Mwanza

1247. WIKIJIWA IWE.

Oliyohi munhu uyo aliobhucha iwe itale ukumabhega gakwe alichalile kukaya yakwe. Umunhu ng’wunuyo agalibhucha iliwe linilo mpaga wambilijiwa na munhu nhebhe uyo agang’wikija unigo gunuyo ukumabhega gakwe. Hunagwene abhanhu bhagayomba giki, “wikijiwa iwe.”

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agatumamaga milimo midamu bho wiyumilija bhutale, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, alina nguzu ijo agajitumilaga bho gutumama milimo midito mpaga opandika majiliwa mingi kunguno ya wiyumilija bhokwe bhunubho, umuwikaji bhokwe. Uweyi agabhalangaga abhanhu bhakwe gutumama milimo midamu mpaga bhadula gung’wambilija gupandika sabho ningi aha kaya yakwe, umubhutumami bhokwe bhunubho.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo oliobhucha liwe litale mpaga wambilijiwa na ng’wiye, kunguno nuweyi agatumamaga milimo midito bho gubhalanga abhanhu bhakwe mpaga bhadule gung’wambilija chiza, a kaya yakwe. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “wikijiwa iwe.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya gwiyumilija gutumama milimo yabho bho bhukamu bhutale mpaga bhadule gupandika sabho jagubhambilija chiza umuwikaji bhobho.

Yohana 12:40.

Mathayo 11:28-30.

KISWAHILI: AMESHUSHIWA JIWE.

Alikuwepo mtu aliyebeba jiwe kubwa kwenye mabega yake akilipeleka nyumbani kwake. Mtu huyo alilibeba kwa uvumilivu jiwe hilo mpaka akasaidiwa na mtu fulani aliyemshushia mzigo huo kutoka kwenye mabega yake. Ndiyo maana watu walisema kwamba, “ameshushiwa jiwe.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye hufanya kazi ngumu kwa uvumilivu mkubwa, katika maisha yake. Mtu huyo, ana nguvu anazozitumia katika kufanya kazi hizo nzito mpaka anapata mazao mengi ya chakula kwa sababu ya uvumilivu wake huo, maishani mwake. Yeye huwafundisha watu wake kufanya kazi hizo ngumu mpaka wanaweza kumsaidia kupata mali nyingi kwenye familia yake, katika maisha yake.

Mtu huyo, hufanana na yule aliyebeba jiwe kubwa mabegani mwake kwa uvumilivu mpaka akasaidiwa na mwenzake, kwa sababu naye pia hufanya kazi nzito kwa kuwafundisha watu wake mpaka wanaweza kumsaidia kutua mzigo mzito katika familia yake. Ndiyo maana watu husema kwamba, “ameshushiwa jiwe.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuvumilia kufanya kazi zao kwa bidii kubwa mpaka waweze kupata mali za kutosha kuwasidia vizuri katika maishani yao yote.

Yohana 12:40.

Mathayo 11:28-30.

ENGLISH: HE HAS BEEN STONED.

There was a man who carried a big stone on his shoulders to his home. This man patiently carried it until he was helped by someone who lowered the burden from his shoulders. That is why people said that, “he has been stoned.”

This saying is equaled to a person who works hard with great patience, in his life. That person has strength of using in doing those heavy tasks until he gets a lot of food crops because of his patience in his life. He teaches his people in doing hard works until they can help him in getting more wealth for his family, in his life.

This person is similar to the one who carried a big stone on his shoulders with patience until he was helped by his colleague, because he also does heavy works by teaching his people until they can help him to land heavy burdens in his family. That is why people say that, “he has been stoned.”

This saying teaches people to persevere in doing their works with great effort until they get enough wealth for supporting them well throughout their lives.

John 12:40.

Matthew 11:28-30.

muay-thai-150006_1280

1246. AGALAGILA JITUNDULU GETE.

Imbuki ya kahayile kenako ilolile bhulagiji bho jitungulu bho ng’wa munhu nhebhe. Umunhu ng’winuyo agasanga abhiye bhalimalija gulya jiliwa jasagaga jigehu duhu.

