Sukuma Proverbs

828. GUFUNYA ILI GUTULA JIDIMILA ADAKWIJAGA.

Olihoyi munhu uyo ohayaga gupandika sabho ningi bho gulima ngunda ntale. Umunhu ng’wunuyo, agafunya hela ja gugulila ilale na gulilimila. Aho alilima ililale linilo, agapandika sabho ningi kugila ijo olinajo igwandya. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “gufunya ili gutula jidimila adakwijaga.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agazunyaga gujitumila ginhu jilebhe kugiki apandika jikolo jitale kukila ijagwandya, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, adajilundikaga sagara isabho jakwe, kunguno ahayile ajikwije bho gujitumila chiza ijo alinajo. Uweyi agapandikaga sabho ningi umubhutumami bhokwe, kunguno ya gujitumila chiza ijo alinajo, umuwikaji bhokwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo agafunya hela ja gugulila ilale na ja gulilimila, mpaga upandika sabho ningi, kunguno nuweyi agajitumilaga chiza isabho jakwe mpaga opandika ningi kukila ija gwandya. Uweyi agabhalangaga abhanhu bhakwe inzila ja gujikwigija isabho jabho, bho gujifunya ijo bhalinajo, kugiki bhadule gupandika jingi ijo jili ningi kulebha ijakale, umukikalile kabho. Hunagwene agabhawilaga abhanhu giki, “gufunya ili kutula jidimila adakwijaga.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gujitumila chiza isabho jabho bho gujifunya, umubhutumami bhobho, kugiki bhadule gupandika sabho ningi, umuwikaji bhobho.

Mathayo 25:14-30.

KISWAHILI: KUTOA NI KUWEKA MSHIKILIAJI HAONGEZI.

Alikuwepo mtu ambaye alitaka kupata mali nyingi kwa kulima shamba kubwa. Mtu huyo, alitoa pesa za kulinunulia shamba hilo na za kulilimia. Alipolilima shamba lake hilo, alipata mali nyingi kupita zile alizokuwa nazo hapo mwanzoni. Ndiyo maana watu husema kwamba, “kutoa ni kuweka mshikiliaji haongezi.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hukubali kutoa kitu fulani ili aweze kupata kile ambacho ni kikubwa zaidi, katika maisha yake. Mtu huyo, huwa hajilundikii hovyo mali zake, kwa sababu anataka kupata nyingi kwa kuzitumia vizuri alizo najo. Yeye hufanikiwa kupata mali nyingi katika utekelezaji wa majukumu yake, kwa sababu ya kuzitumia vizuri mali alizo nazo, maishani mwake.

Mtu huyo, hufanana na yule aliyetoa pesa za kununulia shamba na za kulilimia, mpaka akapata mali nyingi kupita zile za mwanzoni, kwa sababu naye huzitumia vizuri mali zake, mpaka anazipata zile zilizo nyingi zaidi ya zile za mwanzoni. Yeye huwafundisha watu wake njia za kuziongezea mali zao kwa kuziwekeza zile walizo nazo, ili waweze kupata nyingi, katika maisha yao. Ndiyo maana huwaambia watu kwamba, “kutoa ni kuweka mshikiliaji haongezi.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuzitumia vizuri mali zao, kwa kuziwekeza, katika utekelezaji wa kazi zao, ili waweze kupata mafanikio ya kuwa na mali nyingi zaidi, maishani mwao.

Mathayo 25:14-30.

haiti giving

cattle-

cow--

ENGLISH: HELPING  OTHERS IS  SAVING, THE  ONE  WHO  DOES  NOT  GIVE  DOES  NOT  GET  MORE.

There was a man who wanted to make a lot of money by plowing a large field. He gave money to buy the field that was bid enough to cultivate it. When he plowed his field, he gained more wealth than he had at first. That is why people said that, “helping  others is  saving, the  one  who  does  not  give  does  not  get  more.”

This proverb is likened to a man who agrees to give something so that he can get what is greater, in his life. He does not accumulate wealth, because he wants to get more out of it by making good use of what he has. He manages to acquire many properties in the enactments of his duties, because of the good use of the resources he has in life.

This man is like the one who gave money to buy land and cultivate it, until he had more money than what he had before, because he also uses his wealth well, until he gets more than what he had before. He teaches his people various ways for increasing their wealth by investing what they have, so that they can get more in their lives. That is why he tells people that, “helping  others is  saving, the  one  who  does  not  give  does  not  get  more.”

This proverb imparts in people an idea on how to use their wealth wisely, by investing it in fulfilling their daily duties, so that they can be more successful in having more wealth in their families.

