalile oganoga umana igiki gashi yali yamala gucha ikanza idili lihu ilo lyabhitaga. Ku yiniyo, indimu yali itali ugundya ugubhola.

Agandya gwita lusona kuti nu bhulaku bhokwe ubhobholibhomtema umu nyama. Agasola panga yakwe na gutina linofu litale iliginu, agalituula lwande. Lambwe oladamanile igiki imboku yiniyo yaliyabhulagwa na shimba.

Gashi aho likanza alitina inyama yiniyo, ishimba yaliifulile hambeho aho yamalaga gwiguta. Ninga iki yalidikule ugufuma ahenaho, aliyo u Lwambwe adibhonile.

Ninga ulu nioibhona wangu nadagemile ugwegela aha nyama ya mboku yiniyo. Ahenaho, U Lambwe agang’wicha ung’wanokwe na gung’wigasha hasi ukunu uwei ng’winikili agachola manti ga gubegesa moto. Aho obhiza kule hadoo inoni ijo jigashoka na guyoganya umu nyama na gwandya guigombagula inyama yiniyo.

Ishimba nayo igakolwa ugubhona giki inoni jinijo jiliichafula inyama yayo yiniyo. Wangu wangu, ishimba igaja gujujipeja inoni na gwendelea kuilya inyama.

Ung’wana o ng’wa Lambwe bho nduhu gumana agiyegela ishimba bho nduhu bhobha, na gwandya guibabasha giti umo umunhu agibabasijaga imbwa.

U Lambwe aho oshoka ahenaho agibhakila uguibhona ishimba yigundamilaga guidakuna inyama yiniyo. Agahugana ugumona ung’wana okwe aliibabasha ishimba ukungongo bho nduhu bhobha.

U Lambwe agading’wa na lutuga. Adamanile ijagwita. Aho ohaya gung’wegela ishimba igalunduma na gumpeja gitumo yajipegejaga inoni. Ung’wanokwe adibhakile, agendelea du uguibabasha ukungongo.

Ishimba yalidinawasiwasi bhosebhose nu ng’wana ng’wunuyo. Ishimba igendelea gumpeja u Lambwe, nanghwe odubukaga nhambo. Agabhona niyabhiza jidamu ugudula gwibhulaga ishimba yiniyo wei bhung’wene.

Aho oli kule hadoo Lambwe agandya gung’witana ung’wanokwe. Aho ung’witana kuli likanza lilihu, ung’wana agang’wigwa ubhabha okwe huna ugandya gung’wegela.

Aho obhona giki ung’wanokwe aliza, Lambwe agaigwa ingholo yakwe ilitinhinha na bhuyegi. Ikanza iguhi ung’wana agang’wegela, aganfefula na gumhucha kungongo. Wangu wangu agandya lugendo akajije wangu wangu guja kaya. Makanza gose omanaga ulabhula na gulalo inyuma kugiki gumana ulu idanondejije ishimba.

Aho oshika ikaya, unke agakumya aho omona ungoshi adina jilanga nulu jibhukijo ja ng’wana. Aho atali aleshema kubhobha ubho alinabho bhundimilile na ku bhunoge bho lugendo na nzala, Lambwe agandya kunomela unke okwe, pye iyose iyo igampandika umu legendo lokwe. Unke agading’wa na bhukoyakoi na agang’wila ungoshi alekane nu bhulaku bho gulwa nyama bho sagala giti umo yali uko numa.

Kiswahili: Tamaa/Uroho Mbaya

Hapo Zamani palikuwa na mtu mmoja, jina lake Lambwe. Mtu huyo, alikuwa amemuoa mwanamke wa kijiji cha mbali. Inasemekana kwamba Lambwe hakuweza kupata mchumba katika kijiji chake. Alikuwa na kasoro yake, Alipenda mno kula nyama. Siku akipata  nyama, alihakikisha kuwa anaila yote yeye peke yake.

Lambwe alisimamia wakati inapikwa nyama ile, ili asiwepo mtu ye yote wa kuigusa hata kabla haijaiva. Daima Lambwe alichopoa vipande vya nyama mara tu inapoanza kuiva na kuitafuna kwa uchu wa ajabu.

