Collected by: Don Sybertz, with special thanks to Rev Joe Healey (African Proverbs, Sayings and Stories)
Bhugota wingi ubho jiasili bhumanyikile kulina lya manti ga mumalale. Inguno ya guwitana ghiko, nadamanile. Aliyo igwigwiyagwa giki abhakoloni ahobhashika ulukangala ulogwandya umusi munumu, bhagasanga abhanasi bhagutumilaga bhugota bhunubho, jina gudalaha, bhagawitana bhugota bho mumalale.
Ukulwande lyise bhagikala bhafumu bhingi noi abha kiasili. Abhangi umubhenabho, bhali bhafumu bhawiza. Bhabhalagulaga bhasadu bha mbika ijo nijo na bhapijaga bhusadu bho mbika ningi.
Abhasadu bhenabho bhapilaga sada jabho, ningi iki abhafumu bhenabho bhalombaga hela ningi, abhanhu bhali bhabhatogilwe. Amakanza genayo bhalihoi bhafumu bhangi abho bhitaga jigongwanuma ja umo bhitilaga abhafumu abha kawaida.
Abhanebho bhabhakangaga abhanhu kulwa nguno ya bhumani bhobho. Angu, abhenabho bhitangwa bhalogi. Unimo úntale go bhafumu bhenabho yali gubhalisanya abhanhu ku nzila ya bhulongo bhobho. Angu bhalangaga bhanhu gub’iza na guzunya go bhulogi.
Abhangi bhalombaga kodi nhale, bhagukangilaga gubhabhulaga ulu giki ililagilo lyabho lyukija lidatimijiwe. Bhalihoi bhafumu bhangi abho bhayelayelaga umumachalo, abho bhalibhalomolomo.
Bhali bhadibhalogi aliyo unimo gobho guli guyela na mizwi mingi bhagubhalembaga abhanhu.
Abhangi bhagayombaga giki bhadulile gumeja umunhu abhize nsabhi, aliyo abhoi bhalibhahabhi bha gwandya.
Abhangi bhagihaya giki bhadulile gwenha mbula musi umumakanza ayo imbula yaliyalema. Aliyo abhoi bhapandikaga makoye ga gugaiwa mbula sawa na munhu ose ose.
Abhangi bhayombaga giki angu bhali na bhudula bho gungalucha umunhu ngosha ubhiza nkima, nulu unkima ubhiza ngosha.
Abhangi bhayombaga giki bhalinabho ubhudula bho gungalucha umunhu ubhiza munandimu omumapolu guti shimba, subhi, nulu mbiti. Abhangi angu bhahayaga giki bhalinabhudula bho gungalucha munangoso ubhiza munashimba. Ubhulomolomo bho bhafumu bha namna yiniyo bhulihoi bhulendelea kubhanasi bhingi.
Umumapande gamo ga mulibara lise umumachalo jigadumaga ugwiyenhela amaendeleo kunguno ya gubhogobha bhafumu bha mbika yiniyi. Idijagukumwa ugwigwa giki, angu bhalihoi bhalogi bhangi abho bhuhimbulaga mimba go munhu mumajigila na gubhalimisha mumigunda yabho.
Abhangi bhushigilaga guyomba giki, bhali na bhudula bho gwingika nulu gurala bhadizigela bhojinogu. Ulu ulola ugumana igiki alinduhu umunhu uobhudula bho gukamaja guti bhunubho.
Umapande gangi ugwigwa nhulu ja gukamaja. Bhangi bhagayombaga giki bhalinabhudula bho gwibakela mbiti bhujiku bhusiminza lugendo luliihu gete. Abhangi bhagihajaga giki angu bhalinabhudula bho gufuga shimba na mihayo yingi ya gujinjimaja guti yiniyo.
Aliyo uluulola chiza bho gwitegeleja ugumana igiki pye imihayo yiniyo iliyabhulongo nulu ya bhulomolomo duhui ubho bhutinajimelo. Ilibhujo ilitale ilo bhafumu bhingi bhalidumile ugulishosha na bhangi bhingi abho bhadulile gubhubadija ubhulomolomo bhunubho bhagibhujaga liligiki. Kunguno ki abhafumu pye abhabhagihaya giki bhalinabhudula bho gukamaja guti bhunubho bhadabhizile bhagwandya ugushika ukung’weji?
Isayansi iyagwiganika guti yiniyo na guyiyomba munomo duhui idafaile. Idakililwe yitiwe na bhulimunhu wilolekeje. Ijigongwanuma jaho, ugubhona giki nduhu umfumu uyo alinayo numba insoga nulu uyo aliwinula uwikaji bhokwe nulu hadoo. Ihali iyabhafumu abhingi iliyamakoye noi nulu ya nyahabhi noi, iliyanyakoyikoyi noi. Bhasagila gubhalemba abhanasi na kubhakanga bho bhufumu bhobho ubho bhuti na mpelo.
KISWAHILI: MITI SHAMBA
Dawa nyingi za kiasili hujulikana kwa jina la miti shamba. Sababu ya hizo Dawa kuitwa hivyo, siijui, lakini inasadikiwa kuwa wakoloni walipofika kwa mara ya kwanza nchini humu waliwakuta wananchi wanazitumia dawa hizo, kwa dharau, waliziita miti shamba.
Upande wa kwetu waliishi waganga wengi sana wa jadi. Wengine kati ya waganga hao, walikuwa ni waganga wazuri. Waliwatibu wagonjwa mbali mbali na walitibu magonjwa ya aina nyingi. Wagonjwa wale walipona maradhi yao, ingawa waganga hao walitoza ghalama kubwa, lakini walipendwa na watu.