Matthew 25: 14-30.

827. GUSIMIZA BHUNG’WENE GUBIGISA LISO.

Umunhu uyo agumizaga bhung’wene agikalaga ahumulile duhu, kunguno ya gugayiwa uogwiyombwa nang’hwe. Umunhu ng’wunuyo, agabhizaga guti alibigisa liso, kunguno nang’hwe aganogaga umo ligitilaga iliso linilo. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “gusimiza bhung’wene gubigisa liso.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo adatogilwe ugwiyambilija na bhiye, umubhutumami bho milimo yakwe. Umunhu ng’wunuyo, agikalaga bhung’wene uko alisimizila nu kumilimo yakwe, kunguno ya gulema ugwiyamblimajia na bhiye, umukikalile kakwe. Uweyi agadumaga ugupandika isabho iningi, kunguno ya gulema ugwiyambilija na bhiye bhenabho, umuwikaji bhokwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo agasimizaga bhung’wene, kunguno nuweyi adiyambilijaga na bhiye, umuwikaji bhokwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “gusimiza bhung’wene gubigisa liso.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gwiyambilija chiza uguitumama imilimo yabho, bho gulekana ni nhungwa ja gwikala bhung’wene, umukikalile kabho, kugiki bhadule kupandika sabho ningi, umubhutumami bho milimo yabho.

Matendo ya mitume 2:44-46.

Matendo ya mitume 4:32.

KISWAHILI: KUTEMBEA PEKEE NI KUFIKICHA JICHO.

Mtu anayetembea peke yake huwa amenyamaza tu kwa sababu ya kukosa mwenzake wa kuzungumza naye. Mtu huyo, huwa kama ufikichaji wa jicho kwa sababu, naye huchoka kama lifanyavyo jicho hilo lililofikichwa. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “kutembea pekee ni kufikicha jicho.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huwa hapendi kusaidiana na wenzake, katika utekelezaji wa majukumu yake. Mtu huyo, hupendelea kuwa peke yake, anakotembea na kazini mwake, kwa sababu ya kutokupenda kwake kushirikiana na wenzake hao, katika maisha yake. Yeye hushindwa kupata mafanikio ya kuwa na mali nyingi kwa sababu ya kukataa kusaidiana na wenzake hao, maishani mwake.

Mtu huyo, hufanana na yule aliyetembea peke yake, kwa sababu naye huwa hasaidiani na wenzake, katika maisha yake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “kutembea pekee ni kufikicha jicho.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na ushirikiano wa kusaidiana vizuri  katika kuyatekeleza majukumu yao, kwa kuachana na tabia ya kujitenga na wenzao, ili waweze kupata mafanikio ya kuwa na mali nyingi, katika utendaji wa kazi zao.

Matendo ya mitume 2:44-46.

Matendo ya mitume 4:32.

ENGLISH: TO WALK ALONE IS TO SCRATCH AN EYE.

A person who walks alone is often silent because of the lack of a partner to talk to. Such person, in turn, acts as an eye scratchier because of being as tired as an itched eye. That is why people say that, “to walk alone is to scratch an eye.”

This proverb is compared to a person who is reluctant to help others, in the enactments of his/her duties. This person prefers to be alone in walking or working, because of his/her unwillingness to associate with other coworkers in life. He/she fails to achieve success of having many possessions because of his/her refusal to help others in life.

This person is like the one who walked alone, because he/she also does not help others in life. That is why people say to him/her that, “to walk alone is to scratch an eye.”

This proverb instills in people an idea on how to have good cooperation with others in carrying out their duties, by abandoning the habit of isolating themselves from their peers, so that they may have success of having many possessions in fulfilling their daily duties.

Acts 2: 44-46.

Acts 4:32.

826. NOMO GUDAFUNYAGA ILAKA LIBHI.

Ulusumo lunulo, lulolile bhutumami bho nomo uyo gugayombaga mihayo ya bhuli mbika. Unomo gunuyo, guli jiseme ijo jigafunyaga ilaka bho guyomba mihayo iyo ili mugati ya ng’wa munhu. Ugoyi guli bhubhitilo bho mihayo iyo ili mung’holo ya ng’wa munhu. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “nomo gudafunyaga ilaga libhi.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agiganika mihayo ya wiza na oyiyomba, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agiganikaga mihayo iyo ili nikujo umung’holo yakwe, haho atali uguyiyomba, kunguno alina bhutogwa bho gwikala kihamo nabhiye chiza. Uweyi agabhalelaga chiza abhanhu abho agikalaga nabho bho guhoya nabho mihayo ikujo, umuwikaji bhokwe.

