Ikalagu yiniyo ihoyelile higulya ya luyaga. Uluyaga lunulo lugahuyembaga lujile mumabala matale aliyo lulu ludamanyikile uko lulifumila nuko lujile. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “munhu ng’wenuyu nadamanile uko afumilile nuko ajile – Luyaga.”
Ikalagu yiniyo, igalenganijiyagwa kuli munhu uyo adina shimile ishawiza umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agikalaga uyunga sagala bho nduhu ugulenda aha kaya yakwe kunguno ya bhukokolo bho guduma gutumama milimo yakwe bhunubho. Uweyi agadumaga uguyibheja chiza ikaya yakwe kunguno ya bhujidalenda ha ng’wakwe bhunubho, umuwikaji bhokwe.
Umunhu ng’wunuyo agikolaga nu luyaga ulo ludamanyikile uko lufumilile nuko lujile, kunguno nuweyi agikalaga uyunga sagala bho nduhu ugulenda aha kaya yakwe yiniyo, umukikalile kakwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “munhu ng’wenuyu nadamanile uko afumile nuko ajile – Luyaga.”
Ikalagu yiniyo, yalanga bhanhu higulya ya gubhiza na jimile ja nhungwa jawiza ijo jidulile gubhambilija ugujilela chiza ikaya jabho, kugiki bhadule kupandika matwajo mingi, umuwikaji bhobho.
Waebrania 7:1-3.
KISWAHILI: KITENDAWILI – TEGA.
MTU HUYU SIJUI ATOKAKO NA AENDAKO – UPEPO.
Kitendawili hicho huongelea juu ya upepo. Upepo huo huvuma kuelekea sehemu mbalimbali, lakini huwa haujulikani unakotoka na unakoelekea. Ndiyo maana watu husema kwamba, “mtu huyu sijui atokako na aendako – Upepo.”
Kitendawili hicho, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huwa hana msimamo mzuri katika maisha yake. Mtu huyo, hupendelea kutembea hovyo bila kutulia kwenye familia yake kwa sababu ya uvivu wake wa kutokufanya kazi. Yeye hushindwa kuiendeleza vizuri familia yake kwa sababu ya kutokutulia nyumbani kwake huko, maishani mwake.
Mtu huyo, hufanana na ule upepo usiojulikana kule uendako na ulikotoka, kwa sababu naye hudhurura hovyo bila kutulia nyumbani kwake, katika maisha yake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “mtu huyu sijui atokako na aendako – Upepo.”
Kitendawili hicho, hufundisha watu juu ya kuwa na msimamo wenye tabia njema ya kuwawezesha kuzilea vyema familia zao, maishani mwao, ili waweze kupata maendeleo makubwa, maishani mwao.
Waebrania 7:1-3.