Sukuma Stories

69. NGOSHA UYO AKANGEMA NKE AMANE ULU ATOGILWE NG’HANA.

Collected by: Don Sybertz, Scanned by: Cephas Yao Agbemenu

With special thanks to Rev Joe Healey (African proverbs,Sayings and stories)

Bhagosha bhabhili bhidimile bhusumba bhandya kwibhuja, gete abhake bhise bhatutogilwe? Ungi uhaya giki, nke wane, anitogilwe ng’hana.

Ng’wiye uhaya, “Hene witogwa wenubho bhuli wa ng’hana?” nsumba ng’wiye unshokeja, “Nakungema nahene ulu ng’hana anitogilwe, uhaya giki nache nandegeleke.”

Lushiku lumo bhali mu numba kihamo, ngoshi na nke. Ngoshi wali ha bhulili, nu nke nang’hwe waliwigashije hihi. Huna lulu ngosha ung’wila unke, “Nke wane nacha!” Nu ngoshi wichijisha (kwiyitya kiti uchile- kujifanya).

Nkima wahayubhona ngoshi wacha uhaya, “Nite kinehe lulu? Natubhaga no, ulu nandya kulila bhakwiza bhanhu bhanizwanje nikale na nzala gete nalye nigute tame, na nize nalile.

Huna lulu wandya kuzugija, aliyo ikubhi lyalilitiho, bhuki walibhusungile ha lusungo haho na bhulili. Nkima wihamba kusungula uduma iki wali nguhi, nose umpanda ungoshi wakwe mu ng’humbi na usola bhuki.

Aho wamala kulya na kwiguta wandya lulu ugulila bhiza bhanhu. Bhingila mu numba bhumuja, “Kinehe mayu?” Nang’hwe, “Ngoshi wane wachaga.”

Nsumba ng’wiye wa ngoshi ubhawila bhanhu giki, “Fumagi mo pye, nene nanagule, namanile bhugota wa kumpija. Bhusaga ho bhabhili umu numba, wandya kumuja ng’wiye, wabhona kinehe?

Iyo nabhona ya gukamaja, aho nkima wane wanibhona nacha, uhaya, “Umo natubhilaga umu ulu nandye kulila bhakwiza bhanhu bhanizwanje nikale na nzala, hambu hambu nazuge nalye nigute tame, huna lulu wandya kuzuga bhugali, aliyo ikubhi lyalilitiho. Bhuki wali bhusungile haho na bhulili, aho wihamba kwinja ulebha, nose wandya kunipanda mu ng’humbi.

Bhandya lulu guseka, aho bhanhu bhigwa bhaliseka bhuhaya, ng’wichiswe wapilaga lulu. Huna lulu ngosha ung’wila nke, “Gashinaga witogwa wako bhuli bhudo ng’hana, nkima aho wizuka isho witaga usunduhala no.

Kiswahili: Mwanamume aliyemjaribu mke wake afahamu kama kweli anampenda.

Wanaume wawili walikuwa marafiki sana. Siku moja wakaanza kuulizana. “Wake zetu wanatupenda kweli?”  Mmoja akasema kwamba, “Mke wangu ananipenda kweli.”

Mwenzake akasema, “Upendo wenu ni wa kweli kabisa?” Mwenzake akamjibu, “Nimwangalie mke wangu kama kweli ananipenda, akasema kwamba nife nimsikilize.”

Siku moja walikuwa ndani ya nyumba pamoja mume na mwanamke. Mme alikuwa kitandani, na mkewe alikuwa amekaa karibu. Kwa hiyo mme akamwambia mkewe, “Mke wangu nimekufa.” Na mme akajifanya amekufa.

Mwanamke alipoona mmewe amekufa akasema, “Nifanye nini sasa?” Muhimu nile kwanza nishibe ndo nilie.”  Kwa hiyo akaanza kupika. Lakini hakuwa na mboga, alikumbuka kuwa kuna asali ipo juu ya dali usawa wa kitanda.

Mwanamke alijaribu kuchukua ile asali, alishindwa maana alikuwa mfupi. Mwisho akapanda kitandani, akamkanyaga mmewe tumboni, na akachukua asali. Alipomaliza kula na kushiba akatoka nje kulia.

 Wakaja majirani, wakaingia ndani, wakmuuliza vipi mama? Kuna nini? Naye akajibu mme wangu amekufa.