Ijiliwa ijigehu jinijo jigalenganijiyagwa na jitunduhu ja nhumbi kunguno jili gung’wisho go mili go ng’wumbi yiniyo. Uweyi agagelela gulya jutundulu duhu ugalala. Hunagwene abhanhu bhagayomba giki, “agalagila jitundulu gete.”

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu uyo agakelejaga ugushika uko milimo yakwe, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agajaga ukumilimo yakwe bho gukeleja bhuli lushiku kunguno ya bhukokolo bhokwe bhunubho. Uweyi agadumaga ugupandika ijiliwa ija guilisha ikaya yakwe bhuli ng’waka kunguno ya gukeleja ugulima chiniko umuwikaji bhokwe bhunubho.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo agasanga bhalimalija ugulya abhiye, ugelela jitundulu duhu, kunguno nuweyi agakelejaga uguja ukumilimo yakwe mpaka nose oduma ugupandika ijiliwa bhuli ng’waka. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “agalagila jitundulu gete.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya gwanguha ugujutumama imilimo yabho, kugiki bhadule gupandika matwajo mingi umutumami bho milimo yabho yiniyo, umuwikaji bhobho.

KISWAHILI: ALISHINDIA KIWILIWILI CHA MWISHONI KABISA.

 Chanzo cha msemo huo, huangalia ushindiaji wa kiwiliwili wa mtu fulani. Mtu huyo, aliwakuta wenzake wakimalizia kula chakula kikiwa kimebakia kidoto tu.

Chakula hicho kidogo, hulinganishwa na kiwiliwili cha panzi ambacho kiko sehemu ya mwisho wa mwili wa panzi huyo. Yeye alikomea kula kiwiliwili hicho tu akalala. Ndiyo maana watu walisema kwamba, “ameshindia kiwiliwili cha mwishoni kabisa.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huchelewa kufika kwenye kazi zake, katika maisha yake. Mtu huyo, huenda kwenye kazi zake hizo kwa kuchelewa kila siku kwa sababu ya uvivu wake huo. Yeye hushindwa kupata chakula kingi kila mwaka kwa sababu ya kuchelewa kulima kwake huko kwenye familia yake hiyo.

Mtu huyo, hufanana na yule aliyewakuta wenzake wakila akakomea kula kiwiliwili tu, kwa sababu naye huchelewa kwenda kwenye kazi zake mpaka mwishowe anashindwa kupata chakula cha kutosha kila mwaka. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “ameshindia kiwiliwili cha mwishoni kabisa.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuwahi kwenda kuyatekeleza majukumu yao, ili waweze kupata mafanikio mengi katika kazi zao hizo, maishani mwao.

ENGLISH: HE TRULY SPENT THE WHOLE DAY AFTER EATING JUST A LAST BODY PART.

 This saying looks at spending day of a certain person who ate a small portion of food. Such man found his colleagues finishing eating who only ate a small left portion.

This little portion of food is equated to a body of a grasshopper which is at an end of its body. He only ate that body and fell asleep. That is why people said that, “he truly spent the whole day after eating just a last body part.”

This saying is related to a person who is always late to his works in his life. Such person goes to his work late every day because of his laziness. He fails to get much food every year because of such delay in his family farming.

This person is like the one who found his colleagues finished eating food who ate only the small last body part, because he is also late to his works until finally he fails to get enough food every year. That is why people tell him that, “he truly spent the whole day after eating just a last body part.”

This saying teaches people about ever going to carry out their duties on time, so that they can get a lot of success in their works, in their lives.

african-child-1381556_1280

1245. FUJAGA NDIMU, UTIZE’ FUJA NHO-LA


 

SWAHILI: KOSEA KULENGA MNYAMA MAWINDONI, USIKOSEE KUOA.

