Tanzania

1051. NG’WINIKILI LUGENDO

Akahayile kenako kalolile lugendo ulo lugatongelagwa na ng’winikili olo. Alihoyi nhangi uyo obhawilaga abhanhu mihayo iyo eligela aha shigu ja ha bhutongi.

 Unhangi ng’winuyo, olina bhudula bho guyibhona imihayo iyo ililonga aha hashiku ijo jizile kunguno bhuli gwene uyo agabhahangilaga gwilongaga gitumo obhawilila. Hunagwene abhanhu bhagang’witana giki, “ng’winikili lugendo.”

Akahayile kenako, kagalenganijiyagwa kuli ntongeji obhanhu uyo ang’wisanije Mulungu, umubhutongeji bhokwe bhunubho. Umunhu ng’wunuyo, agalombaga kuli Mulungu mihayo ikujo ya gubhalomela abhanhu bhakwe hayo atali ugujuhoya nabho, ulu winhiwa naoja lulu ugujubhalomela kunguno ya bhutungilija bhokwe bhunubho ukuli Mulungu. Uweyi agabhatongelaga chiza abhanhu bhakwe kunguno ya guzunya gokwe gutale ukuli Mulungu, umukikalile kakwe kenako.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nu nhangi uyo ohangaga mihayo ya nhana ukubhanhu bhakwe, kunguno nuweyi agabhawilaga abhanhu bhakwe mihayo ikujo ya gubhatongela chiza umutumami bhobho bhunabho. Hunagwene abhanhu bhagang’witanaga giki, “ng’winikili lugendo.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya gubhatongela chiza abhanhu bhabho bho gubhawila mihayo yikujo iyagubhambilija ugung’wisana Mulungu, kugiki bhadule gwikala bho mholele, na kupandika matwajo minghi, umuwikaji bhobho.

Ufunuo 3:15-16.

Yohana 1:12-13.

 

MMILIKI WA SAFARI.

Msemo huo, huangalia safari ambayo huongozwa na mmiliki wake. Alikuwepo nabii mmoja aliyewaambia watu mambo yatakayotokea kwenye siku za mbeleni.

Nabii huyo, alikuwa na uwezo wa kuyaona matukio yale ambayo yatawapata watu, kwa sababu kila tukio alilolitabiri lilitokea kama alivyosema. Ndiyo maana watu walimuita kwamba ni “mmiliki wa safari.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa kiongozi wa watu yule ambaye humtegemea Mungu katika uongozi wake. Kiongozi huyo, humuomba Mungu kwanza kabla hajaenda kutoa ujumbe kwa watu, ili apewe maneno ya hekima ya kuwasaidia watu wake kuishi vizuri, anapopewa ujumbe huo ndipo anaufikisha kwa watu, kwa sababu ya uaminifu wake kwa Muumba wake. Yeye huwaongoza watu vizuri, kwa sababu ya imani yake hiyo kubwa kwa Mungu, katika maisha yake.

Mtu huyo, hufanana na yule nabii aliyewatabiria watu wake mambo yajayo ambayo ni ya kweli, kwa sababu naye huwaambia watu maneno ya hekima yawezayo kuwaongoza vizuri maishani mwao. Ndiyo maana watu hao walimuita kuwa ni “mmiliki wa safari.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuwaongoza watu wao kwa kutumia maneno ya hekima yawezayo kuwasaidia kumtegemea Mungu, ili waweze kuishi kwa amani na kupata mafanikio mengi maishani mwao.

Ufunuo 3:15-16.

Yohana 1:12-13.

ENGLISH: THE ONE IN CHARGE OF THE JOURNEY.

This saying looks at a journey that is led by its owner. There was a prophet who told people the things that would happen in the future.

This prophet had an ability to see events that will happen to people, because every event which he predicted happened as he said. That is why people called him that, he is “the one in charge of the journey.”

This saying is related to a leader of people who relies on God in his leadership. This leader prays to God first before going to give a message to the people, so that he may be given words of wisdom which can help his people in living well. When he is given such message, he conveys it to the people, because of his loyalty to his Creator. He leads people well, because of his great faith in God, in his life.

This person is similar to the prophet who predicted the future to his people which came true, because he also tells people words of wisdom that can guide them well in their lives. That is why those people called him that, he is “the one in charge of the journey.”

This saying teaches people about leading their people by using words of wisdom that can help them enough to rely on God, so that they can live in peace and achieve many successes in their lives.

Revelation 3:15-16.