Rafiki yake aliwaambia tokeni ndani nimponye maana najua dawa ya kumponya. Walibaki wawili ndani, akaanza kumuuliza mwenzake umeonaje sasa? Rafiki yake alimwambia aliyoyaona, mke wangu aliponiona nimekufa aksema, nilivyo na njaa hivi nianze kulia watakuja watu wanijaze mawazo nishinde njaa, afadhali nipike nile nishibe kwanza, ndio akaanza kupika ugali, ila mboga haikuwepo. Asali ilikuwa juu ya dali karibu na kitanda, alipotaka kutoa hakufikia, sasa akaona anikanyage tumboni.

Wakaanza kucheka sasa, watu waliposikia kicheko wakasema mwenzetu amepona. Mme ndo akamwambia mkewe kwamba, “Kumbe upendo wako ni mdogo kabisa.”  Mwanamke akakumbuka kile alichokifanya na kusikitika.

passed-out

vintage-

ENGLISH: LET ME TEST IF MY WIFE LOVES ME

Two men were very great friends. One day they began to ask each other. “Do our wives really love us?” One of them said, “My wife loves me.”

His companion said, “Is her love  true?” His colleague replied, “I will find out if my wife really loves me. I will pretend to be deadcand listen to her.”

One day,one of the men was in the house with  his wife. A husband was in bed, and his wife was sitting next to him. The husband said to his wife, “My wife I am dead.” And he pretended to be dead.

When the woman saw that her husband is dead, she said, “What am I going to do now?” The first thing I must do is eat enough food.Then I will start crying.”So she started cooking. But she discovered that she did not have vegetables.Then she remembered that there was honey on the roof just above the bed.

The woman tried to take the honey but she failed because she was short. Finally,she went up to the bed, stood her legs on the stomach of her husband, and took honey. When she had finished eating and satisfied,she went out and started crying.

 And the neighbours came in, and asked her, “What is the matter,woman? What is there?” And she answered my husband is dead.

Her husbad’s friend told them “Come out so that I can heal him because I know the cure.”The two remained in the house, and began to ask their partner,“What did you see now?” His friend told him what he saw, “When my wife saw me dead she said, I am hungry I will start crying after eating.” She started cooking, but the was no vegetables there. Honey was on the roof on top of the bed near it.When she wanted to take the honey, she did not reach it, and she walked on my stomach.”

They started laughing now, when the people heard the laughter they realized that our colleague was healed. And he said to his wife, “That your love is very little.” The woman remembered what she had done and was sorry.

 

 

68. Nkima Uyo Waladantogagwa (Antogilwe) Ngoshi

Collected by: Don Sybertz, Scanned by: Cephas Yao Agbemenu

With special thanks to Rev Joe Healey (African proverbs,Sayings and stories)

Ng’waka gumo waliho ngosha na nke wakwe na bhana. Huna iza nzala nhale gete, bhusumilo wali kule. Nkima ung’wila ngoshi, “Jaga ugadukobhele ishiliwa.”

Huna ungosha uja lugendo, lwa kushimiza ji akagwisha. Intondo akifula, ntondo bhungi ushoka wenha shiliwa bhulya.
Lushiku lumo kwike kuhaya akakima, “Jashilaga ishiliwa ng’wana Kweji, shokaga hangi ukubhusumilo.” Aluwe alisiminza na nzala kwike mlugendo. Ulu washoka hakaya kang’wila, “Wenhaga shigehu.” Ntondo shokelaga, nose ungosha ucha. Ubhulagwa nzala na lugendo.

Kiswahili: Mwanamke Ambaye Alikuwa Hampendi (Anampenda) Mme Wake.

Mwaka mmoja alikuwepo mwanamume na mke wake na watoto wao. Basi ilitokea njaa kubwa kabisa, chakula kilipatikana mbali. Mwanamke akamwambia mme wake, “Nenda ukatutafutie chakula.”

Basi mme wake akaanza safari ya kutembea, jua likachwea. Kesho yake akapumzika.  Siku iliyofuata  alirudi akaleta chakula wakala. Siku moja tena  mke wake alisema, “Chakula kimekwisha mwana Kweji rudia tena.