Kumekuwa na mjadala mkubwa kuhusu nafasi ya mwanamke katika mila za Kiafrika. Hili lilinifanya niwe na utafiti wa kina kwenye kabila la Wasukuma, ambapo wazee wa Wakisukuma (takribani 12) walithibitisha kwamba, ili familia ifanikiwe, jukumu la mwanamke haliepukiki. Kwa hivyo miongoni mwa Wasukuma, mwanamke katika familia anachukuliwa kuwa msaidizi wa karibu wa mumewe katika utunzaji na uhandisi wa shughuli zote za nyumbani.

Kwa hiyo wanaume wa Kisukuma hutumia methali hii “Fujaga ndimu, utize’ fuja nho-la.” Ili kutoa ufahamu kwa vijana wa kiume na wa kike kabla ya kupambanua kuingia katika maisha ya familia.

Methali hii ya Wasukuma inaonesha utimilifu mkubwa wa mwanaume na mwanamke katika familia yao, ikimaanisha kuwa mwanaume anapooa mwanamke shupavu, mwenye moyo mzuri, mwenye nidhamu, Wasukuma huamini kuwa familia nzima itafanikiwa kwa sababu mwanamke na mwanaume wanaweza kusaidiana vizuri katika maisha ya familia

Hivyo basi, wanawake wanapaswa kuelewa kwamba, wana nafasi au wajibu mkubwa wa kutekeleza katika familia zao. Wanapaswa kufurahishwa na hali yao kama wanawake katika familia na jamii zao.

Mwanzo 2:18 “Bwana Mungu akasema, si vema huyo mtu awe peke yake; nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.”

Marko 10:6-8 “…Mungu akamfanya mume na mke, kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.

Waefeso 5:31 “Lakini kila mmoja wenu ampende mkewe kama nafsi yake mwenyewe; na mke na amheshimu mumewe.

ENGLISH: MISS A TARGET WHEN HUNTING, RATHER THAN MARRYING A WRONG WOMAN.

There has been a great discussion on the role of women in the African traditions. This made me have a serious search on the Sukuma Ethnic group, where the Sukuma elders (about 12) confirmed that, in order for the family to prosper, the role of a woman is inevitable. Thus among the Sukuma, a woman in a family is regarded as the closer helper of her husband in keeping and engineering of all domestic activities. Hence the Sukuma men use this proverb “Fujaga ndimu, utize’ fuja nhola.” So as to give awareness to young men and women before discerning to enter family life.

This Sukuma proverb shows the great complementarity of man and woman in their family, meaning that when a man marries a strong, good hearted, disciplined woman, the Sukuma believe that the whole family will be prosperous because the woman and man can really help each other in family life

Hence, women should understand that, have a great role or duty to perform in their families.  They should be happy with their status as women in their family and society.

Gen 2:18 “Then the Lord God said, it is not good that the man should be alone; I will make him a helper fit for him.”

Mk 10:6-8 “….God made the male and female, for this reason a man shall leave his father and mother and be joined to his wife, and the two shall become one flesh…”

Eph 5:31 “however, let each one of you love his wife as himself, and let the wife see that she respects her husband.”

bride-5427659__480

family-portrait-5534737__480

engagement-7129147__480

 

 

 

1243. KALANGULAGA GITI NHANA NOI.

Aho kale olihoyi munhu uyo wikalaga muchalo ja Ng’watuju. Umunhu ng’wunuyo, osiminzaga alangulile bho nduhu nugubhagisha abhanhu abho otung’wanaga nabho umunzila yakwe kunguno guhaya gwanguha gushiga ukumilimo yakwe. Hunagwene abhanhu bhaganyomba giki, “kalangulaga giti nhana noi.”

