Ilisongo jiliseme ijo jigabhejiyagwa bho gutumila madala. Amadala genayo, gagalyenhelejaga gubhiza na tujishepo, umo idulie gwingila inhomga ulu yuditilwa moyi. Giko lulu, umunhu uyo aliyikomba imhomba yiniyo aduyimala. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “Ng’homba ya ng’wisonzo udikomba wimale.”
Usulumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatumamaga nimo uyo adagudebhile chiza, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agadumaga uguimala chiza imilimo yakwe, kunguno ya gwandya guitumama bho nduhu uguitila bhukengeji. Uweyi agapandikaga makoye mara hingi ahakaya yakwe, kunguno ya guduma ugubisha ijiliwa, umukikalile kakwe.
Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo agakomba ng’homba ng’wisonzo uduma uguimala, kunguno nuweyi agadumaga uguimala chiza imilimo yakwe, umukikalile kakwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “ng’homba ya ng’wisonzo udikomba wimale.”
Usulumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya kuidebha chiza tamu imilimo yabho, na bhandye uguitumama, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi, umuwikaji bhobho.
Marko 6:40-44.
KISWAHILI: UJI WA KWENYE KISONZO HUWEZI UKAUKOMBA UUMALIZE.
Kisonzo ni chombo ambacho hutengenezwa kwa majani fulani yaitwayo ‘madala.’ Madala hayo, husababisha kuwepo kwa vitundu vidogo vidogo ambavyo vinaweza kuruhusu uji upenye ndani yake. Hivyo basi, mtu anayekomba uji ule hawezi kuumaliza. Ndiyo maana watu husema kwamba, “uji wa kwenye kisonzo huwezi ukaukomba uumalize.”
Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hufanya kazi ambayo haielewi vizuri, katika maisha yake. Mtu huyo, hushindwa kuzimaliza vizuri kazi zake hizo, kwa sababu ya kuanza kuzitekeleza bila ya kuzifanyia utafiti. Yeye huwa anapata matatizo mara nyingi kwenye familia yake, kwa sababu ya kushindwa kuivisha chakula, katika maisha yake.
Mtu huyo, hufanana na yule aliyekomba uji wa kwenye kisonzo, akashindwa kuumaliza, kwa sababu naye hushindwa kuzimaliza kazi zake, katika maisha yake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “uji wa kwenye kisonzo huwezi ukaukomba uumalize.”
Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuzielewa vizuri kazi zao kwanza kabla ya kuanza kuzitekeleza, katika maisha yao, ili waweze kupata maendeleo mengi, maishani mwao.
Marko 6:40-44.
ENGLISH: YOU CANNOT GET RID OF BASKET’S PORRIDGE BY FINGER (NEVER CRY OVER SPLIT MILK).
A basket is a container that is made of certain leaves which are called ‘madala.’ This, in turn, results in the formation of small holes that can allow some porridge to enter into it. Thus, the person who takes porridge from it by using a finger cannot finish it. That is why people say, “you cannot get rid of basket’s porridge by finger.”
This proverb is compared to a person who does a job that he/she does not understand it well in life. Such person fails to complete that task properly, because of starting to perform it without researching it well. He/she often faces problems in the family, because of failing to get enough food for running it.
This person is like the one who failed to finish some porridge from the basket by using a finger, because he/she also fails to finish his/her works in life. That is why people say to him/her, “you cannot get rid of basket’s porridge by finger.”
This proverb teaches people on how to understand their works accurately before they start doing them, in their lives, so that they can make a lot of progress in their lives.
Mark 6: 40-44.