sayings

829. NG’WIKAJI ATINA NGOFYOLO.

Akahayile kenako, kalolile wikaji bho ng’wana munhu uyo wikalaga ha kaya ya ng’wa munhu nhebhe. Umunhu ng’wunuyo otumamaga milimo ya ha kaya yiniyo bho gulipwa gitumo bhiyiigwila. Uweyi olipagwa hela ngehu duhu, kunguno olilaga hayo ijiliwa bhuli lushigu.

Kuyinyo lulu, ung’wikaji ng’wunuyo, oli adikalaga na hela ningi umukikalile kakwe, kunguno ihela ijingi ojililaga hayo ulu otengelwa ijiliwa. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “ng’wikaji atina ngofyolo.”

Akahayile kenako, kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatumamaga nimo uyo gudadulile ugung’wambilija ahashigu ijahabhutongi, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agatumamaga nimo uyo gugang’wenhelaga hela ngehu duhu ijo agajigulilaga jiliwa ja gulya lushigu lumo duhu jashila. Uweyi agagayiyagwa ihela ja gung’wambilija ulu opandikaga makoye guti ga bhusatu, aha kayaya yakwe, kunguno ya gwisanga ojimala pye ihela jakwe bho gujigulila jiliwa, umuwikaji bhokwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nu mwikaji uyo opandikaga hela ngehu, kunguno nu weyi agapandika hela ngehu ijo agajigulilaga jiliwa, mpaka wisanya adina hela, ija gung’wimbilija umu makoye. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “ng’wikaji atina ngofyolo.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya kutumama milimo yabho bho gujilang’hana chiza ihela jabho, kugiki bhadule kubhiza na hela ja gubhambilija umu makoye gabho.

Tito 3:3.

2Petro 2:19.

KISWAHILI: MKAAJI HANA KIPATO.

Msemo huo, huangalia ukaaji wa mtu aliyeishi katika familia ya mtu fulani. Mtu huyo, aliishi kwa kufanya kibarua kwenye familia hiyo ambayo ilimlipa kwa kadiri ya makubariano yao. Yeye alilipwa pesa kidogo tu kwa sababu ya pesa nyingi kukatwa kwa ajili ya chakula alichokula hapo kila siku.

Kwa hiyo basi, hali hiyo ilipelekea kwa yeye kuwa na pesa kidogo katika maisha yake, kwa sababu ya hela yake yingine kukatwa na familia hiyo kwa ajili ya kulipia chakula alichopewa. Ndiyo maana watu husema kwamba, “mkaaji hana kipato.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hufanya kazi isiyoweza kumsaidia katika siku za mbeleni, maishani mwake. Mtu huyo, huwa anafanya kazi ambayo humwingizia hela kidogo tu ambayo huimalizia kwenye mahitaji ya kununulia chakula cha siku moja. Yeye hukosa pesa za kuweza kumsaidia anapokumbwa na matatizo mbalimbali yakiwemo yale ya kuumwa, kwenye familia yake, kwa sababu ya kujikuta amezimalizia pesa zake zote kwenye mahitaji ya kununulia chakula, maishani mwake.

Mtu huyo, hufanana na yule mkaaji aliyekuwa akipata pesa kidogo alizozimalizia kwenye chakula, kwa sababu naye huzimalizia pesa zake kwa kununulia chakula, mpaka anafikia hatua ya kuishi bila pesa. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “mkaaji hana kipato.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuyatekeleza majukumu yao, kwa kuzitunza vizuri pesa zao, ili waweze kuwa na ziada ya kuwatatulia matatizo yatakayokumba, maishani mwao.

Tito 3:3.

2Petro 2:19.

Tanzania1

massai1

ENGLISH: AN OCCUPANT HAS NO INCOME.

This saying looks at a residence of a person who lived in someone’s family. This man made a living by working for that family which paid him according to their agreement. He was paid only a small amount of money because of the large amount of money he was deducted for the food he ate there every day.

As a result, the situation led to him having less money in his life, because of his extra money being cut off by the family to pay for the food which he was given. That is why people said, “an occupant has no income.”

This saying is likened to a man who does an unhelpful work in the future, in his lifetime. This person, in turn, does work that earns him a small amount of money that ends up in the need to buy food for one day. He runs out of money after having various problems which include illness, in his family, because he finds himself spending all his money on necessities to buy food in lifetime.