Jamaa wakiokuwa wanaishi jirani na wazazi wa Lambwe walishindwa kabisa kumsaidia kijana huyo. Hivyo, tabia yake mbaya ilijulikana na kila mmoja katika kijiji.

Hata alipopata umri wa kuoa, kila liyemchumbia alimkataa. Lambwe alipotambua utovu wa tabia yake, aliamua kwenda kuoa kijiji cha jirani. Kumbe hata katika vijiji vya jirani habari zake zilisambaa.

Lambwe ilimpasa kufunga safari ya mbali ambako ataonekana ni mgeni kabisa. Alihangaika hadi nchi ngeni fulani, huko alimchumbia msichana mzuri aliyeitwa Mugoli.

Kwa kweli Mugoli alikuwa mrembo na mwenye adabu na tabia nzuri. Wakakubaliana na kuoana. Lambwe aliporejea kijijini kwake pamoja na mke wake mrembo, kuliwashtusha watu wengi. Hakuna hata mmoja pale kijijini alifikiri kuwa Lambwe angeweza kumwoa mwanamke mzuri kama Mungoli! Maisha kati ya Lambwe na Mugoli yalikuwa mazuri na yakawastaajabisha wote.

Tamaa ya Lambwe ya kutaka kula nyama yote iliendelea. Hiari yashinda utumwa, Mungoli hakujali sana tabia ya mumewe kwa sababu vinginevyo hapakuwa na kasoro nyingine katika mapenzi yao.

Hatimaye, walijaliwa kupata watoto watatu. Kila mtoto alipofikisha umri fulani, alipelekwa kutambulishwa kwa babu yake, jukumu la kuwapeleka watoto  hao lilikuwa la Lambwe.

 Lambwe aliwapeleka kwa zamu watoto wake kwa mkwewe. Njia ya kwenda huko ilipita katikati ya pori lenye wanyama wakali. Siku moja, Lambwe  alikwenda kuwasalimia wakwe zake, alipofika  huko, aligundua kuwa mtoto  wake mmoja alikuwa amechoka kuishi nyumbani kwa babu na bibi. Alianza kumlilia, Lambwe akaamua kurudi naye.

Akamwomba mama mkwe chombo cha kubebea chakula na vifaa vingine vya mwanae. Mama mkwe alimtayarishia kila kitu. Siku ya pili asubuhi, Lambwe alianza safari yake akiwa amembeba mwanae mgongoni. Aidha, hakusahau kubeba rungu, mkuki na upanga.

Alipokuwa katika pori lile alisikia sauti ya ndege wakiimba ikiwa ishara kuwa walimwona mnyama. Aliogopa sana hata akatamani kurudi alikotoka. Hata hivyo hakurudi nyuma, kwani safari yake ilikuwa imefikia robo tatu na ilibakia robo moja tu hadi awasili nyumbani.

Aliendelea na safari yake na huku wale ndege wakiongeza kupaza sauti. Alipoangalia upande mmoja wa njia, alimwona Pofu amelala. Akawafukuza wale ndege, akamsogelea yule mnyama.

Awali alifikiri kuwa pofu yule alikuwa amelala, lakini baadaye  aligundua kuwa kwa kweli alikuwa amekufa si muda mrefu umepita. Kwa hiyo nyama yake ilikuwa bado kuoza.

Mate yakaanza kumdondoka kama uchu wake ulivyomtawala akiona tu nyama. Alichukuwa upanga wake na kukata kipande kikubwa sehemu iliyonona, akaiweka kando.

Lambwe hakufahamu kuwa yule Pofu alikuwa ameuawa na simba. Kumbe wakati akiwa anakata ile nyama, simba alikuwa amejipumzisha kivulini baada ya shibe. Ingawa hapakuwa mbali kutoka pale, lakini Lambwe hakumwona. Laiti angemwona mapema asigethubutu kuusogelea ule mzoga wa pofu.

Hapo, Lambwe akamteremsha mtoto wake na kumkalisha chini huku yeye mwenyewe akienda kutafuta vijiti vya kupekechea moto. Alipokuwa mbali kidogo wale ndege wakarejea na kupiga kelele kwenye ule mzoga na kuanza kudonoa ile nyama. Simba naye alikasirika kuona kuwa wale ndege wakiichafua ile nyama yake. Haraka, simba alikwenda kuwafukuza wale ndege na kuendelea kula nyama.