Wakati huo huo walikuwako waganga wengine ambao walifanya kinyume cha waganga wa kawaida. Hawa waliwatishia watu kwa kutumia ujuzi wao. Hata wakapewa jila la wachawi. Kazi kubwa ya waganga wa aina hii ilikuwa, eti ni kuwaroga wenzao pamoja na watu wengine wasio waganga.
Wengine walidai kodi kubwa, wakitishia kuua kama sharti lao halikutimizwa. Walikuwako waganga wengine ambao walitembeatembea vijijini, hawa walikuwa wadanganyifu. Hawakuwa wachawi, bali kazi yao ilikuwa kutembea na mizizi mingi wakidanganya watu.
Wengine walisema kuwa wana uwezo wa kumfanya mtu awe tajiri, hali wao wenyewe walikuwa mafukara wa kutupwa. Wengine walijidai kuwa wanao uwezo wa kuleta mvua nchini wakati wa shida za ukosefu wa mvua, na wakati huo, wao walizipata shida hizo sawa kabisa na mtu mwingine yeyote.
Wengine walisema kuwa wana uwezo wa kumgeuza mtu mwanamume akawa mwanamke au mwanamke akawa mwanamume. Wengine walisema wanao uwezo wa kumgeuza mtu akawa mnyama wa porini kama vile Simba, Chui au Fisi. Wengine walisikika wakisema kuwa, wana uwezo wa kumgeuza panya akawa Simba. Udanganyifu wa waganga wa aina hii ungali unaendelea kwa wananchi wengi.
Katika sehemu mbali mbali za Bara letu, vijiji vingi vinashindwa kujiendeleza kwa sababu ya kuwaogopa waganga wa aina hii. Si ajabu ukasikia kuwa kuna wachawi wengine ambao hufufua maiti katika makaburi na kuwafanya walime kwenye mashamba yao.
Wengine huthubutu hata kusema kuwa wanao uwezo wa kutoweka au kuruka wasionekane kwa urahisi. Ukitazama utaona kuwa hakuna mtu anayeishi hapa duniani mwenye uwezo wa ajabu kama huo. Katika sehemu zingine utasikia habari za ajabu.
Wengine husema kuwa wanaweza kupanda Fisi usiku wakasafiri maili nyingi. Wengine pia hujitapa kuwa wanafuga Simba na wengine husema mambo mengine ya ajabu kama hayo.
Lakini ukitazama sana mambo hayo yote utagundua kuwa ni ya uongo usio na mfano. Swali kubwa ambalo waganga wengi wanashindwa kulijibu na ambalo watu wengi wenye kutambua uwongo huo hujiuliza ni hili. Kama ingekuwa kweli wasemavyo, kwa sababu gani waganga wote wenye uwezo wa ajabu kama huo hawajaendelea, si tungekuwa watu wa kwanza kufika kwenye mwezi?
Sayansi ya kufikiria kama hiyo na kuisema midomoni tu haifai. Inatakiwa ifanywe na kila mtu ashuhudie. Kinyume chake ni kuwa utaona hakuna hata mganga mmoja mwenye nyumba nzuri au mwenye hali yakuinua maisha yake kidogo. Hali ya waganga walio wengi wa aina hiyo ni duni sana. Wamebaki wakiwadanganya wananchi na kuwatishia kwa uganga wao usio na msingi.

ENGLISH: TRADITIONAL HERBS
Many traditional medicines are known miti shamba (which means traditional herbs). The reason for this, I do not know, but it is believed that when the colonialists arrived for the first time in the country they found the people using the drugs. With disrespect the colonialists called them miti shamba.
In this part of the land lived many traditional healers. Some of these healers were good doctors. They treated different patients and cured many diseases. The sick were healed of their illnesses. As a result, witch doctors were loved by the people.
At the same time, there were other witch doctors who acted against the good traditional healers. These threatened people with their skills. They were given the names of sorcerers. The main task of this kind of physician was, as it was to confuse their colleagues and other non-traditional healers.
Others demanded huge charges. They even threatened to kill if their demands were not met. There were other witch doctors who walked around villages. These were con-men. They were not true healers. Their job was to walk around with many roots deceiving people.
Some of them said that they were able to make a person rich, but they were themselves poor. Others claimed to be able to bring rain in the rainy season when it did not rain for a long time, At the same time, those healers faced the same problems as anyone else.
Some said that they were able to turn a man into a woman or a woman into a man. Others said that they could turn someone into a wild animal like lion, leopard or hyena. Some were heard saying that, they were able to turn a mouse into a Lion. The deception of these healers is still going on among citizens.
In many parts of our continent, villages are unable to develop due to fear of this kind of witch doctors. No wonder you have heard that there are some witch doctors who raise the dead and make them live again and cultivate their farms.
Some witch doctors even dare to say that they are able to disappear or fly without being seen. If you think critically, you will see that no one lives on this earth with those wonderful abilities. In some places you will hear wonderful news.
Some say they can ride hyenas at night travelling for many miles. Others claim to be capable of domesticating lions and yet others say something similar.
But if you carefully examine all these things, you will find that they are unfounded. One major question that many traditional healers fail to answer and which many people who are aware of their lies are asking is this: If they were really telling the truth, why would all the witch doctors with such amazing abilities have not develop? Why would we not be the first people to reach the moon?
The science of thinking like that and just saying words of the mouth is not good. It must be done for everyone to witness. On the contrary, you will see that there is not a single healer who has a good home or standard life. The status of most of the traditional healers is very low. They continue deceiving the people and threatening them with unfounded witchcraft.