Bhalihoyi bhakima abho bhali bhatoililwe na ngosha umo. Aliyo lulu, ungosha ng’wunuyo, agaikala kuli nkima umo duhu, kunguno agantogwa weyi gukila abhangi. Hunagwene abhanhu aho bhadebha chene bhagabhawila abhakima bhangi bhenabho giki, “ng’wa henwa mhali.”
Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agabhuchaga milimo mingi mpaga aduma uguimala chiza, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agandyaga gutumama milimo mingi iyo agadumama uguishisha chiza, kunguno agadumaga ugwigabhanhya umubhutumami bhokwe. Uweyi agayilekanijaga duhu imilimo yakwe yiniyo, kunguno ya guyandya mingi bho likanza limo, umuwikaji bhokwe.
Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo oliotola bhakima bhingi abho agaduma ugwikala nabho chiza, kunguno nuweyi agabhuchaga milimo mingi, mpaga oduma uguyishisha chiza, umubhutumami bhokwe. Hunagwene abhanhu bhagayiwilaga imilimo yakwe yiniyo giki, “ng’wa henwa mhali.”
Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya gubhiza na ng’witoji umo, na gutumama nimo gumo bhulikanza, kugiki bhadule gujilanhala chiza, ikaya jabho, umuwikaji bhobho.
Luka 16:13.
Marko 10: 1-12.
KISWAHILI: MUMETELEKEZWA MITALA.
Walikuwepo wanawake walioolewa kwenye mitala na mwanamume mmoja. Lakini mwanamume huyo, aliishi kwa mwanamke mmoja tu, kwa sababu alimpenda zaidi kuliko wale wengine. Ndiyo maana watu walipogundua hivyo, waliwaambia wale wengine kwamba, “mumetelekezwa mitala.”
Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huanzisha kazi nyingi mpaka anashindwa kuzimaliza, katika maisha yake. Mtu huyo, huanzisha kazi nyingi kwa wakati mmoja ambazo hushindwa kuzikamilisha kwa sababu ya kushindwa kujigawa, katika utumishi wake. Yeye huzitelekeza kazi zake hizo, kwa sababu ya kuzianzisha nyingi kwa wakati mmoja, maishani mwake.
Mtu huyo, hufanana na yule aliyeoa wanawake wengi akashindwa kuishi nao vizuri, kwa sababu naye huanzisha kazi nyingi kwa wakati mmoja mpaka anashindwa kuzimaliza vizuri, katika utumishi wake. Ndiyo maana watu huziambia kazi zake hizo kwamba, “mumetelekezwa mitala.”
Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuwa na ndoa ya mke mmoja na kutekeleza kazi moja kwa wakati mmoja, ili waweze kuzitunza vizuri familia zao, maishani mwao.
Luka 16:13.
Marko 10: 1-12.