Lakini mwanamume alikuwa anatembea na njaa tu safarini. Akirudi nyumbani anaambiwa umeleta kidogo, kesho rudia tena. Mwishowe mwanamume akafa kwa ajili ya njaa na safari.

african-family-

african

ENGLISH: A WOMAN WHO DID NOT LOVE HER HUSBAND

Once upon a time, there was a man and his wife and their children. Then there came a great famine. Food could befound  very far away. The woman said to her husband, “Go and get us food.”

So her husband began to walk. He walked until the sun went down. The following day, he rested. Then he went back home and brought food.They ate it. Another day, his wife said, “The food has been finished, Ng’wana Kweji, go an dbring some more.”

But the man was walking while hungry all the way. Whenever he came home, he was told he had brought little. So, he had to go back and bring some more the following day. Finally, the man died of hunger and travel fatigue.

67. Nashosha Ichimu Kuli Ngabhuji

Collected by: Don Sybertz, Scanned by: Cephas Yao Agbemenu

With special thanks to Rev Joe Healey (African proverbs,Sayings and stories)

Kale bhanhu bhagabhulilagwa nyama na bhanamhala, kiti habhukombe na habhuyobhe na ha lufu na mumalibhilingo.

Kali kajile, uluwagabhulilagwa nyama na namhala (ngabhuji) kushosha nkono kuli ngabhuji. Kwene kuhaya kung’winha ngabhuji ipande lya nyama iyo winhwa. Ili nzila ya kufunya bhulumbi kuli ngabhuji, lumeng’ho lwa giki alinabhulumbi kuli ngabhuji.

Aliyo ulubhatagabhulililwe nyama abhajimbagwa na bhangi bhagabhulilagwa, bhabyaji bhasayaga kibhi no. Gwali mhayo gwa wisu huna lulu, bhubhatuma bhana bhado bhayanda kujung’wisha sumu ngabhuji.

Bhagabhuji bhagwashiwagwa bhingi no, na bhayanda bhakamalwa na bhujimbani wabho kulogwa. Kulishiwa sumu no, ishangilingili (kando kando) hihi hihi mung’hilimbwa na nyanza na Magu, na Nasa, na Masanza, niyo likaluma lya bhudumi.

Ubhebhe wangabhulila nyama ung’wana wakushokejaga bhulogo nulu ichimu. Mu ng’wanya gwa kushosha nkono, kufunya bhulumbi bhashoshaga ichimu bhubhamala abhagabhuji bhingi no umugubhalisha sumu, ichene mapande gakumanyanza bhatalyaga kungi kulwa widumi. Hangi ha walwa ulu ng’wenikili walwa atatogilwe kung’wa bhangi bhatuzunya iki bhogoha kulishiwa.

Kiswahili: Kurudisha Mkono Kwa Mgawaji

Hapo kale walikuwa wanagawiwa nyama na wazee kwa mfano, kwenye harusi, kwenye mkusanyiko wa kazi, kwenye kilio na kwenye mikutano mbali mbali.

Zamani ilikuwa kawaida yao kugawiwa nyama na wazee (mgawaji) kurudisha mkono kwa mgawaji ndiyo kusema kumpa mgawaji kipande cha nyama. Ambayo umepewa, ilikuwa njia mojawapo ya kutoa shukrani kwa mgawaji. Ni alama ya kujulisha kuwa ana furaha kwa mgawaji.

Kama hawatagawiwa nyama, wengine hawatazipata na wengine watapata kidogo. Wazazi walikuwa wanaudhika mno, lilikuwa neno la wivu. Kwa hiyo waliwatuma vijana wa kiume kuwanywesha sumu wagawaji.

Wagawaji walikuwa wananaswa wengi mno na vijana.  Walimalizwa wachoyo kwa kulogwa (kwa wanaoamini hivyo) na kulishwa sumu. Sana sana waliokuwa kando kando ya Ziwa kwa mfano, Bulima, Kwimba, Mwanza, Magu, Nassa na Masanza.

 Ndiyo kusema kuwa kulivuma hali ya kutokuwa na uwezo. Wewe uliyegawiwa nyama yeye amekurudishia sumu, au mkuki  kwenye kazi ya kurudisha mkono yaani kutoa shukrani, walikuwa wanarudisha mkuki, waliwamaliza wagawaji wengi mno kwa kuwalisha sumu.

Ndiyo maana pande za Nyaza (Ziwani) hawali kwingine kwa shida ya kukosana. Na tena kwenye pombe kama mwenye pombe hapendelei kunywa, wengine hawatakubali kwa vile wameogopa kulishwa sumu.

lance man with spear

ENGLISH: TO RETURN A HAND TO THE DISTRIBUTOR

In the past, meat was distributed by the elders. For example, during weddings, gatherings, funerals and in various meetings.