John 1:12-13.

woman-6116276__480

1050. SAMA YATINDIKWA NGOKO.

Akahayile kenako, kalolile bhukeleja bho ng’wa munhu uyo ahayaga gusama bho gulindila gumishiwa na ngoko ulujihila. Umunhu ng’wunuyo, ahayaga gusama bho gulindila gumishiwa na ngoko ulu jahila kunguno oli na tulo nyinghi. Uweyi oduka alalile duhu mpaga nose wela ubhujiku kunguno jalijakeleja uguhila inkogo ulushugu lunulo. Hunagwene abhanhu bhagang’ila giki, “sama yatindikwa ngoko.”

Akahayile kenako, kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agilendejaga uguja tumama imilimo yakwe, mpaga nose lyashila ilikanza lya milimo, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agikala wiyibhiye bhuli makanza uguja ugujutumama imilimo yakwe kunguno ya kutogwa tulo, umuwikaji bhokwe. Uweyi agachelelagwa ugulima bhuli ng’waka kunguno ya wilendeja bhokwe bhunubho ugujutumama imilimo yakwe yiniyo, umukikalile kakwe kenako.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nu nsami uyo olindilaga gumishiwa na ngoko mpaga nose ukeleja ugusama, kunguno nuweyi agilendejaga ugutumama imilimo yakwe mpaga nose lyashila ilikanza lya guitumama imilimo yiniyo, umuwikaji bhokwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “sama yatindikwa ngoko.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya guleka gwilendeja guja gujutumama milimo yabho bho gwanguha ugumisha, kugiki bhadule gutumama milimo mitale iyagubhapandikila sabho ningi jagubhambilija chiza, umuwikaji bhobho.

Mathayo 25:1-13.

Luka 21:36.

KISWAHILI: UHAMAJI ULICHELEWESHWA NA KUKU.

Msemo huo, huangalia uchelewaji wa mtu kuhama aliyesubiri kuamushwa na kuku wanapowika.  Mtu huyo, alitaka kuhama kwa kusubiri kuku wawike ndipo aamuke na kuanza safari yake hiyo ya kuhama. Yeye aliendelea kulala tu mpaka asubuhi kwa sababu jogoo nao walichelewa kuwika siku hiyo. Ndiyo maana watu walimwambia kwamba, “uhamaji ulicheleweshwa na kuku.”

Msemo huyo, hulinganishwa kwa mtu yule anayejisahau kwenda kufanya kazi zake, mpaka muda wa kufanya kazi hizo unapita, katika maisha yake. Mtu huyo, huwa amejisahau kila wakati kwenda kuyatekeleza majukumu yake kwa sababu ya kupenda kwake usingizi, maishani mwake. Yeye huchelewa kulima kila mwaka kwa sababu ya kujisahau kwake huko, katika maisha yake.

Mtu huyo, hufanana na yule mhamaji aliyesubiri kuamushwa na kuku wanapowika, mpaka mwishowe akachelewa kuhama, kwa sababu naye hujisahau kwenda kuyatekeleza majukumu yake, mpaka muda wa kufanya kazi hizo unapita, maishani mwake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “uhamaji ulicheleweshwa na kuku.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuacha uchelewaji wa kwenda kufanya kazi zao, kwa kuwahi kwenda kuzitekeleza kazi zao hizo, ili waweze kufanya kazi kubwa za kuwapatia mali za kutosha kuwasaidia maishani mwao.

Mathayo 25:1-13.

Luka 21:36.

rooster-5544252__480

animal-3242121__480

 

ENGLISH: JOURNEY WAS DELAYED BY CHICKEN.

This saying looks at the delay of a person who waited to be woken up by the roosters when they crow to start his journey. Such man wanted to travel by waiting for the chickens to roost before he got up and started his journey. He continued to sleep until morning because the roosters also crowed late that day. That is why people told him that, “journey was delayed by chickens.”

This saying is compared to the person who forgets to do his works until the time of doing them passes in his life. This person forgets to go to implement his duties because of his love of sleep, in his life. He is late to plow every year because of his self-forgetfulness, in his life.

This person is like the traveler who waited to be woken up by the chickens when they crow, until finally he became late to travel, because he also forgets to go to  accomplish his duties, until the time of doing those jobs passes in his life. That is why people tell him that, “journey was delayed by chickens.”

This saying teaches people on how to stop delaying going to do their jobs, by going to carry out their jobs, so that they can do big jobs enough to provide them with all basic needs in their lives.

Matthew 25:1-13.

Luke 21:36.