This person is like the resident who used to earn a little money on food, because he also spends his money on food, until he reaches the point of living without money. That is why people say to him, “an occupant has no income.”

The saying teaches people on how to fulfill their responsibilities, by taking good care of their money, so that they can have more of it for solving problems that will arise in their future lives.

Titus 3: 3.

2 Peter 2:19.

820. KUNG’WENYA IKIGUTAJA.

Akahayile kenako, kingilile kuli munhu uyo obhasumbilaga abhageni wakwe, bho lihanga lya bhuyegi, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, obhinhaga lubhango logudula gubhigutya abhageni bhakwe bhenabho.

Gashinaga lulu, ung’wikaji ulu ug’wanukula ungeni bho bhuyegi agung’wigutya, kunguno agung’winha wasa bho gwiyigwa guti giki wigutaga, nulu jigabhiza jidololo ijiliwa jakwe.  Ulu jafunyiagwa na moyo ng’wela na bhuyegi ijiliwa jinijo jigutosha duhu ugung’witya ungeni ng’wunuyo. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “kung’wenya ikigutaja.”

Akahayile kenako, kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo alina bhutogwa bho gwikala na bhanhu bho bhuyegi, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agaitumamaga imilimo yakwe bho gwiyambilija na bhiye bhayegile kihamo. Uweyi agabhasumbilaga chiza abhageni bhakwe, kunguno bhagabhubhonaga ubhuyegi bhokwe, bho kikalile kakwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo agabhigutyagwa abhageni bhakwe bho gubhasumbila na bhuyegi, kunguno nu weyi alina bhutogwa bho gwikala nabhiye bho bhuyegi bhunubho. Uweyi agabhalangaga abhanhu bhakwe higulya ya gubhiza na bhutogwa  kubhanhu bhabho, umukikalile kabho. Hunagwene agabhawilaga abhanhu giki, “kung’wenya ikigutaja.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya gubhiza na bhutogwa bho gubhasumbila na bhuyegi abhichabho, umukikalile kabho, kugiki bhadule gwikala bho mholele, umuwikaji bhobho.

Waebrania 13:1-2.

KISWAHILI: TABASAMU HUSHIBISHA.

Msemo huo, ulitokea kwa mtu yule ambaye alikuwa na tabia ya kuwakaribisha wageni wake kwa furaha, katika maisha yake. Mtu huyo, alikuwa akiwapa Baraka wageni wake hao zenye furaha ya kuwawezesha kujisikia kama wameshiba.

Kumbe basi, mwenyeji akimpokea mgeni kwa furaha humshibisha kwa sababu ya kumpatia hali ya kujisikia kama ameshiba, hata kama chakula chake kitakuwa kidogo. Chakula hicho kikitolewa kwa moyo mweupe uliojaa furaha, kitamtosha kumshibisha mgeni wake huyo. Ndiyo maana watu husema kwamba, “tabasamu hushibisha.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ni mwenye upendo wa kuishi na watu kwa furaha na uchangamfu, katika maisha yake. Mtu huyo, huyatekeleza majukumu yake kwa kusaidiana na wenzake akiwa katika hali ya furaha. Yeye huwakaribisha wageni wake vizuri kwa sababu ya wao, kuiona furaha yake hiyo, maishani mwake.

Mtu huyo, hufanana na yule aliyewashibisha wageni wake kwa kuwapokea akiwa na uso wa tabasamu, kwa sababu naye ana upendo wa kuishi na wenzake kwa furaha hiyo. Yeye huwafundisha pia watu wake juu ya kuuishi upendo huo, katika maisha yao. Ndiyo maana huwaambia watu kwamba, “tabasamu hushibisha.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuwa na upendo wa kuwakaribisha wageni wao kwa furaha, katika maisha yao, ili waweze kuishi kwa amani, maishani mwao.

Waebrania 13:1-2.

ENGLISH: A SMILE MAKES ONE SATISFIED.

This saying came from the man who had a habit of welcoming his guests at his family with joy. He was blessing them with sacred sign which gave to them a joy of making them feel as if they were satisfied.