In the past, it was common for the recipients to share the meat they had been given with the distributor as a way of saying thank you.That means,the recipient had to give the distibutor a piece of meat. It was a sign that the recipient was happy with the distributor.

The practice was deemed good because if they didnot distribute the meat, some would not get it and others would get less. Some parents were very angry with the practice. It was a matter of jealousy. So, they conspired with the young men to poison the distributors.

Many distributors were trapped by young people. They were fed poison but they thought that they had beenbewitched (for those whobelieved in witchcraft). It was common in the Lake Zone. For example, it was observed in Bulima, Kwimba, Mwanza, Magu, Nassa and Masanza.

What was obvious is that there came a state of misunderstanding and mistrust. Imagine! Somebody gives you meat and return poison as thanks. In other words,you come with a spear in your hand to give back thanks. In this way of thanks giving, they poisoned so many distributors.

That is why the Nyaza (Lake Victoria) sides, people do not eat in other people’s homes because of being afraid to be poisoned through food. In the same is true for alcohol. If the owner does not drink, some will not accept their alcohol because they are afraid of being poisoned.

66. Jigano Ja Nyanda Na Ng’waniki Bhahayaga Kutunga Ndoa

Collected by: Don Sybertz, Scanned by: Cephas Yao Agbemenu

With special thanks to Rev Joe Healey (African proverbs,Sayings and stories)

Kale bhaliho nyanda na ng’waniki, unyanda ilina lyakwe Fanueli, ung’waniki Joyce. Mu bhubhili wabho bhagahaya kutunga ndoa. Aho loshiga ulushiku lwa kutunga ndoa yabho huna lulu fanueli nu Joyce bhakaja ku chumba ja kuzwalila myenda ya bhukombe nabhaje kujutunga ndoa yabho mu kanisa.

Unyanda Fanueli akazwala sulubhale jakwe ja wikole. Sulubhale igwanda igodi, malole ku miso, jilatu, na saa ya mumakono umala.

Ung’waniki Joyce nang’hwe wandya kuzwala myenda yakwe ya bhukombe, igauni lyakwe, shela, dhahabu gu matu gakwe, jilatu jisoga, Saa mumakono, udimila na bhulabhu bhusoga gete mumakono gakwe.

Ahikanza bhamala pye abhose bhufuma lulu uguchumba jabho ja kuzwalilila. Bhandya lugendo lwabho lwa kuja ku kanisa bhakatunge ndoa lulu.

Ahabhali mu lugendo umunzila Fanuel akamona munhya wakwe Joyce umo wabhelelaga uyomba giki, “Yee!! Munhya wane Joyce wabhelelaga gete, idabhelelile usimize wa magulu, imaga henaha unene naje bomani nagaguchobhele loli na gugushokela nize nagusole.”

Joyce uzunya, Nahene nsumbone ugunisanga henaha nadinga gete. Fanueli uja bomani gujuchola imondoka umo wahayilaga.

Huna lulu ikanza lya kwinga u Fanueli u Joyce usangwa iguku. Inguku yeniyo aho yampandika Joyce yuyomba, “Yee!! Ng’waniki bhebhe wabhelelaga cheniki. Aliyo umanile igiki wabhelelaga?” Ujoyce uyomba, “nduhu natimanaga igiki nabhelelaga, iki nadibhonaga.”

Inguku yung’wila Joyce, “Ulu ulihaya kumana ng’hana igiki wabhelelaga ninhage imyenda yako pye iyose wibhonanikije bhebhe ng’wenekili igiki wabhelelaga ng’hana.

Joyce aho wigwa chene agikungula bho wangu wangu imyenda yakwe pye yose. Akasaga aliduhu, akalinha iliguku pye myenda yakwe. Inguku yuyizwala pye myenda ya ng’wa joyce, inguku aho yazwala myenda yumuja, “wabhona lulu umo nabhelelela?” Joyce uhaya, “ng’hana yi obhelela.” Inguku yandya kwigeta nyadoshi gete.