 

rooster-233898__480

1049. LYAGUKUNGA MIKOB’A.

Imbuki ya kahayile kenako, ilolile bhukungi bholi ginhu litanda. Lyalihoyi ling’ombe ilo lyalilitanda ugusheng’wa kunguno ya bhuhala bholyo. Abhanhu ulu bhahaya ugulishema lyapelaga lyabhashiga bhaduma ugulishema. Nose bhiyangula gulikunga mikanda umumagulu galyo na lyuzunya lulu ugusheng’wa. Hunagwene abhanhu bhenabho bhalitana iliong’ombe linilo giki, “lyagukunga mikob’a.”

Akahayile kenako, kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo alinambu ugutung’wa na bhiye umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agikalaga alemile ugutung’wa josejose nabhiye na hangi agashoshaga mihayo bho makala ukubhiye kunguno ya nhinda jakwe jinijo, umuwikaji bhokwe. Uweyi agadumaga uguibheja ikaya yakwe kunguno ya bhulambu bhokwe ubho gubhashokeja mihayo ya nhani abhiye, umumahoya gakwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga ni ng’ombe inhanda iyo yalemaga ugusheng’wa mpaga yutungwa mikob’a, kunguno nuweyi alinambu uyo alemile ugutung’wa guja kunhimo gosegose na bhiye umuwikaji bhokwe. Hunagwene abhanhu bhagang’witanaga giki, “lyagukunga mikob’a.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya guleka nhungwa ja bhulambu bho guzunya gutung’wa na bhiye umuchalo jabho, kugiki bhadule gwiyambilija gutumama milimo yabho chiza, umuchalo jabho jinijo.

Wagalatia 3:1-8.

KISWAHILI: LA KUFUNGA MIKANDA.

Chanzo cha msemo huo chaangalia ufungaji wa mkanda kwenye kitu ambacho ni kikali kuguswa. Alikuwepo ng’ombe mmoja ambaye alikuwa hataki kukamuliwa kwa sababu ya ukorofi wake. Mwishowe watu waliamua kumfunga mkanda miguuni mwake ndipo akakubali kukamuliwa. Ndiyo maana watu hao walimuita ng’ombe huyo kwamba ni “la kufunga mikanda.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ni mwenye kiburi katika maisha yake. Mtu huyo, huwa hataki kutung’wa kwenda kufanya chochote na wenzake, na tena huwajibu watu kwa kauli mbaya, kwa sababu ya kiburi chake hicho, maishani mwake. Yeye hushindwa kutengeneza familia yake kwa sababu ya kiburi chake hicho cha kuwajibu wenzake kwa maneno mabaya, katika maongezi yake.

Mtu huyo, hufanana na yule ng’ombe mjeuri aliyekataa kukamuliwa, mpaga akafungwa mkanda miguuni mwake ndipo akakubali, kwa sababu naye hukataa kutumwa na wenzake, maishani mwake. Ndiyo maana watu humuita kuwa ni “la kufunga mikanda.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuachana na tabia ya kuwa na kiburi kwa kukubali kutumwa na wenzao, ili waweze kusaidiana vizuri katika kuyatekeleza majukumu yao, kijijini mwao.

Wagalatia 3:1-8.

cow-7301439__480

ENGLISH: IT IS OF FASTENING BELTS.

The source of this saying looks at the tying of a belt on something that is hard to touch. There was a cow that did not like to be milked because of its rudeness. Finally the people decided to tie a belt around her legs and then she agreed to be milked. That is why those people said about such cow that “it is of fastening belts.”

This saying is compared to the person who is proud in his life. Such person does not like to be pushed to do anything by his colleagues, and again he answers people with wicked words, because of his pride, in his life. He fails to form well his family because of his pride in answering his colleagues by using ruthless words, in his speech.

This person is similar to the cow that refused to be milked, until when a belt was tied around her legs and then she accepted, because he also refuses to be sent by his companions, in his life. That is why people say about him that, “it is of fastening belts.”

This saying instills in people a clue of abandoning habit of being proud by accepting to be sent by their nobles, so that they can help each other well in carrying out their duties in their village.

Galatians 3:1-8.

1048. LYANG’WANIKI ADALAB’ULAGA.

Imbuki ya kahayile kenako, yingilile ku bhutuji bho mbula bho likanza lilihu gete iyo igalenganijiyagwa na ng’waniki uyo azimizaga bho nduhu ugulabhula inuma.

Aho kale gulihoyi ng’waka uyo mbula nhale igatula ahikanza lya jidiku iyo igasola makanza malihu gete kunguno yaliidoyaga wangu. Imbula yiniyo, igandya gutula haho lyandya duhu ilijidiku bho nduhu ugugata mpaga giki abhanhu bhuyuduma bhangi agulimila ingese kunguno ya mbula yiniyo. Hunagwene abhanhu bhagayomba giki imbula ya ung’waka gunuyo, “lyang’waniki adalab’ulaga.”