On the other hand, if a host welcomes a visitor, he will satisfy him/her with the feeling of being satisfied, even if his food is meager. This means that, some food which is provided with a happy heart will suffice to satisfy the guest. That is why people say, “a smile makes one satisfied.”

This saying is likened to a person who likes to live with people happily and cheerfully in life. This person, in turn, fulfills his or her responsibilities by helping others in a happy manner. He/she warmly welcomes guests to the point of giving joy to them.

This person resembles the one who entertained his guests by welcoming them with a smile on his face, because he too likes to live happily with his/her friends. He/she also teaches people on how to live peacefully with others in their families. That is why he/she tells people that, “a smile makes one satisfied.”

This saying teaches people about having a genuine love of welcoming their guests happily, in their families, so that they can live in peace with one another in their societies.

Hebrews 13: 1-2.

817. MAKOYE GAGAMANYICHAGA BHUMUNHU.

Amakoye jili jigemelo ja ng’wa munhu ijo jigolecha umo agiyumiligijaga, umukikalile kakwe. Ijigemelo jinijo jigolechaga matwajo gakwe umunhu ng’wunuyo ayo gagamanyichaga igiki alinshikanu, umukikalile kakwe. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “makoye gagamanyichaga bhumunhu.”

Akahayile kenako, kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agolechaga bhushikanu bho gwiyumilija ulu opandikaga mayange, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agolechaga wigulambija bhutale ubho bhugang’wambilija ugugamala wangu amakoye ayo alinago. Uweyi agadulaga uguginja amakoye gakwe genayo, nu gubhambilija abhiye abho bhali na mayange, kunguno ya wiyumilija bhokwe bhunubho, umukikalile kakwe.

Akahayile kenako, kagikolaga nu munhu uyo alina bhushikanu bho gwiyumilija gugamala wangu amakoye gakwe, kunguno nuweyi ali na wiyumilija bho gugamala wangu amakoye ayo alinago, umukikalile kakwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “makoye gagamanyichaga bhumunhu.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya gubhiza na wiyumilija bho gubhambilija abhanhu bhabho ugugamala wangu amakoye gabho, kugiki bhadule gubhulang’hana chiza ubhumunhu bhobho, umuwikaji bhobho.

Yohane 4:1-2.

KISWAHILI: SHIDA HUDHIHIRISHA UTU.

Shida ni jaribu la mwanadamu ambalo huueleza uvumilivu wake katika mahangaiko ya maisha. Jaribu hilo, huonesha matunda ya mtu huyo ambayo huonesha ukomavu alizo nao katika kuvumilia mahangaiko yake. Ndiyo maana watu husema kwamba, “shida hudhihirisha utu.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huonesha hali ya uvumilivu mkubwa katika kuyatatua matatizo yake, maishani mwake. Mtu huyo, hujibidisha kutafuta njia za kuyamaliza matatizo yake kwa uvumilivu mkubwa. Yeye huweza kuyaondoa au kuyamaliza mapema matatizo yanayomkumba, na kuwasaidia pia wenzake walioko kwenye matatizo ili waweze kuondokana nayo, kwa sababu ya uvumilivu mkubwa alio nao, maishani mwake.

Msemo huo, hufanana na mtu yule aliye na uvumilivu wa kuyatatua matatizo yake mapema, kwa sababu naye, anao uvumilivu huo, katika maisha yake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “shida hudhihirisha utu.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuwa na uvumilivu wa kuwasaidia katika kuyamaliza mapema matatizo yao, ili waweze kuulinda vizuri utu wao, maishani mwao.

Yohane 4:1-2.

africa1

injecting

taking madicine

ENGLISH: PROBLEMS MAKE ONE’S CHARACTER KNOWN.

Adversity is a human trial that describes his/her perseverance in anxieties of life. Such test, in turn, reflects person’s fruits, which also reflects his maturity in enduring his anxieties. That is why people say that, “problems make one’s character known.”

This saying is compared to a man who shows great patience in solving his problems in life. This person strives to find ways for solving his problems with great patience. He manages eradicate them that beset him. He can help those who are struggling to solve their problems, because of his great patience in eradicating them.

This man is similar to the person who has patience in solving his problems, because he, too, has that patience in his life. That is why people say to him that, “problems make one’s character known.”