Huna lulu Fanuel aho wipandika imondoka akayega no, alimana giki umunhya wakwe akwenhwa na mondoka ni haha yeniyi gashinaga Nguku. Fanuel agang’winha udeleva lilagilo limo duhu, ung’wila, “jaga lulu bhitilaga ibalabala linili duhu ugunsanga ng’waniki azwalile myenda yape nu ng’unuyo duhu, nduhu ungi ho. Deleva ubhacha gali.

Kiswahili: Hadithi Ya Mvulana Na Msichana Waliotaka Kufunga Ndoa

Hapo kale, palikuwepo vijana wawili, mvulana na msichana. Mvulana aliitwa Fanuel, na msichana aliitwa Joyce. Vijana hao walikubaliana kufunga ndoa.

Siku ya kufunga ndoa yao ilifika, walikwenda kwenye chumba cha kuvalia mavazi ya harusi. Fanuel alivaa suti iliyomkaa vizuri. Pia alivaa miwani, saa ya mkono na kofia.

Naye Joyce alivaa mavazi yake. Shela aliyoivaa ilimpendeza sana, heleni na vidani vya dhahabu vyote vilimfanya apendeze sana. Mikononi alishika maua mazuri.

Baada ya kumaliza kuvaa, wote wawili walitoka nje, wakaanza safari ya kwenda kufunga ndoa Kanisani. Wakati walipokuwa wanakwenda  Kanisani, Fanuel alivutiwa sana na mwendo wa madaha wa mchumba wake. Akasema, “Naam, Mpenzi Joyce, umependeza kweli kweli, haifai sasa utembee kwa miguu, simama hapa hapa, nami niende mjini kukutafutia gari, halafu nitakuja kukuchukua.” Joyce akasema, “sawa mchumba wangu, mimi utanikuta hapa hapa tu sitaondoka kamwe.” Fanuel akaenda mjini kutafuta gari kama alivyosema.

Basi baada ya Fanuel kuondoka, Nyani alikuja alipo Joyce. Nyani huyo alipofikia kwa Joyce akasema, “lo, asi!! Binti umependeza kweli kweli. Lakini je, unafahamu kuwa umependezaje? Joyce  akasema, “mhuu, sifahamu vizuri kwa kweli, maana sijioni sawa sawa.”

Nyani akamwambia Joyce, “Kama unataka kuhakikisha kuwa umependeza, nipe sasa mavazi yako yote nijivalie ili ujionee mwenyewe kuwa kweli umependeza.  Joyce kusikia vile, akavua kwa haraka sana mavazi yake yote, akabaki bila nguo, akampa Nyani mavazi yake yote.

Naye Nyani alijivalia mavazi yote ya Joyce. Baada ya Nyani kujivalia mavazi akasema, “umeona sasa jinsi nilivyopendeza?”  Joyce akasema, “asi!! Safi kweli, Nyani anajirembua kwa madaha kweli kweli.”

Fanuel alipoipata gari alifurahi mno, akijua kuwa mchumba wake ataletwa kwa gari mara  Kumbe Nyani. Fanuel alimpa dreva sharti moja tu, alisema, “nenda sasa, pitia barabara hili tu utamkuta msichana mwenye mavazi meupe, ni huyo huyo tu, umchukue siyo mtu mwingine.” Dreva akawasha gari tayari kwenda kumchukua Joyce.

Gari alipoliona Joyce kuwa tayari linakuja kumchukua limepambwa kwa matawi na maua safi, lo! Ikawa mkiki mkiki sasa kwa Joyce. Joyce anadai sasa mavazi yake kwa Nyani, “Nipe bwana mavazi yangu nivae mimi, gari limefika  ni hilo.”  Lo! Wapi, Nyani anajidai vizuri mno kwa kuwa amependeza, hajali ombi la mwenye mavazi ya arusi.

Dreva akafika vuu! Tayari kumchukua mwenye mavazi meupe. Nyani akaitwa kuingia ndani ya gari bila Joyce. Joyce kuona vile, akamwambia dreva,  “Ni mimi hapa siyo huyo.”  Dreva akasema, “Mimi nimeambiwa nimchukua mtu mwenye mavazi meupe tu na sio wewe.”

Joyce akaachwa pale pale analia ovyo. Fanuel alipomwona Nyani amejivalia mavazi ya arusi, bila Joyce mchumba wake, alikasirika sana, akamvua mavazi ya arusi. Akagoma kufunga ndoa na Joyce, akarudi nyumbani. Arusi haikufungwa.

boy-and bride

monkey-3

ENGLISH: THE STORY OF A BOY AND A GIRL WHO WANTED TO MARRY EACH OTHER

In the past, there were two young people, a boy and a girl. The boy was named Fanuel, and the girl was named Joyce. The two young people agreed to get married.