Umunhu ng’wunuyo, alijigemelo ja gubhalangila abhiye nzila ja gufunya ilaka lya wiza bho guiganika chiza imihayo yabho, haho bhadinayiyomba, kunguno uweyi agiyiganigaga tamu imihayo iyo ili nikujo na oyiyomba, umukikalile kakwe. Hunagwene agabhawilaga abhanhu giki, “nomo gudafunyaga ilaka libhi.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya guiganika chiza imihayo yabho haho bhatali uguyiyomba, umu mahoya gabho, kugiki bhadule gubhiza na malaka ga gubhalela chiza abhanhu bhabho, umuwikaji bhobho.

Mwanzo 8:21.

Mathayo 15:18-20.

KISWAHILI: MDOMO HAUTOI KAULI MBOVU.

Methali hiyo, huangalia utendaji kazi wa mdomo ambao huongea maneno mbalimbali. Mdomo huo, ni chombo cha kutolea sauti kwa kuongea maneno yaliyomo ndani ya moyo wa mtu. Wenyewe ni njia ya kupitishia hayo maneno yalimo moyoni mwa mtu. Ndiyo maana watu husema kwamba, “mdomo hautoi kauli mbovu.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huyafikiria maneno yaliyo ya hekima moyoni mwake, kabla hajayaongea, katika maisha yake. Mtu huyo, huwa anafanya bidii kubwa ya kuyafikiria hayo maneyo yenye hekima, katika moyo wake kwa sababu ya upendo alio nao kwa watu wake unaomuwezesha kuishi nao kwa umoja. Yeye hufaulu kuwalea vyema watu anaoishi nao kwa sababu ya yeye kuendelea kuyatumia hayo maneno ya hekima katika maongezi yake, maishani mwake.

Mtu huyo, huwa ni mfano wa kuigwa na wenzake katika kujifunza njia za kutoa kauli njema kwa kuchagua maneno yenye hekima katika maongezi, kwa sababu ya yeye kuyafikiria maneyo hayo yenye hekima kabla ya kuyaongea, katika maongezi yake. Ndiyo maana yeye huwaambia watu kwamba, “mdomo hautoi kauli mbovu.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kutumia maneno yenye hekima katika maongezi yao, kwa kuyafikiria kwanza maneno hayo kabla ya kuyatumia, ili waweze kuwa na kauli za kuwawezesha kuwalea vyema watu wao, maishani mwao.

Mwanzo 8:21.

Mathayo 15:18-20.

people1

artist-

africa-1

ENGLISH: THE MOUTH DOES NOT SPEAK EVIL THINGS.

This proverb looks at the function of the mouth that speaks a variety of words. Such mouth is an instrument for uttering words that are in a person’s heart. It is way of conveying those words which are in the heart of a person. That is why people say that, “the mouth does not speak evil things.”

This proverb is compared to a person who thinks words of wisdom in his heart before speaking them to others. Such person, in turn, makes an earnest effort to reflect on the wise sayings, in his heart, because of the true love that he has for his people. This kind of love enables him to live in harmony with them. He becomes successful in raising the people whom he lives with because of his continued use of the words of wisdom in his conversations with others.

This person is a role model for his colleagues in learning how to make good statements by choosing wise words in speaking, because of thinking the wise words before speaking them to others. That is why he tells people that “the mouth does not speak evil things.”

This proverb imparts in people an idea on how to use wise words in their discussions with others, by first thinking before using them, so that they can make good statements that will enable them to nicely raise their people in their families.

Genesis 8:21.

Matthew 15: 18-20.

 

 

825. GUPILA GO NG’HABHI GUGAFUMILAGA NG’WA NTEMI.

Ulusumo lunulo, lulolile munhu ung’habhi uyo agapijiwa na Ntemi. Unhabhi ng’wunyo, agibhonelwa na nsabhi umo bho gutajiwa ilale lwakwe. Ijinaguchola wambilijiwa, agahoya na bhazenganwa bhakwe abho bhagang’wila, “jaga ng’wa Ntemi ugang’wila agwambilijie ugulipandike ililale lyako.” Ung’habhi agashosha, “nahene nandye lugendo lo guja kwigulu.”

Unhabhi ng’wunuyo agaja uganomela Untemi umo otagijiwa ililale lwake linilo nu nsabhi ng’wunuyo. Aho wiga chena Untemi, agang’witana unsabhi ung’wila alishoshe kuli ng’winikili ililale linilo, mpaga ulishosha ng’hana. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “gupila go ng’habhi gugafumilaga ng’wa Ntemi.”