Mtoto wa Lambwe bila  kujua alimsogelea Simba bila woga, na kumpasapasa kama vile binadamu anavyompapasa Mbwa. Lambwe aliporejea pale alishitushwa kumwona simba ameinamia kutafuna ile nyama.

Alichanganyiwa alipomwona mtoto wake anampapasa Simba mgongoni bila woga. Lambwe akashikwa na kiwewe. Hakufahamu la kufanya. Alipotaka kumsogelea, Simba aliunguruma (alifoka) na kumfukuza kama alivyofukuza ndege.

Mtoto wake hakushituka, bali aliendelea tu kumpapasa mgongoni. Simba hakuwa na wasi wasi wowote na yule mtoto. Aliendelea kumfukuza Lambwe, naye alikuwa akifyatua mbio.

 Aliona ingekuwa vigumu kuweza kumwua yule Simba peke yake. Alipokuwa mbali kidogo Lambwe alianza kumwita mtoto  wake. Baada ya kumwita kwa muda mrefu, mtoto alimsikia baba yake ndipo alipoanza kumsogelea.

Alipomwona mtoto wake akija, Lambwe aliusikia moyo wake ukimdunda kwa furaha. Mara mtoto alipomkaribia, alimyakua na kumbeba mgongoni. Hima akaanza safari chapuchapu kwenda nyumbani. Daima alikuwa akigeuka na kuangalia nyuma ili kuona kama Simba alimfuata.

Alipowasili nyumbani, mkewe alishangaa alipomwona mumewe hana silaha wala mbeleko. Akiwa bado anahema kwa hofu iliyomwandama pamoja na uchovu wa safari na njaa, Lambwe alianza kumweleza mkewe kisa chote kuhusu yale yaliyowapata katika safari yao. Mkewe alishikwa na mfadhaiko na akamkanya mumewe kuachana na uchu wa kula nyama kwa pupa kama ilivyokuwa huko nyuma.

mammal-

English: Bad Desire/Greed

black-

 

BAD DESIRE/GREED KILLS

In the past, there was one man whose name was Lambwe. Such a man had married a woman from a far away village. It is said that Lambwe could not find a girl in his home village. He had his one defect. He loved meat very much. Whenever he found meat, he made sure that he ate all of it alone.

Whenever meat was cooked, Lambwe was in charge. He could closely observe so that no one could touch the meat even before it was cooked. Lambwe always handled the pieces of meat as soon as it began to be cooked. He could grab it with a strange desire.

Relatives living near Lambwe’s parents were unable to help the boy deal with that greed. This strange behaviour was known to everyone in the village.

When he wanted to get married, everyone refused him. When the Lambwe realized his behavior was not accepted, he decided to go to a nearby village. Even in the neighbouring villages his bad news about him spread.

Lambwe had to travel to a distant place where he was a stranger. He struggled until he finally married a beautiful girl named Mugoli.

Mugoli was beautiful and courteous and well behaved.. When Lambwe returned to his village with his beautiful wife, he shocked many people. No one in the village thought that Lambwe could marry a beautiful woman like Mugoli! The life of Lambwe and Mugoli was beautiful and wonderful.

Lambwe’s desire to eat all the meat continued. Optionally conquered slavery, Mugoli did not care about her husband’s behaviour because otherwise there were no other defects.

Finally, they were blessed with three children. When each child reached a certain age, he was taken to the village to be introduced their grandfather. The responsibility of taking the children to the village was Lambwe’s.

Lambwe took his children to his mother-in-law in shifts. The way to the village went through a a big forest with wild animals. One day, Lambwe went to greet his parents–in- law. When he got there, he found out that one of his children had been tired of living with grandparents. He started crying. Lambwe decided to bring him back.

He asked his mother-in-law something for carrying food and other items for his son. His mother-in-law prepared everything for him. The next morning, Lambwe started his journey,carrying his son on his back. In addition, he did not forget to carry a club, a spear and a sword as was the custom.

When he was in the wilderness, he heard the voice of the birds singing as a sign that theyhad seen a beast. He was so frightened that he wished to go back where he came from. However, he did not go back, as his journey had reached three quarters and only one quarter remained for him to  arrive home.