Akahayile kenako, kagalenjiyagwa kuli munhu uyo agatumama milimo yakwe bho gwigulambija chiza mpaga jashila ijidiku, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, aganguhaga ugumisha ogatumama mimimo yake bho nduhu gwilendeja mpaga oimala chiza, kunguno ya bhukalalwa na bhukamu bhokwe bho guitumama imilimo yiniyo, muwikaji bhokwe.  Uweyi agaponaga majiliwa mingi noyi aha kaya yakwe kunguno ya wigulambija bhokwe ubho gutumama milimo bho bhukamu bhutale chiniko, umukikalile kakwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga ni mbula iyo igatula mpaga jushila ijidiku bho nduhu ugugata, kunguno nuweyi agigulambijaga gutumama milimo yakwe bho nduhu uguyileka mpaka jashila ijidiku, umukikalile kakwe kenako. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki agatumamaga milimo “lya mwaniki adalab’ulaga.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya gwigulambija kutumama milimo yabho chiza, bho gwanguha uguja ukumilimo yabho yiniyo, kugiki bhadule gupandika sabho ningi, umuwikaji bhobho.

 

Mwanzo 2:15.

Mhubiri 11:4.

Mithali 6:9.

 

KISWAHILI: LA MSICHANA ASIYEANGALIA NYUMA.

Chanzo cha msemo huo, chatokea kwenye unyeshaji wa mvua iliyochukua mda mrefu kabisa inayofananishwa na msichana asiyeangalia nyuma katika safari yake kwa sababu ya huleta uhai katika aridhi.

Hapo zamani, ulitokea mwaka ambao mvua kubwa ilinyesha kwa mfuluzo wa siku nyingi bila kukatika wakati wa masika. Mvua hiyo, ilipoanza kunyesha ilindelea hivyo, mpaka watu wakashindwa kupalilia palizi kwenye mashamba ya mazao yao kwa sababu ya ukubwa wake huo. Ndiyo maana watu walisema kwamba mvua ya mwaka huu ni “la msichana asiyeangalia nyuma.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hufanya kazi zake kwa bidii kubwa mpaka anazimaliza, katika maisha yake. Mtu huyo, huanza kufanya kazi wakati yanapoanza masika kwa kujibidisha katika kuyatunza vizuri mazao yake mpaka anayamaliza vizuri kwa sababu ya bidii yake hiyo ya kufanya kazi maishani mwake.  Yeye hupata mavuno mengi katika mashamba yake kwa sababu ya kupenda kwake kuyatekeleza vizuri majukumu yake hayo, katika maisha yake.

Mtu huyo, hufanana na mvua ile iliyonyesha kwa mfululizo mpaka kipindi cha masika kikaisha, kwa sababu naye hujibidisha kuyatekeleza vizuri majukumu yake mpaka anayamaliza vizuri bila kuyaacha, katika maisha yake hayo. Ndiyo maana watu humwambia kwamba yeye hufanya kazi “la msichana asiyeangulia nyuma.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kujibidisha kuyatekeleza vizuri majukumu yao, kwa kuwahi kwenda kazini, ili waweze kupata mafanikio mengi zaidi maishani mwao.

Mwanzo 2:15.

Mhubiri 11:4.

Mithali 6:9.

portrait-11

blue-khruem-1571592__480

 

ENGLISH: IT IS THAT OF A GIRL WHO NEVER LOOKS BACK.

The source of the overhead saying came from the rainfall that lasted for a long time. This rain is compared to a girl who does not look back in her journey because of bringing life to the land.

Once upon a time, there was a year in which heavy rain fell for many days without stopping during the spring season. This rain carried on raining until people were unable to weed their crops because of its non stop. That is why people called that rain that “it is that of a girl who never looks back.”

This saying is compared to the person who does his work with great effort until he finishes it in his life. This person starts working when the spring season starts by taking care of his crops well until he finishes them because of his hard working way in his life. He gets a lot of harvest in his fields because of his love to carry out his duties well in his life.

This person resembles the rain that rained continuously until the end of the spring season, because he also carries out his duties well until he finishes them well without leaving them in his life. That is why people said about his works that, “it is that of a girl who never looks back.”

This saying imparts in people an idea of carrying out their duties well, by working well, so that they can get more success in their lives.

Genesis 2:15.

Ecclesiastes 11:4.

Proverbs 6:9.

 

umbrella-

1047. BHANDYAGA GWILEBHA MAGANDA.

Akahayile kenako, kahoyelile bhanhu abho bhilebyaga maganda muchalo jilebhe. Bhali hoyi bhanhu bhab’ili abho bhali ng’wichobha. Uumo obho agab’iza na jikolo jingi kunebya ung’wiye kunguno ya bhuguji bho sabho bhokwe ubho gutumila mpango go higulya.