Ulusumo lunulo, lugalenagnijiyagwa kuli munhu uyo agibhonelagwa obhuchola ubhung’hana bhokwe, mpaga obhupandika, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, adagwaga ng’holo ulu wibhonelaga kunguno agahoyaga na bhanhu bhingi abho bhagantongelaga inzila ja gubhupandikila ubhung’hana. Uweyi agadulaga uguyipandika ing’hana yakwe, kunguno ya bhudiliji bho bhushauri ubho aging’hagwa nabhiye, umukikalile kakwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nu nhabhi uyo agaichola ing’hana mpaga ulipandika ililale lyakwe, kunguno nuweyi agaicholaga inhana yiniyo, ulu wibhonelaga mpaga oyipandika, umukikalile kakwe. Hunagwene agabhawilaga abhanhu giki, “gupila go ng’habhi gugafumilaga ng’wa Ntemi.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gwigulambija guichola ing’hana bho gubhudilila chiza ubhushauri, ulu bhibhonelagwa mpaga bhayipandika inhana yiniyo, kugiki bhadule gujilanghana chiza isabho jabho, umuwikaji bhobho.

Luka 18:1-8.

KISWAHILI: KUPONA KWA MASKINI HUTOKA KWA MTEMI.

Methali hiyo, huangalia mtu maskini aliyesaidiwa na Mtemi. Maskini huyo, alionewa na tajiri mmoja kwa kunyang’anywa shamba lake. Yeye alitafuta ushauri kwa kuongea na majirani zake ambao walimwambia, “nenda kwa Mtemi ukamwambie akusaidia kulipata shamba lako.” Yule maskini alijibu, “sawa naanza safari ya kwenda ikulu.”

Maskini huyo, alifika kwa Mtemi na kumueleza namna alivyonyang’anywa shamba lake na yule tajiri. Mtemi aliposikia hivyo, alimwita yule tajiri na kumwamuru alimrudishie mali hiyo mwenye shamba lake, mpaka akalirudisha kweli. Ndiyo maana watu husema kwamba, “kupona kwa maskini hutoka kwa Mtemi.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hudhurumiwa na kuitafuta haki yake mpaka anaipata, katika maisha yake. Mtu huyo, hakati tamaa ya kuitafuta haki yake anapoonewa, kwa sababu ya bidii yake ya kuomba ushauri kutoka kwa wale wanaoweza kumpatia njia za kuipata haki hiyo. Yeye hufanikiwa kuipata mali yake iliyonyang’anywa kwa sababu ya kuufanyia kazi ushauri anaopewa na wenzake, katika maisha yake.

Mtu huyo, hufanana na yule maskini aliyeitafuta haki ya kurudishwa shamba lake mpaka akalipata, kwa sababu naye huitafuta haki yake mpaka anaipata, anapoonewa, katika maisha yake. Ndiyo maana yeye huwaambia watu kwamba, “kupona kwa maskini hutoka kwa Mtemi.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na bidii ya kuzitafuta haki zao na kuzitunza kwa kuufuata ushauri uwezao kuwapatia haki hizo, ili waweze kuzilinda vizuri mali zao, maishani mwao.

Luka 18:1-8.

ENGLISH: THE HEALING OF THE POOR COMES FROM THE KING.

This proverb looks at the poor man who was helped by the Chief in getting back his land. The poor man was oppressed by a rich man who had his land confiscated. He sought advice by talking to his neighbors who told him, “Go to the Chief and tell him to help you find your farm.” The poor man replied, “Well I am starting the journey to the palace.”

The poor man went to the chief and told him how he had been robbed of his land by the rich man. Upon hearing this, the chief summoned the rich man and ordered him to return the property to his owner. The rich man returned it to the poor man. That is why people say that “the healing of the poor comes from the King.”

This proverb is likened to a man who is wronged and seeks his own righteousness until he finds it, in his life. He seeks justice when he is oppressed, because of his diligence in seeking advice from those who can give him the means to obtain it. He manages to recover his confiscated property by applying the advice given by his colleagues throughout his life.

This man is like the poor man who sought his right enough to get his land back, because he also seeks his right until he finds it, when he is oppressed in life. That is why he tells the people that “the healing of the poor comes from King.”

This proverb teaches people on how to be diligent in seeking their rights and taking care of them by following the advice which will enable them to get their rights, so that they can better protect their properties in their families.

Luke 18: 1-8.