He went on his way with the birds singing even more loudly. As he looked on one side of the rpath, he saw an eland lying.  He drove out the birds, and came to the beast.

At first, he thought that the animal was asleep. But sooner or later he found that it was actually dead not long ago. So his flesh had not yet decayed.

Lambwe started salivating. He took his sword and cut a piece of that fat eland, and put it aside.

Lambwe did not know that the eland had been killed by the lion. But when Lambwa cut the meat, the lion had rested in the shade after eating enough. Although it was not far from there, but Lambwe did not see it. If he had seen it before, he would not have dared to move to the carcass of the eland.

There, Lambwe dropped his baby and laid him down while he was looking for fire sticks as he wanted to make fire in order to roast the eland’s meat. From a distance the birds returned and shouted at the carcass and began to draw the meat. The lion was also angry to see that the birds were defiling its flesh. Immediately, the lion went to chase the birds and continued to eat meat.

Lambwe’s child did not know to approach the lion with fear, and he kept touching the lion as he touches a dog. When Lambwe came back, he was shocked to see the lion chewing the meat.

He was confused when he saw his son touching the lion on the back without fear. He was caught in trauma. He did not know what to do. When he wanted to move, the lion roared ( angrily) and dismissed him as he drove away the birds.

His child did not panic, but he just kept touching the lion on its back. The lion had no trouble with the baby. The lion continued to chase Lambwe whenever he came closer.

 Finally, Lambwe realized that it would be impossible for him to kill the lion alone. Lambwe then decided to call his son from a far. After calling him for a long time, the child heard his father and he slowly approached oblivious of the danger that surrounded them.

When he saw his son coming, Lambwe felt his heart beating with joy. As soon as the child reached him, he snatched him and carried him on his back. He hurriedly started going home. As he walked home, he was always turning back and looking behind to see if the lion was following him.

When he got home, his wife was surprised to see him without weapons and without  a piece of cloth for carrying the child with. While he was still filled with the fear and the fatigue of the journey, Lambwe started to tell his wife all about what had happened on the journey back home. His wife was depressed and she warned her husband that he should stop his excessive desire for eat meat.

103. Wibhakizu (Hofu) Bhugenhaga Lufu

Collected by: Don Sybertz,

With special thanks to Rev Joe Healey  (African proverbs,Sayings and stories)

Ikale iyo oliho msumba umo witanagwa Kisho. Unsumba uyo olina bhumani (maarifa) noi. Bhabha okwe oliamanyikile mu lina lwa Mapali, agantogwa noi u Kisho.

Aganchala ung’wanokwe agandye shule kugiki asome. Kisho agayega noi ugupandika wasa bhunubho bho guja gujelimiaka ku shule. U Kisho aho omala chiza ielimu ya msingi agachagulwa guja ku sekondari.

Agita chiza umu masomo gakwe mpaka agamala jidato ja kane. Hangi ulinsumba uyo agitogwa noi ku bhutalamu bho mubhusafi bho mili na myenda. Makanza gose aliabhelelile gete gete. Oli na nhungwa ja gudilila bhutalatibhu bho afya bhose ya gwikala na afya ya wiza na wikaji bhulihu.

Lushugu lumo, aho bhalyaga aganomba ntumami okwe ang’wenhele minzi ga gung’wa. Untumami uyo agamana hape gete igiki Kisho alatogilwe gung’wa minzi umo glasi uyo ilinsafi na idina jika.

Umtumami agang’wenhela minzi umu glasi nsafi noi. Aho Kisho omala ugung’wa aminzi, agabhulucha ginhu jilebhe jigasagila umugati ya glasi yiniyo.

U Kisho agajikisia giki iginhu jinijo jali ighi lwa ngoku, wangu wangu agaja ku kusitali gujumhona Daktari. “Bhebhe daktari, nagang’wa minzi mabhi. Naliganikila giki nang’waga maghi ga ngoku. Hambo hambo naligulomba ugafunye wangu wangu amaghi genayo gafume umunda yane.

Udaktari agakumya noi ugwigwa mihayo yiniyo. Aganomela u Kisho. “Udizubhiza na bhuhangayiki. Nadiganikaga igiki uguding’wa na bhusatu bhose bhose.