Ung’wiye agabhiza na mpango go aha silili, ub’iza giki olebhiwa amaganda nu ng’wiyile ng’wunuyo. Hunagwene abhanhu bhagayomba giki, “bhandyaga gwilebha maganda.”

Akahayile kenako, kagalenganijiyagwa kubhanhu abho bhagajitumilaga inguzu jabho chiza, bho gwikija gutumama milimo, umuwijaji bhobho. Abhanhu bhenabho, bhagipunaga diyu bhaja gujutumama milimo yabho ahikanza lya malima kwa kunguno ya bhukamu bho gutumama milimo bhobho bhunubho, umuwikaji bhobho. Abhoyi bhagapandika sabho ningi noyi bhuli ng’wene kunguno ya wikindi bhobho ubho gutumama milimo yabho bhunubho, umukikalile kabho.

Abhanhu bhenabho, bhagikolaga nabho wilebhyaga maganda ga gupandika jikolo bho mpango gohigulya ulu bhaligula ijikolo jinijo, kunguno nabhoyi bhagikindaga ugutumama imilimo yabho bho bhukamu bhutale, umuwikaji bhobho. Hunagwene abhanhu bhagabhawilaga giki, “bhandyaga gwilebha maganda.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya gwikomeja gutumama milimo yabho bho bhukamu bhutale, kugiki bhadule gupandika sabho ningi ubhutumami bho milimo yabho bhunubho, umuwikaji bhobho.

Luka 16:11-13.

Warumi 13:8-10.

Yakobo 1:9.

Warumi 15:1-2.

KISWAHILI: WAMEANZA KUZIDIANA UWEZO.

Msemo huo, huongelea juu ya watu waliokuwa wakizidiana uwezo wa kupata mali kwenye kijiji fulani. Walikuwepo watu wawili waliokuwa wakitafuta mali. Mmoja wao alipata mali nyingi kumzidi mwenzake kwa sababu ya ununuaji wake wa bei ya juu.

Mwenzake alikuwa akinunua vitu kwa bei ya chini, akawa amezidiwa uwezo na mwenzake huyo. Ndiyo maana watu walisema kwamba, “wameanza kuzidiana uwezo.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa watu wale ambao huzitumia nguvu zao vizuri kwa kushindana kufanya kazi, katika maisha yao. Watu hao, huamuka asubuhi na kuwahi kwenda kufanya kazi zao unapofika wakati wa kilimo kwa sababu ya bidii yao hiyo ya kuyatekeleza vizuri majukumu yao, maishani mwao. Wao hupata mali nyingi sana kila mmoja kwa sababu ya ushindani wao huo wa kufanya kazi kwa namna hiyo, katika maisha yao.

Watu hao, hufanana na wale waliokuwa wakizidiana uwezo wa kupata mali kwa bei ya juu, kwa sababu nao, hushindana katika kufanya kazi zao kwa bidii kubwa, maishani mwao. Ndiyo maana watu huwaambia kwamba, “wameanza kuzidiana uwezo.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kujibidisha kufanya kazi zao kwa juhudi kubwa, ili waweze kupata mali nyingi katika utekeleji wa majukumu yao, maishani mwao.

Luka 16:11-13.

Warumi 13:8-10.

Yakobo 1:9.

Warumi 15:1-2.

fight-1564959__480

angolan-509593__480

women-5935801__480

ENGLISH: THEY HAVE BEGUN TO SURPASS EACH OTHER IN TERMS OF WEALTH.

This saying talks about people who were competing with one another to get wealth in a certain village. There were two people who were looking for property. One of them got more wealth than the other because of his high-priced purchases.

His colleague was buying things at a low price, he was overwhelmed by that colleague. That is why people said that, “they have begun to surpass each other in terms of wealth.”

This saying is compared to people who nicely use their energy by competing to work in their lives. These people wake up in the morning and go to do their work when it is time to farm because of their hard working situation which is strong enough to carry out their duties well in their lives. They get a lot of wealth each one of them because of their competition to work in that way in their lives.

These people are similar to those who were competing with each other ing using their abilities to get property at a high price, because they, too, compete in doing their works with great effort, in their lives. That is why people tell them that, “they have begun to surpass each other in terms of wealth.”

This saying teaches people about forcing themselves to do their works with great effort, so that they can get a lot of wealth in fulfilling their responsibilities in their lives.

Luke 16:11-13.

Romans 13:8-10.

James 1:9.

Romans 15:1-2.