On their wedding day, they dressed very well. Fanuel wore a well-suited-suit. He also wore glasses, a wrist watch and a hat.

And Joyce wore her wedding dress. The wedding dress which she wore fit her so well that she looked extra beautiful.The gold and gold jewelry she wore made her look very attractive. In her hands,she held beautiful flowers.

After dressing themselves, they both went out, and started their journey to church where they could make the vows. While they were going to church, Fanuel got very impressed with the romantic gait of the would soon be his spouse. He said, “Yes, dear Joyce.You look great! It is not right for you to walk. You wait here and I will go to the city to find you a car, and then I’ll come and pick you.” Joyce said, “Ok, my dear.You will find me waiting here. I will never leave.” Fanuel went to the city to find the car as he promised.

After Fanuel had left, the Baboon came to Joyce.

The Baboon said, “Wow,!!You are really very well-dressed. But do you know how attractive you are? Joyce said, “I don’t really know it, because I don’t see myself.”

Then the Baboon said to Joyce, “If you want to see how attractive you are, give me all your clothes now so that you can see for yourself that you really look nice.” Joyce quickly took off all her clothes, and was left naked, and she gave the clothes to the Baboon.

The Baboon put on all of Joyce’s clothes. After the Baboon had worn the dresses, she told Joyce, “Have you seen now how attractive you look?” Joyce said, “It is true.The Baboon is telling the truth. I look great.”

When Fanuel got the car, he was very excited, knowing that his fiancé would soon be brought to church in the car. So, Fanuel gave the driver only one condition. He said, “Go now, just go this way and you will find a girl with white clothes.That is one you should pick. Pick only her and no one else.” The driver left with the car ready to pick Joyce.

Then Joyce saw the car well decorated with twigs and fresh flowers coming to pick her. Joyce started claiming her dresses from the Baboon.  “Give me my dress. I want to wear it.”Look, the car has arrived.” The Baboon didn’t care about the fact that he was wearing Joyce’s wedding dress.

When the driver arrived, the Baboon was called into the car as Joyce remained outside. Seeing that, Joyce said to the driver, “I am here, it is not her.” The driver said, “I have been told to pick someone with white clothes and not you.”

Joyce was left there crying madly. When Fanuel saw the Baboon wearing the wedding dress, and not Joyce  his fiancee´, he was very angry, stripped the wedding dress. The wedding could not materialize.

 

65. Jigano Ja Shimba Na Ng’hungulume

Collected by: Don Sybertz, Scanned by: Cephas Yao Agbemenu

With special thanks to Rev Joe Healey (African proverbs,Sayings and stories)

Kale yaliho Shimba na Ng’hungulume. Bhalibhazenganilwe aliyo kwibhona yaya, kwike bhiyigwaga shilaka bhuli ng’wene.

Lushiku lumo muna shimba akigwa lilaka lya ng’hungulume bhujiku bho hingikana kwela (saa 9) akamuja muna Mbiti, “Shilaka sha ng’wa nani isho nashigwaga?” imbiti yuyomba, “Ishilaka shenisho sha Ng’hungulume ilihilila ng’wigunguli.” Shimba yumuja hangi umuna Mbiti, “Umuna Ng’hungulume ng’wenuyu ashikile kinahe, ubhutale ali ntale kiti nene?”

Imbiti yuyomba, “Litale kulebha ubhebhe. Umu yang’wililaga cheniki imbiti bhali bhaditogagwa nu muna shimba. Alinguno opejiwagwa aha nyama, kushisha alye mpaga wigute umuna Shimba.

Ishimba ikadubula bhoya bhoyo wamunhingo, winhwa umuna mbiti anchalile muna ng’hungulume akalibhone ilibhoya lyenilo. Imbiti ikalichala ng’hana ukolimuna ng’hungulume ukalibhona.

Nayo ing’hungulume ikadubula loya loha la ha ngongo winhwa umuna mbiti anchalile muna shimba. Shimba aho yalubhona uloya lwenulo ikakumya no.

Nang’hwe udubula hangi lulezu logwegela hihi na nomo gwakwe, ung’winha muna mbiti na kung’wila anchalile mna ng’hungulume. Ng’hungulume aho yulubhona ululezu lo mnashimba lidakumije.