Ulu ulading’we na bhusatu bhosebhose nzugu aha wangu wangu kugiki upandika bhulaguzi!” UKisho adazunije ubhulomeji bho ng’wa Daktari. Agang’wila u Daktali, “Bhuli nagalangwa kushule ihatari ya maghi ga ngoku. Ku yiniyo, nadizunilijaza nu bhebhe. Hambo hambo daktari itaga iyoudulile ugugafunya amaghi genaya ni lelo iyi, badala ya gulindila mpaga ntondo nandya gusata.”

“Nahene, jijaha ijidonge ja gung’wa, jibhili lushulu mara gadatu. Udulile guja kaya.” Agayomba udaktari.

Aho alimunzila ajile ikaya, u Kisho agiigwa giki umunda jigandwa gulunduma. Uding’wa wibhakizu. Bhukoyakoyi bhugendelea mpaga adahayile ugulwa ijiliwa ija mhindi yiniyo, nulu gung’wa minzi adagemile.

Aho oja gujulala adapandikile itula bhujiku pe alimiso. Aho wela du, Kisho agaja hangi kusitali. Aho daktari opandika ubhulomeji bhulihu gufuma kuli Kisho, agamana giki unsumba ng’wunuyo alina wibhakizu (hofu) noi.

“Jaga ugenhe kalishi (choo) na mine kugiki dudule gujipima, daktari aganomela u Kisho. Udaktari agakomeleja giki opimaga, gashi adapimile josejose.

Agashoka ukunu odimaga glasi yina ighi giti ilo ololibhona u Kisho uko kaya yakwe. Udaktari agang’wolekaja u Kisho iglasi yiniyo na gung’wila, “Lolaga aha ni lighi linilo ilo uliolibhona ilikanza ilo ong’waga minzi. Lwafumaga kunguno ya bhugota ubho ubhumilile. Ihaha udizubhiza na wibhakizu (hofu) hangi.  Jaga gukaya yako na bhuyegi.” “Lo! Obheja noi daktari,” agalumbilija u Kisho ukunu abhizile na bhuyegi bhutale. Agashoka kaya na gwendelea gwikala guti kawaida bho nduhu wibhakizu (hofu).

Udaktari uyo ulu nadatumilile maarifa ga gung’wingija ihofu, Kisho niwendelea gusata ikanza ilihu mpaga gwenheleja nulu gucha kulo hofu.

Kiswahili: Hofu Huleta Mauti

Zama hizo kulikuwa na kijana mmoja aliyeitwa Kisho. Kijana huyo alikuwa na maarifa sana. Baba yake alijulikana kwa jina la Mapali, alimpenda sana Kisho. Alimpeleka mwanaye shule ili apate kusoma.

 Kisho aliifurahia sana nafasi ya kwenda kuelimika shuleni. Alipohitimu vizuri elimu ya msingi alichaguliwa kujiunga na elimu ya sekondari. Alifanya vizuri katika masomo yake hadi alipohitimu kidato cha nne.

Aidha alikuwa ni kijana aliyejipenda sana kwa usafi wa mwili na mavazi, daima alikuwa mtanashati kweli kweli. Alikuwa na tabia ya kuzingatia kanuni zote za afya kwa ajili ya kuishi na afya bora na maisha marefu.

Siku moja, wakati anapata chakula, Kisho alimwomba mtumishi wake ampatie maji ya kunywa. Yule mtumishi alifahamu wazi kabisa kuwa Kisho alipenda kunywa maji katika glasi safi isiyo na doa.

Mtumishi huyo alimletea  maji katika glasi safi sana. Baada ya Kisho kuyanywa aligundua kitu fulani kilibaki ndani ya ile glasi. Alihisi kuwa kile kitu kilikuwa ni yai la konokono,  haraka akaenda hospitali kuonana na daktari. “Bwana daktari, nilikunywa maji machafu. Nahisi nimemeza mayai ya konokono. Tafadhali nakuomba uyatoe haraka mayai hayo kutoka tumboni mwangu.”