824. NGOKO ULU YUYOGANYA YAPUJIAGWA.

Ingoko iyo yilina bhana igabhalang’hanaga noyi kugiki bhadizupulwa na lubhana. Ingoko yiniyo, ulu lwiza lubhala luipuja ng’wana oyo, igayoganyaga noyi kugiki ipandike wambilijiwa bho kufumila kubhichayo. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “ngoko ulu yuyoganya yapujiagwa.”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo, agajilang’hanaga chiza isabho jakwe bho gulomba wambilijiwa gufumila kubhiye, ulu japandikaga makoye. Umunhu ng’wunuyo, agailang’hanaga ikaya yakwe ni sabho jakwe kugiki bhadizujisola abhasambo, kunguno alina bhukalalwa bhutale najo. Uweyi agaibhejaga chiza ikaya yakwe bho gupandika wambilijiwa ubho agabhulombaga gufumila kubhiye ulu opandikaga makoye, umuwikaji bhokwe.

Umunhu ng’wunuyo agikolaga ni ngoko iyo igayoganyaga ulu yapujiagwa ng’wana oyo, kunguno nuweyi agalombaga wambilijiwa bho gufumila kubhiye ulu opandikaga makoye aha kaya yakwe, umukikalile kakwe. Uweyi agabhalangaga abhanhu bhakwe inzila ya kujilang’hanila chiza isabho ni kaya jabho. Hunagwene agabhawilaga abhanhu giki, “ngoko ulu yuyoganya yapujiagwa.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kubhiza na bhumo bho gwiyambilija wangu, ulu ng’wichabho, opandikaga mayange, umukikalile kabho, kugiki bhadule kujibheja na kujilang’hana chiza ikaya jabho, umuwikaji bhobho.

Mathayo 7:7-8.

KISWAHILI: KUKU APIGAPO KELELE AMENYANG’ANYWA.

Kuku mwenye vifaranga huwalinda sana watoto wake hao, ili wasije wakachukuliwa na mwewe. Kuku huyo, hupiga kelele, mwewe akichukua kifaranga chake ili kuomba msaada kutoka kwa wenzake. Ndiyo maana watu husema kwamba, “kuku apigapo kelele amenyang’anywa.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huilinda vizuri familia pamoja na mali yake, na kuomba msaada wa kutoka kwa wenzake anapopata matatizo, katika maisha yake. Mtu huyo, huilinda vizuri familia yake kwa kuzitumia vizuri mali zake, na kuwazuia wezi kuziiba, kwa sababu ana anaithamini sana. Yeye huijenda familia yake kwa kuiendeleza vizuri katika kuipatia mahitaji pamoja na kuomba msaasa kutoka kwa wenzake inapopata matatizo mbalimbali, ili waweze kumsaidia kuyatatua kwa haraka, katika maisha yake. 

Mtu huyo, hufanana na yule kuku aliyepiga kelele ya kuomba msaada wa kutoka kwa wenzake, baada mtoto wake kuchukuliwa na mwewe, kwa sababu naye pia huomba msaada wa kutoka kwa wenzake anapopata matatizo, maishani mwake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “kuku apigapo kelele amenyang’anywa.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuwa na umoja wa kusaidiana haraka katika kuyatatua matatizo yanayojitokeza, katika maisha yao, ili waweze kuzilinda na kuzilea vizuri familia zao, maishani mwao.

Mathayo 7:7-8.

chicken4

mother-hen

hahn

ENGLISH: WHEN A HEN CRIES OUT, SHE HAS BEEN ROBBED (WHEN A HEN CRIES OUT, SHE HAS BEEN TRAPPED).

A hen that has chicks protects them, so that they will not be picked up by hawks. She screams hawks grabs her chicks to ask for help from her companions. That is why people say, “when a hen cries out, she has been robbed (when a hen cries out, she has been trapped).”

This proverb is likened to a man who protects his family and property well, and asks for help from his peers in times of trouble. He protects his family by making good use of his property, by preventing thieves from stealing it, because he has so much value in it. He builds such family by providing it with well-being as well as asking for help from his colleagues when he has various problems, so that they can help him to solve them quickly in life.

This man is like the hen that cried out for help from her peers after her baby had been taken by the hawk, because he also asks for help from his peers when he is having problems in his life. That is why people say to him, “when a hen cries out, she has been robbed (when a hen cries out, she has been trapped).”

This proverb imparts in people an idea on how to be united enough to help each other quickly in solving problems that arise in their lives, so that they can better protect and nurture their families, in their societies.

Matthew 7: 7-8.