Akahayile kenako kagalenganijiyagwa kuli munhu ndoshi uyo adahoyaga na bhiye chiza, umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agadililaga milimo yakwe bho guleka ugubhayombya abhanhu abho agikalaga nabho, kunguno ya bhudoshi ghokwe bhunubho, umuwikaji bhokwe. Uweyi agagayiyagwa abhanhu bha gung’wambilija ulu opandikagaga makoye aha kaya yakwe yiniyo, kunguno ya bhudoshi bhokwe bhunubho ubho guleka guhoya na abhiye, umukikalile kakwe.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo osimizaga alangulile bho ugubhagisha abhanhu, kunguno nuweyi agadililaga milimo yakwe duhu bho nduhu uguhoya na bhiye, umuwikaji bhokwe bhunubho. Hunagwene abhanhu bhaganhayaga giki, “kalangulaga giti nhana noi.”

Akahayile kenako, kalanga bhanhu higulya ya guleka gubhadalaha abhanhu bho guhoya nabho chiza umukikalile kabho, kugiki bhadule gwiyambilija chiza, ugujileka ikaya jabho.

Kutoka 20:12.

1Petro 1:17.

Isaya 29:13.

KISWAHILI: KAMERINGA KAMA KWELI MNO.

Hapo zamani alikuwepo mtu aliyeishi katika kijiji cha Ng’watuju. Mtu huyo, alikuwa akitembea akiwa ameangalia juu bila kuwasalimia watu aliokutana nao njiani, kwa sababu ya kutaka kuwahi kufika katika safari yake. Ndiyo maana watu waliongea juu yake kwamba, “kameringa kama kweli mno.”

Msemo huo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huwa haongei vizuri na wenzake katika maisha yake. Mtu huyo, hujali shughuli zake kwa kuacha kuongea na watu anaoishi nao, kwa sababu ya majivuno yake hayo, maishani mwake. Yeye hukosa watu wa kumsaidia anapopata matatizo katika familia yake kwa sababu ya kuacha kuongea na wenzake hivyo, katika maisha yake.

Mtu huyo, hufanana na yule aliyetembea akiwa ameangalia juu bila kuwasalimia wenzake, kwa sababu naye hujali shughuli zake tu bila kuongea na wenzake, maishani mwake. Ndiyo maana watu humuongelea kwamba, “kameringa kama kweli mno.”

Msemo huo, hufundisha watu juu ya kuacha kuwadharau watu wao kwa kuongea nao vizuri katika maisha yao, ili waweze kusaidiana vizuri, katika kuzilea familia zao.

Kutoka 20:12.

1Petro 1:17.

Isaya 29:13.

ENGLISH: ONE IS PROUD AS IF IT IS TOO TRUE.

Once upon a time there was a man who lived in the village of Ng’watuju. Such man used to walk looking upwards without greeting the people whom he met on the way, because he wanted to arrive on time in his journey. That is why people said about him that, “one is proud as if it is too true.”

This saying is related to a person who does not talk well with his colleagues in his life. That person cares about his activities enough to stop talking to people whom he lives with, because of his pride, in his life. He lacks people to help him when he has problems in his family because he stops talking to his colleagues like that, in his life.

This person is similar to the one who walked looking upwards without greeting his colleagues, because he also only cares about his activities without talking to his colleagues, in his life. That is why people talk about him saying, “one is proud as if it is too true.”

This saying teaches people about stopping belittling their people by talking to them well in their lives, so that they can help each other well, in raising their families.

Exodus 20:12.

1 Peter 1:17.

Isaiah 29:13.

man-6900166_1280

peasant-4962831__480

woman-6116276__480

1242. WITUNGILAGA ING’HINDA HIYIKU ISAJI IMBA UGUITALIGULA GINEHE!

Aho kale olihoyi munhu uyo agayitungila ing’hinda yakwe hiyiku lisaji aho lyalililalile. Aho lyamisha iliyiku linilo ligandya guyumpeja umunhu ng’wunuyo kugiki linkunde kunguno lyali likali noyi. Hunagwene abhanhu bhagang’wila giki, “witungilaga ing’hinda hiyiku isaji imba uguitaligula ginehe!”