The saying teaches people on how to be patient enough to help others solve their problems early, so that they can better protect their personality in their societies.

John 4: 1-2.

816. DIMAGA LUSHU ULYE NYAMA.

Imbuki ya kahayile kenako, ihoyelile munhu uyo agayelaga na lushu lokwe, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agalutumamilaga ulushu lwokwe nululo, bho guchembela ginhu iyo alajibhone uko alisiminzila. Uweyi ulu ushiga aho jiliho nyama adukoya uguichemba inyama yiniyo na guilya, kunguno alinajo ijitumamilo jakwe.

Aliyo lulu, umunhu uyo adina lushu, ulu usanga nyama aguduma ugupandika nulu kanofu, ulu adalombile gubhiye, kunguno adayelaga higiki, bho gwikala na jitumamilo jakwe, umukikalile kakwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “dimaga lushu ulye nyama.”

Akahayile kenako, kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agikalaga higiki bho gujiyelana ijitumamilo jakwe, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agikalaga wibhegelejije chiza ijinabhutumami bho milimo yakwe ni jinagubhambilija abho bhali makoye, kunguno ya kujikalana makanza gose ijitumamilo jakwe.  Uweyi agapandikaga matwajo mingi umubhutumami bho milimo yakwe, kunguno ya gwikala higiki bho gujikalana chiza ijitumamilo jakwe jinijo.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo agikalaga higiki bho guyela na lushu lokwe, kunguno nuweyi agikalaga higiki bho gujikalana chiza ijitumamilo jakwe, umukikalile kakwe. Uweyi agabhalangaga abhanhu bhakwe nzila ja gwikala higiki bho gujikalana chiza ijitumamilo jabho. Hunagwene agabhawilaga abhanhu giki, “dimaga lushu ulye nyama.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya gwikala higiki bho gujikalana chiza ijitumamilo jabho, umukikalile kabho, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi, umuwikaji bhobho.

Mathayo 25:10-13.

KISWAHILI: SHIKA KISU ULE NYAMA.

Chanzo cha msemo huo, chamongelea mtu ambaye hutembea na kisu chake, katika maisha yake. Mtu huyo, hukitumia kisu chake hicho, kwa kukatia kitu chochote anacho kiona kule atembeleako. Yeye akikuta nyama hatahangaika kuikata na kuila kwa sababu anacho kitendea kazi chake.

Lakini basi, mtu yule ambaye hana kisu akituta nyama atashindwa kupata hata mnofu mdogo, kwa sababu ya kutokujiweka tayari, katika maisha yake. Ndiyo  maana watu humwambia kwamba, “shika kisu ule nyama.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huwa amejiweka tayari kwa kutembea akiwa na kitendea kazi chake, katika maisha yake. Mtu huyo, huwa amejiandaa katika utekelezaji wa majukumu yake, yakiwemo yale ya kuwasaidia watu walioko kwenye matatizo, kwa sababu ya kuwa nacho muda wote kitendea kazi chake hicho. Yeye hupata mafanikio mengi katika utendaji wake wa kazi kwa sababu ya kujiweka tayari kwa kutendea akiwa na kitendea kazi chake hicho.

Mtu huyo, hufanana na yule aliyekuwa tayari kwa kutembea akiwa na kisu chake kokote alikoenda, kwa sababu naye huwa yuko tayari kwa kutembea akiwa na kitendea kazi chake hicho, katika maisha yake. Yeye huwafundisha pia watu wake namna ya kuwa na vitendea kazi vyao popote wanapoenda. Ndiyo maana huwaambia watu kwamba, “shika kisu ule nyama.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kujiweka tayari muda wote kwa kutembea wakiwa na vitendea kazi vyao, katika maisha yao, ili waweze kupata mafanikio mengi, maishani mwao.

Mathayo 25:10-13.

cut-meat-

meat-

 ENGLISH: GET HOLD OF A KNIFE AND EAT MEAT.

The cradle of the above saying speaks of a man who walks with a knife in life. This man was using his knife to cut anything which he saw on his way. If he found meat, he would not bother to cut it and eat because he had a tool cutting it.

But then, the man who does not have a knife will not be able to get even a little meat, because of his unpreparedness in his life. That is why people say to him that, “get hold of a knife and eat meat.”