Nayo ing’hungulume ikalwinja loya loyo lohankimbili ululihu gete (lutenga) winhwa umuna mbiti alutwale ukoli muna shimba. Ishimba aha yalibhona yogoha no yung’wila umuna mbiti, dingage henaha dupelage ng’wipolu wangu wangu.

Hangi imbiti yung’wila mna Shimba ilikungulume lyayombaga likwiza likubhone mulwe nalyo. Ishimba aha yigwa chene niyo hangi ogohaga yugang’wila mna mbiti, dingage wangu wangu henaha niyo dusamile ng’wipolu hagati, hangi ibhize kule gete. Kushisha lelo ishimba yasamila ng’wipolu idahayile kwegela muchalo hangi.

Kiswahili: Hadithi Ya SIMBA NA JOGOO

Hapo zamani, kulikuwa na Simba na Jogoo, ingawa  waliishi jirani lakini hawakuonana ana kwa ana. Bali kila mara walikuwa wanasikiana kwa sauti ya kila mmoja.

Siku moja Simba aliisikia sauti ya Jogoo mnamo saa tisa za usiku. Simba akamuuliza Fisi,  “Sauti ninayoisikia ni ya nani?”

“Ni sauti ya Jogoo,” Fisi alijibu. “Huyo Jogoo anaishi wapi?”“Anaishi na kuwika huko kijijini!” “Je, huyo  Jogoo ni mkubwa kama mimi?”

“Ni mkubwa kupita wewe!”

Fisi alimjibu hivyo kwa sababu hakumpenda Simba. Hakumpenda kwa vile mara kwa mara Simba alikuwa anamfukuza Fisi wakati akila nyama. Fisi aliweza kula ile nyama ambayo simba ameila na kuiacha baada ya kushiba.

Hapo Simba akanyofoa unyoya wake wa shingoni na kumpa Fisi ili aende kumpelekea Jogoo. Jogoo aliupokea ule unyoya wa Simba, naye akamkabidhi unyoya wake wa shingoni ili kumpelekea Simba.

 Lo! Simba alipouona ule unyoya wa Jogoo alistaajabu sana. Hapo Simba akang’oa usinga kwenye mashavu yake. Jogoo alipouona usinga wa yule Simba, hakushangaa.

Hapo Jogoo akang’oa unyoya mrefu wa mkiani, akampa Fisi ampelekee Simba. Wakati simba anakabidhiwa ule unyoya wa mkia wa Jogoo, aliogopa sana.

Akamwambia Fisi wahamie mbali ndani ya msitu. Simba aliogopa zaidi Fisi alipomwambia kuwa Jogoo alikusudia kuja kuonana naye, ili wapimane nguvu.

Hapo simba alishikwa na hofu kubwa hata akamlazimisha Fisi kuondoka kijijini na kutokomea mbali porini. Hadi leo Simba haishi kijijini bali huishi porini.

hen-cock

 

 

lion-

ENGLISH: THE STORY OF  THE LION AND THE COCK

In the past, there were the Lion and the Cock. Although they lived in the neighbourhood they did not meet. But each time they heard each other’s voice.

One day Lion heard the crow of the cock at three o’clock. Lion asked Hyena, “Whose voice do I hear?”

“It’s the cock’s voice,” Hyena answered. “Where does the cock live?” “He lives and roars in the village!” “Is that Cock big like me?

“It is bigger than you!”

Hyena answered him that way because he did not like Lion. He did not like him for the Lion used to chase Hyena when eating meat. Hyena used to eat the meat that the lion had eaten and left it after it was satisfied.

Then the Lion took his mane from the neck and gave Hyena to send it to the cock. The cock received the Lion’s fur, and gave her a necklace feather of her neck to take it to the Lion.

 Oops! When the Lion saw the feather of the cock, he was very surprised. Then Simba pulled the mane from his cheeks. When the cock saw the mane of the Lion, he was not surprised.

Then the cock plucked the longer feather of the tail and gave it to the hyena to take to the Lion. When the lion was given the feather of the tail, he was very scared.

Then, he told Hyena to move away into the forest. Simba was more afraid when the Hyena told him that the cock was coming to meet him so that the two could see who was stronger than the other.

The Lion was so frightened that he forced the Hyena to leave the village and disappear into the forest.  Up to now the lion does not live in the village, but he lives in the forests.