Ulusumo lunulo, lugalenganijiyagwa kuli munhu uyo agagikoloshaga mamunhu mashilimu umukikalile kakwe. Umunhu ng’wunuyo, agacholaga mamihayo bho gugikolosha amamunhu amashilimu ayo gagankanyaga ikesi kunguno gajimanile sheria, umuwikaji bhogo. Uweyi agamalaga isabho jakwe bho gugalipa amamunhu ayo agagikoloshaga genayo ulugankinda ahibhanza, kunguno gamanile uguyomba.

Umunhu ng’wunuyo, agikolaga nuyo agaitungila inhinda yakwe hiyiku isaji, kunguno nuweyi agagikoloshaga mamunhu mashilimu ayo gajimanile isheria ja hibhanza, umuwikaji bhogo. Hunagwene abhanhu bhagang’wilaga giki, “witungilaga ing’hinda hiyiku isaji imba uguitaligula ginehe!”

Ulusumo lunulo, lolanga bhanhu higulya ya guleka gwichobhela mamihayo bho gubhikolosha abhichabho, kugiki bhadule gujilanhana chiza isabho jabho, umukaya jabho jinijo.

Mithali 21:24-25.

Mithali 18:23.

KISWAHILI: UMEIFUNGIA NJUGA KWA MAKISAI KICHAA SIJUI UTAIFUNGUAJE!

Hapo zamani alikuwepo mtu aliyeifungia njuga yake kwa makisai kichaa wakati akiwa amelala. Alipoamka makisai huyo alianza kumfukuza ili amugonge kwa sababu alikuwa mkali mno. Ndiyo maana watu walimwambia kwamba, “umeifungia njuga kwa makisai kichaa sijui utaifunguaje.”

Methali hiyo, hulinganishwa kwa mtu yule ambaye huwachokoza watu waliowajanja, katika maisha yake. Mtu huyo, hutafuta kesi kwa kuwachokoza watu hao wenye ujanja wa kujua sheria ambao humshinda kesi kwa sababu ya uelewa wao mzuri wa sheria hizo, katika maisha yao. Yeye huzimaliza mali zake kwa kuwalipa watu hao wenye ujanja wa kuongea vizuri mahakamani wanapomshinda kesi kwa sababu ya wao kuzijua vizuri sheria za hapo mahakamani.

Mtu huyo, hufanana na yule aliyeifungia njuga yake kwa makisai kichaa akashindwa kuifungua, kwa sababu naye hujitafutia kesi kwa kuwachokoza watu wanaozijua sheria vizuri, ambao humshinda kesi na kumlipisha, katika maisha yake. Ndiyo maana watu humwambia kwamba, “umeifungia njuga kwa makisai kichaa sijui utaifunguaje.”

Methali hiyo, hufundisha watu juu ya kuacha kujitafutia kesi kwa kuwachokoza wenzao, ili waweze kuzitunza vizuri mali zao, katika familia zao.

Mithali 21:24-25.

Mithali 18:23.

ENGLISH: YOU HAVE TIED A BELL TO A CRAZY OX, I DO NOT KNOW HOW YOU WILL UNTIE HIM!

Once upon a time, there was a man who tied his rattle to a crazy ox during sleeping time. When the ox woke up started chasing him to hit him because of being too fierce. That is why people told him that, “you have tied a bell to a crazy ox, I do not know how you will untie him!”

This proverb is compared to the person who provokes clever people in his life. Such person, looks for a case by provoking those people who are clever to know the law enough to win the case because of their good understanding of those laws, in their lives. He ends his wealth by paying those people who have skills to speak well in court when they win the case because they know well the rules of those courts.

This person resembles the one who tied his bell to a crazy ox and failed to untie him, because he also seeks a lawsuit by provoking people who know the law well, who normally win the case and tell him to pay them. That is why people tell him that, “you have tied a bell to a crazy ox, I do not know how you will untie him!”

This proverb imparts in people an idea of stopping provoking their people, so that they can take good care of their properties, in their families.

Proverbs 21:24-25.

Proverbs 18:23.

oxen-6257030_1280

cow-5473548_1280

farmer-4485956_1280