Daktari alishangaa sana kusikia maneno yale. Akamweleza Kisho, “Usiwe na wasiwasi. Sidhani kuwa utashikwa na ugonjwa wowote. Endapo utashikwa na ugonjwa wowote njoo hapa haraka ili upate matibabu!” Kisho hakuamini maelezo ya daktari. Akamwambia yule daktari, “Mbona nilifundishwa shuleni hatari ya mayai ya konokono. Kwa  hiyo, sikubaliani nawe. Tafadhali daktari fanya kila unaloweza kuyatoa mayai hayo leo hii, badala ya kungojea hadi nimeanza kuumwa.”

“Haya, hapa ni vidonge vya kumeza, viwili kutwa mara tatu. Unaweza kwenda nyumbani.” Alipokuwa njiani kurejea nyumbani, Kisho alisikia tumbo lake likianza kuunguruma. Akashikwa na hofu.

Wasiwasi huu uliendelea hata hakutaka kula chakula jioni ile, wala kunywa maji. Alipokwenda kulala, hakupata lepe la usingizi usiku kucha. Kulipokucha tu,  Kisho alikwenda tena hospitalini. Baada ya daktari kupata maelezo marefu kutoka kwake, alitambua kuwa kijana huyo alisongwa sana hofu.

“Nenda kalete choo na mkojo ili tuweze kuvipima,” daktari alimwelekeza Kisho. Daktari alisingizia kuwa amepima, kumbe hakupima chochote. Akarudi huku ameshika glasi yenye yai kama lile aliloliona Kisho kule nyumbani kwake. Daktari alimwonyesha Kisho ile glasi na kusema, “Tazama hapa ni lile yai ulilolimeza wakati ukinywa maji. Limetoka kwa sababu ya zile dawa ulizomeza. Sasa usiwe na hofu tena. Nenda nyumbani kwako kwa furaha.” “Lo! Asante sana daktari,”  Alishukuru Kisho huku akiwa na furaha kubwa. Akarudi nyumbani na kuendelea kuishi kama kawaida bila hofu.

Kama daktari yule asingetumia maarifa ya kumtoa hofu, Kisho angeendelea kuugua muda mrefu hata kusababisha kufa kwa hofu.

FEAR CAUSES DEATH

There was a young man named Kisho. Such a young man had a lot of knowledge and skills. His father was known as Mapali. The father loved Kisho very much. When school going age, his father took Kisho to school.

 Kisho enjoyed the opportunity for going to school very much. When he completed primary education, he was selected to join secondary education. He did well in his studies until he graduated at Form Four level of education.

In addition, Kisho was a very young man who loved being smart and clean. He was always smart. He had a tendency to adhere to all health principles. He liked health living and long life.

One day, when he got food, Kisho asked his servant to give him a drink of water. The servant knew very well that Kisho liked to drink water in clean glasses.

The servant brought water in very clean glasses. After Kisho drank, he found something left in the glass. He felt that something was like the snail’s egg, quickly went to hospital to see a doctor. “SDoctor, I drank dirty water. I feel screaming snail eggs in my stomach. Please, hurry up, take these eggs from my stomach.”

The doctor was very surprised to hear the words. Then he told Kisho, “Don’t worry. I don’t think you will get any disease. If you get any illness, come here quickly for treatment!” But he did not believe the doctor’s explanation. He said to the doctor, “I have been taught at school the danger of snail eggs. So, I disagree with you. Please do whatever you can to remove these eggs today, rather than waiting until I get ill.”

“Here, here are tablets for swallowing, two to three times. You can go home”, the doctor instructed him. On his way home, Kisho heard his stomach starting to ache. He was very terrified.

This concern continued. In the evening, he did not want to eat food.  He did not want to drink water either. When he went to bed, he could not sleep all night. Just before dawn, Kisho went back to hospital. After the doctor had received a long explanation from him, he realized that Kisho was only scared.

“Go to the toilet and bring your urine so that we can examine it,” the doctor told Kisho. The doctor pretended to have tested the urine. He came back holding a glass containing egg mixed with water. The doctor showed Kisho the glass and said, “Look, here is the egg you swallowed when you drank water. It has come out because of the medication you are taking. Now don’t be afraid again. Go home happily.” “Oh! Thank you very much doctor,” he thanked Kisho, with great excitement. He returned home and continued to live as usual without any fear.

If the doctor did not use the knowledge of giving fear, Kisho would continue to be sick for a long time even causing death.

comic-

 ENGLISH: FEAR BRINGS DEATH (FEAR LEADS TO DEATH)