Research sponsored by: Don Sybertz, with special thanks to Rev Joe Healey (African proverbs, Sayings and stories)
Imbuki ya kahayile kenako ilolile bhanhu abho b’ib’ilingaga. Abhanhu bhenabho ulu b’ib’ilingaga bhagaholelaga mihayo mingi noi. Iyingi igab’izaga mihayo ya solobho, aliyo iyingi idina solobho. Ahowib’ilingilo henaho, igahoyelegwa mihayo yoseyose. Gashinaga iliho mihayo imo idiyaguja umunhu aguyiyombaga sagala, kunguno itiya wiza.
Imihayo yiniyo iliyaguleka haho wib’ilingilo duhu, kunguno idinayo isolobho umuwikaji bho bhanhu. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, ‘yeniyo igalekagwa haho wib’ilingilo. Yigelelilwe abhanhu bhasole imihayo iyo ilina solobho duhu umuwikaji b’ob’o.
Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo adeb’ile ugusolanya chiza imihayo iyo idulile gub’iza na solobho ahakaya yakwe, nulu ukubhanhu bhakwe. Umunhu ng’wunuyo alina nhungwa ja guiholela imihayo iyo iliyasolobho ulu olumanaga na bhiye. Agilangaga imihayo iya solobho kwingila kub’iye, na guyileka haho mahoyelo iyo iliyasagara.
Akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya guikomanya imihayo iyo iliya solobho kwingila hamahoya gosegose, na kuileka haho mahoya genayo iya sagara. Imihayo iya solobho igambilijaga bhanhu umugujibheja chiza ikaya ni jumuiya jabho.
Ijinagongeja, akahayile kenako kalanga bhanhu higulya ya kuleka uguiyomba imihayo ya sagara, umumahoya gabho, kunguno iyiniyo igakenagulaga kaya na jumuiya ja bhanhu. Yigelelilwe abhanhu b’ab’ize na nhungwa ja guiholela imihayo iyo iliya solobho ukabhanhu ni kaya jabho.
Kuyiniyo, yigelelilwe abhanhu bhachagule chiza imihayo iya solobho umumahoya gabho. Imihayo yiniyo, idulile gubhambilija umugujenghela upandiki bho sabho ikaya ni jumuiya jabho.
KISWAHILI: HAYO HUACHWA HAPO KWENYE MKUSANYIKO
Chanzo cha msemo huo chaangalia watu waliokusanyika mahali fulani. Watu hao huongea maneno mengi mno. Mengine huwa yana faida katika maendeleo ya jamii, lakini mengine niya hovyo.
Kwa maana hiyo, walipokusanyikia watu huongelewa maneno yoyote. Kumbe yapo yaliyo mazuri, ambayo yana faida kwa wanajamii, lakini mengine hayana faida. Hayo ni maneno ya hovyo.
Maneno hayo yaliyo ya hovyo huachwa hapo kwenye mkusanyiko, kwa sababu hayana faida maishani mwa watu. Ndiyo maana watu husema kwamba, ‘hayo huachwa hapo kwenye mkusanyiko.’ Yafaa watu wachukue yale yenye faida na kuyaacha hapo yale yasiyo na faida, maishani mwao.
Msemo huo hulinganishwa kwa mtu afahamuye kuchambua na kuyafanyia kazi maneno yale yawezayo kuwa na faida kwenye familia yake, au kwenye jumuiya yake. Mtu huyo ana tabia ya kuzungumza maneno yenye faida katika maongezi yake na wenzake. Hujifunza kutokana na maneno yenye faida wasemayo wenzake, katika maongezi yao. Mtu huyo pia huyaacha hapo yale yasiyo na faida maishani mwake.
Msemo huo hufundisha watu juu ya kuchambua maneno yenye faida kutoka kwenye maongezi yoyote na wenzao, na kuyaacha yale yaliyo ya hovyo. Maneno yenye faida husaidia watu katika kuziendeleza familia na jumuiya zao.
Zaidi hayo, msemo huo hufundisha watu juu ya kuacha kuongea maneno ya hovyo katika maongezi yao, kwa sababu maneno hayo husambalatisha familia na jumuiya za watu. Yafaa watu wajijengee tabia ya kuongea maneno yenye faida maishani mwao na katika familia zao.
Kwa hiyo, watu watakiwa kuchagua vizuri maneno yenye faida katika maongezi yao. Hayo ndiyo maneno yawezayo kuwasaidia katika kuleta maendeleo kwenye familia na jumuiya zao.
Waebrania 13:7-9.
Luka 10:38-42.
ENGLISH: THOSE ARE LEFT THERE AT THE GATHERING.
The above saying relates to how people in a gathering behave. Many things are said by people whenever they are gathered at a place, some of which can be beneficial to society, yet others which are of no value at all.
People say, ‘Those are left at the gathering’ to imply that those meaningless issues (or words) shared at the gathering need to remain there because they are of no value to people’s lives. Only aspects considered worthwhile in life should be picked out and harnessed.
Such saying is likened to a person who has the capacity to analyse words or issues before applying them, based on how beneficial they are to his/her family or community. Such a person weighs his/her words in conversations, carefully choosing those that are believed to add value in life, and ignoring worthless ones.
People use the above saying to learn about being analytical in their interaction with their peers, and therefore being able to exploit only valuable aspects that can help develop their families and communities.
Additionally, the aphorism is used to discourage empty rhetoric because it destroys society. People ought to develop a habit of saying things that can benefit and build their lives and their families.
They should therefore choose the most profitable words in their conversations. Those are the words that can help them to bring development to their families and communities.
Hebrews 13: 7-9.
Luke 10: 38-42.