This saying is compared to a person who is prepared enough to walk with a tool in life. This person carries out his or her responsibilities, including helping those who are in need, because of being prepared. He/she achieves great success in daily works because of his/her willingness to use his/her tool whenever it is needed.

This person is like the one who walked with his knife wherever he went, because he walks with his tool in his life. He also teaches his people on how to be with their tools wherever they go. That is why he tells them that “get hold of a knife and eat meat.”

This saying teaches people on how to be prepared all the time by walking with their tools, in their lives, so that they can have more success in their societies.

Matthew 25: 10-13.

814. BHUBHING’HOLO BHUGANANULAGA ABHANHU.

Ubhubhing’holo jili jito ja gung’wima ginhu umunhu uyo alina makoye. Umunhu uyo alina makoye ng’winuyo, adulile nulu gunanuka bho gucha na nzala aliyo ijiliwa jilihoyi, kunguno ya wiming’holo bhunubho. Hunagwene abhanhu bhagayombaga giki, “bhubhing’holo bhugananulaga abhanhu.”

Akahayile kenako, kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo alina ng’holo ya bhubhi, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agalemaga ugubhinha ijiliwa ijo alinajo, abhanhu abho bhalina makoye, kunguno ya wiming’holo bhokwe bhunubho. Uweyi agabhalekaga bho nduhu ugubhambilija abho bhali na makoye bhenabho, mpaka nose bhananuka aliyo isabho alinajo, umuwikaji bhokwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo aliming’holo, kunguno nuweyi alina ng’holo ya bhubhi, iyo idabhabhonelaga isungu abhiye abho bhali na makoye, umukikalile kakwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “bhubhing’holo bhugananulaga abhanhu.”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya gulekana na ng’holo ya wiming’holo, bho gubhagunana abhichabho abho bhali na makoye, umukikalile kabho, kugiki bhadule gubhulang’hana chiza ubhupanga bho bhanhu bhabho bhenabho.

Luka 6:9-10.

KISWAHILI: UCHOYO HUUA WATU.

Uchoyo ni kitendo cha kumunyima kitu mtu aliyekumbwa na matatizo. Mtu huyo, mwenye matatizo, huweza hata kupoteza maisha kwa kukosa chakula, pamoja na chakula hicho kuwepo, kwa sababu ya uchoyo huo. Ndiyo maana watu husema kwamba, “uchoyo huua watu.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye ana roho mbaya, katika maisha yake. Mtu huyo, hukataa kuwasaidia wenzake walioko kwenye matatizo ya kukosa chakula hata kama ancho chakula hicho, kwa sababu ya uchoyo wake huo. Yeye huwaacha bila kuwasaidia watu hao, ambao mwishowe huwa wanafikia hatua ya kupoteza maisha, wakati mali anazo, maishani mwake.

Mtu huyo, hufanana na yule ambaye ni mchoyo aliyekataa kuwasaidia wenye shida, kwa sababu naye ana roho mbaya isiyowaonea huruma wenzake hao walioko kwenye matatizo mbalimbali, katika maisha yake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “uchoyo huua watu.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuachana na roho ya uchoyo, kwa kuwasaidiana wenzao waliokumbwa na matatizo, katika maisha yao, ili waweze kuyaokoa na kuyalinda maisha ya wenzao hao.

Luka 6:9-10.

elder

cartoons

chicken1

ENGLISH: GREED KILLS PEOPLE.

Covetousness is an act of denying supporting someone who has problems. This person who has problems may even lose life because of lacking food and other basic needs, despite the food being present, just because of that greed. That is why people say that “greed kills people.”

This saying is likened to a person who has an unkind spirit in life. This person refuses to help his/her colleagues who are suffering from malnutrition, even though he/she has plenty of food because of his/her greed. He/she leaves them without helping those people, who eventually reach the point of losing their lives, while possessions are present in the house.

This person is like the greedy person who refuses to help the needy, because he/she has a bad spirit that does not show compassion to those who are great need of help. That is why people say that “greed kills people.”

This proverb imparts in people an idea of stopping a spirit of greed, by helping each other in trouble, in their lives, so that they can save and protect the lives of their family members.

Luke 6: 9-10.